DOKEZO Kero: Watumishi wilaya ya Momba tumechoka kunyanyaswa na Mwenyekiti wa Halmashauri

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
A

Anonymous

Guest
Habari wakuu,

Inasikitisha sana kuona kiongozi wetu badala awe mstari wa mbele kuwajali na kushirikiana na watumishi, yeye amekuwa ndio mtu wa kuwavunja ari, moyo, kukatisha tamaa na zaidi amekuwa ni mtu anayeongoza kutegeneza migogoro hali inayopelekea kuharibu upelekaji na utoaji wa huduma kwa wananchi.

Huyu kiongozi, hajawahi kuheshimu wala kufuata misingi ya utawala bora na ameshagombana na wakurugenzi kadhaa ambao wamepita na kufanya kazi katika halmashauri ya Momba, ameshaingia migogoro na wakuu wa wilaya kadhaa waliopita na kufanya kazi katika halmashauri ya wilaya ya Momba, ameshagombana na maafisa utumishi wote waliowahi kuhudumu katika halmashauri ya Momba ameshagombana na wabunge wote waliowahi kuhudumu na zaidi huyu anayehudumu sasa vita kubwa ikiwa ni ubunge 2025, ameshagombana na maafisa watendaji wengi na kuchochea wahamishwe kwenye kata yake, ameshagombana na maafisa kilimo wengi na kuchochea wahamishwe katika kata yake na maeneo mengine ya halmashauri, ameshagombana na kila viongozi wa idara kuanzia ngazi ya wilaya mpaka kijiji.

Mbaya zaidi amekuwa ni mla rushwa mkubwa kiasi cha kuathiri maendeleo ya taasisi mbalimbali na halmashauri Kwa ujumla. Hakuna ujenzi ambao hajawahi kuingilia iwe shule, vituo vya afya visima n.k. Kuna mradi wa maji kwenye kata yake ambao ulihitaji kuchimbwa kisima kipya na kujengwa tanki jipya lakini hakuna kilichofanyika badala yake lilikarabatiwa tanki lililokuwepo na kisima kinachotumika ni cha kanisa katoliki hali inayopelekea kuathiri huduma ya upatikanaji wa maji kwa wananchi. Kuna wakuu wa shule kadhaa waliwajibishwa kwa sababu ya kushindwa kukamilisha miradi kwenye taasisi zao kwa sababu huyu mwenyekiti aliwaomba rushwa Kwa vitisho ikiwemo shule ya sekondari Uwanda.

Mbaya zaidi alishawahi kunukuliwa akisema katika hadhara ya watu kwamba Rais Samia hajawahi kumkubali na analazimika kutokuonyesha kwa viongozi wa juu kwa sababu ya kulinda ugali wake kitu ni hatari kwa serikali na ustawi wa Chama Cha Mapinduzi.

Mwisho nashauri chama changu cha mapinduzi na serikali kwa ujumla, ufanyike uchunguzi juu ya haya niliyoyabainisha na ikiwezekana maamuzi magumu yafanyike ili kulinda hadhi ya chama, watumishi kudhalilishwa na kuonewa pasipo sababu za msingi.​
 
Ningependa ieleze kwa kuweka ushahidi hoja moja baada ya nyingine. Inawezekana vipi mtu akosane na halmashauri nzima ya Momba na kuwaonea wote kimakosa momba bila uchunguzi na kuchukuliwa hatua kwa takribani miaka minne sasa na tunakwenda mwaka wa tano mwakani? Yaani kwamba alikosana na wakuu wote wa wilaya kuanzia Mheshimiwa fakili lulandala mpaka sasa Mheshimiwa Kihongosi? Ungeeleza mfano kwa sasa wamekosana na DC wake katika nini? Unapozungumzia habari za rushwa iweje usema mradi fulani umeshindwa kukamilika kwa sababu alimlazimisha mwalimu mkuu fulani kutoa rushwa. Hivi hapo nani atakuwa mjinga? Unawezaje kutoa rushwa au fedha unazojuwa ni kinyume na sheria na ni za kujengea? Huyo Mwalimu bila shaka hajitambui na pengine ana Madudu mengi sana ambayo yanamfanya atoe rushwa kwa hofu ya kuumbuliwa Madudu yake.

Chama kipo chini ya uwenyekiti wa Mheshimiwa Radwell Mwampashe.je taarifa hizo zimefika ofisi za chama? Je taarifa za rushwa zipo ofisi za TAKUKURU? Kwa sababu hapa naona harufu ya kuchafuana pasipo ushahidi wa aina yoyote ile zaidi ya kufanya kazi ya kuorodhesha habari za kusema alikosana na huyu na yule na fulani na fulani ,jambo ambalo haliingia akilini na wala haliwezi kuaminika kwa kuwa halina mashiko wala ushahidi wa aina yoyote ile.

Suala la kusema vita ya ubunge.ningependa kusema ya kuwa mwana chama wa CCM yeyote yule anayo haki ya kutia nia na kugombea wakati ukifika.kwa hiyo hata huyo mwenyekiti wa halimashauri anayo haki hiyo na wala hakuna mwenye hati miliki ya jimbo la momba.kama mbunge aliyepo Mheshimiwa condester Sichalwe hafanyi vizuri basi akubali kuwa lazima atakutana na upinzani mkali pengine hata wa kumuondoa kabisa nafasi ya kugombea kupitia chama chetu cha CCM. Kitakachombeba Ni rekodi za kazi alizozifanya katika ubunge wake.kama hazipo basi ajuwe na ajiandae kuachia kijiti kwa mtu mwingine.na wala yeye hatakuwa mtu wa kwanza wala wa mwisho.

Tuache fitina , Majungu na kuchafuana pasipo ushahidi.acheni kukichafua chama mtandaoni kwa maslahi yenu binafsi.
 
Mbunge mwenyewe wa Momba ndio yule anakuja na pombe za kienyeji Bungeni, what a loss
 
Ningependa ieleze kwa kuweka ushahidi hoja moja baada ya nyingine. Inawezekana vipi mtu akosane na halmashauri nzima ya Momba na kuwaonea wote kimakosa momba bila uchunguzi na kuchukuliwa hatua kwa takribani miaka minne sasa na tunakwenda mwaka wa tano mwakani? Yaani kwamba alikosana na wakuu wote wa wilaya kuanzia Mheshimiwa fakili lulandala mpaka sasa Mheshimiwa Kihongosi? Ungeeleza mfano kwa sasa wamekosana na DC wake katika nini? Unapozungumzia habari za rushwa iweje usema mradi fulani umeshindwa kukamilika kwa sababu alimlazimisha mwalimu mkuu fulani kutoa rushwa. Hivi hapo nani atakuwa mjinga? Unawezaje kutoa rushwa au fedha unazojuwa ni kinyume na sheria na ni za kujengea? Huyo Mwalimu bila shaka hajitambui na pengine ana Madudu mengi sana ambayo yanamfanya atoe rushwa kwa hofu ya kuumbuliwa Madudu yake.

Chama kipo chini ya uwenyekiti wa Mheshimiwa Radwell Mwampashe.je taarifa hizo zimefika ofisi za chama? Je taarifa za rushwa zipo ofisi za TAKUKURU? Kwa sababu hapa naona harufu ya kuchafuana pasipo ushahidi wa aina yoyote ile zaidi ya kufanya kazi ya kuorodhesha habari za kusema alikosana na huyu na yule na fulani na fulani ,jambo ambalo haliingia akilini na wala haliwezi kuaminika kwa kuwa halina mashiko wala ushahidi wa aina yoyote ile.

Suala la kusema vita ya ubunge.ningependa kusema ya kuwa mwana chama wa CCM yeyote yule anayo haki ya kutia nia na kugombea wakati ukifika.kwa hiyo hata huyo mwenyekiti wa halimashauri anayo haki hiyo na wala hakuna mwenye hati miliki ya jimbo la momba.kama mbunge aliyepo Mheshimiwa condester Sichalwe hafanyi vizuri basi akubali kuwa lazima atakutana na upinzani mkali pengine hata wa kumuondoa kabisa nafasi ya kugombea kupitia chama chetu cha CCM. Kitakachombeba Ni rekodi za kazi alizozifanya katika ubunge wake.kama hazipo basi ajuwe na ajiandae kuachia kijiti kwa mtu mwingine.na wala yeye hatakuwa mtu wa kwanza wala wa mwisho.

Tuache fitina , Majungu na kuchafuana pasipo ushahidi.acheni kukichafua chama mtandaoni kwa maslahi yenu binafsi.
Kwa Mara Ya kwanza Nimebubujikwa Na Machozi Kusoma Andiko Lako Lenye Ukweli Mtupu na facts za Kutosha na hivi ndio Nilipenda siku zote uandike andiko La kisomi na Nimefurahi umendika..!

Kuna Vitu Viwili watu wanachanganya Japo mwenyekiti wa Halmashauri ni kiongozi wa Nyanja zote za Halmashauri ila anaongoza Akitetea Upande wa Wananchi..

Ila Mkurugenzi anatetea Upande wa Watumishi hivyo hawa wawili wakiungana na kufanya kazi kwa pamoja Ndiyo tunalata Halmashauri Bora na Yenye Mafanikio na makusanyo safi....

"Huyu akieleza Watumishi wanachangamoto gani kwanini hawajatimiza hiki na huyu anaeleza Wananchi wanasemaje kuhusu hilo muafaka Hupatikana..."

ALichoandika Mtoa Mada Bila shaka hajui majukumu ya Diwani/Mwenyekiti wa Halmashauri Ndani ya Wilaya Yake..

Kuna Mipaka Baina ya Majukumu iliyowekwa Kisheria kati ya Diwani/Meya na Watumishi wa Halmashauri Kuwa Meya/Diwani Haruhusiwi Kuingilia Majukumu yaliwekwa Kutimizwa Kitaaluma na hiyo Ipo kwenye Miongozo wa Sheria na Kila Diwani/M/Kiti halmashauri anajua hilo...
Hivyo hakuna ambaye angethubutu kufanya Hivyo....
hivyo nahisi Tuhuma hizo ni kumchafua Mheshimiwa Diwani tu na wala si kwa lengo lingine....

Hapa Chini nimekuwekea Miongozo kadhaa ili watu wazisome Kupata Uelewa Jinsi Majukumu Yanavyoenda...

  • Majukumu Ya Kazi ya Mwenyekiti wa Halmashauri na wenyeviti wengine ndani ya Halmashauri mwongozo wa mwaka 2006..
  • Mahusiano baina ya Diwani na watumishi Muongozo wa mwaka 2006
  • Majukumu Ya Nafasi Ya Diwani Katika Halmashauri Muongozo wa Mwaka 2006..

Hope Hiyo Itasaidia Kuondoa Sintofahamu na Mtoa mada ataelimika pia
 

Attachments

  • Mahusiano baina ya Madiwani na Watumishi wa Halmashauri.pdf
    61.1 KB · Views: 3
  • 590b0cffd7620081917365.pdf
    58.7 KB · Views: 3
  • MAJUKUMU-NA-KAZI-ZA-MEYA-MWENYEKITI-WA-HALMASHAURI-MADIWANI-NA-WENYEVITI-WA-VIJIJI-MITAA-NA-VI...pdf
    43.2 KB · Views: 3
Kwa Mara Ya kwanza Nimebubujikwa Na Machozi Kusoma Andiko Lako Lenye Ukweli Mtupu na facts za Kutosha na hivi ndio Nilipenda siku zote uandike andiko La kisomi na Nimefurahi umendika..!

Kuna Vitu Viwili watu wanachanganya Japo mwenyekiti wa Halmashauri ni kiongozi wa Nyanja zote za Halmashauri ila anaongoza Akitetea Upande wa Wananchi..

Ila Mkurugenzi anatetea Upande wa Watumishi hivyo hawa wawili wakiungana na kufanya jazi kwa pamoja Huyu akieleza Watumishi wanachangamoto gani kwanini hawajatimiza hiki na huyu anaeleza Wananchi wanasemaje kuhusu hilo muafaka Hupatikana...

ALichoandika Mtoa Mada Bila shaka hajui majukumu ya Diwani/Mwenyekiti wa Halmashauri Ndani ya Wilaya Yake..

Kuna Mipaka Baina ya Majukumu iliyowekwa Kisheria kati ya Diwani/Meya na Watumishi wa Halmashauri Kuwa Meya/Diwani Haruhusiwi Kuingilia Majukumu yaliwekwa Kutimizwa Kitaaluma na hiyo Ipo kwenye Miongozo wa Sheria na Kila Diwani/M/Kiti halmashauri anajua hilo...
Hivyo hakuna ambaye angethubutu kufanya Hivyo....
hivyo nahisi Tuhuma hizo ni kumchafua Mheshimiwa Diwani tu na wala si kwa lengo lingine....

Hapa Chini nimekuwekea Miongozo kadhaa ili watu wazisome Kupata Uelewa Jinsi Majukumu Yanavyoenda...

  • Majukumu Ya Kazi ya Mwenyekiti wa Halmashauri na wenyeviti wengine ndani ya Halmashauri mwongozo wa mwaka 2006..
  • Mahusiano baina ya Diwani na watumishi Muongozo wa mwaka 2006
  • Majukumu Ya Nafasi Ya Diwani Katika Halmashauri Muongozo wa Mwaka 2006..

Hope Hiyo Itasaidia Kuondoa Sintofahamu na Mtoa mada ataelimika pia
Nashukuru sana japo naona nilipofika kufungua file ulizoambatanisha zimegoma kufunguka kwenye simu yangu. Nahisi ni changamoto ya mtandao. Nitajaribu tena baadaye kufungua .
 
Nashukuru sana japo naona nilipofika kufungua file ulizoambatanisha zimegoma kufunguka kwenye simu yangu. Nahisi ni changamoto ya mtandao. Nitajaribu tena baadaye kufungua .
Zisome hizo faili ni faili moja Bora sana Sheria hizo za madiwani na Miongozo ya usimamizi ilitungwa kipindi cha JK yuko madarakani na Ndo inatumika Mpaka hivi leo..

Ukiisoma Hiyo huwezi kumlaumu Meya au Mbunge au Diwani Kutimiza Majukumu yake kwa Kukubana wewe Mtumishi na wala Huwezi kumlaumu Yeye Kusimama upande wa Wananchi..

Asante sana
 
Mwenyekiti wa halmashauri ni diwani tu. Na yawezekana kabisa akawa ni darasa la 7. Sasa diwani ananzaje kuwanyanyasa watumishi ambao wengi wana shahada (na tena baadhi yao wana PhD)?
Mlisimamia wizi WA kura. Tulieni sindano iwaingie
 
Ningependa ieleze kwa kuweka ushahidi hoja moja baada ya nyingine. Inawezekana vipi mtu akosane na halmashauri nzima ya Momba na kuwaonea wote kimakosa momba bila uchunguzi na kuchukuliwa hatua kwa takribani miaka minne sasa na tunakwenda mwaka wa tano mwakani? Yaani kwamba alikosana na wakuu wote wa wilaya kuanzia Mheshimiwa fakili lulandala mpaka sasa Mheshimiwa Kihongosi? Ungeeleza mfano kwa sasa wamekosana na DC wake katika nini? Unapozungumzia habari za rushwa iweje usema mradi fulani umeshindwa kukamilika kwa sababu alimlazimisha mwalimu mkuu fulani kutoa rushwa. Hivi hapo nani atakuwa mjinga? Unawezaje kutoa rushwa au fedha unazojuwa ni kinyume na sheria na ni za kujengea? Huyo Mwalimu bila shaka hajitambui na pengine ana Madudu mengi sana ambayo yanamfanya atoe rushwa kwa hofu ya kuumbuliwa Madudu yake.

Chama kipo chini ya uwenyekiti wa Mheshimiwa Radwell Mwampashe.je taarifa hizo zimefika ofisi za chama? Je taarifa za rushwa zipo ofisi za TAKUKURU? Kwa sababu hapa naona harufu ya kuchafuana pasipo ushahidi wa aina yoyote ile zaidi ya kufanya kazi ya kuorodhesha habari za kusema alikosana na huyu na yule na fulani na fulani ,jambo ambalo haliingia akilini na wala haliwezi kuaminika kwa kuwa halina mashiko wala ushahidi wa aina yoyote ile.

Suala la kusema vita ya ubunge.ningependa kusema ya kuwa mwana chama wa CCM yeyote yule anayo haki ya kutia nia na kugombea wakati ukifika.kwa hiyo hata huyo mwenyekiti wa halimashauri anayo haki hiyo na wala hakuna mwenye hati miliki ya jimbo la momba.kama mbunge aliyepo Mheshimiwa condester Sichalwe hafanyi vizuri basi akubali kuwa lazima atakutana na upinzani mkali pengine hata wa kumuondoa kabisa nafasi ya kugombea kupitia chama chetu cha CCM. Kitakachombeba Ni rekodi za kazi alizozifanya katika ubunge wake.kama hazipo basi ajuwe na ajiandae kuachia kijiti kwa mtu mwingine.na wala yeye hatakuwa mtu wa kwanza wala wa mwisho.

Tuache fitina , Majungu na kuchafuana pasipo ushahidi.acheni kukichafua chama mtandaoni kwa maslahi yenu binafsi.
Ningekushauri upige simu hata Kwa kiongozi yeyote wa chama katika mkoa au wilaya ujifunze jambo juu ya huyu mtu. Binafsi namshukuru aliyeleta hili andiko kwani lengo lake ni kutaka abadilike na aache tabia za kunyanyasa wataalamu badala yake awaheshimu
 
Haya majungu ni hatari. Hakuna diwani anaweza kugombana na watu wote hao akabaki salama. Mkuu mwenyewe Kihongosi ndo apelekeshwe na diwani? Hayo masikhara. WanaCCM MSICHAFUANE.
 
Diwani anawahenyesha watendaji,!!!

Mwenyekiti wa halmshauri hawezi kuzinguana na mkurugenzi aka mtunza maokoto!!! Akimkolome DC anachezea selo.

Maluzaneni 2025
 
Huyo mwenyekiti ni mzinguaji sana nakumbuka tangu ilipokuwa Wilaya moja ya Mbozi alikuwa mtu wa vitisho sana.Kumbe bado anaendelea na tabia hizo.?
Chama na vyombo vya usalama wamfuatilie huyu.
 
Kwanza nakupongeza kwa kuwasemea wengi amboa ni waoga wa kudai haki zao. Pia naungana na wewe keto ya malimbikizo ya pesa za nauli, mshahara na nyinginezo imekithili serekalini na hii inatokana na mtandao wa wezi ambalo umekuwepo ngazi ya halmashauri mpaka taifa. Kiukweli jambo hili si jema kwa afya ya wafanyakazi na kwa taifa kiujumla.

Chanzo cha yote hayo ni kuwa na viongozi wasio na weledi katika majukumu yao ya kila siku. Mfano huku kwetu malimbikizo yanachukua mda mrefu kufanyiwa kazi. Mfano pesa ya nauli ya nauli ya likizo unaweza kulipwa baada ya miaka mitata. Lakini jambo la kushangaza hali hii Iko tu kwa idara ya elimu sekondari, kwa upande wa elimu msingi wao wanapata pesa ya likizo kabla ya likizo. Sasa sijui shida iko wapi kwa nani kati serekali au viongozi wetu?

Kuna muda nafikilia yawezekana pesa zetu zikawa zinamekwa kwenye fixed account ili wapuuzi hawa wapige pesa. Na kama hili ni sahihi naomba wasifanye hivyo maana wanaumiza wafanyakazi.

Mwisho naomba serekali ilifanyie kazi jambo hili kwa kuwalazimisha maafisa utumishi kutumia mfumo wa ess na sio mikaratasi. Hii itasaidia kuweka record vizuri, kwa sasa rafu ni nyingi mfano unapeleka ombi lako la likizo kwa karatasi alafu linachomolewa kwenye jarada na kutupwa. Baada ya hapo unaambiwa omba tena na ukizingatia unadai elfu tisini tu. Chonde chonde nawaomba wausika msilifumbie macho jambo hili. Pia kama serekali hamuwezi kulipa pesa za nauli nawashauri mwapangie wafanyakazi vituo vya kazi karibu na mazingira ya kwao.

Sent from my ZTE T1002 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom