Jicho langu: Tabora walinyimwa goli halali kama la Aziz Ki

Aug 29, 2022
69
133
Jicho langu:Tabora walinyimwa goli halali kama la Aziz Ki

Klabu ya Tabora united katika mchezo wa jana walinyimwa goli la halali katika mchezo wao waligi kuu ya NBCPL waliocheza na Simba katika Dimba la Azam Complex Chamazi na Simba kuibuka kwa ushindi wa magoli mawili.

Kwa Jicho langu la kimchezo lile lilikuwa goli halali kabisa lakini inawezekana mwamuzi hakuwa na utulivu wa kutazama zaidi kujuwa je lilikuwa goli au sio goli

Lakini pia baada ya tukio hilo Simba wakaanzisha shambulizi la haraka na wakapata goli la pili na kuondoka na alama 3 muhimu kwao

Nikukumbushe tu tukio hilo liliwakuta Yanga katika mchezo wa robo fainali ya Klabu Bingwa Afrika msimu huu dhidi ya Mamelod kutokea Afrika ya kusini ,goli alilofunga Azizi Ki lilikuwa kama la jana la Tabora na goli lile lilikataliwa licha kulikuwepo na VAR

Sasa kwa mtazamo wangu si lazima tuwe na VAR maana tutachelewa kufika huko ila kwa sasa shirikisho la mpira wa Miguu TFF waongee na Azam Media ambao ndiyo wenye dhama ya kurusha matangazo ya TV ya ligi yetu wapate tv nyingine ambayo atakuwepo mwamuzi katika kuangalia matukio yenye utata .

Hii inaweza kusaidia kwa udogo kupunguza utata katika michezo ya ligi kuu ya NBCPL
anaweza akawepo mwamuzi waziada katika gari la Azam tv la kurusha matangazo na endapo kutatokea utata wa naama yoyote hile basi mwamuzi aliyekuwepo katika gari ya matangazo amsaidie mwamuzi wa kati kufanya maamuzi yaliosahihi .

Lakini hadi sasa bado kumekuwa na matukio yenye utata katika michezo mingi ya ligi kuu inayoendelea na kupelekea kuumiza timu nyingine ,na ukizingatia timu zimewekeza nguvu ,pesa n.k katika mchezo husika halafu mwisho wa siku wanakutana na mambo yasio rafiki kwako katika mchezo kama viashiria vya uonevu.


 
Tatizo ni Jicho lako halina maamuzi wala filimbi. Linabaki kuwa jicho tu.
 
Jicho langu:Tabora walinyimwa goli halali kama la Aziz Ki
Klabu ya Tabora united katika mchezo wa jana walinyimwa goli la halali katika mchezo wao waligi kuu ya NBCPL waliocheza na Simba katika Dimba la Azam Complex Chamazi na Simba kuibuka kwa ushindi wa magoli mawili.
Lile ni goal la wazi kabisa. Kuna haja ya ku include var kweny vpl tz
 
Hilo jicho ungetumia kwemye maisha yako kuondoa umaskin ungekua mbal sana
 
Siku Simba ikishuka daraja soka letu bongo litapaa na labda Taifa Stars inaweza kucheza World Cup! Hawa Simba ndio vivuruge wa ligi yetu kwa hisani ya Mr Karai kule TFF ,jopo lake na marefa wake wa mchongo!! Kila mechi ya simba ni magumashi tu!! Inaboa sana!!

Yanga na Azam tu ndio kiboko ya makolo, timu zingine zikicheza na simba ni full kuonewa , magoli yao yanakataliwa, wachezaji wao wanakula red cards na Simba wanafunga magoli ya offside na penati za mchongo, mara Simba wasukume na kufunga ilimradi tafrani tupu simba ikicheza, sijui marefa wana kitu gani na simba hii mbovu.

Ila tunachojua simba ni fungu la kukosa msimu huu na hata wafanye nini Azam chama la wanangu litachukua nafasi ya pili na kwenda CAF champions league, uto og niko paleeee!! Msijesema hatukuwaambia!!
 
Siku Simba ikishuka daraja soka letu bongo litapaa na labda Taifa Stars inaweza kucheza World Cup! Hawa Simba ndio vivuruge wa ligi yetu kwa hisani ya Mr Karai kule TFF ,jopo lake na marefa wake wa mchongo!! Kila mechi ya simba ni magumashi tu!! Inaboa sana!!

Yanga na Azam tu ndio kiboko ya makolo, timu zingine zikicheza na simba ni full kuonewa , magoli yao yanakataliwa, wachezaji wao wanakula red cards na Simba wanafunga magoli ya offside na penati za mchongo, mara Simba wasukume na kufunga ilimradi tafrani tupu simba ikicheza, sijui marefa wana kitu gani na simba hii mbovu.

Ila tunachojua simba ni fungu la kukosa msimu huu na hata wafanye nini Azam chama la wanangu litachukua nafasi ya pili na kwenda CAF champions league, uto og niko paleeee!! Msijesema hatukuwaambia!!
Ulichoandika kama kinawahusu Yanga hasa hapo kwenye kubebwa tuanzie na ile ya Kagera Sugar
 
Ulichoandika kama kinawahusu Yanga hasa hapo kwenye kubebwa tuanzie na ile ya Kagera Sugar
Angalia mwanzo mwisho bila ushabiki marudio ya mechi nne za Simba vs Coastal Union, Singida big stars, Azam na Tabora United kisha urudi hapa na useme ulichokiona. Full mbeleko!!

Yanga inashinda kwa uwezo ndio maana nyie makolo mmetupatia points 6 na goli one week!!

Na Kibu tunambeba mzima mzima aje kubeba makombe na kuachana na timu inayokabia macho na kushinda kwa magumashi
 
Back
Top Bottom