Ukweli wa magari kuhusiana na kasumba kwamba kuna gari mbovu au ina makosa

geranteeh

JF-Expert Member
May 21, 2015
266
619
Za siku wakubwa. Leo naomba niwaletee uzi ambao asili yake ni kutoka kwenye group letu la whatsapp la ISAL Motors juu ya malalamiko kwamba kuna gari fulani ni bora kuliko ingine kwamaana ya kudumu na kutokusumbua. Naomba niwaambie kitu kimoja trust me hakuna gari mbaya bali huwa tunajiuliza tunanunua magari kwa sababu zipi waafrika na wazungu tofauti yetu ndo iko hapa.

Wengi wananunua gari sababu eti ina mwonekano mzuri yaani unamkuta mtu anakwambia yani mi gari fulani naipenda tu yani hata nikiwa vipi ntakuja tu kuinunua. Mwingine labda sababu kuna wenzake wengi wanazo mfano vijana wa mjini kuna kipindi huwaambii kitu kuhusiana na Alteza wakazinunua kama njugu baadae upepo ukabadilika ukaamia kwenye crown lakin nakumbuka wakati tunakua kulikua kuna kipindi cha chaser sijui baloon ikaja mark two yan kuna mtu ananunua gari sababu tu its on trending. Alaf kuna mtu ananunua gari fulani sababu tu ataonekana mtu wa hadhi fulani wazungu wanaita for prestige kama sikosei yani ile sifa tu kwamba fulani anamiliki gar fulani kali sana.

Trust me yani kama unanunua gari kwa sababu yoyote kati ya hizo nikizozitaja hapo juu andika wewe utakua ni mtu wa kulia kila siku unless uko na pesa ndefu ambayo si ya mawazo. Yes kuna mwanangu (sitomtaja jina) aliwahi pata ajali pale maeneo ya dar free market ni ajali ambayo wengi watakuwa wanaikumbuka. Yeye alikua na subaru WRX alimgonga mwamba alikuwa na crown kama sikosei. Siwezi elezea hii ajali lakini ile subaru ya jamaa yangu ilipasuka rejeta kioo kilikua na ufa pia alivunja taa na rim ilipinda ya tairi ya mbele moja. Huwez amini jamaa aliagiza WRX mpya afu fresh kabisa coz ni chizi subaru. Mtu kama huyo mwanangu naomba ni mu exclude maana huwez mkuta akikaa akilalamika kwamba labda prado zinachomokaga tyre au zina ubovu fulani ambao hautibiki.

Nishawahi sikia sana watu wakilalamikia nissan x trail na kuna mzee anayo namba b mpaka leo anapeta nayo na hana presha nkimuuliza ananiambia ina shida za kawaida tu kama changamoto nyingine kwenye magari mengine ambazo zinatatulika. Kiufupi wabongo alieturoga ni mtu mmoja maana huwa hatuna sana udadisi wa mambo. Hizi nissan tunazozilalamikia kila siku kwamba gari mbovu sijui nini ndo gari zilizojazana Nairobi na wanaishi nazo vema kama tunavoishi na toyota hapa Tz sasa ushawahi jiuliza shida iko wapi? Nadhani kuna picha mpaka hapo umeipata akilini mwako wakati nakuleta kwenye mada halisi.

Yani bila kupepesa macho niseme tu wabongo huwa hatujui ni nini tunataka kwa wakati gani na kwa matumizi gani. Yani ukishajua haya. Yote basi hutokaa ukalalamika kuhusiana na gari yoyote utakayoimiliki katika maisha yako. Mimi naamini hakuna gari mbovu au yenye shida fulani kwani zimepita na kukaguliwa vitu vingi sana mpaka kufikia wewe unaendesha hiyo gari. Kuna uzi fulani niliusoma twitter jamaa alisema point kubwa sana ingawa sitoielezea kwa mtiririko aliouongea ila ntaielezea kwa namna nilivoelewa kwamba unamiliki ngamia umeishi nae sana ila baadae ukaja kumiliki farasi lakini matunzo yake unayompa ni kama yale ya ngamia mfano ngamia anatoboa wiki hanywi maji wala chakula alaf umekuja kumiliki farasi unaenda nae kama ulivokua unaishi na ngamia trust me broh utasema hawa wanyama ni legelege sana wala si wastahimilivu. Point yangu hapo igeuze kwenye gari mfano unamiliki starlet zile za zamani alaf ukaja kumiliki crown alaf utunzaji wake unaendelea na mazoea ya starlet trust me utaishia kusema hizi gari ni mbovu zina shida fulani fulani na fulani kumbe ni ww tu.

Kuna hii kasumba imekuja kwamba hizi Nissan dualis huwa zinaungua sana sasa ndugu yangu uliponunua corola yako limited ukaenda kwa fundi mtaani akakuwekea mziki taa kali sijui ukaweka na makolokolo kibao alaf maisha yalaemsa ukaona dualis watu wengi wanazo au ukapenda ilivo basi ukajaaliwa ukainunua then ukarudi kwa yule fundi wako ukamwambia "Nifanyie kama ulivofanya kwenye corola kipindi naiununua maana nilifaidi sana mziki na taa nlikua naona vema" alafu ikaja kuungua hiyo dualis kweli utalalamika kwamba gari ni mbovu zinaungua? come on ndugu zangu hakuna kitu ka hiko.

Hivi ni wangapi ambao gari aliyoinunua aliifanyia tafiti au aliisoma kabla ya kuimiliki au hata baada ya kuinunua alitumia muda kusoma kile kipeperushi cha maelezo na maelekezo ya gari? Kiufupi kama huijui gari yako na unaishi nayo basi shukuru Mungu kwa kukulinda kipindi chote ulichokuwa nayo. Si kwamba nawananga wakuu wangu bali ni katika kupeana elimu tu ili mwisho wa siku wote tuwe safe alaf baada ya hapo ndo tuseme ni mipango ya Mungu lakini si sasa kipindi tunafanya uzembe.

JE NI KWELI KWAMBA KUNA GARI ZINA SHIDA?
Kiufupi mimi huwa siamini katika hili bali nachoamini ni kwamba kila gari imetengenezwa kwa mazingira fulani ambayo ukiyatumia abadani hutokuja kuwa mlalamishi . Kiufupi ni kwamba pindi unapotaka kununua gari kikubwa angalia vitu viwili kwanza angalia mfuko wako utaweza kuhudumia gari hiyo? Mfano mzuri ni hizi gari ambazo ni tofauti na toyota mfano Mazda, Isuzu, Honda, Nissan, BMW, FORD nk kwa hapa Bongo huwa vifaa vyake bei ziko juu sasa jiulize nitakapomiliki gari hii ntaweza kuhudumia kwenye upande wa service? Matokeo yake ndo pale unapoimiliki alaf kwenye service unanunua vifaa ambavyo havina ubora kisa tu ni bei rahisi kwakweli kama ni shock up mjomba basi kila baada ya miezi mitano utakuwa unafunga mpya then mwisho wa siku utalalamika bwana hizi gari ugonjwa wake ni shockup maana kila siku nanunua mpya je ni original? Kuna mwingine atakwambia gari fulani ugonjwa wake ni engine zake zinakufa sana je mnatumia Recommended engine fluid au ndo unaenda dukan unaagiza tu. Nadhani point yangu imeeleweka hapo kikubwa kabla ya kununua jiulize utaweza kuimudu? Trust me guys kama gari ukifunga parts genuine au service ukafanya vile inavotakiwa basi watu wakipiga story za vijiweni we utakua unacheka tu na kutabasamu.

Pili angalia pindi unapotaka kununua gari angalia matumizi yako ni yepi je hilo gari litaweza kuhimili mikiki mikiki ya ruti zako? Mfano mtu anamiliki crown afu ruti zake kuiona lami ni kipengele yani yeye ni kupiga shimo mwanzo mwenga broh unachokitafuta utakipata. Kuna gari zimetengenezwa kwaajili ya mikiki mikiki ya off roads na kuna gari zimetengenezwa ni very luxurious yani. Mfano mzuri wengi huwa wanapenda kununua magari kwa wahindi sababu muhindi gari anaendeshea mjini tu yan gari inaweza ikakaa wiki nzima isigonge shimo yani ni palepale city center na ukimkuta mhindi ana gari ya offroad basi anapigaga shimo kwelikweli na wenzetu ni vile tu wengi wana uwezo unakuta ana gari mbili moja ya mjini ingine ni ya safari za kashkash sasa kama umejiona wewe ni mtu wa mazingira ya lami inataftwa kwa tochi au kila siku ni lazma njia yako upige shimo basi fanya maamuzi sahihi kabla hujaanza kulalamika. Na nafurahi kuona sikuhizi wauzaji au waagizaji wa magari huwa wana andaa threads mbalimbali za kuelezea magari na kutoa ushauri wa matumizi yake ni vile tu wabongo wengi sisi ni wavivu kusoma.

Mwisho naomba nielezee kuhusiana na hii kasumba ya spea. Watu wengi huwa wanalalamika Sana kuhusiana na kupatikana kwa spea original za magari. Wakuu dunia sasa ni kijiji hakuna spea ambayo haipatikan ni swala la pesa yako tu but zinapatikana vema kabisa. Binafsi mtu akinitafta na kuulizia spea hata kama inaonekana mpya kabisaa mimi namwambia ni mtumba na kama ni mpya namwambia ni mpya chaguo liwe lakwake but kununua spea mtumba ni safe zaidi kuliko og ambayo huna uhakika nayo kwamba ni kweli og. Now days watu wanakuletea mzigo wenyewe kabisa na wanakwambia ni mpya yenyewe baada ya simu kadhaa unalia. Uzuri wa spea mtumba huwa ni Original ambayo inakuwa imetoka kwenyw gari kama yakwako kwamaana imetengenezwa kiwandani so its pure og ni vile tu inakuwa imetumika kwa muda fulani nisingependa kuelezea sana nisije badilisha mada kuwa bango la biashara lakini naamini wakuu wangu mmepata darasa fulani na madini kadhaa kama kuna kasoro unaweza ongezea kwani namimi naendelea kujifunza na hakuna kitu napenda kama kujifunza. Kwa leo naomba tuishie hapo mpaka wakati mwingine.




IMG_20230124_120849_827.jpg
 
Gari zinapishana ubora.. Hata kwenye bei unaona..
Gari zenye makosa zipo..
Watengenezaji nao wanakosea.. Na kuna muda huwa wanarudisha kiwandani kwa maboresho..

Kuna gari hata uitunze vipi itasumbua tuu..!

Cha msingi ni hicho ulichosema uifanyie tafiti gari yako.. Then utajua unaishi nayo vipi..!
Kama wanandoa wanavyoishi na mapungufu ya wenzao baada ya kuwasoma..!
 
Gari zinapishana ubora.. Hata kwenye bei unaona..
Gari zenye makosa zipo...
Boss makosa yanatokana na matumizi yako hiko ndicho ninachoamini ndo maana nikakupa mfano wa crown uwe unapiga nayo sana shimo lazma uone weakness yake kwenye shockups au kuna gari hazitaki mafuta ya kidebe endapo itakua ndo tabia yako basi kila miezi utabadilisha pump so tabia yako ndiyo inayo onesha udhaifu wa hiyo gari and in fact hakuna gari isiyo na weakness ila matumizi yako ndo yataenda kuonesha ile weakness ambayo sometimes inaepukika vema
 
Ila wabongo kwenye ishu za magari bado tunapenda kuigana Sana ndiyo maana tukiona MTU anamiliki gari tofauti na Toyota huwa tunampa pole bila kujua undani wa gari yenyewe.

Angalau miaka ya hivi karibuni watanzania wameanza kutumia magari tofauti na Toyota Kwa mfano Subaru forester na BMW 320i zipo nyingi Sana mtaani
 
Ila wabongo kwenye ishu za magari bado tunapenda kuigana Sana ndiyo maana tukiona MTU anamiliki gari tofauti na Toyota huwa tunampa pole bila kujua undani WA gari yenyewe.
Angalau miaka ya hivi karibuni watanzania wameanza kutumia magari tofauti na Toyota Kwa mfano Subaru forester na BMW 320i zipo nyingi Sana mtaani
Sure kaka hiki ndo kinachotuua wengi yani mtu anaenda kununua gari sababu fulani anayo ila wengi hawajui kumiliki gari si ishu ishu ni kuiendesha sasa hapa kwenye kuiendesha ndo vitu vingi vinaeingia ikiwemo kuihudumia ndo maana watu wanafeli. Yani mtu akiwa na passo wana wanakucheka akati ndo matumizi yangu yanahitaji hiyo gari
 
Boss makosa yanatokana na matumizi yako hiko ndicho ninachoamini ndo maana nikakupa mfano wa crown uwe unapiga nayo sana shimo lazma uone weakness yake kwenye shockups au kuna gari hazitaki mafuta ya kidebe endapo itakua ndo tabia yako basi kila miezi utabadilisha pump so tabia yako ndiyo inayo onesha udhaifu wa hiyo gari and in fact hakuna gari isiyo na weakness ila matumizi yako ndo yataenda kuonesha ile weakness ambayo sometimes inaepukika vema
Aisee fanya kufuatilia BMW M60 engine na ishu ya Nikasil..!
 
Aisee fanya kufuatilia BMW M60 engine na ishu ya Nikasil..!
BMW M60 Nikasil Damage

This issue is mostly a thing of the past. However, there could be a few M60 engines still out there that went under the radar and weren't fixed. Early M60 cylinder liners are made from Nikasil, which is a combination of aluminum, nickel, and silicone. Unfortunately, that did not work out well for the United States and United Kingdom markets where fuels were high in sulfur at the time.

High sulfur fuels reacted poorly with the Nikasil causing damage to the M60 cylinder bores. This in turn leads to a loss of compression and a total loss of the engine. BMW offered an extended warranty of 6 years and 100,000 miles for internal parts, and the blocks were eventually changed to Alusil instead of Nikasil. The US and UK markets also began lowering sulfur content of fuels.


Jibu umelipata mkuu au nikusaidie kwa ishu ya BMW Nikasil?
 
BMW M60 Nikasil Damage

This issue is mostly a thing of the past. However, there could be a few M60 engines still out there that went under the radar and weren't fixed. Early M60 cylinder liners are made from Nikasil, which is a combination of aluminum, nickel, and silicone. Unfortunately, that did not work out well for the United States and United Kingdom markets where fuels were high in sulfur at the time.

High sulfur fuels reacted poorly with the Nikasil causing damage to the M60 cylinder bores. This in turn leads to a loss of compression and a total loss of the engine. BMW offered an extended warranty of 6 years and 100,000 miles for internal parts, and the blocks were eventually changed to Alusil instead of Nikasil. The US and UK markets also began lowering sulfur content of fuels.


Jibu umelipata mkuu au nikusaidie kwa ishu ya BMW Nikasil?
Naomba msaada..!
 
Naomba msaada..!
Early M60 cylinder liners are made from Nikasil, which is a combination of aluminum, nickel, and silicone. Unfortunately, that did not work out well for the United States and United Kingdom markets where fuels were high in sulfur at the time.

Cylinder liners za M60 za mwanzoni i mean toleo la kwanza kabisa ziliundwa kwa Nikasil ambayo ni muunganiko wa aluminum,nickel na silicone ambazo kiufupi hazipatani na mafuta ambayo yana viambata vya sulfur. Viambata ambavyo vimechanganywa kwenye mafuta ya baadhi ya nchi mfano UK na USA.

Sulfur nyingi kwenye mafuta reaction yake inakua mbaya kwa Nikasil na kusababisha M60 cylinder kuharibika mwisho kupelekea engine kuharibika.

By the way Bmw ilikuja na mpango wa kutoa warranty ya miaka sita gari yako ikipata hilo tatizo unapeleka inaenda kubadilishwa kutoka Nikasil na kuwekwa Alusil.

Point inarudi kwamba unaponunua gari hivi vyote unatakiwa uvijue kwa maana mafuta yetu yana viambata gani sababu kwa nchi ambazo hazikuwa na viambata vya sulfur kwa wingi kwenye mafuta hawakupata hilo tatizo.

Kingine ni kwamba sisi huwa tunanunua gari second hand so gari nyingi mfano hzo bmw kama ni kuja bongo ni baada ya miaka kumi kwenda mbele so magari mengi yaliyoagizwa either yalisharekebishwa hilo tatizo au hayakutoka kwenye nchi zenye matumizi ya kiambata cha sulfur kwa wingi.

Si kama natetea point mkuu upo huru kunirekebisha lakini gari zetu nyingi unakuta ya 2008 leo unaambiwa ndo new model so hili tatizo kama umenunua BMW M60 obviously utakua ushasoma ni nn inataka na namna gani ya kuepukana na hilo tatzo but kwa Tanzania kwa ninachojua mimi mafuta yake yana low sulfur
 
Early M60 cylinder liners are made from Nikasil, which is a combination of aluminum, nickel, and silicone. Unfortunately, that did not work out well for the United States and United Kingdom markets where fuels were high in sulfur at the time...
Aisee sio kila mtu ananunua mtumba.

M60 imetoka watu wakanunua.. Then engine zinafail.

Mafuta yalikuwepo kabla ya M60 kutengenezewa.. Walitakiwa wajue hiyo reaction kabla.

BMW akakubali kosa.. Ndio recall na warranty extension.

Hapa teyari unaona kuwa kuna vitu vibovu vinatoka kiwandani.

2008 haiwezi kuwa new model?

Fanya kufuatilia new model ya Toyota Celica ni ya mwaka gani..!!
 
Aisee sio kila mtu ananunua mtumba.

M60 imetoka watu wakanunua.. Then engine zinafail.

Mafuta yalikuwepo kabla ya M60 kutengenezewa.. Walitakiwa wajue hiyo reaction kabla.

BMW akakubali kosa.. Ndio recall na warranty extension.

Hapa teyari unaona kuwa kuna vitu vibovu vinatoka kiwandani.

2008 haiwezi kuwa new model?

Fanya kufuatilia new model ya Toyota Celica ni ya mwaka gani..!!
Ni wangapi wamanunua zero km mkuu kwa bongo katika asilimia 100%


2008 mkuu unaiita gari new model? Kweli? Huu mwaka 2023

Huwa tunaita new model kwasababu unakuta toleo la mwanzo may be 2005 sasa obviously ya 2008 lazma uiite ni new model sababu ni toleo la juu yake lakini kiu halisia zote ni old model mfano bongo harrier tako la nyani watu wanaita ni new model lakini ni gari ya 2008. Ila kumbuka harrier ya mwisho ni ya 2022 kama sikosei
 
Aisee sio kila mtu ananunua mtumba.

M60 imetoka watu wakanunua.. Then engine zinafail.

Mafuta yalikuwepo kabla ya M60 kutengenezewa.. Walitakiwa wajue hiyo reaction kabla.

BMW akakubali kosa.. Ndio recall na warranty extension.

Hapa teyari unaona kuwa kuna vitu vibovu vinatoka kiwandani.

2008 haiwezi kuwa new model?

Fanya kufuatilia new model ya Toyota Celica ni ya mwaka gani..!!
Alaf kumbuka hiko kiambata cha sulfur si kwa nchi zote boss na unavotengeneza gari kuna mazingira itakubali na kuna mazingira haitakubali so ni jukumu la mnunuzi kujua hii gari inafaa kwa mazingira yangu au laa... Muuzaji yeye atauza tu hawezi sema kwamba watu wa uk siwauzii na alichofanya bmw kutoa guarantee ni kutoku haribu brand lakini kuna nchi hizo gari zili fiti na watu wakaishi nazo vema lakini mwisho wa siku hiko kiambata kimepunguzwa kwa kiasi kikubwa kama si kujaribu kuondoa katika baadhi ya nchi
 
Ni wangapi wamanunua zero km mkuu kwa bongo katika asilimia 100%


2008 mkuu unaiita gari new model? Kweli? Huu mwaka 2023

Huwa tunaita new model kwasababu unakuta toleo la mwanzo may be 2005 sasa obviously ya 2008 lazma uiite ni new model sababu ni toleo la juu yake lakini kiu halisia zote ni old model mfano bongo harrier tako la nyani watu wanaita ni new model lakini ni gari ya 2008. Ila kumbuka harrier ya mwisho ni ya 2022 kama sikosei
Achana na wanunuzi wa Bongo.. Tunaongelea ubovu wa kitu..
Hao ni brand kubwa BMW..
Imagine maboko wanayotoa Toyota halafu wanajikausha..!!

Bado hujafanya homework yako vizuri..
Leo2023..ukinunua LC Prado 150 ya 2010..umenunua Prado new model au old model..!!?
 
Alaf kumbuka hiko kiambata cha sulfur si kwa nchi zote boss na unavotengeneza gari kuna mazingira itakubali na kuna mazingira haitakubali so ni jukumu la mnunuzi kujua hii gari inafaa kwa mazingira yangu au laa... Muuzaji yeye atauza tu hawezi sema kwamba watu wa uk siwauzii na alichofanya bmw kutoa guarantee ni kutoku haribu brand lakini kuna nchi hizo gari zili fiti na watu wakaishi nazo vema lakini mwisho wa siku hiko kiambata kimepunguzwa kwa kiasi kikubwa kama si kujaribu kuondoa katika baadhi ya nchi
Kwahiyo hao walionunua BMW US na UK wali import kutoka Europe au Japan..!!!?
Gari zimenunuliwa kwa dealers wa nchi hiyo hiyo.. Huo uchunguzi alitakiwa afanye dealer au mnunuzi..!!?
 
Achana na wanunuzi wa Bongo.. Tunaongelea ubovu wa kitu..
Hao ni brand kubwa BMW..
Imagine maboko wanayotoa Toyota halafu wanajikausha..!!

Bado hujafanya homework yako vizuri..
Leo2023..ukinunua LC Prado 150 ya 2010..umenunua Prado new model au old model..!!?
Mkuu maboko kama yepi? Mkuu mimi naamini kwamba mazingira utakayotumia hiyo gari ndo yataifanya hiyo gari tatizo fulani liwe common

Okay naomba nkuulize swali. Ni wangapi huwa wanafanya uchunguzi wa kina wa gari kama wewe ulivoichambua BMW kabla ya kununua gari?
Ni wangapi huwa wanasoma manual instruction ya gari yake?

Alaf ishu ya prado as long as kuna latest model hiyo gari si new model boss ni tunaipa tu jina lakini si new model
 
Kwahiyo hao walionunua BMW US na UK wali import kutoka Europe au Japan..!!!?
Gari zimenunuliwa kwa dealers wa nchi hiyo hiyo.. Huo uchunguzi alitakiwa afanye dealer au mnunuzi..!!?
Kwa kesi hii ya uk broh you got a point na nakubaliana nawewe kwa asilimia mia uko sahihi.

Lakini kwa mazingira yetu ya kibongo ni big No kwasababu ukiuliza walionunua hiyo gari zero km yani imetoka wakanunua unaweza kuta ni wachache ama hakuna
 
Kwanini X Trail ilalamikiwe sana kuliko spacio, pamoja na maelezo yako mazuri bado naamini kuna baadhi ya gari ni vimeo
Mkuu walionunua x trail wengi walinunua sababu ni gari ya juu na wengi matumizi yake wengi waliyatumia kama tunavotumia kwenye rav4 old model roho ya paka yan mazingira ya kashkash kitu ambacho ni tofauti. Mfano sasa ununue nissan dualis alaf matumizi yako yawe ya off roads ngingi nganga mjomba hiyo gari utaikataa. Kuna ile mentality kwamba gari ikishakuwa ya juu kidogo basi kuna mikiki mingi itahimili kitu ambacho si kweli. Kwa kesi ya x trail watu wengi walinunua bila kujua gari inataka nini. X trail haikutengenezwa kama gari ya kuhimili mikiki mikiki yani kama unataka gari ya juu ya kuhimili mikiki mikiki dizain ya x trail basi kachukue rav 4 old model.

Nakuhakikishia mkuu kuna watu wapo mjin na x trail wanakula maisha vyedi kabisa na hayo malalamiko hakuna
 
Back
Top Bottom