Mzee wa Twitter
JF-Expert Member
- Nov 5, 2023
- 1,463
- 2,295
Najaribu kuwaza kilichowapata wafanyakazi wenye vyeti fake walibainika kuwa hawana vyeti halali ili kuhalalisha ajira zao.Wafanyakazi hao waliondolewa haraka serikalini na kusitisha mishahara yao na report ya CAG ikataja na fedha walizokuwa wanalipwa kama mishahara.
Halima mdee na wenzake 18 ni sawa na wafanyakazi wenye vyeti fake kwani ubunge wao umethibitika kuwa sio halali kwa kufukuzwa uanachama na chama chao na ufukuzaji huo ukathibitishwa na mahakama kuu kuwa chadema ilifanya uamuzi sahihi kwa mujibu wa katiba yao.Kinachoshangaza ni pamoja na kuthibitika huko kuwa sio wanachama bado wapo bungeni wanaendelea kulipwa mishahara kama wabunge wakati hawana uanachama na kutokuwa na uanachama ni moja ya sifa za kuenguliwa ubunge kwa mujibu wa katiba.
Swali je report ya cag inasemaje juu ya mishahara wanayolipwa halima mdee na wenzake 18 wakati sio wanachama na hivyo sio wabunge kwa mujibu wa katiba?
Je ni halali kuwalipa mishahara wakati hawana sifa ya ubunge?
Nilitarajia mwenezi wa ccm mzee makalla aiagize TAKUKURU ichunguze kwanini halima mdee na wenzake 18 wanalipwa mishahara wakati chama chao kilikwishawafukuza.
Halima mdee na wenzake 18 ni sawa na wafanyakazi wenye vyeti fake kwani ubunge wao umethibitika kuwa sio halali kwa kufukuzwa uanachama na chama chao na ufukuzaji huo ukathibitishwa na mahakama kuu kuwa chadema ilifanya uamuzi sahihi kwa mujibu wa katiba yao.Kinachoshangaza ni pamoja na kuthibitika huko kuwa sio wanachama bado wapo bungeni wanaendelea kulipwa mishahara kama wabunge wakati hawana uanachama na kutokuwa na uanachama ni moja ya sifa za kuenguliwa ubunge kwa mujibu wa katiba.
Swali je report ya cag inasemaje juu ya mishahara wanayolipwa halima mdee na wenzake 18 wakati sio wanachama na hivyo sio wabunge kwa mujibu wa katiba?
Je ni halali kuwalipa mishahara wakati hawana sifa ya ubunge?
Nilitarajia mwenezi wa ccm mzee makalla aiagize TAKUKURU ichunguze kwanini halima mdee na wenzake 18 wanalipwa mishahara wakati chama chao kilikwishawafukuza.