UZUSHI Ulaji wa Ugali husababisha udumavu wa akili

Baada ya tathmini, tumebaini kuwa taarifa hii ni ya uzushi
Kumekuwepo na madai kuwa ulaji wa ugali hudumaza akili. Madai haya yana ukweli kiasi gani?

02692B18-05FE-4851-857F-7A5DA6E174CD.jpeg
 
Tunachokijua
Ugali ni chakula kinachotumika sana Kusini mwa Jangwa la Sahara. Kwa mujibu wa utafiti wa Onu Okpa et al (2019), “Sub-Saharan African Maize-Based Foods - Processing Practices, Challenges and Opportunities” mahindi huchangia 30% ya nishati za vyakula wanavyotumia watu wa ukanda huu kila siku.

Kwa mujibu wa utafiti huu, kila mtu anayepatikana Kusini mwa Jangwa la Sahara hutumia wastani wa kati ya gramu 52-450 za mahindi kwa siku. Ni chanzo kikuu cha ugali unaotumika kila siku kwenye nchi hizi. Kwa Tanzania, 64% ya wananchi wake hula chakula hiki walau mara 5-7 kwa wiki.

Takwimu hizi zinaonesha kuwa ugali ni chakula kinachotumika sana, pengine kuliko aina nyingine za vyakula. Baadhi ya watu huutengeneza kwa kutumia unga wa mhogo, mtama, ulezi pamoja na aina zingine za nafaka.

Bila kujali tofauti ndogo za mgawanyiko wa virutubisho, nafaka zote husifika kwa kuwa na kiasi kikubwa cha nishati na wanga, pia kiasi kidogo cha madini na vitamini muhimu kwa afya.

Kuhusishwa na udumavu wa akili
Kitaalamu, udumavu wa akili husababishwa mambo mengi ikiwemo baadhi ya changamoto za kijenetiki mfano Down’s syndrome, kukosa hewa ya kutosha wakati wa kuzaliwa, maambukizi makali ya homa ya uti wa mgongo, utapiamlo, matumizi ya baadhi ya madawa na pombe wakati wa ujauzito pamoja na sababu zingine siziso wazi sana.

Kwa kurejea mgawanyiko wa virutubusho vinavyopatikana kwenye nafaka zinazotumika kutengenezea ugali, hakuna uhusiano wa moja kwa moja unaoweza kutajwa, au pia kuhusishwa na kusababisha udumavu wa akili kwa watu. Virutubisho na madini yake havina athari hasi kwenye afya ya ubongo.

Pia, JamiiForums imezungumza na wataalamu wa lishe ambao wamethibitisha kuwa chakula hiki ni salama, hakiwezi kusababisha madhara tajwa.

Hivyo, JamiiForums imebaini kuwa madai haya hayana ukweli uliojengwa kwa hoja za kisayansi. Ni uzushi usio na uthibitisho wa tafiti au takwimu.
Nakazia ✍️✍️✍️

Wanaosema ugali unaleta udumavu wa akili walete hapa ushahidi wa kisayansi
Ushadi si wananchi wako?
Jilinganishe wewe unayelalia dhahabu, almasi na Tanzanite ;unapanda ndege kwenda Ulaya na America kuomba msaada wa hela kwa walipakodi ambapo wao wana udongo usio na rutuba, :

Wewe Una-mashamba na mapori na maji yanaingia baharini alafu unaagiza chakula jangwani Israeli;

UNATAKA UDUMAE mara ya ngapi?
 
Mi chakula changu ni ugali napenda sana. Sisi wairaq Ugali ndiyo chakula kikubwa. Wanangu wa Dar, Moro 🤣 mnapenda sana Ubwecheeee kuleni Ugali tena Ugali wa Dona not sembe
 
Ushadi si wananchi wako?
Jilinganishe wewe unayelalia dhahabu, almasi na Tanzanite ;unapanda ndege kwenda Ulaya na America kuomba msaada wa hela kwa walipakodi ambapo wao wana udongo usio na rutuba, :
Wewe Una-mashamba na mapori na maji yanaingia baharini alafu unaagiza chakula jangwani Israeli;

UNATAKA UDUMAE mara ya ngapi?
Kuna tofauti kati ya kutokuwa na akili na kutotumia akili..
We umejadili hilo la mwisho ambalo ni nje ya mada!
 
Nakazia ✍️✍️✍️

Wanaosema ugali unaleta udumavu wa akili walete hapa ushahidi wa kisayansi
Madai yao, au niseme, ujumbe wao unalenga kuwadumaza Watanzania kisaikolojia. Ndiyo kusema, Mtanzania akikataa chakula chake, yeye amekataa mila zake, mila zake na mustakabali wake wa kitamaduni, wa Nchi!

Athari zake ni kubwa, it is self destrucive? na ni kufungua milango ya utamaduni na mila za wageni kupenya kupitia akili na nafsi za watu na hatimaye kuharibu jamii Nzima.....ndio ukoloni mamboleo huo jamani. Viongozi ni kioo cha Jamii nzima, na wanaporuka/wanapokurupuka na kutoa kauli zinazokinzana, inaleta taharuki juu ya Jamii nzima-wale wasiotupenda huwa wanachukua maneno hayo na kuyapa silaha kauli na maneno yao ili kunyanyasa jamii yetu.

Kiongozi akitamka maneno ya kudhalilisha anapaswa kuwajibishwa. Wanapaswa kupunguzwa/kuminywa ulimi saa nyingine kabla hawajatoa matamshi na kauli wanazotoa hadharani.
 
Aione Godbless Lema aliyeingia nchini Tanzania kutoka Canada hivi majuzi!
Lema ni mtu anayejielewa. Anajua anachokifanya, yaani ana makusdi yake.

Walakin

The question is, ni yake au ame mezeshwa bila yeye kujua? na kutathmini madhara yake. i.e The implications
 
Nchi za Watu waliogundua mambo mengi hawali Sana Ugali wa mahindi
Nchi za Watu walioendelea hawakuacha na kutelekeza desturi na mila zao. Japan, Singapore, India Germany just to name a few hawakukubali kuacha mila na desturi zao ili kupisha 'Ubepari' kwani, Ubepari hauna mila au desturi.

Ni wachagizaji wake ndio wenye kudai, kwamba, kuhamisha hiyo, inabidi wahamishe mila na desturi zao kwetu. Mfano Waingereza ambao ndi wadhalimu wakubwa.

Haijalishi. Ugali unalika na wala sio Umasikini kama tunavyo anza kuaminishwa.
 
Kuna watu ambao wanaamini kuwa maendeleo yanaletwa na watu wa nje katika jamii yetu. Wanaamini Ugali, katika kesi hii, ambayo inatokana na mahindi ambayo katika jamii zao hutumika kulisha mifugo (nina shaka) kama mlo wa chini sana.

Na hivyo haufai kama lishe kwa Binadamu Halafu kudai wanyama wapewe haki kama haki za binadamu.....huku nyuma wakiamka kila siku kututukana na kutuita kila aina ya wanyama, tena katili....eboo Shienzztaipuz Kuweni makini na watu kama hao.

Ugali unalika na katika masaa machache nautandika kama daku....mi nimsindikizaji
 
Issue hapa sio ugali ila mlo kamili.
Watanzania wengi hatuli vyakula rafiki kwa ubongo kama vile samaki ili tupate Omega 3, mboga za majani zenye ukijani mwingi(green pigment).
Ugali haupunguzi akili,lakini kama hausindikizwi na kitoweo cha ziada na chenye kuupa ubongo nguvu inakuwa changamoto.

Ugali+samaki+mbogamboga+tunda inatosha kabisa, lakini huo ugali ratio yake isiwe kuuuubwaaa na vitoweo na matunda yakawa kidooogooo
 
Lema ni mtu anayejielewa. Anajua anachokifanya, yaani ana makusdi yake.

Walakin

The question is, ni yake au ame mezeshwa bila yeye kujua? na kutathmini madhara yake. i.e The implications
Mixologist ni Mzushi.
 
3 Reactions
Reply
Back
Top Bottom