Kifurukutu
JF-Expert Member
- Aug 29, 2013
- 4,525
- 6,470
JF
Katika jamii kuna makundi ya watu mbalimbali, wapo watu wanaojiweza kumudu mahitaji yao yote lakini pia kuna makundi ya watu hawajiwezi kumudu mahitaji yao ya kila siku katika maisha
Mahitaji muhimu katika maisha ya mwanadamu ni Chakula, malazi na mavazi,, katika jamii yetu hii kuna watu wanakosa mahitaji hayo
Makundi ya watu wenye uhitaji zaidi ni
•watoto yatima
•waanga wa majanga mbalimbali
•Makundi ya watu wenye ulemavu
•Wazee
•Wakimbizi
kwa uchache makundi hayo hapo juu yanakosa mahitaji muhimu ya kibinadamu
Hebu jaribu kujiuliza wewe hapo unayejiweza, utayamudu vipi maisha endapo huna chakula?
maisha yataenda vipi bila kuwa na sehemu ya kuishi na nguo ubadilishe kila siku?
Kama ulikuwa hufahamu sasa naomba ufahamu kwamba mimi na wewe hapo tunaowajibu (lazima) kuwasaidia watu hawa wenye mahitaji muhimu katika jamii
Ni muhimu sana kuwasaidia watu hawa kwa sababu zifuatazo
•Kulinda na kuheshimu utu..hakika utu huifadhiwa na upatikanaji wa chakula malazi na mavazi!
• upendo, amani na mshikamano vinadumishwa katika jamii
• Haki za watu wengine kuishi zinaheshimika kupitia msaada wako wewe
• Kiroho,, Mungu naye hutukumbuka na kutuongezea zaidi pale tulipopunguza
• Misaada yetu inapunguza makundi tegemezi katika jamii
• Hupunguza umasikini katika jamii
Ni mtu wa aina gani anatakiwa kuwasaidia watu wenye mahitaji?
Mtu yoyote yule mwenye uwezo anaweza kumsaidia mtu mwenye uhitaji kwani waswahili husema wema usizidi uwezo hivyo saidia kadili ya uwezo wako,,, uwe na kidogo au kikubwa wewe saidia tu
Hapa Tanzania watu wenye mahitaji wengi humkumbuka sana marehemu Reginald Mengi..Hakika huyu mtu aliwajali watu wenye uhitaji
Ni zamu yetu sasa, mimi na wewe tujitoe kuisaidia jamii kwa kuwagusa hawa watu wenye mahitaji
Tutoke tuwatembelee yatima na wazee katika vituo vya kulea wazee na watoto yatima vilivyo karibu nasi
Tutoke sasa tuzitembelee public schools huko kuna watoto wengi wenye mahitaji wanatusubiri tuwawezeshe wafanikishe ndoto zao kielimu na kimaisha
Mwisho, ni wajibu wa kila mtu anayejiweza kuwasaidia watu wenye uhitaji,, pia serikali na taasisi binafsi hazina budi kushirikiana kuhakikisha zinayasaidia makundi haya muhumu katika jamii
nawasilisha
Katika jamii kuna makundi ya watu mbalimbali, wapo watu wanaojiweza kumudu mahitaji yao yote lakini pia kuna makundi ya watu hawajiwezi kumudu mahitaji yao ya kila siku katika maisha
Mahitaji muhimu katika maisha ya mwanadamu ni Chakula, malazi na mavazi,, katika jamii yetu hii kuna watu wanakosa mahitaji hayo
Makundi ya watu wenye uhitaji zaidi ni
•watoto yatima
•waanga wa majanga mbalimbali
•Makundi ya watu wenye ulemavu
•Wazee
•Wakimbizi
kwa uchache makundi hayo hapo juu yanakosa mahitaji muhimu ya kibinadamu
Hebu jaribu kujiuliza wewe hapo unayejiweza, utayamudu vipi maisha endapo huna chakula?
maisha yataenda vipi bila kuwa na sehemu ya kuishi na nguo ubadilishe kila siku?
Kama ulikuwa hufahamu sasa naomba ufahamu kwamba mimi na wewe hapo tunaowajibu (lazima) kuwasaidia watu hawa wenye mahitaji muhimu katika jamii
Ni muhimu sana kuwasaidia watu hawa kwa sababu zifuatazo
•Kulinda na kuheshimu utu..hakika utu huifadhiwa na upatikanaji wa chakula malazi na mavazi!
• upendo, amani na mshikamano vinadumishwa katika jamii
• Haki za watu wengine kuishi zinaheshimika kupitia msaada wako wewe
• Kiroho,, Mungu naye hutukumbuka na kutuongezea zaidi pale tulipopunguza
• Misaada yetu inapunguza makundi tegemezi katika jamii
• Hupunguza umasikini katika jamii
Ni mtu wa aina gani anatakiwa kuwasaidia watu wenye mahitaji?
Mtu yoyote yule mwenye uwezo anaweza kumsaidia mtu mwenye uhitaji kwani waswahili husema wema usizidi uwezo hivyo saidia kadili ya uwezo wako,,, uwe na kidogo au kikubwa wewe saidia tu
Hapa Tanzania watu wenye mahitaji wengi humkumbuka sana marehemu Reginald Mengi..Hakika huyu mtu aliwajali watu wenye uhitaji
Ni zamu yetu sasa, mimi na wewe tujitoe kuisaidia jamii kwa kuwagusa hawa watu wenye mahitaji
Tutoke tuwatembelee yatima na wazee katika vituo vya kulea wazee na watoto yatima vilivyo karibu nasi
Tutoke sasa tuzitembelee public schools huko kuna watoto wengi wenye mahitaji wanatusubiri tuwawezeshe wafanikishe ndoto zao kielimu na kimaisha
Mwisho, ni wajibu wa kila mtu anayejiweza kuwasaidia watu wenye uhitaji,, pia serikali na taasisi binafsi hazina budi kushirikiana kuhakikisha zinayasaidia makundi haya muhumu katika jamii
nawasilisha