NADHARIA I.Q ya mtoto aliyezaliwa na binti mwenye umri mdogo ni kubwa kuliko ya mtoto aliyezaliwa na mwanamama mwenye umri mkubwa

Taarifa hii ni nadharia tu, tumeitolea ufafanuzi kwa kadiri ilivyowezekana
Kitaalam imekaa vipi?

1563804682-cover-image-l.jpg
 
Tunachokijua
IQ ni ufupisho wa maneno Intelligent Quotient, kwa tafsiri isiyo sahihi sana kwa Kiswahili tunaweza kuita kipimo cha akili ambacho hupatikana baada ya kufanyika kwa majaribio maalum.

Majaribio haya hulenga kupima mambo mbalimbali ikiwemo lugha, uwezo wa kufikiri, utunzaji wa kumbukumbu, kufanya hesabu pamoja na uwezo wa kutatua changamoto mbalimbali za Maisha ya kila siku.

Baadhi ya watu waliowahi kuthibitishwa kuwa na IQ kubwa
Mtaalam wa hisabati, Terence Tao anatajwa kuwa na IQ inayokadiriwa kufikia 220-230. Alianza Shule ya Msingi miaka ya 1980 akiwa na umri wa miaka 7, alipata shahada ya kwanza akiwa na umri wa miaka 16 na na Shahada ya uzamivu akiwa na umri wa miaka 21.

Mwaka 2017, Jarida la Indian Times lilichapisha makala inayomtaja binti wa miaka 11 anayeishi Uingereza kuwa na IQ ya 162. Pia, chapisho hilo lilibainisha kuwa Wanasayansi Albert Einstein na Steven Hawking wanadhaniwa kuwa na IQ inayofikia 160.

Vitu vinavyochangia uwezo wa IQ
Kiasi cha IQ ya binadamu huathiriwa na mambo mbalimbali ikiwemo;
  • Lishe
  • Hali ya afya ya Mhusika
  • Mfumo wa Elimu
  • Utamaduni na mazingira
Uhusiano wa umri wa mama na IQ ya mtoto
Kwa mujibu wa utafiti uliofanyika kwa miaka 40 unabainisha kuwa mabadiliko mbalimbali yanayotokea duniani yamefanya takwimu za IQ zinazohusianishwa na umri wa mama zibadilike pia. Mathalani, kati ya mwaka 1958-1970, watoto waliozaliwa na wanawake wenye umri wa kati ya miaka 25-29 walikuwa na IQ kubwa zaidi kuliko watoto waliozaliwa na wanawake wenye umri wa miaka 35-39.

Takwimu za utafiti huu zinaonesha kuwa, kuanzia mwaka 2001, watoto waliozaliwa na wanawake wenye umri wa miaka 35-39 au hata zaidi ya hapo walionekana kuwa na IQ kubwa kuliko wale waliozaliwa na wanawake wenye umri wa miaka 25-29.

JamiiForums imefanya marejeo ya tafiti mbalimbali, taarifa za kisayansi na maelezo ya wataalam wa afya na kubaini kuwa;
  1. IQ ya mtu huchangiwa na mambo mengi, hasa yale yanayoathiri makuzi ya mtoto kama vile mazingira, tamaduni, elimu anayopatiwa pamoja na mfumo mzima wa maisha ya kila siku.
  2. Kwa uchache wake, tafiti za sasa zinadai kuwa wanawake wenye umri mkubwa, walau kuanzia miaka 35-40 huwa na uwezekano mkubwa zaidi wa kupata mtoto mwenye IQ kubwa kuliko wale wenye umri chini ya hapo.
  3. Watu wenye IQ kubwa huwa pia na uwezo mkubwa wa kufikiri na kutatua kwa haraka changamoto mbalimbali zinazowakabili.
Hata hivyo, kiasi cha IQ anachokuwa nacho mhusika hakiwezi kutumika kutabiri au kupima mafanikio kwenye maisha. Unaweza kuwa na IQ kubwa lakini ukapata mafanikio madogo na kinyume chake pia ni sawa.

Hivyo, Kutokana na uwepo wa taarifa kinzani zinazohusianisha umri wa mama na ukubwa wa IQ ya mtoto, JamiiForums inachukulia hoja hii kama nadharia inayopaswa kufanyiwa uchunguzi zaidi ili kubaini ukweli wake.
IQ tunaangalia hasa Umri wa mtoto na matendo yake je yanaendana na umri wake ikiwa kuna utofauti hapo ndio unaweza kujua IQ ya mtoto ni katika kundi lipi kulingana na % ambazo zinapatikana

IQ= umri wa matendo ya mtoto/umri wa mtoto x 100%
(IQ= MA/CA x 100%)

Sio kila mtoto ni genius wengine ni gifted and talented

 
Nakumbuka mama mmoja alipata kunambia

"watoto wenye nguvu huzaliwa na vijana"

Hapo nakumbuka ndo nilikuwa nimeoa, sasa huyu mama akawa ananisisitiza kufyatua watoto mapema wakati bado ningali kijana.
 
5 Reactions
Reply
Back
Top Bottom