Nishati Safi ya Kupikia, Mwarobaini tunao na ni Bora kuliko Gesi

Baada ya kuona kwenye Habari Serikali imeanzisha Mfuko wa Nishati Safi ya Kupikia nikaona ni vema tuangalie kwa nchi Yetu Nishati hio ni ipi na ni vipi itatufaa, ili tusije kuingia gharama ambazo zitakuwa hazina manufaa kwetu.

Nishati zilizopo:
Kwenye kila kaya aina ya Nishati inayotumiwa kupikia inategemea upatikanaji na gharama ya Nishati hio. Kwa mtumiaji wa mwisho gharama anayojali ni ya kifedha ingawa kwa mtizamo wa mazingira, gharama ya kifedha inaweza kuwa ndogo lakini athari za hio nishati zikawa ni kubwa zaidi. Kwa mazingira ya Tanzania Nishati ambazo zinaweza kupatikana na kutumika ni kama ifuatavyo.

Kuni
Ni nishati chafu, na kutokana na moshi ina athari za kiafya kwa mtumiaji, vilevile athari za kimazingira kama kuni hizo zinapatikana kwa kukata miti na sio kutumia mabaki ya miti.

Mkaa (Carbonization) kutoka kwenye Miti
Badala ya kutumia kuni moja kwa moja miti hiyo au mabaki ya miti yakifanyiwa carbonization yaani kuchomwa mkaa, nishati hii inakuwa safi kwa mtumiaji kwa kupunguza athari za kiafya ingawa bado kunakuwa na athari ya kukata miti hovyo ili kuchoma mkaa, jambo ambalo athari yake kimazingira ni kubwa sana.

Mkaa (Carbonization) kutoka kwenye Mabaki ya Mimea, Na Mikaa Mbadala
Sababu hii haitumii miti na kukata misitu athari yake kwa mazingira haipo na vilevile inaweza kusaidia kwa kuondoa mabaki / uchafu ambao hautakiwi na kuubadilisha kuwa nishati. Angalizo; Kutengeneza Nishati hii hutumia pia Nishati, hivyo ukiangalia mtiririko mzima huenda Nishati hii isiwe safi kama inavyodhaniwa kutokana na matumizi ya Nishati nyingine kutengeneza hii Nishati.

Mafuta ya Taa, Methanol na Ethanol
Kwa mafuta ya Taa nishati hii tunainunua kutoka nje hivyo kuna gharama ya manunuzi na katika usafirishaji wake mnyororo mzima ni wa gharama. Watu wanaweza kutengeneza Methanol / Ethanol kama vile wanavyopika gongo ila myonyoro mzima wa upatikanaji wa hio nishati ni gharama.

Gesi Asilia (Biogas) na Gesi ya Mtwara
Gesi asilia mtu mmoja mmoja mfugaji au sehemu kama kwenye mashule wanaofuga au kwenye Magereza wanaweza kutumia Kinyesi na kutengeneza Biogas kwa mapishi yao, hii itasaidia katika kuondoa mabaki (uchafu) na kuweza kubadilisha kuwa mbolea. Gesi asilia ya Mtwara inaweza kutumika kwa ufanisi iwapo tu itafungwa moja kwa moja kutoka kwenye Source, na kupelekwa kwa mabomba (kama vile mfumo wa maji ulivyo) mpaka kwa mtumiaji, ingawa utengenezaji wa miundombinu hiyo ni gharama sana na kama kutakuwa kunatokea uvujaji wa hii Gesi tutakuwa tunachafua mazingira kwa gesi hio (methane) kuingia moja kwa moja kwenye mazingira hivyo badala ya kuwa nishati Safi itakuwa moja ya Nishati Chafu....

Gesi ya Mitungi (LPG)
Hii ndio nishati inayopigiwa chapio na wengi na ndio inayotumika majumbani, lakini ina hasara kuu mbili kwa taifa letu, Moja ni kwamba tunaagiza kutoka nje hivyo inahitaji gharama ya kununua, na mbili hata ikishafika usafirishaji wa kutoka point moja mpaka nyingine bado ni matumizi ya Nishati. Na gharama yake bado ni kubwa kuliko uwezo wa watu ndio maana watu wanatumia Nishati nyingine. Na tukisema tuweke ruzuku kusaidia watu kununua, tatizo bado lipo palepale ukizingatia ni pesa hizo hizo tunazochukua kwa hao wasiojiweza kama Kodi na kuwarudishia kama ruzuku ili wanunue kitu ambacho kinanufaisha mataifa ya nje pindi tunapoagiza hii gesi

Umeme
Hii nimeiweka mwisho sababu ndio nishati safi ya kupikia kuliko zote kulingana na mazingira yetu ya Tanzania, kama tutaweza kutumia vyanzo vyetu vizuri, na hili linaweza kufanikiwa ikiwa tutafanya yafuatayo:-

  • Watanzania Wengi ndio Wanafikiwa na Umeme kuliko Nishati nyingine yoyote: Miundombinu tayari ipo watu karibia wote wana plug za umeme majumbani kwao hivyo tunaweza kutumia hio nishati kama umeme utakuwa wa gharama nafuu sana, Kama tukisema tushushe bei kwenye gesi tunaweza kushusha bei mpaka ile bei tunayonunulia lakini umeme ambao tunazalisha tunaweza kupaga bei za units bila kutegemea soko la dunia

  • Vifaa vya Umeme Vipatikane kwa Gharama Nafuu / Kutoa Ruzuku; Kama tukiondoa Ushuru au kutoa Ruzuku katika vifaa vya umeme basi ufanisi wa Kupikia umeme utakuwa zaidi ya Gesi; watu watatumia Oven kuokea, Watatumia Rice Cooker kupikia Wali; Flyers kupikia Chips na Jug Kettles kuchemshia Maji n.k.

  • Matumizi ya Induction Cooker; Ingawa kwa kipindi kirefu majiko ya gesi yalikuwa yanapiku majiko ya umeme katika ufanisi (yaani ilikuwa inachukua muda mchache kwa gesi kupata moto unaotaka wakati coil ya umeme inachukua muda mrefu) ila kwa sasa hivi induction cooker ni instant (wakati huo huo) ukiwasha unapata joto unalotaka na moto unawaka pale tu kwenye sufuria pengine pote kunakuwa hakuna moto (hivyo hakuna upotevu wa nishati)

  • Badala ya Kutoa Ruzuku watu Wanunue Gesi za Kunufaisha wengine Tutoe Ruzuku watu Waunganishwe na Umeme na Kununua Vifaa vya Umeme; Nimeona kwenye Habari Serikali imeanzisha mfuko wa Nishati safi…, sasa badala ya kutumia mfuko huo na Kodi zetu kunufaisha wauzaji wa gesi ambapo mwisho wa siku ni mataifa ya nje tunaweza kutumia pesa hizo kuhakikisha kila mtu anaunganishwa na umeme na umeme unakuwa bei rahisi na vifaa vya umeme kuwekewa ruzuku.


Hitimisho
Kwa Mazingira yetu ya Tanzania Nishati ambayo inaweza ikawa safi ya kupikia na ambayo ni practical na tunaweza kuipata kwa haraka na urahisi ni kwa kutumia Umeme, badala ya kuhangaika na kusambaza gesi asilia majumbani kwa watu kwenye mabomba, ambayo itakuwa ni gharama kubwa tunaweza kusambaza gesi hio asilia mpaka kwenye vyanzo vya uzalishaji wa umeme ili Gesi hio Ibadilishwe kuwa umeme na kuungana na vyanzo vingine (maji, solar, upepo n.k.) na kusambazwa kwenye kila Kaya tayari kwa watu kupikia.

NB: Ushauri wa kuachana na LPG (Mitungi ya Gesi ya Sasa Majumbani) itaacha wengi ambao ndio Biashara yao kwenye hasara ila kwa kurekebisha hilo Serikali inaweza kushauriana nao au kuwawezesha kwa mikopo wawekeze kwenye matengenezo na marekebisho ya vifaa vya Umeme; kwahio badala ya kuagiza majiko kutoka nje assembly plants zinaweza zikawa nchini jambo ambalo litakuza ajira na kuwapa wigo waliopo kwenye biashara ya LPG kunufaika na Umeme - Badala ya Mihan, Oryx, Taifa gesi tutakuwa na Mihan, Oryx, Taifa Cookers
Wansisitiza gas kwa sababu kuna mhuni mmoja kawatia mifukoni ana maslahi na LPG
 
Baada ya kuona kwenye Habari Serikali imeanzisha Mfuko wa Nishati Safi ya Kupikia nikaona ni vema tuangalie kwa nchi Yetu Nishati hio ni ipi na ni vipi itatufaa, ili tusije kuingia gharama ambazo zitakuwa hazina manufaa kwetu.

Nishati zilizopo:
Kwenye kila kaya aina ya Nishati inayotumiwa kupikia inategemea upatikanaji na gharama ya Nishati hio. Kwa mtumiaji wa mwisho gharama anayojali ni ya kifedha ingawa kwa mtizamo wa mazingira, gharama ya kifedha inaweza kuwa ndogo lakini athari za hio nishati zikawa ni kubwa zaidi. Kwa mazingira ya Tanzania Nishati ambazo zinaweza kupatikana na kutumika ni kama ifuatavyo.

Kuni
Ni nishati chafu, na kutokana na moshi ina athari za kiafya kwa mtumiaji, vilevile athari za kimazingira kama kuni hizo zinapatikana kwa kukata miti na sio kutumia mabaki ya miti.

Mkaa (Carbonization) kutoka kwenye Miti
Badala ya kutumia kuni moja kwa moja miti hiyo au mabaki ya miti yakifanyiwa carbonization yaani kuchomwa mkaa, nishati hii inakuwa safi kwa mtumiaji kwa kupunguza athari za kiafya ingawa bado kunakuwa na athari ya kukata miti hovyo ili kuchoma mkaa, jambo ambalo athari yake kimazingira ni kubwa sana.

Mkaa (Carbonization) kutoka kwenye Mabaki ya Mimea, Na Mikaa Mbadala
Sababu hii haitumii miti na kukata misitu athari yake kwa mazingira haipo na vilevile inaweza kusaidia kwa kuondoa mabaki / uchafu ambao hautakiwi na kuubadilisha kuwa nishati. Angalizo; Kutengeneza Nishati hii hutumia pia Nishati, hivyo ukiangalia mtiririko mzima huenda Nishati hii isiwe safi kama inavyodhaniwa kutokana na matumizi ya Nishati nyingine kutengeneza hii Nishati.

Mafuta ya Taa, Methanol na Ethanol
Kwa mafuta ya Taa nishati hii tunainunua kutoka nje hivyo kuna gharama ya manunuzi na katika usafirishaji wake mnyororo mzima ni wa gharama. Watu wanaweza kutengeneza Methanol / Ethanol kama vile wanavyopika gongo ila myonyoro mzima wa upatikanaji wa hio nishati ni gharama.

Gesi Asilia (Biogas) na Gesi ya Mtwara
Gesi asilia mtu mmoja mmoja mfugaji au sehemu kama kwenye mashule wanaofuga au kwenye Magereza wanaweza kutumia Kinyesi na kutengeneza Biogas kwa mapishi yao, hii itasaidia katika kuondoa mabaki (uchafu) na kuweza kubadilisha kuwa mbolea. Gesi asilia ya Mtwara inaweza kutumika kwa ufanisi iwapo tu itafungwa moja kwa moja kutoka kwenye Source, na kupelekwa kwa mabomba (kama vile mfumo wa maji ulivyo) mpaka kwa mtumiaji, ingawa utengenezaji wa miundombinu hiyo ni gharama sana na kama kutakuwa kunatokea uvujaji wa hii Gesi tutakuwa tunachafua mazingira kwa gesi hio (methane) kuingia moja kwa moja kwenye mazingira hivyo badala ya kuwa nishati Safi itakuwa moja ya Nishati Chafu....

Gesi ya Mitungi (LPG)
Hii ndio nishati inayopigiwa chapio na wengi na ndio inayotumika majumbani, lakini ina hasara kuu mbili kwa taifa letu, Moja ni kwamba tunaagiza kutoka nje hivyo inahitaji gharama ya kununua, na mbili hata ikishafika usafirishaji wa kutoka point moja mpaka nyingine bado ni matumizi ya Nishati. Na gharama yake bado ni kubwa kuliko uwezo wa watu ndio maana watu wanatumia Nishati nyingine. Na tukisema tuweke ruzuku kusaidia watu kununua, tatizo bado lipo palepale ukizingatia ni pesa hizo hizo tunazochukua kwa hao wasiojiweza kama Kodi na kuwarudishia kama ruzuku ili wanunue kitu ambacho kinanufaisha mataifa ya nje pindi tunapoagiza hii gesi

Umeme
Hii nimeiweka mwisho sababu ndio nishati safi ya kupikia kuliko zote kulingana na mazingira yetu ya Tanzania, kama tutaweza kutumia vyanzo vyetu vizuri, na hili linaweza kufanikiwa ikiwa tutafanya yafuatayo:-

  • Watanzania Wengi ndio Wanafikiwa na Umeme kuliko Nishati nyingine yoyote: Miundombinu tayari ipo watu karibia wote wana plug za umeme majumbani kwao hivyo tunaweza kutumia hio nishati kama umeme utakuwa wa gharama nafuu sana, Kama tukisema tushushe bei kwenye gesi tunaweza kushusha bei mpaka ile bei tunayonunulia lakini umeme ambao tunazalisha tunaweza kupaga bei za units bila kutegemea soko la dunia

  • Vifaa vya Umeme Vipatikane kwa Gharama Nafuu / Kutoa Ruzuku; Kama tukiondoa Ushuru au kutoa Ruzuku katika vifaa vya umeme basi ufanisi wa Kupikia umeme utakuwa zaidi ya Gesi; watu watatumia Oven kuokea, Watatumia Rice Cooker kupikia Wali; Flyers kupikia Chips na Jug Kettles kuchemshia Maji n.k.

  • Matumizi ya Induction Cooker; Ingawa kwa kipindi kirefu majiko ya gesi yalikuwa yanapiku majiko ya umeme katika ufanisi (yaani ilikuwa inachukua muda mchache kwa gesi kupata moto unaotaka wakati coil ya umeme inachukua muda mrefu) ila kwa sasa hivi induction cooker ni instant (wakati huo huo) ukiwasha unapata joto unalotaka na moto unawaka pale tu kwenye sufuria pengine pote kunakuwa hakuna moto (hivyo hakuna upotevu wa nishati)

  • Badala ya Kutoa Ruzuku watu Wanunue Gesi za Kunufaisha wengine Tutoe Ruzuku watu Waunganishwe na Umeme na Kununua Vifaa vya Umeme; Nimeona kwenye Habari Serikali imeanzisha mfuko wa Nishati safi…, sasa badala ya kutumia mfuko huo na Kodi zetu kunufaisha wauzaji wa gesi ambapo mwisho wa siku ni mataifa ya nje tunaweza kutumia pesa hizo kuhakikisha kila mtu anaunganishwa na umeme na umeme unakuwa bei rahisi na vifaa vya umeme kuwekewa ruzuku.


Hitimisho
Kwa Mazingira yetu ya Tanzania Nishati ambayo inaweza ikawa safi ya kupikia na ambayo ni practical na tunaweza kuipata kwa haraka na urahisi ni kwa kutumia Umeme, badala ya kuhangaika na kusambaza gesi asilia majumbani kwa watu kwenye mabomba, ambayo itakuwa ni gharama kubwa tunaweza kusambaza gesi hio asilia mpaka kwenye vyanzo vya uzalishaji wa umeme ili Gesi hio Ibadilishwe kuwa umeme na kuungana na vyanzo vingine (maji, solar, upepo n.k.) na kusambazwa kwenye kila Kaya tayari kwa watu kupikia.

NB: Ushauri wa kuachana na LPG (Mitungi ya Gesi ya Sasa Majumbani) itaacha wengi ambao ndio Biashara yao kwenye hasara ila kwa kurekebisha hilo Serikali inaweza kushauriana nao au kuwawezesha kwa mikopo wawekeze kwenye matengenezo na marekebisho ya vifaa vya Umeme; kwahio badala ya kuagiza majiko kutoka nje assembly plants zinaweza zikawa nchini jambo ambalo litakuza ajira na kuwapa wigo waliopo kwenye biashara ya LPG kunufaika na Umeme - Badala ya Mihan, Oryx, Taifa gesi tutakuwa na Mihan, Oryx, Taifa Cookers

Makaa ya Mawe coal Tanzania kwa matumizi ya nyumbani, tujifunze kwa wenzetu.

Makaa ya mawe hutumiwa kama chanzo cha ndani cha nishati na kaya za kipato cha chini nchini Afrika Kusini.

Makaa ya mawe ni chanzo cha nishati cha bei nafuu na hutoa matumizi mawili - hupasha joto nyumba na kuruhusu kupikia kufanyika katika kifaa kimoja kwa kutumia mafuta moja tu.

Licha ya bei nafuu na upatikanaji wa nishati , matumizi ya makaa ya mawe husababisha viwango vya juu sana vya uchafuzi wa hewa na magonjwa ya kupumua yanayoambatana - wastani wa dola milioni 160 kwa mwaka nchini Afrika Kusini.

Upatikanaji wa umeme hausababishi kaya kuhama kutoka kwa makaa ya mawe kwa kuwa umeme na vifaa vya umeme vinachukuliwa kuwa haviwezi kumudu.

Mada hii inawasilisha taarifa zilizokusanywa wakati wa utafiti wa msingi wa nishati katika kitongoji cha mijini kilicho na umeme nchini Afrika Kusini, na inaelezea jinsi makaa ya mawe yanatumiwa na kununuliwa na kaya maskini. Njia mbadala ya kuwasha moto, iliyothibitishwa kupunguza moshi na uchafuzi wa hewa fomu moto wa makaa ya mawe imeonyeshwa kwa kaya na matokeo ya kutia moyo chanya.

Mbinu iliyojumuishwa, kushughulikia muundo wa makazi yenye ufanisi wa nishati, usambazaji wa vifaa vya nishati safi na bora pamoja na utumiaji wa njia mbadala ya kuwasha moto, inashauriwa kushughulikia uchafuzi wa mazingira kutokana na matumizi ya makaa ya mawe ya kaya.
1715513502540.png

Mtaa Afrika ya Kusini

Kwa nchini Tanzania juhudi zifanyike nishati hii itumike kwa kuwahusisha wabunifu wa majiko na sufuria za kuhimili nishati ya makaa ya mawe. Mafundi mchundo technicians na viwanda vidogo watiwe moyo kuzalisha majiko ya kuweza kutumia makaa ya mawe ambayo yanapatikana kwa wingi nchini Tanzania na kusafirishwa nchi za nje ili pia yaweze kutumika ndani ya nchi ngazi ya kaya / familia

UNAYAFAHAMU MAKAA YA MAWE?, JIONEE KWENYE BANDARI YA MTWARA TANZANIA YANAVYOSAFIRISHWA KWENDA NJE YA NCHI ..

View: https://m.youtube.com/watch?v=GqXx-H6ZS8Q

2021 17 Julai
Rafael Mbise ambaye ni mkazi wa Wilaya ya Arumeru Mkoa wa Arusha, Tanzania hapa chini katika video amesema amebuni jiko hilo kutokana na kupanda kwa gharama za maisha. UNAWEZA KUWASILIANA NAYE KWA NAMBA HIZI..... 0767390430.


View: https://m.youtube.com/watch?v=GbOvgIebhak
 
Kuwaamini wanasiasa inakupasa uwe zuzu kidogo.
Yaani serikali hii hii iliyopandisha bei ya kuunganisha umeme kutoka 27000 hadi sh 318000 pia ikapandisha na bei za unite za umeme leo wanakuja na swaga za nishati rahisi mnataka kuamini?
Ukiona serikali inataka kufanya mradi na unapambwa jua wazi kuna mtu anatengeneza dili hapo.
Ruzuku itatolewa na gesi haishuki ng'o!
Dili la mhuni mwenye maslahi na LPG hakuna la maana hapo
 
Baada ya kuona kwenye Habari Serikali imeanzisha Mfuko wa Nishati Safi ya Kupikia nikaona ni vema tuangalie kwa nchi Yetu Nishati hio ni ipi na ni vipi itatufaa, ili tusije kuingia gharama ambazo zitakuwa hazina manufaa kwetu.

Nishati zilizopo:
Kwenye kila kaya aina ya Nishati inayotumiwa kupikia inategemea upatikanaji na gharama ya Nishati hio. Kwa mtumiaji wa mwisho gharama anayojali ni ya kifedha ingawa kwa mtizamo wa mazingira, gharama ya kifedha inaweza kuwa ndogo lakini athari za hio nishati zikawa ni kubwa zaidi. Kwa mazingira ya Tanzania Nishati ambazo zinaweza kupatikana na kutumika ni kama ifuatavyo.

Kuni
Ni nishati chafu, na kutokana na moshi ina athari za kiafya kwa mtumiaji, vilevile athari za kimazingira kama kuni hizo zinapatikana kwa kukata miti na sio kutumia mabaki ya miti.

Mkaa (Carbonization) kutoka kwenye Miti
Badala ya kutumia kuni moja kwa moja miti hiyo au mabaki ya miti yakifanyiwa carbonization yaani kuchomwa mkaa, nishati hii inakuwa safi kwa mtumiaji kwa kupunguza athari za kiafya ingawa bado kunakuwa na athari ya kukata miti hovyo ili kuchoma mkaa, jambo ambalo athari yake kimazingira ni kubwa sana.

Mkaa (Carbonization) kutoka kwenye Mabaki ya Mimea, Na Mikaa Mbadala
Sababu hii haitumii miti na kukata misitu athari yake kwa mazingira haipo na vilevile inaweza kusaidia kwa kuondoa mabaki / uchafu ambao hautakiwi na kuubadilisha kuwa nishati. Angalizo; Kutengeneza Nishati hii hutumia pia Nishati, hivyo ukiangalia mtiririko mzima huenda Nishati hii isiwe safi kama inavyodhaniwa kutokana na matumizi ya Nishati nyingine kutengeneza hii Nishati.

Mafuta ya Taa, Methanol na Ethanol
Kwa mafuta ya Taa nishati hii tunainunua kutoka nje hivyo kuna gharama ya manunuzi na katika usafirishaji wake mnyororo mzima ni wa gharama. Watu wanaweza kutengeneza Methanol / Ethanol kama vile wanavyopika gongo ila myonyoro mzima wa upatikanaji wa hio nishati ni gharama.

Gesi Asilia (Biogas) na Gesi ya Mtwara
Gesi asilia mtu mmoja mmoja mfugaji au sehemu kama kwenye mashule wanaofuga au kwenye Magereza wanaweza kutumia Kinyesi na kutengeneza Biogas kwa mapishi yao, hii itasaidia katika kuondoa mabaki (uchafu) na kuweza kubadilisha kuwa mbolea. Gesi asilia ya Mtwara inaweza kutumika kwa ufanisi iwapo tu itafungwa moja kwa moja kutoka kwenye Source, na kupelekwa kwa mabomba (kama vile mfumo wa maji ulivyo) mpaka kwa mtumiaji, ingawa utengenezaji wa miundombinu hiyo ni gharama sana na kama kutakuwa kunatokea uvujaji wa hii Gesi tutakuwa tunachafua mazingira kwa gesi hio (methane) kuingia moja kwa moja kwenye mazingira hivyo badala ya kuwa nishati Safi itakuwa moja ya Nishati Chafu....

Gesi ya Mitungi (LPG)
Hii ndio nishati inayopigiwa chapio na wengi na ndio inayotumika majumbani, lakini ina hasara kuu mbili kwa taifa letu, Moja ni kwamba tunaagiza kutoka nje hivyo inahitaji gharama ya kununua, na mbili hata ikishafika usafirishaji wa kutoka point moja mpaka nyingine bado ni matumizi ya Nishati. Na gharama yake bado ni kubwa kuliko uwezo wa watu ndio maana watu wanatumia Nishati nyingine. Na tukisema tuweke ruzuku kusaidia watu kununua, tatizo bado lipo palepale ukizingatia ni pesa hizo hizo tunazochukua kwa hao wasiojiweza kama Kodi na kuwarudishia kama ruzuku ili wanunue kitu ambacho kinanufaisha mataifa ya nje pindi tunapoagiza hii gesi

Umeme
Hii nimeiweka mwisho sababu ndio nishati safi ya kupikia kuliko zote kulingana na mazingira yetu ya Tanzania, kama tutaweza kutumia vyanzo vyetu vizuri, na hili linaweza kufanikiwa ikiwa tutafanya yafuatayo:-

  • Watanzania Wengi ndio Wanafikiwa na Umeme kuliko Nishati nyingine yoyote: Miundombinu tayari ipo watu karibia wote wana plug za umeme majumbani kwao hivyo tunaweza kutumia hio nishati kama umeme utakuwa wa gharama nafuu sana, Kama tukisema tushushe bei kwenye gesi tunaweza kushusha bei mpaka ile bei tunayonunulia lakini umeme ambao tunazalisha tunaweza kupaga bei za units bila kutegemea soko la dunia

  • Vifaa vya Umeme Vipatikane kwa Gharama Nafuu / Kutoa Ruzuku; Kama tukiondoa Ushuru au kutoa Ruzuku katika vifaa vya umeme basi ufanisi wa Kupikia umeme utakuwa zaidi ya Gesi; watu watatumia Oven kuokea, Watatumia Rice Cooker kupikia Wali; Flyers kupikia Chips na Jug Kettles kuchemshia Maji n.k.

  • Matumizi ya Induction Cooker; Ingawa kwa kipindi kirefu majiko ya gesi yalikuwa yanapiku majiko ya umeme katika ufanisi (yaani ilikuwa inachukua muda mchache kwa gesi kupata moto unaotaka wakati coil ya umeme inachukua muda mrefu) ila kwa sasa hivi induction cooker ni instant (wakati huo huo) ukiwasha unapata joto unalotaka na moto unawaka pale tu kwenye sufuria pengine pote kunakuwa hakuna moto (hivyo hakuna upotevu wa nishati)

  • Badala ya Kutoa Ruzuku watu Wanunue Gesi za Kunufaisha wengine Tutoe Ruzuku watu Waunganishwe na Umeme na Kununua Vifaa vya Umeme; Nimeona kwenye Habari Serikali imeanzisha mfuko wa Nishati safi…, sasa badala ya kutumia mfuko huo na Kodi zetu kunufaisha wauzaji wa gesi ambapo mwisho wa siku ni mataifa ya nje tunaweza kutumia pesa hizo kuhakikisha kila mtu anaunganishwa na umeme na umeme unakuwa bei rahisi na vifaa vya umeme kuwekewa ruzuku.


Hitimisho
Kwa Mazingira yetu ya Tanzania Nishati ambayo inaweza ikawa safi ya kupikia na ambayo ni practical na tunaweza kuipata kwa haraka na urahisi ni kwa kutumia Umeme, badala ya kuhangaika na kusambaza gesi asilia majumbani kwa watu kwenye mabomba, ambayo itakuwa ni gharama kubwa tunaweza kusambaza gesi hio asilia mpaka kwenye vyanzo vya uzalishaji wa umeme ili Gesi hio Ibadilishwe kuwa umeme na kuungana na vyanzo vingine (maji, solar, upepo n.k.) na kusambazwa kwenye kila Kaya tayari kwa watu kupikia.

NB: Ushauri wa kuachana na LPG (Mitungi ya Gesi ya Sasa Majumbani) itaacha wengi ambao ndio Biashara yao kwenye hasara ila kwa kurekebisha hilo Serikali inaweza kushauriana nao au kuwawezesha kwa mikopo wawekeze kwenye matengenezo na marekebisho ya vifaa vya Umeme; kwahio badala ya kuagiza majiko kutoka nje assembly plants zinaweza zikawa nchini jambo ambalo litakuza ajira na kuwapa wigo waliopo kwenye biashara ya LPG kunufaika na Umeme - Badala ya Mihan, Oryx, Taifa gesi tutakuwa na Mihan, Oryx, Taifa Cookers
Haya Sasa ndo madini yanayohotajika hapa JF. Sio notes za mapambio na mashudu mengi yasiyo eleweka..
 
Mafundi mchundo technicians na viwanda vidogo watiwe moyo kuzalisha majiko ya kuweza kutumia makaa ya mawe ambayo yanapatikana kwa wingi nchini Tanzania

Kamati yafika wilaya ya Mbinga kuangalia mojawapo ya mgodi wa makaa ya mawe mkoani Ruvuma nchini Tanzania

View: https://m.youtube.com/watch?v=mrIYzP9g8zw

Juhudi ya kupata nishati ya makaa ya mawe kwa ajili ya matumizi ya kupikia majumbani hii itaokoa miti yetu ktk mapori na misitu isitumike kama kuni na mkaa wa kupikia majumbani
 
Makaa ya Mawe coal Tanzania kwa matumizi ya nyumbani, tujifunze kwa wenzetu.

Makaa ya mawe hutumiwa kama chanzo cha ndani cha nishati na kaya za kipato cha chini nchini Afrika Kusini.

Makaa ya mawe ni chanzo cha nishati cha bei nafuu na hutoa matumizi mawili - hupasha joto nyumba na kuruhusu kupikia kufanyika katika kifaa kimoja kwa kutumia mafuta moja tu.
Kuna watu India wanapikia hadi mavi ya ng'ombe issue ni upatikanaji na bei nafuu kwahio hata haya tukiyapata / kuyatumia hapa yatakuwa nafu, pia sawa yana unafuu wa gharama je kwa afya, sababu wadau wa mazingira ulimwenguni wanaweza kuanza kukupiga majungu.... Mwisho kabisa ushauri wangu kama haya yanapatikana na kwa bei nafuu kuliko vyanzo vingine na bila athari kubwa za kimazingira badala ya kuyasambaza kwenye kila kaya kwanini tusiyapeleke sehemu moja tu ili yakafue umeme na hizi kaya zilitewe umeme (ambao ni rahisi kuutumia)?
Licha ya bei nafuu na upatikanaji wa nishati , matumizi ya makaa ya mawe husababisha viwango vya juu sana vya uchafuzi wa hewa na magonjwa ya kupumua yanayoambatana - wastani wa dola milioni 160 kwa mwaka nchini Afrika Kusini.
Unaona hata kwenye hii article yako wanayapiga vita
Upatikanaji wa umeme hausababishi kaya kuhama kutoka kwa makaa ya mawe kwa kuwa umeme na vifaa vya umeme vinachukuliwa kuwa haviwezi kumudu.
Naam bei ni kubwa ya umeme (ambayo mimi nasema kwa vyanzo vyetu ishuke hata kufikia 25/= kwa unit) bila hivyo watu wataendelea kufanya magendo hata mkipiga vita mkaa au wengine watalala njaa sababu gharama ya chakula itakuwa imeongezeka...
Mada hii inawasilisha taarifa zilizokusanywa wakati wa utafiti wa msingi wa nishati katika kitongoji cha mijini kilicho na umeme nchini Afrika Kusini, na inaelezea jinsi makaa ya mawe yanatumiwa na kununuliwa na kaya maskini. Njia mbadala ya kuwasha moto, iliyothibitishwa kupunguza moshi na uchafuzi wa hewa fomu moto wa makaa ya mawe imeonyeshwa kwa kaya na matokeo ya kutia moyo chanya.

Mbinu iliyojumuishwa, kushughulikia muundo wa makazi yenye ufanisi wa nishati, usambazaji wa vifaa vya nishati safi na bora pamoja na utumiaji wa njia mbadala ya kuwasha moto, inashauriwa kushughulikia uchafuzi wa mazingira kutokana na matumizi ya makaa ya mawe ya kaya.
View attachment 2988769
Mtaa Afrika ya Kusini

Kwa nchini Tanzania juhudi zifanyike nishati hii itumike kwa kuwahusisha wabunifu wa majiko na sufuria za kuhimili nishati ya makaa ya mawe. Mafundi mchundo technicians na viwanda vidogo watiwe moyo kuzalisha majiko ya kuweza kutumia makaa ya mawe ambayo yanapatikana kwa wingi nchini Tanzania na kusafirishwa nchi za nje ili pia yaweze kutumika ndani ya nchi ngazi ya kaya / familia

UNAYAFAHAMU MAKAA YA MAWE?, JIONEE KWENYE BANDARI YA MTWARA TANZANIA YANAVYOSAFIRISHWA KWENDA NJE YA NCHI ..

View: https://m.youtube.com/watch?v=GqXx-H6ZS8Q

2021 17 Julai
Rafael Mbise ambaye ni mkazi wa Wilaya ya Arumeru Mkoa wa Arusha, Tanzania hapa chini katika video amesema amebuni jiko hilo kutokana na kupanda kwa gharama za maisha. UNAWEZA KUWASILIANA NAYE KWA NAMBA HIZI..... 0767390430.


View: https://m.youtube.com/watch?v=GbOvgIebhak

Okay hii ni mbinu ambayo huenda itapunguza makali ya ki-afya je hayo makaa yatakuwa bei gani mtaani ?, Mbili kuna athari za makaa ya mawe katika uchimbaji au utunzaji yanaweza kuathiri ground water na uwakaji wake una emissions zaidi ya LPG...,

Lakini mimi am all for that kama hii nishati inafaa ni bora iende kufua umeme na watumiaji waletewe nishati majumbani inayofanya shughuli zao zote hapo majumbani kuanzia kuchemsha maji mpaka kukaanga chips na kuoka mikate.
 
Kamati yafika wilaya ya Mbinga kuangalia mojawapo ya mgodi wa makaa ya mawe mkoani Ruvuma nchini Tanzania

View: https://m.youtube.com/watch?v=mrIYzP9g8zw

Juhudi ya kupata nishati ya makaa ya mawe kwa ajili ya matumizi ya kupikia majumbani hii itaokoa miti yetu ktk mapori na misitu isitumike kama kuni na mkaa wa kupikia majumbani

Naam kama hayo makaa ya mawe yapo na ni rahisi kuliko vyanzo vingine huoni kwamba itakuwa na ufanisi zaidi kama tukiyatumia kuzalisha umeme alafu tukatumia umeme huo kupikia ? Ukizingatia kama tutakuwa na umeme mwingi kuliko mahitaji basi kuna uwezekano wa umeme kushuka bei kama tutaacha ubinafsi na tamaa za watu wachache za kutumia shida za wengine kama fursa.... (Umeme ni Huduma)
 
Unaona hata kwenye hii article yako wanayapiga vita

Mabeberu tusiwasikilize, tutumie makaa ya mawe kwa matumizi ya kupikia na hii itapelekea misitu yetu kuongezeka hivyo hewa safi zaidi pia mazingira ya kijani kutunzwa
 
Mabeberu tusiwasikilize, tutumie makaa ya mawe kwa matumizi ya kupikia na hii itapelekea misitu yetu kuongezeka hivyo hewa safi zaidi pia mazingira ya kijani kutunzwa
Swali linakuja kipi ni rahisi kuchukua haya makaa ya mawe na kuyauza kama mkaa au kuchukua haya makaa ya Mawe kuyapeleka sehemu ya kufua umeme na huo umeme kuusambaza katika kila Kaya.., Badala ya kusafirisha mizigo ya makaa ya mawe tusafirishe umeme mpaka majumbani
 
Makamu wa Rais amesema Serikali inayoongozwa na Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan imetoa kipaumbele cha juu kukuza matumizi ya nishati safi ya kupikia hapa nchini kwenye ajenda ya Taifa ya maendeleo pamoja na kuongeza rasilimali kuhakikisha ajenda hiyo inafanikiwa. Amesema Rais amefanya maamuzi makubwa ikiwemo kuunda Kamati ya Kitaifa itakayosimamia utekelezaji wa ajenda hiyo, kuanzisha mfuko wa nishati safi ya kupikia ili kuweka ruzuku itakayowawezesha wananchi wa kipato cha chini kumudu bei ya gesi na kuchagiza matumizi ya nishati safi ya kupikia kwa taasisi za Serikali zinazohudumia watu zaidi ya 100 kwa siku.

Hapo kwenye Bold ndio point yangu kubwa huenda tunapotea kabla hatujaanza kwa kutoa ruzuku ili watu wanunue gesi (In short ni kutumia Kodi zetu kunufaisha wauzaji wa gesi ambao ni mataifa ya mbali) na wasambazaji ambao ni wafanyabiashara wachache...
Rosti Tamu ambaye ni mpambe wa Mama na mfanyabiashara maarufu wa gesi tayari ashampanga mama ili apige pesa
Kama ulivyosema nishati rahisi kwa sasa ni umeme ambao upo wa kutosha na ukishushwa bei watu wengi watahama kwenye kupika kwa kuni,mkaa,na gesi na kuamia kwenye umeme na hilo wafanyabishara wa gesi hawawezi kubali kirahisi.
 
Nimesikia Serikali na Wizara ya Nishati inajiweka sawa ili kuongeza miundombinu ya kuweza kupokea gesi nyingi zaidi (yaani kuagiza) kweli nimesikitika sana..., Hii ni kuonyesha kwamba tumeamua kwenda njia ya Propane gesi (gesi ya kuagiza)
 
Nauza gesi huu ushauri siutaki
Faidaya yako kwa gesi kwa mwezi ni kiasi gani kama ni retailer nadhani itakuwa kwenye buku tano.., lakini huoni kwamba badala ya hizo bilioni tulizopewa nje kuwanufaisha makampuni ya ulaya kina Oryx hizo pesa msipewe nyie badala ya kuuza mitungi muuze majiko ya umeme na viwanda vya ku-assemble na ku-repair majiko ?

Na sisi tusiouza gesi badala ya kutumia elfu 50 na kitu kununua mtungi ili tupike labda kwa mwezi gharama ikishuka tukatumia hata elfu 20 au kumi kwa bei hio chenji inayobaki tukafanya mengine huoni kila mtu atanufaika ?
 
Faidaya yako kwa gesi kwa mwezi ni kiasi gani kama ni retailer nadhani itakuwa kwenye buku tano.., lakini huoni kwamba badala ya hizo bilioni tulizopewa nje kuwanufaisha makampuni ya ulaya kina Oryx hizo pesa msipewe nyie badala ya kuuza mitungi muuze majiko ya umeme na viwanda vya ku-assemble na ku-repair majiko ?

Na sisi tusiouza gesi badala ya kutumia elfu 50 na kitu kununua mtungi ili tupike labda kwa mwezi gharama ikishuka tukatumia hata elfu 20 au kumi kwa bei hio chenji inayobaki tukafanya mengine huoni kila mtu atanufaika ?
Nikishakuhudumia utarudi tena lini?
Gesi kila mwezi lazima ujaze gesi
 
Nikishakuhudumia utarudi tena lini?
Gesi kila mwezi lazima ujaze gesi
Utahamia kwenye kuuza maji ya kunywa (Kila siku lazima wanywe) au vijisenti watu watakavyosave badala ya kununua gesi wataweza kununua nyama (Hivyo pesa yao utaipata pengine) na nzuri zaidi hii pesa itazunguka ndani sio kupelekea watu ughaibuni ili kununua gesi jumla tuje kuuza rejareja...
 
Utahamia kwenye kuuza maji ya kunywa (Kila siku lazima wanywe) au vijisenti watu watakavyosave badala ya kununua gesi wataweza kununua nyama (Hivyo pesa yao utaipata pengine) na nzuri zaidi hii pesa itazunguka ndani sio kupelekea watu ughaibuni ili kununua gesi jumla tuje kuuza rejareja...
Logikos, huu ni ushahidi mzuri wa binadamu sisi,

Binadamu ni kiumbe mbinafsi sana, anapoona unataka kuingikia maslahi yake, yupo tayali hata kukupoteza,

Nimekuwa nikisoma maandiko yako, yanaonyesha kabisa upo kwa ajili ya kuona maisha ya Mama zetu , ndugu yanapata unafuu,

Lakini unabypass baadhi ya vitu ambavyo ni logic kabisa.,

Sasa sijui hujui au umeamua kuweka mtego tu,

Ni vitu gani hivyo, nitaeleza.

Hivi kwa ufahamu wako wewe , unadhani haya uliyoelezea hayafahamiki huko kwa watoa maamuzi,

Yanafahamika sana, shida ni UROHO WA PESA, UBINAFSI, ROHO MBAYAUBINADAMU ZIRO,

Haya yote wanajua , lakini wanachoangalia ni kuneemesha matumbo yao.

Mtu anaona aneemeka yeye kwa kuagiza gas, ili mfuko wako utune , lakini sio kumsaidia Mwananchi.

Hivi unajua kwa nini walipiga vita bwawa la Mwalimu,

Ni kwamba walijua ndio mwisho wa kuneemeka.

Na nakwambia hata likiisha vile vinu tisa vyote vya kufua umeme haviwezi kuwashwa.

Magufuli alipunguza mpaka bei ya kuunganisha umeme, na mambo yakaenda, kwa nini hawa leo wamepandisha tena mpaka laki tatu,

Hivi kwa nini hata walishindwa kupandisha mpaka 100000/-, iende mpaka 300000 ? , hii ni kwa manufaa ya nani,

Kingine unachosahau , hawa watu wameshindwa kubunu au kukusanya kodi, sasa wameina njia nafuu ya kukusanya kodi ni kuwaminya wananchi, maana hiyo ni njia njia nyepesi sana ya kukusanyia kodi, sio kukupa unafuu wa maisha wewe mwananchi,

Hawa watu ni wabaya sana, hawana huruma na wananchi, wana mapesa mengi sana lakini hawalidhiki,

Mtu anaona bora kutetea wajengewe majumba wakustaafu , au walipwe posho za waume zao, wakistaafu, pamoja na mapesa yote wakiyonato, lakini sio kumtetea mwananchi hata kumpa unafuu wa kupika chakula tu.

Kwa hiyo kaa ukijua haya unayoyaandika sio kwamba ni mawazo mapya , hapana wanajua sana,

Ika ni roho mbaya tu.

Labda ungeanduka namna ya kuwafanya hawa watu waache riho mbaya.

Nimemnnukia MAMAyangu jiko la gesi na taa ya solar, lakini vyote vimebaki mapambo tu, amerudi kwenda kuokota kuni. Sababu gharama zake sio rahisi jihivyo, leo hawa wanasuport mambo ya gesi, hicho kipato cha wananchi kutumia gas wamekiongeza lini.

Acha ndugu, hata mambo ni magumu.

Magufuli tu ndiye aliyeweza kusema neno moja tu na mambo yakawa. Sio hawa ambao tunao.
 
Hivi kwa ufahamu wako wewe , unadhani haya uliyoelezea hayafahamiki huko kwa watoa maamuzi,

Yanafahamika sana, shida ni UROHO WA PESA, UBINAFSI, ROHO MBAYAUBINADAMU ZIRO,

Haya yote wanajua , lakini wanachoangalia ni kuneemesha matumbo yao.

Mtu anaona aneemeka yeye kwa kuagiza gas, ili mfuko wako utune , lakini sio kumsaidia Mwananchi.
Naam wao wanajua lakini wananchi hawajui ndio maana wanalishwa propaganda kwahio mimi hapa najaribu kuweka upande wa pili ili wananchi wajue ukweli wa mambo..., nimegundua wananchi wanadhani haya ni ya kweli:-
  1. Kwamba hii gesi ya kwenye mitungi majumbani inaweza ikawa ndio gesi yetu asilia ya Mtwara hivyo hatuagizi
  2. Kwamba umeme hautoshi wala hauwezi kutosha kwa watu kupikia
  3. Kwamba umeme hata ukiwa mwingi tukimaliza Bwawa tutauza nje au tumekopa sana hivyo tutakuwa tunalipa wanaotudai hivyo hauwezi kushuka bei
  4. Kwamba umeme sio wa uhakika hivyo utakuwa unakatika katika wakati gesi ipo
  5. Kwamba wanaweza wakapewa ruzuku gesi ishuke (hawajui kwamba pesa ya ruzuku ni pesa yao inachukuliwa kwa mgongo wa nyuma)
  6. Kwamba nishati nafuu ni gesi na umeme hauwezi kuufikia nishati hii
  7. Kwamba hizi units za umeme tunazolipia ni fair kabisa wala hazina tatizo na haziwezi kupungua (wakati ukweli ni kwamba zamani walikuwa na vifaa vya umeme visivyo na ufanisi na bado walivitumia na walimudu gharama)
Sasa motive yangu ni hopefully wakiwa wanapita kumpa mama yako mtungi wa gesi na jiko la gesi bure (ili wamteke kila baada ya ukiisha anunue tena na hatakuwa hana choice sababu mkaa utapigwa marufuku) AWEZE Kuwauliza haya ambayo by the atakuwa anayajua na sasa hayajui....
 
Naam wao wanajua lakini wananchi hawajui ndio maana wanalishwa propaganda kwahio mimi hapa najaribu kuweka upande wa pili ili wananchi wajue ukweli wa mambo..., nimegundua wananchi wanadhani haya ni ya kweli:-
  1. Kwamba hii gesi ya kwenye mitungi majumbani inaweza ikawa ndio gesi yetu asilia ya Mtwara hivyo hatuagizi
  2. Kwamba umeme hautoshi wala hauwezi kutosha kwa watu kupikia
  3. Kwamba umeme hata ukiwa mwingi tukimaliza Bwawa tutauza nje au tumekopa sana hivyo tutakuwa tunalipa wanaotudai hivyo hauwezi kushuka bei
  4. Kwamba umeme sio wa uhakika hivyo utakuwa unakatika katika wakati gesi ipo
  5. Kwamba wanaweza wakapewa ruzuku gesi ishuke (hawajui kwamba pesa ya ruzuku ni pesa yao inachukuliwa kwa mgongo wa nyuma)
  6. Kwamba nishati nafuu ni gesi na umeme hauwezi kuufikia nishati hii
  7. Kwamba hizi units za umeme tunazolipia ni fair kabisa wala hazina tatizo na haziwezi kupungua (wakati ukweli ni kwamba zamani walikuwa na vifaa vya umeme visivyo na ufanisi na bado walivitumia na walimudu gharama)
Sasa motive yangu ni hopefully wakiwa wanapita kumpa mama yako mtungi wa gesi na jiko la gesi bure (ili wamteke kila baada ya ukiisha anunue tena na hatakuwa hana choice sababu mkaa utapigwa marufuku) AWEZE Kuwauliza haya ambayo by the atakuwa anayajua na sasa hayajui....
Yaeh , bahati nzuri hawa watu ni wajuzi wa plopaganda,
Na sisi wananchi wananchi wameshatufanya majuha,

Ndio maana kitu chochote cha kutufanya tuwe na ufahamu wametuzibia,

Utaona mwaka kesho uchaguzi ukifika namna wananchi watakavyowashobokea,

Tunasahau kila kitu,

Wana roho mbaya sana hawa viumbe
 
Yaeh , bahati nzuri hawa watu ni wajuzi wa plopaganda,
Na sisi wananchi wananchi wameshatufanya majuha,

Ndio maana kitu chochote cha kutufanya tuwe na ufahamu wametuzibia,

Utaona mwaka kesho uchaguzi ukifika namna wananchi watakavyowashobokea,

Tunasahau kila kitu,

Wana roho mbaya sana hawa viumbe
Na sisi tunawaachia ndio maana humu nilitegemea niweke uzi huu kama mtego ili watu waje wanibishie au wanieleweshe au wanifahamishe wapi nimekosea..., sasa navyoona kimya nashangaa, na sidhani kama wote wanafaidika na huu ulambaji asali ni kwamba wengi ni kina sisi ambao tunalipia gharama katika matumizi na wajukuu watalipa Madeni ya Mikopo tutakayokopa ili tufanikishe huu mradi wa kuwanufaisha wachache na mataifa ya mbali...
 
Na sisi tunawaachia ndio maana humu nilitegemea niweke uzi huu kama mtego ili watu waje wanibishie au wanieleweshe au wanifahamishe wapi nimekosea..., sasa navyoona kimya nashangaa, na sidhani kama wote wanafaidika na huu ulambaji asali ni kwamba wengi ni kina sisi ambao tunalipia gharama katika matumizi na wajukuu watalipa Madeni ya Mikopo tutakayokopa ili tufanikishe huu mradi wa kuwanufaisha wachache na mataifa ya mbali...
Inasikitisha sana,
Lakini ipo siku isiyokuwa na jina inakuja,

Na mwenyezi Mungu asivyokuwa na haiana , amewapiga upofu mkubwa sana , kiasi kwamba hawasikii wala hawaoni.

Mungu ibariki Nchi yangu,
 
Back
Top Bottom