Kamanda Muliro: Malisa GJ, Boniface Jacob wakamatwe kwa tuhuma za kupotosha taarifa za kifo cha Robart Mushi

Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam linatoa ufafanuzi kuhusiana na taarifa ya uongo na uzushi inayosambaa katika mitandao ya kijamii kuhusiana na kifo cha Robart Mushi @ Babu G. ambaye picha yake imeambatanishwa kwenye taarifa hizo kuwa alipotea tarehe 11 Aprili, 2024 na baadae kugundulika katika Chumba cha kuhifadhi maiti katika Hospitali ya Polisi Kilwa Road huku ikidaiwa Polisi kuhusika na kifo hicho kwa kumuua..

Ukweli ni kwamba tarehe 11 Aprili, 2024 majira ya saa 10 Alfajiri Askari Polisi wa Usalama barabarani alipewa taarifa na mwananchi kuwa eneo laTaa za kuongozea magari za Buguruni, Ilala mtu mmoja mwanaume aliyekuwa akivuka barabara eneo hilo la Kimboka kuelekea Chama aligongwa na gari ambalo halikusimama (hit and Run).

Mtu huyo alipata majeraha makubwa kichwani, kifuani na eneo la chini la mgongo na kisigino cha mguu wa kulia. Eneo hilo lina watu wengi ambao wanakesha kwa biashara mbalimbali na walishuhudia tukio hilo.

Mtu huyo alipelekwa haraka hospitali ya Amana na Polisi lakini baada ya kumfikisha Madaktari walibaini kuwa mtu huyo alikuwa tayari amekwishafariki, Kwa sababu chumba cha kuhifadhi maiti cha hospitali ya Amana kilikuwa hakina nafasi, ilishauriwa akahifadhiwe kwenye Hospitali ya Jeshi la Polisi iliyo barabara ya Kilwa Temeke ambayo inatoa huduma hata kwa raia kuhusiana na suala hilo.Tarehe 21.4,2024 ndugu wa marehemu walipatikana na wakautambua mwili wa ndugu yao kwani hakuwa na kitambulisho wala simu. Taratibu za mwisho za mazishi zinafanywa ili akazikwe.

Kutokana na taharuki iliyotengenezwa na kujengwa kwa makusudi na mtu anayejiita Malisa gj na Bonoface Jacob ambao kwenye “post” zao walionesha nia ya wazi ya kutengeneza chuki dhidi ya Polisi na Serikali kwa wananchi kuwa mtu huyo aliyepata ajali alikuwa ameuawa na Polisi , Kitendo kilichofanywa na watu hao ni kosa kisheria na hakivumiliki na lazima Jeshi lichukue hatua za kisheria dhidi ya wahusika ikiwa ni pamoja na kuwakamata , kuwahoji kwa kina na kuwafikisha mahakamani haraka iwezekanavyo.

Jeshi la Polisi halitavumilia watu ambao wanaibuka na taarifa za uongo na uzushi ambazo zinalenga kujenga chuki na taharuki kwa wananchi. Jeshi litaendelea kusimamia misingi ya kisheria na halitakuwa na huruma kwa mtuhumiwa yoyote wa kihalifu na litamshughulikia haraka iwezekanavyo kwa mujibu wa sheria.

Imetolewa na ;
Muliro J. MULIRO - SACP
Kamanda wa Polisi
Kanda Maalum ya Dar es Salaam

Pia soma:


Mauaji ya Robert Mushi ndugu wa aliyekuwa Meya wa Ubungo Boniface Jacob polisi wanahusika?
Tangu Lini Mochwari za Polisi zikaanza kutunza Maiti za Raia waliokufa kwa ajali ? Huyu Muliro hana hata haya kusimama mbele ye Media na kuwahadaa wananchi ?
 
Tangu tarehe 10 April mpaka jana tarehe 22 April Polisi walishindwa kutangaza kuokotwa kwa maiti ya mtu huyo ‘aliyegongwa na gari’ pamoja na jitihada zote za ndugu zake kumtafuta? Waliuhifadhi huo mwili ili iweje?

Maeneo ambayo ndugu walimtafuta ni pamoja na vituo vua Polisi, je Polisi walishindwa kuangalia kwenye Mortuary yao?
Labda walitaka kuufanya uwe cadaver ( dead human body used in scientific and medical research).

Bure kabisa Hawa jamaa yaani wamekaa na maiti karibu week 2 bila kutoa taarifa wanaona sawa tu.
 
Eti Amana mochwari ilijaa wakampeleka Hospitali ya Jeshi la Polisi ??? Kwa nini hakupelekwa mUhimbili au hospitali ya Temeke ???
Hii kesi nyepesi sana kwa ex mayor Jacob

Inafikirisha sana ,halafu kumbuka kwamba ndugu walitoa taarifa vituo vya polisi na pia walizunguka hospital kubwa kubwa mochwari ,lakini polisi wala hawakukumbuka kusema kwamba waje kuangalia mwili pindi ndugu walivyotoa taarifa ,zimepita karibia wiki mbili ndiyo wanakuja kusema.
 
Napata ukakasi kama Amana ilijaa nimaiti ngapi ziliamishiwa hospitali ya polisi siku hiyo au alikufa Robert tuu kama Kuna mwingine watuambie na wao walipekwa huko au muhimbili hata lugaro!
 
Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam linatoa ufafanuzi kuhusiana na taarifa ya uongo na uzushi inayosambaa katika mitandao ya kijamii kuhusiana na kifo cha Robart Mushi @ Babu G. ambaye picha yake imeambatanishwa kwenye taarifa hizo kuwa alipotea tarehe 11 Aprili, 2024 na baadae kugundulika katika Chumba cha kuhifadhi maiti katika Hospitali ya Polisi Kilwa Road huku ikidaiwa Polisi kuhusika na kifo hicho kwa kumuua..

Ukweli ni kwamba tarehe 11 Aprili, 2024 majira ya saa 10 Alfajiri Askari Polisi wa Usalama barabarani alipewa taarifa na mwananchi kuwa eneo laTaa za kuongozea magari za Buguruni, Ilala mtu mmoja mwanaume aliyekuwa akivuka barabara eneo hilo la Kimboka kuelekea Chama aligongwa na gari ambalo halikusimama (hit and Run).

Mtu huyo alipata majeraha makubwa kichwani, kifuani na eneo la chini la mgongo na kisigino cha mguu wa kulia. Eneo hilo lina watu wengi ambao wanakesha kwa biashara mbalimbali na walishuhudia tukio hilo.

Mtu huyo alipelekwa haraka hospitali ya Amana na Polisi lakini baada ya kumfikisha Madaktari walibaini kuwa mtu huyo alikuwa tayari amekwishafariki, Kwa sababu chumba cha kuhifadhi maiti cha hospitali ya Amana kilikuwa hakina nafasi, ilishauriwa akahifadhiwe kwenye Hospitali ya Jeshi la Polisi iliyo barabara ya Kilwa Temeke ambayo inatoa huduma hata kwa raia kuhusiana na suala hilo.Tarehe 21.4,2024 ndugu wa marehemu walipatikana na wakautambua mwili wa ndugu yao kwani hakuwa na kitambulisho wala simu. Taratibu za mwisho za mazishi zinafanywa ili akazikwe.

Kutokana na taharuki iliyotengenezwa na kujengwa kwa makusudi na mtu anayejiita Malisa gj na Bonoface Jacob ambao kwenye “post” zao walionesha nia ya wazi ya kutengeneza chuki dhidi ya Polisi na Serikali kwa wananchi kuwa mtu huyo aliyepata ajali alikuwa ameuawa na Polisi , Kitendo kilichofanywa na watu hao ni kosa kisheria na hakivumiliki na lazima Jeshi lichukue hatua za kisheria dhidi ya wahusika ikiwa ni pamoja na kuwakamata , kuwahoji kwa kina na kuwafikisha mahakamani haraka iwezekanavyo.

Jeshi la Polisi halitavumilia watu ambao wanaibuka na taarifa za uongo na uzushi ambazo zinalenga kujenga chuki na taharuki kwa wananchi. Jeshi litaendelea kusimamia misingi ya kisheria na halitakuwa na huruma kwa mtuhumiwa yoyote wa kihalifu na litamshughulikia haraka iwezekanavyo kwa mujibu wa sheria.

Imetolewa na ;
Muliro J. MULIRO - SACP
Kamanda wa Polisi
Kanda Maalum ya Dar es Salaam

Pia soma:


Mauaji ya Robert Mushi ndugu wa aliyekuwa Meya wa Ubungo Boniface Jacob polisi wanahusika?
Nafikiri Kamanda Muliro anapaswa kuona aibu kuzungumzia baadhi ya Mambo yanayolichafua Jeshi la Polisi kama tukio hili. Wakati mwingine kukaa kimya ni busara na hekima zaidi kuliko kutoa taarifa ambayo inazua utata mkubwa ktk jamii sambamba kukuondolea credibility ktk jamii hiyo.
 
Ila ukisikiliza maelezo ya Kamanda Muliro, kuna namna Jacob kakosea. Inaonyesha kuwa hata ndugu zake na huyo Marehemu wamekubaliana na maelezo ya Polisi.
Ndugu wepi hao wanaokubaliana na maelezo ya Polisi???
Tukubali tu ukweli kwamba tukio hili lina ukakasi na utata mkubwa sana. Kwa vyovyote itakavyokuwa Jeshi la Polisi haliwezi kukwepa kuhusishwa moja kwa moja na Kifo cha huyu mtu kwa sababu maiti ya huyo mtu 'imekutwa ndani mwao.' Ukikamatwa na ngozi lazima ueleze nyama iko wapi au nyama kala nani!
 
Inasikitisha Serikali kutumia kodi zetu Kumsafirisha Malisa G.J hadi Moshi kwenda kufanya Upekuzi.

Yaani Polisi wanafikiria wakienda moshi watapata ushahidi wowote? Kama ndugu wanajua polisi wanakuja si watatoa kila kitu wabakize makochi na vitanda tu ndani?
 
Inasikitisha Serikali kutumia kodi zetu Kumsafirisha Malisa G.J hadi Moshi kwenda kufanya Upekuzi.

Yaani Polisi wanafikiria wakienda moshi watapata ushahidi wowote? Kama ndugu wanajua polisi wanakuja si watatoa kila kitu wabakize makochi na vitanda tu ndani?
Na wanajua baba yake Malisa GJ ni Inspekta mstaafu anajua figisu zao zote.
 
Na wanajua baba yake Malisa GJ ni Inspekta mstaafu anajua figisu zao zote.

Kabisa yaani sijajua wamewaza nini kuchoma mafuta hadi Moshi labda wanafanya tour na kulamba Over Time tu.,,nina uhakika 100% hawakuti chochote huko.

Ila Boniface mafia wamemuibukia saa saba usiku lakini walimkosa hahaaaa
 
Inasikitisha Serikali kutumia kodi zetu Kumsafirisha Malisa G.J hadi Moshi kwenda kufanya Upekuzi.

Yaani Polisi wanafikiria wakienda moshi watapata ushahidi wowote? Kama ndugu wanajua polisi wanakuja si watatoa kila kitu wabakize makochi na vitanda tu ndani?
Imekuaje tena huko mkuu hebu tuhabarishe
 
Baada ya polisi kumuua Mushi, walienda kuuhifadhi mwili wake kwenye mochwari ya polisi kwa sababu walipompeleka Amana madaktari waliwaomba PF3 wakashindwa kutoa. Na wasingeweza kutoa PF3 kwa kuwa ni wao wenyewe waliomuua. Hivyo, wakaona isiwe tabu wakapeleka mwili kwenye mochwari ya polisi ambayo haina maswali mengi.

Wakati ndugu wanatafuta mwili wa ndugu yao, polisi waliuficha na kukaa kimya kwa kuwa bado walikuwa hawajamaliza kutunga uwongo. Baada ya kumaliza kutunga uwongo ndipo wakasema mwili wanao wao.

Mungu hadhihakiwi. Jiwe alikuwa anauawa watu na kuwafunga kwenye viroba anaenda kutupa baharini. Alimkosakosa Tundu Lissu hivi sasa natembea kwa kuchechemea huku akiwa amejaa vyuma mwili mzima. Hata General Bokasa na madikteta wengine kama Idd Amini na Foday Sanko, waliua mamilioni ya raia wasiokuwa na hatia lakini leo hii wapo kaburini wameoza imebaki mifupa tupu. Na hata huenda mifupa mingine imeoza limebaki fuvu tu.

Hawa polisi wanaowaua raia na kisha kutunga uwongo na kuuhadaa umma, nao kiama chao kinakuja na watakuja kufa vifo vibaya sana. Mungu hadhihakiwi.
 
Back
Top Bottom