Waziri Bashe: Serikali haijazuia kuuza mazao nje ya Nchi, imezuia Watu kufanya biashara bila kufuata utaratibu wa kisheria

Suley2019

JF-Expert Member
Oct 7, 2019
1,831
4,586

Waziri wa Kilimo Hussein Bashe amesema Serikali haijazuia kuuza mazao nje ya Nchi isipokuwa imezuia Watu kufanya biashaea bila kufuata utaratibu wa kisheria .

Bashe ametoa kauli hiyo June 21, 2023 Bungeni Jijini Dodoma wakati akijibu swali la Mbunge wa Jimbo la Tarime Vijijini Mwita Waitara aliyetaka kujua sababu za magari ya mazao kuzuiwa katika mpaka wa Silali baada ya zuio la Waziri kusitisha kuuza mazao nje ya Nchi.

Waziri Bashe amesema ‘’Haiwezekani Mtu unanunua mahindi Songea unapakia kwenye malori hauna leseni ya biashara, hauna TIN namba halafu unataka Nchi ikuruhusu Kwenda kuuza nje mazao hayo , malipo hayaonekani katika mfumo rasmi wa fedha, hatuzipati data , maelekezo ya Rais yako wazi Mtanzania yeyote anayetaka kufanya biashara ya mazao kwaajili ya kuuza nje au ndani akate leseni ya biashara”

‘’Nitumie Bunge lako tukufu kuwambia Wafanyabiasha wa mazao nendeni kwenye Hamashauri kateni leseni za biashara ili muuingie kwenye mfumo rasmi wa biasahara ya mazao ya kilimo, hatuwezi kuendelea katika mfumo huu unaondelea na nia ya Serikali ni kurasimisha shughuli za kilimo na shughuli za biashara za mazao”.

Pia Soma:
- Waziri Bashe apigilia Msumari marufuku ya kuuza Mazao nje ya Nchi
 
Huyu msomali kwakweli hapana kabisa

Rais Samia alieleweka vizuri sana,hakusema kwamba serikali imezuia kuuza nje ya nchi chakula kwa sababu wauzaji wanakiuka taratibu,bali kuhofia upungufu utokanao na mabasi ya tabia nchi ,vita Ukraine,na pengine mavuno kuchechemea,

Sasa Bashe yuko mbioni kumaliza vihenge vya taifa vya chakula kwa vibali maalumu,huyu atumbuliwe haraka sana,hii ni kashifa nyingine inakuja kwa rais Samia kutokana na hawa vijana wa Rostam Aziz
 
Waziri wa Kilimo Hussein Bashe amesema Serikali haijazuia kuuza mazao nje ya Nchi isipokuwa imezuia Watu kufanya biashara bila kufuata utaratibu wa kisheria.

Bashe ametoa kauli hiyo June 21, 2023 Bungeni Jijini Dodoma wakati akijibu swali la Mbunge wa Jimbo la Tarime Vijijini Mwita Waitara aliyetaka kujua sababu za magari ya mazao kuzuiwa katika mpaka wa Silali baada ya zuio la Waziri kusitisha kuuza mazao nje ya Nchi.

Waziri Bashe amesema ‘’Haiwezekani Mtu unanunua mahindi Songea unapakia kwenye malori hauna leseni ya biashara, hauna TIN namba halafu unataka Nchi ikuruhusu Kwenda kuuza nje mazao hayo , malipo hayaonekani katika mfumo rasmi wa fedha, hatuzipati data , maelekezo ya Rais yako wazi Mtanzania yeyote anayetaka kufanya biashara ya mazao kwaajili ya kuuza nje au ndani akate leseni ya biashara”

‘’Nitumie Bunge lako tukufu kuwambia Wafanyabiasha wa mazao nendeni kwenye Hamashauri kateni leseni za biashara ili muuingie kwenye mfumo rasmi wa biasahara ya mazao ya kilimo, hatuwezi kuendelea katika mfumo huu unaondelea na nia ya Serikali ni kurasimisha shughuli za kilimo na shughuli za biashara za mazao”
 
Huyu yuko too theoretical.

Watu wako barabarani na mahindi yao yeye yuko ofc anakula kiyoyozi.

Kwa nini wasingetoa grace period kama hawajazuia?

Anya nyenyenye nyingi sana.

Juzi kati aliapiza kwamba mkulima auze popote pale anapojisikia sasa hivi kaamka asubuhi tu kapandisha. Ili tu mkulima ateseke.
 
Ila hili my minister linafikirisha mno, mbona risks ni kubwa sana kwa hili?,yaani mfanya biashara aingize semi trailer hapa lingusenguse mkoani Ruvuma, ananunue mahindi 40T,then aamue kuendesha hadi Namanga towards Kenya bila permits?

Hili linawezekana kweli? Na Kenya wayapokee mahindi haya bila ya paper work!,upumbavu wa watanzania sasa upo tested to max
 
Huku Kenya we are not even bothered. Hatujui ni nini inaendelea huko kwenu.
 
Hapo kale Bashe alisema hawezi kuwapangia Wakulima sehemu ya kuuza mazao yao; Tukasema ni Vema na Haki.., lakini tuka-caution Siasa za maji taka za Divide and Rule za kuwachonganisha walaji na wazalishaji...


Sasa Bashe anasema hatujazuia watu kuuza nje lakini wawe na Vibali / Biashara / Leseni.

Sasa nauliza hatujawazuia wakulima (peasants) kuuza popote au wafanyabiashara kuuza popote.

Kwahio badala ya kusema ni mtetezi wa wakulima (hawapangii bei) angasema ni mtetezi wa wafanyabiashara.

Unless otherwise hii itakuwa ni FlipFlopping kama kawaida ya Wafanyabiashara
 
Soma hapa kwa makini sana.
Screenshot_20230621-230547.jpg
 
Watu walishaanza kuona umuhimu wa kwenda shambani kulima sasa mnataka tuweke majembe chini tuzurure mjini?
 
Back
Top Bottom