Ipi kampuni nzuri ya kuagiza gari kutoka nje kati ya SBT na Befoward?

mkuu mpaka muda huu najua ulishaagiza gari, tupe basi mmrejesho na sisi wengine tufaidike

Kweli mkuu, niliagiza gari last year na Beforward moja kwa moja kutoka Japan kupitia simu yangu ya Mkononi. Gari ilifika miezi miwili baada ya kuagiza ikiwa katika ubora ule ule kama niliouona kwenye picha. Beforward walinipa nafasi ya kubargain nao bei ya gari na walifanikiwa kunipunguzia USD 450 kutoka bei ambayo walikuwa wameiweka kwenye website Yao.

Kila kitu cha kwenye gari nilikikuta kama kilivyo hakukuwa na wizi wala upotevu wa kitu chochote. Gari niko nayo takribani miezi 6 sasa na wala hakuna tatizo lolote service pekee niliyofanya ni kumwaga oil sijawahi kubadilisha chochote kwenye gari. Narecommend Beforward kuwa ndo kampuni bora kabisa ya uagizaji wa magari kutoka Japan kwa kigezo cha ubora wa magari, uaminifu, huduma bora kwa wateja na nafasi ya kubargain bei ya gari.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwani kuna kampuni isiyoruhusu kubagain? Gari zote huku Japan hununuliwa sawa kwenye minada
Gari yako kutumia bila kupata tatizo sio general rule ya gari zao zote ni nzima.

Uzima wa gari utategemea na bei ulionunulia maana wakati wananunua na wao huwa katika bei tofauti tofauti kulingana na grade kuna 4.5,4,3.5,3 na R.

Nawashauri nunua popote Ila angalia bei unayonunua isiwe chini sana maana utapata low grade, ndio maana kwenye web page za magari, gari aina moja za mwaka mmoja zinaweza kuwa na bei tofauti.

Pia usipende nunua very low mileage car with low price nyingi huwa ni grade R (means repaired) unakuta liligongwa likafanyiwa big repair ndio maana unakuta lipo mileage chini ya 50k lakini linabei ndogo ukilinganisha na yalio juu ya 100k wakati ni aina moja. Mtanzanyika,

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Utingo,
Ebu soma comments za wateja walilofanya biashara na tradecarview utaona jinsi wanavyolalamika kuhusu ubovu wa Magari yao,be forward wako juu zaidi pia hao tradecarview Magari yao wanauza bei ya juu Sana hata kama utafanya negotiation bado watakupiga Tu.

Ukitembelea site Yao utaona Magari ya mwaka Jana Hadi leo bado yapo Tu nahisi uuzaji wao bado ni mdogo mno ukilinganisha na SBT na be forward,ni Bora kufanya biashara na cardealpage, enhancement na autorec kuliko hao jamaa
 
Ebu soma comments za wateja walilofanya biashara na tradecarview utaona jinsi wanavyolalamika kuhusu ubovu wa Magari yao,be forward wako juu zaidi pia hao tradecarview Magari yao wanauza bei ya juu Sana hata kama utafanya negotiation bado watakupiga Tu...
Unaelewa trade car view inavyofanya biashara au unailinganisha na hao wengine bila kujua model of their business?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Unaelewa trade car view inavyofanya biashara au unailinganisha na hao wengine bila kujua model of their business?

Sent using Jamii Forums mobile app
Sikuhizi be forward wamefungua Duka la spare parts pale Kariakoo yaani Kwa spare ya gari yeyote Ile utaweza kuagizia kupitia ofisini kwao na utaipata baada ya siku 30.

Hawa jamaa wapo mpaka Kwenye simu, TV,radio, computer na mashine mbalimbali sidhani Kwa Tanzania kuna kampuni ambayo most trusted kama be forward
 
Ebu soma comments za wateja walilofanya biashara na tradecarview utaona jinsi wanavyolalamika kuhusu ubovu wa Magari yao,be forward wako juu zaidi pia hao tradecarview Magari yao wanauza bei ya juu Sana hata kama utafanya negotiation bado watakupiga Tu...

Siyo kweli mkuu. Mimi nimenunua magari mawili sasa tradecarview si mabovu kama unavyosema na sikupata usumbufu wowote pengine ulichagua accident not repaired car.

Kiti kingine pengine usichojua tradecarview ni link ya wauzaji magari wengi sana pengine wote walioko japani isipokuwa beforward kwa sababu beforward hawataki kumeet standard biashara. Kwa mfano tradecar view deal likiharin=bika unarudishiwa pesa, befowrd mpaka wakurudishie mtiti wake si wa kawaida.

Kwa bei makampuni yanayoongoza kwa bei ya juu ni vwest, car junction, japanese vehicles, sbt pia magari yao yako juu na mileage ya magari yao inatisha, everycar etc...si tradecarview.

shida kubwa ya beforward ni kukosa window for negotiation. Bei wakishaiweka hawapunguzi, hata realmotor wako hivyo.
 
Utingo,
Siwezi kubisha Mkuu Kwa kile ulichosema Ila kuhusu kupunguza bei Kwa be forward wanafanya mwaka Jana mwezi wa 11 nilienda na ndugu Yangu kumnunulia Toyota pro box success na tulipunguziwa 316000/=.

Kwa Mtu kama Mimi ambae sio mzoefu wa kuagiza gari mwenyewe niliona njia sahihi ni kupitia be forward kuliko kuwatumia agencies wa hapa bongo,kama tradecarview wangekuwa na ofisi hapa dar ingekuwa rahisi kutofautisha ubora
 
Ukiagiza gari kupitia makampuni haya, huchukua siku ngapi gari kukufikia?

Sent using Jamii Forums mobile app
Ninauzoefu na beforwad...inachukua mwezi na wiki tatu mpaka miezi miwili gari linakuwa limeshafika bandarini....

Wiki tatu mpaka nne za mwanzo ukishalipia gari, wanatumia muda huo kusubiria meli ijae mizigo na taratibu nyinginezo...

Wiki nne za mwisho ni safari ya meli kutoka Japan mpaka itie nanga bandarini kwetu....inatumia wiki nne kusafiri

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ninauzoefu na beforwad...inachukua mwezi na wiki tatu mpaka miezi miwili gari linakuwa limeshafika bandarini...
Ikishafika inatumia muda gani kulipata mkononi kama ushalipia kila kitu na bima ya gari inatakiwa kuwekwa baada ya muda gani ukishalipokea
 
Ikishafika inatumia muda gani kulipata mkononi kama ushalipia kila kitu na bima ya gari inatakiwa kuwekwa baada ya muda gani ukishalipokea
Hapo inategemea na wewe mwenyewe unachangamka kiasi gani...

Meli ikishaondoka Japan, wanakujuza...zikiisha wiki mbili beforward wanakutumia documents zote za gari kutoka huko Japan kwa kupia DHL au shirika lingine watakalopenda wao.

Ukishapokea hizo docs inakuwa zimebaki wiki mbili meli ifike Dar...hizo wiki mbili ndiyo unazitumia kuchakarika kulipia kodi zote stahiki huko TRA ili meli ikifika unakuwa umeshakamilisha malipo yako karibu yote..

Meli ikifika inatakiwa utoe gari ndani ya siku saba, zaidi ya hapo utakuwa unatozwa gharama ya gari kukaa bandarini kila siku...(penalty after grace period).

Mara nyingi ukiwa umeshakamilisha malipo ndani ya zile wiki mbili kabla ya meli kuwasili, Meli ikifika tu unaweza kulipata gari lako ndani ya siku mbli mpaka nne at most.

Kuhusu bima, ukishafanya registration ya gari TRA na kupewa plate number na kadi, hapo unaweza kwenda na kadi ya gari kulipia bima...coz gari likishakubaliwa kutoka bandarini ina maana limekamilika usajili wake....na polisi wana haki ya kukupiga faini kama huna bima..

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Boeing 747,
Thanks mkuu, nishalipia kila kitu ndo nalisubiri waliniambia linafika jana tareh 29 but nahisi kutokana ni weekend hawajanijulisha
 
Kweli mkuu..... niliagiza gari last year na Beforward moja kwa moja kutoka Japan kupitia simu yangu ya Mkononi. Gari ilifika miezi miwili baada ya kuagiza ikiwa katika ubora ule ule kama niliouona kwenye picha..... Beforward walinipa nafasi ya kubargain nao bei ya gari na walifanikiwa kunipunguzia USD 450 kutoka bei ambayo walikuwa wameiweka kwenye website Yao...
Nmekuelewa sana mwamba.. nakuja pm

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom