Huyu mbwa vipi? Anaumwa au amezeeka?

Ricky Blair

JF-Expert Member
Mar 13, 2023
391
876
Uyu mbwa vp? Ni kwa anaumwa au ndo kazeeka? Coz namuonea huruma sana na km ana vidonda mwili mzima. N

atamani hata ningemchoma sindano ya euthanasia tu apumzike coz anaona anateseka sana hata kutembea kwa shida sasa na iyo ngozi ndo kabisa.

IMG_0387.jpeg
IMG_0386.jpeg
 
Sasa mbwa upo naye hapo si umuulize mwenyewe ana changamoto gani?

Unamuonea huruma huku unataka kumuua? Kwa nini usingesema natamani hata nimpeleke kwenye sehemu za kutoa huduma za wanyama akahudumiwe na kulishaa kwa gharama zako?

Huruma ya kuua? Huo ni UKATILI.

Bora asiyemjali. Kuliko wewe unayedai kumuonea huruma huku unataka kumdedisha.
 
Sasa mbwa upo naye hapo si umuulize mwenyewe ana changamoto gani?

Unamuonea huruma huku unataka kumuua? Kwa nini usingesema natamani hata nimpeleke kwenye sehemu za kutoa huduma za wanyama akahudumiwe na kulishaa kwa gharama zako?

Huruma ya kuua? Huo ni UKATILI.

Bora asiyemjali. Kuliko wewe unayedai kumuonea huruma huku unataka kumdedisha.
Hapana sio ukatili. Kuna wakati hiyo ndio njia pekee ya kumpunguzia mateso na maumivu anayopitia. Kama umewahi kuwa mfugaji wa mbwa utaelewa. Kuna magonjwa ambayo akiyapata mbwa kupona ni ngumu ni lazima afe na kama unampenda mbwa wako kitaalamu inashauriwa kumpumzisha kuliko kuacha ateseke.
Huyo mbwa anakaa kama vile amepata cancer ya ngozi.
 
Hapana sio ukatili. Kuna wakati hiyo ndio njia pekee ya kumpunguzia mateso na maumivu anayopitia. Kama umewahi kuwa mfugaji wa mbwa utaelewa. Kuna magonjwa ambayo akiyapata mbwa kupona ni ngumu ni lazima afe na kama unampenda mbwa wako kitaalamu inashauriwa kumpumzisha kuliko kuacha ateseke.
Huyo mbwa anakaa kama vile amepata cancer ya ngozi.
Kwanza, Euthanasia ni hatua ya mwisho kabisa baada ya matibabu mengine kugonga mwamba. Yaani mbwa ashatibiwa na daktari wa wanyama kushauri kuwa huyu hawezi tena kupona kwa namna yeyote.

Sasa yeye si mmiliki wa mbwa. Wala hajafanya jitihada zozote hata za kumsaidia apate matibabu na chakula. Sasa kwa nini aone njia ya kumsaidia ni kumuua?

Huyo mbwa pengine amekosa chakula tu ama amekula sumu. Anahitaji matibabu kidogo. Sioni dalili za kansa hapo. Unless otherwise, wewe ni mtaalam zaidi.

Nakubaliana nawe kuwa Euthanasia ni njia sahihi lakini hata wanaoshauri hivyo wanasema ni maamuzi magumu mno. Na taratibu za kufanya hivyo zinafanywa na daktari wa mifugo, si mtu baki tu. Na yeye hushauri hivyo baada tu ya kuona HAKUNA njia nyingine yeyote iliyobakia ya kuweza kumuokoa.

Mkuu mtoa mada kama kweli anamhurumia huyo mbwa, ampeleke kwenye matibabu.
 
Mpeleke katika matibabu ,daktari ndo atatoa suluhisho .

Kufunga mnyama ni Kama binadamu unabidi kumuwekea mazingira bora kuanzia chakula
Sehemu ya kulala
Na kufatilia AFYA yake mara kwa Mara kila baada ya muda


Kuua ,huwa ni njia za WATU ambao hawapendi kuwa responsible katika majukumu yao.

Mtafute daktari afanye kazi ya check up , and treatments.
 
Sasa yeye si mmiliki wa mbwa. Wala hajafanya jitihada zozote hata za kumsaidia apate matibabu na chakula. Sasa kwa nini aone njia ya kumsaidia ni kumuua?

Huyo mbwa pengine amekosa chakula tu ama amekula sumu. Anahitaji matibabu kidogo. Sioni dalili za kansa hapo. Unless otherwise, wewe ni mtaalam zaidi.
Baada ya kusoma mchango wako, nikaona nifuatilie zaidi
=
1714017405594.png

=
Ingekuwa katika nchi za wenzetu, hapo ni swala la kupiga simu moja tu, Gari inafika na kumchukua mbwa na kupelekwa kwenye kituo maalumu kwa matibabu na kutunza, Mfano video hizi mbili.


View: https://www.youtube.com/watch?v=oKSN-q9okGA


View: https://youtu.be/gKpQanid194
 
Wewe ungepata vidonda ungekubali kuchomwa sindano na wanaokuonea huruma ili ufe?

Kama unamuonea huruma sana mpeleke kwa vet akatibiwe.

Pia kuwa makini si kila anaonekana mnyama wa mtaani ni mnyama wengine watu wapo kwenye mingo zao. Unajitia kimbelembele kumuua unashangaa mama muuza vitumbua anaangua kilio mumewe kafa.
 
Hapana sio ukatili. Kuna wakati hiyo ndio njia pekee ya kumpunguzia mateso na maumivu anayopitia. Kama umewahi kuwa mfugaji wa mbwa utaelewa. Kuna magonjwa ambayo akiyapata mbwa kupona ni ngumu ni lazima afe na kama unampenda mbwa wako kitaalamu inashauriwa kumpumzisha kuliko kuacha ateseke.
Huyo mbwa anakaa kama vile amepata cancer ya ngozi.
Nani alikufundisha huo uhuni?Unaweza kuumba hata manyoya tu?Huna haki wala sababu ya kuua usichoweza kukiumba na hakijakukosea chochote.
 
Kwanza, Euthanasia ni hatua ya mwisho kabisa baada ya matibabu mengine kugonga mwamba. Yaani mbwa ashatibiwa na daktari wa wanyama kushauri kuwa huyu hawezi tena kupona kwa namna yeyote.

Sasa yeye si mmiliki wa mbwa. Wala hajafanya jitihada zozote hata za kumsaidia apate matibabu na chakula. Sasa kwa nini aone njia ya kumsaidia ni kumuua?

Huyo mbwa pengine amekosa chakula tu ama amekula sumu. Anahitaji matibabu kidogo. Sioni dalili za kansa hapo. Unless otherwise, wewe ni mtaalam zaidi.

Nakubaliana nawe kuwa Euthanasia ni njia sahihi lakini hata wanaoshauri hivyo wanasema ni maamuzi magumu mno. Na taratibu za kufanya hivyo zinafanywa na daktari wa mifugo, si mtu baki tu. Na yeye hushauri hivyo baada tu ya kuona HAKUNA njia nyingine yeyote iliyobakia ya kuweza kumuokoa.

Mkuu mtoa mada kama kweli anamhurumia huyo mbwa, ampeleke kwenye matibabu.
Yeah upo sahihi , kumpumzisha ni hatua ya mwisho baada ya kuona hali haitokuwa sawa baada ya uchunguzi wa kitaalam.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom