JamiiTalks MDAHALO(Mitandao ya Kijamii): Mahususi kwa wanafunzi wa vyuo na wahitimu wa elimu ya juu wa Tanzania

Status
Not open for further replies.

JamiiTalks

JF Advocacy Team
Aug 7, 2018
631
960
MDAHALO KUHUSU MITANDAO YA KIJAMII KWA VIJANA TANZANIA

Katika mwendelezo wa kuibua mawazo na mijadala katika suala la matumizi ya Mitandao ya Kijamii na Mtandao wa Internet kwa ujumla, JamiiForums imeandaa mdahalo kabambe kuhusu Mitandao ya Kijamii nchini Tanzania.

Lengo kuu la mdahalo ni kuibua hoja za msingi kutoka pande mbili zinazokinzana na kuzijadili kujua ukweli, maana, faida na hasara zake. Baada ya mdahalo wabobezi katika fani husika huchambua hoja zilizotolewa kitaalamu na wote kutoka na wazo moja litakalotusaidia katika maisha yetu na hata uhamasishaji kwa wengine.

Mdahalo utakaofanyika jijini Dar es Salaam siku ya Jumamosi tarehe 13 Oktoba 2018, utahusisha wanafunzi wa Vyuo na Wasomi mbalimbali kutoka fani mbalimbali.

=> Je, wewe ni mwanafunzi au mhitimu wa Elimu ya juu? Una umri wa kati ya miaka 20 na 35? Unapendelea kushiriki mijadala kuhusu matumizi ya mitandao ya kijamii(social media)? Basi unaweza Kushiriki.

Maombi ya ushiriki yatafanyika mtandaoni kwa kufuata kiunganishi hiki >> JamiiTalks Debate Application

Mwisho wa kupokea maombi ni Ijumaa tarehe 5 Oktoba 2018 saa 11 jioni.

Karibuni.

Mdahalo uliopita >> "NAFASI ZA MITANDAO YA KIJAMII NCHINI" - Yaliyojiri katika Mdahalo wa Wanachuo New Africa Hotel - JamiiForums
 
Mkuu,

Hili ni Mada ambayo ni rahisi kung’amua na kujadili kwa Washiriki. Lengo moja wapo kuu la midahalo hii ni kujenga uwezo wa vijana (ambao ndiyo viongozi wajao) kujadili kwa hoja na mifano halisi kutoka katika jamii na si kujenga hoja za kulishwa. Hatuna utaratibu dhabiti wa Midahalo nchini, ni wakati wa kuanza kujenga na kupandikiza chembe chembe hizo.

Hivyo ifahamike kufahamu ama kujua mada, si sawa na kuwa na uwezo wa kusimamia hoja yako katika mada.


Yaani mpaka unaingia chuo bado hujajua faida.na hasara za mitandao? Acheni utani wasomi wetu
 
Mkuu,

Hili ni wazo zuri. Ila kutokuwa na idadi kamili ya Washiriki itapelekea kuwe na ugumu wa kufanya maandalizi thabiti. Taratibu nyingi (mfano ukubwa wa ukumbi) unategemea kuwa na makadirio yaliyolengwa ya washiriki tokana uwezo wetu wa kuwamudu.


Kwa nini isiwe free kwa wasomi wote bila kujaza form.
 
Hapana Mkuu,

Hatujamaanisha hivyo, na Kumradhi endapo ndiyo taswira hiyo.

Huu ni moja ya mkakati wa Jamiiforums katika kuwajenga vijana haswa wanafunzi wa chuo na waliohitimu, uwezo wa kujenga hoja katika midahalo na mazungumzo ya kawaida ya kila siku yenye tija kwa Taifa letu pendwa la Tanzania.

Kwa hiyo tusiosoma faida wala hasara hatujui. Duh ndio wasomi wetu nyie tunaowategemea, kweli kazi ipo
 
Mkuu,

Wasomi nje ya lengo ambalo nimelieleza hapo awali, wasomi wanaruhusiwa. Tafadhali usisite kujisajili kuwa mmoja wa Washiriki.

Karibu
Kwa hiyo sisi "Wasomi" huu mjadala hautuhusu? maana si kila mhitimu wa Elimu ya juu ni "Msomi"

Mjadala wa kibaguzi huu.
 
Hili la kusema wasomi na wanafunzi wa elimu za juu na pingana nalo na ni ubaguzi kabisa. Siku hizi sayansi na teknolojia imekuwa hata ambao hawajaenda shule wanatumia mitandao iweje wabaguliwe.

Yawezekana huyo ambaye hajaenda darasa akawa na hoja zenye mashiko za kuibadili jamii nzima yenye mkanganyiko juu ya matumizi ya mitandao.

Kamwe huwezi kupima uzito wa pamba na mawe kwa kutizima mwonekano wa nje kw kusema pamba ni nyepesi zaid kuliko mwawe ili hali zote zinau uzito sawa. Zote ziwekwe katika mizani zipimwe kwa usawa, ndivyo hivyo hivyo katika mdahalo huo.

Wote wapewe fursa
 
MDAHALO KUHUSU MITANDAO YA KIJAMII KWA VIJANA TANZANIA

Katika mwendelezo wa kuibua mawazo na mijadala katika suala la matumizi ya Mitandao ya Kijamii na Mtandao wa Internet kwa ujumla, JamiiForums imeandaa mdahalo kabambe kuhusu Mitandao ya Kijamii nchini Tanzania.

Lengo kuu la mdahalo ni kuibua hoja za msingi kutoka pande mbili zinazokinzana na kuzijadili kujua ukweli, maana, faida na hasara zake. Baada ya mdahalo wabobezi katika fani husika huchambua hoja zilizotolewa kitaalamu na wote kutoka na wazo moja litakalotusaidia katika maisha yetu na hata uhamasishaji kwa wengine.

Mdahalo utakaofanyika jijini Dar es Salaam siku ya Jumamosi tarehe 13 Oktoba 2018, utahusisha wanafunzi wa Vyuo na Wasomi mbalimbali kutoka fani mbalimbali.

=> Je, wewe ni mwanafunzi au mhitimu wa Elimu ya juu? Una umri wa kati ya miaka 20 na 35? Unapendelea kushiriki mijadala kuhusu matumizi ya mitandao ya kijamii(social media)? Basi unaweza Kushiriki.

Maombi ya ushiriki yatafanyika mtandaoni kwa kufuata kiunganishi hiki >> JamiiTalks Debate Application

Mwisho wa kupokea maombi ni Ijumaa tarehe 5 Oktoba 2018 saa 11 jioni.

Karibuni.

Mdahalo uliopita >> "NAFASI ZA MITANDAO YA KIJAMII NCHINI" - Yaliyojiri katika Mdahalo wa Wanachuo New Africa Hotel - JamiiForums

Wasomi wetu ina maana mmekosa mada yenye mashiko kabisa!? Hiyo mada ni ya watoto wa sekondary sio kwa level ya university! Badilisheni mada mtapata washiriki wengi. Badala ya kujadili udikteta na hatima yake kwa nchi za Africa Mashariki, mnaongea habari ya face book na Insta??!
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom