kijana wa leo
JF-Expert Member
- Nov 28, 2011
- 2,856
- 7,005
Leo niliibiwa materials kutoka eneo langu la kazi Mkoa A, baada ya kufatilia nikagundua mwizi amesafiri kwa njia ya Bus kuelekea mkoa B, nikafanya mawasiliano na Police wa mkoa B, wakanipa ushirikiano na kumkamata mwizi wangu akiwa na hayo material kwenye Bus kama nilivo report, na bahati nzuri alikiri kuyaiba kutoka Mkoa A.
Sasa, kwanza police wa Mkoa B wakanishauri kufungua kesi katika mkoa yalipoibiwa ambao ni mkoa A, nimetekeleza hilo na kuandika maelezo katika kituo cha police mkoa A, na kupata RB number ambayo niliwatumia police wa kituo cha Mkoa B wanaomshikiliwa mtuhumiwa.
Sasa, sa hivi nimeambiwa natakiwa kumsafirisha mtuhumiwa, ushahidi pamoja na askari kwa gharama zangu mwenyewe, ili aje kushtakiwa mkoa A, na bado mkoa A na B police wote wanataka posho kwa kushughulikia swala langu.
Sasa najiuliza pamoja na kuibiwa Mali zangu, bado natakiwa kutumia gharama zaidi ili nipate haki yangu.
Nimewambia sina hela kwa Leo ya kumsafirisha wanasema wanamwachia mtuhumiwa pamoja na kuwapa RB number.
Sasa, kwanza police wa Mkoa B wakanishauri kufungua kesi katika mkoa yalipoibiwa ambao ni mkoa A, nimetekeleza hilo na kuandika maelezo katika kituo cha police mkoa A, na kupata RB number ambayo niliwatumia police wa kituo cha Mkoa B wanaomshikiliwa mtuhumiwa.
Sasa, sa hivi nimeambiwa natakiwa kumsafirisha mtuhumiwa, ushahidi pamoja na askari kwa gharama zangu mwenyewe, ili aje kushtakiwa mkoa A, na bado mkoa A na B police wote wanataka posho kwa kushughulikia swala langu.
Sasa najiuliza pamoja na kuibiwa Mali zangu, bado natakiwa kutumia gharama zaidi ili nipate haki yangu.
Nimewambia sina hela kwa Leo ya kumsafirisha wanasema wanamwachia mtuhumiwa pamoja na kuwapa RB number.