Ukweli Mchungu kuhusu Kudanga

Mabinti wengi wanadanga ili kupata mitaji ya biashara lakini mwisho wa siku wakipata mitaji wanashindwa kuendesha biashara na wanajikuta wakifirisika na kurudia tena kudanga/Kuuza Mbususu.
wanaishia tu kupata mimba na kuwa single mother. uzinzi haunaga mwisho mzuri.
 
Anabaki nacho ila kinachakaa..

Gari inabaki na tyre zake ila inapopita njia tofauti tofauti inapata damage mbali mbali.

Kuna tofauti ya gari inayopita njia nzuri yenye lami na ile inayopita kwenye njia za vumbi, makorongo, tope n.k
Kufananisha gari na hii bidhaa ni makosa makubwa..
 
Hizo ni hadithi zinazowapatia ajira, kwa hivyo siwezi kutegemea waseme tofauti.

Kuna muktadha fulani mdogo wako sawa. Lakini, hayo maneno yanaweza kuwa na maana zaidi Marekani ambako watu hata masikini wana options nyingi za kutajirika. Unaweza kufanya maandalizi, fursa ziko nje nje, nyingine zinatafuta watu hazipati, unakutana nazo, unakuwa umesababisha bahati ikutembelee.

Tatizo hawa motivational speakers wanaiga sana maneno ambayo hayakukusudiwa kutolewa kwa watu wa dunia yao, yalikusudiwa kutolewa kwa dunia ya Wamarekani.

Ukizaliwa masikini Tanzania, hata hizo zinazoitwa fursa zenyewe ni mitego ya wewe kupigwa uchukuliwe hata hicho kidogo ulicho nacho, ukijiandaa ukutane na fursa sehemu ambayo fursa zina figisu kibao, kuitoa ni lazima upige ma karate kupita movies za Hong Kong za miaka ya 1970s, hapo ukikosa fursa napo utalaumiwa?
Well said
 
Kazi ambayo haisapotiwi na universe hauwezi kutoboa na kuwa na peace of mind with consistency
 
Watu hawajasoma chochote wala hawajui kitu zaidi ya mavitabu yao ya kidini halafu wanataka kuja kujenga hoja na mtu aliyesoma philosophy, laws of Contradictions, ma quantum physics, ma laws of physics ma universe huko, Scientists karibia wote, Religion karibu zote.....😄😄

Kujenga hoja na wafia dini wa namna hiyo, Ni sawa na kumwelezea mtoto wa darasa la tatu hesabu za Calculus..

Wakati yeye bado anafundishwa hesabu za kujumlisha na kutoa..
 
Mkuu unawezaje kuamini Swala la bahati, ikiwa huamini uwepo wa Mungu,

Labda nikuulize bahati ni nini, unawezaje kuthibitisha mambo ya bahati ,
Inawezekana pia kwa wengi wao sababu zilizowafanya washindwe kutafuta mtaji bila kudanga ndiyo hizo hizo zinawafanya washindwe kufanya biashara baada ya kupata mtaji kwa kudanga.

Mara nyingi sababu ni uwezo mdogo kifikra.

Mtaji mdogo ni sababu nyingine.

Kukosa network hakuwezi kudogoshwa.

Ma mara nyingine mafanikio ninsuala la bahati. Hatuwezi kuacha kuzungumzia bahati.

Mtu aliyejipanga vizuri kila kitu anaweza kutofanikiwa kwa kukisa bahati ya kuwa at the right time, at the right place, halafu, mtu ambaye hajajipanga vyovyote akaipata bahati hiyo.
 
Hauamini kuna Divine power ila unakubali bahati? Make it make sense mkubwa umeanza kuisha makali, and if you are really smart as u potray yo self utakuja kiri someday! Am sure huna u smart wa kumzidi mtu kama Andrew Tate go watch his revert story as a former atheist.

pia kisayansi bahati ni nini kwa uelewa wako coz everything has to be proven scientifically kwa mujibu wako mbona unaji contradict, unasemaga kila kitu kina explaination na visivyokua na maelezo ni binadamu tu hajajua bado! Too many loopholes, karibu upande huu kiongozi ata ku research tu nmekuambia mara kwa mara this world is a biggest puzzle never limit your self kua ume master swala flani, elimu haijawahi kutosha ata usome tangu unajitambua hadi unakufa kuna meeengi utayaacha hujajua!

No God, no spirits, no destiny ila kuna bahati 😂🤔🙌
ameji contradict mwenyewe
 
Mkuu unawezaje kuamini Swala la bahati, ikiws huamini uwepo wa Mungu,

Labda nikuulize bahati ni nini, unawezaje kuthibitisha mambo ya bahati ,
Swali zuri.

Bahati ni jambo kutokea bila kupanga, bila kulifanyia kazi. Randomly. Na bahati haihitaji uwepo wa Mungu.

In fact, bahati/ randomness inaonesha kuwa Mungu hayupo. Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote angekuwepo, bahati isingewezekana kuwapo. Kwa sababu bahati inaweza kumpa kitu kizuri mtu mbaya na kumpa kitu kibaya mtu mzuri.

Mungu wa haki angekuwepo, asingeruhusu bahati iwepo.

Kwa hivyo, hakuna contradiction kusema Mungu hayupo na bahati ipo.

Kuna mambo katika maisha yanatokea kwa bahati tu.

Yule Hasheem Tahabit unafikiri asingezaliwa na bahati ya kuwa mrefu angefika NBA?

Huchagui wala hufanyii kazi kuzaliwa, unajikuta tu umezaliwa kwa bahati tu.

Nchi unayozaliwa, huchagui wala huifanyii kazi, inatokea kwa bahati tu.

Vinasaba unavyozaliwa navyo huvipati kwa kufanyia kazi, unavipata kwa bahati tu.

Wazazi waliokuzaa huwachagui, unajikuta umezaliwa na wazazi hao kwa bahati tu.

Socio economic class unayozaliwa hujaipanga wewe, unajikuta tu umezaliwa familia ya Kifalme ya Uingereza au mtoto wa Kapuku.

Sasa Prince William wa Uingereza akiwa anafurahia maisha mazuri sana kuliko mtoto wa kapuku wa Nangurukulu utasema hakuna bahati ya kuzaliwa iliyosababisha hivyo?
 
ameji contradict mwenyewe
Unaweza kuona contradiction kama tu ume define kuwa ni lazima bahati itokane na Mungu.

Bahati ni mambo kutokea kwa kufuata randomness tu, bila kupangwa. Hatuhitaji Mungu ili mambo yatokee kwa randomness.

In fact mambo kutokea randomly ndiyo kunaonesha Mungu hayupo, kwa sababu Mungu ni order, the opposite of order is randomness. Therefore randomness/bahati inaonesha kutokuwepo Mungu.

Usichoelewa ni nini hapo?

Mnapata vipi hii conclusion wakati bahati inaonesha Mungu hayupo na ukikubali bahati ipo wakati unaamini Mungu yupo ndiyo una ji contradict?

Ulimwengu ulioumbwa na Mungu mjuzi wa yote, mwenye upendo wote , uwezo wote na haki yote hauwezi kuwa na bahati.

Kwa sababu bahati inavunja haki, inaweza kumzawadia mtu muovu mambo mazuri na kumpa mtu mwema mambo mabaya. Sasa Mungu huyo wa haki ataruhusu vipi bahati?

Bahati inaonesha Mungu hayupo, hakuna contradiction kusema sikubali Mungu yupo lakini nakubali kuna randomness, mambo mengine yanatokea kwa bahati tu.

Usichoelewa kipi?
 
Back
Top Bottom