SIMULIZI: Mama mkwe

SEHEMU YA NANE:

Mume wangu aliendesha gari kwa fujo sana ile siku, ni kama alikua amechanganyikiwa, sikutaka kumuongelesha, nilikua namuogopa, mwanaume niliempenda kwa mapenzi yote leo hii namuangalia kama kitu cha kutisha. Tulifika nyumbani nikapitiliza bafuni kuoga na kujitazama vizuri kwenye kioo cha bafuni, Lahaula....sio kwa alama zile mgongoni, ni kama nilichapwa mijeledi ya kustosha , mgongo ulikua na mistari ya kama kamba nene imepita na pia kwenye ile mistari damu ilivilia....

Dominic akaingia bafuni nadhani alihisi kua Kuna tatizo kubwa zaidi ya yale aliyoyaona kwenye gari, alipoingia na kuona ule mgongo alikaa chini akaanza kulia, sikuweza msogelea hata, Dominic alilia akitamka maneno matatu tu, ' Nisamehe Sana Grace' ....aliyarudia mara nyingi isiyo na idadi. Nilitoka nikamuacha dommy hapo bafuni nikaenda chumbani kwangu nikachukua kioo cha kushika na mkono ili nijichunguze zaidi sehemu zangu za siri, nilikuta pameongezeka ukubwa, ni kama paliingizwa kitu kikubwa sana, na ndipo nilipofahamu kua yale maumivu ninayoyasikia sehemu zangu za siri yatakua yametokana na kulazimishwa kuingizwa kitu iko, yaani nilichanika kiasi.

Nikakaa kutafakari ni kosa gani nililomfanyia mama mkwe lenye kustahili adhabu hii, mbona nilimuonesha heshima sana, mbona nilimuonesha upendo mkubwa, sikupata majibu hata...Dominic alinifata pale kitandani akainama akaniangalia pia maumbile yangu jinsi yalivyosulubiwa, akanikumbatia kwa uchungu mnooo...

Tulijikuta tunalia kwa pamoja, akanambia nilikusihi usibishane na mamangu Grace, nilikusihi, sikumudu kua na subira tena, yale mafunzo yote niliyopewa kabla ya ndoa jinsi ya kuongea na mume niliyasahau ghafla, hasira ilishika mahala pake, yaani mama ake amenitendea hivi bado anamtetea? Huyu ni mwanaume wa aina gani?

Nilinyanyuka nikapack nguo zangu na za mtoto, Dominic alikua ananiangalia tu hasemi kitu, nilimfata mtoto kwa dada nikakuta ameshamuogesha, nikamwambia dada jiandae tunaondoka, nikaita bajaji tukaondoka kurudi tabata. Nikiwa njiani nikawa nawaza narudi nyumbani kuwaambia nini wazazi, niwaambie ukweli au nifiche, nikisema ukweli nitakua nimeiabisha familia ya mume wangu, nikikaa kimya pia nitakua nazidi kuumia,oh God, haya ni mazito, namwambia nani anipe japo msaada wa mawazo...

Nyumbani tulipokelewa na dada wa kazi, mama alikua kazini. Nilimwambia dada nahitaji kulala , usimwambie mama kama nipo, niliingia ndani ,nikanywa dawa za maumivu na kulala. Ilichukua mda kupata usingizi, ndoto za mara kwa mara za kutisha hazikuacha kunifata, nilipoamka mume wangu alikua amepiga simu mara nyingi sana, akanambia naomba upokee kuna jambo la msingi sana nataka nikwambie.

Sikupokea simu kwakweli, nilikua nina hasira zisizo kifani, mume gani alieshindwa kunitetea , sina mume...sina mume...alipoona sipokei akatuma ujumbe kua amemtuma bodaboda alete ile dawa aliyopewa na mama mkwe pale nje wakati tunaondoka kwa mara ya pili, akanambia hata kama namchukia kiasi gani, ile dawa lazma ninywe, hakuna dawa ya maumivu itakayonipa nafuu, alisisitiza sana ninywe dawa...akaishia kwa kumalizia kua ananipenda sana, amepambana sana kutulinda lakini yaliyotokea yapo nje ya uwezo wake....

Baada ya nusu saa, dada wa kazi akaja akanambia kua kuna bodaboda ameleta bahasha, nikaipokea nikaiweka kwenye begi tulilotoka nalo nyumbani kwangu, jioni ilifika na mama akarudi kutoka kazini, alifurahi kuniona ila akashangaa mbona mekuja jumatatu, vipi kuhusu biashara yangu...si unajua wamama tena, nilijikaza nikamwambia nimewakumbuka tu, ila mama tayari alishajua hapa pana tatizo, hakutaka kunisumbua sana na maswali, usiku ukafika na baba nae akarudi, sikufahamu ni kipi mama alimwambia baba ila hakuniuliza maswali kabisa, mda wa chakula tulikula wote kwa upendo na ibada ya usiku ikaanza kama ulivyo kawaida yetu...

Katikati ya ibada nilianguka, mama akapata hofu sana , akazidisha maombi , nilikuja kupatwa na fahamu baada ya masaa mawili, nikakuta familia nzima ipo sebuleni inaniangalia, sikua na uelewa wa nini kilitokea, lakini maumivu ya mgongo pamoja na kichwa vilinifanya nianze kulia kama mtoto mdogo....

Kwa maelezo niliyokuja kuyapata baadae baada ya kupona, miaka miwili baada ya tukio la ukweni ni kua, ile siku ya maombi ya usiku pale nyumbani hadi nikaanguka, nilipoamka nilikua nalalamika kua naumwa sana kichwa na mgongo, mama na ndugu wengine wakapambana kunituliza, kumbuka hapo hakuna mtu anaejua kuhusu dawa ya maumivu iliyoletwa na mume wangu. Msimuliaji anasema nilikua nalia kama mtoto mdogo, nikaanza kujikuna na pia nikawa nafanya fujo sana, nadhani maombi pamoja na zile dawa nilizofanyiwa usiku vilikua vinapambana...

Nililia hadi nikapoteza fahamu, baba akaona haya yamekua makubwa, wakanibeba hadi hospitali, hali yangu ikizidi kua mbaya mnooo, nilikua kama kichaaa, ili nilale ni lazma nichomwe sindano ya usingizi. Mume wangu alipewa taarifa akafika hospitali mapema tu asubuhi yake, kwa maelezo ya msimuliaji ambae ni dada angu wa kazi, maana mama aliomba aendelee kubaki ili asaidie kulea mtoto kwa sababu alikua amemzoea sana...

Nilikaa katika hali ya kukosa ufahamu kwa mda wa miaka miwili, nilikua kichaa kamili, lakini nilikua chini ya uangalizi hospitali ya muhimbili, mume wangu alipambana nami kwa kipindi chote cha matatizo yangu, hakuwahi kosa Kuja kuniona kila alipopata wasaa wa kufanya ivyo, kwa taarifa tu za ndugu wasimuliaji ni kua mama mkwe wangu hakuwahi kukanyaga hospitali hata mara moja....

Ile ratiba ya kumchukua mtoto kila inapofika birthday yake ilikoma maana mtoto alikua chini ya uangalizi wa familia yangu, kwahiyo ile ratiba ya kuadhimisha birthday kwa namna yao ya kipekee kwa mda wa miaka miwili haikuwepo. Mume wangu ni kama aliisusa familia yake, inasemekana hakukanyaga kwao tangu siku aliposikia kua nimepatwa na kichaa...

Mungu ni mwema baada ya miaka miwili ya maombi , huduma za hospitali na upendo wa wazazi, mume na ndugu wachache, nikawa sawa kabisaaa....mume wangu aliwaomba wazazi wangu anichukue , mama alisita maana akilini mwake alijua zile alama mgongoni alizoziona wakati ananihudumia hospitali zilisababishwa na kipigo toka kwa mume wangu maana hakuna ambae alikua anaujua ukweli wa nini hasa kilitokea...

Mume wangu aliwasihi sana kua haitojitokeza tena amejifunza kutokana na makosa, tulirudi nyumbani na maisha yakaendelea kama kawaida....ilipita miaka mingine mitatu ,nikabahatika kupata mtoto mwingine wa kiume, kijana wangu wa kwanza akiwa mkubwa sasa...mama alikuja kunihudumia palepale kwangu maana mume wangu aligoma nisiende popote akasema atanihudumia yeye mwenyewe...

Nilidhani vita na mama mkwe ilikua imeisha, nilijidanganya Grace mimi...hakika nilijidanganya sana....

Itaendelea....





Sent from my itel W6004 using JamiiForums mobile app
Nimefarijika kuwa mama mzazi Ni MTU wa fireeeee,kitaeleweka tuu.
Ni true story au?
 
SEHEMU YA TISA:


VITA YA NNE YA DUNIA....


Walisemaga pepo ya Dunia ipo chini ya miguu ya mama zetu eeeh, niliona simanzi ya mume wangu kutengana na familia yake, hasa mama ake kipenzi, mama aliemlea na kumsimamia tangu utoto , mama aliepambana kama single mom baada ya kifo cha mzee, mama aliegoma kuolewa tena kisa hakutaka kuchanganya dam ya Koo mbili kwa familia yake, leo hii hamudu hata kumpa salamu... nikawaza siku ikitokea familia yangu imenitenga nitamudu kusonga kweli?

Nikampigia mamangu mzazi, nikamueleza yanayomsibu mume wangu, jinsi anapambana kua baba bora, na wakati huohuo abaki kua mtoto bora kwa mamake na kaka bora kwa wadogo zake...mamangu kipenzi akanambia atakuja tuzungumze, yapo mambo japo ni ya familia ya mme wangu ,yeye hayamuhusu, lakini mwisho wa siku mimi nabaki kua mwanae, usalama wangu unamuhusu kwa asilimia nyingi sana.

Mamangu kipenzi alikuja baada ya siku kadhaa, alinambia amekawia kuitikia wito maana alikua katika maombi maalumu kuombea ndoa yangu, mama alinisema sana kwa kuacha kusali na kuishi kwa kumtegemea Mungu. Mama alinambia amefunga siku Saba ili apate maono ya kile kinachonisibu maana ni kama ninasita kuelezea kwa undani.

Mama alinambia mambo mazito sana, alinambia kua kitovu cha kijana wangu wa kwanza nilikipeleka wapi? Sikua na kumbukumbu yoyote maana ni miaka nane sasa tangu nimpate mwanangu wa kwanza. Mama akanambia jaribu kukumbuka, kitovu cha mwanao kinabeba uhai wa mwanao, kiroho ina maana kubwa sana. Nilivuta kumbukumbu kwa utulivu sana, nikakumbuka kua nilimuita mama mkwe nikamuonesha, mama mkwe aliondoka nacho hakunambia zaidi.

Mama alinambia ulipata kumuuliza amekihifadhi vipi? wewe kama mama mzazi wa Lameck unapaswa kufahamu wapi kitovu cha mwanao kimehifadhiwa...niliona mama ananichanganya tu, nimemuita tuzungumzie jinsi ya kurudisha uhusiano wa familia yangu na ya mume wangu, ananambia tena habari ya kitovu cha mtoto, mi nitajuaje, ili kumridhisha nikamwambia mama nitamuuliza dommy labda mama mkwe alimwambia kitu.

Tuliongea habari zingine na mama akaniaga na kuondoka, alichonisisitiza ni kusali kama familia jinsi nilivyolelewa. Nikamuitikia na kumshukuru kwa kuja kunitembelea na kunisikiliza. Mume wangu alirudi kazini, baada ya kula na kupumzika pamoja chumbani nikaona ni muda muafaka nimuelezee kua mama alifika hapa nyumbani mchana, na pia nikamuelezea Kwa kifupi lengo la mama kufika. Nikamwambia najisikia vibaya kwa yanayoendelea yeye kujitenga na familia yake sababu yetu, maana hata mtoto wa pili hamjui bibi wala shangazi.

Mume wangu aliniangalia kwa upendo akanambia,wife...najua una umia sana, Mimi naumia zaidi, umelelewa vema na ndio sababu iliyonifanya nikakuoa mama...nahitaji hayo malezi wayapate wanangu, kuhusu familia yangu sitoweza kuzungumzia, na nakuomba usije kumpigia mama...nipo hapa nitawalinda hadi siku yangu ya mwisho.

Nikamueleza kuhusu mama kuulizia habari ya kitovu cha mtoto, mme wangu alishtuka sana, akanambia mama anajua nini kuhusu kitovu, nikamwambia ameniuliza kua kilihifadhiwa vipi, nami kumbukumbu zangu zinanijia kua nilimpatia mama mkwe...mme wangu aliinama chini aliponyanyuka akawa ameloana na machozi uso mzima...nikamuuliza mbona sikuelewi baba? Akanambia umemuua mtoto grace, umemuua...

Sikuelewa chochote, sikujua natakiwa kusema nini na kwa wakati ule, kumuona mwanaume wangu naemuheshimu sana akilia kama mtoto iliniumiza sana, nikamkumbatia kwa upendo mnooo...nikamwambia am your wife, I think it's time I know what is real going on...aibu yako ni yangu na yangu ni yako...sisi ni mwili mmoja baba...Just tell me...

Akanambia nahofia utaniacha, nikamwambia kama kukuacha ningekuacha ile siku napata ufahamu hospitali na kuambiwa niliugua ukichaa kwa miaka miwili mfululizo na hakuna ndugu ako hata mmoja aliekanyaga hospitali, hadi sasa wewe ni fungu langu, nambie...Dommy akanishika mikono miwili na kuanza kunambia simulizi ya kuogofya mnooo....nikiri tu mimi sio mpenzi wa filamu za kutisha, na kwanini niangalie filamu jicho moja ilhali kuna love films za kutosha tu na zingine nyingi za kupendeza.

Dommy anasimulia....

Nakumbuka nilikua darasa la tatu, babangu mpendwa alianguka ghafla wakati tunapata chakula cha usiku, nilikua mtoto pekee kwa wakati huo, mama alipiga simu wakaja ndugu wa baba waliokua karibu....sifahamu nini kiliendelea lakini kesho yake nyumbani palijaa ndugu wengi waliotoka sehemu mbalimbali...ninachokikumbuka hadi sasa na utoto wangu ni hekaheka zisoisha, kuchanjwa chale na kulishwa madawa ya kila namna...mama hakua na usemi maana ndugu wa baba walikua wengi mahala pale.

Nadhani ndio siku iliyotoka utaratibu maalumu jinsi ya kuadhimisha siku zetu za kuzaliwa, nikaja kufahamu baadae baada ya kukua kua marehemu baba baada ya kutoka masomoni ulaya na kumuoa mama hakutaka kujishughulisha na mila hizo, Sasa mambo yamewazidia na kulikua hakuna namna tena. Baba na mama walikubalina kuadhimisha mila za mizimu maana kwa kucheleweshwa huko ingeondoka na uhai wa baba na uzao wake wa kwanza.

Tumekua tukifanya hivyo kwa miaka mingi, na ndio maana palikua na utulivu, na ndio sababu ya sisi sote kusoma shule za kutwa tena ndani ya mkoa wa dar ili iwe rahisi kufanya matambiko...Grace nisamehe sana, hii miaka yote ambayo unaumwa nimejitenga nao na napambana kuhakikisha mnakua salama...Sitaki wanangu waishi kama nilivyoishi, nipo tayari nilipie gharama ya uhai wenu na tayari nimeshalipia kwa kwenda kijijini na kufanya matambiko ya kafara za wanyama, ila sitotaka kujihusisha chochote na mamangu, nahisi mama aliendelea zaidi na akifanyacho ni zaidi ya matambiko, nahisi mamangu imani ya mizimu ilimchukua sana, na baba alipogundua mama amekua mshirikina , mama aliamua kumuua baba.

Nilibaki nimeachama mdomo wazi, ni familia ya aina gani niliyoolewa nayo ?mme wangu mpenzi akanambia naomba usije kumpigia mamangu...hata akija hapa usithubutu kumruhusu kuingia ndani...nikaona huu sasa ni mtihani mwingine jamani, ni nini hiki kinanikuta grace mimi...

Kesho yake nikasubiri mme wangu ameondoka nikampigia mamangu kumueleza yaliyojiri katika mazungumzo na mme wangu,japo si heshima ila niliona sina namna...haya mambo ni mazito kuliko ninavyowaza. Mama akanisikiliza akanambia ndio maana nilikuuliza kuhusu kitovu cha mwanao, nilishaona katika ulimwengu wa roho kua mwanao hayuko salama...Grace sali sana ....sali mnoooo mwanangu...nami nakuombea lakini ulinzi kamili wa nyumba yako ni wewe...nakuonea huruma maana mama ako mkwe ni adui yako...Mungu akupambanie mwanangu.
 
SEHEMU YA KUMI:

Yalipita mawiki kadhaa, ilikua asubuhi najiandaa kutoka kwenda kwenye biashara zangu, school bus inayombeba Lameck ilikua imeshaondoka kama nusu saa hivi, dada alikuja mbio akanambia mama baba amenipigia simu anasema pokea simu yako.
Nilikua metoka bafuni kuoga, kwahiyo simu itakua ilipigwa wakati nipo bafuni...

Nikakuta missed calls kama nne za mme wangu, sio kawaida yake, niseme tu nilipatwa na mshtuko ila nikajikaza...mme wangu akapiga tena wakati najiandaa kununua salio nimpigie, nikaipokea kwa kihoro...dommy akaniuliza kama nimeshatoka nyumbani, nikamwambia hapana...nipo najiandaa, akanambia usitoke nakuja...nikamuuliza dommy mbona hivyo kuna nini? Akanambia naomba tu nisikilize mke wangu, usitoke nyumbani...

Nikakaa katika msongo wa mawazo, nikamuita dada na kumuuliza baba alipokupigia alisemaje? Dada akanambia alinambia nikwambie upokee simu...nikasema sawa hamna tatizo, nikaamua kutumia huo mda kumsaidia dada kumuogesha mwanangu wa pili, huku nikimsubiria dommy arudi, baada ya kama lisaa na nusu dommy akafika, nadhani foleni ilimchelewesha, dommy akanambia chukua mkoba na vitenge kuna mahala tunaenda, nikamwambia vitenge? vya nini tena? akanambia nitakueleza wife...hebu fanya nachokwambia .

Nikawaza tugombane kisa vitenge tu jamani, nikaingia ndani nikatoka na vitenge viwili, hao tukaingia kwenye gari na safari ikaanza...dommy hakua yule niliyemzoea , muongeaji na mcheshi, akaendesha gari kwa umakini sana hadi Amana hospitali, nikaona nivunje ukimya ....honey hospitali asubuhi yote hii tunakuja kumuona nani? mbona hunielezi vizuri...mme wangu akainama aliponyanyuka alikua ameloana machozi, akanambia nisamehe grace...nimeshindwa kwa mara nyingine kuwalinda, nikiwa katika sintofahamu nikaona gari ya nyumbani kwetu inaingia pale hospitali, baba na mamangu walishuka wakiwa wameongozana na wadogo zangu wote wawili...

Nikaona kama wananichanganya, nikataka kushuka, kwa Kasi Dominic akaniwahi nisifungue mlango, mama na baba wakaja pale tulipopaki gari, baba akafungua mlango na kuniambia grace ....pole mwanangu kipenzi...mama akanichukua hadi nyuma ya gari, akanifunga vile vitenge style ya kinyakyusa, kitenge kikakazwa tumboni...mama akanambia nisamehe grace...sikusimama vema katika kuombea ndoa yako kabla hujaolewa, nisamehe mwanangu...

Nikamwambia mama, wewe ni mamangu mpenzi, naomba uniambie nini kimetokea....mama hakujibu kitu akanikumbatia kwa upendo akanambia atakwambia mmeo...dommy akaja akanambia twende tukamuone mtoto...
Nikapatwa na kama mshtuko wa ghafla, mwanangu ameondoka asubuhi na school bus, mwingine memuacha na dada , huyu naekuja kumuona Amana ni yupi? Baba na mama wakazidi kuniambia nijikaze...

Tukaingia ndani hospitali, badala ya kuelekea wodini tukaelekea upande wa mochwari, nikasimama kwanza, nikawaambia ...hata kama mwanangu yupo hapa, ndio awe huku? hebu acheni masikhara jamani..
Nikaanza kuita jina la Lameck kama mtu aliechanganyikiwa, baba na mme wangu wakashauri nirudishwe kwenye gari, nikarudi pamoja na mama, sikua na nguvu nikakaa chini kwanza.

Nikamwambia mama, mnanikosea ....naomba uniambie kilichotokea, mama akanambia niahidi utakua mtulivu grace, nikamwambia naahidi mama...akanambia gari ya shule aliyopanda Lameck imetumbukia mto msimbazi, watoto kumi kati ya 40 waliokuwepo wamefariki hapohapo kwa kunywa maji, watoto wengine wamesombwa na maji...tupo hapa kuweza kutambua mwili wa Lameck...wewe ni mama unamjua vema mwanao katika hali zote, maiti zimevimba sababu ya majeraha na kunywa maji mengi...jikaze uweze kumtambua mwanao....

Huwezi amini sikuweza hata kulia, nilimuangalia mama nikamwambia twende huko kwenye utambuzi , mama akiwa bado hajaamini kama natumia akili yangu ya kawaida au wazimu umenirudia , akashangaa nimeshanyanyuka na kuelekea walipoelekea baba na Dommy.

Mtoto wako uliemuweka miezi tisa tumboni ni wako jamani...ile bond ni ya ajabu sana, nilizipiga hatua kama kichaa, mama alikua anafanya kazi ya kunikimbiza, mamangu ana mwili kiasi, nilimtesa sana ile siku...
Nikafika huko mochuari , mlangoni nakutana na baba na Dommy, wananishangaa nimefikaje pale,.mara wakamuona mama anakuja mbiombio, mama akafikia kukaa kwanza...

Nikamwambia dommy nipeleke nikamuone mwanangu,dommy akanambia hawajamuona labda atakua katika wale waliondoka na maji, nikamwambia mwanangu yupo hapa nipeleke ...baba akamwambia sawa acha aingie na yeye akaangalie...niliingia ndani, masikini vitoto vyote kumi vilikua vimehifadhiwa sakafuni...vimefunikwa na mashuka ya hospitali, wakasema wameshindwa kuwaweka kwa majokofu ili kurahisisha zoezi la utambuzi, nikapiga jicho moja tu, nikagundua alama ya weusi kwa mbali chini ya jicho la Lameck..mwanangu mpenzi alikua amelala pale chini, mwanangu, malaika wangu alikua amelala pale chini bila uhai...oh dear Lord...
 
Back
Top Bottom