Ujio wa TARURA: Sasa Madiwani, Halmashauri zalalama!

Lole Gwakisa

JF-Expert Member
Nov 5, 2008
4,735
2,265
20171009_162216.jpg
TARURA, Tanzania Rural Roads Authority ni kitengo kama TANROADS kilichoanzishwa miezi michache iliyopita.

TARURA inachukua nafasi ya Mhandisi wa Wilaya/Halmashsuri katika kushughulikia barabara.

Kama kuna sehemu Madiwani na Halmashauri zimelalamikiwa kwa miaka mingi, kuingilia michakato ya Ujenzi , kuonba rushwa, kupendelea watu/makampuni kutata tenda basi ilikuwa katika Ujenzi wa barabara nchi nzima.

Wahandisi wa Hamlashauri waligueka kuwa vibarua wa Madiwani na kila siku ni vitisho vya kufukuzwa kazi wasipotii matakwa yao.

Wakandarasi wanaojiamini walisusa kabisa kufanya kazi za Halmashauri.

Ukifanya kazi malipo sharti kwa rushwa, mara hela zote zimeenda kwenye mbio za mwenge, mara kampeni ya madawati, au kampeni ya ujenzi maabara shuleni.

Hivyo basi leo nimecheka sana kuona kichwa cha naneni:

Mameya, wenyeviti walalamikia TARURA

Majira pg 10 leo 9 Oct. 2017.

Nampa heko Rais Magufuli, Madiwani walizoea kugawana kwenye vikao fedha za ujenzi wa barabara.
 
Huu utakuwa muarobaini wa utendaji mbovu wa idara iliyokuwa ya ujenzi katika Halmashauri zetu. Imagine Halmashauri ilikuwa inaletea milioni mia moja kwa ajili ya barabara . katika hizo unakuta kila Diwani anataka apate Mradi kwahiyo hela zinagawanywa milioni kumi kumi unategemea kuna barabara itatengenezeka hapo kweli?
Kuna vitu Magufuli anafanya vizuri na katika hili ni miongoni mwake.
 
Waambie walete na wakala wa maji vijijini, wamtoe huyu wakala wa umeme hana faida kwetu
 
Back
Top Bottom