Uchaguzi 2020 Mwigulu Nchemba: Rais wetu ni Magufuli, waambieni waliowatuma enyi wenye tamaa ya Madaraka

Dr. Mwigulu Nchemba

JF-Expert Member
Feb 25, 2012
416
2,043
1) Kwa Ushupavu wa Rais wetu, Watanzania tumeendelea na shughuli zetu zote, Hatuwazi Jambo moja tu la UCHAGUZI tuseme mazingira ya Corona, TANZANIA uchaguzi na kazi zote zinaendelea vilevile.

2) Tanzania ni nchi HURU, Watanzania tunafanya kazi zote bila uangalizi wa mtu yeyote toka kwa mabeberu, Hatuhitaji KIRANJA kutoka popote awe mwangalizi au MCHOCHEZI aseme ndio kilichofanywa au kilichosemwa kiwe na UHALALI.
KIRANJA wetu ni Rais wetu.

3) Inaudhi Sana, wasio Watanzania waisimange nchi yetu, walioko mbali waisimange nchi yetu, na walioko ndani WATUMIKE kuisimanga nchi yetu, yaani hatuoni kazi zilizofanyika tunaona tu hatuna tume huru???

4) NCHI YETU HATUJAWAHI KUFANYA UCHAGUZI BILA TUME HURU YA UCHAGUZI, MIJITU MINGINE ILIKUWEPO NDANI TANGU UJANA WAO HADI SASA, LEO NDIO WAONE HATUNA TUME HURU?? MLISHAISHI MAISHA YENU TANGU ASUBUHI, JIONI YENU MNATAKA KUTUHARIBIA AMANI YA NCHI YETU, VIJANA TUKO MACHO, "HATUTATUMIKA" HATUTARUHUSU TAMAA ZENU ZA MADARAKA KUVUNJA AMANI YA NCHI YETU.

WALIOWATUMA WAPENI TAARIFA kwamba TANZANIA IPO IMARA, na ina KIONGOZI wa Nchi IMARA zaidi ya JANA.

Pia soma:

Elections 2020 - Bernard Membe: Tunafanyaje Uchaguzi bila Tume Huru ya Uchaguzi na Waangalizi wa Uchaguzi wa Kimataifa?
 
Back
Top Bottom