Dar to Pretoria na gari private: Ushauri na changamoto zake plus gharama

Kuna njia 2 ya Lusaka na ya Harare

Kutoka Dar mpk harare kwa bus ni 150,000 Harare mpk Joburg Rand 200

Kutoka Dar mpk Tunduma 45,000 kutoka tunduma mpk Lusaka sikumbuki na kutoka Lusaka mpk SA Rand 700.
Kamata it mpka Zambia mengine utayajua mbele kwa mbele maana ni cheap sana kupanda gar za it
 
Achana na hiyo biashara kichaa, chukua SAA au Fastjet (kama bado wanaenda) mpaka johanesburg then unapanda train ya umeme mpaka pretoria
 
umetoa muongozo sahihi
Kaka jitahidi muwe wawili au watatu kusaidiana hiyo safari ni safari nzuri lakini inafikia kipindi utatamani utembee kwa miguu

Maandalizi ya safari utaanza na Service yako ya gari vizuri, kisha utalipeleka gari traffic pale makao makuu kwa wakaguzi wa gari (Vehicle Inspector) ukishapata hiyo Report yao, utaenda nayo INTERPOL (pale Wizara ya Mambo ya Ndani) wao watakupa Clearance report kuwa hiyo gari ni yako na haina tatizo lolote hivyo kokote utakofika walihesabie kuwa hilo gari sio la wizi, HIYO REPORT YA INTERPOL NI MUHIMU SANA SAA NYINGINE UNAWEZA KUPATA USUMBUFU UKIWA HAUNA HIYO

Safari za mbali hazihitaji speed zaidi ya 100km/hr , ukiwa na speed kubwa zaidi ya hiyo utahitaji concentration kubwa na utachoka mapema,
Kwanza Ipange safari yako kwamba siku ya kwanza utalala Tunduma, ili asubuhi uanze na paper work, kwa upande wa Tanzania watataka kuona karatasi zote pamoja na hiyo interpol report, KADI YAKO ORIGINAL YA GARI ITABAKI PALE BORDER UPANDE WA TANZANIA (Custom),

Zambia wanakuwa na kausumbufu kadogo, hakikisha gari lako umelibandika vi reflector vidogo. Mbele vyeupe na Nyuma vyekundu, Zambia utalipia insurance kulingana utakaa siku ngapi hapo (Transit status), kisha utalipia Carbon Tax, na vitu vingine vidogvidogo, ukianza procedure hizo za paper work say saa moja na nusu au saa mbili basi ikifika saa tano utakuwa umemaliza na unaweza kuanza safari yako

Umbali wa kutoka Tunduma/ Nakonde mpaka Lusaka unaweza kukuchukua masaa 18 mpaka 20, kuna sehemu za kujaza mafuta kwenye miji mikubwa ya njiani kama Serenje, KapiliMposhi nk, uwe makini na speed kwa upande wa Zambia hasa kutoka Tunduma/Nakonde mpaka Kapilimposhi njia sio nzuri sana,
Kutoka Lusaka njia nzuri ni ya kupitia Botswana, hivyo utaelekea njia ya Livingstone mpaka Kazungula hapo kuna kivuko cha kuingia Botswana, ukishaingia Botswana utaitafuta Gaborone kwa kupitia miji ya Maun, Serowe, Francistown, Palapye, Mahalapye, Mochudi kisha Gabs,

Kutoka Gaborone mpaka Border ya South africa ni Umbali wa kutoka Mwenge mpaka Posta Mpya, na hiyo Border inakuingiza moja kwa moja Gauteng Provence ambayo ndio ina Jos na Pretoria, kutoka Gabs mpaka Jos ni six hrs

PLZ: Kwa safari ndefu kama hizo usisahau Spare tyres hata mbili, spanner zote muhimu zinazofungua gari yako Fix na combine, wheel spanner ile ya msalaba pamoja na jack, set ya Screw drivers, set ya fuse zinazotumika kwenye gari yako, hydraulic na engine oil, ikiwezekana set ya bulb pia uwe nayo
Kidumu cha maji na dumu la liter 20 la Petrol,
 
Gari ya cc 2.5 appx utatembea 8-9 km kwa kutumia lita 1 ya Petroli, sasa piga hesabu kutoka Dar mpaka Pretoria ni kilomita ngapi kwa njia utakazo pita? Hapo utapata atleast an idea ya kujua utatumia Petrol lita ngapi kwenda na kurudi.
Kwenda na kurudi anahitaji kama 700 litres
 
Hapa utatiwa uoga mwingi,mala hyo safari ni ndefu sana sijui fanya hili na lile kwenye gari,hakuna kitu.ukweli ni kuhakiki gari na inaweza kwenda,utatembea 3620km frm Dar mpaka jbrg.labda la msingi sana ni vibali halali vya safari yako ili usije tiwa nguvuni ukiwa ugenini,all the best mkuu.ukifika useme nikuelekeze kwa shemeji yako ukapige ugari na samaki ila usimtokee!
 
Africa's Cowboy Capitalists (Full Length)
Journey by road from Johannesburg in South Africa through Zambia, Tanzania, Uganda and South Sudan

sehemu gani korofi katika njia hiyo ki miundombinu na kiusalama

(3) mipakani regulations kama unatoka na mzigo wa biashara toka pretoria kwenda dar inakuwaje?

(4) vitu gani vya muhimu ambavyo ni lazima niwe navyo standby

(5) na safari inakadiria kuchukua siku ngapi (max)


(6) mwisho kabisa ni changamoto gani nitarajie kukutana nayo kwenye njia hiyo

(7) lakini pia ni mazuri gani nitarajie kukutana nayo kwenye safari hiyo


Source: VICE

Ila kwenye hii safari ya hawa mabwana Tanzania tumuwazingua sana inabidi tubadilishe mifumo yetu
 
Ila kwenye hii safari ya hawa mabwana Tanzania tumuwazingua sana inabidi tubadilishe mifumo yetu

Mkuu,
Naona watu Youtube (comments za kila upande wa dunia) wamepongeza askari wa trafiki wa Tanzania kwa kutoangalia sura wala rangi ya mtu, wote wanapungiwa mkono kusimama kila baada yamwendo mfupi.

Pia safari ya kilomita 3,000 ya huyu jamaa mwingine toka mji wa Lubumbashi katika jimbo la Katanga DRC Congo kupitia Zambia, Tanzania mpaka Kenya na kutupatia maelezo yenye mwangaza juu ya bima ya gari kimataifa, vibali, mapumziko njiani,mafuta, hali ya hewa/mvua n.k ili kupita nchi mbalimbali kwa gari ukiwa umejitayarisha kukabiliana na mambo-tajwa muhimu.
C.C mdau C.T.U
Daring abroad : Kenyan businessman drives from Lubumbashi via Zambia, Tanzania to Kenya

Source: KTN News Kenya
 
Back
Top Bottom