MTAJI: 12.5 Billion TSH. For Education (Secondary)

kotinkarwak

JF-Expert Member
Aug 5, 2010
376
115
I know it is heady to mention such a a figure, na nikiangalia kiwango ambacho mimi mwenyewe ninaweza kuwa nacho bado in 5Million TSH kwa hivyo will come clean on my plans.
Elimu has been mentioned a few times in this forum lakini bado jukumu la kuendeleza elimu imeachiwa serikali na hivi sasa private entities wametuletea mchanganyiko wa syllabus kutoka kona zote za dunia. Nikizingatia hayo mawili, naona kuwa panakosekana mwelekeo madhubuti kujua ni ipi system inatumika Tanzania na je changamoto zipi zinatumika kuhakikisha kizazi kijacho kinapewa elimu sahihi na itakayohitajika in the coming future.
Education costs zinatafuna at least 25% of most families take home money ya mshahara na njia endelevu basi inahitajika katika ku'invest hii pesa on our childrens behalf.
Hiyo ndio personal brief on the idea, but here follows the figures na mapendekezo.

Kuwekeza 5M kwenye project itakayosisimua sector ya elimu kwa kuwaunganisha stakeholders approx 2500 ambao pia watawekeza kiasi hicho cha pesa. Capital base kama hii inaiwezesha hiyo jumuiya kufanya mambo makubwa katika elimu, kufungua independent schools ambazo zitatoza fees ya bei nafuu ili kuhakikisha kuwa uwezo wa kuipata elimu bora haitakuwa limited kwa watu wachache.

Katika kuwekeza, patakuwa na malengo tofauti kati ya hao wawekezaji, capital investors labda wanatarajia capital returns + a profit margin, wawekezaji wengine wanatarajia return of capital na wengine pia kuwa wamechangia education for the country hence no real need of the capital return.

Kumbadirisha stakeholder from one type to another ina/ita tegemea performance of the whole project hence from a management point of view, it will be assumed kuwa return + margins of profit zinatarajiwa.

Stakeholder mwingine pia anaweza kuwa anaji'commit kuwekeza hizi pesa, mwanae apate elimu pale na mwishowe akaitoa hiyo capital (minus some deductions plus normal fees as usual) hapa lengo likiwa ni ku'capitalize the project for further investments at the given time, kwa hiyo, hiyo investment ya stakeholder huyu itakuwa pia imezaa matunda mengi for the jumuiya.

Michango katika thread hii itasaidia kuelewa viewpoints za walio wengi kwa mfumo kama huu wa collective bringing resources for same goals. Pia naomba tuwe na assumptions zifuatazo

1). Management structures zipo
2). Security of investment ipo
3). Audit facilities zipo ku'manage hii business

Hata kama assumption ni kuwa issues hapo juu zipo, pia unaweza kuchangia mapungufu/ issues unazoweza kuziona.
 
Wazo zuri sana, ukizingatia linaongelea mustakabali wa maisha ya vijana katika jamii yetu kwenye sekta ya elimu. Naomba kuwa included kwenye list ya hao investors.
 
mkuu... unaimba imba sana education ..too general..... what type of education.... na je tatizo kubwa la vijana sasa hivi wanahitaji elimu gani kwa mazingira ya nchi yetu ya TZ ambayo ni least developing country..... priority iwe elimu ya level ipi au elimu ya aina gani

mawazo yangu...tunahitaji elimu ya ufundi na ujasiriamali kwa nguvu kubwa sana tukiwalenga vijana wote watakaotoka shule za kata... hizi ziwe ni polytechnics tufundishe vijana kuwa wabunifu na kujiajiri ...period ....
 
Ni kweli ni vyema kuangalia aina ya elimu itakayoweza kumkomboa MTZ kama Mkuu LAT alivyoelekeza kwenye elimu ya ufundi na ujasiliamali; nafikiri vijana wetu tukiwapatia elimu ya KILIMO na UFUGAJI itaweza kuwakomboa kwa haraka zaidi ukizingatia rasilimali ardhi tunayo yakutosha ukilinganisha na elimu nyinginezo ambazo bado zitamuhitaji kutafuta ajira au kutamfuta mtaji mkubwa katika kuendesha hiyo biashara.
 
mkubwa wazo lako ni zuri lakini kama walivyotangulia kusema wachangiaji wengine,uwe specific.Unaataka kijengwa chuo kikuu,sekondari au primary? wazo langu kiwe ni chuo cha kutoa kozi kwa waliohitimu sekondari na high school ili kuwaandaa vijana kujiajiri baada kuhitimu hapo.
Wazo zuri na tupo pamoja.
 
Naona wachangiaji hapo juu hawajanielewa vizuri. Sikusema ni elimu ipi kwani hiyo ndio michango inayotakikana hapa, Pia, huu uzi ni kutoa wazo tu watu tujadili ni vipi such an undertaking inaweza kufanyiwa kazi.

Kwa mchango wa polytechnic, ndio, level hii ya elimu haipo kabisa nchini, licha ya vyuo vya ualimu, hamna elimu mbadala kwa wananfunzi wa level baada ya sekondari. Ndio kuna VETA lakini bado idadi ya wanafunzi wanaohitaji elimu ya kati ni kubwa mno na VETA centres ni chache na labda courses zao hazitoshelezi mahitaji say, ujasiriamali. lakini pia tukumbuke, polytechnic sio catchment ya mbumbumbu... Unahitaji elimu ya awali pia uwe umepitia na kiwango cha kufaulu pia uwe nacho. Kwa hiyo idea kama hii inajaribu ku'pinpoint capital ambayo jumuiya inaweza kukusanya kwa investments kama hii. Tukifanikisha mradi kama huu, imagine spinoff effect inaweza kuwaunganisha watu zaidi kufanya shughuli zingine nyingi. Kwa nini nimesema capital in Billions of TSH? Kwa sababu, hapa JF watu wengi wameomba ideas kuendeleza/kuanzisha biashara in terms of millions, mijadala ya ufisadi tunaongelea sana, na humo tuna'debate investments ambazo zinawekezwa na wageni katika sectors nyingi nchini which are in terms of billions, na sote tunauliza, sisi wenyewe hatuwezi? Simu, TRL, Bia, Bandari nk

Education sector according to some figures on vijana.fm inaonyesha, in 2010, Tanzania imetumia zaidi ya 2000 Billion, (2 Trillion) TSH katika sector hii, matokeo????

Nadhani swali la elimu ipi, ni kuangalia huo mchango wa capital incase hiyo idadi ya stakeholders 2500 inapatikana, je 12.5Billions, zinaweza kujenga a mix of education levels ngapi? 10 Primary, 5 Secondary, 1 University/Polytechnic ili kuwa na end to end education system.

LAT: Ndio Education ni wimbo kwangu lakini lengo ni hii chorus iwe inafahamika na wengi, labda album yake itaisaidia jamii..
 
AIM Trust.png

Diagram. Mockup of web application:- Login to user session page.

P.s on my PC opening in Internet Explorer shows small image, Firefox is ok. You can also download and view with the default paint application.
 
Katika mazungumzo ya kifamilia nimeikumbuka hii nyuzi niliyoanzisha mwaka jana kuhusu hali ya elimu Tanzania. Mazungumzo yalikuwa kuhusu school fees na hesabu niliifanya kichwani kwa idadi yote ya watoto waliopo katika one form of education or another. Timu nzima ni idadi ya wanafunzi 7 (primary/secondary) na hesabu kwa makadirio yangu si chini ya millioni 2.5 ambazo zinatumika kila mwaka. Sijaongelea value yenyewe katika hizo shule.
Sijui kama bado idea ya kuchangia mfuko (as an investment) niliyoitanguliza hapo juu inawezekana, kwani, by the time hawa vijana wanamaliza shule, kweli pesa nyingi itakuwa imetokomea.
Kwa wanafamilia ambao m'na watoto kati ya miaka 5 hadi 17 (class 1 to form 4), tunaweza kujipanga mapema kwa kutayarisha mashule ya hapo baadae?
 
Back
Top Bottom