Nini hatima ya Halima Mdee na wenzake baada ya bunge kuvunjwa?

Dah, mbona shajieleza vya kutosha juu ya hili jambo humu humu kwenye mada hii nikijibishana na mkuu 'Zanzibar-ASP'? Mnataka nijibu nini tena.
Halima na hao wenzake aliowaongoza kwenda Bungeni wasingeweza kuwa na uthubutu wa kufanya jambo zito kiasi kile kwa uamzi wao pekee, au ushawishi toka nje ya chama chao. Waeleweni hawa wanawake walivyokuwa ngangari kwelikweli wakati mgumu sana.
Sijasema hapa, kwamba kiongozi toka CHADEMA aliwashawishi waasi, la hasha, lakini ni lazima mjue kwamba vitisho vya Magufuli tu wakati huo visingetosha hawa mabinti wafanye kama walivyofanya. Ni lazima pawepo na 'consultation' ndani ya chama (hata kama ni kiongozi mmoja bila ya kushirikisha wengine).
You really believe that? Ulielewa jinsi vitisho vya Magufuli vilivyokuwa enzi zile? Jinsi vilivyobadili mazingira ya kisiasa ndani na nje ya CCM na kuuweka mustakabali mzima wa taifa mikononi mwa mtu mmoja?

Halafu hiyo “consultation ndani ya chama” ilikuwa na uzito gani kuzidi vitisho vya Magufuli na manufaa ya aina gani kiasi cha kuwa na ushawishi kwa kina Halima kutupilia mbali legacy na hatma zao za kisiasa?
 
You really believe that? Ulielewa jinsi vitisho vya Magufuli vilivyokuwa enzi zile? Jinsi vilivyobadili mazingira ya kisiasa ndani na nje ya CCM na kuuweka mustakabali mzima wa taifa mikononi mwa mtu mmoja?

Halafu hiyo “consultation ndani ya chama” ilikuwa na uzito gani kuzidi vitisho vya Magufuli na manufaa ya aina gani kiasi cha kuwa na ushawishi kwa kina Halima kutupilia mbali legacy na hatma zao za kisiasa?
Vuta subira mkuu, hakuna lisilowezekana; wakati utakapofika historia itajinyoosha yenyewe.
Unajua, hata Lowassa kwenda CHADEMA stori hiyo hadi leo ina utata; sasa hii ya hawa mabinti unadhani kila kitu kitafunuliwa ili kukuridhisha tu udadisi wako?

Ni mambo gani mengine yanayotokea ndani ya chama, hata kule CCM lakini watu hawajui lolote juu yake.
 
Vuta subira mkuu, hakuna lisilowezekana; wakati utakapofika historia itajinyoosha yenyewe.
Unajua, hata Lowassa kwenda CHADEMA stori hiyo hadi leo ina utata; sasa hii ya hawa mabinti unadhani kila kitu kitafunuliwa ili kukuridhisha tu udadisi wako?

Ni mambo gani mengine yanayotokea ndani ya chama, hata kule CCM lakini watu hawajui lolote juu yake.
Hakika mimi nasubiri sana huo uthibitisho wa wanaodai kuwa viongozi wa CHADEMA walihusika na sakata la Covid 19. Nashangaa huo ushahidi hauji. Ni maneno mengi tu toka circles za wanapropaganda wa CCM na vyama mahasimu wa CHADEMA na Mbowe.

Mbowe mwenyewe na viongozi wa CHADEMA wamejitokeza hadharani kukanusha kwa facts. Mahakamani ushahidi wa facts na documents umetolewa na haukukanushwa. Badala yake ni CCM kushikilia kuwakumbatia Covid 19 na hizi bla bla za underground zinaendelea kama ilivyokuwa kwa kifo cha Chacha Wangwe.

Kinachonishangaza hadi sasa ni serikali ya CCM kutochangamkia fursa ya kumwaga ushahidi wa kuwaumbua CHADEMA katika hili wakati najua wana hamu sana ya kukiangamiza chama hicho na makada wake wanaosumbua sana kama Mbowe, Lissu, Lema, Heche, etc. virtually and literally.
 
Mbowe mwenyewe na viongozi wa CHADEMA wamejitokeza hadharani kukanusha kwa facts. Mahakamani ushahidi wa facts na documents umetolewa na haukukanushwa. Badala yake ni CCM kushikilia kuwakumbatia Covid 19 na hizi bla bla za underground zinaendelea kama ilivyokuwa kwa kifo cha Chacha Wangwe.

Kinachonishangaza hadi sasa ni serikali ya CCM kutochangamkia fursa ya kumwaga ushahidi wa kuwaumbua CHADEMA katika hili wakati najua wana hamu sana ya kukiangamiza chama hicho na makada wake wanaosumbua sana ka
Natumaini hunihusishi mimi kuwa sehemu ya huo uchafu wa CCM. Mawazo ninayoyaweka humu ni yangu na hayamhusu mtu mwingine yeyote. Ninacho kichwa ninachokiamini na kukitegemea, 'independently.'
 
Kinachonishangaza hadi sasa ni serikali ya CCM kutochangamkia fursa ya kumwaga ushahidi wa kuwaumbua CHADEMA katika hili wakati najua wana hamu sana ya kukiangamiza chama hicho na makada wake wanaosumbua sana kama Mbowe, Lissu, Lema, Heche, etc. virtually and literally.
Kuna mengi sana yasiyo eleweka kwenye jambo hili, na siyo rahisi kuyatungia nadharia. Ninachokuwa nacho imani nikuwa , vitisho toka kwa Magufuli visingeweza kumtikisa Halima na wenzake, hasa akina Ester wawili. Kwa hiyo hilo mimi nalikataa.
Pesa? Halima anunuliwe, na asahau kabisa aliyokuwa akipigania ndani ya CHADEMA? Halima alikuwa na uhitaji mkubwa wa pesa kiasi kwamba ajisaliti mwenyewe na chama chake. Hili pia nasita kulipa uwezekano mkubwa. Nalipa kiasi fulani cha uwezekano.

Tatu: Pesa ikiambatana na uaminifu kwa kiongozi aliyejuwa kinachoendelea na wanawake hao..., hili nalipa uzito mkubwa zaidi ya mengine yote.

Umezungumzia yaliyoendelea ndani ya mahakama. Hata huko ukichambua yaliyosemwa utabaki na mashaka ya kutokuwepo na uhusika wa kiongozi mkubwa ndani ya CHADEMA. Naomba unielewe vizuri. Sisemi kuwa kiongozi huyo alibariki moja kwa moja hao wanawake wajitose. Ninachosema ni kuwa taarifa juu ya yanayoendelea ni lazima kuna kiongozi aliyejuwa hata kama alinyamazia.
 
Natumaini hunihusishi mimi kuwa sehemu ya huo uchafu wa CCM. Mawazo ninayoyaweka humu ni yangu na hayamhusu mtu mwingine yeyote. Ninacho kichwa ninachokiamini na kukitegemea, 'independently.'
Sawa.
 
Kuna mengi sana yasiyo eleweka kwenye jambo hili, na siyo rahisi kuyatungia nadharia. Ninachokuwa nacho imani nikuwa , vitisho toka kwa Magufuli visingeweza kumtikisa Halima na wenzake, hasa akina Ester wawili. Kwa hiyo hilo mimi nalikataa.
Pesa? Halima anunuliwe, na asahau kabisa aliyokuwa akipigania ndani ya CHADEMA? Halima alikuwa na uhitaji mkubwa wa pesa kiasi kwamba ajisaliti mwenyewe na chama chake. Hili pia nasita kulipa uwezekano mkubwa. Nalipa kiasi fulani cha uwezekano.

Tatu: Pesa ikiambatana na uaminifu kwa kiongozi aliyejuwa kinachoendelea na wanawake hao..., hili nalipa uzito mkubwa zaidi ya mengine yote.

Umezungumzia yaliyoendelea ndani ya mahakama. Hata huko ukichambua yaliyosemwa utabaki na mashaka ya kutokuwepo na uhusika wa kiongozi mkubwa ndani ya CHADEMA. Naomba unielewe vizuri. Sisemi kuwa kiongozi huyo alibariki moja kwa moja hao wanawake wajitose. Ninachosema ni kuwa taarifa juu ya yanayoendelea ni lazima kuna kiongozi aliyejuwa hata kama alinyamazia.
Endelea na fikra zako kama zinavyokuelekeza. Sina tatizo na hilo.

Sahihisho moja tu. Umezungumzia sana habari ya pesa kumnunua Halima. Sina hiyo habari kabisa wala sijatoa hata hint ya kitu kama hicho katika comments zangu. Nimeipigia mistari kabisa uachane nayo. Siwezi kufikiri kitu kama hicho.

Nilichozungumzia ni kama kweli wewe ulivielewa “vitisho vya Magufuli” labda niongeze “kuelekea uchaguzi wa 2020 na baada”. SIO PESA.

Unadai Halima asingeweza kutishika na “vitisho vya Magufuli”? Seriously? (Mime-highlight ulichoandika kwa red bold). Sijui kama ulikuwa na habari za nchi hii kipindi kile. Umemchukulia Magufuli kirahisi rahisi sana. Uliijua ajenda yake ya 2020 and beyond? Unajua kwa nini wanasisa wengi wa upinzani hata waasi ndani ya CCM wali-toe the line kipindi kile? Na baada ya uchaguzi waliokuwa vichwa maji kumpinga kuanza kutafuta kwa kukimbilia?

Naamini wengi wao inc. Halima “wangefunuliwa” kuwa Magufuli would be no more shortly after his second inauguration, wangefanya maamuzi tofauti. Ni bahati mbaya kuwa Magufuli alitengeneza a state of terror hasa kwenye political circles za nchi kiasi wengi (foes and friends alike) waliamini kuwa huyo mtu ni immortal!
 
Tuachane na hao kwanza, hivi ushawafikilia hao wabunge waliopita bila kupingwa ikitokea uchafuzi ukarudi halafu wakarudi tena mjengoni? Magu katika vitu katukomesha basi ni hao wabunge aisee 😕
 
Dah, mbona shajieleza vya kutosha juu ya hili jambo humu humu kwenye mada hii nikijibishana na mkuu 'Zanzibar-ASP'? Mnataka nijibu nini tena.
Halima na hao wenzake aliowaongoza kwenda Bungeni wasingeweza kuwa na uthubutu wa kufanya jambo zito kiasi kile kwa uamzi wao pekee, au ushawishi toka nje ya chama chao. Waeleweni hawa wanawake walivyokuwa ngangari kwelikweli wakati mgumu sana.
Sijasema hapa, kwamba kiongozi toka CHADEMA aliwashawishi waasi, la hasha, lakini ni lazima mjue kwamba vitisho vya Magufuli tu wakati huo visingetosha hawa mabinti wafanye kama walivyofanya. Ni lazima pawepo na 'consultation' ndani ya chama (hata kama ni kiongozi mmoja bila ya kushirikisha wengine).
Magufuli alihitaji Consultation ya kiongozi wa chama alichotaka kukiua ili awape baraka wanachama wake kwenda bungeni ambalo alipinga kwa maandamano uchaguzi wake ?

Kalamu siku hizi unakunywa nini ?
 
Kuna mengi sana yasiyo eleweka kwenye jambo hili, na siyo rahisi kuyatungia nadharia. Ninachokuwa nacho imani nikuwa , vitisho toka kwa Magufuli visingeweza kumtikisa Halima na wenzake, hasa akina Ester wawili. Kwa hiyo hilo mimi nalikataa.
Pesa? Halima anunuliwe, na asahau kabisa aliyokuwa akipigania ndani ya CHADEMA? Halima alikuwa na uhitaji mkubwa wa pesa kiasi kwamba ajisaliti mwenyewe na chama chake. Hili pia nasita kulipa uwezekano mkubwa. Nalipa kiasi fulani cha uwezekano.

Tatu: Pesa ikiambatana na uaminifu kwa kiongozi aliyejuwa kinachoendelea na wanawake hao..., hili nalipa uzito mkubwa zaidi ya mengine yote.

Umezungumzia yaliyoendelea ndani ya mahakama. Hata huko ukichambua yaliyosemwa utabaki na mashaka ya kutokuwepo na uhusika wa kiongozi mkubwa ndani ya CHADEMA. Naomba unielewe vizuri. Sisemi kuwa kiongozi huyo alibariki moja kwa moja hao wanawake wajitose. Ninachosema ni kuwa taarifa juu ya yanayoendelea ni lazima kuna kiongozi aliyejuwa hata kama alinyamazia.
Pesa inazidi uhai ?
 
Wadau nawasabahi.

Uchaguzi ndio huo unakaribia. CHADEMA wameshinda pambano lao dhidi ya Halima Mdee na kundi lake kwa kuishawishi Mahakama Kuu kuthibitisha uhalali wao wa kuwafukuza Halima Mdee na kundi lake uanachama.

Pia, CHADEMA wametekeleza wajibu wa kikatiba kulijulisha Bunge na Tume ya Uchaguzi kuwa Halima Mdee na kundi lake sio wanachama wao kikatiba, hivyo hawastahili kuwa bungeni. Lakini bunge, serikali, na tume ya uchaguzi kwa pamoja wameamua kuvunja katiba kwa makusudi kwa kuendelea kuwalipa mishahara na posho kinyume na sheria kwa mujibu wa katiba. Kwani katiba inasema moja ya sababu za mbunge kupoteza ubunge wake ni "kufukuzwa uanachama na chama chake".

Hakika, bunge letu limeweka historia ya kuwa "Bunge lenye wabunge wasio na chama".
Najiuliza, nini hatima ya Halima Mdee na kundi lake baada ya bunge kuvunjwa?
Je, watajiunga na CCM?
Je, watajiunga na vyama vingine ila sio CHADEMA?
Je, CCM itawateua kama wabunge wa viti maalum?
Au watastaafu siasa?

Ngoja tusubiri 2025.
chadema wamewashida lini hao miamba ya siasa za upinzani? wasijidanganye kuwa waliwashida hizo zilikuw atamaa za kina mbowe ndiyo ziliwafikisha hapo na si kuvunja katiba
 
Kuna mengi sana yasiyo eleweka kwenye jambo hili, na siyo rahisi kuyatungia nadharia. Ninachokuwa nacho imani nikuwa , vitisho toka kwa Magufuli visingeweza kumtikisa Halima na wenzake, hasa akina Ester wawili. Kwa hiyo hilo mimi nalikataa.
Pesa? Halima anunuliwe, na asahau kabisa aliyokuwa akipigania ndani ya CHADEMA? Halima alikuwa na uhitaji mkubwa wa pesa kiasi kwamba ajisaliti mwenyewe na chama chake. Hili pia nasita kulipa uwezekano mkubwa. Nalipa kiasi fulani cha uwezekano.

Tatu: Pesa ikiambatana na uaminifu kwa kiongozi aliyejuwa kinachoendelea na wanawake hao..., hili nalipa uzito mkubwa zaidi ya mengine yote.

Umezungumzia yaliyoendelea ndani ya mahakama. Hata huko ukichambua yaliyosemwa utabaki na mashaka ya kutokuwepo na uhusika wa kiongozi mkubwa ndani ya CHADEMA. Naomba unielewe vizuri. Sisemi kuwa kiongozi huyo alibariki moja kwa moja hao wanawake wajitose. Ninachosema ni kuwa taarifa juu ya yanayoendelea ni lazima kuna kiongozi aliyejuwa hata kama alinyamazia.
Mbona Kigogo wa wakati ule alizungumzia sana mpango mzima? Nadhani wengi hawakuamini kuwa ingeweza kutokea kwa watu kama Halima na wale Ester wawili.
Tutajua ukweli wakati wa uchaguzi wa 2025.

Amandla...
 
Sahihisho moja tu. Umezungumzia sana habari ya pesa kumnunua Halima. Sina hiyo habari kabisa wala sijatoa hata hint ya kitu kama hicho katika comments zangu. Nimeipigia mistari kabisa uachane nayo. Siwezi kufikiri kitu kama hicho.
Mkuu 'Drifter', hukunielewa, sijasema wewe umependekeza au umesema kuwa hiyo ya pesa inaweza ndiyo ikawa kivutio kwa Halima na wenzake. Hapa nazungumzia mifano tu zinazoweza kuwa ni/au sababu zilizochangia. Siyo wewe uliyetoa sababu hizo kama ushahidi.
Kiujumla, katika majadiliano haya sijaona popote ninapoweza kusema sababu ya hawa mabinti kuasi chama chao ni hii na hii; labda hiyo ya kumwogopa Magufuli, ambayo binafsi, kwa mtu kama Halima kama alivyokuwa amejipambanua kabla ya yote, mtu asingetilia mashaka juu ya hilo. La pesa nalo linaniwia vigumu sana kuliamini.

Kuwepo kwa mpango maalum, ambao ulikuwa ukitazamiwa na ukavurugika katikati ya utekelezaji, hili linawezekana sana.
Lakini, wakati huo huo nikimuwaza Halima na wenzake - hivi ingetokea akawaongoza wenzake kujiuzuru ubunge, hata baada ya mahakama, au wakati wowote ingekuwaje?
Kubaki Bungeni hadi wakati huu inaashiria kitu gani kwa Halima na wenzake; kwamba wanao msimamo thabiti juu ya wanachokiamini, au ni kinyume chake?
Nimekufungulia njia ya kunibana ukutani!
 
Mbona Kigogo wa wakati ule alizungumzia sana mpango mzima? Nadhani wengi hawakuamini kuwa ingeweza kutokea kwa watu kama Halima na wale Ester wawili.
Tutajua ukweli wakati wa uchaguzi wa 2025.

Amandla...
Inasikitisha sana na hawa wanasiasa wetu. Thamani yao ni ndogo sana. Hakuna jambo lolote wanaloweza kulisimamia na wananchi wakawaamini juu ya msimamo wao huo kutotetereka.
 
Pesa inazidi uhai ?
Sijui mkuu 'Al-Watani', inaelekea huo ndio utamaduni mpya unaojengeka katika taifa hili. Wewe huoni watu wanaondoana uhai, hasa huko kwenye siasa, msukumo ukiwa pesa? Mtu awe mbunge, hata kama kuuutafuta ubunge huo uhai wa mtu au watu wanaodhaniwa kuuzuia uondolewe.
Kama Halima tuliyemjua kwa msimamo wake juu ya mambo mengi ya muhimu ndani ya chama chake, anaweza kushawishiwa kwa pesa asahau kabisa huo msimamo ambao watu wengi walimuwekea matumaini juu yake...,!

Hii ni dhana tu, ninayojaribu kuidadisi, kama ilihusika kumdhoofisha Halima na kusahau kila kitu alichopewa heshima kubwa ndani ya nchi hii.
 
Back
Top Bottom