Jifunze kuilinda sadaka yako kama Abram alivyozilinda zake

matunduizi

JF-Expert Member
Aug 20, 2018
6,718
15,696
Mwanzo 15, Ibrahim alielekezwa na Mungu atoe sadaka ili apate kuhakikishiwa hatma ya maisha yake.

Aliziandaa akazilinda hadi jioni tai na mbwa mwitu wasije wakazitafuna. Alifanikiwa hadi jioni mpaka zilipoleta matokeo.

Watu wengi hawanufaiki na sadaka zao kwa sababu hawazilindi. Wanatoa kama wanazitupa tu.

JINSI YA KUZILINDA SADAKA ZAKO.
1: Usitoe sadaka kisha ukaondoka. Jifunze kulinda kwa kuzitamkia maneno ambayo unataka Mungu akufanyie. Hata kama unampa ombaomba mtaani, kabla hujatoa tamka.

2: Usitoe mahala unapopatilia mashaka. Usitoe kwa mtumishi unayemtilia shaka au unauhakika atazifuja na Mungu ameshakuonyesha. Toa mahala ambapo moyo wako hauna tashwishwi. Mungu hampendi mtu mwenye mashaka na wasiwasi.

3: Usitoe kwa kulazimishwa. Kanisani hakuna michango. Kila kitu ni sadaka. Ukitoa kwa lazima uhakikishe ni matokeo ya maamuzi yako sio manipulation au janjajanja ya mtozaji au vitisho au shuruti. Hutabarikiwa.

4: Kubwa kuliko yote, baada ya kutoa, baki ukiwa unaendelea kujitamkia maneno chanya ukiendeleza yale uliyotamka wakati unatoa. Ukijikuta unalaumu au unalalamikia ulichotoa unajiletea laana. Endelea kuwa chanya na sadaka yako hadi kusudi ya kulitoa litakapotimia.

Ni hayo tu.
Kama umeelewa, sema amina.
 
Amin
Uzi kama huu nashangaa kuona why hakuna comments nyingi nakati ni jambo ambalo lina manufaa kwetu wenyewe
 
Mwanzo 15, Ibrahim alielekezwa na Mungu atoe sadaka ili apate kuhakikishiwa hatma ya maisha yake.

Aliziandaa akazilinda hadi jioni tai na mbwa mwitu wasije wakazitafuna. Alifanikiwa hadi jioni mpaka zilipoleta matokeo.

Watu wengi hawanufaiki na sadaka zao kwa sababu hawazilindi. Wanatoa kama wanazitupa tu.

JINSI YA KUZILINDA SADAKA ZAKO.
1: Usitoe sadaka kisha ukaondoka. Jifunze kulinda kwa kuzitamkia maneno ambayo unataka Mungu akufanyie. Hata kama unampa ombaomba mtaani, kabla hujatoa tamka.

2: Usitoe mahala unapopatilia mashaka. Usitoe kwa mtumishi unayemtilia shaka au unauhakika atazifuja na Mungu ameshakuonyesha. Toa mahala ambapo moyo wako hauna tashwishwi. Mungu hampendi mtu mwenye mashaka na wasiwasi.

3: Usitoe kwa kulazimishwa. Kanisani hakuna michango. Kila kitu ni sadaka. Ukitoa kwa lazima uhakikishe ni matokeo ya maamuzi yako sio manipulation au janjajanja ya mtozaji au vitisho au shuruti. Hutabarikiwa.

4: Kubwa kuliko yote, baada ya kutoa, baki ukiwa unaendelea kujitamkia maneno chanya ukiendeleza yale uliyotamka wakati unatoa. Ukijikuta unalaumu au unalalamikia ulichotoa unajiletea laana. Endelea kuwa chanya na sadaka yako hadi kusudi ya kulitoa litakapotimia.

Ni hayo tu.
Kama umeelewa, sema amina.

sadaka utoayo isaidie ulinzi wa kulinda na kuchunga watoto wako na uzao wako wote na hayo ndio matunda ya sadaka njema.
 
Usimwamini kirahisi, hizo alizozitaja siyo mbinu za kulinda sadaka bali ni mbinu za kusaka sadaka.
Yeye amuamini Mungu sio mimi.
Sadaka utatoa tu, kama sio kanisani utatoa kwa mganga, utatoa kwa wazazi, utatoa kama ada kwa mifumo ambayo hujui unachotoa ni sadaka.

Kila mtu anatoa sadaka kwa kutaka au kinyumenyume.
Ila sadaka ya maana ni ile ambayo inakufanya kuwa na financial connection na Mungu mmiliki sio wa kila kitu tu bali hata pumzi isiyonunulika.
 
Back
Top Bottom