Law School of Tanzania: Imeondoka kwenye lengo la msingi na kuingia kwenye biashara /upigaji, kilichotokea ni mwangwi wa mhamo huo!

mbingunikwetu

JF-Expert Member
Feb 17, 2015
13,664
18,041
Kimsingi Law School of Tanzania inapaswa kushughulika na kuwawezesha wanafunzi kupata ujuzi kwa vitendo ndiyo maana inaitwa LEGAL PRACTICAL TRAINING! Inalenga kuwapatia wanafunzi weledi katika utekelezaji wa majukumu yao kwa vitendo zaidi. Hawajaenda pale kushindiliwa tena elimu ya sheria kwa nadharia maana hiyo waliipata vyuoni. Kama kuna vipengele vya kinadharia vimepungua, basi waviingize kwenye mitaala huko vyuoni.

Kinyume na lengo hilo la msingi, law school inalazimisha kutumia semister nzima ya kwanza kufundisha tena kwa nadharia yale ambayo tayari wanafunzi waliyasoma vyuoni. Mwisho wa siku wanafunzi hufanyishwa tena mitihani kwa nadharia zaidi. Haya matokeo yanayovuma ni ya nadharia.

PENDEKEZO: Semister zote mbili zitumike kuwapeleka wanafunzi field maeneo mbali mbali na wapimwe huko huko field kwa vitendo kuonekana wamefaulu au la!! Kusiwepo tena mitihani ya nadharia, ambayo tayari walishaifuzu vyuoni.

WANACHOFANYA: Ni kutengeneza pesa isivyo halali na kutengeneza mazingira ya rushwa zaidi!! Hapo law school kuna rushwa sana!

PIA WENGINE WAMESHAIGA: Bodi ya wafamasia na yenyewe ina mwelekeo huo huo. Baada ya Internship ambayo kimsingi ni mafunzo kwa vitendo, badala ya kuwapima wanafunzi kwa vitendo huko huko field, huwataka kufanya mtihani tena wa NADHARIA ili kuwasajili!! Ebo!! Lengo ni pesa na kulazimisha mazingira ya rushwa!! Kufanya mtihani ni pesa, na kurudia mtihani ni pesa!
 
Hakunab haja ya kuwa na chuo. Internship ifanyikie eneo la kazi kama mahakamani, kampuni za mawakili, ofisi za wanasheria wa serikali, takukuru nk. Upimaji ufanyike kwa vitendo huko huko maeneo ya kazi.

Nadharia na mitihani ya nadharia iishie vyuoni. Kama kuna upungufu wa kozi za nadharia ziongezwe huko huko vyuoni. Wafanye kama bodi ya madaktari ambao hawana chuo cha internship!!
Vinginevyo ni ulaji na kupalilia mazingira ya rushwa!!

Mtu alipiga theory na mitihani yake vyuoni halafu unamrudisha kwenye theory tena na mitihani ya theory huo ni wizi mtupu!
 
Mwakyembe hafai kuongoza tume ya kuchunguza sakata hili la wanafunzi wa chuo cha law school kufeli maana yeye hayuko field!

Sana sana ataiangalia mitihani hiyo hiyo ya nadharia na kusema "hawa watafelije mitihani rahisi hivi lazima watakuwa vilaza!" Wapimwe field na siyo kwenye chumba cha mtihani wa nadharia!!

Mitihani ya nadharia isiwepo kabisa!! Wapimwe kwa vitendo huko field semister zote mbili!!
 
Kwenye sakata la tanzania law school sijaona mtu mwenye hoja,wengi wanatetea ukilaza wanataka kuvuna bila kupanda.Wanaolalamika mjitokeze tuwaone uwezo wenu muache bodi zetu zifanye kazi na nyie bodi muache kubeba uvilaza wanafunzi wote wakifeli wamefeli msiogope kuwapa matokeo.Mimi mwenyewe nilishafeli miaka 6 Lakini siwezi simama kulaumu nakubaliana na matokeo.na naziamini hizi bodi kuliko maelezo kuliko hivi vyuo vya magumashi kutwa wanatoa degree uchwara.
 
Kwenye sakata la tanzania law school sijaona mtu mwenye hoja,wengi wanatetea ukilaza wanataka kuvuna bila kupanda.Wanaolalamika mjitokeze tuwaone uwezo wenu muache bodi zetu zifanye kazi na nyie bodi muache kubeba uvilaza wanafunzi wote wakifeli wamefeli msiogope kuwapa matokeo.Mimi mwenyewe nilishafeli miaka 6 Lakini siwezi simama kulaumu nakubaliana na matokeo.na naziamini hizi bodi kuliko maelezo kuliko hivi vyuo vya magumashi kutwa wanatoa degree uchwara.
Hujaelewa somo: Hiyo ni legal practical training lakini wanaishia kuwapa mitihani ya theory huoni kuna shida mahali?
 
Kimsingi Law School of Tanzania inapaswa kushughulika na kuwawezesha wanafunzi kupata ujuzi kwa vitendo ndiyo maana inaitwa LEGAL PRACTICAL TRAINING! Inalenga kuwapatia wanafunzi weledi katika utekelezaji wa majukumu yao kwa vitendo zaidi. Hawajaenda pale kushindiliwa tena elimu ya sheria kwa nadharia maana hiyo waliipata vyuoni. Kama kuna vipengele vya kinadharia vimepungua, basi waviingize kwenye mitaala huko vyuoni.

Kinyume na lengo hilo la msingi, law school inalazimisha kutumia semister nzima ya kwanza kufundisha tena kwa nadharia yale ambayo tayari wanafunzi waliyasoma vyuoni. Mwisho wa siku wanafunzi hufanyishwa tena mitihani kwa nadharia zaidi. Haya matokeo yanayovuma ni ya nadharia.

PENDEKEZO: Semister zote mbili zitumike kuwapeleka wanafunzi field maeneo mbali mbali na wapimwe huko huko field kwa vitendo kuonekana wamefaulu au la!! Kusiwepo tena mitihani ya nadharia, ambayo tayari walishaifuzu vyuoni.

WANACHOFANYA: Ni kutengeneza pesa isivyo halali na kutengeneza mazingira ya rushwa zaidi!! Hapo law school kuna rushwa sana!

PIA WENGINE WAMESHAIGA: Bodi ya wafamasia na yenyewe ina mwelekeo huo huo. Baada ya Internship ambayo kimsingi ni mafunzo kwa vitendo, badala ya kuwapima wanafunzi kwa vitendo huko huko field, huwataka kufanya mtihani tena wa NADHARIA ili kuwasajili!! Ebo!! Lengo ni pesa na kulazimisha mazingira ya rushwa!! Kufanya mtihani ni pesa, na kurudia mtihani ni pesa!
Mkuu taasisi zote za kitaaluma dunia nzima ni tundu dogo la kuzuia watu wengi kuingia kwenye taaluma husika. That is what they are by nature, and nature can not be created or destroyed
 
Kwenye sakata la tanzania law school sijaona mtu mwenye hoja,wengi wanatetea ukilaza wanataka kuvuna bila kupanda.Wanaolalamika mjitokeze tuwaone uwezo wenu muache bodi zetu zifanye kazi na nyie bodi muache kubeba uvilaza wanafunzi wote wakifeli wamefeli msiogope kuwapa matokeo.Mimi mwenyewe nilishafeli miaka 6 Lakini siwezi simama kulaumu nakubaliana na matokeo.na naziamini hizi bodi kuliko maelezo kuliko hivi vyuo vya magumashi kutwa wanatoa degree uchwara.
Kuna watu wawili walinipigia simu jana wakidai matokeo ya mwaka huu ni balaa? Naweza kuyapata wapi?
 
Back
Top Bottom