Lucas Mwashambwa
JF-Expert Member
- Jul 28, 2022
- 15,651
- 10,048
Ndugu zangu watanzania,
Mwamba Paul Christian Makonda ndio maana anapendwa sana na wananchi wanyonge na wa hali ya chini wenye maisha ya kawaida na ya kutafuta mkate na chakula kila siku pale jua linapochomoza,ndio maana anakubalika sana hapa nchini,ndio maana anaungwa mkono na watu wengi sana,ndio maana mikutano yake hufurika na kumiminika watu utafikiri mchanga wa baharini,ndio maana amekuwa akiwashinda maadui zake wanaomuombea na kumtakia mabaya,ndio maana anapata maombi ya baraka kutoka kwa viongozi mbalimbali wa kidini kutoka madhehebu mbalimbali ya hapa nchini.
Hii ni kwa kuwa ni mtu na kiongozi anayewajali sana wanyonge na watu wa kipato cha chini,hii ni kwa kuwa utumishi wake ni kwa ajili ya kugusa maisha ya watu,kuleta matumaini kwenye mioyo ya watu,kuwasha nuru na mwanga katikati ya giza,kuonyesha njia mahali pasipo na njia,kuleta faraja na furaha mahali penye kukata Tamaa,kuwashika mikono na kuwainua walio chini.
Sasa baada ya Mei Mosi mwezi ujao Arusha kuwa mwenyeji na muandaaji wa sherehe za mei mosi kitaifa mwaka huu ,Mwamba Makonda amefanya kitu cha kitofauti sana ,kitu cha kuigwa ,kitu cha kibunifu,kitu cha kipekee na alama itakayokumbukwa na wajasiriamali wa Arusha na mikoa ya kanda ya kaskazini,kitu kitakacho inua uchumi wa vijana mbalimbali.
Hii ni baada ya kuja na wazo la kibunifu kwa ajili ya wajasiriamali wa Arusha.,ambapo yeye na uongozi wa mkoa wa Arusha wameamua kutenga barabara moja maalumu kando kando ya uwanja wa sheik Abeid ,utakaotumika kwenye maadhimisho kwa ajili ya wajasiriamali kufanyia biashara zao mbalimbali.hii maana yake ni kuwa wajasiriamali watapanga na kuweka bidhaa zao mbalimbali kwa ajili ya wateja wao ambao watakuwa wamefurika katika viwanja hivyo kutoka maeneo mbalimbali hapa nchini.
Hii maana yake ni kuwa amewarahisishia pia wageni mbalimbali kupata huduma na mahitaji karibu kabisa pasipo kusafiri umbali mrefu kutafuta bidhaa au kuamua kuacha kabisa.lakini uwepo wa bidhaa karibu ni fursa kwa pande zote mbili yaani wahudhuriaji pamoja na wajasiriamali ambao wameletewa wateja na kupewa fursa karibu na eneo la kuuzia bidhaa zao bila bugudha wala kukimbizana na migambo wa jiji.
Makonda acheni aitwe Mwamba tu. Huyu jamaa ni mbunifu sijapata kuona.huyu Mwamba nilishawaambieni kuwa hata apewe kuongoza mtaa tu basi amini nawaambieni ya kuwa mtaa huo utafahamika ndani ya nchi na nje ya mipaka ya Tanzania, na kila mtu atatamani kutembelea mtaa huo na kufanya shughuli zake. Mwamba anajuwa afanye nini na kwa wakati gani,huyu ni Mwamba ambaye huwa hapishani na muda bali huwa mbele ya muda ili muda unapofika umkute amejiandaa na yupo eneo husika na siyo kufanya mambo kwa zima moto.
Lakini pia Mwamba Mwenyewe Makonda amewakaribisha wananchi wote kuhudhuria kwa wingi sana katika sherehe hizo za mei mosi ili kuungana na watumishi wa umma ambao wapo kwa ajili ya kuihudumia jamii na kuhakikisha kuwa jamii inapata huduma bora na stahiki.hivyo kuwapa moyo watumishi hawa ni vyema kuhudhuria kwa wingi na kujumuika nao kwa pamoja.maana shughuli ni watu.
Kazi iendelee, mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.
Lucas Hebel Mwashambwa. MAMA ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu muhula wa pili .
Pia soma:
Dkt. Mpango: Serikali imepokea hoja ya kuboresha kikokotoo kwakuwa wafanyakazi hawaridhishwi na kanuni zake
Mwamba Paul Christian Makonda ndio maana anapendwa sana na wananchi wanyonge na wa hali ya chini wenye maisha ya kawaida na ya kutafuta mkate na chakula kila siku pale jua linapochomoza,ndio maana anakubalika sana hapa nchini,ndio maana anaungwa mkono na watu wengi sana,ndio maana mikutano yake hufurika na kumiminika watu utafikiri mchanga wa baharini,ndio maana amekuwa akiwashinda maadui zake wanaomuombea na kumtakia mabaya,ndio maana anapata maombi ya baraka kutoka kwa viongozi mbalimbali wa kidini kutoka madhehebu mbalimbali ya hapa nchini.
Hii ni kwa kuwa ni mtu na kiongozi anayewajali sana wanyonge na watu wa kipato cha chini,hii ni kwa kuwa utumishi wake ni kwa ajili ya kugusa maisha ya watu,kuleta matumaini kwenye mioyo ya watu,kuwasha nuru na mwanga katikati ya giza,kuonyesha njia mahali pasipo na njia,kuleta faraja na furaha mahali penye kukata Tamaa,kuwashika mikono na kuwainua walio chini.
Sasa baada ya Mei Mosi mwezi ujao Arusha kuwa mwenyeji na muandaaji wa sherehe za mei mosi kitaifa mwaka huu ,Mwamba Makonda amefanya kitu cha kitofauti sana ,kitu cha kuigwa ,kitu cha kibunifu,kitu cha kipekee na alama itakayokumbukwa na wajasiriamali wa Arusha na mikoa ya kanda ya kaskazini,kitu kitakacho inua uchumi wa vijana mbalimbali.
Hii ni baada ya kuja na wazo la kibunifu kwa ajili ya wajasiriamali wa Arusha.,ambapo yeye na uongozi wa mkoa wa Arusha wameamua kutenga barabara moja maalumu kando kando ya uwanja wa sheik Abeid ,utakaotumika kwenye maadhimisho kwa ajili ya wajasiriamali kufanyia biashara zao mbalimbali.hii maana yake ni kuwa wajasiriamali watapanga na kuweka bidhaa zao mbalimbali kwa ajili ya wateja wao ambao watakuwa wamefurika katika viwanja hivyo kutoka maeneo mbalimbali hapa nchini.
Hii maana yake ni kuwa amewarahisishia pia wageni mbalimbali kupata huduma na mahitaji karibu kabisa pasipo kusafiri umbali mrefu kutafuta bidhaa au kuamua kuacha kabisa.lakini uwepo wa bidhaa karibu ni fursa kwa pande zote mbili yaani wahudhuriaji pamoja na wajasiriamali ambao wameletewa wateja na kupewa fursa karibu na eneo la kuuzia bidhaa zao bila bugudha wala kukimbizana na migambo wa jiji.
Makonda acheni aitwe Mwamba tu. Huyu jamaa ni mbunifu sijapata kuona.huyu Mwamba nilishawaambieni kuwa hata apewe kuongoza mtaa tu basi amini nawaambieni ya kuwa mtaa huo utafahamika ndani ya nchi na nje ya mipaka ya Tanzania, na kila mtu atatamani kutembelea mtaa huo na kufanya shughuli zake. Mwamba anajuwa afanye nini na kwa wakati gani,huyu ni Mwamba ambaye huwa hapishani na muda bali huwa mbele ya muda ili muda unapofika umkute amejiandaa na yupo eneo husika na siyo kufanya mambo kwa zima moto.
Lakini pia Mwamba Mwenyewe Makonda amewakaribisha wananchi wote kuhudhuria kwa wingi sana katika sherehe hizo za mei mosi ili kuungana na watumishi wa umma ambao wapo kwa ajili ya kuihudumia jamii na kuhakikisha kuwa jamii inapata huduma bora na stahiki.hivyo kuwapa moyo watumishi hawa ni vyema kuhudhuria kwa wingi na kujumuika nao kwa pamoja.maana shughuli ni watu.
Kazi iendelee, mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.
Lucas Hebel Mwashambwa. MAMA ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu muhula wa pili .
Dkt. Mpango: Serikali imepokea hoja ya kuboresha kikokotoo kwakuwa wafanyakazi hawaridhishwi na kanuni zake