Je unajua faida ya kutoa sadaka?

ARGAN MARA

JF-Expert Member
Aug 2, 2016
955
2,555
Laiti mtoa sadaka angejua kwa yakini kwamba sadaka yake inapitia kwenye (mkono) wa Mwenyezi Mungu kabla ya kuingia mkononi mwa masikini, ingekuwa ladha ya mtoaji.. ni kubwa kuliko ladha ya mpokeaji..
-ibn alqayyim

Je unajua faida ya kutoa sadaka?
Sikilizeni enyi watoa sadaka, nyinyi na ambao wanasaidia kufikisha sadaka..

1- Sadaka ni mlango miongoni mwa milango ya pepo

2-Sadaka ni bora ya matendo mema, na sadaka bora ni kulisha chakula

3- Sadaka inamfunika kivuli mtoaji na inamuondosha kwenye moto

4-Sadaka inazima ghadhabu za Mola na joto la kaburi

5- Sadaka ni jambo bora la kumzawadia maiti na inamfaa zaidi, na Mola anaitunza

6-Sadaka ni usafisho, na utakaso wa nafsi na huongeza mema

7- Sadaka ni sababu ya furaha kwa mtoa, na ni sababu ya kung'ara uso wake siku ya kiama

8- Sadaka inaleta amani kutokana na hofu siku ya fazaa kubwa, na humfanya mtoa sadaka asipatwe na huzuni

9- Sadaka ni sababu ya kughufiriwa dhambi na kusamehewa makosa

10- Sadaka ni miongoni mwa bishara za mwisho mwema na sababu ya dua ya Malaika

11- Mtoa sadaka ni mbora wa watu, na sadaka thawabu zake ni kwa kila aliyeshiriki

12- Mwenye kutoa sadaka ameahidiwa kheri nyingi na ujira mkubwa

13- Kutoa ni miongoni mwa sifa za wacha Mungu, na sadaka ni sababu ya mapenzi ya waja wa Mola kwa mtoa sadaka

14- Sadaka ni ishara miongoni mwa ishara za ukarimu na alama miongoni mwa alama za ukarimu na wema

15- Sadaka ni sababu ya kukubaliwa dua na kuondoshewa matatizo

16- Sadaka inaondoa balaa na inaziba milango sabini ya mabaya ya dunia

17- Sadaka inazidisha umri na mali, na ni sababu ya riziki na nusra

18- Sadaka ni ponya, dawa, na shifaa

19- Sadaka inazuia moto, gharika, wizi, na inazuia kifo kibaya

20- Sadaka ujira wake ni ule ule japo ukitoa kwa wanyama au ndege..

Na sadaka bora ni ile unayoifanya sasa.. ni kueneza maneno haya kwa nia ya sadaka kwani kila anayetekeleza maneno haya na akawafundisha wanaokuja, basi ujira wake uko kwa Mola wake kwa idhini yake

Allah atutangulie sote ktk
Hili tuwe wenye kutoa
Kwa ajili ya Allah
(Ammyn)
 

Attachments

  • 1715141874716.jpg
    1715141874716.jpg
    119.4 KB · Views: 1
Oohhhh yes.... Ooohhh hallelujah....

Siku nikiona hizi sadaka zinapaa basi ntaamini, ila kama zinashuka kwenye matumbo ya watu na kwenda chooni (kuzimu) hapanaaaaaa
 
Unazungumzia sadaka kwa mtazamo wa imani ya kiislamu? Utaeleweka kwa waislam wanaoamini dini na imani hiyo
 
Back
Top Bottom