Mtaka umesifiwa mbio mpaka umepapita kwenu.

mie nadhani kwa muajiriwa mpya hakuna haja ya kusumbuana na serikali. Kama huridhiki na mshahara na kikokotoo, si uwe muungwana tu, uachane na hiyo kazi na uende kutafuta na kufanya ile ambayo utafurahia, ili uwape fursa wale ambao wameridhika na sheria ya kikokotoo iliyopo waendelee na kazi 🐒

mbona ni rahisi tu lakini unajitahidi kuifanya kua ngumu 🐒
Unawafahamu watu wangapi walioridhika na kikokotoo?
 
Unafedhehesha sn watu wenye akili timamu. Kwa hiyo hao wanaoanza kazi leo lazima wafike 2070. Hivi tunapohimiza kutunza rasilimali za nchi kwa ajili ya kizazi kijacho unadhani hatuna akili. Kwa nini wa sasa tusingefaidi tu wajao wajijue. Hivi wakati Mwl Nyerere anapigania uhuru unadhani alikuwa na shida gani kwao. Au haujui kuwa alikuwa mtoto wa Chief na wakoloni wali favour sn familia za kichifu. Vipi km nayeye angesema hao wanaonyanyasika shauri lao, baba na mama yako wangekuwa na hali gani au wewe mwenyewe.

Huyo anaeanza kazi hujui km ana wazazi au ndugu au rafiki wanaoumizwa na kikokotoo? Au ndo kusema wagawe kisha uwatawale. Anyway, Wa tz kufikiri kwa kutumia nadharia ni kawaida yao huku kupambana na njaa kikiwa ndo kipaumbele.
sasa kama una akili timamu si utumie hiyo akili timamu yako kufanya kazi nzuri ikupendezayo , unang'ang'ana na hiyo kazi ambayo mwishowe kuna ya kikokotoo kwa nini sasa. ....

ni useless kabisaa, uvivu na uwoga tu wa maisha 🐒

unababaika na kufedheheshwa kikokotoo kwanini sasa? Unaanza kazi na stress na huku unajiona uko timamu kweli?, ndio mwishowe mnajinyonga kwa kung'ag'ana na mambo ambayo hamuwezi kuyastahimili🐒

kwan alipokua hana kazi hakua na wazazi, ndugu jamaa na marafik? ama hakuona ama kujua kuna kikokotoo kwa mujibu wa Sheria? au hajui kwamba Sheria pia zinaweza kubadilika kadiri inavyonekana inafaa? 🐒
 
Alafu unategemea kiongoz kama huyu awe na maono ya kuliletea Taifa Maendeleo Endelevu kwa kizazi kilichopo na kijacho...Yaani Mkuu wa Mkoa unamwambia mtumishi wa Umma amsubiri Rais wake!? Sasa kwa kizazi kijacho si ndio atawaambia watafute nchi au sayari Yao!??...SOO PATHETIC...
Kuna kiongozi mwenzake aliwahi kuwaambia Watanzania kama vipi wahamie Burundi.
 
mie nadhani kwa muajiriwa mpya hakuna haja ya kusumbuana na serikali. Kama huridhiki na mshahara na kikokotoo, si uwe muungwana tu, uachane na hiyo kazi na uende kutafuta na kufanya ile ambayo utafurahia, ili uwape fursa wale ambao wameridhika na sheria ya kikokotoo iliyopo waendelee na kazi 🐒

mbona ni rahisi tu lakini unajitahidi kuifanya kua ngumu 🐒
Kwahiyo unashauri mawakili na wanaharakati waache kuwatetea watu kwa sababu wanayoyapinga hayawahusu! Huyu anayeanza kazi akipunguzwa au akifariki ndipo aanze kukikataa kikokotoo kinachomuhusu!
 
Kwahiyo unashauri mawakili na wanaharakati waache kuwatetea watu kwa sababu wanayoyapinga hayawahusu! Huyu anayeanza kazi akipunguzwa au akifariki ndipo aanze kukikataa kikokotoo kinachomuhusu!
hapana kuzuia mtu kufanya kazi ya kutetea au kupinga jambo fulani, hiyo ni haki na Uhuru wa kila mTanzania 🐒

ile ya maana zaidi ni kuona kwamba unaona kabisaa, kitu kinakupa stress lakini unakomaa na kung'ang'ana nacho kama huna utimamu wa akili vile, na matokeo yake wengine mpaka wanaishia kujinyongaga., huoni kama hii ni kaz ngumu sana na nitatizo? 🐒

kwani huweza kufanya kazi uipendayo na ambayo utakua una uhuru nayo kuliko hii ya kukorogwa na kikokotoo tangu umeandikishwa kazini. sasa utafanya kazi kwa usahihi kweli wew? 🐒
 
Unawafahamu watu wangapi walioridhika na kikokotoo?
watumishi wachapakazi hodari nchi nzima, wameafiki kikokotoo hiki kwa mujibu wa Sheria. Na ndio maana wako na bidii na ari zaidi ya kufanya kazi ya umma na kuwatumikia wanainchi 🐒

hata jimboni pangu wapo wastaafu wanainjoy sana kiinua mgongo chao baada ya kustaafu majuzi kwa kikokotoo hiki hiki kipya 🐒
 
hapana kuzuia mtu kufanya kazi ya kutetea au kupinga jambo fulani, hiyo ni haki na Uhuru wa kila mTanzania 🐒

ile ya maana zaidi ni kuona kwamba unaona kabisaa, kitu kinakupa stress lakini unakomaa na kung'ang'ana nacho kama huna utimamu wa akili vile, na matokeo yake wengine mpaka wanaishia kujinyongaga., huoni kama hii ni kaz ngumu sana na nitatizo? 🐒

kwani huweza kufanya kazi uipendayo na ambayo utakua una uhuru nayo kuliko hii ya kukorogwa na kikokotoo tangu umeandikishwa kazini. sasa utafanya kazi kwa usahihi kweli wew? 🐒
Ingekuwa hivyo usemavyo dunia isingekuwa na vyama vya kutetea wafanyakazi, badala ya kugharamia kuwatetea wafanyakazi kwanini wasishauriwe waache kazi.
 
Ingekuwa hivyo usemavyo dunia isingekuwa na vyama vya kutetea wafanyakazi, badala ya kugharamia kuwatetea wafanyakazi kwanini wasishauriwe waache kazi.
kufanya kazi kwa stress, ama kufanya kazi bila stress au kutokufanya kazi kabisaa ni uamuzi binafsi wa mtu, kulingana na alivyopiama manufaa na hasara ya atakachoaamua kukifanya. Hakuna haja ya ushauri, life forces na life realities zitakusukuma tu uamue mwenyewe 🐒

Muhimu ni kuondoa hofu na woga na kuvaa ujasiri na bidii huku ukimshirikisha Mungu katika kila hatua, nyepesi au ngumu lazma utoboe. kuliko unafanya kazi huku unanung'unika🐒
 
watumishi wachapakazi hodari nchi nzima, wameafiki kikokotoo hiki kwa mujibu wa Sheria. Na ndio maana wako na bidii na ari zaidi ya kufanya kazi ya umma na kuwatumikia wanainchi 🐒

hata jimboni pangu wapo wastaafu wanainjoy sana kiinua mgongo chao baada ya kustaafu majuzi kwa kikokotoo hiki hiki kipya 🐒
Jimboni pako, una jimbo wewe?
 
Back
Top Bottom