Naombeni msaada wa mawazo kuhusu ni nini cha kufanya

mjenziwakale

JF-Expert Member
Sep 24, 2015
738
967
Salaam,

Katika harakati zangu za kusaka tonge, yupo jamaa ambae nilifahamiana Naye katika biashara, tukawa tumezoeana hadi ikafikia kipindi akiwa na shida na hela namuazima ila anaacha gari yake kama bond, akienda akasupply mizigo yake akilipwa ananirejeshea pesa zangu na yeye anachukua gari yake.

Sasa zamu hii nilimpatia pesa milioni 8 akaniachia gari yake Range Rover namba B akiahidi atarejesha baada ya mwezi mmoja akishalipwa na hiyo halmashauri anakosupply mzigo.

Sasa yapita miezi karibia 6 toka achukue hela na gari lake lipo hapa limelala kila Nikimdai pesa yangu ananambia hajalipwa bado, na hili gari hatujaandikishana kwamba akishindwa kulipa gari iwe mali yangu, binafsi sijawahi kumiliki gari na gari lenyewe nikisema niwe nalitumia kupooza machungu siwezi sababu gari inakula mafuta sana hii.

Imefikia hatua namdai ananambia anatafuta mteja akaliuze hili gari aweze kunilipa hata hvo naona kama sound tu. Nimefikia hatua kumwambia walau anilipe tu nusu ya pesa yangu nilompatia na nusu itakayobaki nihesabu hasara tu ili niweze na mm kulipa madeni yanayoniandama ila bado anadai hela hana coz hajalipwa bado.

Wakuu nafanyaje hapa?
 
Sasa kipi auelewi hapo huyo ajalipwa na hana pesa angekuwa nazo asingeacha kukulipa thamani ya gari ni kubwa kuliko hio pesa.

Ulipaji madeni kwa wakati ni shida serikalini wengi wamefilisika kwa kutegemea biashara hio Moja.

Labda usubiri abahatike kumpata mshamba wa kumuuzia namba B Tena range old model atakulipa kuwa mpole tu
 
kuna slow payment za tenda recently mzee. hata usishangae sehemu nyingi pesa amna. so give him time. maisha tu haya.
Mwamba hadi ananipa go ahead nikipata mteja nimstue hii gari tuuze.....kila nikifikiria hii range namba B old model tunamuuzia nani....inafika wakati naishiwa nguvu kabisaa
 
Ushauri hapo ni akupe funguo walahu Mara moja Mara moja uwe unaliwasha lisije kufa.. Na pia akupe tu ufunguo unaweza ukapata bahati ya kukodiwa kwenye harusi... Si Lina muonekano mzuri bado?
 
Ushauri hapo ni akupe funguo walahu Mara moja Mara moja uwe unaliwasha lisije kufa.. Na pia akupe tu ufunguo unaweza ukapata bahati ya kukodiwa kwenye harusi... Si Lina muonekano mzuri bado?
Funguo ninazo kaniachia ila muonekano wake kwa ndani site zimechoka, kwa nje ndo kupo vizuri...
 
Funguo ninazo kaniachia ila muonekano wake kwa ndani site zimechoka, kwa nje ndo kupo vizuri...
Duh me Sina utalaam sana na wakodisha magari ila Nadhani kuliko likae tu ni heri hata lingekuwa linapiga business kidogo huku ukiongea na madalali huenda ukasaidia kuliuza kama anavyotaka mwenyewe
 
Duh me Sina utalaam sana na wakodisha magari ila Nadhani kuliko likae tu ni heri hata lingekuwa linapiga business kidogo huku ukiongea na madalali huenda ukasaidia kuliuza kama anavyotaka mwenyewe
Mkuu nakushukuru sana.
 
Back
Top Bottom