Nini kifanyike ili elimu ya Tanzania iende na mahitaji ya soko la Ajira?

Wild Flower

Member
Jul 20, 2023
87
103
Habari wakuu, nina marafiki wengi walio hitimu chuo mwaka jana lakini mpaka sasa wanahangaika sana na suala la ajira. Nimekuja kugundua kwamba elimu ya Tanznaia haizingatii mahitaji ya soko la ajira kwa sasa na bado tunatumia elimu ya wakolonia aisee. mimi ningeshauri hatua zifuatazo zifanyike ili tupunguze wimbi la "unemployed" mtaani:

Marekebisho ya Mtaala: Mtaala unapaswa kufanyiwa marekebisho ili kuweka msisitizo zaidi katika kutoa stadi za kitaalamu na kiufundi. Mtaala unapaswa kuwa na mchanganyiko wa masomo ya kimsingi na yale ya kitaaluma yanayolingana na mahitaji ya soko la ajira. Unakuta mtu unafundishwa History 2 mambo ya War of roses huko Europe au Fishing in Netherlands kweli?!

Ushirikiano kati ya Vyuo Vikuu na Sekta ya Umma na Binafsi: Vyuo Vikuu vinapaswa kushirikiana na sekta ya umma na binafsi ili kuelewa mahitaji ya soko la ajira na kubadilisha mtaala ili kukidhi mahitaji hayo. Hii itasaidia kuhakikisha kwamba wahitimu wanatoka na stadi zinazohitajika na soko la ajira. chuoni tunafundishwa sana theory na tukija mtaani vile tulivyofundishwa hata haviingii kabisa kwenye kazi zetu. Practical methods zitumike sana. Mtu unafundishwa kuhusu Kompyuta kwenye projector alafu ukipewa huwezi kuitumia. Kuna haja ya kuimarisha mafunzo ya vitendo kwa wanafunzi ili waweze kupata uzoefu halisi wa kazi kabla ya kuhitimu. Hii itasaidia kuwaandaa kisaikolojia na kiuhalisia kwa ajira wanazotafuta.

Napendekeza kwa vyuo hata wasome miaka miwili full alafu mwaka watatu wapangiwe stations za kufanya practical ili kuepuka wimbi kubwa la wahitimu kuangukia kama volunteers au interns sehemu za kazi kwa muda mrefu kwa sababu hawana uwezo mkubwa na ujuzi unaotakiwa kwenye soko la ajira.
 
Toeni kwanza CCM madarakani, kwa sababu inanufaika na mfumo uliopo. Inafaidika na wingi wa wajinga
 
Tuanze na viongozi wenye maono katika secta hiyo ya elimu, pili tuwe na serikali sikivu itakayo weka mawazo ya viongozi wenye maono katika matendo
 
Lugha nayo imechangia pakubwa kuifanya elimu ya Tanzania kuwa ya mwisho ukilinganisha na elimu ya Burundi,Rwanda Uganda na Kenya.

Ukiangalia kwenye mashirika ya kimataifa kama uncef,IAEA,IMF,Fao n.k ni rahisi sana kumuona mrundi,mkenya na mganda kwenye hayo mashirika tofauti na mtanzania.

Elimu ya Tanzania imebobea kuwafanya wtz kuwa chawa ili wapate teuzi
 
Kubadili syllabus sawa,lakini vipi KWA hawa waliomaliza vyuo KWA silabasi ya sasa?

Lugha ya Kiingereza itiliwe mkazo toka msingi Watu waive ili waweze kujiamini na kuajirika duniani kote.

Hata makocha bongo hawaendi kufundishwa nje KWA sababu ya lugha gongana ila wa Burundi wanakuja Bongo, Uganda,Kenya wanakuja Bongo.

Hawa walimu TANZANIA wangeweza kwenda duniani huko kufundishwa,yai babaa
 
Kuna jambo naweza kushare hapa

Sasa ukiangalia labour market imekuwa na stiff competition kubwa Sana .

Hivyo ili upate kazi lazima uwe na mambo matatu.

Bahati
Connection
Kuwa competent

Sasa katika kuwa competent nataka tuzungumzie kwa degree zetu hizi za bongo.

Mfano Unaweza kutenganisha haya mambo mawili.

Professional na para professional

Katika professional yako uliyosoma inaweza kuwa outdated au haina soko kabisa

Sasa unapokuwa chuo unaweza kujaribu kupambania Para professional kupitia kusoma vitabu mbalimbali hadi ukaiva na ukawa smart is possible.

Mfano unaweza ukawa umeso ma Human resources Ila unaweza ukaamua kuwa Afisa masoko au Afisa mahusiano kwa kuhakikisha kampuni inatambulika katika jamii n.k

Hii inaweza kusaidia vijana maana sasa hivi vyeti havifanyi kazi Ila ile Value yako ndo inatumika zaidi.

Hivyo Kama professional yako hailipi usiende chuo Mara ya pili Bali pambania hiyo para professional, kwa kusoma mwenyewe course yoyote unayoipenda yenye soko kwa kutumia vitabu na mtandaoni utapata hiyo para professional na itakulipa vizuri

Kumbuka kusoma vitabu na kufatilia mtandaoni Elimu yake inazidi ya chuo hasa vyuo vya bongo
 
Hata ukishushwa mtaala kutoka mbinguni kama hakuna ajira za kutosha bado msoto utakuwa pale pale
 
Kitu Cha kwanza ni hela ya kutosha iwekwe kwenye elimu angalau kama Ile anayoweka Kaizirege na Feza schools
Mbili ni kuboresha lugha ya kufundishia kuanzia chekechea hadi chuo(kingereza)
Tatu kuwekeza kwenye tafiti za mara kwa mara.
Kupanua mtaala sio uwe kwenye arts science na business,uende hadi kwenye kazi za Mikono na michezo(sio kwa kauli Bali vitendo.)zijengwe maabara na karakana za kutosha shuleni
 
Back
Top Bottom