Kamanda Muliro: Malisa GJ, Boniface Jacob wakamatwe kwa tuhuma za kupotosha taarifa za kifo cha Robart Mushi

Shetani hajawahi kumshinda Mungu
Shetani hajawahi kumshinda Mungu
Kwahiyo Polisi ni Mashetani?
Una mungu wa ajabu sana wewe...

Embu kwa dakika wachana na Ushabiki wa kuchanganya dini na siasa, na UCHADEMA

Rudia tena usome nillichobandika.

Ni hivi, kama ni kweli Polisi wanadhamiria kumkamata , wanashindwa nini kumkamata halafu ndio watoe Taarifa kwamba ameitwa au kukamatwa kwa 'upotoshaji wa umma' na kwa 'lengo la kuleta taharuki' Uchonganishi wa raia na polisi?

Shetani amwingie Jakobo, umsingizie polisi. Jakobo sio Mungu wa yeyote yule.
 
Kwa huko kusema tu kuwa Mochwari imejaa wakaamua kupeleka hospital ya Kilwa inatosha kuonyesha kuna uwalakini kwenye hicho kifo, kwanini wasingepeleka mwili Muhimbili, kwanini siyo Temeke waupeleke hospital yao!!? Mulilo anataka kuwa muongo kama Mambosasa?
 
Hili jeshi la Polisi ni lini liliwahi kukiri kuwa limeua raia wasio na hatia?

Walipomwua Mwangosi walisema eti ameangukiwa na kitu kizito, picha za raia ziliwaumbua kwa uwongo.

Walipowaua wafanyabiashara wa madini na kuwapora pesa zao, walidai kuwa ni majambazi na kuwa waliuawa wakati wa kurushiana risasi. Mpaka wakaenda kupiga risasi nyumba kule Sinza ili kuwahadaa watu kulikuwa na kurushiana risasi. Ushahidi wa mashuhuda na mazingira ya walikowaulia, viliwaumbua na kidhihirishia uwongo wao.

Hawa akina Muliro siyo wa kuwaamini hata kidogo:

Eti mtu agongwe na gari, afikishwe hospitali, athibitike amefariki, halafu eti ikosekane nafasi mortuary, mwili upelekwe mortuary ya polisi. Maswali ya kujiuliza;

1. Ndugu wa marehemu walikwenda vituo vyote vya polisi kuulizia habari za ndugu yao, polisi walikataa kuwa hawana habari yoyote. Mfumo wa polisi ni kwamva matukio yote ya uhalifu, ajali na yote yanayoligusa jeshi la polisi, taarifa hupelekwa vituo vyote. Kwa nini taarifa ya huyo marehemu ilifanywa tofauti na kanuni?

2. Polisi baada kuupeleka mwili wa marehemu kwenye mortuary ya polisi, hawakutoa tangazo lolote kwa umma kueleza kuwa wanashikilia mwili wa marehemu wasiyemfahamu. Tumesikia kutoka kwa ndugu wa marehemu kuwa taarifa kuwa mwili wa marehemu upo mortuary ya polisi ilitolewa kwa siri na askari mmoja. Kwa nini ilifanywa siri?
 
Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam linatoa ufafanuzi kuhusiana na taarifa ya uongo na uzushi inayosambaa katika mitandao ya kijamii kuhusiana na kifo cha Robart Mushi @ Babu G. ambaye picha yake imeambatanishwa kwenye taarifa hizo kuwa alipotea tarehe 11 Aprili, 2024 na baadae kugundulika katika Chumba cha kuhifadhi maiti katika Hospitali ya Polisi Kilwa Road huku ikidaiwa Polisi kuhusika na kifo hicho kwa kumuua..

Ukweli ni kwamba tarehe 11 Aprili, 2024 majira ya saa 10 Alfajiri Askari Polisi wa Usalama barabarani alipewa taarifa na mwananchi kuwa eneo laTaa za kuongozea magari za Buguruni, Ilala mtu mmoja mwanaume aliyekuwa akivuka barabara eneo hilo la Kimboka kuelekea Chama aligongwa na gari ambalo halikusimama (hit and Run).

Mtu huyo alipata majeraha makubwa kichwani, kifuani na eneo la chini la mgongo na kisigino cha mguu wa kulia. Eneo hilo lina watu wengi ambao wanakesha kwa biashara mbalimbali na walishuhudia tukio hilo.

Mtu huyo alipelekwa haraka hospitali ya Amana na Polisi lakini baada ya kumfikisha Madaktari walibaini kuwa mtu huyo alikuwa tayari amekwishafariki, Kwa sababu chumba cha kuhifadhi maiti cha hospitali ya Amana kilikuwa hakina nafasi, ilishauriwa akahifadhiwe kwenye Hospitali ya Jeshi la Polisi iliyo barabara ya Kilwa Temeke ambayo inatoa huduma hata kwa raia kuhusiana na suala hilo.Tarehe 21.4,2024 ndugu wa marehemu walipatikana na wakautambua mwili wa ndugu yao kwani hakuwa na kitambulisho wala simu. Taratibu za mwisho za mazishi zinafanywa ili akazikwe.

Kutokana na taharuki iliyotengenezwa na kujengwa kwa makusudi na mtu anayejiita Malisa gj na Bonoface Jacob ambao kwenye “post” zao walionesha nia ya wazi ya kutengeneza chuki dhidi ya Polisi na Serikali kwa wananchi kuwa mtu huyo aliyepata ajali alikuwa ameuawa na Polisi , Kitendo kilichofanywa na watu hao ni kosa kisheria na hakivumiliki na lazima Jeshi lichukue hatua za kisheria dhidi ya wahusika ikiwa ni pamoja na kuwakamata , kuwahoji kwa kina na kuwafikisha mahakamani haraka iwezekanavyo.

Jeshi la Polisi halitavumilia watu ambao wanaibuka na taarifa za uongo na uzushi ambazo zinalenga kujenga chuki na taharuki kwa wananchi. Jeshi litaendelea kusimamia misingi ya kisheria na halitakuwa na huruma kwa mtuhumiwa yoyote wa kihalifu na litamshughulikia haraka iwezekanavyo kwa mujibu wa sheria.

Imetolewa na ;
Muliro J. MULIRO - SACP
Kamanda wa Polisi
Kanda Maalum ya Dar es Salaam

Pia soma:


Mauaji ya Robert Mushi ndugu wa aliyekuwa Meya wa Ubungo Boniface Jacob polisi wanahusika?
Kwanini hakupelekwa Temeke au Muhimbili, badala yake akapelekwa kwa mtuhumiwa?
 
Daah aisee hii taarifa sio nzuri jamaa kapotea kirahisi tu aisee harafu wanatoa taarifa kuwa aligongwa na gari wao ndio walikua wasamalia wema aisee...
 
Kitendo kilichofanywa na watu hao ni kosa kisheria na hakivumiliki na lazima Jeshi lichukue hatua za kisheria dhidi ya wahusika ikiwa ni pamoja na kuwakamata , kuwahoji kwa kina na kuwafikisha mahakamani haraka iwezekanavyo.
Kwa hiyo Jeshi linamuagiza nani akawakamate?
 
Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam linatoa ufafanuzi kuhusiana na taarifa ya uongo na uzushi inayosambaa katika mitandao ya kijamii kuhusiana na kifo cha Robart Mushi @ Babu G. ambaye picha yake imeambatanishwa kwenye taarifa hizo kuwa alipotea tarehe 11 Aprili, 2024 na baadae kugundulika katika Chumba cha kuhifadhi maiti katika Hospitali ya Polisi Kilwa Road huku ikidaiwa Polisi kuhusika na kifo hicho kwa kumuua..

Ukweli ni kwamba tarehe 11 Aprili, 2024 majira ya saa 10 Alfajiri Askari Polisi wa Usalama barabarani alipewa taarifa na mwananchi kuwa eneo laTaa za kuongozea magari za Buguruni, Ilala mtu mmoja mwanaume aliyekuwa akivuka barabara eneo hilo la Kimboka kuelekea Chama aligongwa na gari ambalo halikusimama (hit and Run).

Mtu huyo alipata majeraha makubwa kichwani, kifuani na eneo la chini la mgongo na kisigino cha mguu wa kulia. Eneo hilo lina watu wengi ambao wanakesha kwa biashara mbalimbali na walishuhudia tukio hilo.

Mtu huyo alipelekwa haraka hospitali ya Amana na Polisi lakini baada ya kumfikisha Madaktari walibaini kuwa mtu huyo alikuwa tayari amekwishafariki, Kwa sababu chumba cha kuhifadhi maiti cha hospitali ya Amana kilikuwa hakina nafasi, ilishauriwa akahifadhiwe kwenye Hospitali ya Jeshi la Polisi iliyo barabara ya Kilwa Temeke ambayo inatoa huduma hata kwa raia kuhusiana na suala hilo.Tarehe 21.4,2024 ndugu wa marehemu walipatikana na wakautambua mwili wa ndugu yao kwani hakuwa na kitambulisho wala simu. Taratibu za mwisho za mazishi zinafanywa ili akazikwe.

Kutokana na taharuki iliyotengenezwa na kujengwa kwa makusudi na mtu anayejiita Malisa gj na Bonoface Jacob ambao kwenye “post” zao walionesha nia ya wazi ya kutengeneza chuki dhidi ya Polisi na Serikali kwa wananchi kuwa mtu huyo aliyepata ajali alikuwa ameuawa na Polisi , Kitendo kilichofanywa na watu hao ni kosa kisheria na hakivumiliki na lazima Jeshi lichukue hatua za kisheria dhidi ya wahusika ikiwa ni pamoja na kuwakamata , kuwahoji kwa kina na kuwafikisha mahakamani haraka iwezekanavyo.

Jeshi la Polisi halitavumilia watu ambao wanaibuka na taarifa za uongo na uzushi ambazo zinalenga kujenga chuki na taharuki kwa wananchi. Jeshi litaendelea kusimamia misingi ya kisheria na halitakuwa na huruma kwa mtuhumiwa yoyote wa kihalifu na litamshughulikia haraka iwezekanavyo kwa mujibu wa sheria.

Imetolewa na ;
Muliro J. MULIRO - SACP
Kamanda wa Polisi
Kanda Maalum ya Dar es Salaam

Pia soma:


Mauaji ya Robert Mushi ndugu wa aliyekuwa Meya wa Ubungo Boniface Jacob polisi wanahusika?
Pale kimboka ni hatari kwa kuua wapita kwa miguu!
 
Kamanda Murilo amechemka kwa 100%. Taarifa yake imepikwa bila kuiva. Uongo wa taarifa yake uko hapa.
1. Anasema marehemu hakuwa na utambulisho wowote (yaani hata polisi walikuwa hawamju, lakini baada ya kufariki na kupelekwa hospitali ya kituo cha Polisi Kilwa, mara moja ndugu zake walifika kuuchukua mwili wake!!!

2. Polisi wanasema mwili wa marehemu ulikosa nafasi ya kuhifadhiwa hospital ya Amana hivyo wakampeleka hospitali ya kituo cha Polisi Kilwa. Hapo ndipo utata mkubwa zaidi wa taarifa ya Polisi ulipo(Tukipata muda tutajadili kwa kina).

3. Polisi wanasema wanahisi marehemu alikufa kwa kugongwa na gari, lakini hapo hapo wameshindwa kuitisha uchunguzi wa kuthibitisha kifo cha marehemu.
 
Sawa.baada ya kumchukua na kumpeleka hospital akiwa maiti je polisi walitangaza wapi kuwa kuna mtu kagongwa na gari na amefariki. Kwanini walikaa kimya?
Inawezekana Malisa na mwenzie wameingia kwenye 18. Huenda palikuwa na ajali kweli. Kama hawana ushahidi wa kukamatwa kwa marehemu na kupelekwa kituoni ambapo wanadai alipigwa basi wana kashughuli.
 
WEWE UMEFIKIRI KWA KUTUMIA BRAIN EMBEDED IN THE RECTUM

Polisi huwezi kuletewa maiti usitangaze, unakaa nayo all this time without alerting the public!
Jamaa sijui anajua kutangaza ni kutoka na kispika barabarani it's very shame
 
Back
Top Bottom