Kuna mwenye uzoefu na mazda demio generation, 2 ya 2005, napenda kujua uimara wake hapa bongo na upatikanaji wa vifaa. Pia gharama zake kuitoa bandarini. Ina 1.3L, CIF $2000
Ukiambiwa tafuta TOYOTA, hiyo mazda spare zake ni shida, maana yake si kwamba hakuna spare kabisa, tatizo ni upatikanaji kwa urahisi. Uwe na gari ambayo hata ukiwa safarini ukipata tatizo spare yake unaipata kwenye duka la karibu hata kama itakua fake, lakini itakufanya ufike na baadaye utatafuta "genuine part". Sasa kama utategemea spare ya "befoward" na wewe uko say Manyoni unaelekea Mwanza, huoni tayari safari imekwama?
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.