SIASA ZA TANZANIA NA UTAWALA WA KESHO
Siasa ni njia ya kufanya maamuzi katika njia tofauti tofauti katika jamii kwa mfano Miji, Taifa au hata dunia nzima, katika demokrasia kila mtu ana kiasi Fulani cha nguvu, Hivyo tunahitaji mwanasiasa awe na ukweli na uwajibikaji kwani siasa haimaanishi udanganyifu kama unaofanyika hapa nchini kwetu, vyama vya siasa vinatumia uongo mwingi na ahadi za uongo kujipatia kura kutoka kwa wananchi. Tunahitaji siasa safi na bora zaidi ya hii ya sasa ili tuijenge Tanzania iliyo bora na viongozi bora Zaidi wanaoweza kujali wananchi Zaidi ya masirahi yao binafsi.
Hivyo Tanzania ya kesho tunahitaji kua Na;- Upinzani imara bila uoga na vitisho. Tunahitaji siasa inayo maanishwa kweli kama kusudi la kufanya mfumo wa vyama vingi nchini, upinzani kwenye serikali kuu ndio unafanya mabadiliko makubwa nchini, kukemea mienendo isiyo na maana kwa viongozi wakuu nchini, inajenga uongozi bora na hiyo ndio siasa tunayo hitaji nchi hii.
Watu wasio waoga, mfano mzuri tutazame bunge letu la sasa baada ya uchaguzi mkuu wa 2020 upinzani umekua mdogo sana bungeni wengi wao ni wabunge wa Chama kimoja, wengi wao ni kusifia raisi wa jamuhuri tu, vipi kuhusu kuwasemea wananchi walio kupeleka bungeni.
Baadhi yao tunaona wakihoji sana kuhusu serikali wanazimiwa maiki au kupunguziwa muda wao wa kuchangia, kwa kisingizio cha TAARIFA SPIKA kwa mfano may 5, 2017 mkutano wa saba wa bunge, joseph mbilinyi alizimiwa maiki, Hivyo kutengeneza wanasiasa wanao sifia tu kiongozi mmoja, na Uoga wa viongozi kuogopa kuhoji . Tanzania hatuwezi kutoka hapa tulipo kwa namna hii ya siasa zetu Tunahitaji watu wenye nguvu ya kuhoji kwani Hakuna alie juu ya sheria kama katiba yetu ya jamuhuri ya muungano wa tanzania yam waka 1977 (CURT) inavyo eleza katika
Ibara ya 13 (Equality before the law) Iki maanisha hakuna alie juu ya sheria. Hii ndio Tanzania
tuitakayo kisiasa na kiutawala pia na vyote vinawezekana kama tutapata viongozi sahihi. Nchi yetu tunahitaji utawala wa sheria kwa vitendo na sio tu kuwepo kwa nadharia kwamba tunao utawala wa sheria wakati wanasiasa wengi wakiikosoa serikali wanawekwa ndani huo, sio utawala wa sheria, wakati tukiwa na mfumo wa vyama vingi nchini.
Uwajibikaji
Ni hatari sana kwa taifa letu lijalo kuona viongozi wetu wengi wanakua na tabia za UCHAWA. Pia taifa letu linakabiliwa na IMPUNITY (Ukosefu wa uwajibikaji) wale wanaotakiwa kuwajibishwa kwa makosa yao kama ubadhilifu wa fedha kutokana na ripoti za mgaguzi mkuu wa serikali wanaendelea kuwepo kinacho fanywa ni kuhamishwa tu, hii sio Tanzania tuitakayo.
Tunahitaji viongozi wenye maono makubwa na wazalendo katika nchi hii kwa mfano Mbunge mmoja kutoka jimbo la Geita vijijini alitoa hoja yake bungeni kwa kusema nanunuku “Viongozi wanotajwa kwenye ripoti ya CAG Mbona hawawajibishwi mnawahamisha tu? Nchi hii inayo maeneo mengi sana ya wazi wakamatwe wafungwe wapewe mashamba walime hadi pesa walizokula zirudi kupitia kazi hizo” Kwa namna moja au nyingine wazo lake linaweza kusaidia sana.
UWAJIBIKAJI na kutengenea taifa lenye viongozi imara na wenye maono mazuri nan chi yao, sasa kwa sasa nani wa kuwawajibisha kwa makossa yao yanayo jirudia kila mara. Katika bunge la la 10 mwaka 2015 aliekua mbunge wa singida mh. Tundu lissu alisema nanukuu “majaji wamekamatwa wamekura rushwa na riporti ipo mpaka sasa wameachwa bado wanafanya nini?
Wakamatwe na wezi wengine wakiwemo mawaziri wasiachiwe kwenda kula pesa za wizi” mwisho wa kunukuu, Hivyo inaonekana bado kuna changamoto sana nchi yetu kwa upande wa siasa. Hatuhitaji uongozi wa namna hii, kujenga Tanzania bora. Vijana imra wenye hoja thabiti na sio Uchawa na Uoga.
Vijana kwa sasa kuingia kwenye siasa kumekua na ugumu sana ukiangalia mwenendo wa siasa nchini kwetu hapa ukisema vibaya serikali unakamatwa kama ilivyo onekana mwaka 2020 kwenye uchaguzi na baadhi ya wanaharakati wengi kukimbia nchi yao. Nikinukuu maneneo ya baba wa taifa mwalimu nyerere Alisema “Tunataka kuona taifa lina vijana jeuri na wenye kujiamini, vijana wanaojoji na kupiga vita mifumo isiyoshabihana na matakwa na matarajio ya kitanzania.
Tunataka vijana waasi dhidi ya mifumo kandamizi, ubwana na ufisadi katika Taifa” Hiyo ndo Tanzania ata baba wa Taifa hili alitamani kuiona kwasasa tutaipata wapi Vijana, wengi wamekua waoga kwa Vitisho na mwenendo wa siasa za nchi yetu Ukihoji sana kuna vikundi vya watu wasiojulikana Serikali haiwatambui pia!? April 10, 2017 mbunge wa nzega mjini aliomba bunge lisikilize kikundi hicho kinatoka idara ya usalama wa Taifa, kinacho teka watu kama ilvyo ripotiwa na millardayo kupitia youtube yake. Hivyo vijana wengi wanatumika vibaya kama machawa kwa pesa wanazo pewa Tunahitaji Vijana imara na bora kama mwalimu nyerere alivyo tamani tutengeneze taifa bora na siasa imara nchini.
Imekua nikwa muda mrefu sasa tangu mfumo wa vyama vingi uanze katika taifa letu hili, Siasa haibadiliki, michezo ndio ileile kwa mfano katika hotuba ya kiongozi wa chama cha siasa hapa nchini akiwa mkoa wa Iringa amesema nanukuu “Kuna mgogoro mkubwa sana ndani ya chama chetu, hasa wakati huu wa uchaguzi ndugu zangu tuwe makini na mtego huu, sababu kubwa ni pesa chama hakina pesa sijui hizi za kugawa zinatoka wapi?” Hii inaonekana ni kama kuna vitu vinaendelea ndani ya chama na kiongozi wa ngazi ya juu kama huyo anashindwa kujua pesa zinatoka wapi. Hivyo unabaki kujiuliza Kwahiyo chama kinanunuliwa? Kama ndivyo ina maana gani kwenye nchi ya kidemokrasia, na vitaisha lini vituko vya namna hii.
Hitimisho; Kazi ya uongozi ni kujenga watu wawe na umoja mambo ya kuchochea, chuki sio lengo la uongozi Hivyo tunahitaji wale wanao weza kuongoza watu kwa kuwaunganisha kupitia hoja zao na sio kwa kutumia njia mbalimbali Zaidi ya hoja zao.
Siasa ni njia ya kufanya maamuzi katika njia tofauti tofauti katika jamii kwa mfano Miji, Taifa au hata dunia nzima, katika demokrasia kila mtu ana kiasi Fulani cha nguvu, Hivyo tunahitaji mwanasiasa awe na ukweli na uwajibikaji kwani siasa haimaanishi udanganyifu kama unaofanyika hapa nchini kwetu, vyama vya siasa vinatumia uongo mwingi na ahadi za uongo kujipatia kura kutoka kwa wananchi. Tunahitaji siasa safi na bora zaidi ya hii ya sasa ili tuijenge Tanzania iliyo bora na viongozi bora Zaidi wanaoweza kujali wananchi Zaidi ya masirahi yao binafsi.
Hivyo Tanzania ya kesho tunahitaji kua Na;- Upinzani imara bila uoga na vitisho. Tunahitaji siasa inayo maanishwa kweli kama kusudi la kufanya mfumo wa vyama vingi nchini, upinzani kwenye serikali kuu ndio unafanya mabadiliko makubwa nchini, kukemea mienendo isiyo na maana kwa viongozi wakuu nchini, inajenga uongozi bora na hiyo ndio siasa tunayo hitaji nchi hii.
Watu wasio waoga, mfano mzuri tutazame bunge letu la sasa baada ya uchaguzi mkuu wa 2020 upinzani umekua mdogo sana bungeni wengi wao ni wabunge wa Chama kimoja, wengi wao ni kusifia raisi wa jamuhuri tu, vipi kuhusu kuwasemea wananchi walio kupeleka bungeni.
Baadhi yao tunaona wakihoji sana kuhusu serikali wanazimiwa maiki au kupunguziwa muda wao wa kuchangia, kwa kisingizio cha TAARIFA SPIKA kwa mfano may 5, 2017 mkutano wa saba wa bunge, joseph mbilinyi alizimiwa maiki, Hivyo kutengeneza wanasiasa wanao sifia tu kiongozi mmoja, na Uoga wa viongozi kuogopa kuhoji . Tanzania hatuwezi kutoka hapa tulipo kwa namna hii ya siasa zetu Tunahitaji watu wenye nguvu ya kuhoji kwani Hakuna alie juu ya sheria kama katiba yetu ya jamuhuri ya muungano wa tanzania yam waka 1977 (CURT) inavyo eleza katika
Ibara ya 13 (Equality before the law) Iki maanisha hakuna alie juu ya sheria. Hii ndio Tanzania
tuitakayo kisiasa na kiutawala pia na vyote vinawezekana kama tutapata viongozi sahihi. Nchi yetu tunahitaji utawala wa sheria kwa vitendo na sio tu kuwepo kwa nadharia kwamba tunao utawala wa sheria wakati wanasiasa wengi wakiikosoa serikali wanawekwa ndani huo, sio utawala wa sheria, wakati tukiwa na mfumo wa vyama vingi nchini.
Uwajibikaji
Ni hatari sana kwa taifa letu lijalo kuona viongozi wetu wengi wanakua na tabia za UCHAWA. Pia taifa letu linakabiliwa na IMPUNITY (Ukosefu wa uwajibikaji) wale wanaotakiwa kuwajibishwa kwa makosa yao kama ubadhilifu wa fedha kutokana na ripoti za mgaguzi mkuu wa serikali wanaendelea kuwepo kinacho fanywa ni kuhamishwa tu, hii sio Tanzania tuitakayo.
Tunahitaji viongozi wenye maono makubwa na wazalendo katika nchi hii kwa mfano Mbunge mmoja kutoka jimbo la Geita vijijini alitoa hoja yake bungeni kwa kusema nanunuku “Viongozi wanotajwa kwenye ripoti ya CAG Mbona hawawajibishwi mnawahamisha tu? Nchi hii inayo maeneo mengi sana ya wazi wakamatwe wafungwe wapewe mashamba walime hadi pesa walizokula zirudi kupitia kazi hizo” Kwa namna moja au nyingine wazo lake linaweza kusaidia sana.
UWAJIBIKAJI na kutengenea taifa lenye viongozi imara na wenye maono mazuri nan chi yao, sasa kwa sasa nani wa kuwawajibisha kwa makossa yao yanayo jirudia kila mara. Katika bunge la la 10 mwaka 2015 aliekua mbunge wa singida mh. Tundu lissu alisema nanukuu “majaji wamekamatwa wamekura rushwa na riporti ipo mpaka sasa wameachwa bado wanafanya nini?
Wakamatwe na wezi wengine wakiwemo mawaziri wasiachiwe kwenda kula pesa za wizi” mwisho wa kunukuu, Hivyo inaonekana bado kuna changamoto sana nchi yetu kwa upande wa siasa. Hatuhitaji uongozi wa namna hii, kujenga Tanzania bora. Vijana imra wenye hoja thabiti na sio Uchawa na Uoga.
Vijana kwa sasa kuingia kwenye siasa kumekua na ugumu sana ukiangalia mwenendo wa siasa nchini kwetu hapa ukisema vibaya serikali unakamatwa kama ilivyo onekana mwaka 2020 kwenye uchaguzi na baadhi ya wanaharakati wengi kukimbia nchi yao. Nikinukuu maneneo ya baba wa taifa mwalimu nyerere Alisema “Tunataka kuona taifa lina vijana jeuri na wenye kujiamini, vijana wanaojoji na kupiga vita mifumo isiyoshabihana na matakwa na matarajio ya kitanzania.
Tunataka vijana waasi dhidi ya mifumo kandamizi, ubwana na ufisadi katika Taifa” Hiyo ndo Tanzania ata baba wa Taifa hili alitamani kuiona kwasasa tutaipata wapi Vijana, wengi wamekua waoga kwa Vitisho na mwenendo wa siasa za nchi yetu Ukihoji sana kuna vikundi vya watu wasiojulikana Serikali haiwatambui pia!? April 10, 2017 mbunge wa nzega mjini aliomba bunge lisikilize kikundi hicho kinatoka idara ya usalama wa Taifa, kinacho teka watu kama ilvyo ripotiwa na millardayo kupitia youtube yake. Hivyo vijana wengi wanatumika vibaya kama machawa kwa pesa wanazo pewa Tunahitaji Vijana imara na bora kama mwalimu nyerere alivyo tamani tutengeneze taifa bora na siasa imara nchini.
Imekua nikwa muda mrefu sasa tangu mfumo wa vyama vingi uanze katika taifa letu hili, Siasa haibadiliki, michezo ndio ileile kwa mfano katika hotuba ya kiongozi wa chama cha siasa hapa nchini akiwa mkoa wa Iringa amesema nanukuu “Kuna mgogoro mkubwa sana ndani ya chama chetu, hasa wakati huu wa uchaguzi ndugu zangu tuwe makini na mtego huu, sababu kubwa ni pesa chama hakina pesa sijui hizi za kugawa zinatoka wapi?” Hii inaonekana ni kama kuna vitu vinaendelea ndani ya chama na kiongozi wa ngazi ya juu kama huyo anashindwa kujua pesa zinatoka wapi. Hivyo unabaki kujiuliza Kwahiyo chama kinanunuliwa? Kama ndivyo ina maana gani kwenye nchi ya kidemokrasia, na vitaisha lini vituko vya namna hii.
Hitimisho; Kazi ya uongozi ni kujenga watu wawe na umoja mambo ya kuchochea, chuki sio lengo la uongozi Hivyo tunahitaji wale wanao weza kuongoza watu kwa kuwaunganisha kupitia hoja zao na sio kwa kutumia njia mbalimbali Zaidi ya hoja zao.