Rostam! - Tafadhali Bwana

Ni lini Rostam Azizi aligundua na kukubali kuwa siasa za Tanzania na hasa CCM ni za 'uchwara' yaani gutter politics? Na nini hasa tafsiri yake ya 'siasa za uchwara? Kupitia hotuba yake ya kujiuzulu, Rostam Azizi ametangaza kuachana na Ubunge pamoja na nafasi yake NEC lakini atabakia kuwa mwanachama wa ccm. Kama kweli nia ni kuachana na siasa za uchwara (whatever that means) kubakia kuwa mwanachama wa chama cha siasa tena chama ambacho alikuwa kiongozi kunamtenganishaje yeye Rostam na siasa uchwara? He is still drinking the same contaminated soup which made him sick in the first place so huu utakaso anaotangaza ataupataje?
 
Makala imetulia sana
hongera Mwanakijiji

ni aibu kusema ROSTAM kafanya uungwana kujiuzulu
 
"Kitu pekee ambacho naweza kumpongeza na kumshukuru Rostam kwa uamuzi wake wa kujiuzulu ni kuwa angalau sasa tumebakiwa na mtu mmoja Bungeni ambaye ana nguvu kuliko mwanasiasa mwingine yeyote nchini na ambaye natumaini naye atafuata mkumbo wa kuachia ngazi na huyo atafanya kweli kwa maslahi ya Taifa. Hapana, siyo Lowassa." (M. M. Mwanakijiji M.M, 2011)

Mkuu hapa umeniacha hoi maana kila nikisugua akili hadi cheche bado moto hautoki, ebu chaguwa mji, nikupe gani?.
 
Mwanakijiji unashindwa kuelewa kuwa umetumia muda mrefu sana kuichambua hotuba ya Rostam kutafuta la kumsingizia lakini ulichokipata hukuelewa kuwa Rostam alikuwa haongei na Taifa alikuwa anaongea na Wazee wa CCM wa jimbo lake. Hakuwa na sababu ya kuyasema ambayo wewe ulitaka ayaseme.

Isitoshe, utaifa na swala la chama ni vitu tofauti. Taifa lina wafuasi wa vyama vingi na wengine wengi zaidi wasiokuwa na chama chochote cha kisiasa. Unataka tukueleweje?

Wacha fitina na ubaguzi, wewe ungekuwa mTaifa sana usingeikimbia Tanzania na kwenda kusaidia kuiendeleza Merekani. Kama una uchungu sana na taifa hili ungebaki hapahapa na kutetea wananchi. Sio kutuma mijadala ya kubagua watu kwa rangi na dini zao kila kukicha.

Rostam amekukaa rohoni siku nyingi sana na nnajua kwa sababu tu unauchungu wa kuona kaweza uliposhindwa wewe.

Hoja yako haina mshiko zaidi ya majungu na ufataani. Namuunga mkono aliesema wewe ni mtu mfupi sana. Unaona haya hata ya kujitokeza mbele za watu iliobaki unajificha nyuma ya pazia la mtandao na kujihisi kuwa una kimo. Kumbe huna na utabaki hivyo hivyo kulalama nyuma ya pazia. Jitokeze kama kweli una urefu wa kuhimili mapigo.
 
Huwasipendi siasa nanina ichukia sana maana kwa sisi Tanzania kilichotupoteza zaidi ni siasa basi, hasa baada ya wanasiasa kugundua kwa dhati kabisa kuwa sisi bado ni wajinga, waoga, na wapumbavu wasiojuwa haki zao, wasiojuwa jinsi ya kuzidai na pia wasiotayari kuzidai kwa nguvu zote; hii ndio dharau ya Rostam Azizi, hii ndio Dharau ya wakina Jairo, kama inafikia mtu anaandika hadi barua kuomba rushwa kwa barua! yote ndio jumla ya dharau juu ya Watanzani.

Tunatakiwa kuangalia hii vita tunashirikisha vipi vyombo vya dola ili viache kuwa sehemu ya huu uchafu, vitoke uoga na viingie ujasiri wa kuona haya, lakini inapaswa kufanywa kwa umakini. Tumekuwa tukifanya kosa moja kubwa sana nalo ni kutaka kila mtu awe mwanasiasa, hili ndio linalo tugarimu sasa. Kuwa mtu akiwa Proffesor Mzuri basi akagombe Ubunge na hata Urais, akiwa Daktari mzuri vivyo hivyo, akiwa kamanda mzuri wa Jeshi pia, hata akiwa mfanyabiashara sasa pia nawe hivyo. Tunahitaji watanzania wote kila kona kuungana dhidi ya huu ugonjwa unaoitwa CCM katika kila kata hatuitaji kuwa wanasiasa wote ndipo tufanikiwe hapana.

Watu kama Lowasa na Rostam hakika wasinge chukuwa sekunde mbele ya Lyatonga Mrema, lakini ni pale alipokuwa Waziri wa Mambo ya ndani tu! Nikatika kosa hilo hilo la kuona kila anayefanya kazi yake katika nafasi fulani basi awe mwanasiasa ndivyo Mrema alipojitosa katika siasa na kufia huko, nafasi yake sasa inapwaya, wakina Mwandosi vivyo hivyo nafasi zao katika Universities zinapwaya. Haiingii akili hata kidogo kuwa tumekuwa na Wataalam waliobobea katika kada za Usalama wa hili Taifa, ndani ya Jeshi, ndani ya Polisi ambao wao hawaoni kuwa CCM hii ya Kikwete inatupereka kwenye hatari haiwezekani labda kama wamenyweshwa valium.

Tumepiga kelele sana, tumefanya sana kazi ya upande wetu tunahita wenzetu katika vyombo vya dola sasa nao waamke kwa nafasi zao.
 
Mwanakijiji unashindwa kuelewa kuwa umetumia muda mrefu sana kuichambua hotuba ya Rostam kutafuta la kumsingizia lakini ulichokipata hukuelewa kuwa Rostam alikuwa haongei na Taifa alikuwa anaongea na Wazee wa CCM wa jimbo lake. Hakuwa na sababu ya kuyasema ambayo wewe ulitaka ayaseme.

Isitoshe, utaifa na swala la chama ni vitu tofauti. Taifa lina wafuasi wa vyama vingi na wengine wengi zaidi wasiokuwa na chama chochote cha kisiasa. Unataka tukueleweje?

Wacha fitina na ubaguzi, wewe ungekuwa mTaifa sana usingeikimbia Tanzania na kwenda kusaidia kuiendeleza Merekani. Kama una uchungu sana na taifa hili ungebaki hapahapa na kutetea wananchi. Sio kutuma mijadala ya kubagua watu kwa rangi na dini zao kila kukicha.

Rostam amekukaa rohoni siku nyingi sana na nnajua kwa sababu tu unauchungu wa kuona kaweza uliposhindwa wewe.

Hoja yako haina mshiko zaidi ya majungu na ufataani. Namuunga mkono aliesema wewe ni mtu mfupi sana. Unaona haya hata ya kujitokeza mbele za watu iliobaki unajificha nyuma ya pazia la mtandao na kujihisi kuwa una kimo. Kumbe huna na utabaki hivyo hivyo kulalama nyuma ya pazia. Jitokeze kama kweli una urefu wa kuhimili mapigo.
Kuna vitu mtu anaweza kuona nimafanikio kwa sababu amefanyia juhudi kuvipata. Lakini vitu vingine sio mafanikio kwakuwa mtu hafanyi juhudi yoyote kuvipata. Sasa wewe unaushambulia ufupi au umbile la mtoa mada kana kwamba kunajuhudi alifanya mtoa mada kupata umbile alilonalo ambalo huna uhakika nalo kwakuwa hujawahi kumuona. Nimesoma kwa makini mada lakini sijaona mahali popote ambapo kabila au rangi ya Rostamu ilipo tajwa, kwa msingi huu wewe ndio mwenye matatizo ya kutaka kumtetea Rostam bila ya hoja zenye nguvu ya utetezi. Hii ni aibu na kukosa uadilifu wa kisomi.
 
ROSTAM, TAFADHALI BWANA!
Na. M. M. Mwanakijiji




Nyerere aliwahi kujiuzulu Ubunge kwa sababu ya msingi
Baba wa Taifa hayati Mwalimu Julius K. Nyerere (mgongano na wale ambao wanajaribu kumvua Ubaba wa Taifa unaendelea) aliwahi kujiuzulu Ubunge wake wa kuteuliwa akikataa kuburuzwa na serikali ya Mkoloni wakati tunaelekea Uhuru. Inanishangaza kuwa leo hii watu wanaojiona ni wanasiasa hasa wameshindwa kufuata mfano wa kujiuzulu katika hali ya kupinga serikali inavyofanya mambo. Wengi bila ya shaka wanajua zaidi kuhusu kujiuzulu kwa Nyerere nafasi ya Uwaziri Mkuu na kumuachia Kawawa baada ya Uhuru, wachache wanakumbuka kuwa Nyerere alijiuzulu Bunge kupinga sera na jinsi wakoloni walivyokuwa wakijaribu kumburuza pamoja na jitihada zake zote za kujaribu kufikia muafaka wa aina fulani.

Mwezi Julai 1957 Nyerere aliteuliwa kuwa Mbunge katika Baraza la Kutunga Sheria. Miezi michache kabla ya hapo alipigwa marufuku kuhutubia mikutano ya hadhara na mkoloni. Tarehe 14 Disemba 1957 aliandika barua ya kujiuzulu na siku mbili baadaye alielezea uamuzi wake wa kwanini alijiuzulu katika makala iliyotoka kwenye kijarida “Sauti ya TANU”. Katika maelezo yake marefu alielezea ni kwanini alikubali kuteuliwa kuingia Bungeni ya kuwa alifanya hivyo akiamini kuwa serikali ilikuwa na malengo ya kweli ya kushughulikia matatizo ya kisasa ya wakati huo. Miezi sita baadaye alijikuta kwamba amekubali kuachilia mambo mbalimbali ya msingi katika bona fide akiamini kwamba serikali nayo itakubali kuachilia madai au kubadilisha hatua zake mbalimbali.


Niandikie: mwanakijiji@jamiiforums.com

Kwa ushauri tu wale ambao wanampongeza walau wangeeleza kwa undani hayo maslahi ya taifa aliyo yatetea? Kwa uwazi kabisa azungumze sababu za kujiuzulu baada ya vitisho vya katibu mkuu mpya wa CCM! Kuendelea ni kujitolea jamani waTanganyika mnakuwa waoga sana kujitoa, kazi iliyobaki ni kusifia mambo yasiyo na ukweli kwa maslahi ya chama badala ya taifa, niwakumbusheni kwamba maneno ya Zito Bungeni kwamba Baraza la mawaziri ninafanyiwa lobbying yalipuuzwa kwa haraka sana, na wanasema kwamba Jairo na wenzake BMW wamezoea! Kumbe wanao ushahidi wa kuhongwa ati leo wapongezwe kwa kukataa hiyo rushwa moja sijui alikosea hatua gani huyo Jairo sasa yupo Isolated, tungependa aseme hayo anayohisi ni maslahi ya taifa ameyatetea!

Yule mwingine wala siyo Lowassa na siyo Chenge
 
Kifupi Rostam kaiita Secretari yote ya Chama Changu MAJUHA. Inasikitisha hakuna hatua yoyote waliyochukua dhidi yake mpaka sasa hivi. Hivi angeweza kumuita Mkapa au Nyerere JUHA akabaki salama?
 
Mwanakijiji unashindwa kuelewa kuwa umetumia muda mrefu sana kuichambua hotuba ya Rostam kutafuta la kumsingizia lakini ulichokipata hukuelewa kuwa Rostam alikuwa haongei na Taifa alikuwa anaongea na Wazee wa CCM wa jimbo lake. Hakuwa na sababu ya kuyasema ambayo wewe ulitaka ayaseme.

Isitoshe, utaifa na swala la chama ni vitu tofauti. Taifa lina wafuasi wa vyama vingi na wengine wengi zaidi wasiokuwa na chama chochote cha kisiasa. Unataka tukueleweje?

Wacha fitina na ubaguzi, wewe ungekuwa mTaifa sana usingeikimbia Tanzania na kwenda kusaidia kuiendeleza Merekani. Kama una uchungu sana na taifa hili ungebaki hapahapa na kutetea wananchi. Sio kutuma mijadala ya kubagua watu kwa rangi na dini zao kila kukicha.

Rostam amekukaa rohoni siku nyingi sana na nnajua kwa sababu tu unauchungu wa kuona kaweza uliposhindwa wewe.

Hoja yako haina mshiko zaidi ya majungu na ufataani. Namuunga mkono aliesema wewe ni mtu mfupi sana. Unaona haya hata ya kujitokeza mbele za watu iliobaki unajificha nyuma ya pazia la mtandao na kujihisi kuwa una kimo. Kumbe huna na utabaki hivyo hivyo kulalama nyuma ya pazia. Jitokeze kama kweli una urefu wa kuhimili mapigo.

Don't kill the messenger!

Assume Mwanakijiji ana urefu wa Bryan Kobe - the American basket ball player , na Rostam Azizi ni Mgogo, then soma tena alichoandika Mwanajiji na utupe conclusion yako!

 
Hii ni makala mzuri sana. Hata mimi nilishangaa sana watu wanavyompongeza Rostam kwa kujiuzulu ili kulinda masilahi ya biashara zake. Swali langu lilikuwa hizo biashara zake zinawasaidia nini watanzania masikini kabisa? Na hata kama zinawasadia hao watanzania, je hizo pesa za kuanzisha hizo biashara amezipata wapi? Sio zile za EPA, Richmond na nyingine zilizoibwa serikalini kijanja janja?
 
Mwanakijiji unashindwa kuelewa kuwa umetumia muda mrefu sana kuichambua hotuba ya Rostam kutafuta la kumsingizia lakini ulichokipata hukuelewa kuwa Rostam alikuwa haongei na Taifa alikuwa anaongea na Wazee wa CCM wa jimbo lake. Hakuwa na sababu ya kuyasema ambayo wewe ulitaka ayaseme.

Isitoshe, utaifa na swala la chama ni vitu tofauti. Taifa lina wafuasi wa vyama vingi na wengine wengi zaidi wasiokuwa na chama chochote cha kisiasa. Unataka tukueleweje?

Wacha fitina na ubaguzi, wewe ungekuwa mTaifa sana usingeikimbia Tanzania na kwenda kusaidia kuiendeleza Merekani. Kama una uchungu sana na taifa hili ungebaki hapahapa na kutetea wananchi. Sio kutuma mijadala ya kubagua watu kwa rangi na dini zao kila kukicha.

Rostam amekukaa rohoni siku nyingi sana na nnajua kwa sababu tu unauchungu wa kuona kaweza uliposhindwa wewe.

Hoja yako haina mshiko zaidi ya majungu na ufataani. Namuunga mkono aliesema wewe ni mtu mfupi sana. Unaona haya hata ya kujitokeza mbele za watu iliobaki unajificha nyuma ya pazia la mtandao na kujihisi kuwa una kimo. Kumbe huna na utabaki hivyo hivyo kulalama nyuma ya pazia. Jitokeze kama kweli una urefu wa kuhimili mapigo.

Huyu muungwana sijui anasoma habari ipi? kama huna cha kuongea ni bora usiingie kabisa JF, vinginevyo unajidhalilisha mno, 'Independently look at the story" kisha kama unaweza changia, usipende kujidhalilisha, ingawa umeficha description yako bado unajitia aibu kukosa hoja!
 
Don't kill the messenger!Assume Mwanakijiji ana urefu wa Bryan Kobe - the American basket ball player , na Rostam Azizi ni Mgogo, then soma tena alichoandika Mwanajiji na utupe conclusion yako!
Unayosema wewe ni kufikirika mimi naongelea analysis za theory ilio maarufu sana, sina haja ya kukuambia ni ipi, fanya homework yako. Sina haja ya ku assume kama utakavyo kwani hiyo itakuwa ni assumption. Mwambie aweke picha yake aliosimama na mtu mwingine yeyote halafu tuithibishe niliyoyasema, simjui hanijui lakini maandiko yake nimeyachambua na kufikia conclusion kuwa huyu ni mtu mfupi sana na anasura mbaya sana kwa hiyo watu wote warefu na wenye sura za kuvutia kama Rostam, Kikwete, kwake huwa ni maadui wa kufikirika na isitoshe wakiwa na mafanikio.
 
Mkuu mara chache huwa nakupinga Post zako kimtazamo.........na unapenda sana kuwaaminisha watu mawazo yako na mitazamo yako.........Lakini kumbuka katika DUNIA ya sasa Nchi nyingi hasa za Dunia ya tatu zinatawaliwa na Nchi zenye Uwezo kiuchumi na kijeshi na siyo SIASA(Demokrasia)......Hivyo ni wajibu wa kila MwanaJF kulijua hili ili tunapotoa michango/Post tusiwachanganye wananchi ambao wamelala usingizi wakidhani bado tupo kwenye DEMOCRASIA wakasahau maisha yao yanaendaje?


MFUMO WA DEMOCRASIA ULISHAPITA.......SASA NI NCHI KUVUNA RASLIMALI ZA NCHI NYINGINE WAKITUMIA RAIA WA NCHI HUSIKA
 
Hii ni makala mzuri sana. Hata mimi nilishangaa sana watu wanavyompongeza Rostam kwa kujiuzulu ili kulinda masilahi ya biashara zake. Swali langu lilikuwa hizo biashara zake zinawasaidia nini watanzania masikini kabisa? Na hata kama zinawasadia hao watanzania, je hizo pesa za kuanzisha hizo biashara amezipata wapi? Sio zile za EPA, Richmond na nyingine zilizoibwa serikalini kijanja janja?
Nenda Igunga na bukene na Rujewa Mbeya ukaulize fedha wamezipata wapi. Ukoo wa Rostam ni wakulima (Farmers sio peasants) na wafanya biashara toka enzi na enzi na hakuna aliyeajiriwa katika ukoo wao. Kumbuka kuna watu wanazaliwa kwenye fedha na kuna watu wanazaliwa kwenye umasikini, na hilo si kosa ni mipango ya mola. Rostam ni kati ya watu waliozaliwa kwenye fedha.
 
Huyu muungwana sijui anasoma habari ipi? kama huna cha kuongea ni bora usiingie kabisa JF, vinginevyo unajidhalilisha mno, 'Independently look at the story" kisha kama unaweza changia, usipende kujidhalilisha, ingawa umeficha description yako bado unajitia aibu kukosa hoja!
Hapo ndipo unapoonesha upunguani wako. Kwanza huna ubavu wa kuniambia nisiingie JF. Halafu umekosa kusoma hoja ya msingi. Hoja ya msingi ni kuwa Rostam hakuwa na haja ya kuongea kama mwanakijiji anavyotaka iwe. Rostam aongee kitaifa kwani anacheoi gani katika Taifa hili? Rostam ni mwanachama wa CCM na alienda kuongea na wazee wa CCM na angetaka kuongea na Taifa zima asingekwenda Tabora, angebaki kwenye maskani yake ya sasa Dar. Akawaita waandishi wa habari akaongea na taifa. Hoja ya pili ni kuwa mwanakijiji anausongo na watu warefu na wenye mafanikio. Yeye mbinu za Tanzania zilimshinda akakimbilia Merekani, sasa roho inamuuma hawa wamewezaje aliposhindwa yeye? Hapo sasa. Inabidi afanye kila njia kujionesha kuwa na yeye nae yumo. Na hiyo ni moja ya matatizo ya watu wafupi. Na nnaapa ni mtu mfupi.
 
Hapo ndipo unapoonesha upunguani wako. Kwanza huna ubavu wa kuniambia nisiingie JF. Halafu umekosa kusoma hoja ya msingi. Hoja ya msingi ni kuwa Rostam hakuwa na haja ya kuongea kama mwanakijiji anavyotaka iwe. Rostam aongee kitaifa kwani anacheoi gani katika Taifa hili? Rostam ni mwanachama wa CCM na alienda kuongea na wazee wa CCM na angetaka kuongea na Taifa zima asingekwenda Tabora, angebaki kwenye maskani yake ya sasa Dar. Akawaita waandishi wa habari akaongea na taifa. Hoja ya pili ni kuwa mwanakijiji anausongo na watu warefu na wenye mafanikio. Yeye mbinu za Tanzania zilimshinda akakimbilia Merekani, sasa roho inamuuma hawa wamewezaje aliposhindwa yeye? Hapo sasa. Inabidi afanye kila njia kujionesha kuwa na yeye nae yumo. Na hiyo ni moja ya matatizo ya watu wafupi. Na nnaapa ni mtu mfupi.

Mhh...unaonesha upo so obsessed na vimo na rangi na sura za watu...ironically wanaume. Saikolojia inaniambia mengi sana kuhusu wewe. Sitaki kusema..
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom