Kuelekea 2025 Tundu Lissu: Abdul (mtoto wa Rais Samia) alitaka tukutane kwenye hoteli moja Masaki anihonge, nikamwambia njoo kwangu

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Makamu mwenyekiti wa CHADEMA, Tundu Lissu akizungumza kwenye kipindi cha Medani za Siasa, Star TV, leo Agosti 17, 2024, amesema Mtoto wa Rais Samia aliyemtaja kwa jina la Abdul alitaka kumhonga pesa Novemba 2023.

Tundu Lissu amesema Abdul hakutaja kiwango cha pesa, na alitaka aende usiku kwenye mojawapo ya hoteli zilizopo Masaki ili apatiwe pesa hizo lakini alikataa, akasema aje nyumbani kwake Tegeta. Lissu amesema Abdul alitumia watu wa chama chake kumfikishia ujumbe huo.

Amefafanua zaidi kuwa kijana huyo alikuja nyumbani kwake, na baada ya kutaka kumpa pesa alizikataa akasema anataka kupewa pesa zenye risiti, siyo hizo za gizani. Kwenye mazungumzo hayo walikuwepo watu wanne, na walinzi wa Abdul wakiwepo nje ya nyumba yake.

Kwa mujibu wake, yeye alizikataa pesa hizo na kumwambia aende akamwambie Rais amlipe stahiki zake kwa mujibu wa sheria na siyo kumhonga, na alimpatia nyaraka zote zinazohusiana na madai yake.

Baada ya hapo hawakuwahi tena kuwasiliana.

Lissu amekataa kumtaja kiongozi wa CHADEMA aliyeambatana na Abdul.

Pia soma
Abdul anatuhumiwa kwa kugawa rushwa mama yake Yuko kimya

Haya ndo mambo huangusha watawala natawala
 
View attachment 3073329

Kwa muhitasari:

Tundu Lissu: "aliwatumia watu wema wa chama changu. Na kwanza aliniomba tukutane katika hotel moja sijui inaitwaje huko maeneo ya Masaki, DSM...."

Tundu Lissu: "Nikawaambia mwambieni kama ana shida na mimi wamlete nyumbani kwangu. Walimleta na tulikaa hivi hivi face to face kama tulivyokaa mimi na wewe hapa mwandishi"

Tundu Lissu: "Alisema anataka kunisaidia. Nikamwambia kama kweli unataka kunisaidia, mwambie mama yako ambaye ni Rais alipe pesa zangu za matibabu zenye risisti. Hizi za kwako ni hongo, hazina risiti"

Tundu Lissu: "Akasema, ooh, mama (Rais Samia) analalamika hujawahi kumwandikia kuomba hizo pesa. Nikamwambia nilishaandika mara mbili. Pamoja na hayo nilimpa nakala ya madai yangu, nikamwambia si anasema sijamwandikia? Mpelekee barua yangu ya madai nakala hii hapa. Mpaka leo kimya, hajawahi kuwasiliana nami tena......!"

Tundu Lissu: "Kwangu hakuna CCTV cameras. Lakini sikiliza, nafahamu mimi ni mwanasheria. Na katika sheria ya ushahidi, ushahidi ulio bora kabisa kisheria ni ule wa mtu kuona, kusikia, kushika na kunusa mwenyewe. Mimi niliona mwenyewe. Zaidi pia ni kuwa katika mazungumzo yale, tulikuwa na watu wanne jumla ndani/au mahali tulipokuwa na huyo mgeni na huko nje kulikuwa na walinzi wa kutosha"

Kwa uelewa zaidi, tumia bundle lako kumsikiliza na kumtazama mwenyewe hatua kwa hatua hadi mwisho...

Moderator unganisha uzi huu na uzi mkuu unaobeba mada hii. Video clip hii ni muhimu sana kuisapoti na kuleta credibility ya mada kuu

..Video clip uliyowasilisha inatakiwa kuwekwa ktk post ya kwanza kwa uzi huu.
 
Makamu mwenyekiti wa CHADEMA, Tundu Lissu akizungumza kwenye kipindi cha Medani za Siasa, Star TV, leo Agosti 17, 2024, amesema Mtoto wa Rais Samia aliyemtaja kwa jina la Abdul alitaka kumhonga pesa Novemba 2023.

Tundu Lissu amesema Abdul hakutaja kiwango cha pesa, na alitaka aende usiku kwenye mojawapo ya hoteli zilizopo Masaki ili apatiwe pesa hizo lakini alikataa, akasema aje nyumbani kwake Tegeta. Lissu amesema Abdul alitumia watu wa chama chake kumfikishia ujumbe huo.

Amefafanua zaidi kuwa kijana huyo alikuja nyumbani kwake, na baada ya kutaka kumpa pesa alizikataa akasema anataka kupewa pesa zenye risiti, siyo hizo za gizani. Kwenye mazungumzo hayo walikuwepo watu wanne, na walinzi wa Abdul wakiwepo nje ya nyumba yake.

Kwa mujibu wake, yeye alizikataa pesa hizo na kumwambia aende akamwambie Rais amlipe stahiki zake kwa mujibu wa sheria na siyo kumhonga, na alimpatia nyaraka zote zinazohusiana na madai yake.

Baada ya hapo hawakuwahi tena kuwasiliana.

Lissu amekataa kumtaja kiongozi wa CHADEMA aliyeambatana na Abdul.

Pia soma
Okay
 
Kwa mamaye. Niulize mamaye anatoa wapi hayo mabulungutu ya hela? Jibu: anaiba kwa watanzania.
 
Back
Top Bottom