Wachezaji wa kike wanaweka mpira tumboni kama kampeni ya kupinga kuachwa na klabu zao wakipata ujauzito. TFF wasema wanajua ni aina ya ushangiliaji

Ndonoman

Member
Feb 21, 2024
9
24
Kwanza nianze kwa kuwapa maua yenu Jamiicheck, binafsi nawakubali sana kazi yenu. Big up sana sana.

Twende kwenye mada.

Naona kuna Picha za wachezaji wa kike wakiwa wanaweka mpira ndani ya jezi tumboni, baadhi ya watu wanasema hiyo ni kampeni ya kuvitaka vilabu wasiachane na wachezaji wao wakipata mimba.

Je, jambo hili ni kweli? Na je kama ni kweli ni sheria za mpira au wanawaonea tu?

20240427_015549.jpg

Screenshot_20240427_015607_X.jpg


=====

Jamiiforums imezungumza na Afisa Habari wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Clifford Ndimbo ili kujua ukweli wa jambo hili naye alikuwa na haya ya kusema:-

Suala la mkataba wa mchezaji na klabu siyo la TFF japokuwa tunafahamu kwa kuwa lazima Shirikisho liwe na taarifa za makubaliano ya pande hizo mbili, suala hilo linahusu pande mbili.

Ikitokea mkataba umevunjwa kwa kuzingatia vipengele vilivyopo katika mkataba huo, ikiwa umevunjwa kwa mazingira tofauti na vipengele husika hapo ndipo TFF tunaweza kuingilia, iwe ni mchezaji kavunja au klabu ndio imevunja.

Kuhusu Wachezaji kuweka mpira tumboni kama ni kampeni, anasema:

Hiyo ni aina ya ushangiliaji, kuhusu kama ni kampeni sisi kama TFF hatufahamu hilo, tunajua ni sehemu ya ushangiliaji kama ilivyo staili za aina hiyo.

Kuhusu kupata kesi au malalamiko ya kuvunjwa kwa mkataba kutokana na ujauzito hilo siwezi kujibu moja kwa moja kwa kuwa sijafuatilia, inawezekana halipo au lipo lakini halijafika mezani kwangu.

Ushauri
Tunatoa wito kwa Klabu kuendelea kutoa elimu kama TFF inavyofanya kuhusu haki za wachezaji na soka la Wanawake kwa jumla.
 
Labda timu za Tanzania tu; kwa timu za Marekani naona wanachukua maternity leave ya miezi sita halafu baada ya kujifungua wanarudi uwanjani kama kawaida.

Mifano ipo mingi tu:
(1) Alex Morgan: baada likizo ya miezi sita na kujifungua, Alex Morgan alirudi kwenye timu yake na mpaka sasa anacheza akiwa analea
1714186308834.jpeg


(2) Sydney Leroux: alishazaa mara mbili na bado anachezea timu yake

1714186492012.png


(3) Jessica MacDonald alijifungua na kurudi kucheza hadi sasa mtoto wake ni mkubwa wakati mama yake bado anachezea timu ya GTaifa ya Marekani.

1714186718006.jpeg
 
Wangeruhusiwa kucheza ila shida ya watanzania wanafanyaga mimba kama ugonjwa ! Mtu akibeba mimba basi atakua mchafu atajiliza liza kila muda hawataki kujishughulisha !! Wakati Selena Williams alipiga tennis mechi za mwisho mwisho wakati anakaribia kujifungua.

Pia utaratibu wa mtu akijifungua anakula nini ni mgumu wengi wakijifungua wamekariri kunywa mauji na mitori mpaka inawatoa kwenye miili yao ya kimichezo !! Hakuna team itakubali !

Na wameweka hivyo ili wawe makini kina dada huwa wakipewa uhuru unaweza kuta team nzima watu wanne wajawazito tena wa kutegemewa ! Mtu karibu miezi tisa huna wachezaji na unawalipa !Mpira ni biashara.
 
Inaweza kuwa kweli kibongobongo.

Kuna case ya yule binti wa kikenya aliyejazwa mimba na kiongozi wa timu aliyokuwa akiichezea hapa bongo na akatemwa.
Ni kweli katika hilo kwani kwa sisi, mwanamke akishajifungua si yule wa awali. Pili, financially tupo vibaya kwani kumtunza mchezaji bila kucheza kwa miezi 6 ni ngumu. Ni vyema wamama hao walivyoanzisha hiyo campaign yao ili nao wathaminike.
 
Haya yote ni matokeo ya kulazimisha na kukiuka asili halisi ya mwanadamu, binafsi sijawahi amini wanawake kucheza mpira ni jambo ambalo lipo sahihi, halifai na haipendezi.

Matokeo ndy hayo sasa mfumo halisi wa maisha kwa muhusika unavurugika.
 
Haya yote ni matokeo ya kulazimisha na kukiuka asili halisi ya mwanadamu, binafsi sijawahi amini wanawake kucheza mpira ni jambo ambalo lipo sahihi, halifai na haipendezi.

Matokeo ndy hayo sasa mfumo halisi wa maisha kwa muhusika unavurugika.
Wenzetu wanachukua likizo ya uzazi wanarudi uwanjani. Sisi ndo ngumu sababu ya kunywa mitori na supu akitoka uzazi kanenepa.
 
KIASILI TU HUU MCHEZO SIO WA WANAWAKE NI VILE TU DUNIA INAFORCE WANAWAKE TUWE SAWA. SASA MTU AKISHAKUWA NA MIMBA YA MIEZI HATA MIWILI ATAWEZA KWELI KUCHEZA DK 90 ????

HAYA AKISHAJIFUNGUA ATARUDU UWANJANI KWA MUDA UNAITAKIWA?? AKIJIFUNGUA KWA OPERATION NDIO KABISA ATAKAA ZAIDI YA MWAKA NA NUSU NJE YA UWANJA. ? BADO TIMU IKUVUMILIE NA IKULIPE MSHAHARA HEWA.???

NB

MPIRA SIO MCHEZO WA WANAWAKE NDIO MAANA WACHEZAJI WENGI WA KIKE WANAKUWA NA TABIA ZA KISELA.
 
Ingekuwa mie ndiye yule mtoa mikataba natoa kabisa kuwa Kila baada ya miezi mitatu tunapima ujauzito , ukigundulika tu una mimba mkataba tunatemana au tunaingia mkataba hakuna mimba mpaka mkataba uishe

Wanawake wazembe sana wanategesheaga tu mimba huku wakiendelea kupakia

Waliyepeana naye mimba ndiyo wagharamie siyo timu
 
Back
Top Bottom