Kwanini madalali wameyashikilia masoko na kusababisha bidhaa kutoshuka bei?

yogan

Senior Member
Feb 26, 2013
133
85
Mimi ninauza genge la mboga mboga na matunda.Kwa muda mrefu nimekuwa nikifuatilia mwenendo wa biashara katika masoko ya jijini Dar es salaam kama Mabibo, Buguruni, Temeke, Stereo na Ilala.

Katika masoko yote haya hakuna mkulima anaruhusiwa kuuza BIDHAA zake sokoni. Mzigo unapofika sokoni Wanakabidhiwa MADALALI ndo wanauza kadiri ya makubaliano na mkulima.

Chakusikitisha ni kwamba hawa jamaa wanafaidika sana hata kuliko wakulima wa nchi hii kwani wanatumia faida ya wakulima kutohusika kuuza BIDHAA nao kupandisha bei za BIDHAA kiholela.

imefikia hatua hata BIDHAA zikiwa zimefurika sokoni bado wanaziuza bei ya juu Jambo linalosababisha wakulima kupata hasara kwani kuna bidhaa huharibika kwa kukosa wateja. Mpaka sasa Mimi sioni umuhimu wa madalali sokoni kwani wanaleta maisha magumu bila sababu za msingi.

Hawa jamaa wakuondolewa bidhaa zitauzwa Kwa mfumo huru WA kibiashara na kuzingatia chain ya demand na supply ambayo inaweza kutupa unafuu wa maisha yetu.
 
Hiyo kukabidhi mzigo kwa dalali ni utaratibu rasmi?

Endapo ukigoma kukabidhi mzigo kwa dalali ili uuze mwenyewe, ni hatua gani zinachukuliwa dhidi ya mkaidi?
 
Wa kusaidia hilo ni Serikali tu,kama kalala usingizi unategemea nini?
Tuwaamshe Kwa kweli hili Jambo linamfanya mkulima anakuwa Masikini kila siku. MADALALI hawana uchungu na mali za mkulima hata kidogo ona hapo ndizi zimeoza wamegoma kushusha bei basi wangetoa hata sadaka Tu lkn MADALALI wamekomaa sana
IMG_20240415_095312.jpg
 
Hiyo kukabidhi mzigo kwa dalali ni utaratibu rasmi?

Endapo ukigoma kukabidhi mzigo kwa dalali ili uuze mwenyewe, ni hatua gani zinachukuliwa dhidi ya mkaidi?
Huu ni utaratibu unaoratibiwa na masoko niliyoyataja
 
Wa kusaidia hilo ni Serikali tu,kama kalala usingizi unategemea nini?
Serikali hakuna kitu wanaweza fanya cha zaidi wataharibu flow ya biashara. Dawa yao hawa ni kuwaondoa katika mnyororo wa biashara na thamani kwa kutumia mbinu za kisasa za kibiashara.

Dawa yao inachemka.
 
Hiyo kukabidhi mzigo kwa dalali ni utaratibu rasmi?

Endapo ukigoma kukabidhi mzigo kwa dalali ili uuze mwenyewe, ni hatua gani zinachukuliwa dhidi ya mkaidi?
Tatizo huwezi lima na kuuza mwenyewe inagharimu muda na fedha, utapata hasara.
 
Serikali hakuna kitu wanaweza fanya cha zaidi wataharibu flow ya biashara. Dawa yao hawa ni kuwaondoa katika mnyororo wa biashara na thamani kwa kutumia mbinu za kisasa za kibiashara.

Dawa yao inachemka.
Tukifanikiwa hawa bidhaa nyingi za masokoni zitashuka bei na mtaona maumivu ya ughali WA maisha unapungua
 
Tukifanikiwa hawa bidhaa nyingi za masokoni zitashuka bei na mtaona maumivu ya ughali WA maisha unapungua
Na kikubwa zaidi mkulima atapata zaidi ya anavyopata sasa wananyonywa Sana
 
Back
Top Bottom