Elton Tonny

JF-Expert Member
Mar 9, 2022
278
1,922
MIMI NA MIMI

A Story by Elton Tonny

Familia, Urafiki, Mapenzi, Kazi, Tamaa, Hila, Usaliti, Siri, Mambo Ysiyotazamiwa

R-rated 18+

Enjoy!


★★★★★★★★★★★★★

SEHEMU YA KWANZA

★★★★★★★★★★★★★


Maisha ni safari ndefu yenye kila aina ya changamoto, na hakuna mwanadamu yeyote azaliwaye kwenye sura ya dunia hii bila kuzipitia. Changamoto huja kwa nyuso tofauti-tofauti kwa kila mmoja, na kamwe haziwezi kufanana wala kuwa na uzito wa aina ile ile kwa watu wote wanaozipitia. Ikitegemea na hali, eneo, nyutu za watu, na mambo yanayowazunguka, sikuzote changamoto huwepo ndani ya maisha ya mtu kumsukuma awe na nia ya kupambana ili kujitoa ndani ya hizo na kuwa na maisha bora.

Tunaambiwa elimu ndiyo ufunguo wa maisha bora lakini hata watu wenye elimu ya juu bado huhangaishwa na matatizo mengi yanayowakosesha amani. Kila mtu mmoja mmoja anatamani kufikia sehemu nzuri maishani kiasi kwamba hata wale waliozifikia sehemu hizo bado wanakuwa hawaridhiki. Ni tamaa yetu sote kuishi maisha yenye kuridhisha, lakini mivurugo ya maisha sikuzote huturudisha nyuma. Iwe ni kwa matajiri, au wenye hali za chini kiuchumi.

Kwa sababu ndivyo ambavyo sisi sote tumezaliwa na kukuta hali zikiwa namna hiyo tokea mwanaume wa kwanza alipoamua kumtandika ndugu yake mpaka akafa, imetubidi tuyaishi maisha kwa namna ambavyo yametutaka tuyaishi. Usione mtu anafanya jambo fulani ambalo linapingana na uasili wa kufanya mambo ukadhani hafai. La. Ni kwamba maisha ndiyo yamemfanya akaona kufanya jambo hilo kuwa sahihi. Analazimika kuishi kwa njia hiyo aidha kwa kupenda ama kusukumwa tu, maadamu aishi.

Hivyo kamwe huwezi kuhukumu maisha ya mtu kwa kumtazama tu bila kujua kiundani ni mambo yapi yaliyopelekea mpaka akafikia hatua za kuishi namna aishivyo. Kujenga taswira nzuri mbele ya jamii ni jambo la muhimu, lakini maisha yanapokulazimu kuishi kwa namna ambayo jamii itayahukumu vibaya, unachopaswa kufanya ni kula ugali wako na kuvuta shuka kulala, ili kesho uamkie mambo mengine na kuendelea kuishi. Basi!

Naandika haya mimi siyo chizi. Mimi siyo mtunga mashairi wala nini. Ila nimeona tu nijaribu kuzama zaidi ndani ya vina virefu visivyoelezeka kwa mapana sana kuhusu neno hili: maisha. Maisha hayawezi kufanana kwa kila mmoja. Hayawezi kuendana. Hayawezi kuingiliana kwa asilimia zote na kumfanya mtu wa hali ya chini aweze kuwa kama kiongozi wa nchi hii kwa ufanisi aupatao kutokana na jasho la huyo huyo "mtu wa hali ya chini."

Kila mtu ana kisa chake mwenyewe cha maisha. Alipo fulani sasa hakufika kwa muujiza, kuna sehemu amepita. Unaweza ukashangaa kwa nini watu wanahangaika sana kufatilia maisha ya watu maarufu zaidi. Ni kwa sababu tayari wameshajijengea umaarufu. Hawakuzaliwa nao, waliutafuta, wakaupata. Wanaoendelea kuwafuatilia tu wanaishia kuwa watu wa kutamani. Hata hao watu maarufu wamepitia changamoto nyingi maishani, lakini hakuna mtu hata mmoja aliyejisumbua kuzijua wala kuziulizia mpaka walipokuja kupata huo ufanisi na kuzigeuza changamoto hizo ziwe kitu cha kuwatia moyo wengine kupambana zaidi.

Hutajali saana kufatilia maisha ya ndani zaidi ya mwanamke abebaye sinia la karanga kichwani, akiwa amebeba mtoto mdogo mgongoni, sura yake ikiwa imechoka, akiziuza karanga hizo stendi ya mabasi na jua likiwa kali sana. Tayari tu una kitu ndani yako kinachojua kwamba ana changamoto zake, kama watu wote, kwa hiyo nawe utabaki kutulia na za kwako tu, si ndiyo? Angalau nunua hata hizo karanga basi, hata ya mia tu. Itampa faraja kuona kwamba hata kesho anaweza kujikwamua na kuendelea kupambana kuzivuka changamoto zake ili ajenge maisha mazuri kwa kiwango ambacho Mungu atambarikia kukipata.

Sina lengo la kuandika mahubiri ili muanze kutenga sura na mistari. Ni kwamba tu nimeangalia hata maisha yangu mwenyewe na kugundua kwamba kuna changamoto nyingi zilizo ngumu maishani mwa mwanadamu, na japo kwa wengi zinatofautiana, mapenzi ni suala lizushalo changamoto kwa KILA MTU. Kubali, kataa. Hakuna mtu apitaye upeo wa ujana bila kukumbwa na changamoto za jambo hilo. Kwa nini?

Kwa sababu hakuna lengo lolote la kuishi isipokuwa upendo. Ni kitu cha kiasili. Kila mtu anacho. Nazungumzia upendo wote, iwe ni wa kindugu, kirafiki, kishkaji, kihuni, vyovyote vile, ni lazima tu kuwe na changamoto nyingi sana. Sasa inapofikia kwenye ule upendo wa kijinsia ndiyo kabisaa! Watu mpaka wanauana kwa sababu ya kuumizwa na mapenzi.

Lakini kwa jinsi ambavyo mambo yamekuwa kufikia kipindi hiki, imeshaonekana kuwa jambo la kawaida sana kwa mapenzi kuwa kitu chenye kuumiza badala ya kutakiwa KUBAKI kuwa kitu chenye kuridhisha. Na kama nilivyosema mwanzoni, kwa sababu tumezaliwa na kuyakuta namna hiyo, basi ndiyo tunaendelea kuyaishi namna hiyo hiyo tu. Lakini kuyaishi namna hiyo hiyo tu si jambo linalofaa.

Ni muhimu kuishi kwa kusudi, na imenichukua visa vingi vilivyotokea katika maisha yangu mpaka kufikia sasa kutambua kwamba mapenzi ya kujifurahisha tu hayana faida yoyote. Yanapaswa kuwa na lengo. Lakini kwa wengi, hata MIMI, hutuchukua muda mrefu mpaka kuja kumpata mtu anayeweza kukufanya ulitamani sana lengo hilo, haijalishi ni changamoto za aina gani utakazopitia, maadamu akiwa na wewe, unajua yote unaweza kuyashinda....


★★★★


Ilikuwa ni kwenye siku ya Alhamisi, nikiwa ndani ya gari kuelekea eneo lingine la jiji la Dar es Salaam. Siku hii kama siku zingine tu ilionekana kuwa na ukawaida wa mambo mengi ya kutarajia kwa maisha tuliyozoea sisi wabongo, na ndani ya gari hili kulikuwa na kioja kilichochangamsha asilimia kubwa ya abiria waliokuwemo. Niliposema gari sikumaanisha nina gari hapa.

Hii ilikuwa ni ndani ya usafiri rahisi wa umma, ama daladala ndogo aina ya Costa, na kutokea nilipokuwa nimekaa siti ya pili kutokea mbele upande wa pembeni alikaa mwanamke mtu mzima kiasi, akiwa amevalia nguo ya batiki na kujifunga kiremba kichwani, masikioni kukiwa na vifaa vidogo vya kuunganisha sauti kutoka kwenye simu.

Bila shaka alifurahia muziki mzuri sana kiasi kwamba alikuwa akiimba kwa sauti ya juu kuufatisha, lakini ilionekana kwamba hakutambua sauti aliyotoa ilizidi kupanda. Watu kadhaa walimzungumzia, wakidhani angekuwa msukuma, walimcheka na kuendelea kumtazama tu, huku yeye akiendelea kuburudika na kudhani wanamfurahia sana kutokana na kuimba kwake.

Nilikuwa nimekaa upande wa kioo cha dirisha nikipulizwa zaidi na upepo uliokipisha kioo kilichokuwa wazi, mara kwa mara nikifungua simu yangu kutazama ujumbe ulioingia na kujibu, kisha kuifunga na kuendelea kutazama nje. Kuna jambo fulani kuhusu mimi ambalo sikuzote lilifanya watu wanitazame sana, na hata bila kujionyesha kwao kwamba wananitazama mno au mimi kutowaangalia, nilijua tu kwamba wangenitazama kwa wingi.

Sitaficha hili nikiwa ndiyo nimeanza kuelezea kisa changu. Sura niliyobarikiwa kuwa nayo ilipendeza. Wazungu huita wanaume wenye sura nzuri sana "handsome," na mimi kiukweli nilikuwa hendisamu. Siyo uzuri ule wa kujitahidi sana kuufikia, bali ule uzuri wa asili unaoonekana hata bila kujitengeneza baada ya kutoka kusinzia.

Labda kingine kilichozidishia jambo hilo utizami wa watu kunielekea ni kutokana na ngozi yangu kuwa nyeupe. Oh najua kuna watu huhangaishwa sana na rangi ya mwili, na ya kwangu ndiyo iliyoongeza utomato mtamu kwa sura yangu. Macho madogo yenye kope na nyusi nyingi kwa juu, pua ya kawaida na midomo yenye uwekundu isiyo ya denda nzito sana vilifanya nionekane kuwa kama mchina ama mwarabu kabisa!

Nywele zangu zikiwa ni laini, sikuzote nilipenda kuzichana vizuri huku pande za kichwa zikiwa zimepunguzwa kidogo sana kufikia nyuma ya usawa wa masikio yangu. Mwonekano wa kimwili ulikuwa wa kiume zaidi, lakini si ule uliopita kiasi. Nilifanya mazoezi kipindi cha nyuma kuujenga lakini kufikia hiki sikujihusisha na mazoezi kwa utaratibu kama ule wa kujenga mwili kuwa imara sana, kwa hiyo nilikuwa na mwili ambao ungeonwa kuwa mwembamba lakini mpana, na nilikuwa mrefu pia.

Kama ni jambo lingine lililoongeza hali ya mvuto kwangu na hata kwa watu niliopendelea kuchangamana nao, basi ilikuwa ni usafi. Kuanzia jinsi nilivyochonga ndevu zangu hafifu kutokea kwenye timba mpaka kidevuni, mavazi mpaka viatu, nilionwa kuwa mtanashati na bishoo, au sharobaro kwa watu wengi. Mwonekano wangu na jinsi nilivyojiweka tu mbele ya watu ilifanya kwa mtazamo wa kwanza yeyote afikiri nilikuwa mtu mwenye kujipa hadhi fulani ya juu, kama mtu mwenye kujisikia sana, na ni kitu ambacho nilikuwa nimeshazoea tangu zamani.

Hata sasa ndani ya safari hii, niligundua kuna watu ambao walipenda mwonekano wangu na kunitazama sana. Nilivalia T-shirt ya rangi ya zambarau iliyopauka yenye mikono mirefu, suruali nyeusi ya kardet, pamoja na viatu vyeupe miguuni. Manukato niliyojipulizia pia yaliongeza kiwango cha mvuto wa kiume niliokuwa nao, ila sikukazia fikira mno suala hilo na kuendelea kukaa kwa utulivu tu nikisubiri kufika kule nilikodhamiria kwenda.

★★

Gari liliendelea kutembea tu, likipita majengo na magari mengi ndani ya barabara pana kwenye jiji hili lililo na shughuli nyingi, na mara kwa mara msongamano wa magari ulifanya tukawizwe njiani kutokana na kusimama kwa muda mrefu barabarani. Joto likiwa kali mchana huu, angalau ndani ya daladala hii kioja cha mwanamke huyo kuimba kwa sauti ya juu kilifanya watu wafurahike zaidi, na alikuwa bize kweli kufatisha maneno ya kila wimbo alioufahamu.

Baada ya kutumia dakika nyingi sana gari likiwa limesimama sehemu moja tu, ikabidi dereva atumie akili nyingine. Akaliingiza gari kwenye barabara ya changarawe ambayo ingezungukia upande wa mbali kiasi ili kuweza kutokea mbele zaidi ya njia tuliyotumia kupita kwa ajili ya safari yetu. Hatukujua kilichosababisha foleni hiyo lakini lilikuwa ni jambo la kawaida sana kwa barabara za jiji hili.

Tukaendelea kusonga. Mdogo mdogo tu, huku mwanamke yule akikomaa kuimba "kekundu, kekunduuuu..." na baadhi ya wadau ndani ya gari wakiitikia pamoja naye, jambo lililofanya tabasamu hafifu liniponyoke midomoni mwangu maana ilikuwa ni kwaya moja ya kitambo kweli. Barabara hii ilifanya gari lipite kwenye kona zilizobanana sana kutokana na nyumba kadha wa kadha kukaribiana, kisha tukaingia sehemu yenye uwazi zaidi ambako miti mingi ilionekana na nyumba chache sana zilizoachana kwa umbali mfupi.

Baada ya dakika chache za mwendo huo wa gari kutembea kama linatubembeleza, likafika sehemu fulani yenye miti zaidi bila nyumba na kusimama baada ya kitu kama kishindo kusikika kutokea kule mbele kwa dereva. Watu wakawa wanauliza nini kimetokea, na sasa ikawekwa wazi kuwa gari liliharibika. Doh! Ikabidi wote tushuke na kusimama nje, huku kondakta na dereva wakijitahidi kulifanyia ukarabati ambao tulijua usingeleta matokeo ya haraka.

Nilikuwa nimebeba begi la mgongoni lililotuna kutokana na kuweka vitu vyangu vingi, nami nikawa nimesimama pembeni tu huku wengine wakijadili ya hapa na pale kuhusiana na jambo hilo. Angalau hata yule mama wa "kekundu" alipumzisha sauti yake wakati huu.

Ni magari machache sana yaliyoanza kupita usawa huu wa barabara, na yalikuwa yamejaa lakini abiria niliosafiri pamoja nao wakawa wanayapanda na kushonana hivyo hivyo ili yawaondoe sehemu hiyo upesi. Tukawa tunapungua tu, mpaka nikabaki mimi mwenyewe na dereva na konda.

Haikuonekana kuwa gari lingetengemaa, kwa hiyo wawili hao wakaanza kuondoka pamoja nami, tukitembea kuelekea mbele zaidi na kuomba kukutana na bodaboda maana magari yaliacha kupita; ikionekana labda foleni ile barabarani ilikuwa imekata.

Kweli tukawa tumepata bodaboda moja, na wawili hao wakanishauri nipande na kwenda zangu lakini mimi nikawaambia wapande tu kwa sababu nilitaka kutembea kidogo, na bila shaka ningepata tu bodaboda nyingine. Wakaridhia na kupanda pikipiki hiyo pamoja, fyuu wakaishia. Nilidhani ingekuwa rahisi tu kutoka ndani ya eneo hilo lakini muda si muda nikatambua kuwa nilikosea.

Njia hii tuliyopita haikuwa rasmi, si kama barabara rasmi za changarawe, na kwa kuwa huko mbele haikuja bodaboda nyingine tena, nikajikuta nimeachwa peke yangu eneo lililoonekana kuwa kama linaelekea kwa Mzee Tambitambi. Mh? Hapana. Kuwa mwanaume na mengi hakukumaanisha nifanye tu vitu bila kujali hali yangu nzuri, kwamba niende mbele tu kwa ujasiri na kujikuta nimeingia nisikokujua, hivyo kwa busara nikaamua kurudi kule nilikotoka.

Nikaenda tena mpaka pale ambapo tuliiacha Costa ile, nami nikajiketisha kwenye nyasi safi na laini chini ya mti wenye kivuli kizuri. Ilionekana kama vile siku hii niliamuliwa maana hakuna usafiri mwingine wowote uliopita tena upande huo. Dakika zikawa saa, saa zikawa masaa, na mchana ukaanza kugeuka kuwa jioni.

Nikajiuliza hii ilikuwa ni adhabu gani ya ghafla namna hii. Yaani from nowhere tu eti magari na pikipiki zikaacha kupita ndani ya eneo nisilofahamu vizuri, na hakuna hata nafsi moja iliyoonekana. Hapa pasingeendelea kukalika maana saa moja ilikuwa inaingia, hivyo wazo la kurudi na barabara tuliyokuja nayo kwa Costa likawa suluhisho zuri kwa wakati huu. Ningehitaji tu kufika eneo lenye makazi kiasi na kutokea hapo ningejua nini la kufanya kupata usafiri mwingine.

Taratibu nikaanza kutembea, begi likiwa mgongoni kwangu, simu ikiwa sikioni kuniruhusu nizungumze na msela wangu mmoja, ambaye alinicheka kwa kusema nimelaaniwa kukutwa na saibu hili, na bila shaka ningekutana na Basilisa huko mbele kwa hiyo eti angeandaa masufuria ya kuchemshia uji wa msiba wangu huko nilikotoka!

Nikiwa bado nasonga taratibu, sauti ya kuunguruma kwa pikipiki kutokea nyuma yangu ikanifanya nigeuke kuitazama, nami nikaingiwa na matumaini. Ilikuja upande wangu kutokea eneo hilo nilikoiacha ile Costa, nami nikaipungia mkono ili mwendeshaji asimame, lakini nikashangaa ananipita tu na kunyoosha mbele. Khh!

Nikatoa begi mgongoni na kusimama hapo. Giza lilikuwa limeshaingia kiasi, nami nilihisi njaa, na kwa kutazama taa za jiji mbele zaidi nikajiamulia kutakiwa kusonga tu ili nifikie sehemu yenye shughuli maana bahati nyingine isingekuja. Lakini Mungu si Athumani bwana, gari lingine dogo likaonekana likija kutokea huko nilikopaacha, nami nikapunga mkono lisimame lakini nalo likanipita tu. Kweli Mungu siyo Athumani!

Hali hii ikaniudhi, lakini nikaelewa vizuri upande wa pili wa mambo. Kikawaida, sehemu kama niliyokuwepo ilionekana kuwa na uhatari, labda wa vibaka, ukitegemea pia na muda, hivyo watu wasingekuwa wenye urafiki sana kwa mtu wasiyemjua na kusimamisha tu vyombo vyao kumsaidia; maana hofu ya kupatwa na madhara ilikuwepo kwa wote. Kwa hiyo ikanibidi nifikirie njia mbadala ya kujiondoa sehemu hii haraka kwa usafiri kabla usiku haujawa mzito zaidi.

Nilipopiga tu hatua zingine chache huku begi langu nikilining'iniza mkononi, gari lingine likasikika likija kutokea nyuma yangu. Sikugeuka. Nikaanza kutembea kwa kuyumba kiasi, kama mlevi, kisha nikaliangusha begi chini na kujishika kifuani, nikianza kuguna kwa sauti ya juu na kujiingiza barabarani kwa njia iliyoonyesha nakaribia kuanguka. Haya yalikuwa maigizo tu, na kama sikuwa nimeweka hili wazi mwanzoni, unapaswa kujua kwamba nina utundu fulani pia. Wengine huuita uhuni. Ila nilikuwa mhuni ilipohitajika tu.

Nilikuwa makini kutambua umbali ambao gari hilo lilifikia, na sasa likiwa karibu zaidi na nilipokuwa, nikajiangusha barabarani huku nikilinyooshea mkono lisimame maana nilikuwa na tatizo la kifua. Maigizo tu! Ikiwa aliyekuwa ndani ya gari hilo alikuwa na moyo mzuri, basi angenionea huruma na kushuka kuja kunipa msaada, hivyo ningeweza kupata lifti kwa wepesi. Akili mtu wangu!

Jaribio langu likazaa matunda mazuri pale gari hilo liliposimama, nami nikajisemea "Yes!" na kisha kuendelea kulia kwa maumivu makali chini hapo. Sikufumbua macho yangu na kuendelea kuigiza tu, nami nikasikia mlango ukibamizwa kidogo, kuashiria umefungwa baada ya kufunguliwa. Nikafungua jicho moja kiduchu na kuona kwamba kuna mtu alikuja upesi, nami nikafumba tena na kuendelea kulia.

"Oooh... aaah!"

Nikahisi shingo yangu ikishikwa kwa viganja na kunyanyuliwa kiasi ili kichwa changu kiwe juu, na sijui ni nini tu kilichofanya nisikazie fikira sana suala hili lakini mikono hiyo ilikuwa laini, na harufu ilikuwa nzuri sana.

"Kaka... nini tatizo?"

Sauti hiyo nyororo ikanifanya nifumbue macho yangu na kumtazama aliyeitoa, na kwa sekunde chache nikajisahau kwamba nilikuwa naumwa. Nilimtazama mwanamke huyo usoni kwa ufupi tu, lakini nilihisi ni kama nimemwangalia kwa muda mrefu. Alikuwa na sura nzuri. Mweupe, yaani mweupe. Mtu mzima kunipita hadi mimi kiumri, lakini kama angeamua kudanganya yeyote yule kwa kusema ana umri mdogo, hata mimi ningekubali.

Alikuwa na macho mazuri ya ufilipino fulani hivi na ya kungu kiasi, midomo laini na mizuri, na nywele zake zilikuwa zake, ndefu kufikia mabegani ambazo bila shaka alizilainisha zaidi kwa dawa. Uso wake mweupe wenye kujali sana ulionyesha huruma nyingi kunielekea, naye alikuwa anatumia kiganja kimoja kupima joto la mwili wangu kwa kukiweka kwenye shingo na paji la uso wangu.

Nikafumba macho yangu tena na kuendelea ku "Oooh... nakufaaa..." naye akanishika usoni kwa kiganja chake.

"Kaka... nini kinakusumbua?" akauliza hivyo.

Sauti yake ilikuwa tamu sana, kama ya mtoto mdogo vile ama ile ya Wema Sepetu anayobania puani.

"Aah... kifua dada... kifua kimekaza..." nikatoa lawama zangu.

"Pole sana. Naomba ujitahidi kusimama nikuingize kwenye gari tukatafute hospitali, hapo mbele tu, eti?" akaniambia.

Nikalibana tabasamu langu na kusema, "Sawa."

Kisha nikaanza kujinyanyua, naye akanipa egamio na kutembea nami mpaka upande wa mlango wa pili wa gari lake. Gari lake lilinishangaza kiasi. Ilikuwa ni zile pickup Toyota za zamani kweli ingawa ilikuwa safi, nyeupe, lakini haikuonekana kuwa gari iliyomfaa mwanamke mwenye uzuri wake. Kwa vyovyote vile hilo halingejalisha kwa kuwa sasa nilipata lifti.

Nikakalishwa siti ya upande wa mbele pembeni ya usukani, kisha mwanamke huyo akaniacha na kuelekea pale aliponitoa. Nikamwangalia na kuona akiliokota begi langu na kuanza kuja nalo upesi kwenye gari, naye akaingia pia kwenye usukani na kuliweka kwenye siti za nyuma. Akaingiza gia na kukanyaga mafuta, nalo gari likaanza kutembea tena huku bado nikiwa nimekaza sura na kuonyesha nina maumivu sana.

"Pole kaka. Una... unakaa wapi... umetokea wapi?" akauliza.

"Nilikuwa... natokea Bamaga kule..."

"Sinza?"

"Ndiyo... usafiri ukaharibikia hapo nyuma... ndiyo nikabaki mwenyewe mpaka oooOOH!" nikaendelea kujikata na wembe bandia.

"Pole... ngoja nikuwahishe hospitali ya karibu," akasema hivyo.

Nikafumbua jicho moja na kumtazama kwa chini, na alikuwa makini kweli kwenye uendeshaji akionekana kutaka kuharakisha kututoa huku. Nikaangalia upande wa nje na kutabasamu tu, kisha maigizo yakaendelea hadi tulipoanza kuzipita nyumba zile zilizokaribiana. Nikaelewa haingechukua muda mrefu kufikia barabara kuu, nami nikamtazama mwanamke huyo tena.

Isingekuwa ya mazingira tuliyokutana kuwa jinsi yalivyokuwa, basi angefaa sana kuwa rafiki mzuri. Alionekana kuwa mwenye kujali, nami nikawaza kuwa bila shaka angekuwa na watoto aliowatendea vizuri mno. Lakini kwa upande mwingine, kufanya naye urafiki ingekuwa ni jambo gumu maana tayari nilimdanganya kuumwa ili tu nitimize haja yangu ya kutoka eneo lile, kwa hiyo ningepaswa kuhakikisha namkimbia kwa spidi zote akishanifikisha huko mbele.

Kweli dakika si nyingi tukawa tumeingia barabara kuu za lami, naye akaonekana kupita kwenye njia ambayo ingetufikisha kwenye moja ya hospitali kwenye maeneo ya Buguruni. Nikiwa sitaki hilo kitokee, nikaanza kumpiga-piga taratibu kwenye mkono wake, naye akanitazama huku bado akiendesha.

"Nishushe dada..." nikamwambia hivyo huku bado nikiwa nimekunja sura.

"Wapi?" akauliza.

"Hapo tu hivi..."

"Lakini hali yako ni mbaya... unatakiwa kufika hospitalini kwanza..." akaongea kwa kujali.

"Hhh... nishushe... nahitaji hewa kidogo..."

"Upepo si unaingia vizuri hapo?"

Nikamtazama kwa konyezo na kuona jinsi alivyokuwa makini, nami nikasema, "Na juice..."

"Juice?"

"Ndiyo... huwa inatuliza moyo..."

"Ni... moyo au kifua?"

"Ah... vyote! Ooooh!" nikaendeleza uwongo wangu.

Akaonekana kujali zaidi hali yangu, naye akalipeleka gari sehemu ya kuegeshea barabarani ambako hakukuwa mbali na viduka vidogo vya bidhaa. Kwa upande aliosimamisha gari, ule wa pili ulikuwa na majengo ya makao makuu ya kampuni ya Azam, na magari mengi ya abiria yalipita na kusimama kushusha na kupakia abiria.

Mwanamke huyu akataka kushuka ili aende kunifatia juice lakini akashangaa baada ya mimi kuufungua mlango wa upande nilioketi na kutoka ndani ya gari. Akabaki kuniangalia mpaka nilipofungua mlango wa nyuma na kulitoa begi langu, kisha nikaufunga na kusogea hapo mbele; nikiinama kiasi kumchungulia.

"Asante sana dada. Mungu akubarikiii!" nikamwambia hivyo huku nikitabasamu.

Alikunja uso wake kimaswali kiasi, naye akasema, "Wewe... uko... uko..."

"Niko sawa," nikamalizia maneno yake.

"Kifua hakiumi tena?"

"Kimeacha sasa hivi tu. Niko poa kabisa. Endelea tu na safari dada na Mungu atakulipa kwa ukarimu wako. Mmmwah!" nikamwambia hivyo na kumrushia busu kwa kiganja.

Alionekana kushangazwa sana na hili, naye akaangalia pembeni kiasi na kusema, "Ulikuwa unadanganya."

"Oh... siyo kudanganya yaani... ni... ile ilikuwa ni njia ya kukuomba msaada maana hakuna aliyetaka kunisaidia hata lifti tu. Ila wewe una moyo mzuri sana dada yangu, yaani hadi ukanipima na joto... hahahah... msaada mdogo tu lakini nimefarijika sana. Utabarikiwa milele," nikamwambia kwa shauku.

"Kwa hiyo... umenipotezea muda wangu, nafikiri unaumwa kumbe..."

"Ona ninaweza kukulipa kama unataka," nikamkatisha.

"Nini?"

Nikatoa wallet yangu na kuchomoa pesa, kisha nikamnyooshea huku nikisema, "Time is money. Pole kwa kuchelewesha ulikokuwa unaenda ila chukulia hii buku mbili kama nauli ya kunibeba kulipia huo muda, mm? Shika."

Akanikazia macho yake na kuniuliza kwa sauti ya chini, "We' ni mjinga?"

"Aaa, usiwe hivyo sister. Huku ni kusaidiana tu. Eh? Nimesema asante na pole hii hapa nakupa. Chukua. Ama niendelee kuigiza nimenigwa kidogo? Eerrgh hahahah..." nikamwambia hayo na kumtania kidogo.

Akaniangalia kwa kutoamini fulani hivi, kisha akakanyaga mafuta na kuliondoa gari bila kuichukua elfu mbili niliyotaka kumpatia.

Nikaendelea kulisindikiza gari lake kwa macho, nami nikashusha pumzi na kusema kwa sauti ya chini, "Asante."

Aliistahili asante hiyo ingawa hangeisikia wala kuijali tena kwa sababu nilikuwa nimemkosea. Nikatoa kitambaa changu safi na kuanza kujifuta hapa na pale kwenye suruali yangu nyeusi ya kardet, iliyochafuka kiasi kutokana na kujilaza chini nilipomfanyia maigizo mwanamke huyo. Nikaangalia saa yangu kwenye simu na kukuta ni saa mbili kasoro sasa, nami nikasimama sehemu ambayo ingeleta daladala za kuelekea kule nilikodhamiria kufika kwa siku hiyo.

Daladala ikaja, nami nikapanda kwa kusimama pamoja na abiria wengine ambao kama kawaida wangenitazama mara kwa mara kuonyesha nilikuwa mtu mwenye utofauti fulani kutokana na sura yangu. Vuuu... gari likapita eneo moja baada ya lingine huku nikiwa nimebanwa kiasi na watu niliosimama pamoja nao, na hatimaye tukafika maeneo ya Rangi Tatu, huko Mbagala, nami nikashuka hapo.

Kwa jiji letu kufanya matembezi sehemu mbalimbali kipindi cha nyuma kulifanya niyajue maeneo mengi, lakini Mbagala ndiyo kati ya maeneo ambayo sikuwa na mazoea nayo kabisa. Hata safari hii fupi kutokea kule nilikoishi ilinibidi niwe nimefanya utafiti wa jinsi ya kufika huku, kwa sababu kuna sehemu hususa niliyokuwa nikielekea.

Isingekuwa kucheleweshwa kule kwa usafiri niliochukua mara ya kwanza basi ningewahi kufika nilikohitaji kufikia, kwa hiyo baada tu ya kushuka nikatafuta daladala nyingine ambayo ingenipeleka kwenye eneo la mbele zaidi lililojulikana kama Mzinga.

Mapema nikapanda gari za Toangoma na mwendo ukaanza. Sikuzote nilifurahia hali fulani ya ugeni nilipoingia kwenye maeneo ambayo sikuyafahamu vizuri, kwa hiyo nilikuwa makini kutazama mambo mengi ya maeneo haya. Hakukuwa na purukushani nzito kama maeneo ya Kariakoo ama maghorofa mengi na vitu maridadi mno, bali mwonekano wa hali ya kawaida ulioitofautisha Mbagala na maeneo mengine yaliyofanisika zaidi.

Dakika kama kumi tu nasi tukawa tumefika Mzinga, nami nikashuka pamoja na wale walioshukia hapo. Bila hata kusumbuka, bodaboda zikanikimbilia, nami nikachagua moja na kumpa maelekezo dereva anipeleke sehemu iliyojulikana kama Masai. Nikapanda, mwendo ukaanza.

Nadhani ni ugeni wa mtu kama mimi kwenye eneo hilo uliofanya wengi wa watu tuliowaopita wanikodolee sana, na upesi nikatambua kwamba vijora ndiyo vazi lililopendelewa zaidi na wanawake wa huko. Nilikuwa makini kukariri njia tuliyotumia kupita mpaka kufika Masai, ingawa ilikuwa giza. Hiyo Masai ilikuwa ni bar pana kiasi yenye ghorofa moja juu na vyumba vya wageni. Tayari kwa muda huu wa saa mbili palikuwa pameshachangamka, muziki ukiwa mnene, na wengi wa waliokuwemo kule ndani waliniangalia sana baada ya kuniona.

Nikamlipa boda, naye akatoweka. Nafikiri wengi walikuwa wanasubiri kuona nikienda pale aidha kunywa ama kuchukua chumba cha kupumzikia kutokana na kuwa sura mpya kwenye eneo lao na kubeba begi mgongoni. Lakini Masai haikuwa shabaha yangu. Nikasogea pembeni na kutoa simu, nami nikatazama ramani ndogo ya nyumba iliyokuwa karibu eneo la bar hii. Nilikuwa na mpango wa kufikia kwenye nyumba hiyo ambayo mwenye nayo alikuwa ametoa tangazo siku chache nyuma kuwa angepangisha mtu hapo.

Ilikuwa ni sehemu sahihi kwangu kutaka kufikia kwa sababu nilitaka mazingira mazuri ya unyumbani, siyo chumba cha kupanga, bali kama alivyoonyesha kwa tangazo lake nililoliona mtandaoni, ilikuwa ni sehemu ya kukaa kama nyumbani. Yaani, kungekuwa na sebule yenye vitu kama samani na makochi tayari, chumba chenye kitanda, bafu, choo, maji, umeme, mambo kama hayo. Na gharama yake ilikuwa nafuu kwa kila mwezi.

Tayari nilikuwa nimeshawasiliana na mwenye kutoa huduma hiyo kwa njia ya WhatsApp na kukubaliana naye kwamba ningekuja hapo siku si nyingi ili asije kumpa mteja mwingine nafasi hii niliyoitaka mimi, naye akawa ameridhia. Kwa hiyo baada ya kuona uelekeo ambao nyumba hiyo ilikuwa, nikaanza kuelekea huko taratibu.

Mtaa huo kwa usiku ulionekana kuwa kimya kiasi, na nyumba nilizozipita zilikuwa za kawaida sana, vijia vyenye uchochoro mwingi, yaani mwonekano sahihi wa uswahilini. Kidoti chekundu cha ramani kikanifikisha mbele ya nyumba hiyo, nami nikaiangalia kwa umakini.

Kutokea nje, ingeweza kuonekana kuwa kubwa kiasi, ikiwa imezungushiwa kuta iliyoitenganisha na nyumba nyingine pembeni lakini kwa ukaribu sana. Geti lilikuwa pana na jeusi. Ningeweza kuona madirisha mapana yaliyowekewa vioo vyeusi, ungo wa king'amuzi cha Azam huko juu, na taa nene ya nje iliyomulika vyema mpaka kufikia niliposimama. Bila shaka palikuwa ndiyo penyewe.

Kupiga jicho upande mwingine wa nyumba za waswahili, nikaona wanawake kadhaa wakiwa wamesimama, wengi wao wakijifunga mikhanga tu kuanzia kifuani, wakiniangalia kama hawanijui. Ah kweli walikuwa hawanijui.

Hivyo nikaenda zangu mpaka kwenye geti hilo na kuligonga kwa wepesi kiasi, nami nikabaki kusubiri. Sikuwa nimeona haja ya kumtafuta mwenye nyumba kwa simu tena maana alisema kuwa muda wowote ule ambao nilijisikia kufika kwenye nyumba hiyo basi ningeenda tu, na ndiyo muda wenyewe ukawa huu. Sauti ya kifungulio kidogo cha mlango wa geti ikasikika baada ya sekunde chache, nao ukafunguka.

Mbele yangu alisimama mwanamke mtu mzima vya kutosha kunizaa, labda hata mara mbili. Umri wake kwa kukadiria ungekuwa wa miaka 50 ya mwishoni na kuendelea, naye alikuwa na ufupi wa kadiri, mnene kiasi, mwenye ngozi yenye weupe uliofifia, na macho yake mazuri yalinitazama kwa umakini.

"Mama shikamoo..." nikampa salamu kwa heshima.

"Marahaba. Hujambo?" akaniitikia.

"Sijambo," nikamwambia.

Alinitazama kwa umakini sana, akiwa kama ananitafakari, nami nikawaza kwamba huenda ndiye aliyekuwa mwenye nyumba, hivyo ingenibidi nimweleze mimi ni nani.

"Pole kwa kuwa nimefika usiku mama, gari niliyokuja nayo iliharibikia njiani. Mimi ni...."

"Ndiyo wewe kumbe?" akanikatisha kwa kuniuliza hivyo.

Kwa kufikiri anamaanisha kile nilichowaza, nikamwambia, "Ndiyo mama, ni mimi."

Akanishusha na kunipandisha huku akitabasamu kiasi, nami nikatabasamu pia kirafiki.

"Umekuja mwenyewe?" akaniuliza.

Sauti yake ilikuwa yenye upole mwingi sana, nami nikasema, "Ndiyo, niko mwenyewe. Gari lisingeharibika nisingechelewa kufika, ila hata hivyo haukujua kama ningefika leo japo nilipanga kufika mapema."

"Ahah, hamna shida baba, nilijua unakuja. Sema... karibu ndani kwanza. Jamani! Utakuwa umechoka kweli..." akasema hayo huku akinipisha ili nipite.

Mh? Sikutarajia angefahamu kwamba nilikuwa nakuja leo lakini njia yake ya kunikaribisha ilikuwa nzuri sana, nami nikaingia tu na kusogea mbele kidogo. Akafunga mlango wa geti na kusogea usawa wangu.

"Pole baba jamani... karibu sana. Twende ndani upumzike kidogo," akaniambia.

"Asante," nikashukuru.

Akaniongoza kufikia ubaraza uliojengewa vigae sakafuni, nami nikaona viatu kadhaa chini hapo kunifanya nitambue kuwa huko ndani kulikuwa na watu wengine zaidi. Labda wengine wa familia yake ambao waliishi naye, na mimi ndiyo ningeongeza idadi kwa kuja kukaa hapo. Yote yalikuwa sawa kwangu, nasi tukaingia ndani ya nyumba hiyo pamoja. Alinisihi niingie na viatu tu nilipoashiria kutaka kuvivua, na baada ya kufika sebuleni akanikaribisha nikae kwenye sofa moja.

Sebule haikuwa pana sana lakini ilikuwa pana. Masofa yalikuwa matatu na marefu yaliyopangwa kwa njia ya ukuta uliozunguka meza ya duara yenye kioo cheusi na kizito hapo katikati. Sofa nililoketi lilinitazamisha moja kwa moja na TV ndogo tu ya flat screen ukutani, na juu kiyoyozi kilionekana kuzunguka na kuipa sebule ubaridi ulioleta ahueni kutokana na joto la jiji hili.

Upande wa nyuma wa sofa nililokalia kulikuwa na sehemu pana iliyokuwa ya lengo la kulia vyakula (dining), na hapo niliona meza ndefu kiasi ya mbao, iliyozungukwa na viti sita vilivyoibana kwa ukaribu. Pembeni na hapo kulikuwa na friji yenye urefu wa kadiri na yenye rangi ya njano, pamoja na sehemu yenye uwazi wa mlango usiokuwa na mlango, ambao ulionyesha uelekeo wa kwenda chumba cha jikoni kutokea hapo 'dining.' Kampangilio kalikuwa kazuri kweli, na safi sana.

Kwenye sofa la upande wa kulia alilala binti mwenye umri mkubwa kufikia miaka 20 hivi, akiwa makini tu kutazama runinga bila kujali kwamba kuna mgeni aliingia. Alivaa dera lililousitiri vyema mwili wake, na kwa kumwangalia haraka nikatambua alikuwa mweupe na mwenye sura nzuri. Alitulia kivyake tu akitazama tamthilia huku aking'atang'ata kucha moja ya kidole chake kiganjani.

Mwanamke yule aliyenikaribisha akasimama pembeni yangu na kusema, "Karibu sana baba'angu."

"Asante mama," nikamwambia.

"Ngoja nikuletee kitu cha kupoza koo kwanza, eti?" akaniambia.

Nikatabasamu na kusema, "Asante sana."

Angekuwa amefanya jambo la maana kwa kuwa sikuweka chochote kile tumboni tokea nilipokunywa chai asubuhi, kwa hiyo kama ni juice angeileta tu nami ningeishusha vizuri sana. Akaondoka na kwenda upande ulioonekana kuelekea jikoni, nami nikakaa kwa utulivu na kumtazama binti yule pembeni. Alionekana kutojali kabisa wageni, nami nikawaza huenda alikuwa mwenye nyodo kupita maelezo.

Sekunde chache kupita na mwanamke yule akawa amerejea tena, isipokuwa wakati huu akawa amekuja pamoja na mwanamke mwingine aliyeonekana kumzidi mpaka na yeye kiumri kiasi. Huyu hakuwa mweupe, bali mweusi wa maji ya kunde, naye alikuwa na nywele fupi zenye mvi kiasi kichwani kwake.

Yule aliyenipokea mara ya kwanza alibeba sinia lenye glasi iliyowekewa juice, bila shaka ya parachichi, pamoja na sahani yenye wali na nyama iliyoonekana kuungwa vizuri sana kutokana na namna ilivyonukia. Yaani vilitamanisha sana, na kwa njaa niliyohisi ningekula mpaka kusafisha sahani yote. Ni kama alijua!

Sikutegemea mapokezi yangu kwa hapo yangekuwa mazuri namna hiyo kutoka kwa watu wazima kama hao, lakini lilikuwa ni jambo la kawaida kwangu mimi kutendewa kwa njia nzuri na watu wengi. Siyo wote, ila wengi. Kwa hiyo sinia hilo likawekwa mezani, nayo ikavutwa mpaka kuifikia miguu yangu, na wanawake hao wakawa wamesimama pembeni huku wakinitazama kwa njia fulani ya... matumaini.

Nikatabasamu kidogo na kusema, "Asanteni sana. Shikamoo mama?"

Nilikuwa nikimsalimu yule mwanamke mwingine, naye akasema, "Marahaba kijana wangu. Karibu sana, jisikie umefika nyumbani."

Nikatikisa kichwa kukubali ukaribisho wake.

"Karibu chakula baba. Pole kwa safari," yule mwanamke mweupe akaniambia.

"Asante."

Kiukweli nilikuwa nimesema asante nyingi sana kwa jioni hiyo, nami nikaanza tu makamuzi taratibu huku wanawake hao wakiwa wamesimama tu na wakiniangalia. Niliona hilo kuwa ajabu kiasi lakini labda hawakuzoea sana ugeni wa wanaume, tena hasa kutokana na mwonekano wangu.

Oh, kwangu mimi sura niliyokuwa nayo ilikuwa kawaida sana, lakini kwa wengine ilikuwa kama vile kigezo fulani cha kuwafanya wanitendee kiyaiyai. Nilitamani kuwaambia watu hawa wazima wakae, lakini tena nikajizuia maana sikuona hilo kuwa adabu kutoka kwa mgeni aliyefika tu na kuanza kujifanya mjuaji. Wafanye vile walivyojisikia.

"Kwa hiyo... haukuja na Shadya?"

Swali hilo lilitoka kwa yule mwanamke mweupe aliyenipokea mwanzoni, nami nikamtazama machoni. Sikuelewa Shadya ilikuwa ni nini, ila nikadhani amemaanisha jina la gari la usafiri kama Mohammed Trans.

"Aa... hapana... sijaja na Shadya. Nilipanda tu daladala, nikaifata ramani ndiyo nikafika. Ni mara yangu ya kwanza," nikawaambia.

Waliangaliana kimaswali kiasi, mimi nisijue sababu, lakini nikaendelea zangu tu kula.

Yule mweusi kiasi akasema, "Tulifikiri ungekuja labda hata na... ndugu zako..."

"Ndugu? Hamna... ni mimi tu mama. Nimekuja kukaa huku peke yangu," nikasema.

"Umekuja... kukaa huku?" akauliza yule mwanamke mweusi.

"Ndiyo. Nafikiri tutaanza kuzungumza kuhusu gharama na kila kitu nimeshaandaa. Nimalize kwanza kula, eh?" nikawaambia.

Yule mweupe akatabasamu kwa furaha na kusema, "Sawa baba. Wewe kula tu. Tutaongea mengi zaidi Miryam akishafika."

Nikakunja uso kimaswali kiasi na kuuliza, "Miryam?"

"Ndiyo. Na yeye amekawia kidogo tu, ila amesema yuko karibu kufika," mwanamke mweupe akaniambia.

Nikaangalia pembeni kiufupi, nikiwa sijaelewa vizuri jambo hilo, na yule mwanamke mweusi alinitazama kwa umakini zaidi tofauti na yule mweupe ambaye aliniangalia kwa furaha zaidi.

"Miryam ndiyo... mwenye nyumba?" nikawauliza.

Wakaangaliana machoni kwa njia ya kuulizana jambo fulani, kisha wakanitazama tena na yule mwanamke mweusi akasema, "Eee... ndiyo... Miryam ndiyo... ndiyo mwenye nyumba."

"Mmmm... sawa basi, haina shida. Nitamsubiri ili tupangane vizuri. Nimepapenda sana hapa," nikawaambia hivyo.

Nikakirudia chakula changu na kuendelea kushuka nacho taratibu, nami nikamwona mwanamke yule mweusi akimpa kiashirio mwenzake kwa kumvuta ili waondoke hapo. Nikawaangalia, naye akasema wanaenda kuandaa mambo fulani kisha wangerudi tena, na mimi ningekuwa nani kuwazuia? Nikasema sawa, nao wakaishia kwenye kona upande mwingine ndani hapo.

Nikaendelea kula na kumwangalia binti yule tena, na bado alikuwa anatafuna tu kucha. Nilipomwangalia vizuri zaidi nikaanza kuona kwamba hali yake haikuwa sawa kwa asilimia zote, lakini nisingeweza kukisia haraka ikiwa alikuwa na tatizo fulani. Macho yake yaliielekea TV, lakini ni kama umakini wake haukuwa kwenye kile kilichoonyeshwa humo.

Nikataka nimsemeshe, lakini ndiyo hapa nikaanza kusikia maongezi baina ya wale wanawake wawili walioondoka muda mfupi nyuma. Nikatambua hawakuwa wameenda chumbani kabisa, bali walisimama nyuma ya ukuta uliowaficha kutokea hapo sebuleni.

Sauti ya chini ya mwanamke yule mweupe ikasikika ikisema, "Dada jamani, huyo kaka ni mzuri! Eh! Sijawahi kuona."

Sauti ya mwenzake ikasema, "Mbona kama mdogo sana?"

"Kinachofanya ufikiri ni mdogo nini?"

"We' humwoni? Anaonekana hadi kutakiwa kumwamkia Mimi."

"Mh? Hamna bwana. Halafu kwani kuna ubaya gani? Sema ni kasura kake tu ndiyo kanamfanya anaonekana mdogo, lakini hata Shadya alisema ni mkubwa. Sidhani kama alikosea. Mimi nimempenda sana jamani..."

"Ndiyo, ni mzuri ila, mbona kama haelewi-elewi mambo? Tunamuuliza hiki, yeye anajibu vingine, kama anavuta sijui..."

"Atakuwa amechoka tu, halafu anaonekana ana njaa, hajala muda huyo..."

"Lakini..."

"Acha hizo bwana. Kijana wetu amechoka tu, tumsubiri Miryam mengine tutajua. Dada nina furaha SANA!"

Mh? Hayo yote niliyasikia, nami sikuweza kuelewa kabisa maongezi hayo mafupi yalilenga suala gani haswa. Kulikuwa na ishu gani nyingine zaidi ya mimi kuja kupangishwa kwenye nyumba hii iliyomfanya mmoja wa wanawake hao afikiri kuwa sielewi mambo, ama navuta bangi? Shadya ndiyo alikuwa nani badala ya nini?

Ningehitaji kujua undani wa mambo hayo ili nisije kujikuta nadumbukia kwenye masuala mengine kabisa tofauti na yaliyonileta huku, na wao kuanza kuja tena kukanifanya nijiandae kuzungumza nao kwa kina kuhusu makazi yangu ya muda mfupi kwenye nyumba hii. Nilitaka kujua ningelala kwenye chumba kipi ndani hapo, na mambo ya kawaida ambayo ningeshiriki kufanya kama mwanajamii mpya katika eneo hilo. Basi.

Waliponifikia tena, walikuwa wakitabasamu tu, bila kujua kwamba mengi ya yale waliyozungumzia niliyasikia, nami pia nikatabasamu na kuigiza kutojua lolote. Tayari nilikuwa nimefuta wali wote na nyama, ikibaki tu juice ya kuendelea kushushia.

"Asanteni sana jamani," nikawaasante tena.

"Nikuongezee ubwabwa?" yule mwanamke mweupe akaniuliza huku akija kuchukua sahani.

"A... hapana. Nimeshiba. Asante..."

Asante nyingine tena? Nikaanza kuhisi naboa.

"Napenda kujua vitu vya kawaida, yaani shughuli za kawaida zifanyikazo hapa. Mmesema napaswa kusubiri mpaka Mariam aje ndiyo tuzungumze?" nikauliza.

"Abee..."

Hilo lilikuwa ni itikio kutoka kwa yule binti aliyelala kwenye sofa, nami nikageuka na kumtazama. Alikuwa ananiangalia sasa. Macho yake yakiwa na ukavu fulani hivi, ilikuwa kama vile sura yake si ngeni sana kwangu, ijapokuwa nilijua kabisa kwamba hii ndiyo ilikuwa mara ya kwanza kukutana naye. Sikujua alikuwa ameitikia mwito kutoka kwa nani, lakini kuniangalia vile kukafanya nijue alidhani mimi ndiyo nimemwita.

"Hajakuita, endelea kuangalia sinema mama, eh?" yule mwanamke mweupe akamwambia hivyo binti, naye akaitazama TV tena.

Jambo hili lilinishangaza kiasi. Nikawatazama wanawake wale, wote wakiwa wamesimama, nami nikauliza, "Kwa nini anafikiri nimemwita?"

Mweupe akajibu kwa kuniambia, "Ulikuwa unataka kusema Miryam, jina la dada yake, ila ukasema hilo ulilolisema, ndiyo la kwake. Aka... akadhani umemwita."

Njia yake ya kuwasilisha taarifa hiyo kwangu ilikuwa kama vile hataki kuendelea kuzungumzia zaidi suala la binti huyo aliyelala kwenye sofa, naye akaondoka pamoja na sahani ile bila shaka kuirudisha jikoni. Nikamwangalia yule mwanamke mweusi, naye akaketi kwenye sofa la upande wa kushoto huku akiniangalia pia. Alionekana kuwa mtu makini, labda mkali kiasi pia, nami nikaendelea kuweka utulivu tu wa kiume.

"Hawajambo nyumbani?" akanisemesha.

Nikamwangalia na kutabasamu kiasi, nami nikasema, "Wazima kabisa. Sijui hapa?"

"Tunaendelea vizuri. Mungu anasaidia. Angalau mara moja moja tukipata wageni kama hivi... ni baraka," akaniambia.

Nilikuwa na kawaida ya kusugua magoti yangu kwa viganja taratibu hasa nilipozungumza na mtu niliyemheshimu sana, na wakati huu nikawa nikifanya hivyo, nami nikamwambia, "Ndiyo wageni huwa ni baraka. Hata sisi kule kwetu... angalau mgeni akifika tunafurahi maana mahanjumati na nyama ndiyo hupikwa kwa sana."

Kauli niliyotoa ikamfanya mwanamke huyo acheke, na yule mwanamke mweupe ndiyo alikuwa anarudi, naye akawa anacheka pia kuonyesha kwamba alinisikia.

Akakaa pembeni ya mwenzake na kusema, "Unasema kweli, maana siku hizi kila kitu ni mfumuko wa bei tu. Wengi kugusa nyama ni mara moja moja sana."

"Wee! Umeona?" nikamwambia hivyo, nasi kwa pamoja tukacheka kidogo.

"Napenda unavyoongea. Wewe ni kabila gani?" yule mwanamke mweusi akaniuliza.

"Ningesema mimi ni msukuma kwa upande wa mama, ila wa baba ni mpemba. Sivijui hivyo vikabila lakini, maana tupo kimjini-mjini zaidi..."

Nikawaambia hivyo, nao wakacheka kidogo.

"Ndiyo hivyo. Sisi ni wa Mwanza huko, ila hapa jijini ndiyo tumezamia kwa kipindi kirefu zaidi," nikawafahamisha.

"Hata sisi tumekaa huku muda mrefu pia. Sisi ni warangi, baba yao kina Miryam alikuwa mpemba pia kama wewe tu..." mwanamke mweupe akaniambia.

"Aaa kumbe..."

"Ndiyo. Tulikaa Tanga sana, then baadaye jiji likatuita. Ndiyo tuko na binti yetu hapa, tumemtunza-tunza na yeye sasa hivi anatutunza-tunza ahahah... Miryam amekua, na amekuwa mwanamke mzuri sana. Ana bidii, anatujali, anachapa kazi, ni mtu mmoja mpambanaji yaani kila mtu anampenda," mwanamke huyo akaniambia.

Nikatikisa kichwa kuonyesha uelewa, lakini nikijiuliza kwa nini angefikiria habari za huyo Miryam zingekuwa na umuhimu sana kwangu. Ila kwa kuwa nilijua kuna jambo lingine lililokuwa linaendelea lililomhusisha huyo mwenye nyumba, nikaona niulize tu.

"Kwa hiyo... Miryam ni mtoto wako?"

Wanawake hao wakaangaliana kimaswali kiasi, kisha wakanitazama kama vile hawakunielewa vizuri, na mimi singeweza kujua sababu ya kupewa itikio hilo.

Mwanamke yule mweusi akaniuliza, "Kwani mliongea nini na Shadya? Hakukuelezea mengi sana, au?"

Shadya ndiyo alikuwa nani? Dalali wa nyumba au? Mimi nilipata tu tangazo mtandaoni mpaka kufika hapa. Kiukweli hali hii ikaanza kunichanganya sasa. Nikashindwa kujua nitoe jibu lipi au niulize kipi kingine, na wanawake hao wakiwa bado wananitazama, sauti ya honi ya gari ikasikika kutokea nje ya geti, nami nilipowaangalia nikaona wakitabasamu kwa furaha.

Mweupe akaniangalia na kusema, "Amefika. Ngoja nikamfungulie."

Bila shaka alikuwa akimaanisha kwamba mwenye nyumba huyo, Miryam, ndiyo alikuwa amefika, naye akanyanyuka na kunipita kuelekea nje ili kufungua geti.

Nikaendelea kukaa kwa utulivu tu, bado nikiwa najiuliza kama kuna sehemu fulani akina mama hawa walijichanganya katika maongezi yao, ama labda mimi, na kwa nini mtu mzima kama mwanamke huyo mweupe ndiyo anyanyuke kwenda kufungua geti badala ya binti kijana aliyelala tu kwenye sofa hapo hapo. Ila mi' ningejua nini? Maisha yao yalikuwa yao.

Geti likasikika likifunguliwa, muungurumo wa gari ukaingia zaidi kuikaribia nyumba, kisha ukakata na geti likafungwa tena. Mwanamke yule aliyebaki akanisihi niendelee kunywa juice yangu kabla haijashuka kiwango cha ubaridi iliyokuwa nacho, nami nikaichukua glasi na kuanza kunywa tena. Bila shaka pale nje kuna maongezi mafupi yaliyofanywa baina ya mwanamke yule mweupe na mwenye nyumba aliyeingia, labda kumwambia kuhusu ujio wangu, nami nikajiweka tayari ili akifika mikakati zaidi iendeshwe.

Mlango ukafunguka, na wa kwanza kupita akawa ni yule mwanamke aliyenipokea, kisha akaingia mwanamke mwingine kumfatia. Nilikuwa tu ndiyo nimetoka kupiga fundo dogo la juice, na ile nimeshusha glasi na kumtazama mwanamke huyo, macho yangu yakashtuka kiasi kufuatisha na pigo la nguvu moyoni ndani ya kifua changu.

Ilikuwa ni yule mwanamke mweupe niliyekutana naye masaa machache yaliyopita jioni hiyo na kumdanganya kwamba niliumwa kifua ili tu anibebe kwa gari lake, naye baada ya kuwa ameniona, akasimama mlangoni hapo hapo na kuniangalia kwa mkazo sana ulioonyesha hasira kali kunielekea!



★★★★★★★★★

ITAENDELEA

★★★★★★★★★

Full Story WhatsApp or inbox

Whatsapp +255 678 017 280
 
MIMI NA MIMI

A Story by Elton Tonny

Familia, Urafiki, Mapenzi, Kazi, Tamaa, Hila, Usaliti, Siri, Mambo Ysiyotazamiwa

R-rated 18+

Enjoy!


★★★★★★★★★★★★★

SEHEMU YA PILI

★★★★★★★★★★★★★


Mshtuko mfupi niliopata ukanifanya nimeze juice na kuvuta pumzi puani kwa wakati mmoja, nami nikapaliwa. Nikakohoa na kudondosha juice kiasi kutoka mdomoni mwangu, kitu ambacho kilifanya wale wanawake wakubwa washtuke na kunitazama kwa kujali. Nikaendelea kukohoa kwa nguvu, nami nikasimama kabisa nikijitahidi kujizuia lakini nikawa nashindwa.

"Hee... pole kijana wangu... umepaliwa?" akaniuliza yule mwanamke mweusi.

"Akh... kkhh... koh... koh..." nikaendelea kubanja.

"Zawadi, mfatie maji..." akasema hivyo mwanamke huyo.

Nafikiri Zawadi ndiyo lililokuwa jina la mwanamke huyu mweupe, naye akaenda upesi kule jikoni huku mwenzake akinisogelea na kunipiga juu ya mgongo kwa kiganja chake. Aisee nilikuwa nimepaliwa vibaya. Machozi yalinitoka, kooni nikihisi kama vile kimiminika kimeunganisha bomba la pua na mdomo kwa pamoja, nami nikawa namwangalia yule mwanamke mlangoni pale aliyenikata jicho la hasira.

Maji yakaletwa, huku binti yule aliyelala sofani bado akiwa anatafuna tu vidole vyake kama vile hayupo. Nikaanza kunywa maji, na kikohozi cha kupaliwa kikawa kinafifia japo kooni palivurugika sana. Nikamwangalia yule dada pale mlangoni, aliyekuwa amesimama kwa utulivu tu, nami nikahisi aibu na kuangalia pembeni.

"Uko sawa baba?" Zawadi mweupe akaniuliza.

"Akh... ndiyo... niko sawa..." nikajibu huku koo imenibana.

"Pole sana baba... pole..." Zawadi akanibembeleza.

"Miryam... karibu mwanangu. Za huko?" yule mama mweusi akamuuliza mwanamke aliyesimama mlangoni.

Ke! Huyo ndiyo alikuwa Miryam? Nimekwisha.

Miryam mwenyewe alionekana kutaka kunipasua kabisa kwa jinsi alivyokuwa ananiangalia, lakini akaacha kunitazama na kumwambia mama huyo, "Ni nzuri. Shikamooni?"

"Marahaba," wakajibu wanawake hawa kwa pamoja.

Mpaka sasa nilikuwa nimesimama kwa ukaribu na Zawadi mweupe, akiwa anausugua mgongo wangu taratibu, nami nikamtazama mwanamke yule aliyetakiwa kuwa ndiyo mwenye nyumba wangu. Kufikia hapa ningeweza kutambua tu kwamba dili lilifeli, na alikuwa na kila haki ya kunikasirikia maana nilimtendea kama mtoto mdogo vile kule tulipotoka. Ah yaani mambo mengine haya! Eti ilipaswa tu kuwa yeye kati ya maelfu ya watu wote walioishi Dar!

Mwanamke huyo ambaye sasa nilijua aliitwa Miryam, akafunga mlango na kusogea usawa wa sofa alilolalia yule binti, nami nikamwona akimshika sehemu ya shingo taratibu na kuibonyeza kidogo. Binti huyo, Mariam bila shaka, akanyanyuka upesi huku akiwa anatabasamu kwa furaha na kumkumbatia Miryam kwa nguvu sana, utadhani alimpamia. Huyo Miryam akatabasamu pia na kukishika kichwa cha mdogo wake kwa upendo.

Kuwaangalia namna hiyo kukanifanya sasa nitambue kwa nini mwanzoni binti huyo aliponitazama nilifikiri sura yake haikuwa ngeni sana. Ni kwa sababu kwa kadiri kubwa alifanana na dada yake, mtu ambaye nilikuwa nimemwona siku hiyo.

Binti akamwachia dada yake na kumwangalia usoni huku akicheka kwa pumzi za kujirudia-rudia kama mtoto vile, na dada yake akaingiza mkono ndani ya mkoba aliokuwa amebeba na kutoa boksi refu la biskuti na kumpatia. Akalipokea kwa furaha sana na kukaa kwenye sofa, naye akaanza kulifungua ili ale biskuti zake.

Macho ya Miryam yakarudi upande wetu tena. Kiukweli, kiukweli, huyu mwanamke alikuwa mrembo. Hata mara ya kwanza tulipokutana niliona hilo lakini hasa baada ya kujua sasa kwamba alikuwa mrangi ndiyo ikawa wazi zaidi ni kwa nini. Alikuwa mrefu kwa kadiri iliyomfaa mwanamke, mwenye mwili mzuri ulionawiri, kiuno chembamba na miguu mirefu yenye unene wa chupa ya Dompo. Alibeba mapaja manene kiasi yaliyoitesa sketi aliyovaa kwa kuivutisha zaidi kila pande, na hapo bado sikuwa nimemchora huko nyuma vizuri ila nilijua kuna hazina matata iliyokuwa imetunishwa huko.

Alionekana kuwa mwanamke makini sana asiyependa mchezo, na ndiyo jambo ambalo lilifanya nisikazie fikira sana masuala ya uanamke wake zaidi ya masuala yaliyonileta huku; ukitegemea tayari nilikuwa na kesi ya mkosaji kwake.

"Tesha amerudi?" Miryam akauliza.

Sauti yake nzuri ikanifanya nikumbuke namna alivyoniongelesha kwa kujali sana kule tulikotoka.

"Hapana, bado hajaja," mwanamke yule mweusi akamwambia.

Kwa jicho la pembeni, niliweza kumwona Zawadi mweupe akimwonyesha Miryam kwa ishara ya macho kuwa niko hapo, na mwanamke huyo akaniangalia. Alinitazama kwa umakini sana, naye akapiga hatua tatu nne kunielekea huku bado nikiwa nimesimama. Nikaweka uso tulivu tu, nikihisi labda hata natakiwa kusema "shikamoo."

"Ndiyo wewe?"

Miryam akaniuliza hivyo, na kama angekuwa ni mtu ambaye amefika akiwa na malengo mengi ya kumfikisha hapo, basi nisingeweza kujua aliuliza hivyo kuelekea lengo lipi. Lakini langu lilikuwa ni moja. Kuja kupangishwa hapo, basi.

Hivyo nikielewa swali lake lililenga ishu hiyo, nikajibu, "Ndiyo."

Sikuendelea kukohoa tena, na wakati huu nilijivika tu ujasiri wangu wa kiume ingawa bado nilihisi vibaya kwa nilichokuwa nimemfanyia. Baada ya kumpa jibu hilo alinishusha na kunipandisha kama kuonyesha haamini vile, nami nilielewa sababu kuwa yeye kutopendezwa nami. Haingejalisha tena kuhusu yaliyotokea ikiwa tu ningemwomba samahani, na kama asingeikubali basi fresh, ningetafuta tu sehemu nyingine ya kukaa.

Nikawaangalia mama zake kwa ufupi, ambao walitutazama sisi wote kwa umakini, nami nikamwangalia Miryam usoni na kusema, "Naomba kuongea nawe Miryam... kibinafsi."

Aliniangalia machoni bila kukwepesha hata kidogo, na wanawake wale wawili wakaendelea kunitazama.

"Kama ni sawa. Twende chumbani, halafu tuzungumze," nikamwambia hivyo kwa sauti yenye uhakika.

Akanikazia macho yake na kuuliza, "Unataka... nikupeleke chumbani?"

"Ndiyo. Nionyeshe chumba... ili tuongee pia," nikamwambia hivyo.

Nilikuwa namwonyesha kwa lugha ya macho kwamba nilihitaji tuzungumze kuhusu tatizo letu, lakini aliniangalia utadhani amechanganyikiwa. Akawatazama wale wanawake kwa mshangao fulani hivi, na hata mimi nilipowaangalia nikaona wananitazama kimaswali kiasi.

Lakini Zawadi mweupe akaachia tabasamu na kusema, "Ni sawa tu... nyie nendeni mkaongee... sisi tutakuwa hapa hahah..."

Nikamwangalia Miryam usoni na kuona ni kama vile anashangazwa na mimi, na nilichukulia hiyo kuwa kwa sababu labda hakutaka kunipeleka chumbani. Lakini akaangalia pembeni kiasi na kushusha pumzi, kisha akaanza kutembea taratibu kuuelekea upande ambao bila shaka ungefikia vyumbani.

Sikuhitaji kupewa agizo, hiyo ilikuwa ishara tosha kwangu. Nikawapa tabasamu hafifu wanawake hao wawili na kubeba begi langu, kisha nikaanza kumfata mwanamke yule. Sijui ni kwa nini lakini eti wakawa kama vile wanashangaa kuona nimelibeba na begi kabisa. Ah ugeni huu! Bora nisingelazimisha kutafuta huduma ya aina hii maana hali yote ya hapa ilizidi kunichanganya.

Kumfata mwanamke yule kulinipeleka upande wa nyumba hiyo uliokuwa na korido fupi lenye milango mitatu ya vyumba vya kupumzikia, na kona nyingine iliyopeleka mtu kwenye choo na bafu. Angalau sasa niliweza kulichora umbo lake huko nyuma, na alikuwa amebarikiwa kubeba mzigo wa maana!

Yeye akaingia ndani ya mlango wa chumba cha mwishoni, na nilipofika hapo nikakuta amesimama mlangoni kama kuniruhusu niingie, nami nikampita na kuingia. Bado alikuwa akinitazama kimashaka fulani hivi, lakini baada ya mimi kuingia ndani humo mashaka yangu ndiyo yakapanda zaidi.

Chumba hicho kilikuwa kizuri; kizuri mno. Lakini ulikuwa uzuri ambao ulimfaa mwanamke, si mwanaume. Vitu vingi sana vilikaa kimaua-maua tu, kuanzia mashuka yaliyotandikwa mpaka kabati la nguo lililopambwa kwa maua, na hata upande mmoja kulikuwa na dressing table, yaani meza ya kujipambia mwanamke iliyo na kioo kirefu pamoja na vipodozi na manukato!

Nikatembea na kuingia ndani zaidi nikiwa nakiangalia kwa umakini, fikira zikiwa kwamba huenda kuna mwanamke aliyekuwa akikaa humo na sasa hakuwepo, ndiyo mimi ningechukua nafasi yake. Siyo kuchukua nafasi ya kuishi kike, ila nafasi ya kulala kwenye chumba!

"Umekuja na begi kabisa?"

Sauti yake Miryam iliyouliza swali hilo ikanifanya nimgeukie na kumtazama. Bado aliniangalia kana kwamba hanielewi hata kidogo, na mimi kiukweli nilikuwa nimeanza kuchanganyikiwa.

"Chumba ndiyo hiki?" nikamuuliza.

"We' unakionaje, ni sebule?" na yeye akaniuliza.

"Hapana, namaanisha... kina mwonekano wa kike sana. Ama ndiyo mnavyopamba siku hizi kwa ajili ya wageni? Nikilala humu nitajihisi kama princess," nikasema.

"Kulala kivipi?" akaniuliza.

"Kulala kulala. Si ndiyo nitalala humu?"

"Hakuna chochote kilichopangwa, unanielewa? Huwezi kulala humu..."

Njia aliyotumia kunisemesha ilijaa kisirani sana, na tayari nilijua sababu kuwa nilimuudhi kwa hiyo nikachukulia yote hayo kuwa majungu tu. Nikaweka begi chini na kusogea mpaka kufikia aliposimama, naye alikuwa ananitazama usoni kwa umakini mno.

"Sikiliza dada. Najua hatujakutana kwenye mazingira mazuri, na ndiyo maana nimeomba uje nami humu ili nikuombe tu samahani. Huna sababu ya kuendelea kunikasirikia, mimi siyo mtu mbaya... muda ule nilihitaji tu msaada, lile eneo sikulifahamu, na usiku ulikuwa unaingia... ndiyo maana nikafanya vile..." nikamwambia hivyo kwa sauti ya chini.

Akaangalia pembeni na kubana midomo kwa njia fulani ya kukerwa kiasi.

"Hayo ya saa zile tuyasahau. Me napenda amani, halafu na hapa nimepapenda. Nataka nikae hapa," nikamwambia.

Macho yake mazuri yakarudi tena kwangu, akinitazama kama vile bado hanielewi, naye akasema, "Na wewe nisikilize. Sipendi michezo isiyo na faida. Umeanza kunifanyia michezo huko nyuma, na umeileta mpaka hapa. Kuna lolote lililopangwa kukuruhusu ulale chumbani kwangu?"

Nikakunja uso kimaswali kiasi. Chumbani kwake? Sikuelewa vizuri.

Akashusha pumzi kiasi kama kujipa utulivu, kisha akaanza kusema, "Nisikilize Festo..."

A-ah! Festo gani tena? Mbona alikuwa ananichanganya?

"Mimi sitakuwa mwongo kwako. Hili suala haliwezi kufanikiwa. Ni sawa wakubwa wetu wanataka kutusaidia lakini siko tayari kuanzisha mahusiano na wewe, achilia mbali kuolewa..."

Eh! Nikabaki kinywa wazi kiasi huku namwangalia kwa umakini, kwa sababu kiukweli alikuwa ameniacha Mbezi.

"Kama wewe ni mtu mzima naweza kuamini kwamba utanielewa, na ndiyo maana niliyaruhusu haya yote ili tukutane, niweze kukwambia wewe kama wewe. Ndoa ni jambo zito, na bado... bado siko tayari. Sijui hata Shadya aliwaza nini kudhani mimi na wewe tungeendana kwa kweli... kwanza unaonekana kabisa ni mdogo kwangu. Mimi kwa ombi hilo... makubaliano yote ambayo amefikiri tunaweza kufanya... siko tayari. Nadhani inaeleweka kaka'angu..." akayasema hayo kwa sauti tulivu.

Niliinamisha uso kiasi nikiwa natafakari yote aliyosema, na sasa kila kitu kikawa kimeeleweka kwangu.

Hawa wanawake walikuwa wanamsubiria mtu mwingine tofauti na mimi, ambaye labda alikuwa na mipango ya kuja kumchumbia huyu dada. Shadya ndiyo alikuwa mshenga, muunganishi wao. Kwa hiyo mimi nilipofika hapa, wale wanawake wawili walifikiri mkwe ndiyo kafika, na kwa kweli hali nyingi zilikuwa zimeingiliana kwa njia iliyofanya nijikute natendewa kwa njia ambayo aliistahili huyo Festo aliyetarajiwa kufika. Mpaka wali wake na nyama niliula!

Nikajikuta naachia tu tabasamu na kutikisa kichwa kwa kutoamini jinsi hali hii ilivyonifikisha mbali namna hiyo.

Miryam alipoona natabasamu, akaniuliza hivi, "Nilichokisema kimekupa furaha, au?"

Nikamwangalia, nami nikashindwa kujizuia kucheka kidogo kwa pumzi, kisha nikasema, "Ndiyo, ndiyo, sawa."

"Usiseme sawa, nimekwambia hapana," akasema.

"Ndiyo, sawa imemaanisha hapana..." nikasema hivyo.

Akaniangalia kama vile hanielewi.

"Pole dada. Kuna mwingiliano umeingiliana hapa... mimi siyo unayemdhania," nikamwambia.

"Nini?" akauliza kwa sauti ya chini.

"Mimi nimekuja huku kwa...."

Maneno yangu yakakatishwa baada ya kumwona Zawadi mweupe akiwa amefika nje ya chumba hicho, na Miryam akageuka kumtazama pia. Uso wa mama huyo ulionekana kutatizika kiasi, naye akaendelea kusimama hapo huku akiniangalia kimaswali.

Miryam akamsogelea karibu na kumuuliza kuna nini, naye akamwambia kwamba Shadya alikuwa amefika, pamoja na wageni. Wote kwa pamoja wakanitazama tena usoni, nami nikalifata begi langu na kulibeba tena, kisha nikawasogelea na kuwaomba turudi pamoja sebuleni, nao wakakubali.

Tulipofika pale sebuleni, watu walikuwa wameongezeka, isipokuwa binti yule mdogo niliyemwacha akila biskuti ndiye ambaye sikumkuta kwa wakati huu. Wageni niliowakuta hapo walikuwa watu wazima wanne, wanawake wawili, wanaume wawili. Wanaume walikuwa watu wazima kwa pamoja kufikia miaka 40 hivi, pamoja na mwanamke mmama mwenye kama miaka 60 hivi. Wote walisimama kukaribiana na masofa baada ya kumwona Miryam. Ukijumuisha na yule mwanamke mweusi pia, sasa kila mtu hapo akawa amesimama.

Kwa wale wageni waliofika, mwanamke mmoja mwenye umri mkubwa kufikia miaka 45 hivi aliyevalia baibui na ushungi, aliniangalia kiudadisi sana, kama kujiuliza mimi ni nani. Kila mmoja wao alielekeza umakini wake kwangu isipokuwa Miryam, ambaye alisimama tu kwa utulivu baada ya kuwaamkia wawili wa wageni wale ambao walimzidi kiumri. Mimi pia nikawaamkia wote, nao wakanijibu vizuri kasoro mwanamke huyo aliyevaa ushungi.

"Huyu ni nani?" mwanamke huyu aliyevaa ushungi akauliza.

Wanawake wale walionikaribisha wakanitazama tu kama vile wanasubiri mimi ndiyo nitoe jibu, na kwa kutumia akili ya haraka, nikamuuliza mwanamke huyo, "Wewe ndiyo Shadya, eti?"

Huyo mvaa ushungi akatikisa kichwa kukubali.

"Aaa sawa. Aisee... kuna mabiti yamemix vibaya sana hapa ahah... nimejichanganya kidogo," nikawaambia.

Wote sasa wakawa wananiangalia.

"Mimi natokea Sinza, nimekuja Mbagala leo kuna hii nyumba nilikuwa natakiwa kufikia, sasa... ramani imenileta mpaka hapa, nikafikiri ndiyo penyewe, sijui nimekosea wapi..." nikawaambia.

"Ulikuwa unaenda kufikia wapi kwani?" Shadya akaniuliza.

Ongea yake ilikuwa sharp, akionekana kuwa mswahili mkomavu, nami nikasema, "Kuna nyumba inafanyiwa upangishaji mpya wa vyumba... niliwasiliana na aliyetoa tangazo, sasa tukakubaliana nije ili... nikae hapo."

"Lakini ramani ikakuleta hapa?" akauliza mwanamke yule mweusi, ndugu ya Miryam.

"Ndiyo," nikamjibu.

Zawadi mweupe akaonekana kutafakari kitu fulani, naye akaniuliza, "Umesema nyumba ya kupangishwa?"

Nikatikisa kichwa kukubali.

"Ahaa... hiyo nyumba ni hapa hivi pembeni, kwa huyu jirani yetu. Ankia si alikuwa ameshatuambia anataka kupanga na mtu juzi juzi?" Zawadi akawasemesha wakina Miryam.

"Eeeh ndiyo..." akajibu yule mwenziye nisiyemjua jina, la sivyo labda na yeye ningemwita Zawadi mweusi.

"Baba ni hapo hivi... ukivuka huu ukuta wetu," Zawadi mweupe akaniambia.

"Hii nyumba ya pembeni kumbe?" nikauliza.

"Eee..." akaitikia.

"Ina maana hukuwa umewasiliana na Ankia akwambie nyumba yake ilipo?" Shadya akaniuliza.

"Tuliwasiliana kwa WhatsApp, nikamwambia nitakuja siku yoyote wiki hii, sema nimechelewa tu kidogo leo... kuna katatizo kalitokea," nikasema hivyo na kumtazama Miryam.

Alikuwa ananitazama usoni kwa umakini, nami nikaangalia pembeni.

"Kwa hiyo alipofika hapa mkafikiri ndiyo Festo?" Shadya akawauliza wale wamama huku akimwonyeshea huyo Festo kwa kiganja chake.

Nikamwangalia jamaa. Alikuwa mmoja wa wale wanaume wawili waliosimama hapo, mrefu kiasi kunipita, mweusi, na mwenye mwonekano nadhifu wa kiutu uzima. Alikuwa na sura tulivu tu, na ndevu nyingi kidevuni pekee, na kwa kumtazama upesi ningeweza kukisia alikuwa mtu mwenye pesa. Bila shaka wale wengine waliokuwa naye walikuwa ndugu zake ama wazazi, nami nikamwangalia Miryam na kuona ameangalia chini tu.

"Eee ndiyo, tukafikiri ni yeye. Jamani! Haya ni makubwa... naombeni radhi sana," Zawadi mweupe akasema hivyo.

Nilijisikia vibaya kiasi ukitegemea na ukweli kwamba wanawake hao walinitendea kwa ukarimu sana. Shadya akawa ananiangalia kama vile hanitaki, yaani hataki niwe hapo, na kiukweli sikutakiwa kuwa hapo. Huenda hata ningesababisha wadhani mchumbiwa ameshaliwa!

Nikalivuta begi langu vizuri mgongoni na kusogea usawa wa Zawadi na mwenzake, nami nikasema, "Asanteni sana, japokuwa tumekutana katika mazingira yenye kuchanganya lakini... nashukuru kwa ukarimu wenu. Msosi ulikuwa mtamu sana."

Zawadi mweupe akatabasamu kiasi na kunishika begani, na mwenzake akatikisa kichwa tu kuonyesha uelewa.

Nikawatazama wageni, ambao bado walikuwa wamesimama wakiniangalia, nami nikasema, "Jamani, msiendelee kusimama, kaeni. Karibuni mkae."

Shadya akaanza kuwaambia wageni wakae kweli, na nilipomwangalia Miryam nikakuta amenikazia sura. Najua alikuwa ananishangaa kwamba mimi si mwenyeji hapo lakini nawaambia wageni wakae kana kwamba palikuwa kwetu, nami nikatabasamu kidogo na kisha kuuelekea mlango.

Nikaufungua na kuwapungia mkono kuwaaga, nikisema ningefika tu kwenye nyumba ya huyo Ankia na kukutana naye kama mwenye nyumba wangu halisi hatimaye, na akina mama wale wakanipa heri na usiku mwema.

Nilipomwangalia Miryam tena, alikuwa amenikazia tu jicho lake kwa umakini, na sijui ni nini tu lakini njia yake ya kununa ilimfanya apendeze sana kiasi kwamba sikuweza kujizuia kutabasamu kila nilipomwona namna hiyo, nami nikafungua tu mlango na kutoka nje.

Nikaanza kuondoka hapo huku nikiwaza jinsi bahati ya leo ilivyokuwa ikipingana sana na mimi, kuanzia kuharibikiwa na daladala mpaka kuingia kwenye sebule ya mhusika nisiyetakiwa kukutana naye. Ila huyo Miryam alikuwa ameifanya jioni hii iburudishe sana siyo siri.

Nikatoka zangu mpaka nje ya geti, na hapo nje lilikuwepo gari aina ya Volkswagen Touareg nyeusi, bila shaka ikiwa ni ya mchumba Festo. Nikawaza ikiwa Miryam alimaanisha kweli kile alichokuwa ameniambia alipofikiri mimi ndiyo nimekuja kumchumbia, basi hata huyo Festo angerudi kwao mikono mitupu. Ila kuna kitu chochote kile ambacho pesa haiwezi kubeba siku hizi? Aa wapi!

Nikavuka tu nyumba hiyo na kwenda ya pembeni. Kwa nje, kulikuwa na duka la bidhaa, na ndani niliweza kumwona mwanamke mwislamu akiwa ameketi huku akinyanyua kichwa chake kunichungulia kutokea ndani humo, nami nikampuuzia tu na kuingia ndani ya geti jepesi la vyuma vyembamba kama milango ya gereza.

Lilikuwa wazi, nikaelekea ndani zaidi ya upande huo, na ukuta ule uliozitenganisha nyumba hizo ulikuwa na... niseme urembo labda, urembo wa matundu manene kuuzungukia ulioruhusu kuiona nyumba ya akina Miryam kwa nje, pale ndani ya geti lao. Yaani kwa hapo ningeweza kuliona lile gari la pickup la Miryam, na bila shaka wao pia wangeona upande huu wa nje wa hii nyumba niliyofikia.

Nikaenda mpaka kwenye mlango wa nyumba hii sasa. Ilikuwa pana pia, lakini si sana kama ya akina Miryam. Kulikuwa na ubaraza mpana uliojengewa matofali madogo-madogo ya simenti yenye mtindo wa urembo, nikaona jengo lingine dogo kwa nje lenye milango miwili kwa ukaribu; bila shaka choo na bafu, sinki fupi la kuoshea vyombo bila shaka likiwa limejengwa kutokea ukutani, na kamba za kuanikia nguo kwa juu.

Hakukuonekana kuwa na watu wengi hapa na inawezekana aliye ndani tayari alikuwa amejifungia kwa ndani maana ilikuwa saa nne hii, ila nisingeweza kujua. Nikaugonga mlango mara tatu na kusimama kwa kusubiri. Haikuchukua muda mrefu sana na mlango ukafunguliwa, na hapo mbele yangu alisimama mwanamke mtu mzima ambaye kwa haraka ningeweza kukisia alikuwa kwenye miaka ya 30 hivi.

Alikuwa na mwili ulioukimbilia unene, mwenye uso wa duara na midomo mikubwa ya denda nzito. Macho yake yakiwa ya kungu kiasi, sura yake ilipendezeshwa kwa weupe fulani hivi uliotokeza sana, aidha wa mapodozi ama kujichubua, kwa kuwa rangi ya mikono yake haikuwa nyeupe namna hiyo. Alivaa kilemba kilichofunika nywele zake ama labda kipara, dera pana mwilini, lakini bado liliuchora mwili wake vyema kuonyesha kwamba alikuwa na mapaja na miguu minene, na puani aliweka pini ndogo ya urembo.

Alinitazama kwa macho fulani... laini, kama vile hajiulizi nilikuwa nani, lakini tena akisubiri kujua mimi ni nani.

Ingawa alionekana kuwa mkubwa kwangu, nikamwambia, "Mambo vipi?" kwa sauti tulivu.

"Poa," akajibu hivyo na kubana midomo yake.

"Wewe ndiyo mwenye mji?" nikamuuliza.

"Ndiyo. Wewe ni nani?" akaniuliza.

"Mimi ni yule kijana tuliyewasiliana WhatsApp, kuhusu ile ishu ya kuishi kwa kulipa kodi kwenye nyumba yako..." nikaeleza.

"Aaaa, ndiyo wewe?"

"Ndiyo."

"Sawa. Karibu, karib... karibu ndani," akanikaribisha.

Aliacha uwazi zaidi ili nipite, nami nikaingia mpaka sehemu ya sebule huku nikisikia anaufunga mlango.

Sebule hii haikuwa pana sana, lakini ilipambwa vizuri mno. Vigae sakafuni, vilivyofunikwa kwa kapeti zito jekundu lililobeba meza ndogo ya kioo, masofa mawili marefu na moja lingine dogo yaliyopangwa kuizunguka meza hiyo, feni kwenye kona moja ya ukuta, na TV ndogo ya flat screen iliyobebwa kwa vyuma vyake vilivyounganika na ukuta juu kiasi. Kulikuwa na mapambo ya midoli kwenye meza ile ya kioo na masofa yalipambwa kwa kutunikiwa vitambaa; bila shaka kuficha zaidi ngozi zake zenye nyufa nyingi kutokana na kuchanika.

Niliona upande mwingine wa mbele zaidi wenye ukuta uliokuwa umetenganisha milango miwili, bila shaka ya vyumba, na upande mwingine ulionyesha sehemu ya jikoni ambayo haikuwa na mlango. Palinukia ile harufu ambayo wanawake waislamu hupenda kuivaa, sijui manukato ya kuchomwa, kitu kama hicho. Lakini huyu hakuonekana kuwa mwislamu.

Nikamgeukia mwenyeji wangu, ambaye alikuwa anasogea upande wangu huku amevibana viganja vyake kwa mbele, na akiniangalia kwa macho yenye subira. Nikamwangalia kwa macho yenye upendezi, naye akatabasamu kwa haya kiasi na kuangalia chini. Athari niliyonayo kwa wanawake!

"Kwa hiyo... nimefika sehemu sahihi?" nikamsemesha.

"Eeee... ndiyo hapa," akajibu.

"Najua hukutarajia nije leo, halafu usiku sana..."

"Hapana, mbona bado mapema? Hamna shida. Karibu sana," akasema kwa sauti yenye kuvutia.

"Asante. Uko mwenyewe?" nikamuuliza.

Akatikisa kichwa kukubali mara moja, kwa njia ya shau.

Nikatabasamu kidogo na kusema, "Poa, basi... nionyeshe chumba af'... tuongee mengine."

Akanipita tu na kuuelekea mlango wa mbele zaidi kati ya ile miwili, nami nikamfata. Ningetaka kumuuliza upesi kwa nini aiishi peke yake kwenye hiyo nyumba, ikiwa alikuwa na familia labda, ama kama haikuwa yake yeye na alikuwa mtunzaji tu, lakini hayo yangepaswa kuja baadaye.

Hapa suala lililokuwepo ni kwamba ningeishi kwenye nyumba hiyo pamoja na mwanamke bila mtu mwingine kuwepo, kwa hiyo ya kutegemea yalikuwa mengi. Yale mambo yetu yale! Mwanamke mwenyewe alikuwa anatembea kwa kutikisa kweli maana na yeye alikuwa na zigo tenteme, nami nikaingia pamoja naye ndani ya chumba hicho.

Kilikuwa na mwonekano safi na mpangilio mzuri wa vitu vichache tu vilivyokuwemo. Kulikuwa na kitanda chenye ukubwa wa nne ya sita, kilichotandikiwa shuka jeupe na safi sana. Mito miwili ilikipendezesha zaidi, na neti ilifungwa juu kwenye ceiling board kukielekea, ama kwa kiswahili tulivyozoea kuiita, basi ni singibodi. Kulikuwa na kabati la kuwekea nguo ukutani, na uwazi mpana kiasi sakafuni kutokea mwisho wa kitanda ambao ungeniruhusu kuwekea vitu vyangu vingine kama viatu. Na palinukia harufu yake huyo mwanamke.

Nikapatazama kwa kuridhishwa sana kwa kuwa palifanana na jinsi nilivyotaka pawe kabisa, kawaida, patulivu, angalau kwa jinsi palivyoonekana. Nikamgeukia mwenyeji wangu na kukuta ananiangalia tu usoni, lakini ndiyo akakwepesha macho yake baada ya yakwangu kugongana na yake.

Nikashusha pumzi na kusema, "Pazuri. Pametulia."

"Ndiyo. Huku hamna makelele yaani unalala vizuri kabisa," akasema.

"Na mbu kama wote..."

"Ahahah... unachoma tu dawa, af' unashusha neti. Hawasumbui. Hata usiposhusha neti, ukishachoma tu dawa wanaisha, unalala kwa amani."

"Sawa. Tutakuwa tunaishi kinyumbani zaidi kwa hiyo mengi ya hapa utanielekeza ili niendane vizuri na mazingira, au siyo?"

"Hamna neno."

"Kwa hiyo, utataka nikulipe kila tarehe ya mwanzo wa mwezi, ama mwishoni?" nikamuuliza.

"Wewe tu," akaniambia hivyo huku akiangalia pembeni.

"We' ndiyo uniambie, si ndiyo mwenye nyumba wangu?"

"Ahah... ni wewe tu, me... hata ukilipia sa'hivi au mwishoni mwa mwezi sawa tu."

"Mh! Mbona kwenye tangazo ulisema malipo kwanza? Je nikikwambia nitakulipa mwishoni halafu nikakimbia kabla mwezi hujaisha?" nikamuuliza kichokozi.

"Hahaah... hapana, huwezi. Kesho tunapaswa kwenda kwa mwenyekiti ukasaini pepa tulani la makubaliano. Kwa hiyo ukikimbia jela inakuhusu," akasema hivyo na kuniangalia kwa ufupi.

Alionekana kunionea aibu, yaani hakutaka kunitazama usoni kwa muda mrefu, nami niliona furaha fulani ndani yake iliyotokana na matarajio mengi ya kupata mteja mwenye sura nzuri. Najua mnaelewa, siyo kwamba najisifu sana!

Nikamwambia, "Aaa, basi poa. Uko makini kumbe."

"Eee... lazima kuwa makini. Hapa mjini, ukizubaa unaachwa kweli," akaniambia huku akitabasamu.

"Safi sana. Ila usijali sitakukimbia. Na... nataka nikulipe sasa hivi ya miezi miwili kabisa," nikamwambia.

"Siyo lazima sasa hivi kaka, wewe... pumzika tu. Mengine hata kesho," akaniambia kwa njia fulani yenye kubembeleza hivi.

Dah! Haya bwana. Nikamwambia, "Asante. Jina lako Ankia, si ndiyo?"

Akaniangalia kimaswali kiasi huku akitabasamu, naye akauliza, "Umejuaje? Hatukuambiana majina WhatsApp. Ama umesoma kwenye namba jina la usajili?"

"Hamna, nimelijua leo, muda sio mrefu. Wakati nakuja nikapotea njia, nikaingia kwenye nyumba hiyo jirani nikifikiri ndo' kwako..." nikasema.

"Wewee!" akanena hivyo kimshangao kiasi.

"Ndiyo. Wakaniambia nimekosea, wakanielekeza hapa na jina lako ndo' nimelijua kutoka kwao."

"Aisee... hahaha pole mwaya," akaniambia huku akitabasamu.

"Sijui ingekuwaje kama ningeingia kwenye nyumba ya wanoa visu," nikamtania.

Akacheka kidogo na kusema, "Wangekunoa. Huku wahuni wengi unajua..."

"Na wewe ukiwemo?"

"Akhaa... mie nakulaga zangu za kistaarabu tu, hayo maisha ya waswahili tunawaachia wengine ndiyo wanayawezea..."

"Eti ehh..."

"Eeeh..."

"Wewe na nani mwingine?"

"Mimi na hao majirani zangu uliotoka hapo kwao, yaani hatuna zile shobo na watu wengi. Tunaishi kivyetu sana. Watu wa huku wakikuzoea mno ni mpaka nguoni..."

"Hahah... hiyo iko kila sehemu," nikasema.

"Yeah, sioni kama inafaa. Kwa hiyo... wewe unaitwa nani?" akaniuliza.

"JC," nikamwambia.

Akatabasamu kidogo na kusema, "JC. Jina zuri."

"Asante."

"Ni kifupi cha?"

"Jina Chafu," nikamwambia kiutani.

Akacheka kidogo na kusema, "Sawa. JC ndiyo inafaa zaidi."

Nikaweka begi kitandani pale, na huwezi amini mpaka kufikia hapo bado nilikuwa nimelibeba.

"Kuna joto," nikasema hivyo.

"Usipime yaani. Tunajimwagiaga kabla ya kulala angalau mwili unakuwa fresh," akasema hivyo.

Sikutoa itikio lolote kwa kauli yake, bali nikawa nafungua zipu ndogo ya begi ili nitoe baadhi ya vitu vyangu. Bado akawa ameendelea kusimama hapo hapo mlangoni kama vile kuna kitu alikuwa anasubiria, nami nikamtazama usoni.

Akaibana midomo yake na kuangalia pembeni kama vile anajishauri hivi, kisha akauliza, "Nikakuwekee maji... bafuni ujimwagie?"

Swali hilo likanifanya nitabasamu kwa mbali huku nikimwangalia kiumakini, naye akatabasamu kwa haya na kuangalia chini. Kiukweli... au basi tu!

Pigo zake za kischana zilieleweka vizuri sana kwangu ingawa alikuwa mkubwa, na hayo madoido aliyoweka yalinifanya nijihisi kweli ni kama nimefika nyumbani kwetu kabisa. Chakula cha nguvu nilikula pale kwa akina Zawadi mweupe, na muda huu nikapewa ofa ya kutengewa maji bafuni. Hayo ndiyo mambo sasa!

"Utakuwa umenisaidia sana, asante," nikamwambia.

Akatabasamu na kuibana midomo yake, kisha akaondoka kwenda kukamilisha zoezi hilo.

Nikacheka kidogo kwa pumzi na kutikisa kichwa, nami nikaendelea kutoa vitu vyangu. Ilikuwa wazi kwamba Ankia alivutiwa na mimi. Sidhani sana ikiwa kama angepata mpangaji mwanamke ama mzee angemtendea kwa njia kama aliyonionyeshea, lakini kwangu hilo lilikuwa jambo la kawaida sana.

Nilitoa vitu kama vyote na kupangilia vingi kabatini, nikiweka viatu vyangu pea mbili sakafuni na kisha kuvaa sendo (sandals) ngumu za kimasai miguuni. Nilikuwa nimeshavua nguo za safari na kubakiza kaushi nyeupe na kaptura ya mazoezi, nami nikaweka taulo yangu ndogo begani ili niweze kuelekea bafuni kupunguza fukuto mwilini. Kabla hata sijafungua mlango kutoka kwenye chumba hicho, ukagongwa taratibu, nami nikimjua mhusika aliye hapo nikasema tu ingia, na Ankia akausukuma na kupita ndani kiasi.

Nilipomwangalia niliona akinitazama mikononi, ikiwa wazi alipendezwa na uimara aliouona, naye akasema, "Nimeshakuwekea maji bafuni."

Nikamwambia, "Asante."

Kisha nikachukua simu yangu pamoja na chaja na kusogea alipokuwa, naye akaanza kuelekea sebuleni huku nikimfuata nyuma. Tulipofika hapo, nikamwomba aniwekee simu ipate chaji, naye akaipokea na kwenda kuichomeka kwenye moja ya matundu ya 'extension' yake.

Mimi nikaenda zangu bafuni, nikatumia dakika chache kujisafisha vizuri maana sabuni ilikuwemo mule mule, kisha nikarejea tena ndani. Nilimkuta mwanamke huyo akiwa amekaa sofani tu, akiikunjia miguu yake kwa pamoja huku akiwa makini kutazama tamthilia ya Ottoman.

Sikumsemesha na kwenda tu chumbani, nami nikajikausha maji, nikajioaka mafuta mazuri ya mwili na kutengeneza nywele vizuri, kisha nikaenda sebuleni tena huku sasa nikiwa nimebadili mavazi kwa kuvalia T-shirt ya njano yenye mikono mifupi pamoja na bukta ya mazoezi.

Nikamtazama mwanamke huyo. Aliniangalia pia upesi na kutabasamu kwa mbali, kisha akasimama na kusema angekwenda kuniwekea chakula. Lakini nikamzuia na kumwambia nilishiba, hivyo labda tu anipatie maji ya kunywa. Akatii kwa kuyafata na kuniletea, kisha akakaa tena huku mimi nikiyashusha kooni taratibu.

Angalau maji ya kunywa aliyachemsha, ingawa bado yalikuwa ni ya chumvi na mimi sikupendelea maji ya chumvi, lakini nikayanywa yote na kumtazama tena. Alikuwa amekaa kama vile ameshika tama, yaani akisikiliza kwa makini tatsiri za kiswahili kwenye tamthilia ile, nami nikamsemesha hatimaye.

Tulianza kwa kuiongelea Ottoman, kisha kuhusu kilichofanya nichelewe kufika huku hadi kuingia kwa jirani yake, na mambo ya mitaa iliyozunguka eneo lote la Mzinga na tabia za watu, na nilijitahidi kufanya maongezi yaburudishe kwa kumchekesha kwa utani wa hapa na pale. Hatukuwa tumezungumza kuhusu maisha yetu ya kibinafsi, na ni kitu kilichofaa kwa mwanzo wa kujuana.

Alikuwa ana nia ya kunichomea dawa za mbu chumbani lakini zilikuwa zimemwishia, na akasema kwa muda huo tayari duka la pale nje lingekuwa limefungwa hivyo asingeweza kwenda kununua zingine maana maduka mengine yalikuwa mbele huko. Nikamwambia aondoe shaka, ningelala ndani ya neti tu, kama yeye vilevile.

Tamthilia ya Ottoman ilipokwisha, akanyanyuka na kusema yeye pia angekwenda kujimwagia maji kabla ya kulala, kisha akaenda chumbani kwake. Hazikupita dakika nyingi sana naye akawa ametoka huko, nami nikamwangalia jinsi alivyokuwa. Alivaa khanga moja kutokea kifuani mpaka kufikia magotini, na mwili wake tepetepe ulinyumbulika kwa makusudi mengi sana alipopiga hatua kuja upande wangu ili atoke mlangoni na kwenda bafuni.

Nikatazama tu runinga na kujitahidi kuweka utulivu, lakini tumawazo twingi twa kihuni tulikuwa tunanisumbua-sumbua sana kichwani. Akanipita na kutoka nje, nami nikajikaza tu nisicheke maana niifurahia sana mchezo wa hapa. Ile kitu unayojua inaweza kutokea lakini unajifanya kama huelewi somo, ndiyo iliyokuwa kitu yangu. Kweli nikaendelea kujifanya kama somo halieleweki kwa kutulia tu.

Simu yangu ikaanza kuita, nami nikaichukua na kuona niibebe tu ili nikazungumzie chumbani; aliyekuwa ananipigia alistahili maongezi ya faragha zaidi, yaani mama yangu. Nilipenda sana kuonngea naye nikiwa sehemu tulivu. Nilitumia dakika nyingi kuzungumza naye kiasi kwamba sikutambua kama muda ulisonga mpaka nilipoona taa za sebuleni zikizimwa, nami nikaelewa bila shaka Ankia alikuwa amesharudi na sasa alijiandaa kwenda kulala.

Nikamaliza maongezi ya kwenye simu na kuamua kutoka chumbani ili niifate chaja maana nilihitaji kuiweka simu ipigwe moto usiku mzima mpaka majogoo. Taa ya upande wa jikoni bado iliwaka kwa hiyo ndani hapo kuelekea sebule palikuwa na mwanga hafifu ulioruhusu kuona mambo vizuri, na ndiyo nilipofika sebuleni tu nikasimama ghafla baada ya kumkuta Ankia akiwa bado hapo.

Nilifikiri labda tayari angekuwa chumbani kwake, lakini haikuwa hivyo. Sasa nilithibitisha kwamba alikuwa na nywele za kusukwa kichwani maana hakuwa na kilemba tena. Alikuwa amesimama usawa wa TV yake akionekana kuifunika kwa kitambaa.

Kwa sababu TV ilikuwa juu kiasi, alinyoosha mikono yake kuiwekea kitambaa hicho huku akiinyanyua nyayo zake za miguu, na hivyo khanga fupi yenye kulowana aliyokuwa amevalia iliyaacha mapaja yake wazi na kulichora umbo lote la nyuma kwa njia iliyoamsha hisia zangu ghafla, na kwa nguvu mno.

Inaonekana hakujua niko nyuma yake, ama labda alijua, lakini hakugeuka upesi, na alipomaliza tu kuifunika TV yake, bila kugeuka akawa ameifungua khanga yake ili airekebishe vizuri na kuifunga tena mwilini, na alipokuwa tu ndiyo anafanya kuirudisha akawa amegeuka.

Kuna kitu chenye kusisimua kiliruka ndani yangu baada ya kuuona mwili wake wa mbele kwa kifupi sana, naye akaonekana kushtuka kiasi baada ya kukuta nimesimama hapo!




★★★★★★★★★

ITAENDELEA

★★★★★★★★★

Full Story WhatsApp or inbox

Whatsapp +255 678 017 280
 
MIMI NA MIMI

A Story by Elton Tonny

Familia, Urafiki, Mapenzi, Kazi, Tamaa, Hila, Usaliti, Siri, Mambo Ysiyotazamiwa

R-rated 18+

Enjoy!

★★★★★★★★★★★★★

SEHEMU YA TATU

★★★★★★★★★★★★★


Nikamwangalia machoni, nikiwa nimetulia tu. Tayari sasa alikuwa ameufunika mwili wake, lakini aliendelea kushikilia pale pa kufungia khanga kwa mikono yake yote kama vile amegandishwa, kwa sababu ya kunitazama kwa umakini, ama labda butwaa. Ni wazi hakuwa amehisi uwepo wangu nyuma yake.

Lakini hali ya utulivu tu aliyoweka, ilinipendeza sana. Hakuwa na makeke. Jinsi nilivyomwangalia machoni, ndivyo ambavyo na yeye pia aliniangalia. Ni kama alikuwa anasubiri niseme ama nifanye chochote kile, na ndiyo kitu ambacho nilipenda, kwamba alisubiri... kuona... nini... kingefata.

Nikatabasamu tu, naye akatabasamu na kuweka vidole vyake kuziba mdomo kwa njia ya aibu. Jambo hili lilikuwa limesababisha mshkaji wangu kule kati aanze kunyanyuka kwa sababu alipenda sana sifa, kwa hiyo nikaamua kupiga hatua zaidi kuelekea pale 'extension' ilipokuwa na kuchukua chaja yangu, na nilipomtazama nikakuta amesimama vilevile huku akiniangalia kwa macho yenye subira.

"Niliacha chaja... nitachomeka simu chumbani..." nikamwambia.

Akatikisa kichwa taratibu kama kusema sawa, huku midomo yake akiibana. Sura yake ilionyesha matarajio fulani hivi, yale matarajio ya mimi ndiyo nipige hatua ya kwanza kwenye wazo moja ambalo najua sisi wote tulikuwa nalo, lakini sikutaka kufanya matarajio hayo yaone mwanga.

Nikamwambia, "Usiku mwema, eti? Tutaonana asubuhi."

Akaangalia chini kiasi na kusema, "Sawa. Ulale salama."

"Haya," nikajibu hivyo na kumpita, nikielekea chumbani kwangu bila kumgeukia tena.

Nafikiri alijihisi vibaya, ama hata kama ikiwa hakujihisi vibaya, basi alijiuliza kwa nini sikufanya jambo lolote kuhusiana na tukio hilo dogo hapo sebuleni. Angefikiria labda sikupendezwa naye, lakini haikuwa hivyo.

Ni kwamba tu sikuona ulazima wa kuchukua hatua yoyote ama kusema lolote kuhusu hilo, na ingepaswa kubaki kuwa namna hiyo maana mimi na yeye bado hatukujuana vizuri, na mambo ya papara hayakuwa kwenye mtindo wangu wa kushughulika na watu; hasa wanawake.

Nikaingia zangu tu chumbani na kushusha neti, mbu wakiwa wengi utadhani wameajiriwa. Nikajilaza kitandani na kutumia muda mfupi kupita Facebook, WhatsApp na Twitch, kisha ndiyo nikaiweka simu chaji na kuanza kuhangaika kuutafuta usingizi huku nyimbo mbovu sana za mbu zikinikera mpaka kunako.


★★★


Nilikuja kuamka pakiwa pameshakucha sana, yaani ile kuamka ya hauwezi kusinzia tena. Mwili wangu ulikuwa na ukawaida wa kuniamsha mapema mno, nami ningeendelea kulala na kusinzia tena mpaka muda ambao ningechoka kuendelea kulala. Ila ilikuwa hivyo tu nyakati ambazo sikuwa na kazi za kufanya, kama wakati huu, na hata leo nilikuwa nimeamka mara kadhaa na kuendelea tu kulala mpaka sasa sasa.

Nikajitoa kitandani na kuchukua simu yangu, nami nikakuta ni saa nne asubuhi. Kulikuwa na missed call kadhaa kutoka kwa watu wangu wa karibu na jumbe kadhaa pia, nami nikawatafuta na kuongea pamoja na baadhi yao kwa ufupi, kisha nikanyanyuka na kwenda kabatini huku napiga mihayo.

Nilipenda sana haka kahali ka kuwa mwenyewe, yaani kama namna ambavyo mtu angechagua kwenda likizo na kutembelea sehemu za kifahari, lakini mimi nikaja sehemu hii yenye mazingira ya kawaida tu, kwenye uswahili zaidi, na nilikuwa na hamu ya kuona namna ambavyo watu kiujumla wangenitendea kadiri ambavyo muda ungepita nikiwa huku.

Kitu ambacho nilihitaji kufanya kwa sasa ilikuwa ni kununua mswaki na dawa mpya za kusafishia meno, ili kinywa kikae fresh. Nikavaa kaushi nikiwa na bukta kwa chini ili nitoke kwanza mpaka nje kwenda kukojoa, lakini nilipofungua mlango wa chumba hicho kidogo, nikaanza kusikia maongezi baina ya wanawake wawili.

Sauti ya mmoja niliifahamu, ikiwa ni Ankia, lakini ya mwenzake sikuijua. Alikuwa rafiki labda, na mada waliyoizungumzia ilimhusu mwanamke yule niliyekutana naye jana mpaka akanipa lifti kwa msisitizo wangu wa kuumwa kimaigizo, yaani Miryam.

"Enhe..." nikasikia Ankia anaitikia.

"Basi, nasikia mchumba amefika, tena na wazazi wake sijui... Miryam hajamtolea nje! Eheee... shoga acha tu..." mwenzake akamwambia hivyo.

"Kamfukuza?" Ankia akauliza.

"Eeeh! Tena limeletwa hadi na gari, huwezi kuamini, lakini limbwende bado tu limekaza vyuma! Ahahaaa... haki ya mama. Miryam hataki kuolewa, yaani hataki. Sijui wamroge?"

"Atakuwa na sababu zake..."

"Sababu zipi Anki? Umri unaenda, anazeeka, hajazaa bado, hayo yote alikuwa ananiambia Shadya leo yaani wameshamtafutia wachumba wa maana wanaoweza kummwagia mipesa ambayo sisi wenzake tunaililia ila haitufikii... shoga! Anaringa huyo! Anafikiri wataendeleaga tu kumpigia magoti eti!"

"Shadya ndiyo kakwambia ya jana?"

"Eeeh, kaniambia wamemletea mpaka na gari lakini kalikataa. Kisa? Eti bado anaitunza familia yake, inamhitaji. Kwani anashindwa kuwatunza hata akishaolewa, ama ni midenguo tu?"

"Asa' unafikiri watafanyaje, watamlazimisha? Kama hataki ndiyo hivyo... inabidi wamwache tu..." Ankia akamwambia.

Inaonekana walikuwa wanapiga umbea kuhusu ile ishu ya jana ya kuchumbiwa kwake Miryam, na ya huko kufika mpaka kwa Ankia namna hii ilimaanisha yangesambaa kwingi.

"Hana lolote mi' nakwambia, huyo mwanamke malaya tu. Usikute hapo alipo anatoka na limme la mtu huko, af' akirudi anajifanyaga mtakatifu kweli... eti familia yangu wananihitaji..." mwenziye akaendelea kusema.

"Huo wivu wako mama Chande unakufanya unamjaji vibaya dada wa watu. Mbona me naona yuko poa tu? Hayo ni maisha yake, acha ajiamulie anachotaka," Ankia akamwambia.

"Mm? Asa' me nimwonee wivu kisa nini? Hako kaweupe ama?"

"Siyo weupe tu, huyo dada mzuri sana ndiyo maana unaona wengi wanajibebisha hapo. Lakini hana shobo za huko, la sivyo angewaacha kweli watu wake wa ukoo na kuolewa na litajiri kama angekuwa hawajali..."

"Aaa wewe mtetee tu, ila tuulize sisi tunaomjua ndiyo utaambiwa. Siku akija kumchukua bwana wako ndiyo utasema mama Chande aliongea kweli..."

Ankia akacheka kidogo na kusema, "Unadhani hata kama ni wewe ukimchukua bwana wangu nitahangaika basi?"

"Wewe huyo? Ulivyo na wivu hivyo?"

"Akhaa, me siko hivyo. Mwanaume akiona abebe ndoo nyingine ya zege me nasubiri mbebaji mwingine aje anichukue, mbona wapo wengi tu?" Ankia akasema hivyo.

Kauli yake ikanifanya nitabasamu. Alionekana kupenda misemo sana, na alikuwa na akili iliyofunguka (open mind).

"Nyoo utaongea hivyo na mtu mwingine asiyekujua, ila me hunidanganyi. We' ndo' wale wanaopiga hadi na magoti, michozi na mikamasi inakuvuja kisa umeachwa na mapenzi!" huyo mama Chande akamwambia hivyo.

Ankia akasikika akicheka.

Mama Chande akacheka kwa nguvu pia na kusema, "Au midadi imeshapanda kwa mchina wako?"

"Eh, wewe, punguza sauti... atakusikia..." Ankia akasikika akisema hivyo.

Mada ikawa imegeukia kwangu, nami nikaweka umakini zaidi.

"Usianze mambo yako. Kwanza umejuaje kuhusiana naye?" Ankia akamuuliza.

"Fatuma kamwona jana anaingia, akaniambia. Mbona umemficha ndani tu shosti, hutaki tumwone mchina nini?" mama Chande akasema.

"Siyo mchina. Ni mpangaji wangu... siyo mtu wangu. Punguza kelele," Ankia akamwambia.

"Mpangaji siku ya kwanza, ya pili ashakunyandua, na najua ndo' unachosubiri..."

"Ila mama Chande..."

"Nini, kwani uwongo? Utasahau hadi kumtoza kodi akishaanza kuku(.....)," mama Chande akasema hivyo.

Nikacheka kidogo kwa pumzi huku nikitikisa kichwa. Huo ndiyo ulikuwa ule uswahili wenyewe, tena na hapo ni kwa kiasi chake tu, nami nilipenda sana.

"Acha sifa mama Chande, nitakufukuza sasa hivi..." Ankia akamwonya hivyo kwa sauti ya chini.

"Unafikiri natoka hapa bila kumwona mchina? Umeliwa! Hatoki mtu hapa hata usipopika," mama Chande akasema.

"Na ukimwona ndiyo itakuongezea nini labda?"

"Buzi... huwezi kujua..." mama Chande akamwambia.

"We' ni mshenzi..." Ankia akamwambia hivyo kwa sauti ya chini.

Mama Chande huyo akacheka kiumbea kiasi huku Ankia akimtuliza, nami nikaona nimpe alichokitaka.

Nikarudi sehemu ya kabati na kurekebisha uso kiasi, kisha nikavaa na T-shirt kusitiri mikono. Nywele zangu zingekuwa na mwonekano fulani wa nywele laini za kiarabu zilizogurugika kila mara nilipotoka kuamka, kwa hiyo sikuzichana kabisa ili nikitoka ionekene kweli ndiyo nilikuwa nimeamka muda huo huo.

Nikaenda kuufungua mlango, nami nikatoka zangu na kuanza kuielekea sebule. Niliweka uso makini, kama vile sijali lolote hapo, nami nilikuta Ankia akiwa amekaa kwenye sofa moja pamoja na huyo mwanamke.

Mama Chande alikuwa mwanamke mwenye umri mkubwa kiasi cha kufikia miaka 40, mweusi wa maji ya kunde, mwenye mwili mwembamba kiasi, na ningeweza kusema urefu wake akisimama ungekaribiana na wangu kabisa. Alikuwa na sura iliyokomaa, akiwa ameweka kope za bandia machoni na lipstick nyekundu mdomoni, huku vazi lake likiwa ni jezi nyeusi ya Yanga iliyoficha matikiti maji makubwa yaliyonyanyuliwa juu bila shaka kwa sidiria, pamoja na suruali nyeupe ya skinny iliyobana mapaja yake yaliyotokeza kiasi. Alikuwa na nywele fupi zilizopakwa dawa na kutiwa rangi ya njano mpauko, naye alifuga kucha ndefu mikononi zilizopakwa rangi nyekundu. Labda zilikuwa za bandia.

Ankia yeye alikuwa amevaa dera la njano lenye maua-maua, huku akijifunga kilemba kichwani kama nilivyomkuta jana tu, na kwa pamoja waliniangalia usoni nilipowakaribia zaidi.

"Za asubuhi?" nikawapa salamu kwa sauti tulivu ya kiume.

Kwa wanawake wa aina yao, shikamoo isingefaa hata kama wangekuwa na miaka 50 maana walijiweka kibinti-binti zaidi.

"Aa salama..." mama Chande akasema hivyo.

"Nzuri tu. Umeamkaje?" Ankia akaniuliza hivyo huku akitabasamu kiasi.

"Vizuri tu, na nyie?" nikawauliza.

"Ah kama unavyotuona. Unalala kweli..." Ankia akaniambia huku akitabasamu.

"Ndiyo, ni uchovu. Wacha niingie uani," nikamwambia.

"Sawa," Ankia akajibu.

Nikawapita na kutoka nje ya mlango wa kuingilia ndani hapo, na sikuwa hata nimetoka sehemu hiyo kabisa nami nikaanza kumsikia huyo mama Chande akisema mimi ni mweupe mno jamani!

Nikakaza tu tabasamu na kwenda kukojoa, nami nilipotoka huko nikatazama upande wa ile nyumba niliyoingiamo jana. Sikuliona gari lile aliloendesha Miryam mnunaji, ikiwa wazi aliondoka bila shaka, lakini nikaweza kumwona kijana fulani akiwa anacheza mpira peke yake kwa kuupigisha mara nyingi kwenye mguu mmoja; tunaita danadana.

Huyo alikuwa mgeni kabisa kwangu, hata jana sikumwona pale. Alikuwa na weupe pia, umri wake si mbali sana kufikia miaka 27 kimakadirio, akiwa na mwili mrefu kiasi na mwembamba pia. Alivalia jezi ya Simba na bukta nyeupe, na alinyoa mtindo wa kiduku bila kuwa na nywele nyingi sana juu ya kichwa. Kiduku kifupi. Nikawaza labda alikuwa ndugu yao mwingine akina Zawadi mweupe, nami nikarudi zangu tu ndani kwa Ankia.

Nikamkuta pamoja na shosti yake, lakini wakati huu Ankia akiwa amesimama usawa wa meza, na mezani hapo alikuwa ameweka chupa ya chai, kikombe, chombo cha kutunzia sukari na kijiko chake, pamoja na bakuli jeupe la udongo lililofunikwa kwa bakuli lingine la aina hiyo hiyo. Mwenzake alikuwa ametulia tu akionekana kuwa bize na simu eti, nami nikamtazama Ankia usoni na kuona anatabasamu kiasi.

"Karibu chai," akaniambia hivyo.

Ahe! Nikarudisha tabasamu hafifu tu, kisha nikamwambia, "Asante. Nahitaji kusafisha mdomo kwanza, sijui hili duka la hapa nje wanauza miswaki?"

"Eee anauza," Ankia akaniambia.

"Aaa basi poa, ngoja nifate kwanza afu'..."

"Hamna, usijali, nipe tu hela nikufatie," Ankia akanikatisha.

Nikamwona kwa jicho la chini rafiki yake akitabasamu kwa kuikunja midomo kwa njia ya kichokozi, nami nikamuuliza Ankia, "Sikusumbui?"

"Hamna wala, haunisumbui," akanijibu.

"Haya, nakuja," nikamwambia hivyo na kisha kumpita kulekea chumbani.

Sijui ikiwa kila alichokifanya kunielekea ilikuwa huduma nilizohitaji kulipia baadaye labda, lakini huo mtindo wa kunifanya mimi nionekane kama mume wake vile haukuwa mbaya sana kwangu. Huenda aliwatendea wageni wake wote namna hiyo.

Nikachukua buku tano na kurejea sebuleni tena, nikimpa anifatie dawa ya meno na mswaki imara, naye huyo akaenda zake. Nikaachwa sebuleni pamoja na mama Chande mwongeaji; aliyeonekana kupenda kusema sana watu pamoja na yule Shadya wa jana. Wakati huu alikuwa kimya tu, akiyapa macho yake ubize mwingi kutazama kilichoonyeshwa kwenye TV, huku mimi nikikaa sofa la pembeni nikipitia mambo fulani kwa simu yangu bila kujishughulisha naye.

Sikumsemesha hata kidogo mpaka Ankia aliporudi, nami nikapokea vifaa vyangu vya usafi wa mdomo pamoja na chenji, shwaa chumbani. Yaani wangeelewa tu mabiti. Kama vile ambavyo Ankia alikuwa ameniambia usiku uliotangulia, mimi pia sikuwa mtu wa kushoboka na mtu yeyote kabisa, labda mpaka awe amenielewa na kunionyesha hilo wazi, ndiyo na mimi ningezisoma naye ikiwa pigo na tabia zingekubaliana. Msemo wa Fid-Q ndiyo uliofaa kuelezea jinsi nilivyokuwa kihalisi; mimi ni mtu wa watu, lakini siyo mtu wa kila mtu!

Nikatoka zangu tena na kwenda kuswaki kwenye lile sinki la kuoshea vyombo pale nje, kisha nikarejea ndani na kukaa sofani ili nishushe chai aliyoniandalia mwenye nyumba wangu. Yaani ilikuwa ni baada ya mimi kukaa tu ndiyo na yeye akanyanyuka na kuanza kuifungua chupa ya chai, kisha akaimimina kwenye kikombe. Ilikuwa ya maziwa kabisa, nami nikawa namtazama tu kwa utulivu.

Mara kwa mara niliweza kuona bila kuangalia kwamba mama Chande alinitupia jicho sana, lakini umakini wangu wote ulikuwa kwa Ankia. Akanisogezea meza taratibu, kisha akarudi kukaa na shosti yake. Mwanaume nikajiongeza kwa kuweka sukari iliyonitosha, kisha nikafunua bakuli kukuta ni maandazi laini, ya moto. Nikawakaribisha, nao wakashukuru na kuendelea kukaa kwa utulivu kama Malaika eti.

Nikaanza kukipa kinywa ladha tamu ya chai, kisha nikaanza kutafuna na maandazi. Chai ilikuwa ni tamu balaa, lakini maandazi, ah yaliniacha hoi. Yalikuwa yale maandazi ambayo ukiyaangalia nje yanakuwa yametuna kinoma ila ukilishika na kuling'ata unaambulia kula ngozi tu maana ndani panakuwa hewa!

Sijui huwa hata wanayapikaje wale wanaoyauza, yaani hamna nyama kwa ndani kabisa, na wanaume hatuyapendagi ya hivyo basi tu ukikuta mwanamke kashayaweka unayapiga kwa kujilazimisha. Wanawake hao wakawa wanaongeleshana tu kwa sauti za chini na kucheka-cheka mpaka nilipomaliza chai yangu tamu.

Ankia akatoa vyombo huku nikimshukuru, kisha akavipeleka jikoni na kurudi kuniletea maji ninawe. Nilishindwa hadi kujizuia kutabasamu bila kumwangalia, lakini nilijua na yeye alikuwa anatabasamu. Akasafisha meza na kupeleka maji hayo huko jikoni, kisha akarudi sofani na kukaa tena.

Nikamuuliza ni muda gani ambao alitaka twende kwa mwenyekiti, naye akasema muda wowote tu ambao mimi ningekuwa tayari. Nikasema sawa, nimwache atumie muda huu na rafiki yake kisha mida ya saa saba hivi twende pamoja huko, ili aweze kunionyesha na njia za mitaa hiyo kwa ufupi. Kama kawaida yake akasema haikuwa na neno, nami huyo nikaelekea chumbani.

Hata kabla sijaufungua mlango wa kuingilia chumbani, nikamsikia mama Chande akisema kwa sauti ya chini eti "linanukia vizuri," nami nikaingia ndani humo tu na kukiendea kitanda ili nipumzike kidogo. Hii sehemu ilinikosha kwa kiasi chake!

★★

Saa kama moja hivi likapita nikiwa nimejilaza tu kitandani. Kulikuwa na joto ingawa niliacha milango ya madirisha wazi, nami nikawa nafikiria kwenda kuoga upesi kulipunguza fukuto baya mwilini.

Nikiwa namalizia kuchat na marafiki zangu kwenye simu mlango wa chumba ukagongwa. Nikasema tu 'karibu,' nao ukafunguka na mwanamke mwenye mji kuingia. Wakati huu nilikuwa nimelitoa T-shirt mwilini na kubaki na kaushi na bukta, nami nikakaa badala ya kulala.

Ankia alikuwa ameingia na mwonekano tofauti. Alivaa T-shirt nyeupe yenye mikono mifupi iliyoubana mwili wake wa juu na kufanya kifua chake kionekane kutuna sana kwa mbele, pamoja na sketi ya zambarau ya kitambaa laini iliyombana haswa na kulichoresha umbo lake la chini vizuri mno. Iliishia magotini, miguu yake yenye unene wa chupa ya bia ikionekana vizuri kwa usafi wake.

Usoni alikuwa amejitengeneza vizuri pia, na sasa hakuwa amevaa kilemba bali nywele zake ndefu za kusukwa aliziacha wazi ili sisi wote tuzione. Na harufu yake tamu ilikijaza vyema chumba hicho.

"JC... jiandae twende. Niko tayari," akaniambia huku akiwa ameushikilia mlango.

"Eh, saa sita na nusu... usingekuja labda hata ningesinzia. Asante," nikamwambia.

Akatabasamu kidogo.

"Ngoja 'nkapige maji faster af' twende. Umedamshi kweli," nikamwambia.

"Ahahah... asante. Nitakusubiri, ukimaliza nishtue... niko chumbani," akasema.

"Poa."

Akataka kugeuka ili aondoke.

"Subiri kwanza, eti hivi..."

Akaniangalia tena baada ya mimi kuanza kusema hivyo.

"Hiyo feni hapo sebuleni inafanya kazi?" nikamuuliza.

"Aa hiyo... hamna. Ilikuwa nzima ikaharibika, nimeshaipeleka kwa mafundi lakini wamenila tu hela halafu haijatengemaa. Nikaikatia tu tamaa," akaniambia hivyo.

"Bado inaonekana nzuri kweli, mafundi wengi unajua ukiwapelekea mashine hata zikiwa na tatizo dogo tu, wanatoa vitu fulani na kuviiba... halafu wanakuja wanakwambia tatizo ni kubwa sana ili wale tu hela yako..."

"Eti eeh..."

"Ndo' hivyo. Sema... nitakuja niiangalie. Ninaweza nikafanya maajabu ikakaa fresh."

Akatabasamu kidogo na kusema, "Utakuwa umenisaidia sana."

"Haya poa. Ngoja nifanye kuoga chap," nikasema hivyo huku nikisimama.

"Poa," akajibu hivyo na kuilamba midomo yake kisha kuibana.

Alipogeuka ili aondoke, nilishusha macho yangu kutazama umbile lake la nyuma, nami nikatabasamu tu kwa jinsi ambavyo lilionekana kuwa zito na lenye mikunjo mingi sana. Ni vitu ambavyo wanaume huwa tunapenda sana, hatushangai bodaboda ikiingia mtaroni shauri ya mwendeshaji kushindwa kujizuia kuvitazama!

Nikavua nguo upesi na kwenda kuoga, na nilikuwa na uhitaji wa kununua sabuni yakwangu peke yangu kwa ajili ya matumizi, lakini iliyokuwemo humo bafuni ikanisogeza tu kwa wakati huu. Nikaingia chumbani na kujiweka vizuri kimwili, kisha nikatupia viwalo safi mwilini. T-shirt laini nyeusi yenye mikono mirefu pamoja na jeans la samawati iliyokoza, zilinikaa vyema sana kwenye mwili wangu wenye uimara.

Nikatengeneza nywele vyema na kuvaa saa yangu niliyokuwa nimeitunza tu kwenye begi, na hiki ni kitu ambacho nilipenda sana kufanya hasa nilipotaka kutoka kutembea sema kwenye safari ya kuja huku sikutaka tu kuivaa mkononi. Kwa hiyo nilipokaa fresh nikajinukishia manukato yangu na kumfata bibie Ankia, kumwambia tujage.

Mwanamke akatoka, akionekana kuwa na furaha kiasi, nami nikamwambia anitangulie maana yeye ndiye aliyekuwa ameibeba dira ya Mzinga. Akatabasamu na kutangulia, nasi tukatoka mpaka nje zaidi baada ya kuifunga milango kwa funguo.

Tukaanza kutembea kuzipita nyumba kadha wa kadha, taratibu, na aisee, kila mtu alitutazama. Nadhani Ankia alikuwa tu na ile akili ya kuzaliwa kufatisha namna ambavyo mimi niliitikia mazingira kwa kutowatazama watu na kujali nyendo zetu tu, lakini angewasemesha kifupi wale waliomfahamu walipompa salamu na kuendelea kutembea pamoja nami.

Nilikuwa wa namna makini sana. Shobo pembeni, ili wenye kushoboka ndiyo washoboke. Tukakata mtaa na kuingia mwingine kuelekea Mzinga, ambako kulikuwa na shughuli nyingi zaidi na masoko, na kama kawaida macho mengi yalikuwa kwa "mchina" mgeni na mwanamke wake. Najua wengi wao walifikiri hivyo.

Tukafika mpaka pale ambapo nilishushwa na daladala ile usiku wakati nakuja, kwenye lami, nasi tukakunja kona kidogo tu na mbele zaidi tukaifikia ofisi ya "Kata ya Mzinga." Oh kumbe ilikuwa ofisi ya kata? Ankia akanipeleka mpaka kuifikia, tukiwa tumepita kijiwe kikubwa cha wadau waliopenda kunywa kahawa na tangawizi kali, nasi tukaenda kuonana na mwenyekiti.

Watu wa humo walitutendea kwa njia fulani ya unyenyekevu, kana kwamba ni watu wakubwa ndiyo walikuwa wameingia, na baada ya Ankia kueleweshana na mwenyekiti kuhusu suala letu la upangishaji, nikapewa makaratasi ya kutia sahihi pamoja na Ankia na kopi za kutunza. Nilihitajika kupigwa picha ndogo za 'passport' ili zibandikwe pia kwenye karatasi, kisha jamaa akaweka mihuri yake, nasi tukasepa. Oh aliomba hela ya soda, nami nikampa elfu mbili kutoka kwenye chenji aliyonirudishia Ankia muda ule.

Tukatoka zetu tena ili turudi pamoja nyumbani. Ndiyo, nyumbani. Angalau Ankia alikuwa ameanza kunipa malezi yaliyonifanya nijisikie kuwa nyumbani, na bado sikuwa nimemwonyesha shobo nyingi sana mwanamke huyu hata kama hali ya kuzoeana ilianza kuwepo baina yetu. Ndivyo nilivyokuwa.

Tulipoanza kurudi tukapita sehemu waliyotengeneza chips, mishikaki, nyama za kuku, na ndizi za kukaangwa. Nikamwambia Ankia twende hapo ili nichukue msosi turudi nao maskani, naye akakubali. Tukaenda, nami nikaomba huduma. Nilihitaji kujua ikiwa Ankia alipenda kula vyakula hivyo, na ni mwanamke gani asiyependa? Basi tu, si unajua swaga?

Nikamuuliza, naye akakubali. Kwa hiyo nikaomba watupatie chips mayai mbili, kuku za kukaangwa vipande vitatu-vitatu kila chips, pamoja na mishikaki mitano-mitano. Kutazamwa sana na aidha wanawake au wanaume bado kuliendelea hata kwa sehemu hiyo, na inaonekana ilimpa Ankia hisia za ufahari kutokana na kujua alielekezewa fikira kuwa pamoja nami. Si ile kwamba angeonewa wivu? Mimi nilielewa.

Tukapatiwa misosi yetu, nasi tukapiga mwendo tena mpaka kule Masai tulipoishi. Zamu hii tulitumia njia nyingine ili Ankia anizoeshe maeneo zaidi, na baada ya kufika pale dukani nikamwambia achukue soda mbili pamoja na sabuni nzuri za kuogea, nami nikatangulia nikiwa na funguo ya mlango wa kule ndani.

Yale makaratasi ya mwenyekiti alikuwa nayo Ankia, yakiwa salama ndani ya bahasha, naye akawa amefika ndani pia pamoja na chupa mbili za Pepsi baridi na kuziweka mezani. Tayari na mimi nilikuwa nimeweka mifuko ya vyakula mezani, hivyo Ankia akanipatia sabuni mbili alizonunua nami nikampa moja, kisha nikaenda chumbani ili nibadili nguo na kuvaa nyepesi.

Nadhani muda mfupi niliotumia kubadili mavazi ulimtosha sana Ankia kufungua vyakula na kuviandaa kwenye sahani safi, kwa hiyo niliporudi sebuleni nikakuta vikiwa wazi tayari kukamuliwa kisawasawa.

Nikakaa sofani na kujiandaa kula, naye akaniletea maji na kuninawisha. Akanawa pia, na alipoanza kusogeza meza upande wangu, simu yangu ikaita, nami nikapokea na kuzungumza na ndugu yangu mmoja aliyekuwa amenipigia.

Ankia akafungua soda zetu na kisha kukaa kwenye lile sofa dogo, lakini nikamwonyesha mshangao kwa sura yangu na kumpa ishara kuwa aje kukaa kwenye sofa nililoketi mimi. Anakaa mbali kufanya nini sasa? Akatabasamu kidogo na kuibana midomo yake kwa shau, kisha akaja na kukaa karibu yangu.

Tukaanza kula pamoja, huku wa kwenye simu akigoma kabisa kutaka kuniacha. Ikabidi nimwambie simu inazimika hivyo ningemtafuta baadaye, nami nikakata na kuhamishia umakini wangu kwa Ankia. Alikuwa akijitahidi kula kistaarabu eti mbele yangu, lakini nikamwambia ajiachie zaidi maana mimi nilipenda kula kwa fujo hasa chakula kikiwa kitamu sana, na kama niko na mtu niliyemzoea.

Muda si muda tukawa tunakula huku tukifurahia maongezi yenye utani mwingi, nami nilimchekesha sana kwa kumsimulia hadithi za baadhi ya mambo mengi niliyojua. Alikuwa na kicheko fulani hivi cha chini-chini chenye kuvutia, nami nilielewa kwamba mbele yangu alikuwa anajitahidi kukibana kile kicheko cha kimbea kama angekuwa anapiga porojo na mwanamke mwenzake.

Tukawa tumemaliza kula chakula hicho kitamu sana, naye eti akanishukuru kwa kumnunulia chips na kuku. Nikamwambia acha zako wewe, naye akatoa vyombo na kuvipeleka jikoni, kisha akarudi na kukaa kwenye sofa pembeni yangu tena bila mimi kumwambia afanye hivyo.

Akachukua rimoti na kuiwasha TV, akianza kubadili chaneli huku mimi nikiwa nimekaa kwa kuegamia mgongo zaidi, nikiwa nimeshiba kweli, kwa hiyo yeye akaonekana mrefu kunipita maana alikaa kitako. T-shirt alilovaa lilikuwa limeinuka juu kidogo kuniruhusu nione nyama laini ya kiuno chake, nami nikamtazama usoni.

Ulionekana kwa upande kutokea nilipokuwa nimekaa maana uso wangu ulikuwa nyuma yake zaidi, na akiwa bado bize kubadili chaneli, nikaona nimchokoze kwa kukigusa kiuno chake kwa kiganja changu.

Akashtuka kidogo na kunigeukia, nami nikamtazama machoni kwa njia ya kichokozi zaidi huku nikiendelea kutembeza vidole viwili kwenye kiuno chake. Akanipa tabasamu fulani hivi la nyodo, kama hataki lakini kwa furaha eti, kisha akaigeukia TV tena bila kunizuia nisiendelee kumfanya hivyo.

Nikaona nimchokoze zaidi kwa kuingiza vidole vyangu ndani ya T-shirt lake kupitia mgongoni mpaka kufikia ubavu wake mmoja, kisha nikamtekenya kidogo.

Akashtuka na kusogeza nyonga mbele huku akisema, "Iih, wewee..."

Aliniangalia kwa macho yaliyoonyesha hisia zinataka kumkolea, nami nikacheka kidogo kwa pumzi, kisha akarudisha mkono wake nyuma na kuutoa wangu mgongoni kwake kama kuonyesha anataka niache.

"Kwa nini mwanamke mzuri kama wewe unaishi peke yako?" nikamuuliza hivyo kwa sauti tulivu.

"Si nimependa tu?" akajibu bila kunitazama.

"Tokea lini umependa tu?"

"Tokea zamani."

"Mbona nasikia haukuwa unaishi peke yako?" nikamuuliza.

"Umesikia kwa nani?" akaniuliza hivyo na kuniangalia.

"Nina mitandao yangu..."

"Mitandao ipi wakati umefika jana tu?"

"Mengi yametokea jana kabla sijafika hapa, utajuaje?"

"Mhm..." akafanya hivyo na kuangalia TV tena.

Nikaingiza tena kiganja changu mgongoni kwake na kuanza kuukuna taratibu, kitu ambacho kilifanya niguse mikanda ya sidiria yake kwa nyuma, nami nikamuuliza, "Mume wako je?"

"Sina mume," akajibu bila kunitazama.

"Alienda wapi?"

"Sijui."

"Kwa nini aliondoka?"

"Si tuliachana?"

"Kwa nini mliachana?"

"Tulichokana."

"Kisa nyimbo za Ali Choki au?"

Akacheka kidogo.

"We' ni mzuri Ankia," nikamsifia kwa sauti zembe, makusudi.

"Uzuri wangu uko wapi?"

"Upo hapo hapo kwako."

"Mhm... huko Sinza ulikotokea hujaona wanawake wazuri?"

"Sijaona..."

"Unanipulizia moshi tu. Huko ndo' kuna pisi sana..."

"Hazikufikii..."

"Kwenda zako! Unanipaka tope tu, me kibonge wa Mbagala nitafanana na hao wanaojiona keki hapa jijini?" akasema hivyo na kukitoa tena kiganja changu mgongoni kwake.

"Me sivitaki hivyo vikeki bwana..." nikamwambia hivyo.

"Umeshapiga vingi eh?"

"Aa wapi, hata sijawahi kabisa..."

"Mh... nhaa..." akacheka kidogo.

"Ni kweli, si unaniona me bado mtoto?"

"Kwa hiyo kama we' bado mtoto?"

"Nahitaji malezi bora. Nani mwingine atanipa hayo sasa?"

"Si wa huko kwenu?"

"Me nataka ya huku..."

"Nenda Rangi Tatu utayapata..."

"Nimeshayapata mbona?"

"Wapi, Rangi Tatu?"

Nikaingiza tena kiganja changu mgongoni kwake na kusema, "Hamna, ni kwenye rangi yako."

"Rangi yangu imefanyaje?"

"Ni nzuri..."

"Mhm..."

"Una katabia fulani hivi nakapenda sana..."

"Kapi hako?"

"Unapozilamba na kuzibana hizo lips... na hayo macho lege..."

Akatabasamu kidogo na kuangalia pembeni, nami nikaushika ubavu wake ndani ya T-shirt lake. Akataka kuutoa mkono wangu, lakini nikauvuta mwili wake na kumfanya aegamie sofa kwa mgongo wake, na mpaka kufikia hapo nilikuwa nimeshasimamisha mnara wangu kule kati kwa hasira kali mno.

Akaweka kiganja chake kifuani kwangu huku akigoma kunitazama machoni, kwa kuwa sasa nyuso zetu zilikaribiana sana.

"Mm... JC..."

"Nini?"

"Hmm... mmhh..." akaishia kushusha pumzi tu.

"Mbona unakuwa hivyo?" nikamuuliza hivyo kibabe.

"Unanipenda... au unanitamani tu?" akaniuliza hivyo.

Khh! Mbona kaanza kuingiza bongo movie tena?

Nikamwambia, "Tunaanzaga kutamani. Kupenda ni baadaye."

Akawa anapumua kilegevu eti, huku mimi nikiwa bado nimemshika kiunoni na mkono mwingine ukilishika paja lake lililo ndani ya sketi aliyovaa, naye akasema, "Me siwezi..."

"Usiweze nini?"

"Kufanya unachotaka..."

"Kwa nini usiweze?" nikamuuliza.

"Wanaume waongo sana..." akaniambia kwa deko.

"Wamekudanganya wengi?"

Hakujibu na kuibana tu midomo yake.

"Lakini me si mtoto? Hapa unafanya tu kunitunza mama," nikambembeleza.

Akaniangalia machoni, nami nikawa bado nampa tabasamu la kichokozi. Nikamvutia zaidi kwangu kwa mkono ulioshika kiuno chake, naye akataka kujirudisha nyuma lakini nikamshika shingoni kwake na kuivuta mpaka karibu zaidi na uso wangu, kisha nikaanza kuibusu.

"...hhh... JC..."

"Nini?"

"Ana'eza akaja mmtu...."

"Nani aje bwana? Em' tulia..."

Nikazinyamazisha kelele zake na kuanza kumbusu kimahaba. Hakuwa mtaalamu sana wa kupiga denda lakini midomo yake mikubwa ilinyonyeka vizuri sana kwangu. Na angalau hakunuka mdomo la sivyo ningesitisha zoezi hilo hapo hapo!

(..........).

(..........).

(..........).

Akawa anaguna kwa pumzi nzito huku akiniangalia kama vile anateswa, maana niliyala kwa fujo na kuzidi kuyala tu. Akakibana kichwa changu kwake zaidi ili niendelee tu kumtafuna, na kiukweli, sikuliona hili likija.

Nikashtukia tu Ankia ameanza kutetemeka, akinibana zaidi, nami nikajitoa kwake baada ya yeye kuonekana anaondoa uchovu fulani ndani yake. Aliniangalia huku amelegea sana, nami nikamwangalia kwenye sketi na kuona imelowana mno.

"Doh! Ankia umeshalimwaga?" nikamuuliza.

Akatikisa kichwa kilegevu kukubali.

"Juu tu? Nikishuka chini je?"

"Nina muda mrefu..." akaniambia kwa deko.

"Maama... pole..." nikamwambia hivyo kwa kuiga ongea yake.

Akacheka kidogo kwa haya.

"Ila tusiishie hapa. Twend'zetu room nikukamue maji zaidi, au vipi?" nikamwambia.

"Mhm... unaongea wewe..." akasema hivyo kwa hisia.

"Hahah... twende bwana."

Nikaanza kusimama, naye akasimama pia kivivu huku akiona aibu kwamba sketi yake ilikuwa imelowana kama vile mtoto aliyejikojolea. Nikaanza kumvulisha, kwa kuishusha mpaka magotini, naye akaikunja na kuinyoosha miguu yake ili itoke yote.

(..........).

(..........).

Labda hisia nzito alizokuwa nazo zilifanya awe mzito mno, kwa hiyo nikawa namvuta kukielekea chumba huku amenishikilia na kutembea kwa kuyumba utadhani hakujiweza. Ni wazi alikuwa legelege, nami ningehakikisha anaishiwa nguvu hata zaidi kwa zawadi niliyoandaa kumpatia.

Kiukweli nilikuwa nimesisimka sana na nilitaka kufanya jambo la maana pamoja na huyu mwanamke, lakini ile tu tumefika mlangoni hizo fikira zikavurugwa.

"Ankiaa!"

Tukaivunja busu yetu na kuangalia upande wa nje, ambako ndiko sauti hiyo ilitokea. Ankia akaniangalia kwa njia ya kubabaika, akionekana kutaka kuniachia hasa baada ya kuutoa mkono wake kwangu, lakini mimi nikambana zaidi. Huyo aliyemwita kutokea huko nje alisikika akiwa anakuja upande wa ndani zaidi, ikiwa ni mwanamke ambaye sikumfahamu.

"Ankia mama, toka nje malaika akuone..." mwanamke huyo akasema hivyo.

Malaika gani huyo amekuja kuniharibia mood tena? Nikamwonyeshea Ankia ishara ya kutoitika, nikimzuia asijibu mwito huo, lakini akajitoa kwangu kwa nguvu kiasi huku akinionyesha ishara kwa kiganja kuwa niingie chumbani.

"We' vipi? Kwani lazima umpokee?" nikamuuliza hivyo kwa sauti ya chini.

"Ni mama Ashura, mwanakikundi mwenzangu mambo ya vikoba na madeni, nilimwambia aje leo tuongee... ingia chumbani..." akasema hivyo.

Alirudi sebuleni upesi na kuzitoa nguo zake pamoja na bukta yangu baada ya kuparekebisha vizuri, kisha akakimbilia chumbani kwake kwa njia ya kunyata. Hii kitu iliniudhi sana, basi tu. Nikasikia mja akiwa amefikia mlango, naye akamwita tena Ankia huku akiugonga.

"Abee..."

Ankia akaitika, nami nikiwa bado pale pale mlangoni kwenye chumba changu nikamwona akitoka huku akiwa ameshavaa dera lingine zuri na akijifunga kilemba kichwani.

"We' naye, unakaa ndani kama umekufa vile?" mwanamke yule huko nje akasikika akisema hivyo.

Ankia akanionyesha kwa ishara ya kiganja kuwa niingie chumbani, akinisisitizia kwa uso uliojaa hisia, nami nikasikia mlango unafunguliwa. Ikanibidi tu niingie chumbani humo na kufunga mlango, huku nikiwasikia walivyoanza kuongea mambo yao ya vikoba na ujorojoro mwingi wa wanawake.

Bonge moja la kata stimu maana hata mtambo wangu haukutaka kushuka chini bado, nami nikajilaza tu kitandani huku sauti za maongezi yao zikiendelea kunipa kero kwa sababu ya kukatishiwa starehe yangu. Angalau nilikuwa nimeshaanza kupiga hatua nzuri na mwanamke huyo lakini nayo ikawa imevurugwa.

Hakuna hisia nzuri sana ya kupiga hatua za jambo hilo kama ile unayoipata unapolifanya kwa mara ya kwanza na mtu fulani; haiwi kama kwenye mara ya pili, na ya tatu, na ya nne. Kwa hiyo huyo mama wa vikoba kuniharibia ishu yangu ya mara ya kwanza na Ankia kuliniboa sana, maana hata kama tungekuja kuwa kivyetu tena, ingeonekana kuwa ni mara ya pili; yaani mzuka hauwi kama vile unavyokuwa kwenye mara ya kwanza!

Ila nikaona fresh tu, labda nijizamishe kwenye jambo lingine ndani hapo mpaka huyo "mazeli" akiondoka. Nikavuta simu yangu, kuingia intaneti, bando limeisha. Agh! Sikuwa hata na mia Tigopesa ama la sivyo ningenunua hapo hapo, hivyo ikanibidi tu ninyanyuke ili niende kuchukua vocha pale kwenye duka la nje kwenye nyumba hiyo. Bado nilikuwa na boksa na T-shirt tu, kwa hiyo nikavaa suruali nyeusi na kuchana nywele vyema, kisha nikatoka kulifata duka.

Kama kawaida, niliweka uso makini na kumkuta Ankia akiwa pamoja na mwanamama huyo mweupe kiasi pia, akiwa amevaa nguo ya kitenge kama gauni. Nikamwamkia na kisha kuwapita tu, bila kumtazama Ankia hata kidogo. Nilionyesha kutojali sana kilichoendelea hapo, nami nikatoka zangu nje na kuvaa masai zangu miguuni, kisha nikaenda upande wa nje.

Ikiwa jioni ndiyo imeingia sasa, jua halikuwa kali sana na watu kadha wa kadha walionekana kupita ama kufanya mambo yao kwenye nyumba za majirani, nami nikafika dukani hapo na kusimama. Kulikuwa na mwanaume aliyesimama bila shaka kupata huduma, lakini alionekana kupata huduma ya maongezi zaidi kutoka kwa mwanamke yule niliyemwona jana usiku dukani humo.

Alivalia gauni lenye mikono mirefu pamoja na ushungi, akionekana kuwa mweupe na mwislamu pia, nao wakaacha kuzungumza baada ya mimi kufika. Nikaona hiyo ndiyo nafasi ya kuomba vocha ya buku nikaperuzike, lakini hapo hapo akawa amekuja mtoto mdogo kwa kasi sana na kuomba apewe unga wa sembe, nusu.

Mwanamke wa dukani alimpuuzia na kuniuliza ninataka nini, lakini nikamwambia amhudumie mtoto kwanza. Mwanamke huyo alikuwa ameweka sura makini zaidi baada ya mimi kufika hapo, na hata yule mwanaume akabaki kimya tu, na wala sikujisumbua kuwaweka akiba akilini.

Nikaangalia pembeni kiufupi wakati mwanamke huyo alipokuwa anampimia dogo unga wake, nami nikaona watoto wengi kiasi, wasichana sanasana, wakiwa wanacheza mchezo wa 'rede' pamoja. Binti mmoja akavuta umakini wangu, lakini ndiyo hapa nikasikia...

"Sh'kamoo..."

Nikamtazama mtoto huyo aliyekuwa ameniamkia hivyo hapo dukani, nami nikasema, "Marahaba. Hujambo?"

"Sijambo," kakajibu, kakiwa ni kasichana.

Kalionekana kuganda kunitazama sana usoni, nami nikarudisha macho yangu kwa yule binti mwingine. Kwa watoto waliocheza pale, ni yeye pekee ndiye ambaye hakuwa "mtoto." Ilikuwa ni yule binti niliyemkuta jana kwa akina Zawadi mweupe, Mariam bila shaka, naye alicheza 'rede' pamoja na wasichana wengine kana kwamba alikuwa mtoto.

Nikamwangalia kwa umakini zaidi. Alisimama usawa wa barabara pamoja na wenzake huku yeye akiwa mrushaji wa mpira ili kumponda aliye katikati, lakini jinsi alivyoitikia mambo mengi ilikuwa kwa njia... tofauti. Angerusha mpira na kuanza kurukaruka kwa shangwe hata kama hajamponda mtu, huku akipiga-piga makofi na kucheka kwa furaha sana.

Uso wake ulipendeza mno alipotabasamu, sura nzuri mno kama ya dada yake mkali ikanifanya niendelee kumwangalia tu, nikijiuliza pia ni kwa nini binti mkubwa angecheza mchezo wa watoto pamoja na watoto. Dogo akawa amepatiwa unga wake, na sasa zamu ikawa yangu kuomba huduma.

"Naomba tigo ya elfu moja," nikamwambia muuzaji.

Akaanza kuchangamka kuitoa vocha, nami nikiwa navuta pesa kutoka mfukoni nikawa nimeangalia tena upande wa Mariam.

Kutokea mbele zaidi kwenye barabara hiyo ya changarawe iliyoelekea pande mbili tofauti lilikuja gari jeupe, taxi aina ya Toyota Corola, taratibu tu, na wakubwa waliokuwa wameketi kwenye vibaraza vya nyumba zao wakawaambia watoto wasogee pembeni kwanza ili isije kutokea ajali.

Watoto kweli wakasogea pande za pembeni, na Mariam akavutwa mkono na wenzake wawili kuja upande wa duka niliposimama mimi. Ilionekana ni kama vile hakuelewa mambo vizuri sijui, lakini ghafla gari lile likaongeza kasi na kuanza kuelekea upande huu ambao Mariam na wenzake walikuja!

Nilishtuka. Mwanaume aliyekuwa hapo dukani akasema 'nyie,' kwa njia ya tahadhari, na wale wasichana wadogo wawili wakakimbia kuliepuka gari hilo lililokuwa likija kwa mwendokasi ulioongezeka. Mariam alibaki kusimama hapo huku akiliangalia kwa hofu, nami sijui niliingiwa tu na nini lakini niliruka na kumfikia karibu zaidi binti huyo, kisha nikampamia na kuanguka naye ardhini kwa kuviringika huku gari lile likiwa limetukosa kidogo tu!

Nilianguka na Mariam mpaka katikati ya barabara ile, na hilo gari likafunga breki ya ghafla kubakiza nafasi ndogo tu kuligonga lile duka. Yule mwanaume alikuwa amekimbilia upande mwingine, na nilisikia kelele za yule mwanamke wa dukani, aliyeogopa bila shaka.

Sasa nilikuwa chini, nikilala kwa juu kuufunika mwili wa binti huyu, nami nikalitazama hilo gari. Halikupitisha upenyo wa kuona kupitia kioo cha mlangoni, hivyo nisingeweza kumwona aliyekuwa ndani. Tairi la mbele likageuza kuielekea barabara, nalo likatoka hapo na kuingia barabarani; likinyoosha mbele kwa kasi mpaka kutokomea upande ule wa bar ya Masai.

Watu walianza kuongezeka sehemu hiyo, kelele zikizidi, vumbi likitawala angani, nami nikamtazama Mariam chini yangu. Alikuwa analia kwa kwikwi, huku viganja vyake vikitetemeka karibu na uso wake, nami nikanyanyuka na kuanza kumsaidia anyanyuke pia. Aliogopa sana mpaka akawa hataki nimguse.

Watu walipotusogelea, kila mtu alikuwa na lake la kuongea, na wanawake kadhaa wakamsaidia Mariam kusimama na kuanza kulipangusa dera lake huku wakimwambia asilie maana Mungu alisaidia ajali ile isitokee.

Nilitazama upande ule ambao lile gari lilielekea, kisha nikamwangalia huyo binti. Kama ni mimi peke yangu ndiye niliyeona kila kitu kilichotokea, basi ningekuwa mtu pekee wa kusema kwamba hiyo haikuwa ajali. Lilikuwa ni jambo lililopangwa kutokea, na mlengwa wa mpango huo usiojulikana ulitokea wapi alikuwa ni Mariam.

Nilijiuliza sana ni sababu ipi ambayo ingefanya binti huyo alengwe shabaha namna hiyo, na ni nani ambaye alitaka kumgeuza awe marehemu. Alikuwa amebeba nini kikubwa msichana huyu kilichofanya mtu yeyote atake kumuua? Kwa nini Mariam?


★★★★★★★★★

ITAENDELEA

★★★★★★★★★

Full Story WhatsApp or inbox

Whatsapp +255 678 017 280
 
MIMI NA MIMI

A Story by Elton Tonny

Familia, Urafiki, Mapenzi, Kazi, Tamaa, Hila, Usaliti, Siri, Mambo Ysiyotazamiwa

R-rated 18+

Enjoy!

★★★★★★★★★★★★★

SEHEMU YA TATU

★★★★★★★★★★★★★


Nikamwangalia machoni, nikiwa nimetulia tu. Tayari sasa alikuwa ameufunika mwili wake, lakini aliendelea kushikilia pale pa kufungia khanga kwa mikono yake yote kama vile amegandishwa, kwa sababu ya kunitazama kwa umakini, ama labda butwaa. Ni wazi hakuwa amehisi uwepo wangu nyuma yake.

Lakini hali ya utulivu tu aliyoweka, ilinipendeza sana. Hakuwa na makeke. Jinsi nilivyomwangalia machoni, ndivyo ambavyo na yeye pia aliniangalia. Ni kama alikuwa anasubiri niseme ama nifanye chochote kile, na ndiyo kitu ambacho nilipenda, kwamba alisubiri... kuona... nini... kingefata.

Nikatabasamu tu, naye akatabasamu na kuweka vidole vyake kuziba mdomo kwa njia ya aibu. Jambo hili lilikuwa limesababisha mshkaji wangu kule kati aanze kunyanyuka kwa sababu alipenda sana sifa, kwa hiyo nikaamua kupiga hatua zaidi kuelekea pale 'extension' ilipokuwa na kuchukua chaja yangu, na nilipomtazama nikakuta amesimama vilevile huku akiniangalia kwa macho yenye subira.

"Niliacha chaja... nitachomeka simu chumbani..." nikamwambia.

Akatikisa kichwa taratibu kama kusema sawa, huku midomo yake akiibana. Sura yake ilionyesha matarajio fulani hivi, yale matarajio ya mimi ndiyo nipige hatua ya kwanza kwenye wazo moja ambalo najua sisi wote tulikuwa nalo, lakini sikutaka kufanya matarajio hayo yaone mwanga.

Nikamwambia, "Usiku mwema, eti? Tutaonana asubuhi."

Akaangalia chini kiasi na kusema, "Sawa. Ulale salama."

"Haya," nikajibu hivyo na kumpita, nikielekea chumbani kwangu bila kumgeukia tena.

Nafikiri alijihisi vibaya, ama hata kama ikiwa hakujihisi vibaya, basi alijiuliza kwa nini sikufanya jambo lolote kuhusiana na tukio hilo dogo hapo sebuleni. Angefikiria labda sikupendezwa naye, lakini haikuwa hivyo.

Ni kwamba tu sikuona ulazima wa kuchukua hatua yoyote ama kusema lolote kuhusu hilo, na ingepaswa kubaki kuwa namna hiyo maana mimi na yeye bado hatukujuana vizuri, na mambo ya papara hayakuwa kwenye mtindo wangu wa kushughulika na watu; hasa wanawake.

Nikaingia zangu tu chumbani na kushusha neti, mbu wakiwa wengi utadhani wameajiriwa. Nikajilaza kitandani na kutumia muda mfupi kupita Facebook, WhatsApp na Twitch, kisha ndiyo nikaiweka simu chaji na kuanza kuhangaika kuutafuta usingizi huku nyimbo mbovu sana za mbu zikinikera mpaka kunako.


★★★


Nilikuja kuamka pakiwa pameshakucha sana, yaani ile kuamka ya hauwezi kusinzia tena. Mwili wangu ulikuwa na ukawaida wa kuniamsha mapema mno, nami ningeendelea kulala na kusinzia tena mpaka muda ambao ningechoka kuendelea kulala. Ila ilikuwa hivyo tu nyakati ambazo sikuwa na kazi za kufanya, kama wakati huu, na hata leo nilikuwa nimeamka mara kadhaa na kuendelea tu kulala mpaka sasa sasa.

Nikajitoa kitandani na kuchukua simu yangu, nami nikakuta ni saa nne asubuhi. Kulikuwa na missed call kadhaa kutoka kwa watu wangu wa karibu na jumbe kadhaa pia, nami nikawatafuta na kuongea pamoja na baadhi yao kwa ufupi, kisha nikanyanyuka na kwenda kabatini huku napiga mihayo.

Nilipenda sana haka kahali ka kuwa mwenyewe, yaani kama namna ambavyo mtu angechagua kwenda likizo na kutembelea sehemu za kifahari, lakini mimi nikaja sehemu hii yenye mazingira ya kawaida tu, kwenye uswahili zaidi, na nilikuwa na hamu ya kuona namna ambavyo watu kiujumla wangenitendea kadiri ambavyo muda ungepita nikiwa huku.

Kitu ambacho nilihitaji kufanya kwa sasa ilikuwa ni kununua mswaki na dawa mpya za kusafishia meno, ili kinywa kikae fresh. Nikavaa kaushi nikiwa na bukta kwa chini ili nitoke kwanza mpaka nje kwenda kukojoa, lakini nilipofungua mlango wa chumba hicho kidogo, nikaanza kusikia maongezi baina ya wanawake wawili.

Sauti ya mmoja niliifahamu, ikiwa ni Ankia, lakini ya mwenzake sikuijua. Alikuwa rafiki labda, na mada waliyoizungumzia ilimhusu mwanamke yule niliyekutana naye jana mpaka akanipa lifti kwa msisitizo wangu wa kuumwa kimaigizo, yaani Miryam.

"Enhe..." nikasikia Ankia anaitikia.

"Basi, nasikia mchumba amefika, tena na wazazi wake sijui... Miryam hajamtolea nje! Eheee... shoga acha tu..." mwenzake akamwambia hivyo.

"Kamfukuza?" Ankia akauliza.

"Eeeh! Tena limeletwa hadi na gari, huwezi kuamini, lakini limbwende bado tu limekaza vyuma! Ahahaaa... haki ya mama. Miryam hataki kuolewa, yaani hataki. Sijui wamroge?"

"Atakuwa na sababu zake..."

"Sababu zipi Anki? Umri unaenda, anazeeka, hajazaa bado, hayo yote alikuwa ananiambia Shadya leo yaani wameshamtafutia wachumba wa maana wanaoweza kummwagia mipesa ambayo sisi wenzake tunaililia ila haitufikii... shoga! Anaringa huyo! Anafikiri wataendeleaga tu kumpigia magoti eti!"

"Shadya ndiyo kakwambia ya jana?"

"Eeeh, kaniambia wamemletea mpaka na gari lakini kalikataa. Kisa? Eti bado anaitunza familia yake, inamhitaji. Kwani anashindwa kuwatunza hata akishaolewa, ama ni midenguo tu?"

"Asa' unafikiri watafanyaje, watamlazimisha? Kama hataki ndiyo hivyo... inabidi wamwache tu..." Ankia akamwambia.

Inaonekana walikuwa wanapiga umbea kuhusu ile ishu ya jana ya kuchumbiwa kwake Miryam, na ya huko kufika mpaka kwa Ankia namna hii ilimaanisha yangesambaa kwingi.

"Hana lolote mi' nakwambia, huyo mwanamke malaya tu. Usikute hapo alipo anatoka na limme la mtu huko, af' akirudi anajifanyaga mtakatifu kweli... eti familia yangu wananihitaji..." mwenziye akaendelea kusema.

"Huo wivu wako mama Chande unakufanya unamjaji vibaya dada wa watu. Mbona me naona yuko poa tu? Hayo ni maisha yake, acha ajiamulie anachotaka," Ankia akamwambia.

"Mm? Asa' me nimwonee wivu kisa nini? Hako kaweupe ama?"

"Siyo weupe tu, huyo dada mzuri sana ndiyo maana unaona wengi wanajibebisha hapo. Lakini hana shobo za huko, la sivyo angewaacha kweli watu wake wa ukoo na kuolewa na litajiri kama angekuwa hawajali..."

"Aaa wewe mtetee tu, ila tuulize sisi tunaomjua ndiyo utaambiwa. Siku akija kumchukua bwana wako ndiyo utasema mama Chande aliongea kweli..."

Ankia akacheka kidogo na kusema, "Unadhani hata kama ni wewe ukimchukua bwana wangu nitahangaika basi?"

"Wewe huyo? Ulivyo na wivu hivyo?"

"Akhaa, me siko hivyo. Mwanaume akiona abebe ndoo nyingine ya zege me nasubiri mbebaji mwingine aje anichukue, mbona wapo wengi tu?" Ankia akasema hivyo.

Kauli yake ikanifanya nitabasamu. Alionekana kupenda misemo sana, na alikuwa na akili iliyofunguka (open mind).

"Nyoo utaongea hivyo na mtu mwingine asiyekujua, ila me hunidanganyi. We' ndo' wale wanaopiga hadi na magoti, michozi na mikamasi inakuvuja kisa umeachwa na mapenzi!" huyo mama Chande akamwambia hivyo.

Ankia akasikika akicheka.

Mama Chande akacheka kwa nguvu pia na kusema, "Au midadi imeshapanda kwa mchina wako?"

"Eh, wewe, punguza sauti... atakusikia..." Ankia akasikika akisema hivyo.

Mada ikawa imegeukia kwangu, nami nikaweka umakini zaidi.

"Usianze mambo yako. Kwanza umejuaje kuhusiana naye?" Ankia akamuuliza.

"Fatuma kamwona jana anaingia, akaniambia. Mbona umemficha ndani tu shosti, hutaki tumwone mchina nini?" mama Chande akasema.

"Siyo mchina. Ni mpangaji wangu... siyo mtu wangu. Punguza kelele," Ankia akamwambia.

"Mpangaji siku ya kwanza, ya pili ashakunyandua, na najua ndo' unachosubiri..."

"Ila mama Chande..."

"Nini, kwani uwongo? Utasahau hadi kumtoza kodi akishaanza kuku(.....)," mama Chande akasema hivyo.

Nikacheka kidogo kwa pumzi huku nikitikisa kichwa. Huo ndiyo ulikuwa ule uswahili wenyewe, tena na hapo ni kwa kiasi chake tu, nami nilipenda sana.

"Acha sifa mama Chande, nitakufukuza sasa hivi..." Ankia akamwonya hivyo kwa sauti ya chini.

"Unafikiri natoka hapa bila kumwona mchina? Umeliwa! Hatoki mtu hapa hata usipopika," mama Chande akasema.

"Na ukimwona ndiyo itakuongezea nini labda?"

"Buzi... huwezi kujua..." mama Chande akamwambia.

"We' ni mshenzi..." Ankia akamwambia hivyo kwa sauti ya chini.

Mama Chande huyo akacheka kiumbea kiasi huku Ankia akimtuliza, nami nikaona nimpe alichokitaka.

Nikarudi sehemu ya kabati na kurekebisha uso kiasi, kisha nikavaa na T-shirt kusitiri mikono. Nywele zangu zingekuwa na mwonekano fulani wa nywele laini za kiarabu zilizogurugika kila mara nilipotoka kuamka, kwa hiyo sikuzichana kabisa ili nikitoka ionekene kweli ndiyo nilikuwa nimeamka muda huo huo.

Nikaenda kuufungua mlango, nami nikatoka zangu na kuanza kuielekea sebule. Niliweka uso makini, kama vile sijali lolote hapo, nami nilikuta Ankia akiwa amekaa kwenye sofa moja pamoja na huyo mwanamke.

Mama Chande alikuwa mwanamke mwenye umri mkubwa kiasi cha kufikia miaka 40, mweusi wa maji ya kunde, mwenye mwili mwembamba kiasi, na ningeweza kusema urefu wake akisimama ungekaribiana na wangu kabisa. Alikuwa na sura iliyokomaa, akiwa ameweka kope za bandia machoni na lipstick nyekundu mdomoni, huku vazi lake likiwa ni jezi nyeusi ya Yanga iliyoficha matikiti maji makubwa yaliyonyanyuliwa juu bila shaka kwa sidiria, pamoja na suruali nyeupe ya skinny iliyobana mapaja yake yaliyotokeza kiasi. Alikuwa na nywele fupi zilizopakwa dawa na kutiwa rangi ya njano mpauko, naye alifuga kucha ndefu mikononi zilizopakwa rangi nyekundu. Labda zilikuwa za bandia.

Ankia yeye alikuwa amevaa dera la njano lenye maua-maua, huku akijifunga kilemba kichwani kama nilivyomkuta jana tu, na kwa pamoja waliniangalia usoni nilipowakaribia zaidi.

"Za asubuhi?" nikawapa salamu kwa sauti tulivu ya kiume.

Kwa wanawake wa aina yao, shikamoo isingefaa hata kama wangekuwa na miaka 50 maana walijiweka kibinti-binti zaidi.

"Aa salama..." mama Chande akasema hivyo.

"Nzuri tu. Umeamkaje?" Ankia akaniuliza hivyo huku akitabasamu kiasi.

"Vizuri tu, na nyie?" nikawauliza.

"Ah kama unavyotuona. Unalala kweli..." Ankia akaniambia huku akitabasamu.

"Ndiyo, ni uchovu. Wacha niingie uani," nikamwambia.

"Sawa," Ankia akajibu.

Nikawapita na kutoka nje ya mlango wa kuingilia ndani hapo, na sikuwa hata nimetoka sehemu hiyo kabisa nami nikaanza kumsikia huyo mama Chande akisema mimi ni mweupe mno jamani!

Nikakaza tu tabasamu na kwenda kukojoa, nami nilipotoka huko nikatazama upande wa ile nyumba niliyoingiamo jana. Sikuliona gari lile aliloendesha Miryam mnunaji, ikiwa wazi aliondoka bila shaka, lakini nikaweza kumwona kijana fulani akiwa anacheza mpira peke yake kwa kuupigisha mara nyingi kwenye mguu mmoja; tunaita danadana.

Huyo alikuwa mgeni kabisa kwangu, hata jana sikumwona pale. Alikuwa na weupe pia, umri wake si mbali sana kufikia miaka 27 kimakadirio, akiwa na mwili mrefu kiasi na mwembamba pia. Alivalia jezi ya Simba na bukta nyeupe, na alinyoa mtindo wa kiduku bila kuwa na nywele nyingi sana juu ya kichwa. Kiduku kifupi. Nikawaza labda alikuwa ndugu yao mwingine akina Zawadi mweupe, nami nikarudi zangu tu ndani kwa Ankia.

Nikamkuta pamoja na shosti yake, lakini wakati huu Ankia akiwa amesimama usawa wa meza, na mezani hapo alikuwa ameweka chupa ya chai, kikombe, chombo cha kutunzia sukari na kijiko chake, pamoja na bakuli jeupe la udongo lililofunikwa kwa bakuli lingine la aina hiyo hiyo. Mwenzake alikuwa ametulia tu akionekana kuwa bize na simu eti, nami nikamtazama Ankia usoni na kuona anatabasamu kiasi.

"Karibu chai," akaniambia hivyo.

Ahe! Nikarudisha tabasamu hafifu tu, kisha nikamwambia, "Asante. Nahitaji kusafisha mdomo kwanza, sijui hili duka la hapa nje wanauza miswaki?"

"Eee anauza," Ankia akaniambia.

"Aaa basi poa, ngoja nifate kwanza afu'..."

"Hamna, usijali, nipe tu hela nikufatie," Ankia akanikatisha.

Nikamwona kwa jicho la chini rafiki yake akitabasamu kwa kuikunja midomo kwa njia ya kichokozi, nami nikamuuliza Ankia, "Sikusumbui?"

"Hamna wala, haunisumbui," akanijibu.

"Haya, nakuja," nikamwambia hivyo na kisha kumpita kulekea chumbani.

Sijui ikiwa kila alichokifanya kunielekea ilikuwa huduma nilizohitaji kulipia baadaye labda, lakini huo mtindo wa kunifanya mimi nionekane kama mume wake vile haukuwa mbaya sana kwangu. Huenda aliwatendea wageni wake wote namna hiyo.

Nikachukua buku tano na kurejea sebuleni tena, nikimpa anifatie dawa ya meno na mswaki imara, naye huyo akaenda zake. Nikaachwa sebuleni pamoja na mama Chande mwongeaji; aliyeonekana kupenda kusema sana watu pamoja na yule Shadya wa jana. Wakati huu alikuwa kimya tu, akiyapa macho yake ubize mwingi kutazama kilichoonyeshwa kwenye TV, huku mimi nikikaa sofa la pembeni nikipitia mambo fulani kwa simu yangu bila kujishughulisha naye.

Sikumsemesha hata kidogo mpaka Ankia aliporudi, nami nikapokea vifaa vyangu vya usafi wa mdomo pamoja na chenji, shwaa chumbani. Yaani wangeelewa tu mabiti. Kama vile ambavyo Ankia alikuwa ameniambia usiku uliotangulia, mimi pia sikuwa mtu wa kushoboka na mtu yeyote kabisa, labda mpaka awe amenielewa na kunionyesha hilo wazi, ndiyo na mimi ningezisoma naye ikiwa pigo na tabia zingekubaliana. Msemo wa Fid-Q ndiyo uliofaa kuelezea jinsi nilivyokuwa kihalisi; mimi ni mtu wa watu, lakini siyo mtu wa kila mtu!

Nikatoka zangu tena na kwenda kuswaki kwenye lile sinki la kuoshea vyombo pale nje, kisha nikarejea ndani na kukaa sofani ili nishushe chai aliyoniandalia mwenye nyumba wangu. Yaani ilikuwa ni baada ya mimi kukaa tu ndiyo na yeye akanyanyuka na kuanza kuifungua chupa ya chai, kisha akaimimina kwenye kikombe. Ilikuwa ya maziwa kabisa, nami nikawa namtazama tu kwa utulivu.

Mara kwa mara niliweza kuona bila kuangalia kwamba mama Chande alinitupia jicho sana, lakini umakini wangu wote ulikuwa kwa Ankia. Akanisogezea meza taratibu, kisha akarudi kukaa na shosti yake. Mwanaume nikajiongeza kwa kuweka sukari iliyonitosha, kisha nikafunua bakuli kukuta ni maandazi laini, ya moto. Nikawakaribisha, nao wakashukuru na kuendelea kukaa kwa utulivu kama Malaika eti.

Nikaanza kukipa kinywa ladha tamu ya chai, kisha nikaanza kutafuna na maandazi. Chai ilikuwa ni tamu balaa, lakini maandazi, ah yaliniacha hoi. Yalikuwa yale maandazi ambayo ukiyaangalia nje yanakuwa yametuna kinoma ila ukilishika na kuling'ata unaambulia kula ngozi tu maana ndani panakuwa hewa!

Sijui huwa hata wanayapikaje wale wanaoyauza, yaani hamna nyama kwa ndani kabisa, na wanaume hatuyapendagi ya hivyo basi tu ukikuta mwanamke kashayaweka unayapiga kwa kujilazimisha. Wanawake hao wakawa wanaongeleshana tu kwa sauti za chini na kucheka-cheka mpaka nilipomaliza chai yangu tamu.

Ankia akatoa vyombo huku nikimshukuru, kisha akavipeleka jikoni na kurudi kuniletea maji ninawe. Nilishindwa hadi kujizuia kutabasamu bila kumwangalia, lakini nilijua na yeye alikuwa anatabasamu. Akasafisha meza na kupeleka maji hayo huko jikoni, kisha akarudi sofani na kukaa tena.

Nikamuuliza ni muda gani ambao alitaka twende kwa mwenyekiti, naye akasema muda wowote tu ambao mimi ningekuwa tayari. Nikasema sawa, nimwache atumie muda huu na rafiki yake kisha mida ya saa saba hivi twende pamoja huko, ili aweze kunionyesha na njia za mitaa hiyo kwa ufupi. Kama kawaida yake akasema haikuwa na neno, nami huyo nikaelekea chumbani.

Hata kabla sijaufungua mlango wa kuingilia chumbani, nikamsikia mama Chande akisema kwa sauti ya chini eti "linanukia vizuri," nami nikaingia ndani humo tu na kukiendea kitanda ili nipumzike kidogo. Hii sehemu ilinikosha kwa kiasi chake!

★★

Saa kama moja hivi likapita nikiwa nimejilaza tu kitandani. Kulikuwa na joto ingawa niliacha milango ya madirisha wazi, nami nikawa nafikiria kwenda kuoga upesi kulipunguza fukuto baya mwilini.

Nikiwa namalizia kuchat na marafiki zangu kwenye simu mlango wa chumba ukagongwa. Nikasema tu 'karibu,' nao ukafunguka na mwanamke mwenye mji kuingia. Wakati huu nilikuwa nimelitoa T-shirt mwilini na kubaki na kaushi na bukta, nami nikakaa badala ya kulala.

Ankia alikuwa ameingia na mwonekano tofauti. Alivaa T-shirt nyeupe yenye mikono mifupi iliyoubana mwili wake wa juu na kufanya kifua chake kionekane kutuna sana kwa mbele, pamoja na sketi ya zambarau ya kitambaa laini iliyombana haswa na kulichoresha umbo lake la chini vizuri mno. Iliishia magotini, miguu yake yenye unene wa chupa ya bia ikionekana vizuri kwa usafi wake.

Usoni alikuwa amejitengeneza vizuri pia, na sasa hakuwa amevaa kilemba bali nywele zake ndefu za kusukwa aliziacha wazi ili sisi wote tuzione. Na harufu yake tamu ilikijaza vyema chumba hicho.

"JC... jiandae twende. Niko tayari," akaniambia huku akiwa ameushikilia mlango.

"Eh, saa sita na nusu... usingekuja labda hata ningesinzia. Asante," nikamwambia.

Akatabasamu kidogo.

"Ngoja 'nkapige maji faster af' twende. Umedamshi kweli," nikamwambia.

"Ahahah... asante. Nitakusubiri, ukimaliza nishtue... niko chumbani," akasema.

"Poa."

Akataka kugeuka ili aondoke.

"Subiri kwanza, eti hivi..."

Akaniangalia tena baada ya mimi kuanza kusema hivyo.

"Hiyo feni hapo sebuleni inafanya kazi?" nikamuuliza.

"Aa hiyo... hamna. Ilikuwa nzima ikaharibika, nimeshaipeleka kwa mafundi lakini wamenila tu hela halafu haijatengemaa. Nikaikatia tu tamaa," akaniambia hivyo.

"Bado inaonekana nzuri kweli, mafundi wengi unajua ukiwapelekea mashine hata zikiwa na tatizo dogo tu, wanatoa vitu fulani na kuviiba... halafu wanakuja wanakwambia tatizo ni kubwa sana ili wale tu hela yako..."

"Eti eeh..."

"Ndo' hivyo. Sema... nitakuja niiangalie. Ninaweza nikafanya maajabu ikakaa fresh."

Akatabasamu kidogo na kusema, "Utakuwa umenisaidia sana."

"Haya poa. Ngoja nifanye kuoga chap," nikasema hivyo huku nikisimama.

"Poa," akajibu hivyo na kuilamba midomo yake kisha kuibana.

Alipogeuka ili aondoke, nilishusha macho yangu kutazama umbile lake la nyuma, nami nikatabasamu tu kwa jinsi ambavyo lilionekana kuwa zito na lenye mikunjo mingi sana. Ni vitu ambavyo wanaume huwa tunapenda sana, hatushangai bodaboda ikiingia mtaroni shauri ya mwendeshaji kushindwa kujizuia kuvitazama!

Nikavua nguo upesi na kwenda kuoga, na nilikuwa na uhitaji wa kununua sabuni yakwangu peke yangu kwa ajili ya matumizi, lakini iliyokuwemo humo bafuni ikanisogeza tu kwa wakati huu. Nikaingia chumbani na kujiweka vizuri kimwili, kisha nikatupia viwalo safi mwilini. T-shirt laini nyeusi yenye mikono mirefu pamoja na jeans la samawati iliyokoza, zilinikaa vyema sana kwenye mwili wangu wenye uimara.

Nikatengeneza nywele vyema na kuvaa saa yangu niliyokuwa nimeitunza tu kwenye begi, na hiki ni kitu ambacho nilipenda sana kufanya hasa nilipotaka kutoka kutembea sema kwenye safari ya kuja huku sikutaka tu kuivaa mkononi. Kwa hiyo nilipokaa fresh nikajinukishia manukato yangu na kumfata bibie Ankia, kumwambia tujage.

Mwanamke akatoka, akionekana kuwa na furaha kiasi, nami nikamwambia anitangulie maana yeye ndiye aliyekuwa ameibeba dira ya Mzinga. Akatabasamu na kutangulia, nasi tukatoka mpaka nje zaidi baada ya kuifunga milango kwa funguo.

Tukaanza kutembea kuzipita nyumba kadha wa kadha, taratibu, na aisee, kila mtu alitutazama. Nadhani Ankia alikuwa tu na ile akili ya kuzaliwa kufatisha namna ambavyo mimi niliitikia mazingira kwa kutowatazama watu na kujali nyendo zetu tu, lakini angewasemesha kifupi wale waliomfahamu walipompa salamu na kuendelea kutembea pamoja nami.

Nilikuwa wa namna makini sana. Shobo pembeni, ili wenye kushoboka ndiyo washoboke. Tukakata mtaa na kuingia mwingine kuelekea Mzinga, ambako kulikuwa na shughuli nyingi zaidi na masoko, na kama kawaida macho mengi yalikuwa kwa "mchina" mgeni na mwanamke wake. Najua wengi wao walifikiri hivyo.

Tukafika mpaka pale ambapo nilishushwa na daladala ile usiku wakati nakuja, kwenye lami, nasi tukakunja kona kidogo tu na mbele zaidi tukaifikia ofisi ya "Kata ya Mzinga." Oh kumbe ilikuwa ofisi ya kata? Ankia akanipeleka mpaka kuifikia, tukiwa tumepita kijiwe kikubwa cha wadau waliopenda kunywa kahawa na tangawizi kali, nasi tukaenda kuonana na mwenyekiti.

Watu wa humo walitutendea kwa njia fulani ya unyenyekevu, kana kwamba ni watu wakubwa ndiyo walikuwa wameingia, na baada ya Ankia kueleweshana na mwenyekiti kuhusu suala letu la upangishaji, nikapewa makaratasi ya kutia sahihi pamoja na Ankia na kopi za kutunza. Nilihitajika kupigwa picha ndogo za 'passport' ili zibandikwe pia kwenye karatasi, kisha jamaa akaweka mihuri yake, nasi tukasepa. Oh aliomba hela ya soda, nami nikampa elfu mbili kutoka kwenye chenji aliyonirudishia Ankia muda ule.

Tukatoka zetu tena ili turudi pamoja nyumbani. Ndiyo, nyumbani. Angalau Ankia alikuwa ameanza kunipa malezi yaliyonifanya nijisikie kuwa nyumbani, na bado sikuwa nimemwonyesha shobo nyingi sana mwanamke huyu hata kama hali ya kuzoeana ilianza kuwepo baina yetu. Ndivyo nilivyokuwa.

Tulipoanza kurudi tukapita sehemu waliyotengeneza chips, mishikaki, nyama za kuku, na ndizi za kukaangwa. Nikamwambia Ankia twende hapo ili nichukue msosi turudi nao maskani, naye akakubali. Tukaenda, nami nikaomba huduma. Nilihitaji kujua ikiwa Ankia alipenda kula vyakula hivyo, na ni mwanamke gani asiyependa? Basi tu, si unajua swaga?

Nikamuuliza, naye akakubali. Kwa hiyo nikaomba watupatie chips mayai mbili, kuku za kukaangwa vipande vitatu-vitatu kila chips, pamoja na mishikaki mitano-mitano. Kutazamwa sana na aidha wanawake au wanaume bado kuliendelea hata kwa sehemu hiyo, na inaonekana ilimpa Ankia hisia za ufahari kutokana na kujua alielekezewa fikira kuwa pamoja nami. Si ile kwamba angeonewa wivu? Mimi nilielewa.

Tukapatiwa misosi yetu, nasi tukapiga mwendo tena mpaka kule Masai tulipoishi. Zamu hii tulitumia njia nyingine ili Ankia anizoeshe maeneo zaidi, na baada ya kufika pale dukani nikamwambia achukue soda mbili pamoja na sabuni nzuri za kuogea, nami nikatangulia nikiwa na funguo ya mlango wa kule ndani.

Yale makaratasi ya mwenyekiti alikuwa nayo Ankia, yakiwa salama ndani ya bahasha, naye akawa amefika ndani pia pamoja na chupa mbili za Pepsi baridi na kuziweka mezani. Tayari na mimi nilikuwa nimeweka mifuko ya vyakula mezani, hivyo Ankia akanipatia sabuni mbili alizonunua nami nikampa moja, kisha nikaenda chumbani ili nibadili nguo na kuvaa nyepesi.

Nadhani muda mfupi niliotumia kubadili mavazi ulimtosha sana Ankia kufungua vyakula na kuviandaa kwenye sahani safi, kwa hiyo niliporudi sebuleni nikakuta vikiwa wazi tayari kukamuliwa kisawasawa.

Nikakaa sofani na kujiandaa kula, naye akaniletea maji na kuninawisha. Akanawa pia, na alipoanza kusogeza meza upande wangu, simu yangu ikaita, nami nikapokea na kuzungumza na ndugu yangu mmoja aliyekuwa amenipigia.

Ankia akafungua soda zetu na kisha kukaa kwenye lile sofa dogo, lakini nikamwonyesha mshangao kwa sura yangu na kumpa ishara kuwa aje kukaa kwenye sofa nililoketi mimi. Anakaa mbali kufanya nini sasa? Akatabasamu kidogo na kuibana midomo yake kwa shau, kisha akaja na kukaa karibu yangu.

Tukaanza kula pamoja, huku wa kwenye simu akigoma kabisa kutaka kuniacha. Ikabidi nimwambie simu inazimika hivyo ningemtafuta baadaye, nami nikakata na kuhamishia umakini wangu kwa Ankia. Alikuwa akijitahidi kula kistaarabu eti mbele yangu, lakini nikamwambia ajiachie zaidi maana mimi nilipenda kula kwa fujo hasa chakula kikiwa kitamu sana, na kama niko na mtu niliyemzoea.

Muda si muda tukawa tunakula huku tukifurahia maongezi yenye utani mwingi, nami nilimchekesha sana kwa kumsimulia hadithi za baadhi ya mambo mengi niliyojua. Alikuwa na kicheko fulani hivi cha chini-chini chenye kuvutia, nami nilielewa kwamba mbele yangu alikuwa anajitahidi kukibana kile kicheko cha kimbea kama angekuwa anapiga porojo na mwanamke mwenzake.

Tukawa tumemaliza kula chakula hicho kitamu sana, naye eti akanishukuru kwa kumnunulia chips na kuku. Nikamwambia acha zako wewe, naye akatoa vyombo na kuvipeleka jikoni, kisha akarudi na kukaa kwenye sofa pembeni yangu tena bila mimi kumwambia afanye hivyo.

Akachukua rimoti na kuiwasha TV, akianza kubadili chaneli huku mimi nikiwa nimekaa kwa kuegamia mgongo zaidi, nikiwa nimeshiba kweli, kwa hiyo yeye akaonekana mrefu kunipita maana alikaa kitako. T-shirt alilovaa lilikuwa limeinuka juu kidogo kuniruhusu nione nyama laini ya kiuno chake, nami nikamtazama usoni.

Ulionekana kwa upande kutokea nilipokuwa nimekaa maana uso wangu ulikuwa nyuma yake zaidi, na akiwa bado bize kubadili chaneli, nikaona nimchokoze kwa kukigusa kiuno chake kwa kiganja changu.

Akashtuka kidogo na kunigeukia, nami nikamtazama machoni kwa njia ya kichokozi zaidi huku nikiendelea kutembeza vidole viwili kwenye kiuno chake. Akanipa tabasamu fulani hivi la nyodo, kama hataki lakini kwa furaha eti, kisha akaigeukia TV tena bila kunizuia nisiendelee kumfanya hivyo.

Nikaona nimchokoze zaidi kwa kuingiza vidole vyangu ndani ya T-shirt lake kupitia mgongoni mpaka kufikia ubavu wake mmoja, kisha nikamtekenya kidogo.

Akashtuka na kusogeza nyonga mbele huku akisema, "Iih, wewee..."

Aliniangalia kwa macho yaliyoonyesha hisia zinataka kumkolea, nami nikacheka kidogo kwa pumzi, kisha akarudisha mkono wake nyuma na kuutoa wangu mgongoni kwake kama kuonyesha anataka niache.

"Kwa nini mwanamke mzuri kama wewe unaishi peke yako?" nikamuuliza hivyo kwa sauti tulivu.

"Si nimependa tu?" akajibu bila kunitazama.

"Tokea lini umependa tu?"

"Tokea zamani."

"Mbona nasikia haukuwa unaishi peke yako?" nikamuuliza.

"Umesikia kwa nani?" akaniuliza hivyo na kuniangalia.

"Nina mitandao yangu..."

"Mitandao ipi wakati umefika jana tu?"

"Mengi yametokea jana kabla sijafika hapa, utajuaje?"

"Mhm..." akafanya hivyo na kuangalia TV tena.

Nikaingiza tena kiganja changu mgongoni kwake na kuanza kuukuna taratibu, kitu ambacho kilifanya niguse mikanda ya sidiria yake kwa nyuma, nami nikamuuliza, "Mume wako je?"

"Sina mume," akajibu bila kunitazama.

"Alienda wapi?"

"Sijui."

"Kwa nini aliondoka?"

"Si tuliachana?"

"Kwa nini mliachana?"

"Tulichokana."

"Kisa nyimbo za Ali Choki au?"

Akacheka kidogo.

"We' ni mzuri Ankia," nikamsifia kwa sauti zembe, makusudi.

"Uzuri wangu uko wapi?"

"Upo hapo hapo kwako."

"Mhm... huko Sinza ulikotokea hujaona wanawake wazuri?"

"Sijaona..."

"Unanipulizia moshi tu. Huko ndo' kuna pisi sana..."

"Hazikufikii..."

"Kwenda zako! Unanipaka tope tu, me kibonge wa Mbagala nitafanana na hao wanaojiona keki hapa jijini?" akasema hivyo na kukitoa tena kiganja changu mgongoni kwake.

"Me sivitaki hivyo vikeki bwana..." nikamwambia hivyo.

"Umeshapiga vingi eh?"

"Aa wapi, hata sijawahi kabisa..."

"Mh... nhaa..." akacheka kidogo.

"Ni kweli, si unaniona me bado mtoto?"

"Kwa hiyo kama we' bado mtoto?"

"Nahitaji malezi bora. Nani mwingine atanipa hayo sasa?"

"Si wa huko kwenu?"

"Me nataka ya huku..."

"Nenda Rangi Tatu utayapata..."

"Nimeshayapata mbona?"

"Wapi, Rangi Tatu?"

Nikaingiza tena kiganja changu mgongoni kwake na kusema, "Hamna, ni kwenye rangi yako."

"Rangi yangu imefanyaje?"

"Ni nzuri..."

"Mhm..."

"Una katabia fulani hivi nakapenda sana..."

"Kapi hako?"

"Unapozilamba na kuzibana hizo lips... na hayo macho lege..."

Akatabasamu kidogo na kuangalia pembeni, nami nikaushika ubavu wake ndani ya T-shirt lake. Akataka kuutoa mkono wangu, lakini nikauvuta mwili wake na kumfanya aegamie sofa kwa mgongo wake, na mpaka kufikia hapo nilikuwa nimeshasimamisha mnara wangu kule kati kwa hasira kali mno.

Akaweka kiganja chake kifuani kwangu huku akigoma kunitazama machoni, kwa kuwa sasa nyuso zetu zilikaribiana sana.

"Mm... JC..."

"Nini?"

"Hmm... mmhh..." akaishia kushusha pumzi tu.

"Mbona unakuwa hivyo?" nikamuuliza hivyo kibabe.

"Unanipenda... au unanitamani tu?" akaniuliza hivyo.

Khh! Mbona kaanza kuingiza bongo movie tena?

Nikamwambia, "Tunaanzaga kutamani. Kupenda ni baadaye."

Akawa anapumua kilegevu eti, huku mimi nikiwa bado nimemshika kiunoni na mkono mwingine ukilishika paja lake lililo ndani ya sketi aliyovaa, naye akasema, "Me siwezi..."

"Usiweze nini?"

"Kufanya unachotaka..."

"Kwa nini usiweze?" nikamuuliza.

"Wanaume waongo sana..." akaniambia kwa deko.

"Wamekudanganya wengi?"

Hakujibu na kuibana tu midomo yake.

"Lakini me si mtoto? Hapa unafanya tu kunitunza mama," nikambembeleza.

Akaniangalia machoni, nami nikawa bado nampa tabasamu la kichokozi. Nikamvutia zaidi kwangu kwa mkono ulioshika kiuno chake, naye akataka kujirudisha nyuma lakini nikamshika shingoni kwake na kuivuta mpaka karibu zaidi na uso wangu, kisha nikaanza kuibusu.

"...hhh... JC..."

"Nini?"

"Ana'eza akaja mmtu...."

"Nani aje bwana? Em' tulia..."

Nikazinyamazisha kelele zake na kuanza kumbusu kimahaba. Hakuwa mtaalamu sana wa kupiga denda lakini midomo yake mikubwa ilinyonyeka vizuri sana kwangu. Na angalau hakunuka mdomo la sivyo ningesitisha zoezi hilo hapo hapo!

(..........).

(..........).

(..........).

Akawa anaguna kwa pumzi nzito huku akiniangalia kama vile anateswa, maana niliyala kwa fujo na kuzidi kuyala tu. Akakibana kichwa changu kwake zaidi ili niendelee tu kumtafuna, na kiukweli, sikuliona hili likija.

Nikashtukia tu Ankia ameanza kutetemeka, akinibana zaidi, nami nikajitoa kwake baada ya yeye kuonekana anaondoa uchovu fulani ndani yake. Aliniangalia huku amelegea sana, nami nikamwangalia kwenye sketi na kuona imelowana mno.

"Doh! Ankia umeshalimwaga?" nikamuuliza.

Akatikisa kichwa kilegevu kukubali.

"Juu tu? Nikishuka chini je?"

"Nina muda mrefu..." akaniambia kwa deko.

"Maama... pole..." nikamwambia hivyo kwa kuiga ongea yake.

Akacheka kidogo kwa haya.

"Ila tusiishie hapa. Twend'zetu room nikukamue maji zaidi, au vipi?" nikamwambia.

"Mhm... unaongea wewe..." akasema hivyo kwa hisia.

"Hahah... twende bwana."

Nikaanza kusimama, naye akasimama pia kivivu huku akiona aibu kwamba sketi yake ilikuwa imelowana kama vile mtoto aliyejikojolea. Nikaanza kumvulisha, kwa kuishusha mpaka magotini, naye akaikunja na kuinyoosha miguu yake ili itoke yote.

(..........).

(..........).

Labda hisia nzito alizokuwa nazo zilifanya awe mzito mno, kwa hiyo nikawa namvuta kukielekea chumba huku amenishikilia na kutembea kwa kuyumba utadhani hakujiweza. Ni wazi alikuwa legelege, nami ningehakikisha anaishiwa nguvu hata zaidi kwa zawadi niliyoandaa kumpatia.

Kiukweli nilikuwa nimesisimka sana na nilitaka kufanya jambo la maana pamoja na huyu mwanamke, lakini ile tu tumefika mlangoni hizo fikira zikavurugwa.

"Ankiaa!"

Tukaivunja busu yetu na kuangalia upande wa nje, ambako ndiko sauti hiyo ilitokea. Ankia akaniangalia kwa njia ya kubabaika, akionekana kutaka kuniachia hasa baada ya kuutoa mkono wake kwangu, lakini mimi nikambana zaidi. Huyo aliyemwita kutokea huko nje alisikika akiwa anakuja upande wa ndani zaidi, ikiwa ni mwanamke ambaye sikumfahamu.

"Ankia mama, toka nje malaika akuone..." mwanamke huyo akasema hivyo.

Malaika gani huyo amekuja kuniharibia mood tena? Nikamwonyeshea Ankia ishara ya kutoitika, nikimzuia asijibu mwito huo, lakini akajitoa kwangu kwa nguvu kiasi huku akinionyesha ishara kwa kiganja kuwa niingie chumbani.

"We' vipi? Kwani lazima umpokee?" nikamuuliza hivyo kwa sauti ya chini.

"Ni mama Ashura, mwanakikundi mwenzangu mambo ya vikoba na madeni, nilimwambia aje leo tuongee... ingia chumbani..." akasema hivyo.

Alirudi sebuleni upesi na kuzitoa nguo zake pamoja na bukta yangu baada ya kuparekebisha vizuri, kisha akakimbilia chumbani kwake kwa njia ya kunyata. Hii kitu iliniudhi sana, basi tu. Nikasikia mja akiwa amefikia mlango, naye akamwita tena Ankia huku akiugonga.

"Abee..."

Ankia akaitika, nami nikiwa bado pale pale mlangoni kwenye chumba changu nikamwona akitoka huku akiwa ameshavaa dera lingine zuri na akijifunga kilemba kichwani.

"We' naye, unakaa ndani kama umekufa vile?" mwanamke yule huko nje akasikika akisema hivyo.

Ankia akanionyesha kwa ishara ya kiganja kuwa niingie chumbani, akinisisitizia kwa uso uliojaa hisia, nami nikasikia mlango unafunguliwa. Ikanibidi tu niingie chumbani humo na kufunga mlango, huku nikiwasikia walivyoanza kuongea mambo yao ya vikoba na ujorojoro mwingi wa wanawake.

Bonge moja la kata stimu maana hata mtambo wangu haukutaka kushuka chini bado, nami nikajilaza tu kitandani huku sauti za maongezi yao zikiendelea kunipa kero kwa sababu ya kukatishiwa starehe yangu. Angalau nilikuwa nimeshaanza kupiga hatua nzuri na mwanamke huyo lakini nayo ikawa imevurugwa.

Hakuna hisia nzuri sana ya kupiga hatua za jambo hilo kama ile unayoipata unapolifanya kwa mara ya kwanza na mtu fulani; haiwi kama kwenye mara ya pili, na ya tatu, na ya nne. Kwa hiyo huyo mama wa vikoba kuniharibia ishu yangu ya mara ya kwanza na Ankia kuliniboa sana, maana hata kama tungekuja kuwa kivyetu tena, ingeonekana kuwa ni mara ya pili; yaani mzuka hauwi kama vile unavyokuwa kwenye mara ya kwanza!

Ila nikaona fresh tu, labda nijizamishe kwenye jambo lingine ndani hapo mpaka huyo "mazeli" akiondoka. Nikavuta simu yangu, kuingia intaneti, bando limeisha. Agh! Sikuwa hata na mia Tigopesa ama la sivyo ningenunua hapo hapo, hivyo ikanibidi tu ninyanyuke ili niende kuchukua vocha pale kwenye duka la nje kwenye nyumba hiyo. Bado nilikuwa na boksa na T-shirt tu, kwa hiyo nikavaa suruali nyeusi na kuchana nywele vyema, kisha nikatoka kulifata duka.

Kama kawaida, niliweka uso makini na kumkuta Ankia akiwa pamoja na mwanamama huyo mweupe kiasi pia, akiwa amevaa nguo ya kitenge kama gauni. Nikamwamkia na kisha kuwapita tu, bila kumtazama Ankia hata kidogo. Nilionyesha kutojali sana kilichoendelea hapo, nami nikatoka zangu nje na kuvaa masai zangu miguuni, kisha nikaenda upande wa nje.

Ikiwa jioni ndiyo imeingia sasa, jua halikuwa kali sana na watu kadha wa kadha walionekana kupita ama kufanya mambo yao kwenye nyumba za majirani, nami nikafika dukani hapo na kusimama. Kulikuwa na mwanaume aliyesimama bila shaka kupata huduma, lakini alionekana kupata huduma ya maongezi zaidi kutoka kwa mwanamke yule niliyemwona jana usiku dukani humo.

Alivalia gauni lenye mikono mirefu pamoja na ushungi, akionekana kuwa mweupe na mwislamu pia, nao wakaacha kuzungumza baada ya mimi kufika. Nikaona hiyo ndiyo nafasi ya kuomba vocha ya buku nikaperuzike, lakini hapo hapo akawa amekuja mtoto mdogo kwa kasi sana na kuomba apewe unga wa sembe, nusu.

Mwanamke wa dukani alimpuuzia na kuniuliza ninataka nini, lakini nikamwambia amhudumie mtoto kwanza. Mwanamke huyo alikuwa ameweka sura makini zaidi baada ya mimi kufika hapo, na hata yule mwanaume akabaki kimya tu, na wala sikujisumbua kuwaweka akiba akilini.

Nikaangalia pembeni kiufupi wakati mwanamke huyo alipokuwa anampimia dogo unga wake, nami nikaona watoto wengi kiasi, wasichana sanasana, wakiwa wanacheza mchezo wa 'rede' pamoja. Binti mmoja akavuta umakini wangu, lakini ndiyo hapa nikasikia...

"Sh'kamoo..."

Nikamtazama mtoto huyo aliyekuwa ameniamkia hivyo hapo dukani, nami nikasema, "Marahaba. Hujambo?"

"Sijambo," kakajibu, kakiwa ni kasichana.

Kalionekana kuganda kunitazama sana usoni, nami nikarudisha macho yangu kwa yule binti mwingine. Kwa watoto waliocheza pale, ni yeye pekee ndiye ambaye hakuwa "mtoto." Ilikuwa ni yule binti niliyemkuta jana kwa akina Zawadi mweupe, Mariam bila shaka, naye alicheza 'rede' pamoja na wasichana wengine kana kwamba alikuwa mtoto.

Nikamwangalia kwa umakini zaidi. Alisimama usawa wa barabara pamoja na wenzake huku yeye akiwa mrushaji wa mpira ili kumponda aliye katikati, lakini jinsi alivyoitikia mambo mengi ilikuwa kwa njia... tofauti. Angerusha mpira na kuanza kurukaruka kwa shangwe hata kama hajamponda mtu, huku akipiga-piga makofi na kucheka kwa furaha sana.

Uso wake ulipendeza mno alipotabasamu, sura nzuri mno kama ya dada yake mkali ikanifanya niendelee kumwangalia tu, nikijiuliza pia ni kwa nini binti mkubwa angecheza mchezo wa watoto pamoja na watoto. Dogo akawa amepatiwa unga wake, na sasa zamu ikawa yangu kuomba huduma.

"Naomba tigo ya elfu moja," nikamwambia muuzaji.

Akaanza kuchangamka kuitoa vocha, nami nikiwa navuta pesa kutoka mfukoni nikawa nimeangalia tena upande wa Mariam.

Kutokea mbele zaidi kwenye barabara hiyo ya changarawe iliyoelekea pande mbili tofauti lilikuja gari jeupe, taxi aina ya Toyota Corola, taratibu tu, na wakubwa waliokuwa wameketi kwenye vibaraza vya nyumba zao wakawaambia watoto wasogee pembeni kwanza ili isije kutokea ajali.

Watoto kweli wakasogea pande za pembeni, na Mariam akavutwa mkono na wenzake wawili kuja upande wa duka niliposimama mimi. Ilionekana ni kama vile hakuelewa mambo vizuri sijui, lakini ghafla gari lile likaongeza kasi na kuanza kuelekea upande huu ambao Mariam na wenzake walikuja!

Nilishtuka. Mwanaume aliyekuwa hapo dukani akasema 'nyie,' kwa njia ya tahadhari, na wale wasichana wadogo wawili wakakimbia kuliepuka gari hilo lililokuwa likija kwa mwendokasi ulioongezeka. Mariam alibaki kusimama hapo huku akiliangalia kwa hofu, nami sijui niliingiwa tu na nini lakini niliruka na kumfikia karibu zaidi binti huyo, kisha nikampamia na kuanguka naye ardhini kwa kuviringika huku gari lile likiwa limetukosa kidogo tu!

Nilianguka na Mariam mpaka katikati ya barabara ile, na hilo gari likafunga breki ya ghafla kubakiza nafasi ndogo tu kuligonga lile duka. Yule mwanaume alikuwa amekimbilia upande mwingine, na nilisikia kelele za yule mwanamke wa dukani, aliyeogopa bila shaka.

Sasa nilikuwa chini, nikilala kwa juu kuufunika mwili wa binti huyu, nami nikalitazama hilo gari. Halikupitisha upenyo wa kuona kupitia kioo cha mlangoni, hivyo nisingeweza kumwona aliyekuwa ndani. Tairi la mbele likageuza kuielekea barabara, nalo likatoka hapo na kuingia barabarani; likinyoosha mbele kwa kasi mpaka kutokomea upande ule wa bar ya Masai.

Watu walianza kuongezeka sehemu hiyo, kelele zikizidi, vumbi likitawala angani, nami nikamtazama Mariam chini yangu. Alikuwa analia kwa kwikwi, huku viganja vyake vikitetemeka karibu na uso wake, nami nikanyanyuka na kuanza kumsaidia anyanyuke pia. Aliogopa sana mpaka akawa hataki nimguse.

Watu walipotusogelea, kila mtu alikuwa na lake la kuongea, na wanawake kadhaa wakamsaidia Mariam kusimama na kuanza kulipangusa dera lake huku wakimwambia asilie maana Mungu alisaidia ajali ile isitokee.

Nilitazama upande ule ambao lile gari lilielekea, kisha nikamwangalia huyo binti. Kama ni mimi peke yangu ndiye niliyeona kila kitu kilichotokea, basi ningekuwa mtu pekee wa kusema kwamba hiyo haikuwa ajali. Lilikuwa ni jambo lililopangwa kutokea, na mlengwa wa mpango huo usiojulikana ulitokea wapi alikuwa ni Mariam.

Nilijiuliza sana ni sababu ipi ambayo ingefanya binti huyo alengwe shabaha namna hiyo, na ni nani ambaye alitaka kumgeuza awe marehemu. Alikuwa amebeba nini kikubwa msichana huyu kilichofanya mtu yeyote atake kumuua? Kwa nini Mariam?


★★★★★★★★★

ITAENDELEA

★★★★★★★★★

Full Story WhatsApp or inbox

Whatsapp +255 678 017 280
Shukhran
 
MIMI NA MIMI

A Story by Elton Tonny

Familia, Urafiki, Mapenzi, Kazi, Tamaa, Hila, Usaliti, Siri, Mambo Ysiyotazamiwa

R-rated 18+

Enjoy!


★★★★★★★★★★★★★

SEHEMU YA NNE

★★★★★★★★★★★★★


Mlango wa geti la nyumba ile aliyoishi binti huyo ukafunguliwa, na hapo wakatoka watu watatu kuja nje bila shaka kuangalia nini kilikuwa kimetokea. Ilikuwa ni Zawadi mweupe na yule mwanamke mweusi, pamoja na yule kijana niliyemwona asubuhi hiyo hapo kwao akiwa anacheza mpira.

Huyo kijana akaja upesi mpaka alipokuwa amesimama Mariam, akianza kumwangalia na kumshika hapa na pale kumkagua kama aliumia, na akiuliza nini kilikuwa kimetokea. Mariam akamkumbatia kwa nguvu sana huku akilia mno, na watu walioona tukio lile, hasa yule mwanaume aliyekuwa amesimama pale dukani kabla ya ajali, wakawa wanamwelezea huyo kijana mambo yote yaliyojiri.

Zawadi mweupe na mwenzake wakafika hapo pia wakionekana kuwa na hofu mno, huku watu wakiwaambia isingekuwa ya mimi kumsukuma binti huyo basi mabaya mengi yangekuwa yamempata. Ni muda huo huo tu ndiyo Ankia akawa amefika hapo nje pia na yule mmama aliyekuwa naye ndani, pamoja na muuzaji wa dukani, naye akanisogelea na kunishika mkononi, akiniuliza ikiwa nilikuwa sawa.

Nilitambua kwamba wengi walitaka kunisikia nikiongea kwa sababu walinitazama mno, lakini sikusema lolote maana bado mapigo ya moyo yalidunda kwa nguvu mno na nilihisi miguu ikitetemeka kiasi kutokana na nguvu kunitoka.

"Ma' mkubwa, mpeleke Mamu ndani..."

Huyo kijana aliyekumbatiwa na Mariam akamwambia hivyo Zawadi mweupe, na mwanamke huyo akamchukua binti kweli na kuanza kwenda naye huku akimbembeleza. Yule mwenzake mweusi akanisogelea huku akinitazama kwa hisia sana.

"Asante sana baba'angu. Mungu akubariki, yaani sijui bila wewe ingekuwaje jamani..." akaniambia hivyo.

"Kaka... nashukuru sana kwa kumsaidia mdogo wangu. Sina uwezo wa kukulipa, lakini naomba ujue Mungu atakubariki mara mia zaidi. Yaani... ninakushukuru sana," huyo kijana akaniambia hivyo.

Ahaa! Kumbe alikuwa kaka yake Mariam pia? Basi bila shaka huyu alimfata Miryam kiukubwa kwa ndugu hawa, nami nikamwambia, "Haina shida kaka. Hakuna malipo yoyote yanayoweza kulinganishwa na uhai wa mdogo wako, kwa hiyo usijali. Nafurahi tu yuko salama."

Hatimaye watu wakawa wamenisikia nikiongea.

"Ubarikiwe sana baba," yule mwanamke akaniambia.

"Amina," nikamwitikia.

"JC, unatoka damu..." Ankia akasema hivyo huku akiushika mkono wangu.

Kweli nilihisi maumivu ya kukwaruza kwenye mkono, lakini sasa nilipojiangalia, nikaona damu zikiwa zinavuja kutokea kwenye kiwiko.

"Eh! Pole baba jamani... twende tuka... Tesha si kuna dawa ndani?" huyo mama akasema.

"Ndiyo, ipo. Twende bro tukapasafishe..." huyo kijana, Tesha, akaniambia hivyo.

"Hamna shida mama... nitamnawisha tu huku kwetu na kupatibu. JC, twende ndani," Ankia akaniambia hivyo.

"Ankia, tunaomba tumpe tu huo msaada angalau, maana amemsaidia sana Mariam. Tafadhali," huyo mama akasema.

Tesha akanisogelea na kunishika begani kwa njia ya msisitizo kuwa niende pamoja nao, nami nikamtazama Ankia machoni kwa ufupi. Alionekana kuhuzunika mno kwa ajili yangu, nami nikaamua kwenda pamoja na Tesha na mama yule mpaka ndani kwao. Ankia akatufata, huku watu wengine wakitutazama mpaka tulipoishia ndani.

Sikuwa nimefikiri ningeiona siku hii ikibadilika ghafla namna hiyo, na bado nilikuwa nikijiuliza maswali mengi kuhusiana na huyo Mariam. Tesha akaniongoza kufikia bombani, naye Ankia akanisaidia kuinawisha mikono yangu sehemu ilipochafuka na kuumia. Mavazi yangu yalijaa vumbi chafu sana, yakiwa na uhitaji wa kufuliwa upesi kabla uchafu haujakomalia hapo.

Tukaenda kibarazani pale baada ya kumaliza, na yule mwanamke mweusi alikuwa ameshaleta boksi lenye pakti nyingi za pamba, bendeji, na dawa. Akanisaidia kunipaka dawa kali sana kwenye michubuko yangu na kisha kufuta-futa kwa pamba, kisha Ankia akanifunga bendeji mkononi usawa wa kiwiko na kuniwekea plasta kwenye michubuko. Nikashauri afanye mambo yote hayo kwa njia nyepesi kuruhusu vidonda vipumue.

Baada ya hapo, nikawashukuru kwa msaada wao na kuwaambia ningekwenda kuyatoa mavazi machafu na kujisafisha sasa, nao wakakubali hilo na kunipa karibu ya mara nyingine tena kufika hapo kwao.

Tesha alionekana kuwa kijana imara, mjanja, na mwenye kujiamini. Huo ulikuwa ni mtazamo wangu wa kwanza tu kumwelekea kwa kuwa singeweza kujua utu wake kihalisi, kwa hiyo tukaagana vizuri tu huku akiniambia angekuja kunicheki baadaye kuona kama hali yangu ilikuwa nzuri. Nikatambua tu kwamba alipendezwa nami upesi sana, kwa hiyo nikaondoka pamoja na Ankia kurudi ndani kwetu.

Ankia alionekana kujali sana kilichonipata. Aliniuliza ilikuwaje-kuwaje mpaka kilichotokea kutokea, nami nikaeleza tu kwa ufupi namna mambo yalivyokuwa. Hamu ilinitoka kabisa shauri ya jambo hilo. Nikamwambia ningeenda tu kuoga na kisha kupumzika, nami nikafanya hivyo bila kusumbuka tena kuwaza kuhusu ile ishu yangu ya awali pamoja na mwanamke huyu.

Nilianza kujali zaidi kuhusu hali ya yule mwanadada niliyemsaidia asigongwe na gari. Alikuwa na matatizo gani? Ni mimi tu ndiye niliyeona kwamba alikuwa na shida ama labda watu wote pia? Kujiingiza sana kwenye maisha ya watu wasionihusu haikuwa njia yangu ya maisha, lakini baada ya kilichotokea muda mfupi nyuma, nilitaka sana kujua. Yaani nilitaka kumwelewa Mariam.

★★

Masaa kama matatu yakapita baada ya mimi kuwa nimeoga tena na kubadili mavazi. Yale yaliyochafuka yalifuliwa na Ankia, ambaye alikuwa amesisitiza nimpe ayafue. Huduma nyingine tena. Kwa hiyo nilikaa tu chumbani kwa kujilaza kitandani mpaka giza lilipoingia, na bado maumivu ya vidonda vya mikwaruzo mkononi niliyahisi; ingawa sikuyatilia sana maanani.

Mbu kuanza kuongezeka kukafanya wazo la kwenda kutafuta hizo dawa za kuwaua lije akilini ilipofika saa mbili usiku, nami nikajinyanyua kutoka kitandani ili nikazifate. Kwa sababu fulani, Ankia hakuwa amekuja kuniangalia tokea alipozichukua nguo ili afue, na mimi nilichukulia tu kwamba alikuwa na kazi zake ama alitaka tu kuniacha nipumzike, kwa hiyo hakuwemo sana akilini.

Nikavaa T-shirt langu la mikono mifupi, na oh... nilikuwa napendelea kuvaa maT-shirt sanasana, hivyo nilikuwa na nguo nyingi za aina hii. Kwa hiyo nikatoka hapo na kwenda kufungua mlango, na salamu ya kwanza niliyoipata ilikuwa ni harufu nzuri sana ya mboga iliyopikwa kwa viungo vilivyoifanya inukie; kwa makisio ikiwa ni nyama au samaki.

Niliposimama nje chumba hicho, ningeweza kumwona Ankia akiwa upande wa jikoni, akikoroga-koroga na kisha kufunika sufuria lenye mapishi hayo baada ya kuonja kidogo. Wakati huu alikuwa amevalia T-shirt lile lile alilovaa wakati tunaenda kwa mwenyekiti, na kutokea kiunoni alijifunga khanga.

Akawa ameniona, naye akaanza kuja upande wangu taratibu. Alikuwa na tembea fulani hivi ya kudunda iliyofanya kifua chake kitikisike kwa mbwembwe, nami nikasimama hapo hapo mlangoni nikimwangalia mpaka alipofika karibu na kuuegamia ukuta kwa bega lake. Kilemba kichwani kama kawaida.

"Umeamka?" akaniuliza hivyo.

"Sikusinzia, nilijilaza tu. Ulidhani nimesinzia?" nikamuuliza pia.

Akatikisa kichwa mara moja kukubali.

"Vinanukia kweli. Unaonekana unajua kupika," nikamwambia.

Akatabasamu kidogo na kusema, "Kawaida. Mwanamke anatakiwa kujua kupika."

"Hivi... samahani kuuliza...."

"Usiombe samahani, niulize tu."

"Si na chakula natakiwa kuwa nalipia kama vile maji na umeme?"

"Chakula tunashiriki wote JC. Ukitaka kula kivyako sawa, lakini mimi nikipika changu lazima na we' ule," akasema hivyo.

Kauli hiyo ikanifanya nitabasamu.

"Vipi mkono?" akaniuliza.

"Uko poa. Nataka nikachukue dawa za mbu..."

"Leta nikufatie."

"Hapana, si hapa tu nje? Nafata."

"Hamna, leta bwanaa... usitoke nje tena, usije'anguka."

"Ahahah... ila wewe! Ukiunguza je?"

"Nimepunguza moto. Nipe hela nikufatie..."

"Hapana, nafata mwenyewe. Usijali," nikamwambia hivyo kwa uhakika.

Jinsi alivyotazama pembeni baada ya mimi kusema hivyo ilikuwa kwa njia ya kukwazika, naye akaniangalia tena machoni.

"Vipi, mbona hivyo?" nikamuuliza.

Akaangalia chini kiasi na kusema, "JC..."

"Nambie..." nikaitika.

"Muda ule... mama Ashura alipokuwa amekuja... najua ulijisikia vibaya..." akasema hivyo kwa sauti ya chini.

Nikatazama pembeni tu.

"Nisamehe JC... najua nilikukwaza..." akasema hivyo.

"Usiniombe samahani Ankia. Tena nafikiri ni jambo zuri huyo mama kuja hapa na kutukatisha..." nikamwambia.

"Kwa nini?"

"Asingekuja, nisingetoka nje, Mariam angeumia. Nadhani ilikuwa ni Mungu tu aliongoza mambo hivyo kwa hiyo... usijali. Sijakwazika wala," nikamwambia kwa upole.

"Kweli?" akauliza.

"Ndiyo, tuko poa. Mpangaji na mwenye nyumba marafiki."

"Mhm... kumbe marafiki?"

"Eee... ama we' siyo rafiki?"

"Ni kweli. Sisi marafiki."

"Aina hiyo," nikamwambia hivyo bila kuacha kumtazama.

Akatabasamu kwa haya kiasi na kuangalia chini.

"Halafu hivi... huyo Mariam... ana tatizo la kiakili au?" nikamuuliza hivyo.

Akaniangalia na kusema, "Ndiyo, hata mimi nadhani hivyo. Kuna mambo mengi kwenye hiyo familia kwa hiyo... sijui sana."

"Umemjua tokea muda?"

"Eeeh... tuko hapa muda. Huyo msichana hakuwaga hivyo unajua? Alianza tu... kuchizika ghafla..."

"Kuchizikaje?"

"Sijui sana, ila watu huwa wanasema alirogwa eti," akaniambia hivyo.

Nilibaki kimya tu nikimtazama kwa umakini.

"Mambo tu yalianza kumwendea vibaya wazazi wao walipofariki kwenye ajali kwa pamoja. Dada yake ameshajaribu kumtafutia matibabu lakini inasemekana hospitali huko wamemwambia huyo binti ni wa kupeleka wodi za vichaa... lakini yeye Miryam anasisitiza kwamba mdogo wake siyo kichaa. Hataki kumwacha huko. Ndiyo kama unavyomwona..." Ankia akaeleza.

"Sidhani sana kama neno 'kichaa' linamfaa huyo msichana. Asingeweza kucheza na watoto kama vile alivyokuwa anacheza nao leo ikiwa asingeweza kuelewa mambo vizuri," nikamwambia.

"Ndiyo kama hivyo sasa, we' hebu fikiria amezaliwa normal tu halafu akageuka kuwa haelewi-elewi vitu. Watu wanaisomaje hiyo? Hata kwa Mwamposa wameenda lakini wapi... hamna lolote huko," Ankia akasema.

"Mh? Kumbe ni wakristo?"

"Ulifikiri ni waislamu?"

"Ndiyo."

"Hamna, siyo. Ila hata waislamu mbona wanaendaga kwa huyo jamaa? Wanasema kikubwa imani lakini kwa wengi wanachoenda kuambulia ni kukombwa tu hela... sadaka," Ankia akasema hivyo.

Nikatabasamu kidogo na kusema, "Si ndiyo imani yenyewe sasa?"

"Mh... sidhani sana..."

"Ankia, siku hizi imani bila pesa, imekufa," nikamwambia.

Akacheka na kuniambia, "Unabadili kauli za biblia ziendane na mambo ya siku hizi eh?"

"Me ndiyo nahisi hivyo. Kwa hiyo... wazazi wao walikufa kwenye ajali ya gari au?" nikamuuliza hivyo.

"Eee, yaligongana siku wametoka safari ya wapi sijui. Mabasi. Ndiyo ikawa hivyo. Lakini unajua nini, kwa shida kama alizonazo huyo Mariam ni ku..."

"Hodii..."

Sauti yenye kusema neno hilo ikamkatisha Ankia kwa kile alichotaka kuniambia, nasi tukatazama upande wa sebuleni. Ilikuwa sauti ya kiume, na sote tulifahamu mmiliki wake.

Ankia akasema, "Karibu..." kisha akaniangalia na kuniambia, "Tesha huyo."

Nikatikisa kichwa kukubali hilo, naye akaelekea mlangoni ili amfungulie jamaa.

Bila shaka kuja kwake Tesha kulikuwa kwa kusudi la kutimiza ahadi yake aliyonipa ya kuja kuniona, nami nikasogea mpaka hapo sebuleni nikimtazama Ankia alipomfungulia mlango na kuanza kusemeshana naye kiutani. Walionekana kuwa na uhusiano mzuri wa kaka na dada pia, naye Tesha akaingia ndani humo na kuniona.

Alikuwa amevalia T-shirt pana la mikono mifupi, lenye rangi ya kijani (Manga), pamoja na suruali ya jeans yenye rangi ya samawati iliyokoza. Na alinukia vizuri pia. Mwonekano wake ulitoa taarifa ya haraka kwamba alipenda kupendeza na kuonekana msafi, na hilo lilikuwa jambo nililopenda pia.

"Ah, kaka vipi?" akanisalimu kirafiki.

"Fresh tu, karibu," nikaitikia salamu yake.

Tukagonga tano kwa ngumi zetu, kisha akakaa kwenye sofa moja, vilevile na mimi pia la pembeni.

"Unakunywa soda gani we' mbwa?" Ankia akamuuliza hivyo Tesha.

Nikacheka kidogo kwa pumzi.

"Asa' soda ya nini, mi' mgeni hapa? Ushaniita mbwa, unajua ni nyama tu ndo' natumia," Tesha akamwambia hivyo.

"Na mifupa tu," Ankia akamwambia.

"Hahahah... aloo... hiyo ishu ya saa zile imekuwa mkosi kitaa hiki, kila kona nasikia unaongelewa mchina tu..." Tesha akaniambia hivyo, nasi kwa pamoja tukacheka.

"Kwa mazuri lazima mchina wetu aanze kusifika," Ankia akasema hivyo, akiwa amekaa kwenye mkono wa sofa karibu na mimi.

"Ah siyo poa," Tesha akasema.

"Hahah... me nafanana vipi na mchina bwana?" nikasema hivyo kiutani.

"Ah, si washamba wa huku tu kaka? Me mwenyewe naitwaga mpaka msudani eti kisa ngozi tu hii..." Tesha akaniambia.

"Sasa ndiyo kila mtu hapa atataka mazoea. JC hakuna kwenda nje," Ankia akasema.

"Aa wee... nisiende nje? Natoka nikitaka, na hakuna mtu ananisogelea. Sipendi shobo zisizo na maana..." nikasema hivyo.

"Wewe uko kama mimi bro, nawapaga gongo hili wanaoshoboka sana bila maana, yaani mtindo mmoja," Tesha akasema hivyo.

"Basi unajichetuaa..." Ankia akamwambia hivyo.

"Fact hiyo. We' mwenyewe unajua sisi tukoje, tunawapenda watu wakitupenda...."

"Na tunawatenda tusiowapenda," nikamalizia maneno yake Tesha.

Akacheka kwa nguvu sana na kusema, "Aminia, aminia," huku akigongesha kiganja chake kwenye ngumi yangu niliyomkunjia aipige.

Alionekana kuwa mjanja kweli na mwongeaji, hivyo nilijua kabisa angekuwa mwepesi kuzoeleka.

"Haya bwana, mapacha mmekutana. JC, leta nikafate basi..." Ankia akasema hivyo, akimaanisha nimpe hela afate dawa za mbu.

Nikampatia elfu moja.

"Zote?" akaniuliza hivyo.

Nikatikisa kichwa kukubali, naye akaenda upande wa jikoni kwanza kuiangalia mboga bila shaka. Nilipomtazama Tesha, alinifanyia ishara kwa mdomo wake kunionyeshea mwanamke huyo alipokuwa ameondoka, nasi kwa pamoja tukacheka kidogo bila kutoa sauti.

"Vipi, mdogo wako anaendelea vizuri?" nikamuuliza.

"Eh, yuko poa, yuko poa. Kichwa kilikuwa kinamsumbua kidogo, ila ameshusha dawa akalala. Akiamka atakuwa fresh zaidi," akasema.

"Miryam amerudi?" sauti ya Ankia ikauliza hivyo kutokea jikoni.

"Bado. Ma' mkubwa kamwambia kuhusu hiyo ajali akasema atajitahidi kuwahi. Unaelewa anavyojua kupanick," Tesha akaongea kwa sauti ya juu kiasi.

"Hata me ningepanick, we! Ajali siyo mchezo," Ankia akasema hivyo.

"Kwa hiyo... hawa walio hapo kwenu ni, mama zako?" nikamuuliza Tesha.

"Yah, mama wakubwa. Huyo aliyekupaka dawa saa zile ni mdogo wake na aliyemzaa mshua wetu... na huyo white ni dada yake na mama yetu. Ila... sisi wazazi wetu walishafariki," Tesha akaeleza.

"Aaa... sawa. We' unapiga mishe gani huku?" nikabadili mada upesi.

"Ah, nipo tu bro. Ajira kama unavyojua, ngumu kinoma kupata. Nimepiga-piga mishe kule Arusha miaka ya nyuma ila nilipofika huku, haba! Miezi inapita, lakini nitapata tu pa kuegamia," akaeleza.

"Ungemwomba sister akuunganishe sehemu," Ankia akasema hivyo akiwa anarudi sebuleni sasa.

"Ameshajaribu, ila michongo ya siku hizi haisimami fresh. Anataka nitulie mpaka apate panaponifaa," Tesha akasema.

"Na anavyowadekezaga sasa!" Ankia akasema hivyo na kutupita mpaka kuufikia mlango.

"Hiyo lazima, kupendwa kunaanzia nyumbani, we' vipi?" Tesha akamwambia hivyo kiutani.

"Halafu kunaishia wapi?" Ankia akamuuliza hivyo huku akifungua mlango.

"Masai," Tesha akamjibu.

Nikacheka kidogo, naye Ankia akakisukuma kichwa cha Tesha kwa kidole chake na kisha kutoka nje huku jamaa akimsindikiza kwa macho.

"Wali nazi..." Tesha akaniambia hivyo huku akinionyeshea ishara ya nyusi kuelekea upande wa Ankia.

"Usipime," nikasema hivyo.

"Ushaharibu mitambo mtu wangu?"

"Hahah... hamna, sijafika huko..."

"Uko nalo alone hapa, kamata tu."

"Napendaga kufanya vitu kwa mikakati..." nikamwambia.

"Hahahah... liko vizuri, usichelewe sasa," akaniambia hivyo.

"Vipi, ushaangukia nini?"

"We! Natamanigi tu, kuguswa halitaki eti. Aidha linaogopa ngoma ama mashauzi tu. Ila kwa wewe nafikiri litalegea."

"Kwani me nina nini?"

"Ah, HB. Halafu na vile umepiga action kama stelingi wa kihindi leo, nani asikutake?"

Nikacheka kidogo na kutikisa kichwa kwa kufurahishwa na utani wake.

"Una maumivu makali bado?" akaniuliza.

"Hamna, ni huu mkono kidogo tu unakwangua ila niko poa," nikasema.

"Sawa. Kama vipi... twende hapo Masai tukazimue kidogo, ama nini?"

"Hapo bar?"

"Ee. Ama bia hupigi?"

"Nakunywa."

"Yah, twende tu mtu wangu tupige mbili tatu, urudi ulale umechangamka," akasema hivyo.

"Na huyu?" nikamuuliza hivyo, nikimaanisha Ankia.

"Tunaenda naye. Anapenda bia huyo!"

"Kumbe?"

"Wee! Sema humtoi humu ndani kama huendi kumnunulia za maana ila kwa wewe HB hata kwa moja tu atakubali kutoka," Tesha akaongea kiutani.

"Ahahah... acha kufanya hivyo bana..." nikamwambia.

Akacheka kwa nguvu, nasi tukagongesha tano kirafiki tena.

"Vipi, mnanisema au?"

Ankia akawa ameuliza hivyo baada ya kurudi muda huo huo. Mkononi alishika kifuko kigumu chenye kuonyesha dawa ndefu za kuchoma za mbu, na sisi wote tukamwangalia.

"Ee, sugar mommy wetu we' ndo' mada kuu hapa. Tulikuwa tunafanya revision kidogo," Tesha akamwambia hivyo.

Ankia akasonya kiutani na kufunga mlango, naye akaanza kuja upande niliokaa mimi huku akisema, "Eti sugar mommy. Kuna sugar mommy hapa?"

"Si ndiyo wewe?" nikamwambia hivyo.

"Kwa ushuga upi? Nina miaka 32 tu mie msinizeeshe namna hiyo," Ankia akasema hivyo na kukaa pembeni yangu.

"Kwani mashuga mommy huwa wanaanzia miaka mingapi?" Tesha akamuuliza.

"32," nikampa jibu, naye Tesha akacheka.

Ankia akanikata jicho la kuudhika eti, nami nikatabasamu tu.

"Baby mama, twend'zetu Masai," Tesha akamwambia.

"Kufanyaje? Me napika sa'hivi," Ankia akasema.

"Acha kupika wewe, utapika badae. Twende tukanywe pombe!" Tesha akaongea kwa msisitizo.

Nikacheka kidogo.

"Akili yako yote iko hapo tu. Me siwezi kwenda, nenda mwenyewe," Ankia akasema hivyo.

"Unazingua. Basi baki mwenyewe, me naenda na JayZee..." Tesha akamwambia hivyo.

Nikacheka sana pamoja na Ankia, na mwanamke huyu akamwambia Tesha, "Siyo JayZee, ni JC."

"Aaaa dah, nimechapia," Tesha akakiri.

"Mwishowe atakuita Chelsea," Ankia akaniambia.

"Wewe baki kupika, si unataka kupika? Sisi twende JC," Tesha akaniambia.

"Mh? Huna lolote. Eti kweli unaenda?" Ankia akaniuliza.

Nikamtikisia kichwa mara moja kukubali.

"Sasa je! Kwa hiyo?" Tesha akamuuliza hivyo Ankia.

Mwanamke huyu akaibana midomo yake kama kuonyesha anatafakari, huku sisi tukimwangalia, naye akasema, "Basi, ngoja nikachange nguo... halafu twende."

"Hahaaa... umeona? Si nilikwambia?" Tesha akasema hivyo kwa shauku.

Nikasimama huku nikicheka pia, naye Ankia akasimama pia.

"Amekwambia nini?" Ankia akaniuliza.

"Hajaniambia kitu, nenda kavae. Na mimi ngoja nikabadili gwanda," nikasema hivyo na kuanza kuelekea upande wa chumba.

Aisee! Tesha alikuwa amenifanya nimkumbuke rafiki yangu mmoja aliyekuwa na vituko vingi sana katika njia yake ya kuongea, na hali ya urafiki niliyokuwa nimeanza kujenga pamoja na wawili hawa ilinichangamsha sana.

Nikaingia chumbani na kubadili mavazi; nikivaa T-shirt zito kiasi mithili ya sweta laini, lililokuwa na mikono mirefu lenye rangi nyekundu mchanganyiko na nyeupe, pamoja na suruali nyeusi ya jeans. Nikachana nywele vyema, nikajiweka sawa kabisa mwilini na kujipulizia manukato, kisha nikarejea pale sebuleni. Tesha akasifia mwonekano wangu na kutania kwamba ningeenda kuua macho ya wengi pale Masai, nami nikakaa sofani kumsubiri Ankia.

Dakika si nyingi sana mwanamke huyo akawa ametoka, akiwa amevaa gauni fupi jeupe lenye urembo wa maua-maua na lenye kuvutika lililoyaonyesha mapaja yake kiasi. Nilimtazama kwa umakini kiasi maana mwonekano huo ulimwelekezea sana fikira.

Nguo hiyo yenye kuubana mwili wake ilikuwa na mikono mirefu, iliyoficha hadi shingo lakini ikiacha uwazi wa duara kifuani kwake kuonyesha mstari ulioyatenganisha matiti yake yaliyonyanyuliwa juu. Tumbo lake lilijichora kwa unyama-nyama aliokuwa nao, na usoni alipendeza pia kwa kujiremba kiasi, huku nywele zake za kusukwa mtindo wa rasta fupi akiwa ameziachia tu pande za masikio yake.

Alikuwa akiniangalia kwa njia iliyoonyesha alitaka kuona ningesemaje kuhusu mwonekano wake, nami nikamwambia amependeza sana. Tesha kama kawaida akawa anamsifia kwa utani mwingi, naye Ankia akasema mboga ilikuwa imeshaiva na alikuwa amebakiza kupika ugali, kwa hiyo angepika muda ambao tungerudi. Haikuwa na neno.

Tesha alionekana kutaka sana kwenda kutubariki kwa vinywaji, bila shaka aonekane na rafiki mpya, na kwa hilo mimi pia nilikuwa tayari ili hiyo Masai na yenyewe niijue. Tukatoka baada ya Ankia kuzichoma dawa kwenye vyumba vyetu ili tukirudi mbu wasiwe vikwazo tena, taa za ndani zikazimwa, milango ikafungwa, nasi tukavaa vya miguuni na kuanza kutembea kuelekea huko Masai.

Nilimuuliza Tesha ikiwa dada yake alikuwa na kawaida ya kuingia nyumbani usiku, naye akasema mara kwa mara alirudi usiku mpaka kufikia saa nne kabisa ikiwa kazi zilimhitaji zaidi, lakini kama sivyo basi angerudi mapema tu, ama hata siku zingine kutokwenda huko kazini kwake kabisa. Bado nilitaka kujua mambo mengi kuhusu mdogo wake, Mariam, na hizi hatua za mwanzo za urafiki baina yangu na Tesha huenda zingesaidia niweze kujiingiza zaidi kwenye kuielewa vizuri zaidi hali ya yule binti.

Tukawa tumeifikia Masai. Kwa saa mbili hii joto bado lilikuwa halijapanda sana ndani humo, lakini tulipoingia tu kweli macho ya wengi yakawa kwetu; hasa mimi. Na mimi kama kawaida nilikuwa nimeweka mwonekano makini usoni, nikitembea nyuma yake Tesha huku Ankia akiwa karibu nami.

Tesha alikuwa anasalimiana kwa ufupi pamoja na watu aliofahamiana nao mpaka tulipofikia meza ndefu iliyotengenezwa kwa mbao nene, ikiwa imezungukwa na viti virefu vya plastiki ngumu vya kukalia, nasi tukaketi hapo. Hatukuwa tumeingia ndani sana kwenye sehemu hii, kwa hiyo Tesha akawa ananiambia ni wapi kulikuwa na vyoo na kumbi maalumu ya maVIP, pamoja na vyumba vya kulala wageni.

Kwa watu waliokuwepo upande kwa upande wakishusha bia zao taratibu, niliona hawakuweza kujizuia kuniangalia sana, na Ankia aliliona hilo na kuanza kunitania kwamba bila shaka ningejikuta napigwa kwa chupa kichwani kwa sababu ya demu wa mtu kunitamani. Nikacheka kidogo tu na kuendelea kutulia.

Mhudumu mwanamke akaja na kutuuliza vinywaji gani tungependa kutumia, akiwa amevalia T-shirt nyeupe na kikaptura chenye kubana sana na kuyaacha mapaja yake wazi. Tesha akatuambia tuagize, naye Ankia akasema aletewe bia tamu ya Savannah, nami nikaomba niletewe Serengeti Lite ya moto. Tesha angekunywa Serengeti Lager, naye akamwambia mhudumu atuletee sisi wanaume tatu tatu na Ankia aletewe Savannah mbili maana ni katamu ila kakali.

Inaonekana Tesha alifahamika sana hapa kwa hiyo mhudumu akaondoka tu bila kuchukua pesa, ikimaanisha malipo yangekuja baadaye. Sikutarajia jamaa aagize bia tatu kabisa lakini order ikawa imeshaenda na mimi nisingeizuia, hivyo tukaendelea kusubiri huku tunapiga story.

Muziki uliochezwa ulisikika kwa sauti nzito kwenye spika za sehemu hiyo, na TV za flat screen zilizokuwa zimetundikwa juu sehemu kadha wa kadha kwenye kumbi hiyo zilionyesha mechi ambayo sidhani watu wengi waliifatilia.

Kukawa na watu wachache ambao walifahamiana na Tesha pamoja na Ankia waliokuja mezani hapo kutoa salamu, nao wakawa wanatambulishwa kwangu. Nilitendewa kana kwamba nilikuwa mtu mashuhuri saaana, nikijua wazi wengi wangetaka kujenga ukaribu zaidi pamoja nami, lakini kwangu mie salamu na kucheka kidogo tu ndiyo yaliyokuwa maitikio niliyowapa.

Sikuona "pisi" yenye maajabu makali hata kumzidi Ankia sehemu hiyo, kwa hiyo sikuelekeza fikira kwa mwanamke yeyote hapo ingawa wengi walinitazama kwa macho ya uvutio. Bia zikaletwa, nasi tukaanza kunywa taratibu.

Nilikuwa najitahidi kusoma mazingira ya hapo ili nipazoee upesi. Nadhani labda ni shauri ya muda kutokwenda sana ndiyo sababu hapakuwa pamechangamka kivile, ama labda kwa sababu haikuwa wikiendi, kwa vyovyote tu ila palikuwa kawaida sana. Ndipo akaja mwanamke fulani mweusi kiasi mpaka kufikia mezani hapo. Alifahamiana na Tesha na Ankia, naye akasalimiana nao kwa kuwakumbatia na kuanza kuzungumza kwa shauku.

Alikuwa mzuri. Mwili wake haukuwa mnene, urefu wa kadiri, na alionekana kuwa mwongeaji sana. Alisuka nywele ndefu laini na kuzibana nyuma ya kichwa chake, akiwa amevalia nguo ndefu kama kijora iliyochoresha kalio lake vizuri kwa jinsi alivyoivuta kwa mbele, na alikuwa na macho madogo ambayo yangefanya aonekane kama mchina endapo angekuwa na ngozi nyeupe. Aliitwa Joy.

Akawa ametambulishwa kwangu, nami nikampa salamu huku nikimwangalia kwa upendezi. Nadhani njia yangu ya kutazama mwanamke kila naposema nimemwangalia kwa upendezi sikuzote ilikuwa inatoa ujumbe fulani wenye kuamsha hisia nzuri kwake, na huyo Joy alinitazama kwa macho yaliyonipa ujumbe wa "tukutane chumbani."

Nikacheka kidogo tu, naye Tesha akacheka pia kwa sababu alinielewa sana inaonekana, hivyo akaanza kumsukumia Joy upande wangu eti; akae hapo hapo, tena karibu na mimi. Joy alikuwa amefika na marafiki zake hapo ambao walienda kukaa kwenye meza nyingine kabla hajaja upande wetu kutusalimia, kwa hiyo akawa akisema anahitaji kwenda huko.

Lakini Tesha akawa anamsisitizia akae na sisi, akiniambia nimshawishi pia, nami nikaushika mkono wa huyo Joy na kuuvutia kwangu taratibu. Aliniangalia huku akitabasamu kiasi, naye akaja polepole kama vile amepumbazika. Nadhani jambo hilo lilimfanya Ankia ajisikie vibaya kiasi, lakini akajikaza tu na kuendelea kuweka utulivu huku akinywa.

Nikamwambia Joy akae kiti kilichokuwa pembeni yangu, naye akakubali na kuketi. Tesha akamwagizia bia mbili za Serengeti Lite pia, nasi tukaendelea kunywa taratibu huku Tesha akiongea na Joy sanasana.

Nilipomwangalia Ankia, alikuwa ametulia tu akicheza muziki taratibu kwa kupeleka kichwa huku na huko bila kuniangalia, nami nikalishika paja lake kwa chini. Akaniangalia, na jinsi nilivyomtazama kwa macho yangu ya uchokozi kukamfanya ashindwe kujizuia kutabasamu kwa haya, na hapo nikawa nimefanikiwa kumtuliza.

"Oy, sister huyo..." Tesha akaniambia hivyo huku akitazama upande wa nje kabisa.

Nikageuka na kuliona lile gari la Miryam likipita kuuelekea upande tuliotokea kule nyumbani, kumaanisha dada mtu ndiyo alikuwa anarudi.

Nikamwangalia Tesha tena, naye akasema, "Yaani sasa hivi ndiyo amewahi."

Alihitaji kuongea kwa sauti ya juu ili nimsikie, nami nikatabasamu kidogo.

"Dada'ako hatakuchapa ukienda home unanuka pombe kweli?" Ankia akamuuliza.

"Acha zako wewe, nani achapwe?" Tesha akamuuliza.

"Tena zile mboko za kuzunguka!" Joy akasema hivyo, nasi wote tukacheka.

"Sister hamaindi kabisa, sisi ndo' mayai yake bana," Tesha akajisifia.

"Unavimbaga kweli kisa dada'ako anawapenda sana. Siku akiolewa sijui nawe utaolewa naye?" Joy akamwambia hivyo.

Ankia akacheka na kusema, "Lilivyo hili, litaenda naye kabisa ili malezi likayapate na huko ukweni."

"Aaa mnanichoresha vibaya, au mnadhani sijui kama sitakaa na sister tu maisha yote?" Tesha akasema.

"Kumbe unalijua?" Joy akamwambia.

Tesha akanywa bia na kuvimbisha mashavu kwa njia ya masihara, nasi tukacheka kidogo.

"Ila dada yako Tesha hataki kuolewa kabisa, eti? Ama hapendi tu wanaume?" Ankia akamuuliza.

"Eeh Tesha, nasikiaga wanakujaga hadi kumtolea posa ila anawatimua," Joy akamwambia.

"Siyo hivyo. Mambo magumu tu sa'hivi, sister anatutunza kwanza. Kama kuolewa ataolewa tu baadaye. Jana kuna bwege mwingine alikuja, na yeye akabebeshwa virago alivyovileta. Hapana cheza na Mimi!" Tesha akasema.

"Wewe ndiyo ulimfukuza?" nikamuuliza.

"Hamna, sister..." Tesha akajibu.

"Huwa wanamwita Mimi..." Ankia akanijulisha.

"Ooh..." nikasema hivyo kwa uelewa sasa.

Na hiyo ingefanya mambo yawe rahisi hata kwangu pia, kumwita Mariam Mamu, na dada yake, Miryam, kumwita Mimi.

"Unatiaga michumvi wewe! Eti akamfukuza. Alivyo mstaarabu dada'ako najua alimwambia tu, 'pole... nimeshawahiwa,'" Joy akasema hivyo.

Tukacheka kidogo mimi na Ankia.

"Halafu bro, waliniambia ulifika kwanza wewe... sijui ulipotea eti..." Tesha akaniambia.

"Ee bana, nilikuwa naitafuta nyumba ya Ankia kwa kutumia ramani. Sasa kidoti chekundu kikanileta kwenu, siunajua zimekaribiana sana..." nikamwambia.

"Eee dah! Ma' mkubwa ndiyo aliniambia, nawe ukajikuta unachangamkiwa kuwa mchumba..." Tesha akasema.

Tukacheka sana kwa pamoja.

"Kweli? Walifikiri ni yeye?" Joy akauliza.

"Ee..." Tesha akajibu.

"Hahah... mbona hukuniambia?" Ankia akaniuliza.

"Nilisahau tu," nikamwambia hivyo.

"Asa' si unaona, matatizo tu. Yote hayo kumfosi sister aolewe. Yaani wanawake na ndoa bana!" Tesha akaniambia hivyo.

"Ndoa sifa kwa mwanamke, hujui hilo baba, basi umeachwa..." Joy akamwambia.

"We' ya kwako iko wapi?" Tesha akamuuliza.

"Si nakusubiri wewe?" Joy akamwambia.

"Sawa, utasubiri sana," Tesha akasema hivyo, naye Joy akacheka.

Tukaendelea kunywa na kupiga story, mpaka inaingia saa nne hivi, tulipokuwa mwishoni kumalizia vileo vyetu, bia zingine zikaongezeka mezani hapo. Tesha hakuwa ameagiza zingine, hivyo akauliza zimetokea wapi. Mhudumu akamwambia kwamba kuna mtu alikuwa amenunua kwa ajili yangu mimi, kwa hiyo tayari zilikuwa zimeshalipiwa na sisi tungetakiwa kunywa tu. Bia kiujumla zilikuwa Serengeti Lite 20!

Tesha akamwambia mhudumu asepe, meza ikiwa imefurika bia, naye Ankia akaniambia inaonekana kuna sugar mommy hapo ndiye aliyekuwa amezituma hizo ili kuanza kunichokonoa. Nikamwambia hilo halingeniongezea wala kunipunguzia kitu chochote kile kutoka kwa mtu ambaye sikumjua, kwa hiyo kama amezileta zinywewe, zingenyweka tu. Tesha alikuwa akiniambia hayo ndiyo mambo sasa, na bila shaka masaa ya kukaa hapo yangeongezeka mpaka suala la Ankia kupika ugali nyumbani lingesahaulika kabisa.

Tukaendelea kunywa taratibu tu, huku mzuka wa hapo Masai ukizidi kupanda kadiri dakika zilivyoendelea kutembea, nami ningetoka mara kwa mara kwenda nje kuzungumza na simu ama kutoa haja ndogo chooni. Vibe la pombe liliwaingia vyema Tesha na Joy, hata mimi na Ankia pia, lakini sisi tulikuwa watulivu zaidi.

★★

Mpaka kufikia saa sita bado tulikuwa hapo, na hata kabla ya kumaliza bia tulizoongezewa, zikaletwa zingine 20. Inaonekana huyo mtu alikuwa amenipenda ama kunitaka, lakini bado hakujitambulisha kwangu, na mimi sikujisumbua kumtafuta wala. Kuna watu waliokuwa wanakuja kuomba bia, nasi tukawa tunawapa, na mzuka ukazidi kuongezeka.

Watu walicheza, waliimba, na sisi tukaendelea kunywa na kupiga story za kufurahisha hadi saa nane kufika. Nilikuwa nimekunywa bia 7 tu, na wenge la kulewa lilifanya macho yangu yawe mazito kiasi. Wenzangu walishusha pombe 10 na bado walikuwa wanaendelea, kwa hiyo mimi mtegeaji nikawa macho zaidi yao.

Ankia angenilalia begani na kuongea mambo mengi sana, na mimi niliendelea kutulia tu. Joy alianza kupitisha kiganja chake kwenye paja langu, akilipapasa na kulifinya mara kwa mara, na nilipomwangalia niliona hiyo kuwa sababu ya kuingiwa zaidi na pombe kichwani kwake. Nilifurahia kwa kweli. Siku ya pili tu ugenini tayari nikajihisi kuwa mwenyeji.

Nilipoona uzito wa pombe unamlemea Tesha, nikasimama na kwenda kumtoa kwenye kiti, nami nikamwambia tuelekee nyumbani kwa kuwa tayari bia zetu za mwanzo alizoagiza alikuwa ameshalipia. Alikuwa amelewa siyo poa.

Nikamwambia na Ankia tuondoke, naye akatii na kusimama huku akiyumba. Joy alikuwa amelewa pia lakini siyo ile ya kumyumbisha, akionekana kuwa mzoefu zaidi wa pombe, naye akatufata pia tulipotoka sehemu hiyo kwa pamoja. Tesha hakuweza kutembea vizuri, akiyumba huku na huko na akiongea sana, nami nikamsindikiza mpaka getini kwao, nikiwaacha Ankia na Joy wanaenda kule ndani kwetu. Usiku wa saa nane huo.

Tesha alikuwa anasema ana kama wiki hajanywa pombe ila furaha niliyompa leo kwa sababu ya kumwokoa mdogo wake ilimfanya ajiachie namna hiyo, nami nikawa namwangalia tu kwa kujali kiasi. Alionekana kuwa mtu mwenye huzuni, na sikujua ni kwa nini niliwaza hivyo.

Geti likawa limefunguliwa, na aliyefungua hakuwa mwingine ila bibie Miryam. Alikuwa na mwonekano wa mtu aliyetoka usingizini, lakini si ule mzito mno. Alitutazama kwa umakini. Nilihisi labda angekuwa mkali kwa Tesha kutokana na kurudi usiku akiwa amelewa, lakini haikuwa hivyo.

Akaacha uwazi ili kuturuhusu kuingia, naye Tesha akatangulia huku nikiwa nimemshika mkono kuhakikisha hajigongi getini.

"Mimi... ulikuwa umeshalala? Ungekuja nawe tukapiga bia kidogo," Tesha akamsemesha hivyo.

"Kulewa ndiyo bia kidogo? Em' ingia ndani..." Miryam akamwambia kwa sauti tulivu.

Tesha akiwa ananesanesa, macho mazito mno, akaniangalia na kusema, "Umemwona? Huyu ndiyo mkurugenzi hapa. Chochote anachosema tunafata. Nampenda mno... naweza nikaua kwa ajili yake."

Tesha aliyasema maneno hayo kilevi, lakini yalibeba uzito nilioelewa kuwa ulitoka ndani ya moyo wake. Nikamwangalia Miryam usoni, naye akamshika mdogo wake mkononi ili amwongoze kwenda ndani. Lakini Tesha akaweka mgomo kiasi na kuingiza kiganja chake mfukoni, kisha akaitoa simu yake na kuiwasha, halafu akanipatia.

"Andika namba bro... nakukubali sana," akaniambia hivyo na macho yake kama yanataka kudondoka.

"Atakupa hata kesho," Miryam akamwambia.

"Ee kaka, nitakugei kesho," mimi pia nikamwambia.

"Hamna... andika bana, kwani saa ngapi? Mwishowe kuku awike. Andika hapo..." Tesha akasisitiza.

Nilihisi hali yote ya hapo ilimletea picha mbaya sana dada yake, lakini nikaichukua tu simu yake na kuandika namba upesi. Nikamrudishia, naye akanisonta kwa kidole chake kwa kurudia-rudia kuonyesha jinsi alivyonielewa, halafu akaanza kuelekea huko ndani.

Miryam akanitazama usoni, kasura kake ka kuvimba kakiwa na mwonekano wa kitoto shauri ya kutoka kulala. Sikujua alikuwa amepanga kunirushia maneno gani wakati huu, lakini nilikuwa nimeshalewa pia kwa hiyo nisingeyajali sana. Hapa kilichokuwepo ilikuwa kuondoka tu maana mdogo wake nilimrudisha kwao salama.

"Angalia asiangukie meza huyo..."

Nikamwambia hivyo kwa sauti tulivu tu. Alinitazama machoni kwa njia fulani yenye kujali, na nilikuwa sijalitambua hilo hata kidogo mpaka aliponisogelea karibu zaidi na kisha kunikumbatia taratibu!


★★★★★★★★★

ITAENDELEA

★★★★★★★★★

Full Story WhatsApp or inbox

Whatsapp +255 678 017 280
M
 
MIMI NA MIMI

A Story by Elton Tonny

Familia, Urafiki, Mapenzi, Kazi, Tamaa, Hila, Usaliti, Siri, Mambo Ysiyotazamiwa

R-rated 18+

Enjoy!


★★★★★★★★★★★★★

SEHEMU YA NNE

★★★★★★★★★★★★★


Mlango wa geti la nyumba ile aliyoishi binti huyo ukafunguliwa, na hapo wakatoka watu watatu kuja nje bila shaka kuangalia nini kilikuwa kimetokea. Ilikuwa ni Zawadi mweupe na yule mwanamke mweusi, pamoja na yule kijana niliyemwona asubuhi hiyo hapo kwao akiwa anacheza mpira.

Huyo kijana akaja upesi mpaka alipokuwa amesimama Mariam, akianza kumwangalia na kumshika hapa na pale kumkagua kama aliumia, na akiuliza nini kilikuwa kimetokea. Mariam akamkumbatia kwa nguvu sana huku akilia mno, na watu walioona tukio lile, hasa yule mwanaume aliyekuwa amesimama pale dukani kabla ya ajali, wakawa wanamwelezea huyo kijana mambo yote yaliyojiri.

Zawadi mweupe na mwenzake wakafika hapo pia wakionekana kuwa na hofu mno, huku watu wakiwaambia isingekuwa ya mimi kumsukuma binti huyo basi mabaya mengi yangekuwa yamempata. Ni muda huo huo tu ndiyo Ankia akawa amefika hapo nje pia na yule mmama aliyekuwa naye ndani, pamoja na muuzaji wa dukani, naye akanisogelea na kunishika mkononi, akiniuliza ikiwa nilikuwa sawa.

Nilitambua kwamba wengi walitaka kunisikia nikiongea kwa sababu walinitazama mno, lakini sikusema lolote maana bado mapigo ya moyo yalidunda kwa nguvu mno na nilihisi miguu ikitetemeka kiasi kutokana na nguvu kunitoka.

"Ma' mkubwa, mpeleke Mamu ndani..."

Huyo kijana aliyekumbatiwa na Mariam akamwambia hivyo Zawadi mweupe, na mwanamke huyo akamchukua binti kweli na kuanza kwenda naye huku akimbembeleza. Yule mwenzake mweusi akanisogelea huku akinitazama kwa hisia sana.

"Asante sana baba'angu. Mungu akubariki, yaani sijui bila wewe ingekuwaje jamani..." akaniambia hivyo.

"Kaka... nashukuru sana kwa kumsaidia mdogo wangu. Sina uwezo wa kukulipa, lakini naomba ujue Mungu atakubariki mara mia zaidi. Yaani... ninakushukuru sana," huyo kijana akaniambia hivyo.

Ahaa! Kumbe alikuwa kaka yake Mariam pia? Basi bila shaka huyu alimfata Miryam kiukubwa kwa ndugu hawa, nami nikamwambia, "Haina shida kaka. Hakuna malipo yoyote yanayoweza kulinganishwa na uhai wa mdogo wako, kwa hiyo usijali. Nafurahi tu yuko salama."

Hatimaye watu wakawa wamenisikia nikiongea.

"Ubarikiwe sana baba," yule mwanamke akaniambia.

"Amina," nikamwitikia.

"JC, unatoka damu..." Ankia akasema hivyo huku akiushika mkono wangu.

Kweli nilihisi maumivu ya kukwaruza kwenye mkono, lakini sasa nilipojiangalia, nikaona damu zikiwa zinavuja kutokea kwenye kiwiko.

"Eh! Pole baba jamani... twende tuka... Tesha si kuna dawa ndani?" huyo mama akasema.

"Ndiyo, ipo. Twende bro tukapasafishe..." huyo kijana, Tesha, akaniambia hivyo.

"Hamna shida mama... nitamnawisha tu huku kwetu na kupatibu. JC, twende ndani," Ankia akaniambia hivyo.

"Ankia, tunaomba tumpe tu huo msaada angalau, maana amemsaidia sana Mariam. Tafadhali," huyo mama akasema.

Tesha akanisogelea na kunishika begani kwa njia ya msisitizo kuwa niende pamoja nao, nami nikamtazama Ankia machoni kwa ufupi. Alionekana kuhuzunika mno kwa ajili yangu, nami nikaamua kwenda pamoja na Tesha na mama yule mpaka ndani kwao. Ankia akatufata, huku watu wengine wakitutazama mpaka tulipoishia ndani.

Sikuwa nimefikiri ningeiona siku hii ikibadilika ghafla namna hiyo, na bado nilikuwa nikijiuliza maswali mengi kuhusiana na huyo Mariam. Tesha akaniongoza kufikia bombani, naye Ankia akanisaidia kuinawisha mikono yangu sehemu ilipochafuka na kuumia. Mavazi yangu yalijaa vumbi chafu sana, yakiwa na uhitaji wa kufuliwa upesi kabla uchafu haujakomalia hapo.

Tukaenda kibarazani pale baada ya kumaliza, na yule mwanamke mweusi alikuwa ameshaleta boksi lenye pakti nyingi za pamba, bendeji, na dawa. Akanisaidia kunipaka dawa kali sana kwenye michubuko yangu na kisha kufuta-futa kwa pamba, kisha Ankia akanifunga bendeji mkononi usawa wa kiwiko na kuniwekea plasta kwenye michubuko. Nikashauri afanye mambo yote hayo kwa njia nyepesi kuruhusu vidonda vipumue.

Baada ya hapo, nikawashukuru kwa msaada wao na kuwaambia ningekwenda kuyatoa mavazi machafu na kujisafisha sasa, nao wakakubali hilo na kunipa karibu ya mara nyingine tena kufika hapo kwao.

Tesha alionekana kuwa kijana imara, mjanja, na mwenye kujiamini. Huo ulikuwa ni mtazamo wangu wa kwanza tu kumwelekea kwa kuwa singeweza kujua utu wake kihalisi, kwa hiyo tukaagana vizuri tu huku akiniambia angekuja kunicheki baadaye kuona kama hali yangu ilikuwa nzuri. Nikatambua tu kwamba alipendezwa nami upesi sana, kwa hiyo nikaondoka pamoja na Ankia kurudi ndani kwetu.

Ankia alionekana kujali sana kilichonipata. Aliniuliza ilikuwaje-kuwaje mpaka kilichotokea kutokea, nami nikaeleza tu kwa ufupi namna mambo yalivyokuwa. Hamu ilinitoka kabisa shauri ya jambo hilo. Nikamwambia ningeenda tu kuoga na kisha kupumzika, nami nikafanya hivyo bila kusumbuka tena kuwaza kuhusu ile ishu yangu ya awali pamoja na mwanamke huyu.

Nilianza kujali zaidi kuhusu hali ya yule mwanadada niliyemsaidia asigongwe na gari. Alikuwa na matatizo gani? Ni mimi tu ndiye niliyeona kwamba alikuwa na shida ama labda watu wote pia? Kujiingiza sana kwenye maisha ya watu wasionihusu haikuwa njia yangu ya maisha, lakini baada ya kilichotokea muda mfupi nyuma, nilitaka sana kujua. Yaani nilitaka kumwelewa Mariam.

★★

Masaa kama matatu yakapita baada ya mimi kuwa nimeoga tena na kubadili mavazi. Yale yaliyochafuka yalifuliwa na Ankia, ambaye alikuwa amesisitiza nimpe ayafue. Huduma nyingine tena. Kwa hiyo nilikaa tu chumbani kwa kujilaza kitandani mpaka giza lilipoingia, na bado maumivu ya vidonda vya mikwaruzo mkononi niliyahisi; ingawa sikuyatilia sana maanani.

Mbu kuanza kuongezeka kukafanya wazo la kwenda kutafuta hizo dawa za kuwaua lije akilini ilipofika saa mbili usiku, nami nikajinyanyua kutoka kitandani ili nikazifate. Kwa sababu fulani, Ankia hakuwa amekuja kuniangalia tokea alipozichukua nguo ili afue, na mimi nilichukulia tu kwamba alikuwa na kazi zake ama alitaka tu kuniacha nipumzike, kwa hiyo hakuwemo sana akilini.

Nikavaa T-shirt langu la mikono mifupi, na oh... nilikuwa napendelea kuvaa maT-shirt sanasana, hivyo nilikuwa na nguo nyingi za aina hii. Kwa hiyo nikatoka hapo na kwenda kufungua mlango, na salamu ya kwanza niliyoipata ilikuwa ni harufu nzuri sana ya mboga iliyopikwa kwa viungo vilivyoifanya inukie; kwa makisio ikiwa ni nyama au samaki.

Niliposimama nje chumba hicho, ningeweza kumwona Ankia akiwa upande wa jikoni, akikoroga-koroga na kisha kufunika sufuria lenye mapishi hayo baada ya kuonja kidogo. Wakati huu alikuwa amevalia T-shirt lile lile alilovaa wakati tunaenda kwa mwenyekiti, na kutokea kiunoni alijifunga khanga.

Akawa ameniona, naye akaanza kuja upande wangu taratibu. Alikuwa na tembea fulani hivi ya kudunda iliyofanya kifua chake kitikisike kwa mbwembwe, nami nikasimama hapo hapo mlangoni nikimwangalia mpaka alipofika karibu na kuuegamia ukuta kwa bega lake. Kilemba kichwani kama kawaida.

"Umeamka?" akaniuliza hivyo.

"Sikusinzia, nilijilaza tu. Ulidhani nimesinzia?" nikamuuliza pia.

Akatikisa kichwa mara moja kukubali.

"Vinanukia kweli. Unaonekana unajua kupika," nikamwambia.

Akatabasamu kidogo na kusema, "Kawaida. Mwanamke anatakiwa kujua kupika."

"Hivi... samahani kuuliza...."

"Usiombe samahani, niulize tu."

"Si na chakula natakiwa kuwa nalipia kama vile maji na umeme?"

"Chakula tunashiriki wote JC. Ukitaka kula kivyako sawa, lakini mimi nikipika changu lazima na we' ule," akasema hivyo.

Kauli hiyo ikanifanya nitabasamu.

"Vipi mkono?" akaniuliza.

"Uko poa. Nataka nikachukue dawa za mbu..."

"Leta nikufatie."

"Hapana, si hapa tu nje? Nafata."

"Hamna, leta bwanaa... usitoke nje tena, usije'anguka."

"Ahahah... ila wewe! Ukiunguza je?"

"Nimepunguza moto. Nipe hela nikufatie..."

"Hapana, nafata mwenyewe. Usijali," nikamwambia hivyo kwa uhakika.

Jinsi alivyotazama pembeni baada ya mimi kusema hivyo ilikuwa kwa njia ya kukwazika, naye akaniangalia tena machoni.

"Vipi, mbona hivyo?" nikamuuliza.

Akaangalia chini kiasi na kusema, "JC..."

"Nambie..." nikaitika.

"Muda ule... mama Ashura alipokuwa amekuja... najua ulijisikia vibaya..." akasema hivyo kwa sauti ya chini.

Nikatazama pembeni tu.

"Nisamehe JC... najua nilikukwaza..." akasema hivyo.

"Usiniombe samahani Ankia. Tena nafikiri ni jambo zuri huyo mama kuja hapa na kutukatisha..." nikamwambia.

"Kwa nini?"

"Asingekuja, nisingetoka nje, Mariam angeumia. Nadhani ilikuwa ni Mungu tu aliongoza mambo hivyo kwa hiyo... usijali. Sijakwazika wala," nikamwambia kwa upole.

"Kweli?" akauliza.

"Ndiyo, tuko poa. Mpangaji na mwenye nyumba marafiki."

"Mhm... kumbe marafiki?"

"Eee... ama we' siyo rafiki?"

"Ni kweli. Sisi marafiki."

"Aina hiyo," nikamwambia hivyo bila kuacha kumtazama.

Akatabasamu kwa haya kiasi na kuangalia chini.

"Halafu hivi... huyo Mariam... ana tatizo la kiakili au?" nikamuuliza hivyo.

Akaniangalia na kusema, "Ndiyo, hata mimi nadhani hivyo. Kuna mambo mengi kwenye hiyo familia kwa hiyo... sijui sana."

"Umemjua tokea muda?"

"Eeeh... tuko hapa muda. Huyo msichana hakuwaga hivyo unajua? Alianza tu... kuchizika ghafla..."

"Kuchizikaje?"

"Sijui sana, ila watu huwa wanasema alirogwa eti," akaniambia hivyo.

Nilibaki kimya tu nikimtazama kwa umakini.

"Mambo tu yalianza kumwendea vibaya wazazi wao walipofariki kwenye ajali kwa pamoja. Dada yake ameshajaribu kumtafutia matibabu lakini inasemekana hospitali huko wamemwambia huyo binti ni wa kupeleka wodi za vichaa... lakini yeye Miryam anasisitiza kwamba mdogo wake siyo kichaa. Hataki kumwacha huko. Ndiyo kama unavyomwona..." Ankia akaeleza.

"Sidhani sana kama neno 'kichaa' linamfaa huyo msichana. Asingeweza kucheza na watoto kama vile alivyokuwa anacheza nao leo ikiwa asingeweza kuelewa mambo vizuri," nikamwambia.

"Ndiyo kama hivyo sasa, we' hebu fikiria amezaliwa normal tu halafu akageuka kuwa haelewi-elewi vitu. Watu wanaisomaje hiyo? Hata kwa Mwamposa wameenda lakini wapi... hamna lolote huko," Ankia akasema.

"Mh? Kumbe ni wakristo?"

"Ulifikiri ni waislamu?"

"Ndiyo."

"Hamna, siyo. Ila hata waislamu mbona wanaendaga kwa huyo jamaa? Wanasema kikubwa imani lakini kwa wengi wanachoenda kuambulia ni kukombwa tu hela... sadaka," Ankia akasema hivyo.

Nikatabasamu kidogo na kusema, "Si ndiyo imani yenyewe sasa?"

"Mh... sidhani sana..."

"Ankia, siku hizi imani bila pesa, imekufa," nikamwambia.

Akacheka na kuniambia, "Unabadili kauli za biblia ziendane na mambo ya siku hizi eh?"

"Me ndiyo nahisi hivyo. Kwa hiyo... wazazi wao walikufa kwenye ajali ya gari au?" nikamuuliza hivyo.

"Eee, yaligongana siku wametoka safari ya wapi sijui. Mabasi. Ndiyo ikawa hivyo. Lakini unajua nini, kwa shida kama alizonazo huyo Mariam ni ku..."

"Hodii..."

Sauti yenye kusema neno hilo ikamkatisha Ankia kwa kile alichotaka kuniambia, nasi tukatazama upande wa sebuleni. Ilikuwa sauti ya kiume, na sote tulifahamu mmiliki wake.

Ankia akasema, "Karibu..." kisha akaniangalia na kuniambia, "Tesha huyo."

Nikatikisa kichwa kukubali hilo, naye akaelekea mlangoni ili amfungulie jamaa.

Bila shaka kuja kwake Tesha kulikuwa kwa kusudi la kutimiza ahadi yake aliyonipa ya kuja kuniona, nami nikasogea mpaka hapo sebuleni nikimtazama Ankia alipomfungulia mlango na kuanza kusemeshana naye kiutani. Walionekana kuwa na uhusiano mzuri wa kaka na dada pia, naye Tesha akaingia ndani humo na kuniona.

Alikuwa amevalia T-shirt pana la mikono mifupi, lenye rangi ya kijani (Manga), pamoja na suruali ya jeans yenye rangi ya samawati iliyokoza. Na alinukia vizuri pia. Mwonekano wake ulitoa taarifa ya haraka kwamba alipenda kupendeza na kuonekana msafi, na hilo lilikuwa jambo nililopenda pia.

"Ah, kaka vipi?" akanisalimu kirafiki.

"Fresh tu, karibu," nikaitikia salamu yake.

Tukagonga tano kwa ngumi zetu, kisha akakaa kwenye sofa moja, vilevile na mimi pia la pembeni.

"Unakunywa soda gani we' mbwa?" Ankia akamuuliza hivyo Tesha.

Nikacheka kidogo kwa pumzi.

"Asa' soda ya nini, mi' mgeni hapa? Ushaniita mbwa, unajua ni nyama tu ndo' natumia," Tesha akamwambia hivyo.

"Na mifupa tu," Ankia akamwambia.

"Hahahah... aloo... hiyo ishu ya saa zile imekuwa mkosi kitaa hiki, kila kona nasikia unaongelewa mchina tu..." Tesha akaniambia hivyo, nasi kwa pamoja tukacheka.

"Kwa mazuri lazima mchina wetu aanze kusifika," Ankia akasema hivyo, akiwa amekaa kwenye mkono wa sofa karibu na mimi.

"Ah siyo poa," Tesha akasema.

"Hahah... me nafanana vipi na mchina bwana?" nikasema hivyo kiutani.

"Ah, si washamba wa huku tu kaka? Me mwenyewe naitwaga mpaka msudani eti kisa ngozi tu hii..." Tesha akaniambia.

"Sasa ndiyo kila mtu hapa atataka mazoea. JC hakuna kwenda nje," Ankia akasema.

"Aa wee... nisiende nje? Natoka nikitaka, na hakuna mtu ananisogelea. Sipendi shobo zisizo na maana..." nikasema hivyo.

"Wewe uko kama mimi bro, nawapaga gongo hili wanaoshoboka sana bila maana, yaani mtindo mmoja," Tesha akasema hivyo.

"Basi unajichetuaa..." Ankia akamwambia hivyo.

"Fact hiyo. We' mwenyewe unajua sisi tukoje, tunawapenda watu wakitupenda...."

"Na tunawatenda tusiowapenda," nikamalizia maneno yake Tesha.

Akacheka kwa nguvu sana na kusema, "Aminia, aminia," huku akigongesha kiganja chake kwenye ngumi yangu niliyomkunjia aipige.

Alionekana kuwa mjanja kweli na mwongeaji, hivyo nilijua kabisa angekuwa mwepesi kuzoeleka.

"Haya bwana, mapacha mmekutana. JC, leta nikafate basi..." Ankia akasema hivyo, akimaanisha nimpe hela afate dawa za mbu.

Nikampatia elfu moja.

"Zote?" akaniuliza hivyo.

Nikatikisa kichwa kukubali, naye akaenda upande wa jikoni kwanza kuiangalia mboga bila shaka. Nilipomtazama Tesha, alinifanyia ishara kwa mdomo wake kunionyeshea mwanamke huyo alipokuwa ameondoka, nasi kwa pamoja tukacheka kidogo bila kutoa sauti.

"Vipi, mdogo wako anaendelea vizuri?" nikamuuliza.

"Eh, yuko poa, yuko poa. Kichwa kilikuwa kinamsumbua kidogo, ila ameshusha dawa akalala. Akiamka atakuwa fresh zaidi," akasema.

"Miryam amerudi?" sauti ya Ankia ikauliza hivyo kutokea jikoni.

"Bado. Ma' mkubwa kamwambia kuhusu hiyo ajali akasema atajitahidi kuwahi. Unaelewa anavyojua kupanick," Tesha akaongea kwa sauti ya juu kiasi.

"Hata me ningepanick, we! Ajali siyo mchezo," Ankia akasema hivyo.

"Kwa hiyo... hawa walio hapo kwenu ni, mama zako?" nikamuuliza Tesha.

"Yah, mama wakubwa. Huyo aliyekupaka dawa saa zile ni mdogo wake na aliyemzaa mshua wetu... na huyo white ni dada yake na mama yetu. Ila... sisi wazazi wetu walishafariki," Tesha akaeleza.

"Aaa... sawa. We' unapiga mishe gani huku?" nikabadili mada upesi.

"Ah, nipo tu bro. Ajira kama unavyojua, ngumu kinoma kupata. Nimepiga-piga mishe kule Arusha miaka ya nyuma ila nilipofika huku, haba! Miezi inapita, lakini nitapata tu pa kuegamia," akaeleza.

"Ungemwomba sister akuunganishe sehemu," Ankia akasema hivyo akiwa anarudi sebuleni sasa.

"Ameshajaribu, ila michongo ya siku hizi haisimami fresh. Anataka nitulie mpaka apate panaponifaa," Tesha akasema.

"Na anavyowadekezaga sasa!" Ankia akasema hivyo na kutupita mpaka kuufikia mlango.

"Hiyo lazima, kupendwa kunaanzia nyumbani, we' vipi?" Tesha akamwambia hivyo kiutani.

"Halafu kunaishia wapi?" Ankia akamuuliza hivyo huku akifungua mlango.

"Masai," Tesha akamjibu.

Nikacheka kidogo, naye Ankia akakisukuma kichwa cha Tesha kwa kidole chake na kisha kutoka nje huku jamaa akimsindikiza kwa macho.

"Wali nazi..." Tesha akaniambia hivyo huku akinionyeshea ishara ya nyusi kuelekea upande wa Ankia.

"Usipime," nikasema hivyo.

"Ushaharibu mitambo mtu wangu?"

"Hahah... hamna, sijafika huko..."

"Uko nalo alone hapa, kamata tu."

"Napendaga kufanya vitu kwa mikakati..." nikamwambia.

"Hahahah... liko vizuri, usichelewe sasa," akaniambia hivyo.

"Vipi, ushaangukia nini?"

"We! Natamanigi tu, kuguswa halitaki eti. Aidha linaogopa ngoma ama mashauzi tu. Ila kwa wewe nafikiri litalegea."

"Kwani me nina nini?"

"Ah, HB. Halafu na vile umepiga action kama stelingi wa kihindi leo, nani asikutake?"

Nikacheka kidogo na kutikisa kichwa kwa kufurahishwa na utani wake.

"Una maumivu makali bado?" akaniuliza.

"Hamna, ni huu mkono kidogo tu unakwangua ila niko poa," nikasema.

"Sawa. Kama vipi... twende hapo Masai tukazimue kidogo, ama nini?"

"Hapo bar?"

"Ee. Ama bia hupigi?"

"Nakunywa."

"Yah, twende tu mtu wangu tupige mbili tatu, urudi ulale umechangamka," akasema hivyo.

"Na huyu?" nikamuuliza hivyo, nikimaanisha Ankia.

"Tunaenda naye. Anapenda bia huyo!"

"Kumbe?"

"Wee! Sema humtoi humu ndani kama huendi kumnunulia za maana ila kwa wewe HB hata kwa moja tu atakubali kutoka," Tesha akaongea kiutani.

"Ahahah... acha kufanya hivyo bana..." nikamwambia.

Akacheka kwa nguvu, nasi tukagongesha tano kirafiki tena.

"Vipi, mnanisema au?"

Ankia akawa ameuliza hivyo baada ya kurudi muda huo huo. Mkononi alishika kifuko kigumu chenye kuonyesha dawa ndefu za kuchoma za mbu, na sisi wote tukamwangalia.

"Ee, sugar mommy wetu we' ndo' mada kuu hapa. Tulikuwa tunafanya revision kidogo," Tesha akamwambia hivyo.

Ankia akasonya kiutani na kufunga mlango, naye akaanza kuja upande niliokaa mimi huku akisema, "Eti sugar mommy. Kuna sugar mommy hapa?"

"Si ndiyo wewe?" nikamwambia hivyo.

"Kwa ushuga upi? Nina miaka 32 tu mie msinizeeshe namna hiyo," Ankia akasema hivyo na kukaa pembeni yangu.

"Kwani mashuga mommy huwa wanaanzia miaka mingapi?" Tesha akamuuliza.

"32," nikampa jibu, naye Tesha akacheka.

Ankia akanikata jicho la kuudhika eti, nami nikatabasamu tu.

"Baby mama, twend'zetu Masai," Tesha akamwambia.

"Kufanyaje? Me napika sa'hivi," Ankia akasema.

"Acha kupika wewe, utapika badae. Twende tukanywe pombe!" Tesha akaongea kwa msisitizo.

Nikacheka kidogo.

"Akili yako yote iko hapo tu. Me siwezi kwenda, nenda mwenyewe," Ankia akasema hivyo.

"Unazingua. Basi baki mwenyewe, me naenda na JayZee..." Tesha akamwambia hivyo.

Nikacheka sana pamoja na Ankia, na mwanamke huyu akamwambia Tesha, "Siyo JayZee, ni JC."

"Aaaa dah, nimechapia," Tesha akakiri.

"Mwishowe atakuita Chelsea," Ankia akaniambia.

"Wewe baki kupika, si unataka kupika? Sisi twende JC," Tesha akaniambia.

"Mh? Huna lolote. Eti kweli unaenda?" Ankia akaniuliza.

Nikamtikisia kichwa mara moja kukubali.

"Sasa je! Kwa hiyo?" Tesha akamuuliza hivyo Ankia.

Mwanamke huyu akaibana midomo yake kama kuonyesha anatafakari, huku sisi tukimwangalia, naye akasema, "Basi, ngoja nikachange nguo... halafu twende."

"Hahaaa... umeona? Si nilikwambia?" Tesha akasema hivyo kwa shauku.

Nikasimama huku nikicheka pia, naye Ankia akasimama pia.

"Amekwambia nini?" Ankia akaniuliza.

"Hajaniambia kitu, nenda kavae. Na mimi ngoja nikabadili gwanda," nikasema hivyo na kuanza kuelekea upande wa chumba.

Aisee! Tesha alikuwa amenifanya nimkumbuke rafiki yangu mmoja aliyekuwa na vituko vingi sana katika njia yake ya kuongea, na hali ya urafiki niliyokuwa nimeanza kujenga pamoja na wawili hawa ilinichangamsha sana.

Nikaingia chumbani na kubadili mavazi; nikivaa T-shirt zito kiasi mithili ya sweta laini, lililokuwa na mikono mirefu lenye rangi nyekundu mchanganyiko na nyeupe, pamoja na suruali nyeusi ya jeans. Nikachana nywele vyema, nikajiweka sawa kabisa mwilini na kujipulizia manukato, kisha nikarejea pale sebuleni. Tesha akasifia mwonekano wangu na kutania kwamba ningeenda kuua macho ya wengi pale Masai, nami nikakaa sofani kumsubiri Ankia.

Dakika si nyingi sana mwanamke huyo akawa ametoka, akiwa amevaa gauni fupi jeupe lenye urembo wa maua-maua na lenye kuvutika lililoyaonyesha mapaja yake kiasi. Nilimtazama kwa umakini kiasi maana mwonekano huo ulimwelekezea sana fikira.

Nguo hiyo yenye kuubana mwili wake ilikuwa na mikono mirefu, iliyoficha hadi shingo lakini ikiacha uwazi wa duara kifuani kwake kuonyesha mstari ulioyatenganisha matiti yake yaliyonyanyuliwa juu. Tumbo lake lilijichora kwa unyama-nyama aliokuwa nao, na usoni alipendeza pia kwa kujiremba kiasi, huku nywele zake za kusukwa mtindo wa rasta fupi akiwa ameziachia tu pande za masikio yake.

Alikuwa akiniangalia kwa njia iliyoonyesha alitaka kuona ningesemaje kuhusu mwonekano wake, nami nikamwambia amependeza sana. Tesha kama kawaida akawa anamsifia kwa utani mwingi, naye Ankia akasema mboga ilikuwa imeshaiva na alikuwa amebakiza kupika ugali, kwa hiyo angepika muda ambao tungerudi. Haikuwa na neno.

Tesha alionekana kutaka sana kwenda kutubariki kwa vinywaji, bila shaka aonekane na rafiki mpya, na kwa hilo mimi pia nilikuwa tayari ili hiyo Masai na yenyewe niijue. Tukatoka baada ya Ankia kuzichoma dawa kwenye vyumba vyetu ili tukirudi mbu wasiwe vikwazo tena, taa za ndani zikazimwa, milango ikafungwa, nasi tukavaa vya miguuni na kuanza kutembea kuelekea huko Masai.

Nilimuuliza Tesha ikiwa dada yake alikuwa na kawaida ya kuingia nyumbani usiku, naye akasema mara kwa mara alirudi usiku mpaka kufikia saa nne kabisa ikiwa kazi zilimhitaji zaidi, lakini kama sivyo basi angerudi mapema tu, ama hata siku zingine kutokwenda huko kazini kwake kabisa. Bado nilitaka kujua mambo mengi kuhusu mdogo wake, Mariam, na hizi hatua za mwanzo za urafiki baina yangu na Tesha huenda zingesaidia niweze kujiingiza zaidi kwenye kuielewa vizuri zaidi hali ya yule binti.

Tukawa tumeifikia Masai. Kwa saa mbili hii joto bado lilikuwa halijapanda sana ndani humo, lakini tulipoingia tu kweli macho ya wengi yakawa kwetu; hasa mimi. Na mimi kama kawaida nilikuwa nimeweka mwonekano makini usoni, nikitembea nyuma yake Tesha huku Ankia akiwa karibu nami.

Tesha alikuwa anasalimiana kwa ufupi pamoja na watu aliofahamiana nao mpaka tulipofikia meza ndefu iliyotengenezwa kwa mbao nene, ikiwa imezungukwa na viti virefu vya plastiki ngumu vya kukalia, nasi tukaketi hapo. Hatukuwa tumeingia ndani sana kwenye sehemu hii, kwa hiyo Tesha akawa ananiambia ni wapi kulikuwa na vyoo na kumbi maalumu ya maVIP, pamoja na vyumba vya kulala wageni.

Kwa watu waliokuwepo upande kwa upande wakishusha bia zao taratibu, niliona hawakuweza kujizuia kuniangalia sana, na Ankia aliliona hilo na kuanza kunitania kwamba bila shaka ningejikuta napigwa kwa chupa kichwani kwa sababu ya demu wa mtu kunitamani. Nikacheka kidogo tu na kuendelea kutulia.

Mhudumu mwanamke akaja na kutuuliza vinywaji gani tungependa kutumia, akiwa amevalia T-shirt nyeupe na kikaptura chenye kubana sana na kuyaacha mapaja yake wazi. Tesha akatuambia tuagize, naye Ankia akasema aletewe bia tamu ya Savannah, nami nikaomba niletewe Serengeti Lite ya moto. Tesha angekunywa Serengeti Lager, naye akamwambia mhudumu atuletee sisi wanaume tatu tatu na Ankia aletewe Savannah mbili maana ni katamu ila kakali.

Inaonekana Tesha alifahamika sana hapa kwa hiyo mhudumu akaondoka tu bila kuchukua pesa, ikimaanisha malipo yangekuja baadaye. Sikutarajia jamaa aagize bia tatu kabisa lakini order ikawa imeshaenda na mimi nisingeizuia, hivyo tukaendelea kusubiri huku tunapiga story.

Muziki uliochezwa ulisikika kwa sauti nzito kwenye spika za sehemu hiyo, na TV za flat screen zilizokuwa zimetundikwa juu sehemu kadha wa kadha kwenye kumbi hiyo zilionyesha mechi ambayo sidhani watu wengi waliifatilia.

Kukawa na watu wachache ambao walifahamiana na Tesha pamoja na Ankia waliokuja mezani hapo kutoa salamu, nao wakawa wanatambulishwa kwangu. Nilitendewa kana kwamba nilikuwa mtu mashuhuri saaana, nikijua wazi wengi wangetaka kujenga ukaribu zaidi pamoja nami, lakini kwangu mie salamu na kucheka kidogo tu ndiyo yaliyokuwa maitikio niliyowapa.

Sikuona "pisi" yenye maajabu makali hata kumzidi Ankia sehemu hiyo, kwa hiyo sikuelekeza fikira kwa mwanamke yeyote hapo ingawa wengi walinitazama kwa macho ya uvutio. Bia zikaletwa, nasi tukaanza kunywa taratibu.

Nilikuwa najitahidi kusoma mazingira ya hapo ili nipazoee upesi. Nadhani labda ni shauri ya muda kutokwenda sana ndiyo sababu hapakuwa pamechangamka kivile, ama labda kwa sababu haikuwa wikiendi, kwa vyovyote tu ila palikuwa kawaida sana. Ndipo akaja mwanamke fulani mweusi kiasi mpaka kufikia mezani hapo. Alifahamiana na Tesha na Ankia, naye akasalimiana nao kwa kuwakumbatia na kuanza kuzungumza kwa shauku.

Alikuwa mzuri. Mwili wake haukuwa mnene, urefu wa kadiri, na alionekana kuwa mwongeaji sana. Alisuka nywele ndefu laini na kuzibana nyuma ya kichwa chake, akiwa amevalia nguo ndefu kama kijora iliyochoresha kalio lake vizuri kwa jinsi alivyoivuta kwa mbele, na alikuwa na macho madogo ambayo yangefanya aonekane kama mchina endapo angekuwa na ngozi nyeupe. Aliitwa Joy.

Akawa ametambulishwa kwangu, nami nikampa salamu huku nikimwangalia kwa upendezi. Nadhani njia yangu ya kutazama mwanamke kila naposema nimemwangalia kwa upendezi sikuzote ilikuwa inatoa ujumbe fulani wenye kuamsha hisia nzuri kwake, na huyo Joy alinitazama kwa macho yaliyonipa ujumbe wa "tukutane chumbani."

Nikacheka kidogo tu, naye Tesha akacheka pia kwa sababu alinielewa sana inaonekana, hivyo akaanza kumsukumia Joy upande wangu eti; akae hapo hapo, tena karibu na mimi. Joy alikuwa amefika na marafiki zake hapo ambao walienda kukaa kwenye meza nyingine kabla hajaja upande wetu kutusalimia, kwa hiyo akawa akisema anahitaji kwenda huko.

Lakini Tesha akawa anamsisitizia akae na sisi, akiniambia nimshawishi pia, nami nikaushika mkono wa huyo Joy na kuuvutia kwangu taratibu. Aliniangalia huku akitabasamu kiasi, naye akaja polepole kama vile amepumbazika. Nadhani jambo hilo lilimfanya Ankia ajisikie vibaya kiasi, lakini akajikaza tu na kuendelea kuweka utulivu huku akinywa.

Nikamwambia Joy akae kiti kilichokuwa pembeni yangu, naye akakubali na kuketi. Tesha akamwagizia bia mbili za Serengeti Lite pia, nasi tukaendelea kunywa taratibu huku Tesha akiongea na Joy sanasana.

Nilipomwangalia Ankia, alikuwa ametulia tu akicheza muziki taratibu kwa kupeleka kichwa huku na huko bila kuniangalia, nami nikalishika paja lake kwa chini. Akaniangalia, na jinsi nilivyomtazama kwa macho yangu ya uchokozi kukamfanya ashindwe kujizuia kutabasamu kwa haya, na hapo nikawa nimefanikiwa kumtuliza.

"Oy, sister huyo..." Tesha akaniambia hivyo huku akitazama upande wa nje kabisa.

Nikageuka na kuliona lile gari la Miryam likipita kuuelekea upande tuliotokea kule nyumbani, kumaanisha dada mtu ndiyo alikuwa anarudi.

Nikamwangalia Tesha tena, naye akasema, "Yaani sasa hivi ndiyo amewahi."

Alihitaji kuongea kwa sauti ya juu ili nimsikie, nami nikatabasamu kidogo.

"Dada'ako hatakuchapa ukienda home unanuka pombe kweli?" Ankia akamuuliza.

"Acha zako wewe, nani achapwe?" Tesha akamuuliza.

"Tena zile mboko za kuzunguka!" Joy akasema hivyo, nasi wote tukacheka.

"Sister hamaindi kabisa, sisi ndo' mayai yake bana," Tesha akajisifia.

"Unavimbaga kweli kisa dada'ako anawapenda sana. Siku akiolewa sijui nawe utaolewa naye?" Joy akamwambia hivyo.

Ankia akacheka na kusema, "Lilivyo hili, litaenda naye kabisa ili malezi likayapate na huko ukweni."

"Aaa mnanichoresha vibaya, au mnadhani sijui kama sitakaa na sister tu maisha yote?" Tesha akasema.

"Kumbe unalijua?" Joy akamwambia.

Tesha akanywa bia na kuvimbisha mashavu kwa njia ya masihara, nasi tukacheka kidogo.

"Ila dada yako Tesha hataki kuolewa kabisa, eti? Ama hapendi tu wanaume?" Ankia akamuuliza.

"Eeh Tesha, nasikiaga wanakujaga hadi kumtolea posa ila anawatimua," Joy akamwambia.

"Siyo hivyo. Mambo magumu tu sa'hivi, sister anatutunza kwanza. Kama kuolewa ataolewa tu baadaye. Jana kuna bwege mwingine alikuja, na yeye akabebeshwa virago alivyovileta. Hapana cheza na Mimi!" Tesha akasema.

"Wewe ndiyo ulimfukuza?" nikamuuliza.

"Hamna, sister..." Tesha akajibu.

"Huwa wanamwita Mimi..." Ankia akanijulisha.

"Ooh..." nikasema hivyo kwa uelewa sasa.

Na hiyo ingefanya mambo yawe rahisi hata kwangu pia, kumwita Mariam Mamu, na dada yake, Miryam, kumwita Mimi.

"Unatiaga michumvi wewe! Eti akamfukuza. Alivyo mstaarabu dada'ako najua alimwambia tu, 'pole... nimeshawahiwa,'" Joy akasema hivyo.

Tukacheka kidogo mimi na Ankia.

"Halafu bro, waliniambia ulifika kwanza wewe... sijui ulipotea eti..." Tesha akaniambia.

"Ee bana, nilikuwa naitafuta nyumba ya Ankia kwa kutumia ramani. Sasa kidoti chekundu kikanileta kwenu, siunajua zimekaribiana sana..." nikamwambia.

"Eee dah! Ma' mkubwa ndiyo aliniambia, nawe ukajikuta unachangamkiwa kuwa mchumba..." Tesha akasema.

Tukacheka sana kwa pamoja.

"Kweli? Walifikiri ni yeye?" Joy akauliza.

"Ee..." Tesha akajibu.

"Hahah... mbona hukuniambia?" Ankia akaniuliza.

"Nilisahau tu," nikamwambia hivyo.

"Asa' si unaona, matatizo tu. Yote hayo kumfosi sister aolewe. Yaani wanawake na ndoa bana!" Tesha akaniambia hivyo.

"Ndoa sifa kwa mwanamke, hujui hilo baba, basi umeachwa..." Joy akamwambia.

"We' ya kwako iko wapi?" Tesha akamuuliza.

"Si nakusubiri wewe?" Joy akamwambia.

"Sawa, utasubiri sana," Tesha akasema hivyo, naye Joy akacheka.

Tukaendelea kunywa na kupiga story, mpaka inaingia saa nne hivi, tulipokuwa mwishoni kumalizia vileo vyetu, bia zingine zikaongezeka mezani hapo. Tesha hakuwa ameagiza zingine, hivyo akauliza zimetokea wapi. Mhudumu akamwambia kwamba kuna mtu alikuwa amenunua kwa ajili yangu mimi, kwa hiyo tayari zilikuwa zimeshalipiwa na sisi tungetakiwa kunywa tu. Bia kiujumla zilikuwa Serengeti Lite 20!

Tesha akamwambia mhudumu asepe, meza ikiwa imefurika bia, naye Ankia akaniambia inaonekana kuna sugar mommy hapo ndiye aliyekuwa amezituma hizo ili kuanza kunichokonoa. Nikamwambia hilo halingeniongezea wala kunipunguzia kitu chochote kile kutoka kwa mtu ambaye sikumjua, kwa hiyo kama amezileta zinywewe, zingenyweka tu. Tesha alikuwa akiniambia hayo ndiyo mambo sasa, na bila shaka masaa ya kukaa hapo yangeongezeka mpaka suala la Ankia kupika ugali nyumbani lingesahaulika kabisa.

Tukaendelea kunywa taratibu tu, huku mzuka wa hapo Masai ukizidi kupanda kadiri dakika zilivyoendelea kutembea, nami ningetoka mara kwa mara kwenda nje kuzungumza na simu ama kutoa haja ndogo chooni. Vibe la pombe liliwaingia vyema Tesha na Joy, hata mimi na Ankia pia, lakini sisi tulikuwa watulivu zaidi.

★★

Mpaka kufikia saa sita bado tulikuwa hapo, na hata kabla ya kumaliza bia tulizoongezewa, zikaletwa zingine 20. Inaonekana huyo mtu alikuwa amenipenda ama kunitaka, lakini bado hakujitambulisha kwangu, na mimi sikujisumbua kumtafuta wala. Kuna watu waliokuwa wanakuja kuomba bia, nasi tukawa tunawapa, na mzuka ukazidi kuongezeka.

Watu walicheza, waliimba, na sisi tukaendelea kunywa na kupiga story za kufurahisha hadi saa nane kufika. Nilikuwa nimekunywa bia 7 tu, na wenge la kulewa lilifanya macho yangu yawe mazito kiasi. Wenzangu walishusha pombe 10 na bado walikuwa wanaendelea, kwa hiyo mimi mtegeaji nikawa macho zaidi yao.

Ankia angenilalia begani na kuongea mambo mengi sana, na mimi niliendelea kutulia tu. Joy alianza kupitisha kiganja chake kwenye paja langu, akilipapasa na kulifinya mara kwa mara, na nilipomwangalia niliona hiyo kuwa sababu ya kuingiwa zaidi na pombe kichwani kwake. Nilifurahia kwa kweli. Siku ya pili tu ugenini tayari nikajihisi kuwa mwenyeji.

Nilipoona uzito wa pombe unamlemea Tesha, nikasimama na kwenda kumtoa kwenye kiti, nami nikamwambia tuelekee nyumbani kwa kuwa tayari bia zetu za mwanzo alizoagiza alikuwa ameshalipia. Alikuwa amelewa siyo poa.

Nikamwambia na Ankia tuondoke, naye akatii na kusimama huku akiyumba. Joy alikuwa amelewa pia lakini siyo ile ya kumyumbisha, akionekana kuwa mzoefu zaidi wa pombe, naye akatufata pia tulipotoka sehemu hiyo kwa pamoja. Tesha hakuweza kutembea vizuri, akiyumba huku na huko na akiongea sana, nami nikamsindikiza mpaka getini kwao, nikiwaacha Ankia na Joy wanaenda kule ndani kwetu. Usiku wa saa nane huo.

Tesha alikuwa anasema ana kama wiki hajanywa pombe ila furaha niliyompa leo kwa sababu ya kumwokoa mdogo wake ilimfanya ajiachie namna hiyo, nami nikawa namwangalia tu kwa kujali kiasi. Alionekana kuwa mtu mwenye huzuni, na sikujua ni kwa nini niliwaza hivyo.

Geti likawa limefunguliwa, na aliyefungua hakuwa mwingine ila bibie Miryam. Alikuwa na mwonekano wa mtu aliyetoka usingizini, lakini si ule mzito mno. Alitutazama kwa umakini. Nilihisi labda angekuwa mkali kwa Tesha kutokana na kurudi usiku akiwa amelewa, lakini haikuwa hivyo.

Akaacha uwazi ili kuturuhusu kuingia, naye Tesha akatangulia huku nikiwa nimemshika mkono kuhakikisha hajigongi getini.

"Mimi... ulikuwa umeshalala? Ungekuja nawe tukapiga bia kidogo," Tesha akamsemesha hivyo.

"Kulewa ndiyo bia kidogo? Em' ingia ndani..." Miryam akamwambia kwa sauti tulivu.

Tesha akiwa ananesanesa, macho mazito mno, akaniangalia na kusema, "Umemwona? Huyu ndiyo mkurugenzi hapa. Chochote anachosema tunafata. Nampenda mno... naweza nikaua kwa ajili yake."

Tesha aliyasema maneno hayo kilevi, lakini yalibeba uzito nilioelewa kuwa ulitoka ndani ya moyo wake. Nikamwangalia Miryam usoni, naye akamshika mdogo wake mkononi ili amwongoze kwenda ndani. Lakini Tesha akaweka mgomo kiasi na kuingiza kiganja chake mfukoni, kisha akaitoa simu yake na kuiwasha, halafu akanipatia.

"Andika namba bro... nakukubali sana," akaniambia hivyo na macho yake kama yanataka kudondoka.

"Atakupa hata kesho," Miryam akamwambia.

"Ee kaka, nitakugei kesho," mimi pia nikamwambia.

"Hamna... andika bana, kwani saa ngapi? Mwishowe kuku awike. Andika hapo..." Tesha akasisitiza.

Nilihisi hali yote ya hapo ilimletea picha mbaya sana dada yake, lakini nikaichukua tu simu yake na kuandika namba upesi. Nikamrudishia, naye akanisonta kwa kidole chake kwa kurudia-rudia kuonyesha jinsi alivyonielewa, halafu akaanza kuelekea huko ndani.

Miryam akanitazama usoni, kasura kake ka kuvimba kakiwa na mwonekano wa kitoto shauri ya kutoka kulala. Sikujua alikuwa amepanga kunirushia maneno gani wakati huu, lakini nilikuwa nimeshalewa pia kwa hiyo nisingeyajali sana. Hapa kilichokuwepo ilikuwa kuondoka tu maana mdogo wake nilimrudisha kwao salama.

"Angalia asiangukie meza huyo..."

Nikamwambia hivyo kwa sauti tulivu tu. Alinitazama machoni kwa njia fulani yenye kujali, na nilikuwa sijalitambua hilo hata kidogo mpaka aliponisogelea karibu zaidi na kisha kunikumbatia taratibu!


★★★★★★★★★

ITAENDELEA

★★★★★★★★★

Full Story WhatsApp or inbox

Whatsapp +255 678 017 280
M
shukhran mkuu
 
Okay
MIMI NA MIMI

A Story by Elton Tonny

Familia, Urafiki, Mapenzi, Kazi, Tamaa, Hila, Usaliti, Siri, Mambo Ysiyotazamiwa

R-rated 18+

Enjoy!


★★★★★★★★★★★★★

SEHEMU YA KWANZA

★★★★★★★★★★★★★


Maisha ni safari ndefu yenye kila aina ya changamoto, na hakuna mwanadamu yeyote azaliwaye kwenye sura ya dunia hii bila kuzipitia. Changamoto huja kwa nyuso tofauti-tofauti kwa kila mmoja, na kamwe haziwezi kufanana wala kuwa na uzito wa aina ile ile kwa watu wote wanaozipitia. Ikitegemea na hali, eneo, nyutu za watu, na mambo yanayowazunguka, sikuzote changamoto huwepo ndani ya maisha ya mtu kumsukuma awe na nia ya kupambana ili kujitoa ndani ya hizo na kuwa na maisha bora.

Tunaambiwa elimu ndiyo ufunguo wa maisha bora lakini hata watu wenye elimu ya juu bado huhangaishwa na matatizo mengi yanayowakosesha amani. Kila mtu mmoja mmoja anatamani kufikia sehemu nzuri maishani kiasi kwamba hata wale waliozifikia sehemu hizo bado wanakuwa hawaridhiki. Ni tamaa yetu sote kuishi maisha yenye kuridhisha, lakini mivurugo ya maisha sikuzote huturudisha nyuma. Iwe ni kwa matajiri, au wenye hali za chini kiuchumi.

Kwa sababu ndivyo ambavyo sisi sote tumezaliwa na kukuta hali zikiwa namna hiyo tokea mwanaume wa kwanza alipoamua kumtandika ndugu yake mpaka akafa, imetubidi tuyaishi maisha kwa namna ambavyo yametutaka tuyaishi. Usione mtu anafanya jambo fulani ambalo linapingana na uasili wa kufanya mambo ukadhani hafai. La. Ni kwamba maisha ndiyo yamemfanya akaona kufanya jambo hilo kuwa sahihi. Analazimika kuishi kwa njia hiyo aidha kwa kupenda ama kusukumwa tu, maadamu aishi.

Hivyo kamwe huwezi kuhukumu maisha ya mtu kwa kumtazama tu bila kujua kiundani ni mambo yapi yaliyopelekea mpaka akafikia hatua za kuishi namna aishivyo. Kujenga taswira nzuri mbele ya jamii ni jambo la muhimu, lakini maisha yanapokulazimu kuishi kwa namna ambayo jamii itayahukumu vibaya, unachopaswa kufanya ni kula ugali wako na kuvuta shuka kulala, ili kesho uamkie mambo mengine na kuendelea kuishi. Basi!

Naandika haya mimi siyo chizi. Mimi siyo mtunga mashairi wala nini. Ila nimeona tu nijaribu kuzama zaidi ndani ya vina virefu visivyoelezeka kwa mapana sana kuhusu neno hili: maisha. Maisha hayawezi kufanana kwa kila mmoja. Hayawezi kuendana. Hayawezi kuingiliana kwa asilimia zote na kumfanya mtu wa hali ya chini aweze kuwa kama kiongozi wa nchi hii kwa ufanisi aupatao kutokana na jasho la huyo huyo "mtu wa hali ya chini."

Kila mtu ana kisa chake mwenyewe cha maisha. Alipo fulani sasa hakufika kwa muujiza, kuna sehemu amepita. Unaweza ukashangaa kwa nini watu wanahangaika sana kufatilia maisha ya watu maarufu zaidi. Ni kwa sababu tayari wameshajijengea umaarufu. Hawakuzaliwa nao, waliutafuta, wakaupata. Wanaoendelea kuwafuatilia tu wanaishia kuwa watu wa kutamani. Hata hao watu maarufu wamepitia changamoto nyingi maishani, lakini hakuna mtu hata mmoja aliyejisumbua kuzijua wala kuziulizia mpaka walipokuja kupata huo ufanisi na kuzigeuza changamoto hizo ziwe kitu cha kuwatia moyo wengine kupambana zaidi.

Hutajali saana kufatilia maisha ya ndani zaidi ya mwanamke abebaye sinia la karanga kichwani, akiwa amebeba mtoto mdogo mgongoni, sura yake ikiwa imechoka, akiziuza karanga hizo stendi ya mabasi na jua likiwa kali sana. Tayari tu una kitu ndani yako kinachojua kwamba ana changamoto zake, kama watu wote, kwa hiyo nawe utabaki kutulia na za kwako tu, si ndiyo? Angalau nunua hata hizo karanga basi, hata ya mia tu. Itampa faraja kuona kwamba hata kesho anaweza kujikwamua na kuendelea kupambana kuzivuka changamoto zake ili ajenge maisha mazuri kwa kiwango ambacho Mungu atambarikia kukipata.

Sina lengo la kuandika mahubiri ili muanze kutenga sura na mistari. Ni kwamba tu nimeangalia hata maisha yangu mwenyewe na kugundua kwamba kuna changamoto nyingi zilizo ngumu maishani mwa mwanadamu, na japo kwa wengi zinatofautiana, mapenzi ni suala lizushalo changamoto kwa KILA MTU. Kubali, kataa. Hakuna mtu apitaye upeo wa ujana bila kukumbwa na changamoto za jambo hilo. Kwa nini?

Kwa sababu hakuna lengo lolote la kuishi isipokuwa upendo. Ni kitu cha kiasili. Kila mtu anacho. Nazungumzia upendo wote, iwe ni wa kindugu, kirafiki, kishkaji, kihuni, vyovyote vile, ni lazima tu kuwe na changamoto nyingi sana. Sasa inapofikia kwenye ule upendo wa kijinsia ndiyo kabisaa! Watu mpaka wanauana kwa sababu ya kuumizwa na mapenzi.

Lakini kwa jinsi ambavyo mambo yamekuwa kufikia kipindi hiki, imeshaonekana kuwa jambo la kawaida sana kwa mapenzi kuwa kitu chenye kuumiza badala ya kutakiwa KUBAKI kuwa kitu chenye kuridhisha. Na kama nilivyosema mwanzoni, kwa sababu tumezaliwa na kuyakuta namna hiyo, basi ndiyo tunaendelea kuyaishi namna hiyo hiyo tu. Lakini kuyaishi namna hiyo hiyo tu si jambo linalofaa.

Ni muhimu kuishi kwa kusudi, na imenichukua visa vingi vilivyotokea katika maisha yangu mpaka kufikia sasa kutambua kwamba mapenzi ya kujifurahisha tu hayana faida yoyote. Yanapaswa kuwa na lengo. Lakini kwa wengi, hata MIMI, hutuchukua muda mrefu mpaka kuja kumpata mtu anayeweza kukufanya ulitamani sana lengo hilo, haijalishi ni changamoto za aina gani utakazopitia, maadamu akiwa na wewe, unajua yote unaweza kuyashinda....


★★★★


Ilikuwa ni kwenye siku ya Alhamisi, nikiwa ndani ya gari kuelekea eneo lingine la jiji la Dar es Salaam. Siku hii kama siku zingine tu ilionekana kuwa na ukawaida wa mambo mengi ya kutarajia kwa maisha tuliyozoea sisi wabongo, na ndani ya gari hili kulikuwa na kioja kilichochangamsha asilimia kubwa ya abiria waliokuwemo. Niliposema gari sikumaanisha nina gari hapa.

Hii ilikuwa ni ndani ya usafiri rahisi wa umma, ama daladala ndogo aina ya Costa, na kutokea nilipokuwa nimekaa siti ya pili kutokea mbele upande wa pembeni alikaa mwanamke mtu mzima kiasi, akiwa amevalia nguo ya batiki na kujifunga kiremba kichwani, masikioni kukiwa na vifaa vidogo vya kuunganisha sauti kutoka kwenye simu.

Bila shaka alifurahia muziki mzuri sana kiasi kwamba alikuwa akiimba kwa sauti ya juu kuufatisha, lakini ilionekana kwamba hakutambua sauti aliyotoa ilizidi kupanda. Watu kadhaa walimzungumzia, wakidhani angekuwa msukuma, walimcheka na kuendelea kumtazama tu, huku yeye akiendelea kuburudika na kudhani wanamfurahia sana kutokana na kuimba kwake.

Nilikuwa nimekaa upande wa kioo cha dirisha nikipulizwa zaidi na upepo uliokipisha kioo kilichokuwa wazi, mara kwa mara nikifungua simu yangu kutazama ujumbe ulioingia na kujibu, kisha kuifunga na kuendelea kutazama nje. Kuna jambo fulani kuhusu mimi ambalo sikuzote lilifanya watu wanitazame sana, na hata bila kujionyesha kwao kwamba wananitazama mno au mimi kutowaangalia, nilijua tu kwamba wangenitazama kwa wingi.

Sitaficha hili nikiwa ndiyo nimeanza kuelezea kisa changu. Sura niliyobarikiwa kuwa nayo ilipendeza. Wazungu huita wanaume wenye sura nzuri sana "handsome," na mimi kiukweli nilikuwa hendisamu. Siyo uzuri ule wa kujitahidi sana kuufikia, bali ule uzuri wa asili unaoonekana hata bila kujitengeneza baada ya kutoka kusinzia.

Labda kingine kilichozidishia jambo hilo utizami wa watu kunielekea ni kutokana na ngozi yangu kuwa nyeupe. Oh najua kuna watu huhangaishwa sana na rangi ya mwili, na ya kwangu ndiyo iliyoongeza utomato mtamu kwa sura yangu. Macho madogo yenye kope na nyusi nyingi kwa juu, pua ya kawaida na midomo yenye uwekundu isiyo ya denda nzito sana vilifanya nionekane kuwa kama mchina ama mwarabu kabisa!

Nywele zangu zikiwa ni laini, sikuzote nilipenda kuzichana vizuri huku pande za kichwa zikiwa zimepunguzwa kidogo sana kufikia nyuma ya usawa wa masikio yangu. Mwonekano wa kimwili ulikuwa wa kiume zaidi, lakini si ule uliopita kiasi. Nilifanya mazoezi kipindi cha nyuma kuujenga lakini kufikia hiki sikujihusisha na mazoezi kwa utaratibu kama ule wa kujenga mwili kuwa imara sana, kwa hiyo nilikuwa na mwili ambao ungeonwa kuwa mwembamba lakini mpana, na nilikuwa mrefu pia.

Kama ni jambo lingine lililoongeza hali ya mvuto kwangu na hata kwa watu niliopendelea kuchangamana nao, basi ilikuwa ni usafi. Kuanzia jinsi nilivyochonga ndevu zangu hafifu kutokea kwenye timba mpaka kidevuni, mavazi mpaka viatu, nilionwa kuwa mtanashati na bishoo, au sharobaro kwa watu wengi. Mwonekano wangu na jinsi nilivyojiweka tu mbele ya watu ilifanya kwa mtazamo wa kwanza yeyote afikiri nilikuwa mtu mwenye kujipa hadhi fulani ya juu, kama mtu mwenye kujisikia sana, na ni kitu ambacho nilikuwa nimeshazoea tangu zamani.

Hata sasa ndani ya safari hii, niligundua kuna watu ambao walipenda mwonekano wangu na kunitazama sana. Nilivalia T-shirt ya rangi ya zambarau iliyopauka yenye mikono mirefu, suruali nyeusi ya kardet, pamoja na viatu vyeupe miguuni. Manukato niliyojipulizia pia yaliongeza kiwango cha mvuto wa kiume niliokuwa nao, ila sikukazia fikira mno suala hilo na kuendelea kukaa kwa utulivu tu nikisubiri kufika kule nilikodhamiria kwenda.

★★

Gari liliendelea kutembea tu, likipita majengo na magari mengi ndani ya barabara pana kwenye jiji hili lililo na shughuli nyingi, na mara kwa mara msongamano wa magari ulifanya tukawizwe njiani kutokana na kusimama kwa muda mrefu barabarani. Joto likiwa kali mchana huu, angalau ndani ya daladala hii kioja cha mwanamke huyo kuimba kwa sauti ya juu kilifanya watu wafurahike zaidi, na alikuwa bize kweli kufatisha maneno ya kila wimbo alioufahamu.

Baada ya kutumia dakika nyingi sana gari likiwa limesimama sehemu moja tu, ikabidi dereva atumie akili nyingine. Akaliingiza gari kwenye barabara ya changarawe ambayo ingezungukia upande wa mbali kiasi ili kuweza kutokea mbele zaidi ya njia tuliyotumia kupita kwa ajili ya safari yetu. Hatukujua kilichosababisha foleni hiyo lakini lilikuwa ni jambo la kawaida sana kwa barabara za jiji hili.

Tukaendelea kusonga. Mdogo mdogo tu, huku mwanamke yule akikomaa kuimba "kekundu, kekunduuuu..." na baadhi ya wadau ndani ya gari wakiitikia pamoja naye, jambo lililofanya tabasamu hafifu liniponyoke midomoni mwangu maana ilikuwa ni kwaya moja ya kitambo kweli. Barabara hii ilifanya gari lipite kwenye kona zilizobanana sana kutokana na nyumba kadha wa kadha kukaribiana, kisha tukaingia sehemu yenye uwazi zaidi ambako miti mingi ilionekana na nyumba chache sana zilizoachana kwa umbali mfupi.

Baada ya dakika chache za mwendo huo wa gari kutembea kama linatubembeleza, likafika sehemu fulani yenye miti zaidi bila nyumba na kusimama baada ya kitu kama kishindo kusikika kutokea kule mbele kwa dereva. Watu wakawa wanauliza nini kimetokea, na sasa ikawekwa wazi kuwa gari liliharibika. Doh! Ikabidi wote tushuke na kusimama nje, huku kondakta na dereva wakijitahidi kulifanyia ukarabati ambao tulijua usingeleta matokeo ya haraka.

Nilikuwa nimebeba begi la mgongoni lililotuna kutokana na kuweka vitu vyangu vingi, nami nikawa nimesimama pembeni tu huku wengine wakijadili ya hapa na pale kuhusiana na jambo hilo. Angalau hata yule mama wa "kekundu" alipumzisha sauti yake wakati huu.

Ni magari machache sana yaliyoanza kupita usawa huu wa barabara, na yalikuwa yamejaa lakini abiria niliosafiri pamoja nao wakawa wanayapanda na kushonana hivyo hivyo ili yawaondoe sehemu hiyo upesi. Tukawa tunapungua tu, mpaka nikabaki mimi mwenyewe na dereva na konda.

Haikuonekana kuwa gari lingetengemaa, kwa hiyo wawili hao wakaanza kuondoka pamoja nami, tukitembea kuelekea mbele zaidi na kuomba kukutana na bodaboda maana magari yaliacha kupita; ikionekana labda foleni ile barabarani ilikuwa imekata.

Kweli tukawa tumepata bodaboda moja, na wawili hao wakanishauri nipande na kwenda zangu lakini mimi nikawaambia wapande tu kwa sababu nilitaka kutembea kidogo, na bila shaka ningepata tu bodaboda nyingine. Wakaridhia na kupanda pikipiki hiyo pamoja, fyuu wakaishia. Nilidhani ingekuwa rahisi tu kutoka ndani ya eneo hilo lakini muda si muda nikatambua kuwa nilikosea.

Njia hii tuliyopita haikuwa rasmi, si kama barabara rasmi za changarawe, na kwa kuwa huko mbele haikuja bodaboda nyingine tena, nikajikuta nimeachwa peke yangu eneo lililoonekana kuwa kama linaelekea kwa Mzee Tambitambi. Mh? Hapana. Kuwa mwanaume na mengi hakukumaanisha nifanye tu vitu bila kujali hali yangu nzuri, kwamba niende mbele tu kwa ujasiri na kujikuta nimeingia nisikokujua, hivyo kwa busara nikaamua kurudi kule nilikotoka.

Nikaenda tena mpaka pale ambapo tuliiacha Costa ile, nami nikajiketisha kwenye nyasi safi na laini chini ya mti wenye kivuli kizuri. Ilionekana kama vile siku hii niliamuliwa maana hakuna usafiri mwingine wowote uliopita tena upande huo. Dakika zikawa saa, saa zikawa masaa, na mchana ukaanza kugeuka kuwa jioni.

Nikajiuliza hii ilikuwa ni adhabu gani ya ghafla namna hii. Yaani from nowhere tu eti magari na pikipiki zikaacha kupita ndani ya eneo nisilofahamu vizuri, na hakuna hata nafsi moja iliyoonekana. Hapa pasingeendelea kukalika maana saa moja ilikuwa inaingia, hivyo wazo la kurudi na barabara tuliyokuja nayo kwa Costa likawa suluhisho zuri kwa wakati huu. Ningehitaji tu kufika eneo lenye makazi kiasi na kutokea hapo ningejua nini la kufanya kupata usafiri mwingine.

Taratibu nikaanza kutembea, begi likiwa mgongoni kwangu, simu ikiwa sikioni kuniruhusu nizungumze na msela wangu mmoja, ambaye alinicheka kwa kusema nimelaaniwa kukutwa na saibu hili, na bila shaka ningekutana na Basilisa huko mbele kwa hiyo eti angeandaa masufuria ya kuchemshia uji wa msiba wangu huko nilikotoka!

Nikiwa bado nasonga taratibu, sauti ya kuunguruma kwa pikipiki kutokea nyuma yangu ikanifanya nigeuke kuitazama, nami nikaingiwa na matumaini. Ilikuja upande wangu kutokea eneo hilo nilikoiacha ile Costa, nami nikaipungia mkono ili mwendeshaji asimame, lakini nikashangaa ananipita tu na kunyoosha mbele. Khh!

Nikatoa begi mgongoni na kusimama hapo. Giza lilikuwa limeshaingia kiasi, nami nilihisi njaa, na kwa kutazama taa za jiji mbele zaidi nikajiamulia kutakiwa kusonga tu ili nifikie sehemu yenye shughuli maana bahati nyingine isingekuja. Lakini Mungu si Athumani bwana, gari lingine dogo likaonekana likija kutokea huko nilikopaacha, nami nikapunga mkono lisimame lakini nalo likanipita tu. Kweli Mungu siyo Athumani!

Hali hii ikaniudhi, lakini nikaelewa vizuri upande wa pili wa mambo. Kikawaida, sehemu kama niliyokuwepo ilionekana kuwa na uhatari, labda wa vibaka, ukitegemea pia na muda, hivyo watu wasingekuwa wenye urafiki sana kwa mtu wasiyemjua na kusimamisha tu vyombo vyao kumsaidia; maana hofu ya kupatwa na madhara ilikuwepo kwa wote. Kwa hiyo ikanibidi nifikirie njia mbadala ya kujiondoa sehemu hii haraka kwa usafiri kabla usiku haujawa mzito zaidi.

Nilipopiga tu hatua zingine chache huku begi langu nikilining'iniza mkononi, gari lingine likasikika likija kutokea nyuma yangu. Sikugeuka. Nikaanza kutembea kwa kuyumba kiasi, kama mlevi, kisha nikaliangusha begi chini na kujishika kifuani, nikianza kuguna kwa sauti ya juu na kujiingiza barabarani kwa njia iliyoonyesha nakaribia kuanguka. Haya yalikuwa maigizo tu, na kama sikuwa nimeweka hili wazi mwanzoni, unapaswa kujua kwamba nina utundu fulani pia. Wengine huuita uhuni. Ila nilikuwa mhuni ilipohitajika tu.

Nilikuwa makini kutambua umbali ambao gari hilo lilifikia, na sasa likiwa karibu zaidi na nilipokuwa, nikajiangusha barabarani huku nikilinyooshea mkono lisimame maana nilikuwa na tatizo la kifua. Maigizo tu! Ikiwa aliyekuwa ndani ya gari hilo alikuwa na moyo mzuri, basi angenionea huruma na kushuka kuja kunipa msaada, hivyo ningeweza kupata lifti kwa wepesi. Akili mtu wangu!

Jaribio langu likazaa matunda mazuri pale gari hilo liliposimama, nami nikajisemea "Yes!" na kisha kuendelea kulia kwa maumivu makali chini hapo. Sikufumbua macho yangu na kuendelea kuigiza tu, nami nikasikia mlango ukibamizwa kidogo, kuashiria umefungwa baada ya kufunguliwa. Nikafungua jicho moja kiduchu na kuona kwamba kuna mtu alikuja upesi, nami nikafumba tena na kuendelea kulia.

"Oooh... aaah!"

Nikahisi shingo yangu ikishikwa kwa viganja na kunyanyuliwa kiasi ili kichwa changu kiwe juu, na sijui ni nini tu kilichofanya nisikazie fikira sana suala hili lakini mikono hiyo ilikuwa laini, na harufu ilikuwa nzuri sana.

"Kaka... nini tatizo?"

Sauti hiyo nyororo ikanifanya nifumbue macho yangu na kumtazama aliyeitoa, na kwa sekunde chache nikajisahau kwamba nilikuwa naumwa. Nilimtazama mwanamke huyo usoni kwa ufupi tu, lakini nilihisi ni kama nimemwangalia kwa muda mrefu. Alikuwa na sura nzuri. Mweupe, yaani mweupe. Mtu mzima kunipita hadi mimi kiumri, lakini kama angeamua kudanganya yeyote yule kwa kusema ana umri mdogo, hata mimi ningekubali.

Alikuwa na macho mazuri ya ufilipino fulani hivi na ya kungu kiasi, midomo laini na mizuri, na nywele zake zilikuwa zake, ndefu kufikia mabegani ambazo bila shaka alizilainisha zaidi kwa dawa. Uso wake mweupe wenye kujali sana ulionyesha huruma nyingi kunielekea, naye alikuwa anatumia kiganja kimoja kupima joto la mwili wangu kwa kukiweka kwenye shingo na paji la uso wangu.

Nikafumba macho yangu tena na kuendelea ku "Oooh... nakufaaa..." naye akanishika usoni kwa kiganja chake.

"Kaka... nini kinakusumbua?" akauliza hivyo.

Sauti yake ilikuwa tamu sana, kama ya mtoto mdogo vile ama ile ya Wema Sepetu anayobania puani.

"Aah... kifua dada... kifua kimekaza..." nikatoa lawama zangu.

"Pole sana. Naomba ujitahidi kusimama nikuingize kwenye gari tukatafute hospitali, hapo mbele tu, eti?" akaniambia.

Nikalibana tabasamu langu na kusema, "Sawa."

Kisha nikaanza kujinyanyua, naye akanipa egamio na kutembea nami mpaka upande wa mlango wa pili wa gari lake. Gari lake lilinishangaza kiasi. Ilikuwa ni zile pickup Toyota za zamani kweli ingawa ilikuwa safi, nyeupe, lakini haikuonekana kuwa gari iliyomfaa mwanamke mwenye uzuri wake. Kwa vyovyote vile hilo halingejalisha kwa kuwa sasa nilipata lifti.

Nikakalishwa siti ya upande wa mbele pembeni ya usukani, kisha mwanamke huyo akaniacha na kuelekea pale aliponitoa. Nikamwangalia na kuona akiliokota begi langu na kuanza kuja nalo upesi kwenye gari, naye akaingia pia kwenye usukani na kuliweka kwenye siti za nyuma. Akaingiza gia na kukanyaga mafuta, nalo gari likaanza kutembea tena huku bado nikiwa nimekaza sura na kuonyesha nina maumivu sana.

"Pole kaka. Una... unakaa wapi... umetokea wapi?" akauliza.

"Nilikuwa... natokea Bamaga kule..."

"Sinza?"

"Ndiyo... usafiri ukaharibikia hapo nyuma... ndiyo nikabaki mwenyewe mpaka oooOOH!" nikaendelea kujikata na wembe bandia.

"Pole... ngoja nikuwahishe hospitali ya karibu," akasema hivyo.

Nikafumbua jicho moja na kumtazama kwa chini, na alikuwa makini kweli kwenye uendeshaji akionekana kutaka kuharakisha kututoa huku. Nikaangalia upande wa nje na kutabasamu tu, kisha maigizo yakaendelea hadi tulipoanza kuzipita nyumba zile zilizokaribiana. Nikaelewa haingechukua muda mrefu kufikia barabara kuu, nami nikamtazama mwanamke huyo tena.

Isingekuwa ya mazingira tuliyokutana kuwa jinsi yalivyokuwa, basi angefaa sana kuwa rafiki mzuri. Alionekana kuwa mwenye kujali, nami nikawaza kuwa bila shaka angekuwa na watoto aliowatendea vizuri mno. Lakini kwa upande mwingine, kufanya naye urafiki ingekuwa ni jambo gumu maana tayari nilimdanganya kuumwa ili tu nitimize haja yangu ya kutoka eneo lile, kwa hiyo ningepaswa kuhakikisha namkimbia kwa spidi zote akishanifikisha huko mbele.

Kweli dakika si nyingi tukawa tumeingia barabara kuu za lami, naye akaonekana kupita kwenye njia ambayo ingetufikisha kwenye moja ya hospitali kwenye maeneo ya Buguruni. Nikiwa sitaki hilo kitokee, nikaanza kumpiga-piga taratibu kwenye mkono wake, naye akanitazama huku bado akiendesha.

"Nishushe dada..." nikamwambia hivyo huku bado nikiwa nimekunja sura.

"Wapi?" akauliza.

"Hapo tu hivi..."

"Lakini hali yako ni mbaya... unatakiwa kufika hospitalini kwanza..." akaongea kwa kujali.

"Hhh... nishushe... nahitaji hewa kidogo..."

"Upepo si unaingia vizuri hapo?"

Nikamtazama kwa konyezo na kuona jinsi alivyokuwa makini, nami nikasema, "Na juice..."

"Juice?"

"Ndiyo... huwa inatuliza moyo..."

"Ni... moyo au kifua?"

"Ah... vyote! Ooooh!" nikaendeleza uwongo wangu.

Akaonekana kujali zaidi hali yangu, naye akalipeleka gari sehemu ya kuegeshea barabarani ambako hakukuwa mbali na viduka vidogo vya bidhaa. Kwa upande aliosimamisha gari, ule wa pili ulikuwa na majengo ya makao makuu ya kampuni ya Azam, na magari mengi ya abiria yalipita na kusimama kushusha na kupakia abiria.

Mwanamke huyu akataka kushuka ili aende kunifatia juice lakini akashangaa baada ya mimi kuufungua mlango wa upande nilioketi na kutoka ndani ya gari. Akabaki kuniangalia mpaka nilipofungua mlango wa nyuma na kulitoa begi langu, kisha nikaufunga na kusogea hapo mbele; nikiinama kiasi kumchungulia.

"Asante sana dada. Mungu akubarikiii!" nikamwambia hivyo huku nikitabasamu.

Alikunja uso wake kimaswali kiasi, naye akasema, "Wewe... uko... uko..."

"Niko sawa," nikamalizia maneno yake.

"Kifua hakiumi tena?"

"Kimeacha sasa hivi tu. Niko poa kabisa. Endelea tu na safari dada na Mungu atakulipa kwa ukarimu wako. Mmmwah!" nikamwambia hivyo na kumrushia busu kwa kiganja.

Alionekana kushangazwa sana na hili, naye akaangalia pembeni kiasi na kusema, "Ulikuwa unadanganya."

"Oh... siyo kudanganya yaani... ni... ile ilikuwa ni njia ya kukuomba msaada maana hakuna aliyetaka kunisaidia hata lifti tu. Ila wewe una moyo mzuri sana dada yangu, yaani hadi ukanipima na joto... hahahah... msaada mdogo tu lakini nimefarijika sana. Utabarikiwa milele," nikamwambia kwa shauku.

"Kwa hiyo... umenipotezea muda wangu, nafikiri unaumwa kumbe..."

"Ona ninaweza kukulipa kama unataka," nikamkatisha.

"Nini?"

Nikatoa wallet yangu na kuchomoa pesa, kisha nikamnyooshea huku nikisema, "Time is money. Pole kwa kuchelewesha ulikokuwa unaenda ila chukulia hii buku mbili kama nauli ya kunibeba kulipia huo muda, mm? Shika."

Akanikazia macho yake na kuniuliza kwa sauti ya chini, "We' ni mjinga?"

"Aaa, usiwe hivyo sister. Huku ni kusaidiana tu. Eh? Nimesema asante na pole hii hapa nakupa. Chukua. Ama niendelee kuigiza nimenigwa kidogo? Eerrgh hahahah..." nikamwambia hayo na kumtania kidogo.

Akaniangalia kwa kutoamini fulani hivi, kisha akakanyaga mafuta na kuliondoa gari bila kuichukua elfu mbili niliyotaka kumpatia.

Nikaendelea kulisindikiza gari lake kwa macho, nami nikashusha pumzi na kusema kwa sauti ya chini, "Asante."

Aliistahili asante hiyo ingawa hangeisikia wala kuijali tena kwa sababu nilikuwa nimemkosea. Nikatoa kitambaa changu safi na kuanza kujifuta hapa na pale kwenye suruali yangu nyeusi ya kardet, iliyochafuka kiasi kutokana na kujilaza chini nilipomfanyia maigizo mwanamke huyo. Nikaangalia saa yangu kwenye simu na kukuta ni saa mbili kasoro sasa, nami nikasimama sehemu ambayo ingeleta daladala za kuelekea kule nilikodhamiria kufika kwa siku hiyo.

Daladala ikaja, nami nikapanda kwa kusimama pamoja na abiria wengine ambao kama kawaida wangenitazama mara kwa mara kuonyesha nilikuwa mtu mwenye utofauti fulani kutokana na sura yangu. Vuuu... gari likapita eneo moja baada ya lingine huku nikiwa nimebanwa kiasi na watu niliosimama pamoja nao, na hatimaye tukafika maeneo ya Rangi Tatu, huko Mbagala, nami nikashuka hapo.

Kwa jiji letu kufanya matembezi sehemu mbalimbali kipindi cha nyuma kulifanya niyajue maeneo mengi, lakini Mbagala ndiyo kati ya maeneo ambayo sikuwa na mazoea nayo kabisa. Hata safari hii fupi kutokea kule nilikoishi ilinibidi niwe nimefanya utafiti wa jinsi ya kufika huku, kwa sababu kuna sehemu hususa niliyokuwa nikielekea.

Isingekuwa kucheleweshwa kule kwa usafiri niliochukua mara ya kwanza basi ningewahi kufika nilikohitaji kufikia, kwa hiyo baada tu ya kushuka nikatafuta daladala nyingine ambayo ingenipeleka kwenye eneo la mbele zaidi lililojulikana kama Mzinga.

Mapema nikapanda gari za Toangoma na mwendo ukaanza. Sikuzote nilifurahia hali fulani ya ugeni nilipoingia kwenye maeneo ambayo sikuyafahamu vizuri, kwa hiyo nilikuwa makini kutazama mambo mengi ya maeneo haya. Hakukuwa na purukushani nzito kama maeneo ya Kariakoo ama maghorofa mengi na vitu maridadi mno, bali mwonekano wa hali ya kawaida ulioitofautisha Mbagala na maeneo mengine yaliyofanisika zaidi.

Dakika kama kumi tu nasi tukawa tumefika Mzinga, nami nikashuka pamoja na wale walioshukia hapo. Bila hata kusumbuka, bodaboda zikanikimbilia, nami nikachagua moja na kumpa maelekezo dereva anipeleke sehemu iliyojulikana kama Masai. Nikapanda, mwendo ukaanza.

Nadhani ni ugeni wa mtu kama mimi kwenye eneo hilo uliofanya wengi wa watu tuliowaopita wanikodolee sana, na upesi nikatambua kwamba vijora ndiyo vazi lililopendelewa zaidi na wanawake wa huko. Nilikuwa makini kukariri njia tuliyotumia kupita mpaka kufika Masai, ingawa ilikuwa giza. Hiyo Masai ilikuwa ni bar pana kiasi yenye ghorofa moja juu na vyumba vya wageni. Tayari kwa muda huu wa saa mbili palikuwa pameshachangamka, muziki ukiwa mnene, na wengi wa waliokuwemo kule ndani waliniangalia sana baada ya kuniona.

Nikamlipa boda, naye akatoweka. Nafikiri wengi walikuwa wanasubiri kuona nikienda pale aidha kunywa ama kuchukua chumba cha kupumzikia kutokana na kuwa sura mpya kwenye eneo lao na kubeba begi mgongoni. Lakini Masai haikuwa shabaha yangu. Nikasogea pembeni na kutoa simu, nami nikatazama ramani ndogo ya nyumba iliyokuwa karibu eneo la bar hii. Nilikuwa na mpango wa kufikia kwenye nyumba hiyo ambayo mwenye nayo alikuwa ametoa tangazo siku chache nyuma kuwa angepangisha mtu hapo.

Ilikuwa ni sehemu sahihi kwangu kutaka kufikia kwa sababu nilitaka mazingira mazuri ya unyumbani, siyo chumba cha kupanga, bali kama alivyoonyesha kwa tangazo lake nililoliona mtandaoni, ilikuwa ni sehemu ya kukaa kama nyumbani. Yaani, kungekuwa na sebule yenye vitu kama samani na makochi tayari, chumba chenye kitanda, bafu, choo, maji, umeme, mambo kama hayo. Na gharama yake ilikuwa nafuu kwa kila mwezi.

Tayari nilikuwa nimeshawasiliana na mwenye kutoa huduma hiyo kwa njia ya WhatsApp na kukubaliana naye kwamba ningekuja hapo siku si nyingi ili asije kumpa mteja mwingine nafasi hii niliyoitaka mimi, naye akawa ameridhia. Kwa hiyo baada ya kuona uelekeo ambao nyumba hiyo ilikuwa, nikaanza kuelekea huko taratibu.

Mtaa huo kwa usiku ulionekana kuwa kimya kiasi, na nyumba nilizozipita zilikuwa za kawaida sana, vijia vyenye uchochoro mwingi, yaani mwonekano sahihi wa uswahilini. Kidoti chekundu cha ramani kikanifikisha mbele ya nyumba hiyo, nami nikaiangalia kwa umakini.

Kutokea nje, ingeweza kuonekana kuwa kubwa kiasi, ikiwa imezungushiwa kuta iliyoitenganisha na nyumba nyingine pembeni lakini kwa ukaribu sana. Geti lilikuwa pana na jeusi. Ningeweza kuona madirisha mapana yaliyowekewa vioo vyeusi, ungo wa king'amuzi cha Azam huko juu, na taa nene ya nje iliyomulika vyema mpaka kufikia niliposimama. Bila shaka palikuwa ndiyo penyewe.

Kupiga jicho upande mwingine wa nyumba za waswahili, nikaona wanawake kadhaa wakiwa wamesimama, wengi wao wakijifunga mikhanga tu kuanzia kifuani, wakiniangalia kama hawanijui. Ah kweli walikuwa hawanijui.

Hivyo nikaenda zangu mpaka kwenye geti hilo na kuligonga kwa wepesi kiasi, nami nikabaki kusubiri. Sikuwa nimeona haja ya kumtafuta mwenye nyumba kwa simu tena maana alisema kuwa muda wowote ule ambao nilijisikia kufika kwenye nyumba hiyo basi ningeenda tu, na ndiyo muda wenyewe ukawa huu. Sauti ya kifungulio kidogo cha mlango wa geti ikasikika baada ya sekunde chache, nao ukafunguka.

Mbele yangu alisimama mwanamke mtu mzima vya kutosha kunizaa, labda hata mara mbili. Umri wake kwa kukadiria ungekuwa wa miaka 50 ya mwishoni na kuendelea, naye alikuwa na ufupi wa kadiri, mnene kiasi, mwenye ngozi yenye weupe uliofifia, na macho yake mazuri yalinitazama kwa umakini.

"Mama shikamoo..." nikampa salamu kwa heshima.

"Marahaba. Hujambo?" akaniitikia.

"Sijambo," nikamwambia.

Alinitazama kwa umakini sana, akiwa kama ananitafakari, nami nikawaza kwamba huenda ndiye aliyekuwa mwenye nyumba, hivyo ingenibidi nimweleze mimi ni nani.

"Pole kwa kuwa nimefika usiku mama, gari niliyokuja nayo iliharibikia njiani. Mimi ni...."

"Ndiyo wewe kumbe?" akanikatisha kwa kuniuliza hivyo.

Kwa kufikiri anamaanisha kile nilichowaza, nikamwambia, "Ndiyo mama, ni mimi."

Akanishusha na kunipandisha huku akitabasamu kiasi, nami nikatabasamu pia kirafiki.

"Umekuja mwenyewe?" akaniuliza.

Sauti yake ilikuwa yenye upole mwingi sana, nami nikasema, "Ndiyo, niko mwenyewe. Gari lisingeharibika nisingechelewa kufika, ila hata hivyo haukujua kama ningefika leo japo nilipanga kufika mapema."

"Ahah, hamna shida baba, nilijua unakuja. Sema... karibu ndani kwanza. Jamani! Utakuwa umechoka kweli..." akasema hayo huku akinipisha ili nipite.

Mh? Sikutarajia angefahamu kwamba nilikuwa nakuja leo lakini njia yake ya kunikaribisha ilikuwa nzuri sana, nami nikaingia tu na kusogea mbele kidogo. Akafunga mlango wa geti na kusogea usawa wangu.

"Pole baba jamani... karibu sana. Twende ndani upumzike kidogo," akaniambia.

"Asante," nikashukuru.

Akaniongoza kufikia ubaraza uliojengewa vigae sakafuni, nami nikaona viatu kadhaa chini hapo kunifanya nitambue kuwa huko ndani kulikuwa na watu wengine zaidi. Labda wengine wa familia yake ambao waliishi naye, na mimi ndiyo ningeongeza idadi kwa kuja kukaa hapo. Yote yalikuwa sawa kwangu, nasi tukaingia ndani ya nyumba hiyo pamoja. Alinisihi niingie na viatu tu nilipoashiria kutaka kuvivua, na baada ya kufika sebuleni akanikaribisha nikae kwenye sofa moja.

Sebule haikuwa pana sana lakini ilikuwa pana. Masofa yalikuwa matatu na marefu yaliyopangwa kwa njia ya ukuta uliozunguka meza ya duara yenye kioo cheusi na kizito hapo katikati. Sofa nililoketi lilinitazamisha moja kwa moja na TV ndogo tu ya flat screen ukutani, na juu kiyoyozi kilionekana kuzunguka na kuipa sebule ubaridi ulioleta ahueni kutokana na joto la jiji hili.

Upande wa nyuma wa sofa nililokalia kulikuwa na sehemu pana iliyokuwa ya lengo la kulia vyakula (dining), na hapo niliona meza ndefu kiasi ya mbao, iliyozungukwa na viti sita vilivyoibana kwa ukaribu. Pembeni na hapo kulikuwa na friji yenye urefu wa kadiri na yenye rangi ya njano, pamoja na sehemu yenye uwazi wa mlango usiokuwa na mlango, ambao ulionyesha uelekeo wa kwenda chumba cha jikoni kutokea hapo 'dining.' Kampangilio kalikuwa kazuri kweli, na safi sana.

Kwenye sofa la upande wa kulia alilala binti mwenye umri mkubwa kufikia miaka 20 hivi, akiwa makini tu kutazama runinga bila kujali kwamba kuna mgeni aliingia. Alivaa dera lililousitiri vyema mwili wake, na kwa kumwangalia haraka nikatambua alikuwa mweupe na mwenye sura nzuri. Alitulia kivyake tu akitazama tamthilia huku aking'atang'ata kucha moja ya kidole chake kiganjani.

Mwanamke yule aliyenikaribisha akasimama pembeni yangu na kusema, "Karibu sana baba'angu."

"Asante mama," nikamwambia.

"Ngoja nikuletee kitu cha kupoza koo kwanza, eti?" akaniambia.

Nikatabasamu na kusema, "Asante sana."

Angekuwa amefanya jambo la maana kwa kuwa sikuweka chochote kile tumboni tokea nilipokunywa chai asubuhi, kwa hiyo kama ni juice angeileta tu nami ningeishusha vizuri sana. Akaondoka na kwenda upande ulioonekana kuelekea jikoni, nami nikakaa kwa utulivu na kumtazama binti yule pembeni. Alionekana kutojali kabisa wageni, nami nikawaza huenda alikuwa mwenye nyodo kupita maelezo.

Sekunde chache kupita na mwanamke yule akawa amerejea tena, isipokuwa wakati huu akawa amekuja pamoja na mwanamke mwingine aliyeonekana kumzidi mpaka na yeye kiumri kiasi. Huyu hakuwa mweupe, bali mweusi wa maji ya kunde, naye alikuwa na nywele fupi zenye mvi kiasi kichwani kwake.

Yule aliyenipokea mara ya kwanza alibeba sinia lenye glasi iliyowekewa juice, bila shaka ya parachichi, pamoja na sahani yenye wali na nyama iliyoonekana kuungwa vizuri sana kutokana na namna ilivyonukia. Yaani vilitamanisha sana, na kwa njaa niliyohisi ningekula mpaka kusafisha sahani yote. Ni kama alijua!

Sikutegemea mapokezi yangu kwa hapo yangekuwa mazuri namna hiyo kutoka kwa watu wazima kama hao, lakini lilikuwa ni jambo la kawaida kwangu mimi kutendewa kwa njia nzuri na watu wengi. Siyo wote, ila wengi. Kwa hiyo sinia hilo likawekwa mezani, nayo ikavutwa mpaka kuifikia miguu yangu, na wanawake hao wakawa wamesimama pembeni huku wakinitazama kwa njia fulani ya... matumaini.

Nikatabasamu kidogo na kusema, "Asanteni sana. Shikamoo mama?"

Nilikuwa nikimsalimu yule mwanamke mwingine, naye akasema, "Marahaba kijana wangu. Karibu sana, jisikie umefika nyumbani."

Nikatikisa kichwa kukubali ukaribisho wake.

"Karibu chakula baba. Pole kwa safari," yule mwanamke mweupe akaniambia.

"Asante."

Kiukweli nilikuwa nimesema asante nyingi sana kwa jioni hiyo, nami nikaanza tu makamuzi taratibu huku wanawake hao wakiwa wamesimama tu na wakiniangalia. Niliona hilo kuwa ajabu kiasi lakini labda hawakuzoea sana ugeni wa wanaume, tena hasa kutokana na mwonekano wangu.

Oh, kwangu mimi sura niliyokuwa nayo ilikuwa kawaida sana, lakini kwa wengine ilikuwa kama vile kigezo fulani cha kuwafanya wanitendee kiyaiyai. Nilitamani kuwaambia watu hawa wazima wakae, lakini tena nikajizuia maana sikuona hilo kuwa adabu kutoka kwa mgeni aliyefika tu na kuanza kujifanya mjuaji. Wafanye vile walivyojisikia.

"Kwa hiyo... haukuja na Shadya?"

Swali hilo lilitoka kwa yule mwanamke mweupe aliyenipokea mwanzoni, nami nikamtazama machoni. Sikuelewa Shadya ilikuwa ni nini, ila nikadhani amemaanisha jina la gari la usafiri kama Mohammed Trans.

"Aa... hapana... sijaja na Shadya. Nilipanda tu daladala, nikaifata ramani ndiyo nikafika. Ni mara yangu ya kwanza," nikawaambia.

Waliangaliana kimaswali kiasi, mimi nisijue sababu, lakini nikaendelea zangu tu kula.

Yule mweusi kiasi akasema, "Tulifikiri ungekuja labda hata na... ndugu zako..."

"Ndugu? Hamna... ni mimi tu mama. Nimekuja kukaa huku peke yangu," nikasema.

"Umekuja... kukaa huku?" akauliza yule mwanamke mweusi.

"Ndiyo. Nafikiri tutaanza kuzungumza kuhusu gharama na kila kitu nimeshaandaa. Nimalize kwanza kula, eh?" nikawaambia.

Yule mweupe akatabasamu kwa furaha na kusema, "Sawa baba. Wewe kula tu. Tutaongea mengi zaidi Miryam akishafika."

Nikakunja uso kimaswali kiasi na kuuliza, "Miryam?"

"Ndiyo. Na yeye amekawia kidogo tu, ila amesema yuko karibu kufika," mwanamke mweupe akaniambia.

Nikaangalia pembeni kiufupi, nikiwa sijaelewa vizuri jambo hilo, na yule mwanamke mweusi alinitazama kwa umakini zaidi tofauti na yule mweupe ambaye aliniangalia kwa furaha zaidi.

"Miryam ndiyo... mwenye nyumba?" nikawauliza.

Wakaangaliana machoni kwa njia ya kuulizana jambo fulani, kisha wakanitazama tena na yule mwanamke mweusi akasema, "Eee... ndiyo... Miryam ndiyo... ndiyo mwenye nyumba."

"Mmmm... sawa basi, haina shida. Nitamsubiri ili tupangane vizuri. Nimepapenda sana hapa," nikawaambia hivyo.

Nikakirudia chakula changu na kuendelea kushuka nacho taratibu, nami nikamwona mwanamke yule mweusi akimpa kiashirio mwenzake kwa kumvuta ili waondoke hapo. Nikawaangalia, naye akasema wanaenda kuandaa mambo fulani kisha wangerudi tena, na mimi ningekuwa nani kuwazuia? Nikasema sawa, nao wakaishia kwenye kona upande mwingine ndani hapo.

Nikaendelea kula na kumwangalia binti yule tena, na bado alikuwa anatafuna tu kucha. Nilipomwangalia vizuri zaidi nikaanza kuona kwamba hali yake haikuwa sawa kwa asilimia zote, lakini nisingeweza kukisia haraka ikiwa alikuwa na tatizo fulani. Macho yake yaliielekea TV, lakini ni kama umakini wake haukuwa kwenye kile kilichoonyeshwa humo.

Nikataka nimsemeshe, lakini ndiyo hapa nikaanza kusikia maongezi baina ya wale wanawake wawili walioondoka muda mfupi nyuma. Nikatambua hawakuwa wameenda chumbani kabisa, bali walisimama nyuma ya ukuta uliowaficha kutokea hapo sebuleni.

Sauti ya chini ya mwanamke yule mweupe ikasikika ikisema, "Dada jamani, huyo kaka ni mzuri! Eh! Sijawahi kuona."

Sauti ya mwenzake ikasema, "Mbona kama mdogo sana?"

"Kinachofanya ufikiri ni mdogo nini?"

"We' humwoni? Anaonekana hadi kutakiwa kumwamkia Mimi."

"Mh? Hamna bwana. Halafu kwani kuna ubaya gani? Sema ni kasura kake tu ndiyo kanamfanya anaonekana mdogo, lakini hata Shadya alisema ni mkubwa. Sidhani kama alikosea. Mimi nimempenda sana jamani..."

"Ndiyo, ni mzuri ila, mbona kama haelewi-elewi mambo? Tunamuuliza hiki, yeye anajibu vingine, kama anavuta sijui..."

"Atakuwa amechoka tu, halafu anaonekana ana njaa, hajala muda huyo..."

"Lakini..."

"Acha hizo bwana. Kijana wetu amechoka tu, tumsubiri Miryam mengine tutajua. Dada nina furaha SANA!"

Mh? Hayo yote niliyasikia, nami sikuweza kuelewa kabisa maongezi hayo mafupi yalilenga suala gani haswa. Kulikuwa na ishu gani nyingine zaidi ya mimi kuja kupangishwa kwenye nyumba hii iliyomfanya mmoja wa wanawake hao afikiri kuwa sielewi mambo, ama navuta bangi? Shadya ndiyo alikuwa nani badala ya nini?

Ningehitaji kujua undani wa mambo hayo ili nisije kujikuta nadumbukia kwenye masuala mengine kabisa tofauti na yaliyonileta huku, na wao kuanza kuja tena kukanifanya nijiandae kuzungumza nao kwa kina kuhusu makazi yangu ya muda mfupi kwenye nyumba hii. Nilitaka kujua ningelala kwenye chumba kipi ndani hapo, na mambo ya kawaida ambayo ningeshiriki kufanya kama mwanajamii mpya katika eneo hilo. Basi.

Waliponifikia tena, walikuwa wakitabasamu tu, bila kujua kwamba mengi ya yale waliyozungumzia niliyasikia, nami pia nikatabasamu na kuigiza kutojua lolote. Tayari nilikuwa nimefuta wali wote na nyama, ikibaki tu juice ya kuendelea kushushia.

"Asanteni sana jamani," nikawaasante tena.

"Nikuongezee ubwabwa?" yule mwanamke mweupe akaniuliza huku akija kuchukua sahani.

"A... hapana. Nimeshiba. Asante..."

Asante nyingine tena? Nikaanza kuhisi naboa.

"Napenda kujua vitu vya kawaida, yaani shughuli za kawaida zifanyikazo hapa. Mmesema napaswa kusubiri mpaka Mariam aje ndiyo tuzungumze?" nikauliza.

"Abee..."

Hilo lilikuwa ni itikio kutoka kwa yule binti aliyelala kwenye sofa, nami nikageuka na kumtazama. Alikuwa ananiangalia sasa. Macho yake yakiwa na ukavu fulani hivi, ilikuwa kama vile sura yake si ngeni sana kwangu, ijapokuwa nilijua kabisa kwamba hii ndiyo ilikuwa mara ya kwanza kukutana naye. Sikujua alikuwa ameitikia mwito kutoka kwa nani, lakini kuniangalia vile kukafanya nijue alidhani mimi ndiyo nimemwita.

"Hajakuita, endelea kuangalia sinema mama, eh?" yule mwanamke mweupe akamwambia hivyo binti, naye akaitazama TV tena.

Jambo hili lilinishangaza kiasi. Nikawatazama wanawake wale, wote wakiwa wamesimama, nami nikauliza, "Kwa nini anafikiri nimemwita?"

Mweupe akajibu kwa kuniambia, "Ulikuwa unataka kusema Miryam, jina la dada yake, ila ukasema hilo ulilolisema, ndiyo la kwake. Aka... akadhani umemwita."

Njia yake ya kuwasilisha taarifa hiyo kwangu ilikuwa kama vile hataki kuendelea kuzungumzia zaidi suala la binti huyo aliyelala kwenye sofa, naye akaondoka pamoja na sahani ile bila shaka kuirudisha jikoni. Nikamwangalia yule mwanamke mweusi, naye akaketi kwenye sofa la upande wa kushoto huku akiniangalia pia. Alionekana kuwa mtu makini, labda mkali kiasi pia, nami nikaendelea kuweka utulivu tu wa kiume.

"Hawajambo nyumbani?" akanisemesha.

Nikamwangalia na kutabasamu kiasi, nami nikasema, "Wazima kabisa. Sijui hapa?"

"Tunaendelea vizuri. Mungu anasaidia. Angalau mara moja moja tukipata wageni kama hivi... ni baraka," akaniambia.

Nilikuwa na kawaida ya kusugua magoti yangu kwa viganja taratibu hasa nilipozungumza na mtu niliyemheshimu sana, na wakati huu nikawa nikifanya hivyo, nami nikamwambia, "Ndiyo wageni huwa ni baraka. Hata sisi kule kwetu... angalau mgeni akifika tunafurahi maana mahanjumati na nyama ndiyo hupikwa kwa sana."

Kauli niliyotoa ikamfanya mwanamke huyo acheke, na yule mwanamke mweupe ndiyo alikuwa anarudi, naye akawa anacheka pia kuonyesha kwamba alinisikia.

Akakaa pembeni ya mwenzake na kusema, "Unasema kweli, maana siku hizi kila kitu ni mfumuko wa bei tu. Wengi kugusa nyama ni mara moja moja sana."

"Wee! Umeona?" nikamwambia hivyo, nasi kwa pamoja tukacheka kidogo.

"Napenda unavyoongea. Wewe ni kabila gani?" yule mwanamke mweusi akaniuliza.

"Ningesema mimi ni msukuma kwa upande wa mama, ila wa baba ni mpemba. Sivijui hivyo vikabila lakini, maana tupo kimjini-mjini zaidi..."

Nikawaambia hivyo, nao wakacheka kidogo.

"Ndiyo hivyo. Sisi ni wa Mwanza huko, ila hapa jijini ndiyo tumezamia kwa kipindi kirefu zaidi," nikawafahamisha.

"Hata sisi tumekaa huku muda mrefu pia. Sisi ni warangi, baba yao kina Miryam alikuwa mpemba pia kama wewe tu..." mwanamke mweupe akaniambia.

"Aaa kumbe..."

"Ndiyo. Tulikaa Tanga sana, then baadaye jiji likatuita. Ndiyo tuko na binti yetu hapa, tumemtunza-tunza na yeye sasa hivi anatutunza-tunza ahahah... Miryam amekua, na amekuwa mwanamke mzuri sana. Ana bidii, anatujali, anachapa kazi, ni mtu mmoja mpambanaji yaani kila mtu anampenda," mwanamke huyo akaniambia.

Nikatikisa kichwa kuonyesha uelewa, lakini nikijiuliza kwa nini angefikiria habari za huyo Miryam zingekuwa na umuhimu sana kwangu. Ila kwa kuwa nilijua kuna jambo lingine lililokuwa linaendelea lililomhusisha huyo mwenye nyumba, nikaona niulize tu.

"Kwa hiyo... Miryam ni mtoto wako?"

Wanawake hao wakaangaliana kimaswali kiasi, kisha wakanitazama kama vile hawakunielewa vizuri, na mimi singeweza kujua sababu ya kupewa itikio hilo.

Mwanamke yule mweusi akaniuliza, "Kwani mliongea nini na Shadya? Hakukuelezea mengi sana, au?"

Shadya ndiyo alikuwa nani? Dalali wa nyumba au? Mimi nilipata tu tangazo mtandaoni mpaka kufika hapa. Kiukweli hali hii ikaanza kunichanganya sasa. Nikashindwa kujua nitoe jibu lipi au niulize kipi kingine, na wanawake hao wakiwa bado wananitazama, sauti ya honi ya gari ikasikika kutokea nje ya geti, nami nilipowaangalia nikaona wakitabasamu kwa furaha.

Mweupe akaniangalia na kusema, "Amefika. Ngoja nikamfungulie."

Bila shaka alikuwa akimaanisha kwamba mwenye nyumba huyo, Miryam, ndiyo alikuwa amefika, naye akanyanyuka na kunipita kuelekea nje ili kufungua geti.

Nikaendelea kukaa kwa utulivu tu, bado nikiwa najiuliza kama kuna sehemu fulani akina mama hawa walijichanganya katika maongezi yao, ama labda mimi, na kwa nini mtu mzima kama mwanamke huyo mweupe ndiyo anyanyuke kwenda kufungua geti badala ya binti kijana aliyelala tu kwenye sofa hapo hapo. Ila mi' ningejua nini? Maisha yao yalikuwa yao.

Geti likasikika likifunguliwa, muungurumo wa gari ukaingia zaidi kuikaribia nyumba, kisha ukakata na geti likafungwa tena. Mwanamke yule aliyebaki akanisihi niendelee kunywa juice yangu kabla haijashuka kiwango cha ubaridi iliyokuwa nacho, nami nikaichukua glasi na kuanza kunywa tena. Bila shaka pale nje kuna maongezi mafupi yaliyofanywa baina ya mwanamke yule mweupe na mwenye nyumba aliyeingia, labda kumwambia kuhusu ujio wangu, nami nikajiweka tayari ili akifika mikakati zaidi iendeshwe.

Mlango ukafunguka, na wa kwanza kupita akawa ni yule mwanamke aliyenipokea, kisha akaingia mwanamke mwingine kumfatia. Nilikuwa tu ndiyo nimetoka kupiga fundo dogo la juice, na ile nimeshusha glasi na kumtazama mwanamke huyo, macho yangu yakashtuka kiasi kufuatisha na pigo la nguvu moyoni ndani ya kifua changu.

Ilikuwa ni yule mwanamke mweupe niliyekutana naye masaa machache yaliyopita jioni hiyo na kumdanganya kwamba niliumwa kifua ili tu anibebe kwa gari lake, naye baada ya kuwa ameniona, akasimama mlangoni hapo hapo na kuniangalia kwa mkazo sana ulioonyesha hasira kali kunielekea!



★★★★★★★★★

ITAENDELEA

★★★★★★★★★

Full Story WhatsApp or inbox

Whatsapp +255 678 017 280
Okay
 
MIMI NA MIMI

A Story by Elton Tonny

Familia, Urafiki, Mapenzi, Kazi, Tamaa, Hila, Usaliti, Siri, Mambo Ysiyotazamiwa

R-rated 18+

Enjoy!


★★★★★★★★★★★★★

SEHEMU YA TANO

★★★★★★★★★★★★★


Nilishangaa. Alihitaji kunyanyua miguu yake ili aweze kuizungushia vyema mikono yake mgongoni kwangu sababu ya mimi kuwa mrefu, na niliweza kuzihisi vyema sana pumzi zake laini shingoni kwangu. Yaani hata kama ningekuwa nimebarikiwa kuishi kwa karne mia moja, hiki ni kitu ambacho singetarajia kuja kukipata ndani ya muda huo wote.

Kumbatio lake lilikuwa laini, yaani, hakuubana sana mwili wake kwangu, na mimi kutolirudisha upesi ndiyo kulifanya nisiuhisi vyema zaidi mwili wake mbele yangu. Kusudi la yeye kunikumbatia hivi lilikuwa nini?

"Asante."

Neno hilo lilisikika kutoka kwenye kinywa chake nyuma yangu, nami nikajipa tu ujasiri wa kurudisha kumbatio la mwanamke huyu kwa kuubana mwili wake kwa mikono yangu taratibu.

Hata pombe haikuwa imenichanganya sana kunizuia nisielewe shukrani aliyotoa ilihusiana na nini. Alikuwa ananishukuru kwa kumsaidia mdogo wake, yaani Mariam, bila shaka akiwa ameambiwa yote yaliyotokea jioni ya siku iliyotangulia; maana hii ilikuwa mpya sasa.

Kuubana mwili wa mwanamke huyu namna hii kulinipa hisia ya joto lenye kutuliza, siyo mwilini, ila moyoni. Sikuelewa ni kwa nini ila nilihisi amani yenye nguvu sana.

Akaniachia taratibu na kusogea mbele, nami nikawa namwangalia tu machoni. Mpaka kufikia hapo sikuwa nimetilia maanani kuwa alivaa night dress laini na ndefu yenye rangi ya shaba iliyong'aa, ila ndiyo sasa nikawa nimeiona vizuri.

"Haya, usiku mwema. Nenda kalale," akaniambia hivyo huku akijifunika vizuri kwa nguo ya juu ya hiyo night dress.

Kuna kitu kiliniambia kwamba alifanya hivyo akidhani nimelewa sana, kwa hiyo labda nisingekuja kukumbuka namna alivyonikumbatia ama shukrani yake ya moyoni aliyoitoa. Lakini niliithamini mno, na hilo ni jambo ambalo sidhani kama alifikiri nililichukulia kwa uzito.

Nikatazama upande wa mlangoni ambako tayari Tesha alikuwa ameshaingia ndani, nami nikamtazama machoni na kutikisa kichwa kidogo kuonyesha uelewa, kisha nikatoka nje. Sauti za makomeo ya geti kufungwa zilisikika mpaka nilipofika upande wa pili wa ukuta uliotenganisha nyumba zetu, nami nikasimama kumtazama mwanamke huyo kupitia yale matobo ukutani.

Alikuwa anaingiza viatu vya mdogo wake ndani, kisha akafunga geti dogo la mlangoni na mlango pia, akitokomea huko. Nikashusha pumzi kujipa utulivu maana angalau hali ya hapo ilikwenda vyema zaidi ya nilivyotazamia, nami nikaenda mpaka kule ndani ili nikawaangalie wale walimbwende. Sijui walikuwa wameshazimia huko?

Nikaenda mpaka ndani na kumkuta Joy sebuleni, akiwa amekaa kwenye sofa moja huku mkononi akiwa ameshikilia bakuli la plastiki na kijiko. Alionekana kuwa anakunywa mchuzi wa nyama pamoja na kutafuna nyama, nami nikasogea usawa wa meza na kusimama.

"Ankia yuko wapi?" nikamuuliza kwa sauti ya chini.

"Ameingia kulala," akajibu.

"Na wewe?"

"Nilikuwa nakusubiri uje."

"Sawa. Ngoja nikafunge geti kwanza. Sijui hata funguo huwa anaweka wapi..."

"Hapo juu ya mlango," akaniambia.

Nikageuka na kunyoosha mkono wangu mpaka juu ya mlango wa kuingilia, nami nikazichukua funguo.

"Siyo mara yako ya kwanza kuja hapa, eh?" nikamuuliza.

"Hamna, hapa ni nyumbani. Tushalala sana hapa," akaniambia.

Nikafungua tu mlango tena ili niende kule nje kulifunga geti.

"Utakuta nimekuwekea nyama, sawa?" akaniambia hivyo.

"A-ah... usiniwekee. Nikija ni kulala tu," nikamzuia namna hiyo na kisha kutoka nje.

Nikaenda na kuhakikisha nimelifunga vizuri geti letu dogo huko nje, na kiukweli bado pombe ilikuwa inazunguka kichwani lakini nilikuwa naweza kujiongoza vizuri sana. Nikarudi zangu ndani na kuifunga milango pia, na Joy alikuwa amekaa tu kwenye sofa bado huku bakuli akiwa ameshalishusha. Nikaweka funguo juu ya mlango, kisha nikamgeukia.

"Me naenda kulala. Nizime taa, au bado upo?" nikamuuliza.

"Hamna, zima tu. Twende tukalale," akaniambia hivyo na kusimama.

Ka!

"Tukalale wapi?" nikamuuliza.

"Chumbani kwako," akajibu.

"Aa wee... nenda kalale na mwenzako huko. Sitaki bughudhi," nikasema hivyo na kuzima taa.

Nikaanza kutembea na kumpita, lakini akakishika kiuno changu kutokea nyuma na kunifanya nimgeukie.

"JC..."

"Nini?"

"Me nataka tukalale wote," akaongea kwa sauti ya utongozi.

"Kwa nini?"

"Mhh... nakupenda..."

"Eh... Joy, naomba uniachie. Utanipenda siku nyingine, leo hapana," nikamwambia hivyo.

"Nisikilize JC..."

"A-ah..."

Nikaitoa mikono yake kwangu na kumwacha akiwa amesimama hapo, nami nikaenda tu chumbani. Si unajua tu huwa kuna kale kakitu kanakokusukuma ukifate kitanda baada ya kunywa pombe na kupiga usingizi bila kujali chochote? Ndiyo kalikokuwa kameniteka sasa hivi. Nilitaka kulala zaidi ya jambo lingine lolote.

Nikaweka simu yangu chaji, nikavua suruali, saa, T-shirt, na kubaki na boksa tu mwilini, nami nikakaa kwanza kitandani. Kahisia kazuri kanakotokana na kulewa kiasi nilikuwa nakasikilizia, huku nikijishauri sijui nishushe neti, sijui niache? Ah neti kwenda kule! Ningelala hivyo hivyo tu maana mbu wengi walikuwa wamenyamazishwa kwa dawa hata hivyo, kwa hiyo kilichokuwepo ilikuwa ni kuzima tu taa na kulala.

Lakini kabla sijatoka kitandani kwenda ukutani kuizima, mlango ukafunguliwa. Nikaangalia hapo kwa umakini na kumwona Joy anaingia, naye akasimama tu hapo hapo mlangoni huku akinitazama kwa macho yaliyolegezwa na pombe.

"We... funga mlango bana, mbu wanaingia," nikamwambia hivyo.

Akaingia ndani na kuufunga mlango, na sasa nikaweza kumwona vyema zaidi. Wakati huu alikuwa ameshaitoa nguo yake aliyokuwa amevaa, akiwa amebaki na sidiria nyeupe iliyoficha mapacha ya kifua chake, pamoja na nguo nyeupe ya ndani pia mtindo wa kandambili iliyonifanya niyaone mashavu manene kiasi ya mlima wake kwa nyuma.

Akanigeukia na kunitazama kwa ujasiri wa kianamke, naye akaanza kuja mpaka kufikia nilipokaa na kusimama mbele yangu.

"Mbona umeufunga mkono bandeji? Umeumia?" akaniuliza.

"Nilikwambia ufunge mlango, sikukwambia uingie," nikamwambia hivyo.

"Acha mashauzi yako bwana..." akanisemesha kwa nyodo.

"Nani anajishaua?"

Akanishika usoni kwa viganja vyake, lakini nikavikwepa na kuitoa mikono yake karibu nami.

"Mbona unakuwa hivyo?" akaniuliza.

"Ni sehemu ipi ya maneno 'nataka kulala' ambayo huelewi?" nikamuuliza pia.

"Kulala tutalala... me nataka unidinye hata kidogo tu JC..."

"Sitaki, hata kama ni kikubwa. Nataka kulala. Naomba uondoke..."

"Kwa nini unanifanyia hivyo? Kwamba me siyo mzuri sana kama Ankia wako, au?"

"Eee... utajua mwenyewe. Nenda."

"Amekupa nini ambacho mi' siwezi kukupa?"

"Ah aisee!" nikasema hivyo kwa kuchoshwa na hali hii.

Akanishika mapajani na kupiga magoti chini, huku akiniangalia kwa macho yaliyoonyesha hamu nzito, naye akasema, "JC nipe tu hata kidogo. Nina ugwadu mwenzio..."

"Nenda kachukue koleo, uukokoe. Utatoka tu," nikamwambia hivyo.

Akacheka kidogo huku akinipapasa kwa viganja vyake mapajani.

"Una mwili mzuri... huwa unaenda gym?" akauliza kwa madaha.

"Joy nielewe basi..."

"Usinifanyie hivi JC... nipe tu kama kunisaidia. Sitakuomba tena..."

"Kulikuwa na wanaume wengi Masai, ulikosa wa kumwomba akusaidie?"

"Ningeenda kwao, lakini we' si ukaniita?"

"Mimi nilikuita?"

"Ndiiiyo... ukaniambia nikae... na mimi naitaka yako, siyo ya hao wengine..." akaongea kwa deko eti.

"Unaitaka nini?" nikamuuliza.

"Hii hapa..." akasema hivyo na kuishika sehemu yangu ya siri.

Alikuwa amesababisha nivimbishe mtambo bila kupenda, nami nikautoa mkono wake hapo na kumwambia kwa umakini, "Joy naomba utoke. Nitakuzibua sasa hivi."

Nilimwambia hivyo huku nimemnyooshea kiganja kuashiria kumpiga kofi, naye akasema, "Nipige tu... lakini mi' siondoki."

"Hivi we'... saa tisa sa'hivi Joy, nina usingizi, mbona huelewi? Haya, basi nenda... nitakupa siku nyingine. Sawa? Nenda."

"Sitaki JC, nipe sasa hivi. Hata kimoja tu..."

"Kimoja changu, au chako?" nikamuuliza hivyo.

"Chako," akajibu kwa matumaini.

Nikashindwa kujizuia kutabasamu, kwa kuwa hali hii yote ilifurahisha sana. Nikamwona anaivuta-vuta midomo yake kwa tabasamu la haya.

"Mbona unang'ang'aniza sana? Unataka kuniambukiza eti?" nikamuuliza.

"Sina magonjwa mbona..."

"Nitajuaje?"

"Basi vaa mpira..."

Ai kudadeki! Wanawake!

"Situmiagi mipira mimi..." nikamwambia.

"Hata me napenda peku, ila si unaogopa magonjwa?"

"Kwani ni lazima? Si ukafanye na mtu mwingine?" nikamuuliza kwa njia yenye hasira.

"Me nakutaka wewe..." akasisitiza.

Akaishika boksa yangu usawa wa kibofu na kuifunua ili aweze kuweka huru msuli wangu uliovimba.

Nikafumba macho na kukaza meno kwa hasira, nami nikamwambia, "Joy nakuomba kwa mara ya mwisho utoke. Nikinyanyuka!"

"Nipige tu... lakini humu sitoki..."

"Eee?"

"Eee..."

Alionekana kuwa mkaidi zaidi sasa hivi, mpaka nikahisi kama vile pombe imeniisha kichwani shauri ya hisia hizi mpya kuamka ndani yangu, hasira na mhemko wa kimahaba, na zote alikuwa amezilazimisha yeye. Akaifunua boksa yangu, na msuli wangu ukawa wazi mbele yake, ukisimama kuelekea juu.

Akaachama na kusema, "Eh!"

Nikamwangalia kwa kuudhika na kuuliza, "Nini?"

Akanitazama na kusema, "Nyeupe... nzuri..."

(..........).

Sikutaka hata kumshika maana alikuwa amenikera kwa kadiri fulani, lakini nikamwacha tu afanye kilichomridhisha. Akawa ananiongelesha kwa njia ya matusi, akiniambia ningefurahia sana penzi lake maana alijua kupagawisha mwanaume, nami nikawa namwangalia tu. Alijiamini.

(..........).

(..........).

(..........).

Mzuka si ukanipanda? Nikakaa vizuri na kuivuta mikono yake, kisha nikapitisha kiganja changu kwenye shingo yake kwa mbele na kuwa kama nimemkaba. Alikuwa ameilaza shingo yake usawa wa bega langu huku ametazama juu, nami nikasimama pamoja naye na kuendelea na kazi.

Piga, piga, piga, piga, mwanamke akawa ni wa kuguna tu na kutetemeka miguu. Nilimpa dozi kama namwonea vile, sote tukiwa tumesimama, nikiwa bado nimemkaba, naye akamwaga tena. Alikuwa lege vibaya mno lakini kila mara msuli wangu ulipomtoka alikuwa anaurudisha mwenyewe, nami nikaendelea kumlabua huku akiguna na kutamka maneno machafu kuonyesha yuko mbali kihisia.

Akapasua bomba kwa mara ya tatu huku akishtuka-shtuka, nami nikaona nimtulize. Akawa anapumua kama hajiwezi, hivyo nikamgeuzia kitandani na kisha kumwachia. Akakidondokea na kulalia tumbo huku miguu bado ikiwa chini, nami nikaanza kujisafisha.

"Haya, imetosha. Nenda sasa," nikamwambia hivyo.

"Hhh... si twende nyingine tena... hata kimoja chako bado..."

"Wewe, em' nyanyuka. Halafu fata dekio ufute haya maji hapa chini," nikamwambia hivyo na kuanza kuvaa boksa.

"Dekio huwa analiacha njee," akaniambia hivyo kwa deko.

"Kafate nguo yako ufute. Sitaki panuke mikojo humu..."

Akakaa na kusema, "Lakini wewe... acha masihara basi..."

"Masihara? Naonekana kama nakutania?"

"Mh... haya bwana. Me napafuta."

"Harakisha, nataka kulala."

Akacheka kidogo kwa mguno, kisha akanyanyuka na kuanza kuvaa sidiria yake. Nikalitoa shuka maana lilikuwa limelowana kiasi, nami nikalikunja-kunja na kulirusha pembeni chini, kisha nikaenda kabatini kuchukua lingine.

"Sijui una tenki la maji humo? Utanipa kazi kuyafua mashuka ya Ankia..."

Nikasema hivyo, naye sasa akawa amemaliza kuvaa sidiria na kuiokota chupi yake iliyolowana.

"Unaonekana mjeuri, ila penzi lako la kibabe sana. Siyo mzembe. Ankia lazima anafaidi," akaniambia hivyo.

"Sana tu. Sema una king'ang'anizi mno, ungenikuta vizuri ungepata utamu hata zaidi," nikamwambia hivyo huku natandika shuka lingine.

"Nikiamua kumwambia tumefanya, je?" akaniuliza hivyo.

"Ish! Mwambie tu, kwani shida iko wapi? Hiki ni chumba chako? Aliyenifata huku nani? Nimekwambia kafate kitu uje ufute hapa, usijisahaulishe," nikamwambia hivyo.

Joy akacheka kidogo na kupiga kofi laini kiganjani mwake, naye akatoka ndani humo hatimaye.

Nikawa nimemaliza kutandika shuka, nikiwa nahisi uchovu na kichwa kuanza kuuma kwa mbali, naye akarudi pamoja na dekio lililolowanishwa na kuanza kupafuta hapo chini. Eti ooh anaachaga dekio nje, kumbe lilikuwa linataka mikojo yake ibaki tu humo!

Akamaliza kupafuta, naye akaniambia nimpe namba yangu ili tuje kutafutana tena, lakini nikamwambia atazichukua kwa Ankia akishamwambia tuliyoyafanya. Akaanza kuniambia alikuwa anatania tu, nisifikiri yeye ni mbeya, lakini nikamwambia sijali kabisa. Kwa kuwa alikuwa ameshapata zaidi hata ya kile alichotaka, nikamwambia aondoke na kuniacha mimi nilale.

Nikaenda kuzima taa kabla hata hajatoka, naye akanisogelea na dekio lake na kunibusu shavuni, lakini nikausukuma taratibu mwili wake kuelekea nje ya chumba huku akicheka, kisha nikafunga mlango. Nikashusha pumzi na kushika kiuno kwa mikono yangu yote. Mambo mengi!

Nafikiri pombe niliyokuwa nimekunywa ilisaidia sana kunipa nguvu zaidi ya kumtandika mwanamke huyo mpaka akapasua bomba mara tatu bila mimi kudondosha wanangu, nami nikakikimbilia tu kitanda na kujitupia kama mzigo mzito wa kuni, nikianza kuutafuta kwa bidii usingizi mtamu niliokuwa nauhitaji.


★★★


Nilikuja kuamka muda ukiwa umeenda sana. Macho pamoja kichwa kwa pamoja viliuma kiasi, nikihisi uzito kama vile dunia ilikuwa inanivuta chini. Nafikiri shauri ya kupitisha muda pia bila kuwa nimekunywa kama jana.

Nikajitoa kitandani na kuchukua simu nitazame muda, nami nikakuta ni saa saba mchana. Nilihisi kichefuchefu kwa mbali, nami nikaamua kuvaa t-shirt na bukta ili cha kwanza kwenda kufanya iwe ni kunywa maji baridi sana kupunguza uzito wa hali hiyo.

Nilipotoka chumbani, nilimkuta Ankia akiwa amekaa kwenye sofa akitazama TV. Akaangalia upande wangu mara moja, kisha akaendelea kutazama runinga bila kunionyesha hisia yoyote. Nikasogea mpaka hapo na kumwangalia usoni.

Alionekana kuudhika. Mimi nisijue sababu kuu ni ipi, makisio yakawa kwamba huenda alijua kilichotokea baina yangu na Joy usiku uliopita, kwa hiyo alikuwa amekasirika. Pamoja na hilo, nikajivisha utakatifu na kumpa salamu.

"Mambo vipi Ankia?"

Hakujibu. Akaendelea tu kuangalia tamthilia yake, nami nikaona nimsemeshe tu tena.

"Joy yuko wapi?" nikamuuliza.

"Sijui, labda nikuulize wewe," akajibu hivyo bila kuniangalia.

Ohohoo! Msumari kwenye kidonda!

Nikatabasamu kidogo na kusema, "Kinachokufanya unune nini sasa?"

Akabaki kimya.

"Sikiliza Ankia. Ishu ya jana na Joy ilikuwa..."

"Usiniambie mimi. Ukiamua kuanza kuwaleta na kuwaingiza mahawala kwenye hicho chumba ni juu yako. We' si ni mtu mzima? Jiamulie unachotaka..." akaniambia hivyo.

"Iih! Ankia unanisemesha namna hiyo?" nikamuuliza kwa sauti ya upole.

"Kwani nimeongea vibaya? Au umesahau kwamba mimi ni mwenye nyumba wako?" akasema hivyo na kuniangalia kwa mkazo.

"Sijasahau hilo."

"Sasa? Unawaingiza tu wanawake humo na..."

"Wanawake gani Ankia? Unajua kilichotokea jana... ama niseme leo. Unajua kilichotokea kikweli au?"

"Kwa hiyo nini, unataka kukataa? Kwamba mi' kipofu, au sisikii? Najua ulichofanya na Joy ulipomleta hapa..."

"Mimi ndiyo nilimleta Joy hapa? Si alikuja na wewe? Kama hukutaka aje ungemzuia toka tumeondoka Masai, halafu kwanza..."

"Agh, usinisemeshe bana! Utajua mwenyewe," akasema hivyo kwa kuudhika.

Eeh? Nisimsemeshe? Sawa.

Nikapita zangu na kwenda nje, moja kwa moja mpaka uani. Nikashusha mzigo kwanza huku nikiwa nimepokea kero kama kitu cha kwanza tu baada ya kutoka kuamka. Kwa mambo mengi, Ankia alikuwa sahihi. Hapo palikuwa kwake, na mimi kutambua hilo ndiyo moja ya mambo yaliyofanya nisitake kutoa penzi kwa Joy usiku huo.

Lakini king'ang'anizi cha yule mwanamke machachari kikanifanya nimpe tu alichotaka ili anitolee kelele, ukitegemea nilikuwa nimechangamshwa na pombe pia. Sasa sijui lilikuwa limemwambia nini Ankia kilichofanya anikasirikie hivyo, si unajua wanawake kwa chumvi? Usikute hata lilimwambia mimi ndiyo nililipeleka chumbani!

Yote kwa yote, sasa ningetakiwa kushughulika na hii hali kwa namna ambavyo mwenye nyumba wangu alitaka tuisongeshe mbele. Si alitaka nisimsemeshe? Hilo lilikuwa jambo rahisi sana kwangu kufanya.

Nikamaliza haja zangu na kujisafisha, kisha nikarudi ndani. Nilimpita mwanamke huyo kama simwoni vile. Nikaenda na kuchukua hela kidogo ili nifate maji baridi sana dukani, nami nikaenda tena nje kuchukua pale dukani. Mwanga wa jua uliyatesa kweli macho yangu mpaka nilipofanikiwa kurudi tena ndani, nami nikakaa zangu chumbani na kuyanywa taratibu hadi yalipoisha.

Sikutaka kujishughulisha sana na simu baada ya kuangalia mambo machache tu ya humo kutokana na kuhisi njaa, hivyo nikaamua kwenda kuoga kwanza halafu nitoke kutafuta sehemu ya kuchukulia msosi; labda kule kule tulipochukua chips siku ile na huyu mama mnunaji.

Sikutaka kutibuliwa kabisa na mtu yeyote, halafu sikuzote endapo kama mtu angenipa bega la baridi, mimi ningemrudishia mgongo wa baridi zaidi. Eti uninunie au kunichunia halafu labda nihangaiiike, sikuwa na kitu kama hicho. Ikiwa Ankia alifikiri kwamba ningejipeleka kwake na kuanza kumbembeleza kwa kuwa tu mwanzoni tulikuwa tumeanza kuchokozana kimapenzi, basi alikuwa amekosea mno.

Nikatoka zangu na kwenda bafuni kuoga, wakati huu mwenye nyumba wangu akiwa jikoni kuandaa chakula nafikiri. Nijali nini? Nikaoga, nikaingia ndani, nikavaa vizuri na kujitengeneza vyema, kisha nikatoka tena bila kuaga mtu. Kivyangu, kivyake.

★★

Mwendo wa taratibu tu mpaka Mzinga kwenye shughuli nyingi za wapambanaji ukanifikisha sehemu ile tuliyonunua chakula siku ile. Nikaagiza tu chips kavu na mishikaki minne, Pepsi baridi, nami nikaenda kukaa kwenye kiti cha wazi na kusubiri huduma yangu.

Kulikuwa na wanawake kadhaa waliojaza meza moja wakiwa wamevalia madera ya aina moja. Walionekana kuwa kama wanakamati wa vigodoro au michambo, nao walinitazama mno mpaka ikawa siyo poa. Walikuwa watano, wote wakila chips za buku jero inaonekana kwenye sahani moja, tena kwa madoido kweli!

Nikawa naongea na simu pamoja na rafiki yangu, nikimsimulia machache ya huku ili kumtamanisha aje Mbagala pia, lakini akawa ananiambia bado hajashawishika. Chakula na kinywaji kikaletwa, nami nikala mpaka kumaliza. Nikatoka na kuacha malipo, kisha nikaanza kurudi mdogo mdogo kuelekea nyumbani kwake Ankia.

Sikuzote kujua kwamba ninaangaliwa mno kulinipa aina fulani ya ujasiri, au kujiamini, lakini inaonekana kwa wengi nilionekana kuwa mtu mwenye kujisikia sana. Kwa hiyo mimi kama mimi kuwaacha watu wawe na mtazamo wowote kunielekea ndiyo lililokuwa jambo sahihi la kufanya, kwa sababu ni mimi tu ndiye niliyejijua kihalisi jinsi nilivyo.

Hapa siongelei tu kutazamwa na watu kutokana na sura yangu, bali kuhukumiwa kwa tabia zangu na watu wanaofikiri wanajua sana kuhukumu. Inaeleweka namwongelea Ankia. Alionekana kuwa mwanamke mwenye kushikilia sana mambo, yaani hata ukimuudhi kwa jambo dogo, anaumia kiasi kwamba hawezi kuliachilia kiurahisi.

Mtu kama huyo sikuzote inatakiwa kumwacha tu achukulie mambo jinsi anavyoona kuwa sahihi, kwa sababu huwezi kamwe kubadili mawazo ya binadamu kwa kulazimisha waone mambo jinsi wewe unavyoyaona. Hivyo hata kwa ishu hii iliyokuwa imezuka sasa, ningetakiwa kutulia tu, njia sahihi ya kufanya mambo kwa mwanaume. Nimpe anachotaka, maisha yaendelee. Namaanisha kutomsemesha.

Nikafika hapo nyumbani na kuingia ndani, nami nikamkuta Tesha akiwa amefika hapo. Nikaingiwa na furaha, hasa kwa sababu jamaa alinyanyuka na kunipa salamu iliyojaa uchangamfu, na bado midomo yake ilitoa harufu ya mbali ya pombe. Ankia alikuwa amekaa kwenye sofa lile dogo, nami nikakaa pamoja na rafiki yangu mpya kwenye sofa moja.

"Dah, kaka nimelala kichizi leo! Yan' sasa hivi tu ndiyo nimetoka kuoga, nimelala mpaka nikaamka kupumzika!" Tesha akaniambia hivyo.

"Ahahaha... me mwenyewe nimelala masaa yameenda kwa hiyo nikachelewa kuamka. Kweli ndiyo mida hii umeamka?" nikamuuliza.

"Sasa hivi tu yaani. Ila... kwenye asubuhi nilishtuka, nikakojoa, nikarudi tena kulala. Nimelala kaka!" akaniambia tena.

"Si joto la jana..." nikasema.

"Ah usipime! Vibe lilinipanda kweli jana, sikutukana mbele ya sister kweli?" Tesha akaniuliza.

"Haukuwa umelewa kihivyo bwana, unazingua," nikamwambia hivyo.

Akacheka kidogo na kumwangalia Ankia.

Mwanamke huyo alikuwa amekaa kwa utulivu tu sofani, miguu yake iliyopandishwa juu kwa pamoja ikiwa imefunikwa kwa khanga. Juu alivalia jezi nyeusi ya Yanga, huku akiwa kimya tu akitazama TV kwa umakini.

"Mwone huyo alivyotulia... hangover kali la asubuhi halijamtoka eti," Tesha akasema.

Nikatabasamu kidogo tu. Sikumwangalia Ankia hata kidogo, lakini macho si yana upana wake bwana? Nikaweza kuona kwamba alitutazama baada ya Tesha kusema hivyo.

"Ananiambia eti kichwa kinauma. Mama na bado! Leo tena tunaenda kuzimua," Tesha akasema hivyo akimwambia Ankia.

Ankia akacheka kwa pumzi, ile cheko ya mara moja huku ameikunja midomo kwa njia wafanyayo wanawake.

"Ulikuwa mbali mwanangu?" Tesha akaniuliza.

"Hamna, nilienda tu hapo Mzinga," nikamjibu.

"Ndo' umetokelezea hivi?" akaniuliza.

"Kawaida tu. Nilienda kupiga msosi," nikamwambia hivyo Tesha.

"Aaaa... Ankita, hujapika mamaa? Mbona unamtesa mwarabu wetu?" Tesha akamuuliza hivyo Ankia.

"Chakula kipo mbona? Hajataka tu kula," Ankia akasema hivyo huku ameangalia TV.

Tesha akanitazama usoni, nami nikamwangalia kwa ufupi, kisha nikatoa simu yangu mfukoni kuangalia ujumbe ulioingia. Nafikiri kijana huyo aliweza kusoma mchezo haraka kwamba hali baina yangu na Ankia haikuwa nzuri, kwa hiyo akaamua kuanzisha mada nyingine.

"Oy, kwa hiyo na leo tutaingia Masai, au siyo?" akaniuliza.

"Kuna ishu gani? Tusije tukatoka usiku mno tena, dada yako anaweza ku...."

"Sister siyo mzinguaji JC. Yuko peace sana. Hata yeye huwa tunaenda naye akiwa free. Muulize hata Ankia," Tesha akaniambia hivyo.

Nikamtazama Ankia machoni kwa ufupi, nami nikakuta ananiangalia pia. Nikakatisha utizami huo taratibu na kusema, "Fresh tu kaka, tutaenda."

"Ee... af' leo kuna game ya Simba saa moja, tutaicheki. Nataka tuingie VIP kule," Tesha akaniambia.

"Aaa sawa," nikasema hivyo.

"Unashabikia timu gani?" akaniuliza.

"Simba," nikamjibu.

"Aina hiyo kaka. Umeona chibonge? Wanaume halisi wako Simba! Unajiweka kwa hao vyura wa kijani kufanya nini?" Tesha akamwambia Ankia.

"E-eeh... niache. Yanga ndiyo timu yangu tokea wakati ambao haukujua kutamka neno 'Simba,'" Ankia akamwambia hivyo.

Tesha akacheka na kusema, "Unalo bibie!"

Ankia akasonya kidogo.

"Twende VIP wewee... acha unyonge," Tesha akamwambia.

"Akha! VIP yenyewe imekaa kama sebule yangu. Nendeni tu," Ankia akasema hivyo na maudhiko yake.

"Kwa hiyo tunatulia mpaka saa moja?" nikamuuliza jamaa ili kukwepa kisirani cha mwanamke huyo.

"Ee, ila, nilikuwa nimekuja kuangalia kama hauna mambo mengi sana, tutoke tukazurure Mbagala hapo," Tesha akaniambia.

"Hauna kazi za kufanya?" Ankia akamuuliza.

"Naongea na wewe kwani? Huyu amekuwaje?" Tesha akasema hivyo.

"Fresh tu kaka, twende hata sa'hivi," nikamwambia hivyo.

"Poa," akaitikia.

Sikutaka kujizungusha na mengi. Nikanyanyuka na kuanza kutoka nje bila kujishughulisha na Ankia, nami nikawa namsikia Tesha akimwambia kiutani kwamba ananiiba mchina wake kwa hiyo akitaka kuvimba mpaka apasuke basi aufunge mlango vizuri ili asirushe mautumbo yake nje.

Tukatoka baada ya jamaa kuvaa viatu vyake; vyenye mtindo wa kandambili zinazofunika vidole vyote na kuacha uwazi mdogo wa mguu kufikia kisigino. Alikuwa amevalia T-shirt jeupe na pana, suruali-modo nyeusi, pamoja na kofia ya kumkinga na jua. Mimi nilikuwa nimetupia tu T-shirt jeusi la mikono mifupi pamoja na jeans, na miguuni masai zangu safi. Ndivyo nilivyokuwa nimeenda pale Mzinga, na sasa rafiki yangu mpya angenipeleka Rangi Tatu "kuzurura," kama alivyosema.

Tukiwa tunatembea taratibu tu kwa mitindo ya kujiamini, Tesha akaniambia, "Mwanangu inabidi uwe unavaa cap. Jua kali kinoma, litakubabua uwe mweusi."

"Unasema kweli. Halafu linaniumiza kweli macho. Nataka nichukue kama hiyo yako tukifika Mbagala. Angalau kuzurura kama hivi kutanizoesha maeneo shuta," nikamwambia.

"Asilimia mia. Pamekaa nyuma kidogo siyo kama mitaa mikali mikali kama kule kwenu Sinza ama Kigamboni, ila pana janja zake. Wakati nimefika sikufikiri kuna chimbo hata moja, ila yapo!" akasema hivyo.

Nikatabasamu na kumuuliza, "Na we' unaendaga kwenye hayo machimbo?"

"Ah, ya huku hamna, wanawake wa kizee tu ni mabaka! Ubungo, Sinza, ndiyo kuna pisi kalee!"

Nikacheka sana na kutikisa kichwa.

Akacheka kidogo na kusema, "Au nadanganya? We' mwenyewe najua ushapita sana huko."

"Hapana, sipitagi."

"Ah wewee! Unazingua..."

"Ih, unafikiri? Siendagi huko mimi. Kama kuja huwa wanakuja wenyewe tu, me mpaka kumfata hivi mwanamke Tesha... ujue nimemwelewa sana. Haya mambo ya gusa mara moja na kupokezana naonaga hayana faida. Sema me kwangu yakija kama yamenikuta vibaya, ndo' unakuta napiga. Ila sishobokei kivile kaka..."

"Au siyo?"

"Ndiyo hivyo."

"Dah, haya bana. Ndo' maana kumbe hata na jimama Ankia humtaki?" akaniuliza.

Nikacheka kidogo tu.

"Halafu mbona kama amevimba sana leo? Mmetibuana wapi?" akauliza.

"Ah... si ndo' mambo kama hayo?" nikamwambia.

"Imekuwaje?"

"Amenikasirikia kisa jana."

"Nini?"

"Nilimpiga Joy," nikamwambia.

Tesha akasimama na kunishika mkononi, naye akasema kwa sauti ya juu, "Weweee! Acha basi mwanangu, unasema kweli?"

"Kweli."

"Muda gani?"

"Muda ule nimekuacha kwenu, nilipofika ndani Joy akakitaka..."

"Kwo' ukamwingiza chumbani?" akauliza huku tukianza kutembea tena.

"Alikuja mwenyewe, kang'ang'ania kweli. Ikabidi nimpige tu aridhike, aondoke. Sasa ndiyo Ankia kanikasirikia mwana, hataki nimsemeshe," nikamwambia hivyo.

Tesha akacheka kidogo na kusema, "Ah! We' noma! Ushakula hadi na Joy usiku wa kwanza mmekutana? Utamaliza wake wengi za watu sisi tunakuangalia tu."

"Kwani Joy ameolewa?"

"Hamna, ila yule mwanamke huwa anatoka na wanaume wenye pesa sana. Yaani hata pale Masai, nasikia huwa anapigwa miti na mwenye Masai, halafu huyo jamaa ana kahoteli kengine kakubwa huko Buza. Hapo hivi Joy huwa anawaleta mademu wakali wanaouza, si unaelewa? Yuko kama Kingpin wa kike yaani, halafu hizi ishu hakuna wengi wanaojua..."

"We' umejuaje?"

"Kuna jamaa hapo ndiyo meneja Masai anaitwa Bobo, sema jana hakuwepo, ni mshkaji wangu pia nitakuonyesha. Ndiyo huwa ananiambia vitu. Wale wana ishu nyingi sana halafu Joy anapitisha mambo mengi kona na kona, biashara zinaendelea. Si unajua mjini? Macho mengi yako kwa huyo demu maana anajiwekaga fresh sana. Halafu nasikia analindwa, kuwa mwangalifu asije akakutafutia balaa mapema," Tesha akaniambia.

"Mbona anaonekana wa kawaida sana?"

"Kwani mwanangu jambazi atakwambia yeye ni jambazi? Si mpaka aje agongwe risasi ndiyo unabaki kinywa wazi?"

Nikacheka kidogo tu.

"Kwa hiyo mtoto akaililia?" akaniuliza.

"Ah, we' acha tu. Nilikuwa namwambia toka, hasikii. Akanikera mpaka nikampiga vya kukomesha!" nikasema hivyo.

Tesha akacheka na kusema, "Anaonekanaga mtamu kweli. Me mwenyewe nawakubali sana hawa wanawake, sema Masai hapo fitina nyingi, ndiyo maana naendaga zangu Ubungoo. Kwa hiyo Ankia akamaindi sana ulivyompiga Joy?"

"Sana. Na unajua ni kweli, kufanyia hivyo kwake siyo fresh. Si pombe tu jana na king'ang'anizi cha Joy? Ila sema Ankia ameniudhi, hataki kunisikiliza. Anasema nimeshaanza kuingiza mahawala... ah kaka..."

Tulikuwa tunaikaribia lami sasa, naye Tesha akanishika begani huku bado tukiwa tunatembea taratibu.

"Kinachomuuma ni kwamba umefanya mapenzi na mwanamke nyumbani kwake, au kwa sababu tu umefanya mapenzi na mwanamke mwingine bali si yeye?" akaniuliza hivyo.

"Inaonekana ni vyote... sijui sana," nikamwambia.

"Ahah... ngoja kwanza..."

Alisema maneno hayo na kunisimamisha kabisa ili nimsikie kwa umakini, nami kweli nikaweka umakini wangu kwake hata zaidi.

"Nafikiri Ankia amekupenda. Tena siyo ile kupenda kama ya mwanamke wa aina ya Joy ya kutaka penzi tu kumridhisha, ila ile kupenda ya moyoni. Sasa kwa Ankia hiyo ni shida kwa saabu'... huyo mwanamke amepitia magumu na mume wake. Unafahamu alikuwa ameolewa?"

"Ndiyo."

"Ee... alikuwa anakaa hapo na mumewe na mtoto wake wa kike, miaka kama sita hivi. Ila huyo mtoto akawa amekufa. Aliumwa sana. Ankia ye' hana wazazi, ndugu zake wengine sijui wako wapi huko, na hiyo nyumba aliachiwa na baba yake aliyekufa siyo muda mrefu sana baada ya Ankia kuolewa... ndiyo walikuwa wanaishi na familia yake hapo..."

Nikatikisa kichwa kuonyesha uelewa.

"Asa' ile mtoto wake kufa vile, badala ya mume wake na ndugu zao kumfariji, wakawa wanamrushia lawama kwamba... hajui kutunza, hawezi malezi, kama vile kusema..."

"Yeye ndiyo alimuua."

"Eeeh kaka, imagine! Mume wake sijui walikuwa wa kabila gani huko, wajinga-wajinga tu, watu wake wakamshawishi aachane naye, halafu Ankia alikuwa anampenda kweli huyo jamaa. Biashara za baba'ake alimwachia msela aongoze, jamaa akawa anamletea dharau tu. Alipoamua kumwacha kabisa... Ankia alivurugika wewe! Sisi tumekaa naye hapo... alikuwa wa kulia tu, da' Miryam alijitoaga kweli kumsaidia mpaka akajikakamua tena. Angalau siku hizi kama unavyomwona, anajitahidi kuchangamka. Lakini hayo ndiyo mambo yaliyomfanya asitake mwanaume tena... kama mwaka sasa hivi sijamwona na mtu kabisa... amekuwa wa nyumbani tu."

Nikaangalia chini kiasi na kusema, "Hiyo siyo poa."

"Ee. Hakuwa hata na ile... nguvu ya kutaka kuendelea na kazi, agh akaamua tu kuuza-uza vitu vyao vingi na kurudisha biashara za baba'ake... ila sijui mengi sana kuhusu hayo. Umeona? Kwa hiyo... ni mtu ambaye tunamwelewa sana. Nadhani hata hii ya kupangisha mtu hapo kwake ilikuwa njia ya kujiingizia kapesa ili asogee-sogee kimaisha zaidi... na sasa wewe kuja ndiyo naona kumemchangamsha zaidi. Kuna kammama kamoja kanaitwa mama Chande kalikuwa kananiambia... kabla sijakufahamu... kwamba Ankia alikuwa anakutendea kama vile umemwoa tayari maana alifurahia mno kuwa na wewe hapo..."

"Dah, halafu huyo mama mbeya..."

"Wee! Kumbe unamfahamu? Hata hujamuuliza kitu, tayari kashasambaza ubuyu! Masai kote wanamjua," Tesha akasema hivyo.

"Aisee! Kwa hiyo unasema kwamba Ankia kujua nimetoka na Joy kunaziumiza sana hisia zake za moyoni?"

"Ndiyo hivyo kaka. Anaweza akaanza kuwa kama kipindi kile."

"Lakini Tesha me nimekuja juzi tu. Hajui natoka wapi, nimeishi vipi... sawa, ni normal sana haya mambo ya kuvutiana na nini lakini mimi sijaja huku kwa misingi ya kuwa kitulizo cha moyo wake. Je kama nina mpenzi wangu mwingine? Ama labda kama ningekuwa nimeoa? Hatakiwi kuweka matarajio ya namna hiyo kwangu mimi kwa sababu bado hajanijua vizuri... haya mambo ya kufurahishana... yanabaki kuwa ya kufurahishana tu... ila kama ni kwenda kule anakotaka twende, sidhani kama nitaweza," nikamwambia ukweli.

Akanishika begani na kusema, "Ndiyo maana nimekwambia haya, ili uje kuongea naye. We' ni mwanaume, mwambie tu unamwelewa, na kama atataka mwende mpaka sehemu fulani, basi mweke wazi kabisa kwamba utaishia mahala fulani... ili asije kukuzoea mno ikawa shida. We' mwenyewe utajua cha kufanya mwanangu. Niliposema hatakagi kuguswa shauri ya kuogopa ngoma nilikuwa natania tu... hivyo ndiyo hali ilivyo kwake..." Tesha akanipa ushauri huo.

Nikatikisa kichwa kidogo kwa njia ya kusikitika kiasi, naye akaniambia tuvuke sasa barabara ili tukapande daladala za kuelekea Rangi Tatu.

Sikufikiri Tesha angeyageuza mazungumzo hayo kuwa yenye kugusa namna hiyo, lakini ni kweli, yalinigusa sana. Tena hadi nikawa nimeingiwa na kale kahisia ka hatia kutokana na matendo yangu ya kuanza kumwonyesha uvutio wa kimapenzi mwanamke yule bila kuelewa vizuri zaidi hisia zake kwa ujumla. Ni kitu cha kawaida sana kwetu sisi wanaume kufanya, na Tesha kunielezea kisa cha maisha ya Ankia kukaanza kunipa mwanga kuona kwamba jambo hilo halikufaa.

Hivyo kutokea hapa ningetakiwa kushughulika na mwanamke huyo kwa njia ambayo isingemwachia maumivu niliyofikiri yangekuwa ya kawaida kwa sababu ya kuchuniana tu. Ningetakiwa kuzungumza na Ankia, anielewe, nimwelewe... tuelewane.



★★★★★★★★★

ITAENDELEA

★★★★★★★★★

Full Story WhatsApp or inbox

Whatsapp +255 678 017 280
 
MIMI NA MIMI

A Story by Elton Tonny

Familia, Urafiki, Mapenzi, Kazi, Tamaa, Hila, Usaliti, Siri, Mambo Ysiyotazamiwa

R-rated 18+

Enjoy!


★★★★★★★★★★★★★

SEHEMU YA SITA

★★★★★★★★★★★★★


Tukapanda daladala, nasi hao tukaianza safari fupi kuelekea Rangi Tatu. Tesha alikuwa amesimama mbele yangu, kukiwa na mwanamke mbele yake ambaye alibananiza mwili wake kwake. Kutokana na nywele za mwanamke huyo zilizobanwa kwa nyuma kusababisha ziutekenye uso wa jamaa, akawa anahamisha uso wake huku na huko, na kila mara mwanamke huyo alipojigeuza ama kugeuza shingo angefanya nywele zake zimtekenye jamaa usoni.

Basi tukawa tunageukiana na kucheka kivyetu tu, nikielewa pia kwamba Tesha alipenda sana vitu vingi vilivyohusisha wanawake. Asili yetu yaani. Mpaka tumefika Rangi Tatu, mwanamke huyo mtu mzima kiasi na mwenye mwili mnono usio mrefu wala mfupi sana, alikuwa amesimama tu kwa ukaribu na Tesha, naye jamaa akaanza kumsemesha.

Sikujua alimpiga swaga zipi lakini nilijua tu zilifanikiwa baada ya Tesha kumpa simu yake na mwanamke huyo kuipokea, kisha akaandika namba zake kabla ya sisi kushukia eneo hilo. Tukamwacha mwanamke huyo akikaa kwenye siti iliyoachwa wazi, ikionekana aliendelea na safari kuelekea Tandika.

Tesha akawa ananiambia jinsi gani ilivyokuwa rahisi kwake kubeba namba za wanawake wengi na kisha kuja kuyajenga pamoja nao ili ajifurahishe, na alipendelea sana wanawake wenye umri mkubwa. Akaniambia kwa jinsi ambavyo nilikuwa nikitazamwa sana kutokana na sura yangu nzuri basi na mimi ningepaswa kuhakikisha naondoka na namba ya mwanamke mmoja maeneo hayo, lakini nikamwambia kiutani kuwa kitabu cha kutunza namba kwenye simu kilikuwa kimeshajaa baada ya yeye kunipa yake ile jana.

Tulitembea eneo hilo kuelekea mpaka mitaa ya Zakhem, tukazunguka na kutazama sehemu nyingi zenye shuhuli na wanaharakati wengi. Palikuwa na uchangamfu unaoendana kiasi na eneo kama la Kariakoo ingawa si sana, naye Tesha akawa ameniambia anataka twende sehemu fulani iitwayo Kijichi ili akachukue pesa.

Hakuniweka wazi wapi hasa, nami nikaridhia tu. Alionekana kuwa mtu aliyependa kuchukua maamuzi mengi mapya kufaana na hali inayokuwepo, yaani kama vile ambavyo alikuwa amepanga tuje tu kuzurura Mbagala Rangi Tatu halafu akapata wazo la kuchukua pesa sehemu nyingine ili mizunguko iongezeke zaidi. Na mimi nilipenda sana kuona maeneo mapya, kwa hiyo nikakubali na kumwacha aniongoze.

Tukachukua usafiri wa bajaji kutokea Zakhem, nasi tukashuka na barabara ndefu mpaka maeneo ya Kijichi. Huku palikuwa na aina fulani ya utulivu zaidi, kusiwe na pilika kubwa kubwa sana kama kule tulikotoka, na baada ya kufika kituo cha Upendo, tukashuka. Tesha akalipa nauli na kuanza kunipeleka upande wa mbele zaidi, kisha tukaingia kwenye barabara ya kokoto za lami mpaka kufikia usawa wa jengo kubwa kiasi la bidhaa.

Kwa haraka ningeweza kutambua kwamba sehemu hiyo ilihusika na shughuli za uuzaji wa bidhaa mbalimbali za jumla, ikiwa kama duka kubwa ama supermarket tu kutokana na muundo wake pamoja milango mipana ya vioo, na baada ya kuliona gari jeupe la Toyota pickup nililolifahamu vizuri sana, nikaelewa Tesha alikuwa amenipeleka wapi.

"Oy, hapa ndiyo kazini kwa sister," akaniambia hivyo.

"Naona. Hukuniambia kama tunakuja hapa lakini," nikamwambia.

"Si ndo' surprise sasa? Nyie watoto wa kishua si mnapenda hayo mambo?"

"Ah... nani kakwambia me wa kishua?"

"Unaonekana tu we ni wa kishua. Ama nimewrong namba?"

"Hahah... me mtoto wa mtaani tu kaka..."

"Acha kuzingua bana..." akasema hivyo huku tukielekea mlangoni.

"Ndiyo anafanyia kazi hapa?" nikamuuliza.

"Duka lake kabisa," akasema.

"Aaa... kumbe..."

"Yah..." akajibu.

Eneo la kuzunguka jengo hilo lilikuwa safi sana, na baada ya kuingia ndani humo, nikaona kukiwa na maboksi mengi yenye bidhaa za matumizi mbalimbali ya nyumbani, vyakula vilivyofunikwa, pamoja na vinywaji. Kulikuwa na friji kubwa kubwa zilizotunza vyakula baridi, barafu na vinywaji, na upande wa pembeni tu kutokea kwenye mlango huo wa kuingilia ilikuwa ni meza laini ya mbao iliyowekewa kompyuta.

Kwenye kiti katikati ya meza hiyo aliketi mwanamke mweupe aliyevalia baibui jeusi pamoja na ushungi mweupe uliofunika kichwa na kuacha uso wake nje. Macho yake makubwa kiasi yalituelekea sisi, na Tesha akasogea mpaka hapo mezani huku mimi nikiwa nyuma yake.

"Mamacita... nakuona..." Tesha akamwambia hivyo huku akitabasamu.

Mwanamke huyo alikuwa Mamacita kwelikweli, naye akatoa tabasamu lililofanya mashavu yake yatokeze vishimo vilivyompendezesha zaidi, halafu akaniangalia usoni. Nikasimama usawa wa meza pia na kumtazama machoni.

"Mtoto umependeza kama kawaida yako. Uko poa?" Tesha akamsemesha hivyo.

Akasema, "Niko poa. Karibu."

"Eeeh? 'Korribu' yaani umeing'ata kama mzungu vile! Shauri ya kumwona pedeshee hapa, ama nini?" Tesha akamtania.

Mwanamke huyo akacheka kidogo kwa haya, huku mimi nikimwangalia tu kwa macho yenye upendezi na tabasamu hafifu.

"Oy, huyu ni Soraya... au Tausi. Mtoto mweupee na mwepesi zaidi ya tausi," Tesha akaniambia hivyo.

Soraya akasema, "Ila wewe, nishakukataza kuniita mtoto. Si nalingana na dada yako?"

"Aaa kwo' unataka niwe nakuita kikongwe?" Tesha akamuuliza.

"Eee, tena ndiyo inafaa..." Soraya akasema.

"Mm? Haya bana. Sister yupo?" Tesha akauliza.

"Yupo," Soraya akajibu.

"Ngoja nimcheki Mimi faster. Nakuja," Tesha akaniambia.

"Poa," nikamjibu.

Akaanza kuuelekea mlango wa chumba kingine ndani hapo ulioonekana kwenda ndani ya ofisi ya dada yake, naye akawa anamwonyesha Soraya ishara ya vidole kunielekea mimi; kama kusema amemwachia mimi ili tuongee.

Nikatabasamu kidogo tu na kumwona akiingia ofisini humo, nami nikamtazama Soraya usoni. Alikuwa na mwonekano fulani hivi wa kiarabu kutokana tu na namna alivyojiweka, nami nikaanzisha maongezi.

"Mambo vipi?" nikamsemesha.

"Poa tu. Karibu sana," akanijibu.

"Asante. Sehemu nzuri sana hapa..."

"Ee... mwanzoni hapakuwaga pamejaa namna hii, sa'hivi angalau vitu vinaongezeka... biashara inakua," akaniambia.

"Mnauzaga bidhaa kutoka kampuni moja?"

"Hamna, tunachukua kutoka kampuni mbalimbali. Azam, Jambo, Mo... ndiyo tumevijaza hapa..."

"Ahaa... na kwa huku wateja wengi wanasogea eh?"

"Sana. Hii mitaa tuko sisi tu hapa, kwa hiyo wa madukani na watu wengi binafsi huwa wanachukulia vitu kutokea humu... then wanaenda kuendeshea shughuli zao pia..." akasema hivyo.

Alikuwa na sauti nzuri, isiyo nyembamba sana, nami nikampa tu uhakikisho wa kwamba nimeelewa alichosema kwa kutikisa kichwa kidogo.

Akashika mouse ya kompyuta kwa kiganja chake cheupe kilichorembwa kwa michoro ya yna na kucha ndefu vidoleni zilizopakwa rangi nyekundu, na kwa sauti ya chini kiasi akauliza, "Unaitwa nani?"

"JC," nikamjibu.

"JC?"

"Ndiyo. Herufi mbili tu," nikamfahamisha zaidi.

"Sawa," akajibu hivyo.

Niliona aina fulani ya uvutio kutokana na namna alivyonitazama, na alionekana kuwa mpole sana.

Nikamuuliza, "Umeolewa?"

Akaniangalia na kutabasamu kiasi, naye akatikisa kichwa kukubali.

"Wanao hawajambo?" nikamuuliza.

"Wazima. Sijui wakwako?"

Alipouliza swali hili, nikatulia kidogo nikitazama chini, kisha nikamwambia, "Sina watoto."

"Kwa nini?"

"Muda bado."

"Kwani unataka kupata mtoto ukifikisha miaka mingapi?"

"Labda 40 hivi..."

Akacheka kidogo na kutikisa kichwa.

"Kweli, ama ni vibaya?"

"Hamna siyo vibaya, ila wanao watakuita babu maana utazeeka bado wadogo..."

"Hamna... wanaume hatuwahi kuzeeka kihivyo..."

"Sawa. Ni jambo jema," akaniambia.

"Yeah..."

"Kwa hiyo bado haujaoa?"

"Bado."

"Kwa nini usioe sasa?"

"Ndoa siyo jambo la mchezo dada. Ni kitu kizito. Muda ukifika nitaoa tu. Na hata nikisema niamue kuwa na mwanamke na kuishi naye kama mke wangu, naweza... lakini ile kufunga kabisa pingu za maisha linakuwa jambo la kuweka akiba ya mbeleni kwanza..." nikamwambia.

"Mh? Hayo mawazo vijana wengi wanayo, lakini sioni kama ni sahihi. Unakuwa unacheza na watoto wa watu tu..." akaniambia hivyo.

Nikacheka kidogo.

"Hahah... si ndiyo? Na wewe ndiyo unafanya hivyo?" akaniuliza.

"Hamna bwana. Ama naonekana kama muhuni sana?"

"A-ah sijasema hivyo. Ila vijana wengi ndiyo mnafanya hivyo siku hizi. Ni bora kuoa mwanamke ukatulia naye ndani tu," akasema.

"Hakuna kitu kama kutulia ndani tu siku hizi dada'angu. Ndoa nyingi ziko kwa ajili ya fashion... kujionyesha tu, lakini bado hakuna anayetulia na mwenziye mmoja bila kutoka nje. Nadanganya?"

"Hapana, ni kweli..."

"Eee... ni vyema ukipata mtu aliyetulia, kweli mtatulia. Ila muda ukipita tu mkaanza kuonana kama ng'ombe aaa imeisha hiyo..."

Kauli hiyo ikamfanya acheke na kufunika mdomo wake kwa vidole viwili; shau yaani.

"Umeona? Na hayo mambo siyo kwa sisi wanaume tu, mpaka wanawake. Ukishajua mwenzio anacheat na we' unatafuta wa kukutuliza... kinachofata ni kuachana kama siyo kuuana, watoto wanabaki kuteseka. Faida gani? Ila ni bora tu kufanya vile moyo wako umeridhia, yatakayokuja ndiyo yatakayokuja. Basi," nikamwambia hivyo huku nikitabasamu.

Akawa anatabasamu pia, naye akasema, "Yote hayo ni kweli. Kila mtu ana maamuzi yake."

"Ndiyo hivyo. Mume wako anaweza kuamua kutembea na dada yako au rafiki yako na wewe usijue. Hata wewe ukiamua kuzaa na mimi na ukampeleka huyo mtoto alelewe na mume wako akidhani ni wake, unashindwa nini? Ndiyo system zililivyo siku hizi. Watu wanaishi kwa maamuzi wanayoona yanawafaa, kwa hiyo unaishi tu upendavyo ili life lisonge," nikamwambia hivyo.

Inaonekana aliingiza maneno hayo akilini mwake kwa utafakari wa kina sana, kwa sababu alinitazama machoni kwa mkazo mwepesi; yaani kama anajaribu kunisoma vile. Mimi kwa ubora wangu wa kuzungumza nilikuwa nimemwonyesha tu kwa maneno namna ninavyoona mambo, lakini nadhani nikawa nimeiingizia akili yake jambo fulani ambalo lilisisimua fikira zake.

Akaangalia chini na kutabasamu kwa njia ya shau, nami nikasema, "Kwa hiyo watoto na ndoa... vitakuja tu. Sa'hivi ni kutulia."

Akaniangalia na kuuliza, "Na kuula ujana?"

"Haswa!" nikamwambia hivyo kiutani.

Sote tukacheka kidogo, na hapo hapo mlango wa ofisi alikoingia Tesha ukafunguka. Jamaa akatokeza kidogo na kuniita kwa ishara ya kiganja, nami nikajiweka sawa na kuanza kwenda. Labda dada yake alitaka kuniona, ama Tesha ndiyo alitaka nimsalimie, yote ningeyajua hapo ndani.

Nikaingia ofisini humo. Palikuwa pazuri sana. Sehemu simple tu yenye usafi wa hali ya juu. Kulikuwa na masofa mawili mafupi upande wa mbele zaidi usawa wa dirisha lenye vioo vyeusi, picha kadhaa zilizotundikwa ukutani na hati za utambulisho wa masuala ya kikazi kama karatasi za TRA vile, na shehena fupi yenye madaftari na makablasha.

Pembeni kutokea kwenye yale masofa ndiyo kulikuwa na meza ndefu kiasi ya mbao nzito iliyotengenezwa kwa ubunifu, iliyowekewa viti vyeusi vitatu kuizunguka; kimoja upande mmoja na viwili ule mwingine. Kwenye hicho kiti kimoja ndiyo alikaa mkurugenzi niliyetambulishwa kwake jana usiku, bibie Miryam. Na alionekana makini kweli.

Kama kawaida, mwonekano wake ulivutia. Alivaa blauzi ya njano yenye mikono mirefu, bila shaka kwa chini akiwa amevaa sketi ndefu ingawa sikuiona vyema, na niliweza kuona ndala laini za kike zenye rangi ya njano miguuni. Uso wake ulipendeza sana, naye alikuwa ameweka viwiko vyake vyote mezani huku akiwa ameshika kalamu na kuizungusha-zunguza vidoleni, na mezani hapo pia kulikuwa na laptop aina ya HP.

Tukasimama na Tesha usawa wa viti vile viwili, naye Miryam akawa ananitazama machoni kwa utulivu.

"Umemwona bosi?" Tesha akaniuliza hivyo.

"Nimemwona," nikasema hivyo bila kuacha kumtazama Miryam usoni.

Miryam akamwangalia mdogo wake.

"Si ulikuwa unafikiri nakudanganya? Huyu hapa sasa," Tesha akamwambia hivyo.

Miryam akaniangalia tena.

"Habari za kazi?" nikamuuliza.

"Nzuri. Uko poa?" akaniuliza na mimi.

Aisee! Hako kasauti! Yaani hata hakuilazimisha iwe tamu namna hiyo lakini iliposikika kwangu yaani niliipenda sana. Sijui alikuwa anafanyaje tu hapo kooni!

"Niko fresh kabisa," nikamjibu kiunyoofu.

"Da' Mimi nimemwambia niko nawe tunatembea, akafikiri namzingua. Ndo' nimekuita akuone. Unajua sister anakukubali kinoma toka umemwokoa Mariam..." Tesha akaniambia hivyo.

Nikamwangalia Miryam na kuona anatazama chini huku akitoa tabasamu hafifu la kuhukumu, ile njia fulani ya mtu mzima kuona kila kitu mdogo wake anachosema kuwa upuuzi au utoto tu, nami nikajikaza nisitabasamu na kumwambia Tesha kwa ishara ya mdomo 'ila wewe!'

Jamaa akacheka kidogo kwa pumzi, naye akamwambia dada yake, "Tumezunguka hapo Zakhem ndo' nikaona tupite na huku kukusalimu. Unapiga sana kazi dada."

Tayari nilikuwa nimeshasoma kile ambacho Tesha alikuwa amekuja kufanya hapa, na dada yake akanipa uthibitisho zaidi. Hakuzungumza wala. Akatoa tu shilingi elfu ishirini na kumpatia mdogo wake, naye Tesha akazipokea huku akitabasamu. Akaniangalia kwa yale macho ya kuonyesha kwamba alikuwa amepata ushindi, ikiwa wazi alikuja pamoja nami sehemu hii kumwomba dada yake hela.

"Asante Mimi. Sisi ngoja tusepe sasa. Bado namwonyesha shujaa wetu mitaa," Tesha akamwambia hivyo.

"Haya. Umemwachaje Mamu lakini?" Miryam akamuuliza hivyo.

"Yuko poa. Tukitoka mizunguko tunaingia skani tena kumcheki," Tesha akamwambia.

"Sawa. Matembezi mema," Miryam akatuambia hivyo.

"Poa," Tesha akamjibu.

Tukiwa tunaanza kuuelekea mlango, nikamwambia Miryam, "Kwa heri."

Macho yake yalinikazia tu mimi kwa umakini, naye hakutoa jibu isipokuwa kunitikisia kichwa kidogo kuonyesha ameikubali salamu yangu ya kuaga. Nikatoka ndani ya ofisi hiyo huku nikiwa natabasamu kiasi, shauri ya kukumbukia jinsi nilivyokutana na mwanamke huyo mara ya kwanza kabisa mpaka kufikia sasa.

Tukawa tumeifikia meza aliyoketi Soraya hapo nje ya ofisi, ikiwa wazi zaidi sasa kwamba mwanamke huyo alifanya kazi kama msaidizi wa Miryam, na nilipendezwa na jinsi walivyojiweka kiumakini wa kikazi; wazungu wanasema "professionalism."

"Mtoto Soraya, sisi tunaenda sasa," Tesha akamwambia hivyo.

"Haya sawa, karibuni," Soraya akasema hivyo na kuniangalia.

"Haumuulizi pedeshee atarudi lini?" Tesha akamuuliza hivyo.

Nikatabasamu kidogo, naye Soraya akacheka kidogo pia.

"Kwetu lini sasa?" Tesha akamuuliza tena.

"Nitakuja tu," Soraya akamjibu.

"Lini?" Tesha akauliza kwa msisitizo.

"Nitakapoamua. Siyo lazima ujue kama wewe ulivyofika tu hapa," Soraya.

"Au siyo? Oya, chukua namba za mtoto. Mali safi hii, siyo ya kula kwa macho tu," Tesha akaniambia hivyo.

Nikacheka kwa pumzi tu.

"We! Nitakuchapa? Niheshimu, mi' dada'ako..." Soraya akamwambia hivyo huku akimnyooshea kidole.

"Acha kuzingua, JC ndo' habari ya jiji. Ama unaona aibu? Basi ngoja nitangulie, nimwache. Oy... changamka..." Tesha akasema hivyo.

Akanipiga begani kidogo na kunipita, akitoka nje kabisa na kuniacha hapo.

"Huyu mtoto huyu!" Soraya akasema hivyo.

"Ahahah... ni mtundu. Ungependa tuwe tunawasiliana lakini?" nikamuuliza hivyo.

Akaniangalia na kutabasamu kiasi, naye akatikisa kichwa kukubali.

Nikatoa simu yangu na kuweka sehemu ya kuandikia namba, nami nikampatia. Hatukusemeshana lolote lile mpaka alipomaliza kuandika na kunirudishia, kisha nikaipigia namba yake kwa ufupi ili yakwangu ifike kwake. Simu yake iliyokuwa mezani ikaita, naye akaichukua na kuniangalia huku anatabasamu kwa mbali.

"Sora..."

Soraya na mimi tukaangalia upande wa mlango wa ofisi ya Miryam, na hapo tukamwona mwanamke huyo akiwa ametoka huku ameshika karatasi mkononi. Nadhani ndiyo alikuwa ametoka tu na kutaka kumwita msaidizi wake ili amwambie jambo fulani, lakini baada ya kuniona hapo maneno yake yakakatishwa.

Soraya akasimama na kuitika, "Abee..."

Miryam akaendelea tu kuniangalia, nami nikabana midomo kiasi na kumtikisia kichwa mara moja kama kuaga, kisha nikatoka ndani hapo.

Sasa kilichoendelea hapo ndani ndiyo ambacho sikukijua, lakini ilikuwa rahisi kufikiri kwamba Miryam angedhani nilikuwa namtongoza msaidizi wake huyo. Angeniona kuwa bonge moja la muhuni, na hiyo ingeniharibia CV yangu nzuri kwake niliyoijenga kwa kumwokoa mdogo wake.

Ila nisingeweza kujua saaana yaliyoendelea mpaka kuhukumu mambo kwa njia hiyo kwa sababu Miryam hakuonekana kuwa mwanamke mwenye kujali mno mambo ya wengine. Sema ni kale kahisia tu ka 'atanifikiriaje tena' hasa kutokana na historia yetu ya mara ya kwanza tulipokutana.

Nikamfikia Tesha, ambaye alikuwa akizungumza na simu, nasi tukaanza kutembea kuielekea barabara. Tukasimama sehemu ya kusubiria bajaji ili turudi kule Mbagala, nayo ikafika na kutubeba. Alipomaliza kuongea na mtu wake ndiyo story zikaanza.

Aliuliza kama niliondoka na namba ya Soraya, nami nikakubali. Akasema nihakikishe natoka na yule mwanamke yaani kwa hali na mali zote, hata nikitaka anilipie chumba kwingine ili nisimuudhi Ankia kwa kupeleka mwanamke pale nyumbani basi angenilipia. Tesha alipenda sana hizi mambo!

Mimi nikamweka wazi tu kwamba Soraya nilimwelewa, lakini haikuwa kwa njia hiyo ya kunisukuma nianzishe uhusiano naye wa kimapenzi, hasa kwa sababu wake za watu sikuzote ni sumu. Nikamwambia hayo mambo niliyafanya zamani sana kwa hiyo niliviona kuwa vitu vya kawaida mno, na sikuhitaji papara kushughulika navyo.

Soraya angekuwa kama rafiki tu, na kuchukua namba yake ilikuwa njia ya kumridhisha tu jamaa lakini haikuwa imeniongezea uzito wowote wala haingepunguza lolote kwangu hata kama nisingeichukua.

Kwa Tesha maoni kama hayo yalikuwa ya kizee maana yeye alikuwa amechacharika vibaya mno, lakini alinielewa vizuri zaidi kuona kwamba nisingeweza kusukumwa kufanya mambo nisiyotaka kufanya hata kama aliyetaka niyafanye alikuwa mtu wa karibu; labda tu iwe ili kuondoa kero, na hali za kuyafanya ziwe zinaruhusu.

★★

Hatukuchukua muda mrefu sana kuondoka Mbagala baada ya mimi kuwa nimenunua kofia ya kunikinga na jua, pamoja na Tesha kununua kacha nzuri za mkononi na kunipatia moja kama zawadi. Nilimuuliza Tesha ikiwa dada yake hufanya kazi mpaka usiku kwenye siku za wikiendi, naye akasema Jumamosi tu ndiyo Miryam huenda huko dukani kwake kwa siku za wikiendi, na huwa anawahi kurudi tu labda kama akitaka kupita sehemu zingine baada ya kumaliza shughuli zake.

Tukarudi nyumbani ikiwa imeingia saa kumi na moja na nusu, naye Tesha akanipeleka mpaka pale kwao. Sikwenda hata mara moja kwa Ankia. Ndani pale, tuliwakuta mama zake wakubwa, pamoja na yule mwanamke aliyeitwa Shadya, bila shaka wakiwa wanaongea mambo fulani.

Zawadi mweupe akanikaribisha vyema, na mwenzake akiwa anachambua mchele akawa amenikaribisha vyema zaidi kwa kutoka kwenye sofa alilokuwa amekaa ili mimi ndiyo nikae hapo, naye akakaa pamoja na Zawadi mweupe. Tesha akaketi sofa moja na Shadya, mwanamke huyo akiwa ananitazama sana usoni.

"Za huko mlikokuwa?" Zawadi mweupe akaniuliza.

"Nzuri tu mama," nikamjibu kiunyoofu.

"Mlienda mpaka wapi?" yule mwenzake mweusi akamuuliza Tesha.

"Hapo Zakhem, tukaenda mpaka kwa da' Mimi pia," Tesha akamwambia.

"Aaa... mmemkuta? Anasemaje?" Zawadi mweupe akaniuliza hivyo.

Nikatabasamu na kusema, "Yupo. Anaonekana makini na kazi."

"Eee... mchapakazi sana," Zawadi mweupe akasema.

"Siyo kama hili," Shadya akasema hivyo, akimaanisha Tesha.

Sote tukacheka kidogo, naye Tesha akamwambia Shadya, "Ih, hivi kumbe nawe upo hapa? Umefika saa ngapi?"

"Unachange mosheni eh?" Shadya akamuuliza hivyo kwa nyodo.

"Ah... umeniingiza kwenye mada isiyonihusu..." Tesha akamwambia.

"Baba, unaendeleaje? Mkono bado unauma?" yule mama mkubwa mweusi akaniuliza.

"Ah, si sana. Kufikia kesho utakuwa umepoa zaidi, nitaitoa na hii bendeji," nikamjibu.

"Hivi unaitwa nani?" Shadya akaniuliza.

"JC," nikamjibu, huku nikimwangalia kwa umakini.

"JC. We' ni mtu wa wapi?" akaniuliza tena.

"Mwanza," nikamjibu kifupi.

"Unafanya kazi gani?" akaniuliza tena.

Sikumjibu haraka, bali nikawa namwangalia tu machoni kwa mkazo.

"Ushaanza upelelezi wako Shadya..." Tesha akamwambia.

"We' naye, nimeongea na wewe?" Shadya akamuuliza kwa kukereka.

"Si umwache amjibu?" Zawadi mweupe akamwambia hivyo Tesha.

"Ah, ma' mkubwa kwani hujui mambo ya Shadya? JC akishamsemesha kidogo tu yatafika kwa mjumbe!" Tesha akasema.

"Unapenda kudakia maongezi ya wakubwa ili iweje? Nilikusemesha wewe?" Shadya akamuuliza.

"Basi jamani..." Zawadi mweupe akajaribu kuwatuliza.

"Sitaki umsemeshe sasa! Tuzoee sisi wengine, JC usimzoee..." Tesha akamwambia hivyo.

"Tesha..." mama mkubwa wake mweusi akamwambia hivyo kama kumzuia.

"Sijui linajionaje!" Shadya akasema hivyo.

"Najionaje nini? We' nakujua. Hata hiyo ishu ya juzi na da' Mimi najua ushaisambaza kwa watu maana una mdomo mrefu kweli! Utafikiri alikulazimisha umlete yule jamaa..." Tesha akamwambia.

"He! Yamekuwa hayo? We' yanakuhusu nini? Nilimleta akuoe wewe?" Shadya akamuuliza.

"Si alitimuliwa lakini?" Tesha akamwambia.

Zawadi mweupe akacheka kidogo.

"Ulikuwepo? Si ulikuwa huko unazurura tu? Una kiherehere wewe, na siyo ajabu unampandikizia dada yako ujinga mpaka anakataa kuolewa wakati umri unaenda. Umemgeuza awe kama mama yako, we' umekaa tu halafu unajiita mwanaume!" Shadya akamshushua.

"Eee! Usinitibue, n'takufukuza sasa hivi!" Tesha akamwambia kwa kuudhika.

"Unifukuze we' ndo' umenileta?" Shadya akamuuliza kwa shari.

Ilikuwa imegeuka kuwa ugomvi sasa. Kisa? Shadya kanisemesha. Nikatulia tu na kuangalia chini.

"Ila nyie, yaani hamwoni hata kuna mgeni hapa jamani?" mama mkubwa mkubwa akasema.

"Eti? Utafikiri mmeoana!" Zawadi mweupe akasema hivyo.

Nikacheka kidogo kwa pumzi.

"Ah, anazingua..." Tesha akasema.

"Nazingua nini? Yaani we' hauna adabu. Dawa yako inachemka," Shadya akasema.

"Ichemshe tu mpaka ikauke! Mwaka huu sikuachi. Uache umbeya, na uache kumtafutia dada wachumba. Hataki!" Tesha akamwambia hivyo.

"Haya Tesha, naomba ukae kimya! Inatosha," mama mkubwa mweusi akamwambia.

Tesha na Shadya wakaangaliana kwa chuki, na mama zake wakubwa wakanitazama na kutikisa vichwa vyao tu.

"Mariam anaendeleaje?" nikauliza hivyo ili kukatisha ukimya.

"Ah, salama. Yuko ndani, ngoja nimwite akusalimie. Mariam..." Zawadi mweupe akasema hivyo na kumwita binti.

Haikusikika sauti ya binti yule akiitika, naye Zawadi mweupe akamwita kwa mara nyingine tena bila kurudishiwa jibu.

"Ngoja nikamfate..." Tesha akasema hivyo.

Akanyanyuka na kuanza kuelekea upande wa vyumba, ikionekana alikwenda kwenye kile chumba cha Miryam alikonipeleka mwanamke huyo siku ya kwanza nimefika hapo.

Mama mkubwa mweusi akanyanyuka pia pamoja na ungo wake wenye mchele na kwenda jikoni, kisha akarudi mikono mitupu na kukaa pamoja na mwenzake. Shadya alikuwa ananiangalia sana, yaani akinionyeshea wazi kabisa kwamba alitaka nimwone ananitazama ili nami nimpe umakini wangu, lakini nikawa nawaangalia tu mama wakubwa.

"Ankia alikuja hiyo mida ya mchana kumsalimia pia... ndiyo akatuambia mmeondoka na Tesha kwenda kutembea. Tesha amekupenda sana," mama mkubwa mweusi akaniambia.

"Aaa... ahah... ndiyo. Ananikubali sana. Hata mimi pia namkubali," nikasema.

"Unamaanisha, hata Mimi pia unamkubali?" Zawadi mweupe akaniuliza.

"Ah... hapana... nimemaanisha..."

"Amemaanisha YEYE pia anamkubali Tesha. Hajasema Mimi ya Miryam..." mama mkubwa mweusi akamwambia Zawadi mweupe kumsahihisha.

"Aaaa... hahahah... nimeelewa kushoto. Kama ujuavyo, majina na mazoea..." Zawadi mweupe akasema.

Sote tukacheka kidogo kwa pamoja.

"Basi hiyo jana jioni baada ya ile ajali, nilimshukuru sana Mungu kwa kukuleta hapa baba. Yaani umekuja ghafla tu lakini ni kama Mungu alikuleta ili umwokoe msichana wetu. Ulitufariji sana," Zawadi mweupe akasema hivyo kwa sauti tulivu.

Nikatabasamu kidogo na kutikisa kichwa kwa uelewa. Nikatambua pia alikuwa mtu wa imani sana.

"Tulimwambia Miryam... yaani! Alikuwa amechanganyikiwa akidhani mdogo wake ameumia vibaya. Mliongea kuhusu hiyo ishu?" mama mkubwa mweusi akaniuliza.

"Ee... ndiyo, tuliongea. Ali... alinishukuru," nikampaka Miryam mafuta mazuri.

"Hata sisi tunakushukuru sana. Hawa watoto tunawapenda mno," Zawadi mweupe akasema hivyo.

"Nimesikia ulimrukia kama Tarzan eti..." Shadya akanisemesha pia.

Nikatabasamu kidogo, na ni hapo ndiyo nikamwona Tesha akiwa anakuja pamoja na mdogo wake hatimaye.

Akiwa ameshikwa mkono kuongozwa na kaka yake, Mariam alionekana kuwa kama ametoka usingizini vile, uso wake ukiwa umevimba kiasi na macho kuwa lege. Alikuwa amevaa dera pana, huku nywele zake ndefu zikiwa zimevurugika kiasi, naye Tesha akamleta mpaka kwenye sofa nililoketi na kumkalisha karibu yangu, naye akakaa nasi pia. Yaani Mariam akawa katikati yetu mimi na Tesha, nami nikaingiza puani harufu nzuri ya manukato kama ya dada yao kutoka kwa binti huyu.

Nikawa namwangalia tu huku nikitabasamu kirafiki, lakini nikitumia sekunde hizo chache kumtathmini zaidi.

"Mariam, umemwona kaka?" Zawadi mweupe akamsemesha.

Mariam akanitazama usoni kifupi sana, kisha akaangalia chini tena.

"Mwamkie," Tesha akamwambia hivyo huku akiwa amelishika bega lake kwa ukaribu.

Lakini binti huyo hakutamka neno lolote. Nikamwangalia vizuri zaidi na kuona jinsi kichwa chake na macho yake yalivyokuwa na aina fulani ya mtikisiko wa mbali sana, mtu mwingine angefikiria labda ni madoido, lakini nikatambua kwamba haikuwa hivyo.

Kihalisi, kwa mwonekano wake wa miaka ya utineja, kuambiwa na kaka yake amwamkie mtu mzima ni jambo lililoonyesha kuwa alihitaji kukumbushwa kufanya vitu fulani rahisi sana hata kwa mtoto mwenye miaka 10 kukumbuka kufanya.

Shadya akamsisitizia jambo hilo kwa kusema, "Mwamkie kaka. Si unamkumbuka? Alikusaidia jana usigongwe na pshh... gari."

Lakini hata kwa msisitizo huo, Mariam akaendelea tu kutazama chini. Nikaona nijaribu jambo fulani. Nikakichukua kiganja chake cha mkono wa kulia na kukinyanyua mpaka kufikia kwenye paji la uso wangu, nami nikakiweka hapo. Alinitazama usoni, na wengine wakawa wanatutazama pia.

Nikamwambia binti, "Marahabaaa... hujambo?"

Mariam akaachia tabasamu pana huku pumzi zake zikipanda na kushuka haraka kuonyesha furaha, uso wake ukipendeza sana alipotabasamu namna hiyo, naye akaangalia pembeni huku akiendelea kufanya hivyo.

Nikakiachia kiganja chake huku mimi pia nikiwa natabasamu, na kwa kiasi fulani nikiwa nimeanza kuielewa hali ya huyu binti. Mama zake wakubwa walikuwa wanatutazama huku wakitabasamu, naye Tesha akaniangalia kwa umakini.

"Alikuwa amesinzia kabisa?" nikamuuliza hivyo jamaa.

"Ee... alikuwa amelala," akanijibu.

"Ungemwacha tu apumzike, si unajua usingizi ulivyo mtamu?" nikamwambia hivyo.

"Haina shida sana," mama mkubwa mweusi akasema.

"Eeh, akilala sana mchana usiku anaanza kusumbu..."

Nikiwa namwangalia Shadya alipokuwa anataka kusema jambo fulani kwa maneno hayo, ndiyo akawa ameyakatishia hapo kwa kilichoonekana kuwa kuzuiwa asiendelee kuzungumza. Labda kwa ishara ambayo mmoja wa wale mama wakubwa alimpa bila mimi kuiona.

Nikamgeukia Tesha na kuuliza, "Akilala sana mchana... ni vibaya?"

"Hamna... yaani... anaumwa-umwa, sawa? Anapata shida kulala usiku akitumia masaa mengi mno kulala mchana yaani... usingizi hapati. Hivyo," Tesha akaniambia.

Nikatikisa kichwa kuonyesha uelewa.

Ilionekana kuwepo na mambo mengi sana kuelekea suala la msichana huyo kuwa namna hiyo lakini watu hawa hawakutaka kuzama zaidi ndani ya hizo mada; hasa kuziongelea na mgeni kama mimi. Na ilieleweka.

Lakini, kutokana na mambo yote ambayo Ankia alikuwa amegusia kwangu kuhusu Mariam, na hilo jaribio dogo nililofanya hapo la kutoa salamu, nikawa nimeingiwa na wazo fulani kuhusu hali ya binti huyu; wazo ambalo bado sikuwa na uhakika wa asilimia zote kwamba lilikuwa sahihi. Kwa hiyo ningetakiwa kumwangalia vizuri hata zaidi ili niweze kumwelewa. Ni kwa sababu tu nilitaka kumwelewa, na labda kwa njia fulani... kumsaidia.

Basi baada ya hapo, Zawadi mweupe akawa ameuliza ikiwa tulikuwa tumeshakula ili aweze kuharakisha maandalizi ya kupika nasi tule pamoja, lakini Tesha akamwambia asiwe na hofu; tulikuwa vizuri tu, na tulipanga kutoka kwenda kutazama mechi. Tukaendelea kukaa-kaa hapo mpaka ilipofika saa moja kasoro robo saa, nasi ndiyo tukaaga kutoka.

Mpaka kufikia muda ambao tulitoka ndani hapo, Mariam hakuwa amenena chochote kile zaidi ya kututazama mara moja moja sana, akiwa na zoea la kucheza na vidole vyake mwenyewe na kung'ata kucha kwa wingi, nami nikaondoka na Tesha huku akiba ya suala la binti huyo bado likiwa akilini.

★★

Mguu mmoja na rafiki yangu mpya mpaka kufikia Masai, nasi tukaingia kwenye kumbi hiyo na kukuta watu wakiwa ni wengi sana. Waliojaza nafasi za kukaa walikuwa ni mashabiki wa Simba, pamoja na mashabiki wachache wa Yanga waliokuja kuwazomea bila shaka, na wahudumu wa hapo walionekana kuwa bize kusambaza huduma.

Nilikuwa nimemuuliza Tesha kuhusu Shadya, nikitaka kujua walikuwa na undugu wa karibu kiasi gani. Akawa ameniambia Shadya hapo kwao wanamwona kama shangazi kwa sababu alikuwa ni rafiki wa karibu zaidi na marehemu mama yao, na walisaidiana kwa mengi mno. Akasema amemjua tokea yupo darasa la tano, kwa hiyo wanamwona kama ndugu wa karibu zaidi.

Akaeleza kwamba mwanamke huyo alikuwa na duka la nguo kule Mbagala, na alikuwa ameolewa pia. Watoto wake wawili kwa wakati huu walikuwa Tanga kimasomo, huku yeye akiishi na mume wake maeneo ya Kongowe kusiko mbali sana na mitaa hii ya Mzinga. Akawa amenionya eti niwe mwangalifu naye maana alipenda sana porojo, lakini akakazia kuwa alimpenda pia na alimwona kuwa wa muhimu mno kwa sababu ya ushikamanifu wake na familia yao. Hilo likawa limeniingia vizuri kichwani.

Kwa sababu hii ilikuwa ni Jumamosi yenye uwepo wa mechi ya timu pendwa kama Simba, nilikuwa nimetarajia idadi ya watu kuwa kubwa mapema tu, na kuingia kwetu hapo kukafanya macho yatuelekee kama kawa. Tesha akaniongoza kufikia sehemu aliyosimama DJ, DJ huyo akiwa amekingwa na kiukuta kifupi cha mbao zilizochorwa majina kwa mitindo ya kibunifu, naye Tesha akaanza kusalimiana na wanaume wawili waliokuwa wamesimama hapo.

Mmoja alikuwa mfupi kwangu, lakini mwingine alikuwa mrefu hadi kunipita, mweusi, mwenye ndevu nyingi kutokea kwenye timba mpaka kufikia kidevu. Alisalimiana na Tesha kwa njia yenye uchangamfu mkubwa, na jamaa akanitambulisha kwake kwa kusema huyo ndiyo alikuwa Bobo. Yeah. Yule rafiki yake ambaye ni meneja wa hapo Masai, Bobo, ndiyo alikuwa huyo jamaa tolu.

Alionekana kuwa mtu makini na mwenye nguvu sana, nasi tukasalimiana na kufanya maongezi mafupi ya kupatana, na akaonekana kunielewa sana. Tesha akamwambia tunatafuta sehemu ya kukaa ili tulicheki game vizuri, lakini hapo palionekana kujaa, hivyo Bobo akamwita mhudumu mmoja wa hapo na kumwelekeza atupeleke kule kwenye kumbi ya VIP.

Kalikuwa keusi, kembamba, kamekomaa, nako kakatupeleka huko huku Bobo akisema angekuja kujiunga pamoja nasi. Tesha alikuwa amefikiria kuniingiza VIP mapema sana leo ila muda huo hata kama tungepata viti pale kwa watu wengi, basi tungekaa.

Huyo mdada akatufungulia mlango wa chumba cha maVIP, nasi tukaingia. Hakikuwa kipana, bali kirefu. Kulikuwa na masofa mazuri pande zote za ukuta, meza za mbao nzito katikati, michoro ya urembo kwenye kuta, mlango wa chumba kingine mbele zaidi kilichoonekana kuwa choo, na TV kubwa ya flat screen iliyotundikwa juu kwenye ukuta wa usawa wa mlango tulioingilia.

Tayari kwenye runinga hiyo ilikuwa imeshawekwa chaneli yenye kuonyesha mechi hiyo, wachezaji wakiwa ndiyo wanaanza kucheza, nasi tukakaa. Tesha akamwambia huyo dada atuletee bia za Serengeti Lite nne za moto kwanza, naye akachukua hela na kutuacha.

"Ah, mwana unaona vile watu wanatuangalia tukiingia hapa?" Tesha akaniuliza.

"Naona. Wanafikiri tuna pesa sana, au?"

"Wewe sanasana. Halafu wanafikiri mimi ndiyo nimekuleta huku ili kukudandia sasa..."

"Hahah... wakati wewe ndiyo pedeshee hapa..."

"Umeona? Hahahah... ila umepaonaje hapa? KaVIP kazuri eh? Kametulia, hakana mambo mengi, ama nini?" Tesha akaniuliza.

"Yeah. Pako poa. Ankia hakukosea lakini aliposema inafanana na sebule yake," nikasema hivyo.

Akacheka kidogo na kuniambia, "Fitina tu. Amekorogwa leo."

"Naona kama Chama hayupo..." nikamwambia hivyo kuelekea mechi.

"Ee, hajaingia. Shauri ya ile red aliyopigwa mechi iliyopita..."

"Aaa kweli... Moses Phiri ndo' anarekebisha mitambo leo... labda na Kibu..."

"Ah, Kibu hamna lolote. Mwana ana kasi, nguvu, lakini kufunga hawezagi..."

"Ahahah... uliona lile goli alilofunga Kariakoo Derby wakati mvua inanyesha? Ndiyo mpaka linatumiwa kwenye maPromo..."

"Ah, bahati sana. Yaani Kibu huwa anafunga kwa bahati sana. Umeshaona goli lake lingine toka amefunga hilo?"

Nikacheka kidogo tu, na hapo ndiyo mlango ukafunguliwa na mhudumu mwingine kuingia.

Alikuwa mwanamke wa miaka ishirini na kitu hivi, mweusi wa maji ya kunde, mfupi kiasi, aliyevalia T-shirt jeupe la Simba na suruali ya jeans yenye kubana. Alibeba hips nene, kalio lake likitokeza vyema sana nyuma, ikiwa wazi ni moja ya vivutio maalumu vya wateja hapo. Alikuwa na macho makubwa, domo nene, nywele alizosuka mtindo wa rasta ndefu zenye rangi ya samawati, naye alishika kontena dogo lenye vinywaji kwa ndani. Akaviweka mezani, huku Tesha akianza kumchokoza kwa kumshika-shika pajani na kumpiga kalioni, nami nikawa natabasamu tu.

Alipotufungulia bia, akataka kuondoka na kontena lake, lakini Tesha akaushika mkono wake na kumvuta, na mwanamke huyo akamwangukia na wote kulala sofani hapo.

"Hee... wewe..." mwanamke huyo akalalamika.

"Unaenda wapi?" Tesha akamuuliza hivyo huku akitabasamu.

"Niachie, nina wateja bwana..." akamwambia.

"Kwani sisi fisi?" Tesha akamuuliza.

"Aa..."

Mwanamke huyo akajitoa kwa kutumia nguvu kiasi, naye Tesha akamwambia, "Nenda kwanza kwa huyo jamaa, anataka akwambie kitu."

Mwanamke akasimama vizuri na kusema, "Si niko hapa aniambie?"

"Msogelee, akwambie..." Tesha akamwambia hivyo kwa msisitizo.

"Ahah... ila jamaa wewe! Dada nenda, kaendelee na kazi..." nikamwambia hivyo mhudumu.

Akabeba kontena lake na kutoka.

"Asa' ndo' nini JC? Unazingua. Hujaona kishundu hicho?" Tesha akasema kwa kuudhika.

Nikacheka kidogo na kusema, "Na Soraya je? Ye' kwani hana?"

"Aaaa kwa hiyo umemkubali Tausi kumbe! Mtafute sasa, la sivyo chukua na namba za huyu... ayaa! Baleke amekosa goli bro!"

Nikatazama TV pia na kuona rudio la mshambuliaji Baleke akikosa kufunga goli kwa shuti la karibu kwenye dimba la timu pinzani.

"Na huwa anakosa mengi..." nikasema hivyo.

"Ah, bwege tu. Turudi kwa mtoto Soraya..."

"Tesha tulia. Nimekwambia me siyo wa hivyo. Mwanamke mpaka niwe nimemkubali sana, ndiyo napita naye..."

"Unaangalia wale wazuri-wazuri eti? Hata me nawakubali, sema bei..."

"Dah! Angalia usife mapema kaka...."

"Ah, kufa kupo tu, kwanza...."

Maneno yake yakakatishwa baada ya mlango kufunguliwa tena, na hapo wakaingia wanaume watatu.

Aliyekuwa mbele alionekana kuwa kama baunsa sijui, maana mwili wake ulikuwa mkubwa na alivaa kwa njia fulani kama jasusi eti, na miwani myeusi machoni. Niliona hilo kuwa kama ushamba maana tayari giza lilikuwa limeshaingia, sasa sijui alivaa miwani ya nini! Aliyefata alikuwa mbaba mwenye mwili mnene kiasi, mweupe, na mrefu pia, na nyuma zaidi ilikuwa ni Bobo.

Sikujua sababu ilikuwa nini iliyomfanya Tesha akae vizuri zaidi kwenye sofa na si kwa mkao wa kujiachia, na wanaume hao wawili waliponipita, nikamtazama huyo mweupe kwa nyuma na kuona kitu fulani kikiwa kimetuna usawa wa kiuno. Nilipokiangalia kwa umakini zaidi, nikatambua ilikuwa ni bastola!

Bobo akanipita pia na kwenda upande wa mbele zaidi ambao wanaume wale walienda kukaa, nami nikamtazama Tesha usoni. Uso wake ulionyesha hali ya utulivu zaidi, na kwa ishara ya mdomo akaniambia kitu fulani ambacho sikuelewa vizuri. Akarudia tena na kutazama upande wa TV upesi, nami nikawa nimeyaelewa maneno hayo kuwa, 'mwenye Masai.'

Nikamtazama kiufupi mwanaume huyo na kukuta ananiangalia pia. Sijui ni nini tu ila kuna kitu kikawa kimeniambia kwamba hapa kuna jambo halikuwa sawa. Si sanasana kuhusu yale mambo aliyoniambia Tesha kumwelekea Joy aliyoyafanya kwa udhamini wa huyu jamaa wake?

Nikakumbuka kweli Tesha alinionya kutocheza sana na Joy hata kama mwanamke huyo alinitaka, kwa sababu huenda ningepatwa na matatizo ambayo yangeletwa na huyu jamaa yake. Sasa sijui ujio wake wa ghafla namna hii ndiyo uliokuwa umeyaleta matatizo hayo kwangu?

Ikiwa labda aliambiwa niliondoka na manzi wake usiku wa jana, huenda mimi kufika tena Masai leo ndiyo kukafanya aitwe ili aje kuniona. Na alionekana kutokuwa mtu mwenye masihara kwelikweli mpaka Tesha kuamua kushusha miguu alipomwona. Vipi kama bastola hiyo ilinihusu mimi? Ningetokaje hapa?



★★★★★★★★★

ITAENDELEA

★★★★★★★★★

Full Story WhatsApp or inbox

Whatsapp +255 678 017 280
 
MIMI NA MIMI

A Story by Elton Tonny

Familia, Urafiki, Mapenzi, Kazi, Tamaa, Hila, Usaliti, Siri, Mambo Yasiyotazamiwa

R-rated 18+

Enjoy!


★★★★★★★★★★★★★

SEHEMU YA SABA

★★★★★★★★★★★★★


Lakini nikatuliza zaidi akili na kuanza kuona mawazo ya namna hiyo kuwa ya kipuuzi. Ikiwa mwanaume huyo alikuwa na lengo la kunidhuru eti kisa nimetoka na mwanamke wake, basi ningehakikisha naanguka chini pamoja naye akifanya jambo lolote kuniangusha. Hii ni njia ya kumaanisha kwamba nilikuwa na ujasiri wa kupokea lolote lile ambalo angelileta upande wangu, kwa hiyo nikaamua kuendelea kutulia na kutazama mechi.

Bobo akaanza kumsemesha Tesha kirafiki kuhusiana na mechi iliyokuwa inaendelea, na kijana akawa anazungumza naye pia. Ni mimi pamoja na yule "mwenye Masai" ndiyo pekee ambao hatukuongea, na kila mara nilipovuta chupa ya bia ili kunywa, ningekuta ananitazama usoni, nami ningeonyesha kutojali kabisa alichowaza kunielekea kwa kurudisha umakini wangu kwenye TV.

Lakini nadhani alikuwa anajaribu kunisoma, hasa shauri ya mimi kuwa mgeni hapa. Alitaka kuona shobo zangu zimekaa vipi, na mimi kiukweli sikuwa mtu wa shobo, kwa hiyo aidha nilimpa ama sikumpa kile alichotarajia; angejua mwenyewe.

Dakika si nyingi sana kupita na wahudumu wawili wakawa wamekuja. Yule aliyetuletea bia mwanzoni pamoja na kengine kafupi na keupe kenye mwili namba nane, mmoja akiwa amebeba kontena lenye bia na mwingine sahani yenye mishikaki ya nyama za mbuzi kama miti 20 hivi. Bila shaka zilikuwa zinapelekwa kwa "boss," navyo vikawekwa kwenye meza yao na vinywaji kufunguliwa.

Sikujishughulisha nao kabisa. Bobo alikuwa ameanza kuongea na huyo jamaa kuelekea mechi pia, nami nikawa namsikia akitoa maoni yake kuhusu uchezaji wa Simba. Alikuwa na sauti nzito lakini iliyotulia, akionekana kuwa na aina fulani hivi ya mridhiko.

Nilipovuta bia tena, nikamwona anamsemesha mhudumu mmoja huku akinyooshea kidole chake upande wangu, naye Tesha akaniangalia kwa yale macho yenye kumaanisha aliona jambo hilo, nasi tukaendelea tu kutulia mpaka wahudumu hao walipotoka ndani hapo.

Bobo akanisemesha kwa kunikaribisha nichukue mshkaki, mimi pamoja na Tesha, nami nilipomwangalia bosi mkuu, akanionyesha ishara kwa kiganja chake kwamba nichukue kweli. Ilikuwa kwa njia tulivu tu, nami nikatikisa kichwa kukubali.

Tesha akaanza kuchukua huku akitabasamu kiasi, nami pia nikabeba mmoja na kuanza kutafuna. Sikuwa nimesahau kuhusu bastola ya jamaa huko nyuma ya kiuno, na kama hili lilikuwa jaribio lake kwangu ama basi tu aliamua kufanya haya kwa nia zozote, mimi ningeendelea kutulia tu mpaka mechi iishe, kisha niamshe na Tesha. Basi.

Si dakika nyingi sana kupita nao Simba wakawa wamefunga bao moja. Tukashangilia pamoja, na Bobo, yule baunsa, pamoja na Tesha ndiyo ambao walikuwa na kelele za ushabiki kutokana na furaha waliyopata, ila mimi na jamaa mkuu, ilionekana kama tulikuwa tunavutiana manati vile halafu mawe hatuyaachii. Utulivu niliokuwa nao na yeye ndiyo alikuwa nao hivyo hivyo, tukijiweka kama watu fulani maalumu kweli sehemu hiyo. Na nafikiri alipendezwa na hilo.

Wale wahudumu wakawa wamerudi tena, wakiwa na makontena yenye bia za Serengeti Lite 20. Zikawekwa mezani kwetu mimi na Tesha, kumi kwangu, kumi kwake. Tesha akamwambia mwanaume huyo anashukuru sana, ikiwa wazi ni huyo jamaa ndiye aliyekuwa ametununulia, na Tesha akasema hapo angezipiga zote kusherehekea ushindi wa Simba ambao bila shaka ungeletwa kwa magoli mengine zaidi.

Lakini mimi hata sikutoa shukrani. Nikaendelea tu kutulia, nikinywa taratibu tu, nikitoka kwenda kukojoa na kurudi tena kukaa, na mara kwa mara tulipoangaliana na jamaa, angenitikisia kichwa kidogo kuonyesha uwana, nami ningemrudishia kutikisa kichwa kidogo na kuendelea na mambo mengine.

★★

Tukaendelea kukaa humo mpaka kufikia kipindi cha pili cha mechi, Simba wakiongeza magoli mengine mawili bila kurudishiwa hata moja, na ndiyo kwenye dakika za mwishoni akawa amefika Joy ndani hapo. Mwanamke huyo alikuwa amependeza sana pamoja na wanawake wengine wanne alioingia nao.

Alivalia blauzi nyepesi kama kaushi, iliyoacha sehemu kubwa ya kifua chake ionekane wazi, fupi kuonyesha kitovu chake, pamoja na pensi ya skinny nyeusi iliyovutwa juu kufikia kiunoni na kumchora vizuri sana pale kati. Mapaja yake yalikuwa wazi, miguuni akivaa ndala za manyoya, na kichwani alikuwa amesuka kwa mtindo mwingine leo hii wa nywele laini kama za wazungu, huku usoni akijidodeka mapodozi na kope fupi za bandia machoni.

Wenzake pia walikuwa wamevaa blauzi laini, suruali zenye kubana, vikaptura, misuko ya aina mbalimbali na mawigi, wakionekana kuwa na lengo la kuja kufanya umalaya tu sehemu hiyo; kunywa na kutafuta pesa kwa wanaume yaani.

Joy alipoingia na macho yetu kukutana, akaachia tu tabasamu la kirafiki kutuelekea sisi wote ndani hapo, huku Bobo akianza kumsemesha na yeye kuongea naye. Akamsalimia Tesha kwa kumshika kiganja, kisha akaja kwangu pia na kukishika cha kwangu kisalamu.

Tulipokuwa tumeviunganisha viganja vyetu, nikahisi kucha ya kidole chake kilichokunjwa ikinisugua katikati ya kiganja kwa makusudi kabisa, nami nikakitoa changu kwake na kuendelea kupokea salamu za wenziye.

Akanipita na kwenda mpaka kwa bwana wake, naye akakaa karibu naye na kuanza kuzungumza. Wale wanawake wengine wakawa wamekaa kwenye masofa pia, mmoja mwenye mwili mnene kiasi akiwa karibu nami zaidi, naye Bobo akatoka nje kidogo.

Nilikuwa nimeshakunywa bia nne hivi, Tesha kama sita, nami nikamwona huyo jamaa anamwonyesha Joy ishara ya kidole kunielekea. Nisingeweza kujua kilichoongelewa, lakini nilikuwa tayari kwa lolote. Walilete tu, nami ningewaonyesha nini maana ya jina langu!

Mechi ya Simba ikaisha, na jamaa akaanza kupiga makofi kufurahia ushindi wa magoli matatu kwa bila. Wengine pia wakaanza kumsindikiza kwa makofi na wanawake waliomo humo kusimama ili kuanza kucheza muziki uliowekwa na Bobo. Jamaa ndiyo alikuwa amerudi tu pamoja na wahudumu walioleta vinywaji zaidi, bila shaka kwa ajili ya Joy na wenzake.

Nikawa nimeingia chupa ya tano, vibe likiwa limeshaniingia kitambo, nami nikamwangalia Tesha na kumwona alivyojiburudisha kwa kuongea na mwanamke mmoja kati ya wale wanawake walioingia na kumshika-shika mapajani. Ni wazi alikuwa amelewa, na bila shaka angeendelea kunywa tu. Kwa hiyo ningetakiwa kunywa kistaarabu sana ili kuhakikisha usalama wa huyu kijana pia, hasa ukitegemea dada yake alijua tuko pamoja.

Wahudumu walikuwa wamemletea kiongozi vinywaji kama Konyagi, K-Vant, na Valeur, glasi kadhaa pamoja na soda, bila shaka za kuchanganyia na bia hizo kali. Na wakaanza kuzichanganya kweli. Wale wanawake wakawa wanakunywa na kucheza taratibu muziki ulioendelea, naye Bobo akaniletea michanganyiko hiyo ya pombe ili nami ninywe pia.

Lakini nikakataa, nikisema zingenifanya nijihisi vibaya, naye akampelekea Tesha. Kijana akatae? Nadhani alikuwa ameshaanza kuufurahia huu upendo wa "maVIP" kutoka kwa bosi wa Masai, lakini mimi bado nilikuwa na mashaka yangu. Nikawa nakunywa kwa kutegea tu, huku mwanamke yule pembeni yangu akinishika hapa na pale na mimi kuitoa mikono yake kwangu.

Nilikuwa nimeweka umakini wangu mzuri kujitahidi kuendelea kuwa macho maana haya mambo ya kunyooshewa-nyooshewa vidole sikuyapenda kabisa, na kufikia mida ya saa nne usiku ikawa wazi kwamba wengine humo ndani walikuwa wamelewa vibaya mno. Ni mimi na Joy tu ndiyo ambao tulitegea kunywa sana, mimi nikiwa nazijua sababu zangu, lakini nisiweze kuzijua za kwake. Hata ile michanganyiko hakuinywa japo mtu wake alimsisitizia sana.

Bobo, Tesha na baunsa walikuwa wanaongea kweli, wakicheza na wale wanawake kwa mitindo ya kimahaba, huku bosi mkuu, Joy na mimi pekee ndiyo tukiwa tumekaa tu. Hadi nilikuwa nasogezewa makalio na mwanamke mmoja humo karibu na uso wangu na kitikiswa! Si basi tu? Bangi!

Tesha alipoanza kupasua mpaka na chupa, nikaona hiyo ilitosha sasa. Ningehitaji kumrudisha kijana huyu kwao na nije kujitahidi kutoweka mazoea mengi ya kuwa natoka naye kulewa, maana kufanya hivyo kila siku kungeleta picha mbaya pale kwao.

Nikaimalizia chupa yangu ya tano na kusimama, nisijali kuhusu zingine, nami nikamfata Tesha na kumsihi tuondoke. Akawa ananiambia bado mapema, na nadhani kwa kuniona kuwa nataka kuondoka, yule jamaa akaniponda na kisoda ili avute umakini wangu kwake.

Nikamwangalia, naye akaniita kwa ishara ya kiganja chake. Hata Bobo akanionyeshea ishara kwa kidole kuwa niende hapo, huku kichwa chake kikiyumba, nami nikamwacha Tesha na kwenda kwa jamaa. Serious.

Joy si alikuwa amekaa karibu yake? Jamaa akamwambia asogee pembeni kwenye sofa hilo ili mimi nije kukaa katikati yao, na mwanamke akatii. Wakati mwafaka wa kuijua akili yake kunielekea ndiyo ulikuwa umewadia, nami nikakaa karibu naye.

Akapitisha mkono wake begani kwangu, kirafiki eti, mimi nikiona wazi jinsi pombe ilivyomkonga nyoyoni, hivyo nikaweka umakini zaidi ili nisikie alichotaka kusema.

"Uko poa?" akaniuliza.

Wakati akiwa ananiuliza hivyo, nilianza kuhisi vidole vyake Joy vikinishika pajani na kuanza mipapaso na kunibonyeza sehemu yangu ya siri. Nikajikausha tu.

"Fresh tu," nikamjibu jamaa.

"Kijana uko vizuri sana. Yaani vizuri sana. Na wewe mwanasimba, au siyo?" akaniuliza hivyo.

Nikatikisa kichwa kukubali.

"Penyewe hapo! Unajua nini? Unanijua mimi?"

"Hapana. Ndiyo nakuona leo," nikamwambia.

"Aaa... mimi ndiyo Charles Gonga. Ulizia Chalii Gonga hapa Masai kila kona nafahamika... huwezi kunikosa..." akasema.

Nikatikisa kichwa kukubali, huku kero za Joy bado zikiendelea kunisumbua.

"We' unaitwa nani?" Gonga akaniuliza.

"JC."

"Aaa... kama JC Penney?" akauliza na kucheka.

Nikatabasamu kidogo tu, nikihisi huyu jamaa alikuwa amesoma sana, ama ni utashi tu wa kujua mambo.

"Sasa ngoja nikwambie kitu JC. Unajua kwa nini nimesema uko vizuri sana?" akaniuliza.

Nikatikisa kichwa kukataa.

"Wewe dogo... hauna show za kishamba. Sijui unanielewa? Nimekuangalia hapo... haushoboki kifala yaani. Napenda sana watu wa hivyo. Wewe ni mgeni si ndiyo? Huku Masai?"

Nikatikisa kichwa kukubali.

"Hata mimi nimeona. Wa huku washamba sana. Napenda watu wa level yako. Sijui umenisoma? Yaani... ngoja nikwambie kitu... hapa hivi... wanawake hawa wote hawa... wanakutaka. Sijui umenielewa? Wote. Hadi huyu... Joy... ila hawezi akamwambia maana niko hapa anafikiri nitazingua. Lakini wewe ni mwanaume bwana au siyo? Unajua sisi hatuingizagi miguu yote, uwongo dogo langu?" akaniambia hayo.

"Hamna. Ni kweli kabisa," nikamjibu hivyo, nami nikakishika kiganja chake Joy na kukikandamizia kwenye sofa bila kumgeukia.

"Eee... asa'... nimekuangalia. Haupapariki na wanawake. Wewe kwa mwonekano wako... mimi kwa mwonekano wangu... hivi vitu unajua ni vya kuchezea tu, au siyo? Ukitaka naweza kukupeleka sehemu yenye wanawake, tena nikisema wanawake ni wanawake kweli... huku pamekaa kisenge, Joy ndo' anafunika. Haya yanachojali ni pesa, pombe na kuzaa tu... lakini nataka nije nikutoe... nikupeleke sehemu ambayo utakutana na warembo kaka... wanaojua mikakati na wananyonya mpaka unakufwa ganzi! Sijui unanielewa?"

Kauli hiyo ya mwishoni ikanifanya nicheke kidogo kwa pumzi, nikiwa nimeshaelewa kwamba mwanaume huyo alipenda sana wanawake, na ilieleweka kwa nini hasa kwa sababu alijihusisha na biashara za wanawake kama nilivyoambiwa.

Nikamwambia, "Fresh. Me nimekuelewa."

"Kama vipi tutoke sa'hivi? Bado mapema..." akaniambia.

"Aa... kwa sa'hivi siwezi, kuna ishu nataka kufanya. Labda siku nyingine," nikamwambia.

"Aaa... kwani umeoa? Mapema hii, twende nikuonyeshe mambo mingi wewe! Hizo bia mbili nilizokuwekea hapo? Ndogo sana. Twende upige bia na watoto wa ukweli. Huwezi kuresist..." akanishawishi.

Nadhani alikuwa anataka kunitumia ili kujionyeshea kwa watu fulani, ama labda anihusishe kwenye ishu zake batili, ama huenda hata kuniumiza. Alitoa viashiria fulani vya mtu wa magendo sana, na mimi nilijua jinsi ya kushughulika naye.

Nikamwambia, "Usikonde brother, tutaenda tu. Leo kuna mambo tu nilipanga kufanya mapema kwo' ratiba haitaruhusu. Siku nyingine."

"Au siyo?"

"Yeah," nikamwambia kwa uhakika.

Akanipiga begani kidogo huku akitabasamu, kisha akatoa wallet yake mfukoni na kunipa shilingi elfu kumi. Nikaipokea huku nikimtazama kimaswali.

"Hiyo weka. Nauli. Nitakapokuita usije kusingizia hauna nauli. Ushan'soma? Nipe namba yako..." akaniambia hivyo.

Nikacheka kidogo na kutikisa kichwa kwa kutoamini mambo haya, naye akanipa simu yake ili niandike namba. Nikakiachia kiganja cha Joy ambacho mpaka sasa nilikuwa nimekikandamiza bado, nami nikamwandikia namba upesi na kisha kuitunza kwenye kitabu cha majina cha simu.

"Huyu ni ndugu yako?" Gonga akaniuliza hivyo.

Alimaanisha Tesha, nami nikamwambia, "Ni rafiki yangu."

"Aaa... anapenda kuparty ila hana hela. Tembea kwenye njia moja na mimi JC... utafurahia sana," akaniambia hivyo kilevi.

Kazi nilikuwa nayo! Hili suala la kutengeneza marafiki mpaka wale wanaotembea na bastola liliikereketa sana akili yangu, lakini nikamkubalia tu jamaa na kwenda upande wa choo ili nikojoe kwanza.

Kwa kiasi kikubwa, sikutaka kujenga ukaribu na huyo Chalii Gonga. Yeye ndiyo alikuwa analazimisha, maana aliona simshobokei kama wengine walivyofanya, na hivyo akafikiri nina kitu fulani cha pekee sana cha kumfaidisha nacho. Sijui ikiwa ilikuwa ni sura na mwonekano wangu tu, au labda Joy alimwambia vitu fulani, lakini kwa muda huu sikutaka kujali sana.

Nikamaliza haja na kutoka, na Gonga akanitikisia kichwa kunionyesha namna anavyonikubali pale nilipompita. Nikiwa makini tu, nikamfata Tesha na kumwambia twende, akiwa ameshadata na mpenzi wake mpya wa kulipwa.

Tukatoka, ikiwa ni saa tano sasa, naye Tesha akaniambia kulikuwa na geti lingine la kutokea nyuma ya jengo hilo kwa hiyo tuitumie njia hiyo kuondoka badala ya kupita kule mbele, nami nikaridhia.

Tukaanza kwenda, mwenzangu akiwa amelewa kweli lakini akijitahidi kutembea kwa mhimili mzuri, na ile tumekaribia kutoka getini, nikaitwa.

"JC..."

Kugeuka? Ni Joy. Agh! Pozi likaniisha. Nilitaka tuendelee tu kwenda maana sikuona haja ya kubaki kumsikiliza mwanamke huyo, nami nikamwambia Tesha tuondoke.

Joy akaongeza kasi ya kuja na kusema, "JC, subiri basi..."

"Oyo... mtoto huyo..." Tesha akaniambia hivyo kilevi.

"Ah... twende bana..." nikasema hivyo.

"J... naomba unisikilize..." Joy akasema hivyo baada ya kutufikia.

"Tulia... me nawasubiri hapo nje... ah... nakusubiri hapo nje..." Tesha akaniambia hivyo.

Akatoka nje ya geti na kutuacha hapo, naye Joy akajisogeza karibu yangu zaidi na kunishika kiunoni. Nikawa namwangalia tu kwa mkazo.

"JC... nimekumiss..." akaniambia hivyo.

Nikaendelea tu kutulia.

"Unajua... jana penzi lako lilikuwa tamu sana. Sijakojoa muda mrefu kweli, yaani sijui una nini tu kilichofanya nilegee kama jana..."

Aisee! Nilimwangalia kwa njia isiyoonyesha hisia kabisa, nisiwe na chochote cha kusema maana yote aliyoniambia hayakunipa athari yoyote ile.

"Najua nilikwambia naitaka kwa jana tu, ila leo nimekaa siku nzima nakuwaza mpenzi. Nataka niwe ndani ya mikono yako tena. Nataka unipe... na mimi nikupe mahaba matamu JC..."

Nikaangalia pembeni kiufupi, kisha nikamtazama tena.

"Sema kitu basi..." akaniambia.

"Kitu," nikamjibu.

Akacheka kwa madaha kidogo na kusema, "Nimekupenda sana JC. Ulivyo yaani... ni tofauti na wanaume wengine."

"Na Chalii je?" nikamuuliza.

"Ah, Chalii... unaweza kuchukulia hiyo kama biashara tu. Haniridhishi. Naridhika kwako wewe tu," akaniambia hivyo huku akisugua kiuno changu kwa makucha yake.

"Mbona yeye anakupenda? Ukiwa naye hata kama unapata kidogo si unapaswa kuridhika?"

"Ndiyo haniridhishi sasa!"

"Si umwambie? Amekukazimisha uwe naye?"

"Nitamwambia, ila..."

"Siku ukimwambia, mkaachana, ndiyo tutakuwa pamoja. Umenielewa?"

"JC... jamani..."

"Nini? Si Umesema hakuridhishi? Mwambie, mwachane, ndiyo tutakuwa wote. Sawa? Mimi mambo ya kushare siwezi. Ila nakuomba kitu kimoja..." nikamwambia.

"Kitu gani?"

"Itoe mikono yako kiunoni kwangu," nikasema hivyo.

"JC... usinifanyie hivi...."

Kuna watu wakawa wanakuja upande wetu, nami nikaitoa mikono yake kwangu na kuondoka hapo. Alaa!

Nilikuwa nimejitahidi sana kumwonyesha ustaarabu ili aelewe, hii ikiwa mara ya pili. Nadhani alifikiri kwamba ningelegeza tu tena kama jana, lakini alikuwa amekosea. Sasa hivi ndiyo angeuona uchuma wangu uko wapi; tena yeye pamoja na bwana wake mbeba vyuma.

Nikamkuta Tesha akiwa anatembea mdogo mdogo tu kuelekea nyumbani, nami nikajiunga naye mpaka tulipofika getini kwao. Akanishauri kwamba niende tu pale kwa Ankia nikapumzike, akinipa sifa kwa kuwa rafiki mwenye kujali mpaka kuhakikisha nimemfikisha kwao salama, nami nikaona nimkubalie tu.

Nikamwacha na kwenda upande wetu, na gari la Miryam lilionekana mule ndani kwao nilipopatazama kupitia matobo ya uzio, kuonyesha dada mtu alikuwepo tayari. Nikaelekea uani kwanza kukojoa maana ulikuwa umeshanibana tena, kisha ndiyo nikaelekea ndani.

Eh! Tokea tulipoondoka na Tesha ile mchana ndiyo mpaka sasa hivi nilikuwa naingia ndani hapo, nami nikamkuta Ankia akiwa ameketi kwenye sofa huku akiangalia TV.

Wakati huu alikuwa amevaa T-shirt nyeupe yenye mikono mifupi, nyepesi kuonyesha michoro ya sidiria aliyovalia kwa ndani, pamoja na khanga iliyofunika umbo lake la chini mpaka kufikia miguuni. Alikuwa amekaa kwa njia ya kushika tama huku akiniangalia sasa baada ya mimi kuingia, akitarajia nimpe salamu bila shaka, lakini nikaufunga tu mlango na kisha kumpita bila kumsemesha hata kidogo.

Nikaingia chumbani kwangu, nami nikavua nguo zote na kisha kuvaa pensi nyepesi na kaushi ili niende kujimwagia maji kisha nirudi kupumzika. Ingawa pombe ilikuwa inazunguka kichwani, niliweza kutambua kwamba chumba hicho kilitoa harufu ya mbali ya dawa za mbu, kitu kilichoonyesha kwamba Ankia alikuwa amenifanyia wepesi wa kuchoma dawa humo ili kuniondolea kero za mbu.

Nikajikuta natabasamu tu kwa mbali, nami nikaweka taulo begani na kubeba sabuni kisha kutoka. Nikakuta Ankia akiwa upande wa jikoni akionekana kupakua chakula, naye akaniangalia, lakini mimi nikapita zangu tu na kwenda bafuni. Yeyote angeyaita haya niliyofanya kuwa maringo lakini nilikuwa na maana yangu.

Nikaoga vizuri, joto la mwili likapungua, nami nikarudi ndani tena. Nikakuta Ankia akiwa amekaa kwenye sofa tena, huku mezani kukiwa na sahani ya udongo iliyofunikwa kwa sahani nyingine ya udongo; bila shaka kukiwa na chakula alichopakua. Mimi nikapita zangu tu kama vile sielewi somo, na kabla sijaufikia mlango wa chumba changu, akaniita.

"JC..."

Nikasimama na kumgeukia, nikiona wazi jinsi alivyonionyesha hisia za msisitizo wa kitu fulani kwa namna alivyoniangalia.

"Chakula... uje ule..." akaniambia hivyo kwa sauti ya upole.

Nikakitazama chakula hicho mezani, kisha nikaingia tu chumbani bila kutoa jibu lolote.

Nilielewa jinsi gani ya kushughulika na huyu mwanamke, na mpaka kufikia hapo ilikuwa wazi kwamba alitaka kunionyesha ananijali. Sikumlipa kwa haya yote aliyokuwa ananifanyia, lakini ikiwa kuna sehemu yoyote ndani ya fikira zake iliyotegemea nimlipe fadhila alizonionyesha kwa njia YOYOTE ile, basi nilitakiwa kuhakikisha anafuta mawazo hayo. Nilikumbuka vizuri sana yote ambayo Tesha alinieleza kuhusu Ankia, kwa hiyo hili suala ningelikamilisha muda huu huu; ndiyo mambo mengine yafate.

Nikajipaka mafuta yangu na kuzitengeneza nywele vyema, nikiwa na lengo la kutaka kwenda tena sebuleni ili nizungumze na Ankia kikubwa, lakini mlango wa chumba ukagongwa. Nikijua wazi huyo ni nani, sikutoa itikio lolote na kuendelea kurudishia vitu vyangu sehemu yake ili nikaufungue, ila nadhani kwa kufikiri sikutaka kumfungulia, Ankia akaufungua mwenyewe na kuingia taratibu.

Nikamwangalia. Mikononi aliibeba ile sahani yenye chakula, naye alikuwa ananiangalia kwa macho yenye kutia huruma sana. Yaani ilikuwa kama vile mtu ambaye amefanya kosa kubwa na sasa anatafuta njia za kupata msamaha, na mimi kiukweli sikufurahishwa na hali ya namna hiyo kutokana na kunipa hisia ya kujiona mwonevu.

Akasema, "JC... nimekuletea chakula."

Sikumjibu. Nikaendelea tu kutulia.

"JC nakuomba tu upokee... ule hata kama umekunywa. Nimekupikia chakula kizuri," akaniambia hivyo.

Nikakaa kimya.

"Nijibu basi. Mbona unakuwa hivyo?"

"Uliniambia nisikusemeshe," nikamjibu hatimaye.

"JC... nisamehe. Naomba tuyasahau hayo... niliongea tu kwa hasira. Nisamehe..."

"Kwa nini unahitaji sana nikusamehe, Ankia?" nikamuuliza.

Akabaki kunitazama tu.

"Njoo. Kiweke chakula hapo..." nikamwambia hivyo.

Nikakaa kitandani, naye akakipeleka chakula kwenye meza na kukiweka kwenye nafasi ndogo iliyoachwa, kisha akaja usawa wangu na kusimama. Nikaushika mkono wake na kumvuta ili akae kitandani kabisa, naye akakaa. Alikuwa ananiangalia kwa macho yenye hisia sana, nami nikawa namwangalia kwa umakini.

"Sijalewa sana, kwa hiyo yote nitakayokwambia ujue nayamaanisha. Umenielewa?" nikamsemesha.

Akatikisa kichwa kukubali.

"Sisi ni binadamu, sawa? Kila mtu ana mapungufu... unajua hilo. Ukiona mtu anafanya jambo usilokubaliana nalo na ukahitaji kuzungumza naye, jitahidi tu kuwa msikilizaji mzuri pia. Huwezi kujua mambo yako vipi kwa upande wake mpaka na yeye uwe umemsikiliza. Hiyo ni kitu ambayo sisi sote tunatakiwa kuwa nayo, na wengi kuikosa ndiyo kunafanya migogoro iwepo. Ukipanick na kuzungumza tu kwa hasira bila kusikiliza... ndiyo mambo kama haya hutokea. Sasa... mimi nakuweka wazi kwa jambo moja. Huwa sipendi kuhukumiwa vibaya hasa na mtu ambaye hanijui vizuri. Wewe ni mwanamke. Nimekukuta hapa. Hatufahamiani vizuri. Ikiwa kuna mambo hupendi nifanye hapa kwako, hasa, ukiwa kama mwanamke, unaniambia, na ninayafata. Ikitokea nimekiuka sheria za hapa, ongea nami, nisikilize pia... kwamba aa, hapa kweli Ankia nimekosea, basi tuangalie hili lisijitokeze tena. Lakini ukianza tu kunirushia maneno... unajiweka position mbaya mpaka nami naanza kutenda vibaya... sipendi hivyo..." nikamwambia hayo kwa upole.

"Ndiyo maana nimekuomba msamaha. Sipendi unikasirikie JC... muda ule nilikuwa najihisi vibaya tu ila..."

"Ankia... nisikilize. Mimi, ama mtu mwingine yeyote yule, kamwe... narudia, kamwe, hapaswi kukufanya uogope kuongoza maisha yako kwa njia unayotaka. Sijui unanielewa?" nikamwambia hivyo.

Akatikisa kichwa kuonyesha uelewa.

"Nimekukuta hapa, una style ya maisha yako, nami nina style ya maisha yangu. Tunapoishi pamoja ndiyo tunajikuta tunafaana ama kutoendana kwa mambo mengi, lakini usiwe mtu wa kuyumbishwa kutoka kwenye misimamo yako eti kisa unaogopa nitakukasirikia kwa sababu nina ya kwangu. Mimi ni nani? Si nimekuja juzi tu? Haukuwa unaendesha maisha kivyako kabla sijaja?"

Akatikisa kichwa kukanusha hilo.

"Sasa? Kwa nini uwe hivyo? Ankia wewe bado ni kijana. Mtu mzima kijana. Sasa hivi mambo siyo kama yalivyokuwa zamani. Usipende kushikilia sana vitu ambavyo vimepita, hautabadili chochote kwenye maisha na utu wako. Hebu jiachie. Kuwa mtu bora unayeweza kuwa badala ya kubaki kujiona kama mnyonge kwa mambo ambayo yameshapita..."

Akawa ananiangalia kwa macho makini zaidi, akionekana kuivuta maana ya maneno yangu kwa kina.

"Mimi Ankia nakwambia ukweli. Nimekuja huku kupumzika tu. Kuishi maisha mengine. Sijaja kuwa kiongozi wa maisha ya mtu. Sijaja kuwa mume wako Ankia. Usinione mimi kama mume wako. Mimi ni rafiki yako. Ukitaka sukari, nakupa kama ninayo. Nikikuomba kitu kizuri ukakataa kunipa kwa sababu zako, me ni nani nikulazimishe?"

"Me siwezi kukunyima..."

"Umeona? Ni WEWE. Ni maamuzi yako. Haya mambo tunayofanya kufurahishana, ni ya kawaida tu. Usiwe unayashikilia sana cause at the end of the day, mwenzako akija kuachia, anayebaki kuumia ni wewe..." nikamwambia hivyo kwa upole.

Akatazama chini na kusema, "Natakiwa kujiachia. Niishi kwa uhuru zaidi."

"Eeeh. Usijali yaani just... ishi. Free kabisa," nikasema.

Akaniangalia na kusema, "Je kama nikisema nakupenda? Utaishi nami kwa kujiachia namna hiyo hiyo hata tukifanya mahusiano?"

"Hilo neno naambiwa sana Ankia kiasi kwamba lilishagakuwa la kawaida mno. Nakwambia hivi kwa sababu nakuona wewe ni rafiki... mimi maisha ya kupendana mpaka kuishi wote, sijui, mume na mke... siwezi. Ukinikubali nikakuelewa, tunatoka. Nikiona unazingua, ninang'oka. Ndivyo nilivyo. Masuala ya kufatiliana sana... a-ah. Nikikwambia nakupenda kama rafiki, elewa iko hivyo tu. Lakini hata kama nikitaka tulale wote na tukalala, hiyo haimaanishi ndiyo nimekupa kibali cha kuning'ang'ania. Hivyo ndivyo JC alivyo... nadhani umeelewa..."

Aliniangalia kwa macho yenye hisia sana, lakini kama vile hisia za kuvunjika moyo, naye akatikisa kichwa kuonyesha uelewa.

"Me nakuelewa sana Ankia. Wewe mwenye nyumba wangu, una moyo mzuri, ndiyo maana nakuweka wazi kwa haya mambo. Usiwe mtu wa kuweka matarajio mengi sana kwenye mambo mengi ili yasije kukuachia maumivu pale yakienda kinyume na ulivyodhania. Umeelewa?" nikamwambia hivyo.

"Ndiyo. Nimeelewa."

"Wala hata hukuwa na haja ya kuomba samahani kwa sababu jana kiukweli... nilikosea. Joy alilazimu tu mambo ila nakuahidi haitatokea tena. Hii ni nyumba yako, na hiki ni chumba chako pia. Sawa?" nikasema.

Akatikisa kichwa kukubali.

"Halafu ulikuwa unapiga hodi ya nini wakati hadi dudu langu ushashika?" nikamuuliza hivyo kiutani.

Akaniangalia na kucheka kwa haya kiasi, nami nikatabasamu pia.

"Umepika nini?" nikamuuliza.

"Ubwabwa, nyama, mchicha. Nikupe ule?" akaniuliza pia.

Nikamshika kiunoni kichokozi na kumwambia, "Vipi ukinipa hiyo tamu nyingine kwanza?"

Akacheka kwa aibu na kufunika uso wake kwa kiganja.

Nikamwambia, "Nakutania tu. Singependa u..."

"Hapana JC... nataka. Nimekuelewa vizuri, usijali. Sitakuwa namna hiyo tena. Ila nakuhitaji sana. Toka juzi ulivyokuja... ninawashwa mno kwa ajili yako..." akaniambia hivyo.

"Wee! Sikujua una maneno ya namna hiyo..."

"Haujui mengi kunihusu mimi pia... na ndo' nataka nikuonyeshe..."

"Wacha we!"

Akacheka kidogo.

"Em' nionyeshe basi..." nikamwambia.

"Nitakuonyesha kesho. Sa'hivi kula, me naenda kulala. Sawa?" akaniambia.

"Aaaa... kwa nini siyo sa'hivi?"

"Ahahah... umelewa wewe..."

"Sijalewa bwana..."

"Hata kama... me nataka unipe ukiwa fresh..."

"Au siyo?"

"Ndiyo."

"Ahahah... fresh. Naona umeanza kujiachia kweli, na ninafurahi tu kujua umenielewa. Ngoja nile msosi wako ili kesho kweli niyaonje hayo mahanjumati yako," nikamwambia hivyo na kumbonyeza pajani.

Akacheka kidogo na kisha kusimama.

Nikawa namwangalia tu kiunoni, naye akanishika shavuni na kisha kunibusu kwenye paji la uso wangu kama wazungu eti, kisha akaanza kuondoka. Nikashusha pumzi ya utulivu na kuinamisha uso wangu. Nilikuwa nimeamua kumwonyesha Ankia upande wa utu wangu ambao sikuufurahia sana; sababu nikizijua mimi mwenyewe.

Nilihitaji atambue kuwa mimi nisingeweza kuwa kile alichodhani ningekuwa katika maisha yake, na nilipanga kumfanya awe mtu wa kuona mambo kwa njia nyepesi zaidi badala ya kuruhusu mapito tu ndiyo yamwogopeshe kuishi maisha mengine. Kama angeona hayo hayafai, basi sawa tungeishi kawaida tu. Lakini kama alitaka kujichanganya na mimi, basi chochote ambacho ningempa ingekuwa kwa njia ya kirafiki tu. Si ndiyo kazi ya marafiki? Kusaidiana.

Lakini sikuwa nimekuja hapa kutengeneza maisha pamoja na mwanamke huyu, na kama hilo alilielewa kweli basi tungeendesha maisha vyema, nami ningemwonyesha namna ya kuishi maisha mengine ya kujifurahisha bila kushikilia sana vitu mpaka impe wakati mgumu kuviachia. Maisha ndiyo yalivyo siku hizi, na inaonekana yeye aliyataka yale ya akina Dev na Ottoman, lakini hii ni Bongo, kwa hiyo angetakiwa kuishi kama mbongo kweli.

Mimi nikavuta tu chakula chake baada ya hayo na kula kiasi, kikiwa kitamu kweli, na baada ya kushiba nikarudisha sahani mezani na kisha kwenda kuzima taa; huyoo kitandani kuutafuta usingizi. Bila shaka kesho ingekuwa na mambo kama yote yenye kusisimua, nami nikajiachia zaidi kitandani hapo ili usingizi uje kunibabua vizuri.


★★★


Nilikuja kuamka kukiwa kumeshakucha vyema, nami nikawa nasikia sauti za mbali kiasi za mtu akifoka kutokea huko nje. Ah sikuzijali sana na kuchukulia kuwa mambo ya waswahili tu, nami nikajinyoosha-nyoosha wee mpaka nilipoamua kunyanyuka kutoka kitandani.

Bado nilikuwa na wenge la usingizi, nami nikafikicha macho na kuvuta simu yangu. Muda ukiwa ni saa nne asubuhi, kukiwa na jumbe kadhaa kutoka kwa marafiki na missed call pia. Nikajibu nilizoziona kuwa muhimu, na ya mtu mmoja ikanifanya nitabasamu.

Ilikuwa ni ujumbe kutoka kwa Soraya, mwanamke mweupe aliyefanya kazi dukani kwa bibie Miryam, naye alikuwa amenitumia jumbe za salamu na kuniambia niamke maana ilionekana nilipenda sana kulala. Nikamjibu kuwa ndiyo nimeamka sasa hivi na kuuliza kama alikuwa poa.

Nikiwa nasubiri jibu, nikaweka umakini zaidi juu ya hiyo sauti iliyokuwa ikiongea kwa njia ya kufoka huko nje, au kulalamika, sikujua. Ilikuwa ya mwanaume, akizungumza kwa hasira, lakini maneno yake hayakufikia vyema masikio yangu.

Kwa kuona Soraya amekawia kujibu, ikabidi niweke simu pembeni na kisha kuvaa pensi na T-shirt ili kwanza nikaonane na mama mwenye nyumba wangu. Bila shaka nilitarajia mambo mazuri kutoka kwake kwa asubuhi hii, na nilipotoka chumbani kwangu kuelekea sebuleni, hakukuwa na mtu.

Usafi na mpangilio mzuri wa vitu ulionekana vyema kumaanisha Ankia alikuwa amekwishaamka, lakini hakuwepo hapo. Sauti ya mwanaume huyo huko nje iliendelea kutoa maneno kwa njia ya kulalamika, ikiwa kama ugomvi, nami nikagonga mlango wa chumba cha Ankia na kumwita, lakini hakuitika. Nikaamua nitoke ndani.

Nilipofika hapo nje, yaani siyo kule nje ya geti kabisa, niliweza kuona kupitia yale matobo kwenye ukuta uliotenganisha nyumba yetu na ya kina Tesha watu wakiwa wamesimama usawa wa geti, na japo sikuwaona vyema sana lakini niliwatambua wawili kuwa Tesha mwenyewe pamoja na mama mkubwa mweusi. Sauti ya mwanaume huyo ilitokea nje ya geti lao, na kwa hapo sikuweza kumwona.

Nilipoangalia upande wa geti letu kuelekea nje, ningeweza kuona kwamba idadi ya watu waliokuwa wamekusanyika huko ilikuwa kubwa, kama kuonyesha wanashuhudia tukio fulani, nami nikawa nasikia malalamiko ya mwanaume huyo.

"...umekalia ujinga tu! Watoto hawa? Mtoto huyu? Unamwendekeza tu... nazipata habari zake ZOTE! Anarudi usiku amelewa, unamwangalia tu! Ndiyo matunzo bora hayo? Eti wanajamii, hivyo ndiyo tunalea watoto siku hizi? Jitu zima limekaa kubebwa tu... na wewe ni mpumbavu sana! Unawaleaje? Eh? Kwa misingi ipi? Unajionyesha una msimamo sana wakati huwezi hata kusimamia vyote vilivyoachwa na kubaki umejibweteka tu...."

Mh? Huyu mtu alikuwa nani? Alikuwa akiongea na nani?

Nikasikia sauti ya Zawadi mweupe ikisema, "Joshu... hebu acha! Unatudhalilisha hivi kisa nini? Eh? Umeshindwa kuingia ndani mpaka..."

"Niingie ndani kufanyaje? Nataka watu wote wajue na kuziona rangi za huyu mpumbavu leo... ataelewa tu!" mwanaume huyo akasema.

"Joshu!" sauti ya Zawadi mweupe ikanena hivyo.

Hapo kulikuwa na jambo zito lililokuwa likiendelea, nami nikawaza kuwa bila shaka Ankia angekuwa huko nje. Ni nini kingine ambacho kingesisimua zaidi kwa asubuhi hii kama siyo kujua familia ya Miryam ilikumbwa na nini? Ningehitaji kujua.



★★★★★★★★★

ITAENDELEA

★★★★★★★★★

Full Story WhatsApp or inbox

Whatsapp +255 678 017 280
 
MIMI NA MIMI

A Story by Elton Tonny

Familia, Urafiki, Mapenzi, Kazi, Tamaa, Hila, Usaliti, Siri, Mambo Yasiyotazamiwa

R-rated 18+

Enjoy!


★★★★★★★★★★★★★

SEHEMU YA SABA

★★★★★★★★★★★★★


Lakini nikatuliza zaidi akili na kuanza kuona mawazo ya namna hiyo kuwa ya kipuuzi. Ikiwa mwanaume huyo alikuwa na lengo la kunidhuru eti kisa nimetoka na mwanamke wake, basi ningehakikisha naanguka chini pamoja naye akifanya jambo lolote kuniangusha. Hii ni njia ya kumaanisha kwamba nilikuwa na ujasiri wa kupokea lolote lile ambalo angelileta upande wangu, kwa hiyo nikaamua kuendelea kutulia na kutazama mechi.

Bobo akaanza kumsemesha Tesha kirafiki kuhusiana na mechi iliyokuwa inaendelea, na kijana akawa anazungumza naye pia. Ni mimi pamoja na yule "mwenye Masai" ndiyo pekee ambao hatukuongea, na kila mara nilipovuta chupa ya bia ili kunywa, ningekuta ananitazama usoni, nami ningeonyesha kutojali kabisa alichowaza kunielekea kwa kurudisha umakini wangu kwenye TV.

Lakini nadhani alikuwa anajaribu kunisoma, hasa shauri ya mimi kuwa mgeni hapa. Alitaka kuona shobo zangu zimekaa vipi, na mimi kiukweli sikuwa mtu wa shobo, kwa hiyo aidha nilimpa ama sikumpa kile alichotarajia; angejua mwenyewe.

Dakika si nyingi sana kupita na wahudumu wawili wakawa wamekuja. Yule aliyetuletea bia mwanzoni pamoja na kengine kafupi na keupe kenye mwili namba nane, mmoja akiwa amebeba kontena lenye bia na mwingine sahani yenye mishikaki ya nyama za mbuzi kama miti 20 hivi. Bila shaka zilikuwa zinapelekwa kwa "boss," navyo vikawekwa kwenye meza yao na vinywaji kufunguliwa.

Sikujishughulisha nao kabisa. Bobo alikuwa ameanza kuongea na huyo jamaa kuelekea mechi pia, nami nikawa namsikia akitoa maoni yake kuhusu uchezaji wa Simba. Alikuwa na sauti nzito lakini iliyotulia, akionekana kuwa na aina fulani hivi ya mridhiko.

Nilipovuta bia tena, nikamwona anamsemesha mhudumu mmoja huku akinyooshea kidole chake upande wangu, naye Tesha akaniangalia kwa yale macho yenye kumaanisha aliona jambo hilo, nasi tukaendelea tu kutulia mpaka wahudumu hao walipotoka ndani hapo.

Bobo akanisemesha kwa kunikaribisha nichukue mshkaki, mimi pamoja na Tesha, nami nilipomwangalia bosi mkuu, akanionyesha ishara kwa kiganja chake kwamba nichukue kweli. Ilikuwa kwa njia tulivu tu, nami nikatikisa kichwa kukubali.

Tesha akaanza kuchukua huku akitabasamu kiasi, nami pia nikabeba mmoja na kuanza kutafuna. Sikuwa nimesahau kuhusu bastola ya jamaa huko nyuma ya kiuno, na kama hili lilikuwa jaribio lake kwangu ama basi tu aliamua kufanya haya kwa nia zozote, mimi ningeendelea kutulia tu mpaka mechi iishe, kisha niamshe na Tesha. Basi.

Si dakika nyingi sana kupita nao Simba wakawa wamefunga bao moja. Tukashangilia pamoja, na Bobo, yule baunsa, pamoja na Tesha ndiyo ambao walikuwa na kelele za ushabiki kutokana na furaha waliyopata, ila mimi na jamaa mkuu, ilionekana kama tulikuwa tunavutiana manati vile halafu mawe hatuyaachii. Utulivu niliokuwa nao na yeye ndiyo alikuwa nao hivyo hivyo, tukijiweka kama watu fulani maalumu kweli sehemu hiyo. Na nafikiri alipendezwa na hilo.

Wale wahudumu wakawa wamerudi tena, wakiwa na makontena yenye bia za Serengeti Lite 20. Zikawekwa mezani kwetu mimi na Tesha, kumi kwangu, kumi kwake. Tesha akamwambia mwanaume huyo anashukuru sana, ikiwa wazi ni huyo jamaa ndiye aliyekuwa ametununulia, na Tesha akasema hapo angezipiga zote kusherehekea ushindi wa Simba ambao bila shaka ungeletwa kwa magoli mengine zaidi.

Lakini mimi hata sikutoa shukrani. Nikaendelea tu kutulia, nikinywa taratibu tu, nikitoka kwenda kukojoa na kurudi tena kukaa, na mara kwa mara tulipoangaliana na jamaa, angenitikisia kichwa kidogo kuonyesha uwana, nami ningemrudishia kutikisa kichwa kidogo na kuendelea na mambo mengine.

★★

Tukaendelea kukaa humo mpaka kufikia kipindi cha pili cha mechi, Simba wakiongeza magoli mengine mawili bila kurudishiwa hata moja, na ndiyo kwenye dakika za mwishoni akawa amefika Joy ndani hapo. Mwanamke huyo alikuwa amependeza sana pamoja na wanawake wengine wanne alioingia nao.

Alivalia blauzi nyepesi kama kaushi, iliyoacha sehemu kubwa ya kifua chake ionekane wazi, fupi kuonyesha kitovu chake, pamoja na pensi ya skinny nyeusi iliyovutwa juu kufikia kiunoni na kumchora vizuri sana pale kati. Mapaja yake yalikuwa wazi, miguuni akivaa ndala za manyoya, na kichwani alikuwa amesuka kwa mtindo mwingine leo hii wa nywele laini kama za wazungu, huku usoni akijidodeka mapodozi na kope fupi za bandia machoni.

Wenzake pia walikuwa wamevaa blauzi laini, suruali zenye kubana, vikaptura, misuko ya aina mbalimbali na mawigi, wakionekana kuwa na lengo la kuja kufanya umalaya tu sehemu hiyo; kunywa na kutafuta pesa kwa wanaume yaani.

Joy alipoingia na macho yetu kukutana, akaachia tu tabasamu la kirafiki kutuelekea sisi wote ndani hapo, huku Bobo akianza kumsemesha na yeye kuongea naye. Akamsalimia Tesha kwa kumshika kiganja, kisha akaja kwangu pia na kukishika cha kwangu kisalamu.

Tulipokuwa tumeviunganisha viganja vyetu, nikahisi kucha ya kidole chake kilichokunjwa ikinisugua katikati ya kiganja kwa makusudi kabisa, nami nikakitoa changu kwake na kuendelea kupokea salamu za wenziye.

Akanipita na kwenda mpaka kwa bwana wake, naye akakaa karibu naye na kuanza kuzungumza. Wale wanawake wengine wakawa wamekaa kwenye masofa pia, mmoja mwenye mwili mnene kiasi akiwa karibu nami zaidi, naye Bobo akatoka nje kidogo.

Nilikuwa nimeshakunywa bia nne hivi, Tesha kama sita, nami nikamwona huyo jamaa anamwonyesha Joy ishara ya kidole kunielekea. Nisingeweza kujua kilichoongelewa, lakini nilikuwa tayari kwa lolote. Walilete tu, nami ningewaonyesha nini maana ya jina langu!

Mechi ya Simba ikaisha, na jamaa akaanza kupiga makofi kufurahia ushindi wa magoli matatu kwa bila. Wengine pia wakaanza kumsindikiza kwa makofi na wanawake waliomo humo kusimama ili kuanza kucheza muziki uliowekwa na Bobo. Jamaa ndiyo alikuwa amerudi tu pamoja na wahudumu walioleta vinywaji zaidi, bila shaka kwa ajili ya Joy na wenzake.

Nikawa nimeingia chupa ya tano, vibe likiwa limeshaniingia kitambo, nami nikamwangalia Tesha na kumwona alivyojiburudisha kwa kuongea na mwanamke mmoja kati ya wale wanawake walioingia na kumshika-shika mapajani. Ni wazi alikuwa amelewa, na bila shaka angeendelea kunywa tu. Kwa hiyo ningetakiwa kunywa kistaarabu sana ili kuhakikisha usalama wa huyu kijana pia, hasa ukitegemea dada yake alijua tuko pamoja.

Wahudumu walikuwa wamemletea kiongozi vinywaji kama Konyagi, K-Vant, na Valeur, glasi kadhaa pamoja na soda, bila shaka za kuchanganyia na bia hizo kali. Na wakaanza kuzichanganya kweli. Wale wanawake wakawa wanakunywa na kucheza taratibu muziki ulioendelea, naye Bobo akaniletea michanganyiko hiyo ya pombe ili nami ninywe pia.

Lakini nikakataa, nikisema zingenifanya nijihisi vibaya, naye akampelekea Tesha. Kijana akatae? Nadhani alikuwa ameshaanza kuufurahia huu upendo wa "maVIP" kutoka kwa bosi wa Masai, lakini mimi bado nilikuwa na mashaka yangu. Nikawa nakunywa kwa kutegea tu, huku mwanamke yule pembeni yangu akinishika hapa na pale na mimi kuitoa mikono yake kwangu.

Nilikuwa nimeweka umakini wangu mzuri kujitahidi kuendelea kuwa macho maana haya mambo ya kunyooshewa-nyooshewa vidole sikuyapenda kabisa, na kufikia mida ya saa nne usiku ikawa wazi kwamba wengine humo ndani walikuwa wamelewa vibaya mno. Ni mimi na Joy tu ndiyo ambao tulitegea kunywa sana, mimi nikiwa nazijua sababu zangu, lakini nisiweze kuzijua za kwake. Hata ile michanganyiko hakuinywa japo mtu wake alimsisitizia sana.

Bobo, Tesha na baunsa walikuwa wanaongea kweli, wakicheza na wale wanawake kwa mitindo ya kimahaba, huku bosi mkuu, Joy na mimi pekee ndiyo tukiwa tumekaa tu. Hadi nilikuwa nasogezewa makalio na mwanamke mmoja humo karibu na uso wangu na kitikiswa! Si basi tu? Bangi!

Tesha alipoanza kupasua mpaka na chupa, nikaona hiyo ilitosha sasa. Ningehitaji kumrudisha kijana huyu kwao na nije kujitahidi kutoweka mazoea mengi ya kuwa natoka naye kulewa, maana kufanya hivyo kila siku kungeleta picha mbaya pale kwao.

Nikaimalizia chupa yangu ya tano na kusimama, nisijali kuhusu zingine, nami nikamfata Tesha na kumsihi tuondoke. Akawa ananiambia bado mapema, na nadhani kwa kuniona kuwa nataka kuondoka, yule jamaa akaniponda na kisoda ili avute umakini wangu kwake.

Nikamwangalia, naye akaniita kwa ishara ya kiganja chake. Hata Bobo akanionyeshea ishara kwa kidole kuwa niende hapo, huku kichwa chake kikiyumba, nami nikamwacha Tesha na kwenda kwa jamaa. Serious.

Joy si alikuwa amekaa karibu yake? Jamaa akamwambia asogee pembeni kwenye sofa hilo ili mimi nije kukaa katikati yao, na mwanamke akatii. Wakati mwafaka wa kuijua akili yake kunielekea ndiyo ulikuwa umewadia, nami nikakaa karibu naye.

Akapitisha mkono wake begani kwangu, kirafiki eti, mimi nikiona wazi jinsi pombe ilivyomkonga nyoyoni, hivyo nikaweka umakini zaidi ili nisikie alichotaka kusema.

"Uko poa?" akaniuliza.

Wakati akiwa ananiuliza hivyo, nilianza kuhisi vidole vyake Joy vikinishika pajani na kuanza mipapaso na kunibonyeza sehemu yangu ya siri. Nikajikausha tu.

"Fresh tu," nikamjibu jamaa.

"Kijana uko vizuri sana. Yaani vizuri sana. Na wewe mwanasimba, au siyo?" akaniuliza hivyo.

Nikatikisa kichwa kukubali.

"Penyewe hapo! Unajua nini? Unanijua mimi?"

"Hapana. Ndiyo nakuona leo," nikamwambia.

"Aaa... mimi ndiyo Charles Gonga. Ulizia Chalii Gonga hapa Masai kila kona nafahamika... huwezi kunikosa..." akasema.

Nikatikisa kichwa kukubali, huku kero za Joy bado zikiendelea kunisumbua.

"We' unaitwa nani?" Gonga akaniuliza.

"JC."

"Aaa... kama JC Penney?" akauliza na kucheka.

Nikatabasamu kidogo tu, nikihisi huyu jamaa alikuwa amesoma sana, ama ni utashi tu wa kujua mambo.

"Sasa ngoja nikwambie kitu JC. Unajua kwa nini nimesema uko vizuri sana?" akaniuliza.

Nikatikisa kichwa kukataa.

"Wewe dogo... hauna show za kishamba. Sijui unanielewa? Nimekuangalia hapo... haushoboki kifala yaani. Napenda sana watu wa hivyo. Wewe ni mgeni si ndiyo? Huku Masai?"

Nikatikisa kichwa kukubali.

"Hata mimi nimeona. Wa huku washamba sana. Napenda watu wa level yako. Sijui umenisoma? Yaani... ngoja nikwambie kitu... hapa hivi... wanawake hawa wote hawa... wanakutaka. Sijui umenielewa? Wote. Hadi huyu... Joy... ila hawezi akamwambia maana niko hapa anafikiri nitazingua. Lakini wewe ni mwanaume bwana au siyo? Unajua sisi hatuingizagi miguu yote, uwongo dogo langu?" akaniambia hayo.

"Hamna. Ni kweli kabisa," nikamjibu hivyo, nami nikakishika kiganja chake Joy na kukikandamizia kwenye sofa bila kumgeukia.

"Eee... asa'... nimekuangalia. Haupapariki na wanawake. Wewe kwa mwonekano wako... mimi kwa mwonekano wangu... hivi vitu unajua ni vya kuchezea tu, au siyo? Ukitaka naweza kukupeleka sehemu yenye wanawake, tena nikisema wanawake ni wanawake kweli... huku pamekaa kisenge, Joy ndo' anafunika. Haya yanachojali ni pesa, pombe na kuzaa tu... lakini nataka nije nikutoe... nikupeleke sehemu ambayo utakutana na warembo kaka... wanaojua mikakati na wananyonya mpaka unakufwa ganzi! Sijui unanielewa?"

Kauli hiyo ya mwishoni ikanifanya nicheke kidogo kwa pumzi, nikiwa nimeshaelewa kwamba mwanaume huyo alipenda sana wanawake, na ilieleweka kwa nini hasa kwa sababu alijihusisha na biashara za wanawake kama nilivyoambiwa.

Nikamwambia, "Fresh. Me nimekuelewa."

"Kama vipi tutoke sa'hivi? Bado mapema..." akaniambia.

"Aa... kwa sa'hivi siwezi, kuna ishu nataka kufanya. Labda siku nyingine," nikamwambia.

"Aaa... kwani umeoa? Mapema hii, twende nikuonyeshe mambo mingi wewe! Hizo bia mbili nilizokuwekea hapo? Ndogo sana. Twende upige bia na watoto wa ukweli. Huwezi kuresist..." akanishawishi.

Nadhani alikuwa anataka kunitumia ili kujionyeshea kwa watu fulani, ama labda anihusishe kwenye ishu zake batili, ama huenda hata kuniumiza. Alitoa viashiria fulani vya mtu wa magendo sana, na mimi nilijua jinsi ya kushughulika naye.

Nikamwambia, "Usikonde brother, tutaenda tu. Leo kuna mambo tu nilipanga kufanya mapema kwo' ratiba haitaruhusu. Siku nyingine."

"Au siyo?"

"Yeah," nikamwambia kwa uhakika.

Akanipiga begani kidogo huku akitabasamu, kisha akatoa wallet yake mfukoni na kunipa shilingi elfu kumi. Nikaipokea huku nikimtazama kimaswali.

"Hiyo weka. Nauli. Nitakapokuita usije kusingizia hauna nauli. Ushan'soma? Nipe namba yako..." akaniambia hivyo.

Nikacheka kidogo na kutikisa kichwa kwa kutoamini mambo haya, naye akanipa simu yake ili niandike namba. Nikakiachia kiganja cha Joy ambacho mpaka sasa nilikuwa nimekikandamiza bado, nami nikamwandikia namba upesi na kisha kuitunza kwenye kitabu cha majina cha simu.

"Huyu ni ndugu yako?" Gonga akaniuliza hivyo.

Alimaanisha Tesha, nami nikamwambia, "Ni rafiki yangu."

"Aaa... anapenda kuparty ila hana hela. Tembea kwenye njia moja na mimi JC... utafurahia sana," akaniambia hivyo kilevi.

Kazi nilikuwa nayo! Hili suala la kutengeneza marafiki mpaka wale wanaotembea na bastola liliikereketa sana akili yangu, lakini nikamkubalia tu jamaa na kwenda upande wa choo ili nikojoe kwanza.

Kwa kiasi kikubwa, sikutaka kujenga ukaribu na huyo Chalii Gonga. Yeye ndiyo alikuwa analazimisha, maana aliona simshobokei kama wengine walivyofanya, na hivyo akafikiri nina kitu fulani cha pekee sana cha kumfaidisha nacho. Sijui ikiwa ilikuwa ni sura na mwonekano wangu tu, au labda Joy alimwambia vitu fulani, lakini kwa muda huu sikutaka kujali sana.

Nikamaliza haja na kutoka, na Gonga akanitikisia kichwa kunionyesha namna anavyonikubali pale nilipompita. Nikiwa makini tu, nikamfata Tesha na kumwambia twende, akiwa ameshadata na mpenzi wake mpya wa kulipwa.

Tukatoka, ikiwa ni saa tano sasa, naye Tesha akaniambia kulikuwa na geti lingine la kutokea nyuma ya jengo hilo kwa hiyo tuitumie njia hiyo kuondoka badala ya kupita kule mbele, nami nikaridhia.

Tukaanza kwenda, mwenzangu akiwa amelewa kweli lakini akijitahidi kutembea kwa mhimili mzuri, na ile tumekaribia kutoka getini, nikaitwa.

"JC..."

Kugeuka? Ni Joy. Agh! Pozi likaniisha. Nilitaka tuendelee tu kwenda maana sikuona haja ya kubaki kumsikiliza mwanamke huyo, nami nikamwambia Tesha tuondoke.

Joy akaongeza kasi ya kuja na kusema, "JC, subiri basi..."

"Oyo... mtoto huyo..." Tesha akaniambia hivyo kilevi.

"Ah... twende bana..." nikasema hivyo.

"J... naomba unisikilize..." Joy akasema hivyo baada ya kutufikia.

"Tulia... me nawasubiri hapo nje... ah... nakusubiri hapo nje..." Tesha akaniambia hivyo.

Akatoka nje ya geti na kutuacha hapo, naye Joy akajisogeza karibu yangu zaidi na kunishika kiunoni. Nikawa namwangalia tu kwa mkazo.

"JC... nimekumiss..." akaniambia hivyo.

Nikaendelea tu kutulia.

"Unajua... jana penzi lako lilikuwa tamu sana. Sijakojoa muda mrefu kweli, yaani sijui una nini tu kilichofanya nilegee kama jana..."

Aisee! Nilimwangalia kwa njia isiyoonyesha hisia kabisa, nisiwe na chochote cha kusema maana yote aliyoniambia hayakunipa athari yoyote ile.

"Najua nilikwambia naitaka kwa jana tu, ila leo nimekaa siku nzima nakuwaza mpenzi. Nataka niwe ndani ya mikono yako tena. Nataka unipe... na mimi nikupe mahaba matamu JC..."

Nikaangalia pembeni kiufupi, kisha nikamtazama tena.

"Sema kitu basi..." akaniambia.

"Kitu," nikamjibu.

Akacheka kwa madaha kidogo na kusema, "Nimekupenda sana JC. Ulivyo yaani... ni tofauti na wanaume wengine."

"Na Chalii je?" nikamuuliza.

"Ah, Chalii... unaweza kuchukulia hiyo kama biashara tu. Haniridhishi. Naridhika kwako wewe tu," akaniambia hivyo huku akisugua kiuno changu kwa makucha yake.

"Mbona yeye anakupenda? Ukiwa naye hata kama unapata kidogo si unapaswa kuridhika?"

"Ndiyo haniridhishi sasa!"

"Si umwambie? Amekukazimisha uwe naye?"

"Nitamwambia, ila..."

"Siku ukimwambia, mkaachana, ndiyo tutakuwa pamoja. Umenielewa?"

"JC... jamani..."

"Nini? Si Umesema hakuridhishi? Mwambie, mwachane, ndiyo tutakuwa wote. Sawa? Mimi mambo ya kushare siwezi. Ila nakuomba kitu kimoja..." nikamwambia.

"Kitu gani?"

"Itoe mikono yako kiunoni kwangu," nikasema hivyo.

"JC... usinifanyie hivi...."

Kuna watu wakawa wanakuja upande wetu, nami nikaitoa mikono yake kwangu na kuondoka hapo. Alaa!

Nilikuwa nimejitahidi sana kumwonyesha ustaarabu ili aelewe, hii ikiwa mara ya pili. Nadhani alifikiri kwamba ningelegeza tu tena kama jana, lakini alikuwa amekosea. Sasa hivi ndiyo angeuona uchuma wangu uko wapi; tena yeye pamoja na bwana wake mbeba vyuma.

Nikamkuta Tesha akiwa anatembea mdogo mdogo tu kuelekea nyumbani, nami nikajiunga naye mpaka tulipofika getini kwao. Akanishauri kwamba niende tu pale kwa Ankia nikapumzike, akinipa sifa kwa kuwa rafiki mwenye kujali mpaka kuhakikisha nimemfikisha kwao salama, nami nikaona nimkubalie tu.

Nikamwacha na kwenda upande wetu, na gari la Miryam lilionekana mule ndani kwao nilipopatazama kupitia matobo ya uzio, kuonyesha dada mtu alikuwepo tayari. Nikaelekea uani kwanza kukojoa maana ulikuwa umeshanibana tena, kisha ndiyo nikaelekea ndani.

Eh! Tokea tulipoondoka na Tesha ile mchana ndiyo mpaka sasa hivi nilikuwa naingia ndani hapo, nami nikamkuta Ankia akiwa ameketi kwenye sofa huku akiangalia TV.

Wakati huu alikuwa amevaa T-shirt nyeupe yenye mikono mifupi, nyepesi kuonyesha michoro ya sidiria aliyovalia kwa ndani, pamoja na khanga iliyofunika umbo lake la chini mpaka kufikia miguuni. Alikuwa amekaa kwa njia ya kushika tama huku akiniangalia sasa baada ya mimi kuingia, akitarajia nimpe salamu bila shaka, lakini nikaufunga tu mlango na kisha kumpita bila kumsemesha hata kidogo.

Nikaingia chumbani kwangu, nami nikavua nguo zote na kisha kuvaa pensi nyepesi na kaushi ili niende kujimwagia maji kisha nirudi kupumzika. Ingawa pombe ilikuwa inazunguka kichwani, niliweza kutambua kwamba chumba hicho kilitoa harufu ya mbali ya dawa za mbu, kitu kilichoonyesha kwamba Ankia alikuwa amenifanyia wepesi wa kuchoma dawa humo ili kuniondolea kero za mbu.

Nikajikuta natabasamu tu kwa mbali, nami nikaweka taulo begani na kubeba sabuni kisha kutoka. Nikakuta Ankia akiwa upande wa jikoni akionekana kupakua chakula, naye akaniangalia, lakini mimi nikapita zangu tu na kwenda bafuni. Yeyote angeyaita haya niliyofanya kuwa maringo lakini nilikuwa na maana yangu.

Nikaoga vizuri, joto la mwili likapungua, nami nikarudi ndani tena. Nikakuta Ankia akiwa amekaa kwenye sofa tena, huku mezani kukiwa na sahani ya udongo iliyofunikwa kwa sahani nyingine ya udongo; bila shaka kukiwa na chakula alichopakua. Mimi nikapita zangu tu kama vile sielewi somo, na kabla sijaufikia mlango wa chumba changu, akaniita.

"JC..."

Nikasimama na kumgeukia, nikiona wazi jinsi alivyonionyesha hisia za msisitizo wa kitu fulani kwa namna alivyoniangalia.

"Chakula... uje ule..." akaniambia hivyo kwa sauti ya upole.

Nikakitazama chakula hicho mezani, kisha nikaingia tu chumbani bila kutoa jibu lolote.

Nilielewa jinsi gani ya kushughulika na huyu mwanamke, na mpaka kufikia hapo ilikuwa wazi kwamba alitaka kunionyesha ananijali. Sikumlipa kwa haya yote aliyokuwa ananifanyia, lakini ikiwa kuna sehemu yoyote ndani ya fikira zake iliyotegemea nimlipe fadhila alizonionyesha kwa njia YOYOTE ile, basi nilitakiwa kuhakikisha anafuta mawazo hayo. Nilikumbuka vizuri sana yote ambayo Tesha alinieleza kuhusu Ankia, kwa hiyo hili suala ningelikamilisha muda huu huu; ndiyo mambo mengine yafate.

Nikajipaka mafuta yangu na kuzitengeneza nywele vyema, nikiwa na lengo la kutaka kwenda tena sebuleni ili nizungumze na Ankia kikubwa, lakini mlango wa chumba ukagongwa. Nikijua wazi huyo ni nani, sikutoa itikio lolote na kuendelea kurudishia vitu vyangu sehemu yake ili nikaufungue, ila nadhani kwa kufikiri sikutaka kumfungulia, Ankia akaufungua mwenyewe na kuingia taratibu.

Nikamwangalia. Mikononi aliibeba ile sahani yenye chakula, naye alikuwa ananiangalia kwa macho yenye kutia huruma sana. Yaani ilikuwa kama vile mtu ambaye amefanya kosa kubwa na sasa anatafuta njia za kupata msamaha, na mimi kiukweli sikufurahishwa na hali ya namna hiyo kutokana na kunipa hisia ya kujiona mwonevu.

Akasema, "JC... nimekuletea chakula."

Sikumjibu. Nikaendelea tu kutulia.

"JC nakuomba tu upokee... ule hata kama umekunywa. Nimekupikia chakula kizuri," akaniambia hivyo.

Nikakaa kimya.

"Nijibu basi. Mbona unakuwa hivyo?"

"Uliniambia nisikusemeshe," nikamjibu hatimaye.

"JC... nisamehe. Naomba tuyasahau hayo... niliongea tu kwa hasira. Nisamehe..."

"Kwa nini unahitaji sana nikusamehe, Ankia?" nikamuuliza.

Akabaki kunitazama tu.

"Njoo. Kiweke chakula hapo..." nikamwambia hivyo.

Nikakaa kitandani, naye akakipeleka chakula kwenye meza na kukiweka kwenye nafasi ndogo iliyoachwa, kisha akaja usawa wangu na kusimama. Nikaushika mkono wake na kumvuta ili akae kitandani kabisa, naye akakaa. Alikuwa ananiangalia kwa macho yenye hisia sana, nami nikawa namwangalia kwa umakini.

"Sijalewa sana, kwa hiyo yote nitakayokwambia ujue nayamaanisha. Umenielewa?" nikamsemesha.

Akatikisa kichwa kukubali.

"Sisi ni binadamu, sawa? Kila mtu ana mapungufu... unajua hilo. Ukiona mtu anafanya jambo usilokubaliana nalo na ukahitaji kuzungumza naye, jitahidi tu kuwa msikilizaji mzuri pia. Huwezi kujua mambo yako vipi kwa upande wake mpaka na yeye uwe umemsikiliza. Hiyo ni kitu ambayo sisi sote tunatakiwa kuwa nayo, na wengi kuikosa ndiyo kunafanya migogoro iwepo. Ukipanick na kuzungumza tu kwa hasira bila kusikiliza... ndiyo mambo kama haya hutokea. Sasa... mimi nakuweka wazi kwa jambo moja. Huwa sipendi kuhukumiwa vibaya hasa na mtu ambaye hanijui vizuri. Wewe ni mwanamke. Nimekukuta hapa. Hatufahamiani vizuri. Ikiwa kuna mambo hupendi nifanye hapa kwako, hasa, ukiwa kama mwanamke, unaniambia, na ninayafata. Ikitokea nimekiuka sheria za hapa, ongea nami, nisikilize pia... kwamba aa, hapa kweli Ankia nimekosea, basi tuangalie hili lisijitokeze tena. Lakini ukianza tu kunirushia maneno... unajiweka position mbaya mpaka nami naanza kutenda vibaya... sipendi hivyo..." nikamwambia hayo kwa upole.

"Ndiyo maana nimekuomba msamaha. Sipendi unikasirikie JC... muda ule nilikuwa najihisi vibaya tu ila..."

"Ankia... nisikilize. Mimi, ama mtu mwingine yeyote yule, kamwe... narudia, kamwe, hapaswi kukufanya uogope kuongoza maisha yako kwa njia unayotaka. Sijui unanielewa?" nikamwambia hivyo.

Akatikisa kichwa kuonyesha uelewa.

"Nimekukuta hapa, una style ya maisha yako, nami nina style ya maisha yangu. Tunapoishi pamoja ndiyo tunajikuta tunafaana ama kutoendana kwa mambo mengi, lakini usiwe mtu wa kuyumbishwa kutoka kwenye misimamo yako eti kisa unaogopa nitakukasirikia kwa sababu nina ya kwangu. Mimi ni nani? Si nimekuja juzi tu? Haukuwa unaendesha maisha kivyako kabla sijaja?"

Akatikisa kichwa kukanusha hilo.

"Sasa? Kwa nini uwe hivyo? Ankia wewe bado ni kijana. Mtu mzima kijana. Sasa hivi mambo siyo kama yalivyokuwa zamani. Usipende kushikilia sana vitu ambavyo vimepita, hautabadili chochote kwenye maisha na utu wako. Hebu jiachie. Kuwa mtu bora unayeweza kuwa badala ya kubaki kujiona kama mnyonge kwa mambo ambayo yameshapita..."

Akawa ananiangalia kwa macho makini zaidi, akionekana kuivuta maana ya maneno yangu kwa kina.

"Mimi Ankia nakwambia ukweli. Nimekuja huku kupumzika tu. Kuishi maisha mengine. Sijaja kuwa kiongozi wa maisha ya mtu. Sijaja kuwa mume wako Ankia. Usinione mimi kama mume wako. Mimi ni rafiki yako. Ukitaka sukari, nakupa kama ninayo. Nikikuomba kitu kizuri ukakataa kunipa kwa sababu zako, me ni nani nikulazimishe?"

"Me siwezi kukunyima..."

"Umeona? Ni WEWE. Ni maamuzi yako. Haya mambo tunayofanya kufurahishana, ni ya kawaida tu. Usiwe unayashikilia sana cause at the end of the day, mwenzako akija kuachia, anayebaki kuumia ni wewe..." nikamwambia hivyo kwa upole.

Akatazama chini na kusema, "Natakiwa kujiachia. Niishi kwa uhuru zaidi."

"Eeeh. Usijali yaani just... ishi. Free kabisa," nikasema.

Akaniangalia na kusema, "Je kama nikisema nakupenda? Utaishi nami kwa kujiachia namna hiyo hiyo hata tukifanya mahusiano?"

"Hilo neno naambiwa sana Ankia kiasi kwamba lilishagakuwa la kawaida mno. Nakwambia hivi kwa sababu nakuona wewe ni rafiki... mimi maisha ya kupendana mpaka kuishi wote, sijui, mume na mke... siwezi. Ukinikubali nikakuelewa, tunatoka. Nikiona unazingua, ninang'oka. Ndivyo nilivyo. Masuala ya kufatiliana sana... a-ah. Nikikwambia nakupenda kama rafiki, elewa iko hivyo tu. Lakini hata kama nikitaka tulale wote na tukalala, hiyo haimaanishi ndiyo nimekupa kibali cha kuning'ang'ania. Hivyo ndivyo JC alivyo... nadhani umeelewa..."

Aliniangalia kwa macho yenye hisia sana, lakini kama vile hisia za kuvunjika moyo, naye akatikisa kichwa kuonyesha uelewa.

"Me nakuelewa sana Ankia. Wewe mwenye nyumba wangu, una moyo mzuri, ndiyo maana nakuweka wazi kwa haya mambo. Usiwe mtu wa kuweka matarajio mengi sana kwenye mambo mengi ili yasije kukuachia maumivu pale yakienda kinyume na ulivyodhania. Umeelewa?" nikamwambia hivyo.

"Ndiyo. Nimeelewa."

"Wala hata hukuwa na haja ya kuomba samahani kwa sababu jana kiukweli... nilikosea. Joy alilazimu tu mambo ila nakuahidi haitatokea tena. Hii ni nyumba yako, na hiki ni chumba chako pia. Sawa?" nikasema.

Akatikisa kichwa kukubali.

"Halafu ulikuwa unapiga hodi ya nini wakati hadi dudu langu ushashika?" nikamuuliza hivyo kiutani.

Akaniangalia na kucheka kwa haya kiasi, nami nikatabasamu pia.

"Umepika nini?" nikamuuliza.

"Ubwabwa, nyama, mchicha. Nikupe ule?" akaniuliza pia.

Nikamshika kiunoni kichokozi na kumwambia, "Vipi ukinipa hiyo tamu nyingine kwanza?"

Akacheka kwa aibu na kufunika uso wake kwa kiganja.

Nikamwambia, "Nakutania tu. Singependa u..."

"Hapana JC... nataka. Nimekuelewa vizuri, usijali. Sitakuwa namna hiyo tena. Ila nakuhitaji sana. Toka juzi ulivyokuja... ninawashwa mno kwa ajili yako..." akaniambia hivyo.

"Wee! Sikujua una maneno ya namna hiyo..."

"Haujui mengi kunihusu mimi pia... na ndo' nataka nikuonyeshe..."

"Wacha we!"

Akacheka kidogo.

"Em' nionyeshe basi..." nikamwambia.

"Nitakuonyesha kesho. Sa'hivi kula, me naenda kulala. Sawa?" akaniambia.

"Aaaa... kwa nini siyo sa'hivi?"

"Ahahah... umelewa wewe..."

"Sijalewa bwana..."

"Hata kama... me nataka unipe ukiwa fresh..."

"Au siyo?"

"Ndiyo."

"Ahahah... fresh. Naona umeanza kujiachia kweli, na ninafurahi tu kujua umenielewa. Ngoja nile msosi wako ili kesho kweli niyaonje hayo mahanjumati yako," nikamwambia hivyo na kumbonyeza pajani.

Akacheka kidogo na kisha kusimama.

Nikawa namwangalia tu kiunoni, naye akanishika shavuni na kisha kunibusu kwenye paji la uso wangu kama wazungu eti, kisha akaanza kuondoka. Nikashusha pumzi ya utulivu na kuinamisha uso wangu. Nilikuwa nimeamua kumwonyesha Ankia upande wa utu wangu ambao sikuufurahia sana; sababu nikizijua mimi mwenyewe.

Nilihitaji atambue kuwa mimi nisingeweza kuwa kile alichodhani ningekuwa katika maisha yake, na nilipanga kumfanya awe mtu wa kuona mambo kwa njia nyepesi zaidi badala ya kuruhusu mapito tu ndiyo yamwogopeshe kuishi maisha mengine. Kama angeona hayo hayafai, basi sawa tungeishi kawaida tu. Lakini kama alitaka kujichanganya na mimi, basi chochote ambacho ningempa ingekuwa kwa njia ya kirafiki tu. Si ndiyo kazi ya marafiki? Kusaidiana.

Lakini sikuwa nimekuja hapa kutengeneza maisha pamoja na mwanamke huyu, na kama hilo alilielewa kweli basi tungeendesha maisha vyema, nami ningemwonyesha namna ya kuishi maisha mengine ya kujifurahisha bila kushikilia sana vitu mpaka impe wakati mgumu kuviachia. Maisha ndiyo yalivyo siku hizi, na inaonekana yeye aliyataka yale ya akina Dev na Ottoman, lakini hii ni Bongo, kwa hiyo angetakiwa kuishi kama mbongo kweli.

Mimi nikavuta tu chakula chake baada ya hayo na kula kiasi, kikiwa kitamu kweli, na baada ya kushiba nikarudisha sahani mezani na kisha kwenda kuzima taa; huyoo kitandani kuutafuta usingizi. Bila shaka kesho ingekuwa na mambo kama yote yenye kusisimua, nami nikajiachia zaidi kitandani hapo ili usingizi uje kunibabua vizuri.


★★★


Nilikuja kuamka kukiwa kumeshakucha vyema, nami nikawa nasikia sauti za mbali kiasi za mtu akifoka kutokea huko nje. Ah sikuzijali sana na kuchukulia kuwa mambo ya waswahili tu, nami nikajinyoosha-nyoosha wee mpaka nilipoamua kunyanyuka kutoka kitandani.

Bado nilikuwa na wenge la usingizi, nami nikafikicha macho na kuvuta simu yangu. Muda ukiwa ni saa nne asubuhi, kukiwa na jumbe kadhaa kutoka kwa marafiki na missed call pia. Nikajibu nilizoziona kuwa muhimu, na ya mtu mmoja ikanifanya nitabasamu.

Ilikuwa ni ujumbe kutoka kwa Soraya, mwanamke mweupe aliyefanya kazi dukani kwa bibie Miryam, naye alikuwa amenitumia jumbe za salamu na kuniambia niamke maana ilionekana nilipenda sana kulala. Nikamjibu kuwa ndiyo nimeamka sasa hivi na kuuliza kama alikuwa poa.

Nikiwa nasubiri jibu, nikaweka umakini zaidi juu ya hiyo sauti iliyokuwa ikiongea kwa njia ya kufoka huko nje, au kulalamika, sikujua. Ilikuwa ya mwanaume, akizungumza kwa hasira, lakini maneno yake hayakufikia vyema masikio yangu.

Kwa kuona Soraya amekawia kujibu, ikabidi niweke simu pembeni na kisha kuvaa pensi na T-shirt ili kwanza nikaonane na mama mwenye nyumba wangu. Bila shaka nilitarajia mambo mazuri kutoka kwake kwa asubuhi hii, na nilipotoka chumbani kwangu kuelekea sebuleni, hakukuwa na mtu.

Usafi na mpangilio mzuri wa vitu ulionekana vyema kumaanisha Ankia alikuwa amekwishaamka, lakini hakuwepo hapo. Sauti ya mwanaume huyo huko nje iliendelea kutoa maneno kwa njia ya kulalamika, ikiwa kama ugomvi, nami nikagonga mlango wa chumba cha Ankia na kumwita, lakini hakuitika. Nikaamua nitoke ndani.

Nilipofika hapo nje, yaani siyo kule nje ya geti kabisa, niliweza kuona kupitia yale matobo kwenye ukuta uliotenganisha nyumba yetu na ya kina Tesha watu wakiwa wamesimama usawa wa geti, na japo sikuwaona vyema sana lakini niliwatambua wawili kuwa Tesha mwenyewe pamoja na mama mkubwa mweusi. Sauti ya mwanaume huyo ilitokea nje ya geti lao, na kwa hapo sikuweza kumwona.

Nilipoangalia upande wa geti letu kuelekea nje, ningeweza kuona kwamba idadi ya watu waliokuwa wamekusanyika huko ilikuwa kubwa, kama kuonyesha wanashuhudia tukio fulani, nami nikawa nasikia malalamiko ya mwanaume huyo.

"...umekalia ujinga tu! Watoto hawa? Mtoto huyu? Unamwendekeza tu... nazipata habari zake ZOTE! Anarudi usiku amelewa, unamwangalia tu! Ndiyo matunzo bora hayo? Eti wanajamii, hivyo ndiyo tunalea watoto siku hizi? Jitu zima limekaa kubebwa tu... na wewe ni mpumbavu sana! Unawaleaje? Eh? Kwa misingi ipi? Unajionyesha una msimamo sana wakati huwezi hata kusimamia vyote vilivyoachwa na kubaki umejibweteka tu...."

Mh? Huyu mtu alikuwa nani? Alikuwa akiongea na nani?

Nikasikia sauti ya Zawadi mweupe ikisema, "Joshu... hebu acha! Unatudhalilisha hivi kisa nini? Eh? Umeshindwa kuingia ndani mpaka..."

"Niingie ndani kufanyaje? Nataka watu wote wajue na kuziona rangi za huyu mpumbavu leo... ataelewa tu!" mwanaume huyo akasema.

"Joshu!" sauti ya Zawadi mweupe ikanena hivyo.

Hapo kulikuwa na jambo zito lililokuwa likiendelea, nami nikawaza kuwa bila shaka Ankia angekuwa huko nje. Ni nini kingine ambacho kingesisimua zaidi kwa asubuhi hii kama siyo kujua familia ya Miryam ilikumbwa na nini? Ningehitaji kujua.



★★★★★★★★★

ITAENDELEA

★★★★★★★★★

Full Story WhatsApp or inbox

Whatsapp +255 678 017 280
Simulizi imejaa maelezo kuliko matukio. Inakata hamu ya kuifatilia
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom