Serikali izimulike shule binafsi. Watoto wa darasa la 4 wanaumizwa na ratiba ngumu ya shule hizi

Somoche

JF-Expert Member
Oct 6, 2010
6,215
7,220
Ndg wanabodi sisi wazazi tunatakiwa kuwalinda na kuwaelimisha watoto kadri Mungu anavyotujaalia.Hivi karibuni imeibuka tabia ya hizi shule zinazoitwa English Medium, academy au vyovyote ziitwavyo kulazimisha watoto wa darasa la 4 au la 7 wahamie boarding walale hapo hapo. Kama mjuavyo mtoto wa darasa la 4 wengi wana miaka 9 au 10 ni mtoto ambae bado anahitaji sana uangalizi wa mzazi wake. katika umri huu ni hatari sana kwa mtoto kuhamia boarding na kuishi mbali na wazazi au walezi wake unless mzazi au mlezi ama hujali au una matatizo..

Kibaya zaidi katika hizi shule wanalazimisha ratiba ngumu na katiri sana kwa watoto mtoto wa darasa la 4 analazimishwa kuanza kusoma saa 12 asubuhi hapo anapambana na marathon mpaka saa 11 baada ya hapo atapumzika kidogo saa 1 anaingia tena kusoma mpaka saa 3 usiku.Huu ni ukatiri ..huu ni uuaji wa watoto sio haki NAOMBA SERIKALI IINGILIE HILI JAMBO.

Wazazi mnaambiwa kama hutaki mhamishe au mfikishe shule saa 11 alfajiri umbebe saa 3 usiku. Vyovyote iwavyo kama umesoma unaelewa kichwa cha mwanadamu hakiwezi kuhimiri mshindo mkubwa wa kusoma mfululizo kwa umri huo mdogo mpaka ssaa 3 usiku ndio mana natoa wito Wizara ya Elimu chonde pigeni marufuku watoto wadogo kukandamizwa na shule hizi binafsi ili tu wapate No ya juu kwa ajili ya maslahi ya kutangaza biashara na jina la shule..Elimu haipaswi kuwa biashara hii inafanywa kibiashara...
 
Mbona mimi nmesoma boarding la saba, sa kumi na mja kamili asubuh mnaaingia darasan mnaanza na test. Baada ya hapo wanaacha mjisomee halafu assembly. Mkitoka assembly ni mda wa fimbo maana ile test inakuwa imesahishwa. Mnachapwa fimbo zenu za maana ndo siku inaanza sasa.

Jumamosi ni siku ya test ya masomo yote. Jumatatu ni siku ya fimbo yaan mnaingia shule ratiba ya siku zote ila baada ya chakula saa nane ni mda wa fimbo kwa wale waliofeli. Yaan mnachambuliwa somo moja mnaitwa... wanajipanga kama walimu kumi unakula fimbo mbili mbili. Mnaingia somo jingine. Kwaivyo kama umefeli yote pole yako maana hutoki salama.


Pamoja na yote sijawah kujuta kusoma hyo shule. Maana kusema ukweli ilinijenga kwenye kusoma mwenyew.
 
Kuna kipindi mwalimu mkuu anawaita la saba wote mnaongea nae vizur tu. Afu anauliza wale wanaohisi watafeli terminal watapata chini ya c waje upande huu. Kama ww unaamini utafaulu kaa upande huu.... anakwambia anataka ajue atawasaidiaje wale ambao wanahisi watafeli....

jichanganye uende sasa. Mkishajitenga vizur anaagiza fimbo.... loooo... wale wte mliosema mnafeli mnapanga foleni ya kuchapwa. Afu baadae unaandika barua ya kuahidi utafaulu....
Hahahahahaha.... yaan mwalm mkuu anauliza kwann ufel wkt walimu wanafundsha kila kitu....
sitosahau
 
Ndg wanabodi sisi wazazi tunatakiwa kuwalinda na kuwaelimisha watoto kadri Mungu anavyotujaalia.Hivi karibuni imeibuka tabia ya hizi shule zinazoitwa English Medium,Academy au vyovyote ziitwavyo kulazimisha watoto wa darasa la 4 au la 7 wahamie boarding walale hapo hapo.Kama mjuavyo mtoto wa darasa la 4 wengi wana miaka 9 au 10 ni mtoto ambae bado anahitaji sana uangalizi wa mzazi wake. katika umri huu ni hatari sana kwa mtoto kuhamia boarding na kuishi mbali na wazazi au walezi wake unless mzazi au mlezi ama hujali au una matatizo.. Kibaya zaidi katika hizi shule wanalazimisha ratiba ngumu na katiri sana kwa watoto mtoto wa darasa la 4 analazimishwa kuanza kusoma saa 12 asubuhi hapo anapambana na marathon mpaka saa 11 baada ya hapo atapumzika kidogo saa 1 anaingia tena kusoma mpaka saa 3 usiku.Huu ni ukatiri ..huu ni uuaji wa watoto sio haki NAOMBA SERIKALI IINGILIE HILI JAMBO. wazazi mnaambiwa kama hutaki mhamishe au mfikishe shule saa 11 alfajiri umbebe saa 3 usiku..vyovyote iwavyo kama umesoma unaelewa kichwa cha mwanadamu hakiwezi kuhimiri mshindo mkubwa wa kusoma mfululizo kwa umri huo mdogo mpaka ssaa 3 usiku ndio mana natoa wito Wizara ya Elimu chonde pigeni marufuku watoto wadogo kukandamizwa na shule hizi binafsi ili tu wapate No ya juu kwa ajili ya maslahi ya kutangaza biashara na jina la shule..Elimu haipaswi kuwa biashara hii inafanywa kibiashara...

Kuna suala la kuongeza siku ya jumamosi kuwa ya masomo kama kawaida daahh hii siyo fair kabisa

Huku kwetu ilikuwa eti saa kumi kamili alfajiri hadi saa kumi na nusu
Ni sawa kuwaonea watoto huruma. Kwasbb ya kusoma lakini usimuoneshe mtoto.
Kama hujajua mda wa primary ndo mda wa kumjenga mtoto kuwa na nidhamu ya kusoma. Ndo maana wanaita shule ya msingi. Yaan anajengewa msingi wa kusoma na kuthamini elimu. Mtoto akiharibu primary kuja kumrudisha kwenye mstari ni gharama sana.

Samahanini kama nimewakwaza
 
Binafsi nilianza kujitambua darasa la4. Sikukaa boarding na sikuwahi kuamshwa nisome nilikua naamka mwenyewe najisomea kila siku somo 1 pia usiku kabla ya kulala somo1.....Niliongoza watoto zaidi ya 400 kwa kuwa wa kwanza kwa wastani mkubwa na kupata sifa na zawadi kedekede zilizonichochea kuongeza juhudi zaidi
Hakuna haja ya povu ndugu mtoa mada kama hauko tayari mtoto wako apitie hayo hamisha tu shule maana si kila shule ina utaratibu huo.
 
Kwani umelazimishwa umpeleke mwanao kwenye hizo shule??? Tafuta isiyokuwa na hiyo programe umpeleke mwanao.


Shule zina ushindani siku hizi. Watoto wa siku hizi wengi wao wana uelewa mdogo na wanamambo mengi wanajaza kwenye akili yao.

So ili kuwafanya wasome ni lazima kuwabana. Japo ni wadogo but unakuta kama shule unahitaji wapaform at the best lazima uwabane.
 
Kwani umelazimishwa umpeleke mwanao kwenye hizo shule??? Tafuta isiyokuwa na hiyo programe umpeleke mwanao.


Shule zina ushindani siku hizi. Watoto wa siku hizi wengi wao wana uelewa mdogo na wanamambo mengi wanajaza kwenye akili yao.

So ili kuwafanya wasome ni lazima kuwabana. Japo ni wadogo but unakuta kama shule unahitaji wapaform at the best lazima uwabane.
taratibu za ufundishaji na muda hupangwa na serikali kupitia mitaala, watoto hawafundishwi tu hovyo hovyo hata kama shule ni yako. Nadhani mtoa mada ana jambo la msingi kabisa, mashindano yasiwe sababu ya kuharibu taratibu
 
taratibu za ufundishaji na muda hupangwa na serikali kupitia mitaala, watoto hawafundishwi tu hovyo hovyo hata kama shule ni yako. Nadhani mtoa mada ana jambo la msingi kabisa, mashindano yasiwe sababu ya kuharibu taratibu
Serikali inasema watoto wasiende nyumban kabla ya saa 10 jioni. Haijakataza kuzidsha masaa.

Kama kuna sehemu inayokataza wanafunzi kwenda shule jumamosi iweke hapa kila mtu ajue.

Cha ajabu hizo shule za serikali madarasa ya mitihani yanaenda darasani hadi kipindi cha likizo.
 
taratibu za ufundishaji na muda hupangwa na serikali kupitia mitaala, watoto hawafundishwi tu hovyo hovyo hata kama shule ni yako. Nadhani mtoa mada ana jambo la msingi kabisa, mashindano yasiwe sababu ya kuharibu taratibu
Nyinyi wazazi hamjui chochote. Tafuteni ada. Na subirieni matokeo.

Kama unaona shida mpeleke st kayumba.
 
Hapa nimetoa hoja ya msingi kabisa enzi zetu ulikua unaanza darasa la kwanza ukiwa na miaka 7 manake darasa la 4 una miaka 11 angalau unajitambua hivi sasa mtoto ana miaka 9 yuko darasa la 4...kila kitu ni tofauti hapa naongea kama mzazi na sio kwamba wote mnaochangia hapa ni Wazazi...

Wengineo mnaosema hamisha kama hutaki au peleka st kayumba mbona hao mnaoita kayumba wanasoma na chuo kikuu mnakula nao pasu kwa pasu au unafikiri chuo wanaenda tu wenye hizo private??? Issue hapa ni kwamba hii ni nchi hata kama una shule lazima ufuate sheria..murua na taratibu sio kujifanyia unavyotaka..kingine wale mnaosema wakifeli lawama ni walimu..sio kweli kwamba kukandamiza mtoto kwa level hiyo ndio ataelewa..

Kwanza kwa umri huo atateseka na hataeza kuelewa mana anachoka sana na hapa ndio naweka mssisitizo kwamba elimu inauwawa na tamaa za kibiashara...ili mshindane wafaulu waje kuleta watoto kibiashara
 
Duuh yani watoto wa siku hizi aisee.Mimi nikiwa shule ya msingi nilikua hata sisomi .Akishafundisha mwalimu basi ndio ishatoka hiyo .Nilipofika darasa la saba nilikua naenda pale Nyamagana Primary napiga pepa za kujipima za ticha Mhando

Sasa hizo ratiba si za form six kabisa
 
Hapa nimetoa hoja ya msingi kabisa enzi zetu ulikua unaanza darasa la kwanza ukiwa na miaka 7 manake darasa la 4 una miaka 11 angalau unajitambua hivi sasa mtoto ana miaka 9 yuko darasa la 4...kila kitu ni tofauti hapa naongea kama mzazi na sio kwamba wote mnaochangia hapa ni Wazazi...wengineo mnaosema hamisha kama hutaki au peleka st kayumba mbona hao mnaoita kayumba wanasoma na chuo kikuu mnakula nao pasu kwa pasu au unafikiri chuo wanaenda tu wenye hizo private??? Issue hapa ni kwamba hii ni nchi hata kama una shule lazima ufuate sheria..murua na taratibu sio kujifanyia unavyotaka..kingine wale mnaosema wakifeli lawama ni walimu..sio kweli kwamba kukandamiza mtoto kwa level hiyo ndio ataelewa..
Kwanza kwa umri huo atateseka na hataeza kuelewa mana anachoka sana na hapa ndio naweka mssisitizo kwamba elimu inauwawa na tamaa za kibiashara...ili mshindane wafaulu waje kuleta watoto kibiashara
Peleka mwanao kayumba. Arudi mapema. Ukae nae.
 
Kitaalamu concentration ya mtoto kuanzia darasa la kwanza mpaka form four si zaidi ya saa sita darasani ndo maana masomo yanaañza saa mbili mpaka saa nane mpak nane na nusu zadi ya hapo ni kumchosha mtoto hawezi kuwa na concentration tena
 
Back
Top Bottom