Webabu
JF-Expert Member
- Apr 29, 2010
- 7,283
- 11,147
Madaktari na watu wa afya kwenye eneo la Gaza wameshughulika sana kufukua makaburi ya halaiki baada ya vikosi vya Israel kuondoka maeneo ya mahospital waliyokuwa wakiyakalia.
Hali ni ya kutisha na kusikitisha sana baada ya watu waliokuwa wanatafuta ndugu zao kugundua maiti wengi wakiwa na dalili za kuzikwa wakiwa hai.
Maiti hao wengine walikuwa na pingu mikononi kuashiria ni wale waliodhaniwa ni wapiganaji wa Hamas.Wengine kati yao wamekuta na dripu mikononi mwao kuashiria kuwa walikuwa ni wagonjwa waliolazwa kwenye hospitali hizo.
Kazi hiyo mpaka sasa imefanyika kwenye hospitali chache kubwa katika mji mkuu wa Gaza na katikati ya eneo hilo.
Itakumbukwa kuwa jeshi la Israel mara kadhaa bila kutoa uthibitisho lilishutumu kuwa mahospitali ndiko walikokuwa wamejificha wapiganaji wa Hamas waliokuwa wakiwawinda.
La kushangaza ni kuwa kwa sasa hospitali karibu zote za Gaza ukiondoa chache zilizobaki Rafah zimepigwa na kugeuzwa kifusi.Wakati huo huo vita bado havijamalizika.
Hali ni ya kutisha na kusikitisha sana baada ya watu waliokuwa wanatafuta ndugu zao kugundua maiti wengi wakiwa na dalili za kuzikwa wakiwa hai.
Maiti hao wengine walikuwa na pingu mikononi kuashiria ni wale waliodhaniwa ni wapiganaji wa Hamas.Wengine kati yao wamekuta na dripu mikononi mwao kuashiria kuwa walikuwa ni wagonjwa waliolazwa kwenye hospitali hizo.
Kazi hiyo mpaka sasa imefanyika kwenye hospitali chache kubwa katika mji mkuu wa Gaza na katikati ya eneo hilo.
Itakumbukwa kuwa jeshi la Israel mara kadhaa bila kutoa uthibitisho lilishutumu kuwa mahospitali ndiko walikokuwa wamejificha wapiganaji wa Hamas waliokuwa wakiwawinda.
La kushangaza ni kuwa kwa sasa hospitali karibu zote za Gaza ukiondoa chache zilizobaki Rafah zimepigwa na kugeuzwa kifusi.Wakati huo huo vita bado havijamalizika.