Nyenyere
JF-Expert Member
- Sep 9, 2010
- 14,770
- 10,660
Wakuu, nawatakieni amani na furaha mioyoni mwenu. Leo nina mada fupi tu kwa wote ambayo naomba tujadili.
Katika mahusiano ya mapenzi, hasa kwenye ndoa, kuna tofauti kubwa sana kati ya nini atakacho mwanamume na nini atakacho mwanamke.
1. Kwako mwanamke- Elewa kwamba heshima (respect) pekee ndiyo inayomweka mwanamume kwenye nafasi yake. Mwanamume anaweza kuwa anapendwa na kila aina ya mwanamke hapa duniani lakini ni heshima ndiyo itamtofautisha mwanamke wa maisha kwa mwanamume wala sio upendo. Mwanamke hakupewa kupenda, hii ni fact, ndio maana kwa wanawake utu wa ndani sio muhimu kuliko mafanikio ya nje. Kila mwanamke angetamani aolewe na Bill Gates au SS Bhakresa, ila tu kutokana na nafasi finyu na ushindani.
Hii ni kwa sababu mwanamke hana uwezo wa hisia za mapenzi ambazo ziko wazi (clear) bali huwa zimechanganyika hovyo (vague). Kama uko kwenye ndoa ama unataka ndoa imara, ni vema ukajifunza kumheshimu huyo aliye karibu yako, kwani hiyo ndio aina pekee ya upendo kutoka kwa mwanamke ambayo kila mwanamume huutafuta. Heshima humaanisha mapenzi ya kweli.
2. Kwenu wanaume - Mwanamke anataka upendo. Kama ni heshima, mwanamume huwaheshimu wanawake wote, kuanzia makahaba mpaka masista. Huu ni wajibu wa kila mwanamume hali, kumheshimu mwanadamu mwenye jinsia ya kike. Ndio maana zamani zetu haikuingia akilini mwanamke amesimama kwenye usafiri wa umma halafu kuna dume limekalia kiti, huu ulikuwa ni ukatili wa kijinsia. Kwa hiyo kinachomtofautisha mwenzi wako na wanawake wengine ni jinsi unavyompenda. Kumbuka heshima ni kwa wanawake wote lakini upendo ni kwa mkeo pekee.
Tatizo vijana wa siku hizi wamevurugwa kweli kweli na upuuzi wa kimagharibi. Unakuta kwa vile mwanamume anataka kuheshimiwa, mwanamke naye anatilia heshima, tena kwa kuwa mwanamke ànataka upendo basi mwanamume naye analilia kupendwa na mkewe. Aina hii ya mahusiano huwa haina safari ndefu kwani kila mmoja ataishi kwa kuigiza ili kumridhisha mwenza wake, lakini ikitokea tofauti ndogo tu ukweli hujidhihirisha.
Ndiyo hapo utasikia kauli mfano, nimekuvumilia sana. Ukweli si kwamba kakuvumilia bali kavimilia kuigiza kama anakuheshimu ama anakupenda, bali tangu mwanzo haikuwa hivyo. Alifanya tu ili akupate, na sasa hajakuchoka kama anavyodai ila amechoka kuishi maisha yasiyo halisi ya kuigiza, sasa anakuonysha rangi yake halisi.
Kumbuka, upendo wa mke kwa mume ni kumheshimu na heshima ya mume kwa mke kumpenda. Vyote vitoke moyoni kwa dhati, hapo mtaishi.
Katika mahusiano ya mapenzi, hasa kwenye ndoa, kuna tofauti kubwa sana kati ya nini atakacho mwanamume na nini atakacho mwanamke.
1. Kwako mwanamke- Elewa kwamba heshima (respect) pekee ndiyo inayomweka mwanamume kwenye nafasi yake. Mwanamume anaweza kuwa anapendwa na kila aina ya mwanamke hapa duniani lakini ni heshima ndiyo itamtofautisha mwanamke wa maisha kwa mwanamume wala sio upendo. Mwanamke hakupewa kupenda, hii ni fact, ndio maana kwa wanawake utu wa ndani sio muhimu kuliko mafanikio ya nje. Kila mwanamke angetamani aolewe na Bill Gates au SS Bhakresa, ila tu kutokana na nafasi finyu na ushindani.
Hii ni kwa sababu mwanamke hana uwezo wa hisia za mapenzi ambazo ziko wazi (clear) bali huwa zimechanganyika hovyo (vague). Kama uko kwenye ndoa ama unataka ndoa imara, ni vema ukajifunza kumheshimu huyo aliye karibu yako, kwani hiyo ndio aina pekee ya upendo kutoka kwa mwanamke ambayo kila mwanamume huutafuta. Heshima humaanisha mapenzi ya kweli.
2. Kwenu wanaume - Mwanamke anataka upendo. Kama ni heshima, mwanamume huwaheshimu wanawake wote, kuanzia makahaba mpaka masista. Huu ni wajibu wa kila mwanamume hali, kumheshimu mwanadamu mwenye jinsia ya kike. Ndio maana zamani zetu haikuingia akilini mwanamke amesimama kwenye usafiri wa umma halafu kuna dume limekalia kiti, huu ulikuwa ni ukatili wa kijinsia. Kwa hiyo kinachomtofautisha mwenzi wako na wanawake wengine ni jinsi unavyompenda. Kumbuka heshima ni kwa wanawake wote lakini upendo ni kwa mkeo pekee.
Tatizo vijana wa siku hizi wamevurugwa kweli kweli na upuuzi wa kimagharibi. Unakuta kwa vile mwanamume anataka kuheshimiwa, mwanamke naye anatilia heshima, tena kwa kuwa mwanamke ànataka upendo basi mwanamume naye analilia kupendwa na mkewe. Aina hii ya mahusiano huwa haina safari ndefu kwani kila mmoja ataishi kwa kuigiza ili kumridhisha mwenza wake, lakini ikitokea tofauti ndogo tu ukweli hujidhihirisha.
Ndiyo hapo utasikia kauli mfano, nimekuvumilia sana. Ukweli si kwamba kakuvumilia bali kavimilia kuigiza kama anakuheshimu ama anakupenda, bali tangu mwanzo haikuwa hivyo. Alifanya tu ili akupate, na sasa hajakuchoka kama anavyodai ila amechoka kuishi maisha yasiyo halisi ya kuigiza, sasa anakuonysha rangi yake halisi.
Kumbuka, upendo wa mke kwa mume ni kumheshimu na heshima ya mume kwa mke kumpenda. Vyote vitoke moyoni kwa dhati, hapo mtaishi.