SoC04 Uwekezaji wa viwanda vya uzalishaji na utengenezaji simu ni muhimu kwa maendeleo ya Tanzania

Tanzania Tuitakayo competition threads
Jun 25, 2023
45
31
Utangulizi

Zipo teknolojia nyingi sana ambazo ni kama zimetupita barani Afrika hususan nchi za Kusini mwa Jangwa la Sahara ikiwemo Taifa la Tanzania. Katika teknolojia hizi zilizotupita kidogo, ipo teknolojia ya kifaa cha ajabu ambayo hatupaswi tuendelee kuiacha itupite, na kifaa hiki si kingine bali ni simu. Ndiyo, ni Teknolojia ya Simu; simu yako hiihii unayotumia kusomea andiko hili au pengine unayotumia kuwasiliana na uwapendao.

IMG_20240504_120914.jpg

(Chanzo Picha: Global TV)


View: https://youtu.be/o9Mq7PYUjT0?si=dqGLkbmKdalgzyWQ


Simu ni kifaa cha ajabu, kilichobeba teknolojia mbalimbali kwa wakati mmoja, hivyo kuifanya uhitaji wake kuwa mkubwa zaidi kuliko teknolojia yoyote ile duniani. Hapa nazungumzia simu janja, ambayo mwanadamu yeyote anapoikosa anakuwa kama aliye gizani nyuma ya dunia, kwani yapo mambo mengi atashindwa kufanya.

Wapo watu mbalimbali mitandaoni ambao wamekuwa wakiwasilisha changamoto zao ili waweze kusaidiwa mfano mitaji ya biashara na mahitaji mengine muhimu, lakini cha ajabu baadhi yao huishia kuambiwa: "si uuze hiyo simu ukatatue changamoto yako?"

Ukweli wa mambo ni kwamba, inawezekana kabisa kuwa simu ina thamani kwa mmiliki kuliko kiasi kadhaa cha fedha, kwani simu inapotumika vizuri kwa njia halali, inaweza kumsaidia mmiliki kuingiza kipato kizuri sana kwa siku nyingi na kwa muda mrefu.

Kama kuna biashara na uwekezaji muhimu zaidi unatakiwa kuanzishwa nchini Tanzania ili kuwa Tanzania Tuitakayo; basi ni VIWANDA VYA UTENGENEZAJI NA UZALISHAJI SIMU; lakini kutokana na hali ya bara letu la Afrika kuwa changa katika teknolojia ya simu; ili tutengeneze simu zenye kiwango na ubora wa hali ya juu, inatupasa viwanda hivi vigawanywe katika makundi matatu ambayo ni:-

  1. Viwanda vya hatua ya mwanzo kabisa yaani viwanda vya utengenezaji wa malighafi ngumu (hard raw materials) za simu kama vile nyaya, vioo, majalada, haptic engines, uchakataji wa madini simu kama vile copper, zink, gold, n.k. (mobile hardwares)​
  2. Viwanda vya hatua ya kati vya utengenezaji wa malighafi tepe (soft raw materials) za simu kama vile softwares, language programs, font style designing, camera programs, n.k. (mobile softwares)​
  3. Viwanda vya hatua ya mwisho ya utengenezaji simu ambavyo vinahusika na Mawazo ya Ubunifu (Idea), Utengenezaji Taswira (Imaging and Sketching), Uthibitishaji wa Michoro (Sketch Proof), Uumbaji Michoro (Physical Product Sampling), Majaribio (Physical Product Test) na Uundaji wa Simu mpaka iingie sokoni. (Manufacturers)​

Kwanini viwanda vya utengenezaji na uzalishaji simu ni muhimu kwa TANZANIA TUITAKAYO?

Kwanza,
simu ni chombo cha mawasiliano ambacho kinaunganisha dunia. Mataifa na Makampuni makubwa duniani, yanahusika sana na utengenezaji na uzalishaji wa simu au viambata vya simu; mfano Microsoft na Apple. Lakini pia mataifa makubwa yaliyoendelea, yanajihusisha sana na Masuala ya Vyombo vya Mawasiliano; Japan (Sony), Korea Kusini (Samsung na LG), Marekani (Microsoft, Apple, Motorola na Google Pixel), Finland (Nokia), Ujerumani (Siemens), China (Huawei, Infinix, Vivo, Oppo na Tekno), n.k.
IMG_20240503_081452.jpg

(Chanzo Picha: Freepik)

Pili, simu ni maktaba na album nzuri ya uhifadhi wa matukio, kumbukumbu, picha, nyaraka, sauti, n.k. Kwa kutumia simu, tunaweza kuhifadhi nyimbo, vitabu, picha, na kumbukumbu nzuri; za kwetu na tuwapendao.

IMG_20240503_083809.jpg

(Chanzo Picha: Guiding Tech)

Tatu, simu ni mkusanyiko wa idhaa mbalimbali; redio, television, magazeti, n.k., ambayo hutuwezesha kupata habari kwa wakati kutoka duniani kote. Simu huweza kufanya kazi kama chombo cha habari.

IMG_20240503_092353.jpg

(Chanzo Picha: Slash Gear)

Nne, simu huchukua nafasi ya kompyuta. Kutokana na wepesi na urahisi wa kubeba, kuishika pamoja na uwezo wake makubwa wa kuhimili teknolojia mbalimbali, simu imechukua nafasi kubwa ya kazi za kompyuta mfano uandishi (typing) wa nyaraka kwa njia ya simu ni rahisi kuliko uandishi kwa njia ya kompyuta, vilevile usomaji wa nyaraka kwa njia ya simu ni rahisi kuliko usomaji wa nyaraka kwa njia ya kompyuta; kwani simu zinatuwezesha kusoma au kuandika nyaraka wakati wowote mahali popote.

IMG_20240503_083637.jpg

(Chanzo Picha: Coin Market Cap)

Tano, simu huchukua nafasi ya mashine mbalimbali kama vile scan machine. Hii ni kwasababu, simu inayo uwezo wa kuhifadhi programu mbalimbali zikiwemo programu zenye uwezo wa kuscan nyaraka na kuileta kwenye format ya PDF.

IMG_20240503_083654.jpg

(Chanzo Picha: Bruceb Consulting)

Sita, simu inachukua nafasi ya taa. Mara paap! Umeme unapokatika, kifaa cha kwanza ambacho wengi huwa tunakikimbilia ni simu, ili kuwasha tochi na tuweze kupata mwanga (nuru)

IMG_20240503_085755.jpg

(Chanzo Picha: MOSAIC Lille)

Saba, simu huweza kutumika kama dira ya kumwongoza mgeni katika eneo husika. Hii, ni pale ambapo mgeni anaamua kuitumia ramani (map) kwenye simu yake ili iweze kumwonesha mahali anapokwenda.

IMG_20240503_083513.jpg

(Chanzo Picha: Dreams Time)

Nane, simu inachukua nafasi ya saa na kalenda. Miaka ya nyuma, saa na kalenda zilikuwa zinatumika kweli kwa ajili ya kuonesha muda, siku, mwezi na mwaka, tofauti na miaka ya sasa ambapo saa na kalenda zimebaki kuwa urembo wa mkono au pambo la ukuta kwa wengi, kwani asilimia kubwa ya watu hutumia simu zao kusoma saa, siku, mwezi na mmwaka.
IMG_20240503_113648.jpg

(Chanzo Picha: Scott Stein, CNET)

Tisa, simu ni kifikishi cha watu kwenye teknolojia. Dunia ya sasa ambayo imezungukwa na teknolojia mbalimbali kama vile mitandao ya kijamii, platforms na forums mbalimbali ikiwemo Jamii Forums, zinahitaji simu yaani simu janja ili tuweze kuzifikia.

IMG_20240503_094447.jpg

(Chanzo Picha: Alamy)

Kumi, simu ni kichapuzo kizuri cha talanta na vipaji, kwani kupitia simu tunaweza kukuza vipaji vya uandishi, uchoraji, muziki, uigizaji na uzungumzaji au usimulizi kwa hadhira.

IMG_20240503_081530.jpg

(Chanzo Picha: Walmart)

Kumi na Moja, simu huweza kutumika kama chombo cha miamala na benki ya kuhifadhia fedha, kwa kutumia Mobile Money Apps, fedha mtandao, Huduma za kifedha za taasisi za fedha na mitandao ya simu.

IMG_20240503_101035.jpg

(Chanzo Picha: Concept Phones)

Kumi na Mbili, kamera za simu huweza kutumika katika huduma mbalimbali iwapo itakuwa kamera ya kawaida, kamera ya CCTV au Kamera ya Thermal. Huduma hizi huweza kuwa za afya, ulinzi, usalama, n.k.

IMG_20240503_100110.jpg

(Chanzo Picha: Atlantis Blog - Atlantis Worldwide)

IMG_20240503_100143.jpg

(Chanzo Picha: Medical News Today)

IMG_20240503_100234.jpg

(Chanzo Picha: Black View)


Hitimisho

Hivyo basi, uwekezaji wa VIWANDA VYA UZALISHAJI NA UTENGENEZAJI SIMU ni muhimu kwa Taifa la Tanzania ili iweze kuwa Tanzania Tuitakayo; Tanzania yenye ajira nyingi kwa wenyeji na wageni, Tanzania ya Mapinduzi Makubwa ya Viwanda na Tanzania yenye uchumi imara barani Afrika na duniani kote.

Mpendwa msomaji, tafadhali naomba uniorodheshee faida na kazi nyingine za simu janja, ambazo sijaziorodhesha katika andiko hili ili tujifunze pamoja.

Natanguliza shukrani zangu za dhati.​
 
Kama kuna biashara na uwekezaji muhimu zaidi unatakiwa kuanzishwa nchini Tanzania ili kuwa Tanzania Tuitakayo; basi ni VIWANDA VYA UTENGENEZAJI NA UZALISHAJI SIMU; lakini kutokana na hali ya bara letu la Afrika kuwa changa katika teknolojia ya simu; ili tutengeneze simu zenye kiwango na ubora wa hali ya juu, inatupasa viwanda hivi vigawanywe katika makundi matatu ambayo ni:-
Kabla haujaendelea, je ipo faida gani kushindana na makampuni ambayo tayari yameshapiga hatua kwenye teknolojia.

Sio kwa ubaya lakini wazo la kupambana ambapo sio uimara wetu linakuwa wazo la kujimaliza. Kuna haja gani kuiingia mbio race, katika njia mpya tena ukiwa na gari bovu na dereva amelewa!??

Mfano, tumuache mchina atuletee toothpick sie labda tushindane naye kwa kuzalisha karanga. Biashara ni mabadilishano
Viwanda vya hatua ya mwanzo kabisa yaani viwanda vya utengenezaji wa malighafi ngumu (hard raw materials) za simu kama vile nyaya, vioo, majalada, haptic engines, uchakataji wa madini simu kama vile copper, zink, gold, n.k. (mobile hardwares)
Kipande hiki though tunakimudu. Viwanda vijikite hapa maana malighafi zenyewe zatoka hukuhuku kwetu. Ipo ndani ya uimara tulionao.

Mpendwa msomaji, tafadhali naomba uniorodheshee faida na kazi nyingine za simu janja, ambazo sijaziorodhesha katika andiko hili ili tujifunze pamoja.
Umezieleza vizuri sana mleta mada. Simu imeshakuwa kitu tusichoweza tena kutengana nacho. Ahsante.
 
Kabla haujaendelea, je ipo faida gani kushindana na makampuni ambayo tayari yameshapiga hatua kwenye teknolojia.

Sio kwa ubaya lakini wazo la kupambana ambapo sio uimara wetu linakuwa wazo la kujimaliza. Kuna haja gani kuiingia mbio race, katika njia mpya tena ukiwa na gari bovu na dereva amelewa!??

Mfano, tumuache mchina atuletee toothpick sie labda tushindane naye kwa kuzalisha karanga. Biashara ni mabadilishano
Asante sana ndugu yangu kwa kuendelea kutoa maoni yako katika uzi au andiko hili.

Kwa namna ambavyo nimewaorodhesha Wajapan, Wamarekani, Wachina, Wakorea, Wajerumani, Wafini, n.k, nimemaanisha tujifunze kutoka kwao na si kushindana nao.

Lengo si kushindana nao, bali lengo ni kujifunza kutoka kwao na kuendeleza yale mazuri kisha kuboresha madhaifu yaliyomo kwenye kiwanda cha simu duniani.

Lengo si kushindana, lengo ni kutatua udhaifu uliomo katika kiwanda cha simu duniani ili madhaifu yake yawe utimilifu.

We never aim to compete, we aim to COMPLETE the mobile industry.
 
Kipande hiki though tunakimudu. Viwanda vijikite hapa maana malighafi zenyewe zatoka hukuhuku kwetu. Ipo ndani ya uimara tulionao.
Hapana, tunaweza kuanzisha, kutekeleza na kuendeleza aina zote tatu za viwanda vya simu nilivyoviorodhesha, haijalishi raw materials and resources zinatoka wapi, kikubwa ni hapahapa duniani; TUNAWEZA!!!
 
Asante sana ndugu yangu kwa kuendelea kutoa maoni yako katika uzi au andiko hili.

Kwa namna ambavyo nimewaorodhesha Wajapan, Wamarekani, Wachina, Wakorea, Wajerumani, Wafini, n.k, nimemaanisha tujifunze kutoka kwao na si kushindana nao.

Lengo si kushindana nao, bali lengo ni kujifunza kutoka kwao na kuendeleza yale mazuri kisha kuboresha madhaifu yaliyomo kwenye kiwanda cha simu duniani.

Lengo si kushindana, lengo ni kutatua udhaifu uliomo katika kiwanda cha simu duniani ili madhaifu yake yawe utimilifu.

We never aim to compete, we aim to COMPLETE the mobile industry.
Hapa nimekupata vema. Tujifunze kwa hao ma 'giants'
 
Semiconductor ndio msingi wa hii industry ndio maana USA inajaribu kuikaba China kwenye kipengele hiki, kwenye mada yako sijaona sehemu yoyote ikizungumzia hii Nyanja ambayo haipo hapa TZ. Tazamq case study ya Taiwan jinsi ITRI(Industrial Technology Research Institute) ilivyodevelop electronic industry taiwan
 
Semiconductor ndio msingi wa industry ndio maana USA inajaribu kuikaba China kwenye kipengele hiki, kwenye mada yako sijaona sehemu yoyote ikizungumzia hii Nyanja ambayo haipo hapa TZ. Tazamq case study ya Taiwan jinsi ITRI(Industrial Technology Research Institute) ilivyodevelop electronic industry taiwan
Nashukuru sana kwa kuchangia andiko hili na karibu sana ndugu yangu.

Kwanza kabisa nadhani semiconductor uliyoimaanisha wewe wanaita "Brains of Modern Electronics" yaani maana yake ndiyo injini yenyewe.

Katika andiko hili, ukisoma kile kipengele cha aina za viwanda, kiwanda cha mwanzoni kabisa cha mobile hardwares, kuna kitu kinaitwa 'haptic engines' nimekiorodhesha, hiki ndicho kwangu mimi nimemaanisha injini ya simu hivyo nadhani maana ni moja na semiconductor (kama sivyo niombe unisahihishe ndiyo maana nimeruhusu uongezeaji nyama kwenye andiko hili mpaka KIELEWEKE; KUELEKEA TANZANIA TUITAKAYO).

Kuhusu case study ya Taiwan jinsi ITRI(Industrial Technology Research Institute) ilivyodevelop electronic industry taiwan, naomba nikasome na nashukuru sana kwa kushare info hii na mimi.

Shukrani sana.
 
Kwa faida ya msomaji wangu, kutokana na andiko hili kuhusu Simu, ipo mada na maswali ambayo yameibuka kupitia andiko hili la VIWANDA VYA SIMU. Mada hii ni mada inayoitwa Semiconductor Industry ambayo kwa mujibu wa andiko letu, inaingia kwenye kundi la viwanda vya hatua ya mwanzo kabisa la mobile hardwares; nikiijumuisha katika Hactic Engines kwani hizi zote ni transistors na ni msingi wa simu. Mada hii ni kwa Lugha ya Kiingereza; naomba tujifunze pamoja.

"The semiconductor industry has been growing at a rapid pace over the past few years, and it shows no signs of slowing down. Semiconductors, also known as chips, are an essential component in electronic devices such as smartphones, computers, and cars. As the demand for these devices continues to rise, so does the demand for semiconductors. The top semiconductor chip manufacturers in the world are responsible for producing the majority of these chips. These companies are known for their cutting-edge technology and innovative designs, which have helped them become leaders in the industry.

IMG_20240503_235736.jpg


The competition among these companies is fierce, and each one is constantly striving to improve their products and stay ahead of the game. In this post, we will take a closer look at the top semiconductor chip manufacturers in the world and explore what makes them stand out from the rest.

We will examine their history, products, and market share, and provide insights into their future plans. Whether you are an investor looking to make informed decisions or simply interested in the latest technology, this post will provide valuable information about the semiconductor industry and its top players.

Global Semiconductor Industry Overview
The semiconductor industry is an essential part of modern technology, powering everything from smartphones and computers to cars and medical devices. The global semiconductor market has been growing steadily over the past few years, with a market size of USD 527.88 billion in 2021, projected to reach USD 1,380.79 billion in 2029, exhibiting a CAGR of 12.2% during the forecast period.

Market Dynamics
The semiconductor industry is highly cyclical and has a significant impact on the global economy. The industry has experienced several boom-and-bust cycles, with periods of rapid growth followed by sharp downturns.

The market dynamics of the semiconductor industry are influenced by several factors such as supply and demand, technological advancements, geopolitical tensions, and economic conditions.

Key Growth Drivers
The growth of the semiconductor industry is driven by several factors, including the increasing demand for electronic devices, the rise of the Internet of Things (IoT), the growing adoption of artificial intelligence (AI), and the increasing demand for electric vehicles (EVs)

The largest semiconductor companies in the world include Taiwan Semiconductor Manufacturing Co. Ltd. (TSMC), Intel Corporation, Qualcomm Incorporated, SK hynix Inc., Micron Technology, Inc., Nvidia Corporation, Broadcom Inc., AMD, Inc., Texas Instruments Incorporated, and MediaTek Inc.

These companies have a significant market cap and are responsible for a large percentage of global semiconductor production.

In conclusion, the global semiconductor industry is a vital part of modern technology and has a significant impact on the global economy."
(Source: Piyush Gupta, Digital Marketing)
 
Back
Top Bottom