Kwanini Utumishi wanatumia muda mrefu kuita watu kazini?

wakuu lazima tutoe mrejesho hapa
hatimaye nimeangukia halmashauri leo

Nawashukuru ndugu zangu
nawashukuru psrs

Dah! Mkuu mfwende sawadogo hongera sana. Nikiona watu tuliokuwepo muda mrefu kwenye huu uzi bila ya kupata shuhuda nao wanaleta shuhuda za kupata ajira namimi napata nguvu zaidi kwamba kuna siku dogo ninayemuhangaikia apate nafasi naye atapata.

Hongera tena, japo naamini inawezekana moyo wako uko kwenye vyombo vya ulinzi na usalama lakini huu sio mwisho wa mapambano, ndio njia zinazidi kufunguka kwa kasi.
 
wakuu lazima tutoe mrejesho hapa
hatimaye nimeangukia halmashauri leo

Nawashukuru ndugu zangu
nawashukuru psrs

katika watu nilikua naenda nao bega kwa bega kimya kimya asee ni wewe bwana mfwende, ulikua unatoa hamasa kwa sisi jobless tusikate tamaa hatimae umetuaga sasa ni mtumishi, nikupe pongezi sana bruv kawe mtumishi mwema alama yako kwenye uzi itadumu. bless up
 
Back
Top Bottom