FEBIANI BABUYA
JF-Expert Member
- Mar 5, 2022
- 1,098
- 2,012
- Thread starter
- #81
Mkuu hakika unaweza
Mkuu hakika unaweza
Nakubali kiongozi. Upo makini sanaHADITHI: JIJI LA KAMARI (GAMBLING CITY)
MTUNZI: FEBIANI BABUYA
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
WHATSAPP: 0621567672
AGE: 18+
Episode 34
“Kazi imefikia wapi?”
“Sumu tayari ipo ya kutosha na ishapakiwa tayari”
“Inafanya kazi kama tulivyo kubaliana?”
“Ndiyo kiongozi” mwanasayansi mkuu alikuwa anajibu kwa hofu sana.
“Unajua kabisa kama ukiniletea uhuni ni kitu gani nitakifanya kwa familia yako”
“Ndiyo ndiyo naelewa ndiyo maana nipo makini sana na kazi”
“Huwa siwezi kumuamini mtu kwa maneno tu”
“Unamaanisha nini?”
“Tunatakiwa kupata mtu wa kuweza kuijaribu”
“Unataka niwaue watu ambao hawana hatia kwa sumu?”
“Kwani wewe unahisi hiyo sumu inatumika kwenye nini? Na hao watu ambao hawana hatia kwahiyo familia yako ina hatia?”
“Nitafanya hivyo” mwanasayansi huyo aliongea kinyonge sana huku akimimina chai na kuweka tone moja tu la sumu ambayo ilikuwa kwenye kichupa kidogo kwnye mikono yake kisha akamuita mwanasayansi mmoja na kumpa ile chai ambapo mwanaume huyo alikuwa na wasiwasi sana lakini aliambiwa anywe.
Hakuwa na namna zaidi ya kufanya hivyo, baada ya kuinywa chai hiyo alianza kutetemeka, damu ikaanza kumtoka puani na masikioni na hakuchukua hata muda akaanza kukakamaa na kuakuka kabisa.
“Safi sana, wateja wetu wa nje wanaihitaji haraka sana. Ni sumu ambayo inauzwa bei ghali mno kwahiyo nina imani kwamba itatupatia mabilioni ya fedha, kazi nzuri dokta” alimpiga piga mgongoni na kutoka humo ndani dokta akiwa anakaa chini na kusikitika sana maana mambo ambayo yalikuwa yanaendelea yalikuwa yamevuka kwenye ubinadamu wa kawaida.
Wakati watu wanalalamika kwa baridi kali ambayo ilikuwa inaendelea ndani ya jiji la Dar es salaam kwa sababu ya hali ya mvua ambayo ilikuwepo, ilikuwa ni tofauti kabisa kwa watu wawili, watu ambao miili yao ilikuwa sehemu ya kuwapa burudani ambayo huenda watu wengi sana walikuwa wameikosa kabisa kwenye maisha yao. Max na Brandina walikuwa wanavinyoosha viungo vyao kitandani huku kila mmoja wao akiwa anamsifia mwenzake kwa namna alivyokuwa anajua kukitumia kiungo chake kuweza kumnyooshea mwenzake viungo vyake.
Mapenzi yao yalikuwa ya muda mfupi sana lakini walijikuta wanaanza kuaminiana kiasi kwamba mara nyingi walianza kulala pamoja na kazini wangewahi pamoja kisha wangeachana pamoja kwa sababu ilikuwa ni hatari sana kama wangejulikana kwamba walikuwa wamezama kwenye mapenzi kutokana na asili ya kazi yao hawakuwa wanatakiwa kabisa kuingia kwenye mapenzi kwa namna yoyote ile hata kwa bahati mbaya tu.
Mwanaume baada ya kutoka kitandani akiwa uchi, alikaa kwenye sofa ambalo lilikuwa karibu na kitanda huku akiwa anamwangalia mrembo Brandina naye akiwa uchi kabisa kwenye mwili wake. Alikuwa anamkadiria mrembo huyo anashindwa kummaliza, licha ya kwamba alikuwa ameanza kumzoea sana na kumpenda kwenye moyo wake lakini alikuwa na wasiwasi naye kwani alikuwa amekuja kwa kasi sana na kazi yake haikumruhusu yeye kuweza kumwamini mtu yeyote yule na kwa namna yoyote ile.
“Unataka nini kwangu?” ndilo swali ambalo alimuuliza mwanamke huyo akiwa amemkazia macho. Mrembo huyo licha ya kushtuka sana kutokana na aina ya swali ambalo alikuwa ameulizwa ila hakutaka kuonyesha mshtuko huo kwani ungethibitisha kwamba alikuwa na jambo lake. Alijizoa zoa na kusogea kwenye kile kiti ambacho Max alikuwa ameketi, alimkalia na kuanza kumnyongea kiuno chake mithili ya feni iliyokuwa inaongezeka kasi sana mwisho wakajikuta wamezama tena kwa penzi zito sana.
“Mimi nahitaji msaada wako Max” lilikuwa ni jibu lake baada ya kumaliza shughuli nzito ambayo iliwaweka kitandani kwa muda huo.
“Msaada upi?”
“Unajua nimepewa nafasi kubwa sana ya kumlinda raisi wa nchi nikiwa kama mlinzi wake mkuu”
“Brandina hayo siyo mambo ya kuongelea hapa saivi ni hatari sana, achana kabisa na hayo mambo”
“Nadhani wewe umeniuliza kwamba ni kwanini nimekuja kweye maisha yako”
“Sasa suala la raisi linatokea wapi?”
“Ndiyo sehemu hasa ambayo nahitaji msaada wako Max kwani nipo hatarini sana kuuawa”
“Whaaaat?”
“Ndiyo”
“Nani anataka kukuua?”
“Unamwamini mkurugenzi wa shirika letu”
“Brandina, what are you talking about?”
“Niligoma kufanya kazi yake Max, sijajua nyuma yake kuna nani na nani ila yule ni mtu hatari sana”
“Umeyajuaje haya?”
“Kwa sababu alitaka mimi nimuue raisi”
“Whaaaaat?”
“Yeah Max, niliogopa sana na ukizingatia sina mtu hata mmoja upande wangu nimebaki na wasiwasi sana”
“Ilikuaje?”
“Alinipa maagizo tu kwamba natakiwa kumuua mheshimiwa raisi bila kuacha ushahidi”
“Na wewe ukamjibu nini?” Max aliuliza akiwa anazunguka humo ndani na kushika kichwa, alikuwa hajui kama kwenye huo mchezo hata mrembo huyo alikuwa ameingizwa, hilo kwake lilikuwa ni jambo la hatari sana.
“Nilimwambia siwezi kuifanya hiyo kazi, siwezi kumsaliti raisi wa nchi yangu wala kulisaliti taifa langu kwa namna yoyote, ila aliniambia kwamba kama nikishindwa kufanya hivyo mimi ndiye natakiwa kufa. Naomba msaada wako Max” mwanamke huyo aliongea akiwa analia na kukaa chini akiwa bado uchi kabisa. Max alimsogelea na kumkumbatia kwa hisia sana, ilimuuma sana mrembo huyo kuingizwa kwenye michezo mibaya na ni wakati ambao alijihakikishia kwamba kweli mkurugenzi huyo alikuwa msaliti kama ambavyo raisi alimtahadharisha.
“Natakiwa kuongea na raisi hili jambo”
“Hapana Max usifanye hilo kosa”
“Kwanini?”
“Kwa sababu raisi atapaniki na mchezo wote unaweza ukaharibika, mimi nimekushirikisha wewe kwa sababu nimeona ndiye mtu pekee ambaye naweza kumwamini”
“Unahitaji nini?”
“Nataka unisaidie hawa watu na huu umoja wao tuweze kuupoteza na kuupoteza inatakiwa tufanye kazi bila wao kuwa na taarifa kwamba sisi tunawatafuta”
“Siwezi kukaa kimya nitakuweka kwenye hatari kubwa sana B”
“Hatuna namna Max naomba tu kujua kama unaweza kuwa na mimi kwenye hii safari maana kama tukiwaacha hawa watu wananchi wa taifa hili watateseka sana”
“Kwani kuna mengine unayajua zaidi ya haya?”
“Ndiyo”
“Unaweza kuniambia?”
“Baada ya kufuatilia kwa umakini sana nimekuja kugundua kwamba kumbe raisi mstaafu ni miongoni mwa watu ambao wapo nyuma ya haya mambo yote ambayo yanatokea na huenda ndiye yupo nyuma ya mkurugenzi”
“Una muda gani tangu umeyajua haya?”
“Siku tano sasa. Max mbona hata haushtuki kwamba unayajua haya?” Max alihema kwa nguvu sana na kuchungulia nje hakuona mtu yeyote yule.
“Yeah”
“Whaaaat?”
“Najua kila kitu Brandina”
“Niambie kwamba unanitania sio?”
“Hapana, sina utani na wewe”
“Why unajua na haufanyi jambo lolote?”
“Brandina haya mambo ni magumu sana kuliko unavyo fikiria wewe, ni watu wazito sana ambao unashauri kuingia nao kwenye vita na tangu ulipo amua kupambana nao basi maisha yako yapo hatarini sana”
“Kipi kinaendelea Max?”
“Naweza kukuamini B?”
34 naweka nukta hapa.
Tchao
Sawa mkuu.Huyu mwandishi hana maajabu tena kwa mwendo huu maybe story yake ni ya kukopi sehem then anatuma huku au hawa ndiyo wale akina mtibeli ambao hawamalizagi story au sifa zimemlevya au hana bando la kuja huku au yuko busy sna au hana lolote ..... Na mia na yule jamaa singanojr huyu jamaa atawadanganya lakini lazima atume huyu naye sasa......
Mkuu kumbe upo kabisa,,,, kwanza nakusalimu kwa jina la zakaria mansour..... Weka ata kipisi mkuu tutulize arostoSawa mkuu.
Hahaha 😂 😂 😂 ulivyopoa SasaMkuu kumbe upo kabisa,,,, kwanza nakusalimu kwa jina la zakaria mansour..... Weka ata kipisi mkuu tutulize arosto
Ndiyo maana akaleta uzi uku mkuuhHahaha 😂 😂 😂 ulivyopoa Sasa
Mchangie mwamba bwana umalizie story buku 2 sio kitu boss
Umeeleweka mkuu, karibu tenaGood morning.
Ni muda kidogo tangu niposti simulizi humu. Nimeona wengi wakidhihaki mara unasubiri waandike ndipo ucopy (unajua kabisa hii ni hoja ya mtu ambaye kala ugali kashiba kichwani kinakuja chochote kile naye anakwenda nacho hivyo watu wa namna hii huwa nawapuuza maana sometime sio wao ni mihemko tu) wengine wakilaumu na wengine wakitoa ushauri.
Siku zote huwa napenda kuwa positive hivyo no hard feelings..... Sitaeleza sababu za moja kwa moja ambazo zilifanya nikastop kuja kuendelea kupost humu kwa sababu zina mjumuiko wa sababu za kifamilia na sababu binafsi ambazo zilinikumba na kwa vile wengi walijudge before kuuliza basi wanatakiwa kubaki na hizo judgement zao kama zilivyo ila ukiona kila kitu kinanyooka kwako shukuru Mungu
tu kuna misala mingi inawatokea watu na sio lazima mtu aje akuhadithie wewe.
Kwa sasa kiasi chake nipo sawa hivyo hii simulizi nitaimaliza hapa hapa na kesho nitaitambulisha simulizi mpya "BADO NINAISHI (ASHRAFU NDILO JINA LANGU) hivyo zitakuwa zinakuja zote mbili.
Kama unajiona unapenda kutukana au ndiyo Hobby yako basi unaweza kwenda jukwaa na mahusiano ukamalizia hasira zako kwa wale ambao wanafanya maamuzi ya kipuuzi kwenye mapenzi ila sitapenda kuona matusi hapa (kosoa uwezavyo ni sawa ila sio matusi). Ukiona huwezi kuvumilia bila kutukana basi unaweza ukaachana na uzi tu ili baadae usianze kutafuta sababu za kutukana watu (Ustaarabu)
Siku njema kwenu.