LATRA yapiga Stop usafirishaji kwa kutumia magari madogo kuepuka ajali za kila siku

Mwanahabari wa Taifa

JF-Expert Member
May 27, 2020
1,452
805

RC Kafulila apiga marufuku ‘michomoko’ kusafirisha abiria Mkoa wa Simiyu​

AJALI PIC

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu (RC) nchini Tanzania, David Kafulila amepiga marufuku magari madogo maarufu michomoko kusafirisha abiria mkoani humo.

Ni baada ya kuhusika kwenye matukio ya ajali yaliyosababisha vifo vya watu 10 na majeruhi 17 ndani ya siku 12 zilizopita.

Amri ya Kafulila imetolewa leo Jumatano Julai 13, 2022 ikiwa ni siku moja baada ya ajali iliyotokea eneo la Magereza nje kidogo ya mji wa Bariadi mkoani Simiyu usiku wa kuamkia jana ikihusisha "michomoko" na kusababisha vifo vya watu watano na majeruhi 11.

Wakati majina ya marehemu watano waliofariki kwenye ajali ya Simiyu bado hayajawekwa wazi na waliojeruhiwa ni Elizabeth Nestory (26), Yohana Mwita (22), Sumai Mabula (43), Joseph Masanja (32) na Neema Samson (20).

Wengine ni, Felister Maganda (54), Happy Manyama (23), Oscar Nsolo (47), Stephano Stephene (22) na Joyce Manyama (27) huku majeruhi mmoja ambaye yuko kwenye hali mbaya hajafahamika.

soma pia hii​

Ajali hiyo litokea baada ya magari madogo mawili madogo aina ya Toyota pro box na Toyota wish yanayosafirisha abiria kati ya miji wa Bariadi Wilaya ya Bariadi na Lamadi wilayani Busega kugongana uso kwa uso.

Tukio hilo limetokea siku 12 pekee baada ya ajali nyingine iliyohusisha “mchomoko” aina Toyota wish iliyotokea eneo la Luguru Wilaya ya Itilima mkoani Simiyu na kusababisha vifo vya watu watano na majeruhi watano.

Akizungumza na waandishi wa habari mjini Bariadi yaliko makao makuu ya Mkoa wa Simiyu, Kafulila amesema magari hayo madogo yanafanya shughuli ya kusafirisha abiria kinyume cha sheria na maelekezo ya Serikali kupitia Mamlaka ya Usafirishaji wa ardhini (Latra).

"Wamiliki na waendeshaji wa nigari haya ya michomoko wamepewa maelekezo ya kufuata ili kuwaruhusu waendelee kufanya kazi ya kusafirisha abiria, lakini ni zaidi ya miezi sita sasa hawajatekeleza,” amesema Kafulila

Mkuu huyo wa mkoa amesema kutokatana na ukaidi wa wamiliki hao huku watu wakiendelea kupoteza maisha na kujeruhiwa katika ajali zinazohusisha magari hayo, Serikali inasitisha shughuli za magari hayo ya kusafirisha abiria kwa mujibu wa kifungu cha 25 cha Sheria ya Usafirishaji inayoipa mamlaka ya kufanya hivyo.

Ametumia fursa hiyo kuwaalika wawekezaji katika sekta ya usafirishaji wa abiria kwenda mkoani Simiyu kuwekeza katika usafirishaji salama kwa mujibu wa sheria.

Naye ofisa mfawidhi wa Latra mkoa wa Simiyu, Amaniel Sekulu amesema kwa mujibu wa leseni, magari madogo yanayofahamika kwa jina maarufu ya ‘mchomoko’ yanayosafirisha abiria katika miji mbalimbali mkoani humo yamesajiliwa kama Taxi, akini badala yake, wamiliki wamebadilisha shughuli kwa kusafirisha abiria kinyume cha sheria.

“Magari haya yanatakiwa kusajiliwa, kupakwa rangi, kuandikwa namba za utambulisho ubavuni na kubandika vibao maalum vinavyoonyesha kuwa ni Taxi na zinatakiwa kupakia abiria kwa idadi inayoruhusiwa kisheria,” amesema Sekulu

======================
WAKATI HUOHUO LATRA YAPIGILIA MSUMALI AGIZO LA KAFULILA, MICHOMOKO YOTE KUONDOLEWA BARABARANI NCHI NZIMA!

Baraza la Ushauri la watumiaji wa huduma za usafiri ardhini( LATRA) limetoa tamko kali kuunga mkono maamuzi magumu aliyochukua Mkuu wa Mkoa Simiyu, David Kafulila ya kupiga marufuku gari ndogo zinazotumika kusafirisha abiria maarufu kama michomomoko kuanzia Julai13, 2022.

Kafulila alipiga marufuku gari hizo kuendelea kutumika kutokana na kuwa sababu kuu ya ajali mkoani Simiyu kufuatia gari hizo kutimika kubeba abiria wengi na kukaidi agizo lake la muds mrefu kutaka zitumike kama taxi badala ya kujigeuza daladala kwa kubeba abiria wengi zaidi ya uwezo. " Kwakua kutokana na mwenendo usioridhisha gari hizi zimekuwa chanzo kikubwa cha ajali, na kwakuwa gari hizi zimekaidi maelekezo ya serikali kutaka zifuate taratibu za kujiendesha kama taxi kwa kisingizio kuwa mfumo huo haulipi kibiashara, basi kuanzia leo Julai13, 2022, nasitisha usafiri wa MICHOMOKO mpaka hapo itakapoamuliwa vinginevyo" alisisitiza RC Kafulila.

Katika tamko Lao, LATRA wamesisitiza mikoa wakuu wa mikoa mingine kufuata mfano huo kukabili tatizo la ajali nchini kwani gari hizo sio salama , nihatari kwa usalama wa wananchi kwani zimekuwa chanzo cha ajali maeneo mengi nchini na kuahidi kushirikiana na vyombo vingine ikiwemo jeshi la polisi kuhakikisha inafanyika opareshen nchi nzima

IMG-20220716-WA0043.jpg
IMG-20220716-WA0042.jpg


RC Kafulila anatumia kifungu cha 25 cha kwenye sheria ya Land Transport Reguratory Act

Long image 07-16-2022 06.00.jpg

Nae kamanda wa kikosi cha Usalama barabarani ACP Wilbroad Mtafungwa amekandamizia kuwa sasa Tanzania michomoko basi kwa usalama wa Watanzania na mali zao, msikilize mpaka mwisho huyu Mwamba,
 
View attachment 2292276

RC Kafulila apiga marufuku ‘michomoko’ kusafirisha abiria Mkoa wa Simiyu​

AJALI PIC

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu (RC) nchini Tanzania, David Kafulila amepiga marufuku magari madogo maarufu michomoko kusafirisha abiria mkoani humo.

Ni baada ya kuhusika kwenye matukio ya ajali yaliyosababisha vifo vya watu 10 na majeruhi 17 ndani ya siku 12 zilizopita.

Amri ya Kafulila imetolewa leo Jumatano Julai 13, 2022 ikiwa ni siku moja baada ya ajali iliyotokea eneo la Magereza nje kidogo ya mji wa Bariadi mkoani Simiyu usiku wa kuamkia jana ikihusisha "michomoko" na kusababisha vifo vya watu watano na majeruhi 11.

Wakati majina ya marehemu watano waliofariki kwenye ajali ya Simiyu bado hayajawekwa wazi na waliojeruhiwa ni Elizabeth Nestory (26), Yohana Mwita (22), Sumai Mabula (43), Joseph Masanja (32) na Neema Samson (20).

Wengine ni, Felister Maganda (54), Happy Manyama (23), Oscar Nsolo (47), Stephano Stephene (22) na Joyce Manyama (27) huku majeruhi mmoja ambaye yuko kwenye hali mbaya hajafahamika.

soma pia hii​

Ajali hiyo litokea baada ya magari madogo mawili madogo aina ya Toyota pro box na Toyota wish yanayosafirisha abiria kati ya miji wa Bariadi Wilaya ya Bariadi na Lamadi wilayani Busega kugongana uso kwa uso.

Tukio hilo limetokea siku 12 pekee baada ya ajali nyingine iliyohusisha “mchomoko” aina Toyota wish iliyotokea eneo la Luguru Wilaya ya Itilima mkoani Simiyu na kusababisha vifo vya watu watano na majeruhi watano.

Akizungumza na waandishi wa habari mjini Bariadi yaliko makao makuu ya Mkoa wa Simiyu, Kafulila amesema magari hayo madogo yanafanya shughuli ya kusafirisha abiria kinyume cha sheria na maelekezo ya Serikali kupitia Mamlaka ya Usafirishaji wa ardhini (Latra).

"Wamiliki na waendeshaji wa nigari haya ya michomoko wamepewa maelekezo ya kufuata ili kuwaruhusu waendelee kufanya kazi ya kusafirisha abiria, lakini ni zaidi ya miezi sita sasa hawajatekeleza,” amesema Kafulila

Mkuu huyo wa mkoa amesema kutokatana na ukaidi wa wamiliki hao huku watu wakiendelea kupoteza maisha na kujeruhiwa katika ajali zinazohusisha magari hayo, Serikali inasitisha shughuli za magari hayo ya kusafirisha abiria kwa mujibu wa kifungu cha 25 cha Sheria ya Usafirishaji inayoipa mamlaka ya kufanya hivyo.

Ametumia fursa hiyo kuwaalika wawekezaji katika sekta ya usafirishaji wa abiria kwenda mkoani Simiyu kuwekeza katika usafirishaji salama kwa mujibu wa sheria.

Naye ofisa mfawidhi wa Latra mkoa wa Simiyu, Amaniel Sekulu amesema kwa mujibu wa leseni, magari madogo yanayofahamika kwa jina maarufu ya ‘mchomoko’ yanayosafirisha abiria katika miji mbalimbali mkoani humo yamesajiliwa kama Taxi, akini badala yake, wamiliki wamebadilisha shughuli kwa kusafirisha abiria kinyume cha sheria.

“Magari haya yanatakiwa kusajiliwa, kupakwa rangi, kuandikwa namba za utambulisho ubavuni na kubandika vibao maalum vinavyoonyesha kuwa ni Taxi na zinatakiwa kupakia abiria kwa idadi inayoruhusiwa kisheria,” amesema Sekulu

======================
WAKATI HUOHUO LATRA YAPIGILIA MSUMALI AGIZO LA KAFULILA, MICHOMOKO YOTE KUONDOLEWA BARABARANI NCHI NZIMA!

Baraza la Ushauri la watumiaji wa huduma za usafiri ardhini( LATRA) limetoa tamko kali kuunga mkono maamuzi magumu aliyochukua Mkuu wa Mkoa Simiyu, David Kafulila ya kupiga marufuku gari ndogo zinazotumika kusafirisha abiria maarufu kama michomomoko kuanzia Julai13, 2022.

Kafulila alipiga marufuku gari hizo kuendelea kutumika kutokana na kuwa sababu kuu ya ajali mkoani Simiyu kufuatia gari hizo kutimika kubeba abiria wengi na kukaidi agizo lake la muds mrefu kutaka zitumike kama taxi badala ya kujigeuza daladala kwa kubeba abiria wengi zaidi ya uwezo. " Kwakua kutokana na mwenendo usioridhisha gari hizi zimekuwa chanzo kikubwa cha ajali, na kwakuwa gari hizi zimekaidi maelekezo ya serikali kutaka zifuate taratibu za kujiendesha kama taxi kwa kisingizio kuwa mfumo huo haulipi kibiashara, basi kuanzia leo Julai13, 2022, nasitisha usafiri wa MICHOMOKO mpaka hapo itakapoamuliwa vinginevyo" alisisitiza RC Kafulila.

Katika tamko Lao, LATRA wamesisitiza mikoa wakuu wa mikoa mingine kufuata mfano huo kukabili tatizo la ajali nchini kwani gari hizo sio salama , nihatari kwa usalama wa wananchi kwani zimekuwa chanzo cha ajali maeneo mengi nchini na kuahidi kushirikiana na vyombo vingine ikiwemo jeshi la polisi kuhakikisha inafanyika opareshen nchi nzima

View attachment 2292287View attachment 2292289

RC Kafulila anatumia kifungu cha 25 cha kwenye sheria ya Land Transport Reguratory Act

View attachment 2292293
Nae kamanda wa kikosi cha Usalama barabarani ACP Wilbroad Mtafungwa amekandamizia kuwa sasa michomoko basi kwa usalama wa Watanzania na mali zao, msikilize mpaka mwisho

Kafulila anayo akili ya kiuongozi.

Asante LATRA
 
Mikoa mingi usafiri ni shida hasa kati ya wilaya na wilaya

Mbadala wake nini baada ya kupiga marufuku? Je upo kwa sasa huo.mbadala? Sababu unakuta route zingine kwa basi hazipiti sababu abiria wachache hivyo mabasi unakuta hakuna au machache mno .Hao akina mchomoko ndio mkombozi wa hiyo route. Unatakiwa tu usimamizi mkali. Bodaboda zinaua na kujeruhi watu kila siku mbona hazipigwi marufuku?

Aadhibiwe dereva kwa uzembe wa kidereva sio mwenye gari. Napinga uamuzi wa kuzuia michomoko. Hayo makosa ya kugongana uso kwa uso ni makosa ya madereva sio wamiliki wa magari. Unamkomoaje mwenye gari kwa uzembe wa dereva?

Maamuzi hayako sahihi ukizingatia shida za usafiri mikoani hasa mawilayani. Latra na Kafulila hawajatendea haki wananchi.

Waziri husika atengue huo uamuzi wa kijinga wa kukurupuka.
 
Haya ndio mambo anayoyaweza Kafulila ila kukuza elimu, uchumi na ku-improve maisha ya wananchi wanyonge kwa ujumla wake ni sifuri...

Anyways, ni uamuzi utakaopunguza kidogo kasi ya ukuaji uchumi kwa kupunguza ajira na kuongeza shida ya usafiri lakini utakaopunguza ajali na kuokoa uhai na kupunguza vilema.

I think it's worth it.
 
Kwa mkoa km kigoma kupiga marufuku michomoko ni kuwataka waha watembee kwa miguu michomoko ndo mkombozi wa huku hakuna mabasi njia mbovu hakuna tajiri anayeweza kurisk Basi lake kulileta kwenye njia za mbavu za mbwa km kigoma cha muhimu wazuiwe kujaza kupita kiasi traffic barabarani walisimamie hilo
 
Kafulila kila siku ana-trend... Anyways, ni uamuzi utakaopunguza kidogo kasi ya ukuaji uchumi kwa kupunguza ajira na kuongeza shida ya usafiri lakini utakaopunguza ajali na kuokoa uhai na kupunguza vilema. I think it's worth it.
Kafulila jembe sio jembe
 
Hizo gari na Noah hazipaswi tumika safirisha abiria
Hujafika maeneo ya wilayani yenye shida za usafiri wewe

Haya mambo ya ku.copy na ku paste sheria za wazungu na kuzifanya za Latra bila kuangalia mazingira yetu na hali ya uchumi wa watu wetu ni ujinga

Maeneo mengi mabasi hamna hasa mawilayani na yakiwepo.machache kuna route njia mbaya wenye basi hawapendi au hawataki sababu ya gharama za.mafuta wanaona hailipi.Mchomoko unatumia mafuta kidogo na waweza enda route zenye watu wachache ambako mabasi machache au hayapo au route mbaya
 
Kwa jicho la kibiashara kupeleka coaster njia ya bugando ni kujitafutia hasara tu. Abiria wengi huwepo mida ya kuona wagonjwa. Baada ya hapo abiria wa kutafuta sana. Dar tu daladala nyingi mbovu sana . Bongo tupo nyuma kwenye kila kitu
Ni aibu jiji kama Mwanza kuwa na hiace, bajaji na michomoko ya Bugando katikati ya jiji. Ni vyema sasa wakapush coaster ziwe nyingi kwenye majiji na hivyo vihiace vikafanye kazi za michomoko huko vijijini.
 
Back
Top Bottom