Hii ndio maana ya ndugu lawama

Ukiwa alosto huna mia ya kutu wanakukwepa. Kipindi kile cha kujitafuta ukiwapiga kirungu cha buku ya nauli au bundle ili uweze kufanya mawasiliano wanakupa majibu ya kilokole.

Utasikia asiefanya kazi na asile. Au, wewe una mikono miwili na miguu miwili na macho mawili unaomba walemavu wafanyaje. Hapo umeomba haujamfosi. Na bado ataenda kukupiga majungu kwa ndugu wengine na pamoja watakuchukulia poa sana mixer dharau za wazi wazi. Utatumwa hadi mafuta ya kupikia dukani ili mradi wakuonyeshe wewe hauna maana sasa kwenye familia.

Unakubaliana na hali maana kama Yesu mwana wa MUNGU aliteswa na wanadamu sembuse mimi. Unapiga moyo konde unasema ngoja ufosi kupambana na mitaa na walimwengu kuliko kupambana na ndugu ambao wamekuonyesha kuwa kumbe si muda wote damu ni nzito kuliko maji.

Unaenda kwa wanao mtaani unawapa ya moyoni na kutubu sana. Wana wanaingia na huruma wanakushika mkono na hizo hizo buku buku za mawazo mixer kuingia madeni kwa niaba yako.

Unajikaza unaweka mitego sawa, uhakika wa elfu 10,30,50 80 na hata laki kwa wiki na mwezi unakuwepo. Unalipa madeni unajiimarisha kiuchumi. Muda wa shukrani nawatafuta wanangu maana siwezi watupa maana ndio walinishika mkono gizani. Tunakula kitimoto pamoja na hata kusaidiana shida ndogo ndogo bila husuda.

Ndugu wanaona post, simu zao zinapigwa wanasema unajiweka mbali na familia siku hizi. Umepata mafanikio unakula na marafiki siku ukianguka hao hawatakubeba wala kukuuguza ni sisi ndugu zako wa damu.

Hapo ndipo unajua si muda wote damu ni nzito kuliko maji. Unaamua kupiga kimya tu sms za kikuda kama hizo haujibu unaamua kuwa outcast maana sometimes familia ndizo chanzo cha watu kukosa uelekeo badala kuwa chanzo cha uelekeo.

Haya maisha haya.
umepiga mlemle kabisa
 
Ndugu wa nyokooo.......

Hawana wanangu niliokutana kutana Kwenye harakati na kusapotiana Kwa Kila Hali mm km mm ndio nawaonaga ndugu zangu maana daaaa aiseé hatujawahi angushana akitokea yyt kt yetu anazinguaaa tunaweka chini tunabonga tunasongeshaa ..
Ila ma bro na ma sister na ma anko wengi wao n wanafiki haswaaaa...
Kipindi hicho unalianza life la kukaa mwenyewe chumba kimoja. Umechacha mfukoni unampigia simu bi mkubwa akutupie hata 50K uweke mambo sawa maana uchumi umekaa tenge, unashangaa sijui walijuaje kuwa ulimuomba bi mkubwa mzigo wanakusagia kunguni kuwa wewe hela unapata unahonga videmu ila shida unamletea bi mkubwa yeye anatoa wapi pesa?

Wewe mwanaume pambana na Maisha yako. Dah kummke unajiuliza huyu msnge si ni ndugu yangu, yaani anajua mimi nateseka badala ya kuwa wakili wangu ndio kwanza anakuwa mpinzani wangu ananisagia kunguni maisha yanikaange vizuri.

Unaongea nao unamuuliza kwann anakuwekea kauzibe hivyo kwan ulimuomba yeye anakujibu kuwa anakusaidia ujifunze kutegemea ukomae usipende kukimbilia kuomba msaada pale unapokwama unapiga simu home badala ya kupambana utafute. Unasema haina noma.

Hapo sio kwamba bi mkubwa kachacha, hapana, na wala hashindwi kukusapoti hiyo 50K ila ni ile shida watu wenye akili za kishamba kuwa kila anachopewa fulani na mimi natakiwa kupewa pia sote ni watoto wa familia bila kujali muda huo pengine una dharula yeye analeta upuuzi wake.

Unamvutia "mwanangu wa damu" simu au kumtext kwa adabu anarespond, na fasta anakurushia muamala wa 60K yaani usipate shida hata ile ya kutolea iwepo.

Yaani unashukuru MUNGU unamuuliza "MUNGU unataka nambia ujumbe gani hapa? Iweje rafiki ajali shida zangu na kulia na mimi halafu ndugu awe snitch kwangu na kuniwekea kauzibe, kwann ulisema asimpenda ndugu yake hawezi kunipenda mimi" why huu mtihani unanipa na siwezi.

Aiseee. Ukipata siblings wanakupenda na wanakulinda wapende kuliko chochote ila ukizaliwa na mafreemason uzao m'moja kwa wazazi unaweza tamani kwenda Rita ukafute ubini yasiwe familia moja na wewe.
 
Duh sijui ndugu wa aina hyo mna watoa wapi.

Mm kwetu ni masikini. Lkn katika safari ya kusoma kwangu. Sina ninacho wadai ndugu zangu. Walinibeba walivo weza wakaja kunitua SUA mwaka wa kwanza.

Siku nilivo kamilisha usajili na kuanza kupewa boom ndo ikawa mwisho wa mbeleko wakasema sasa umekua jibebe. Na kweli ilinisaidia kujitambua nikiwa chuo. Mpaka sasa sijawai lilia mtu shida, na nikikwama nakopa kama mdau yeyote yule.

Hivyo swala la ndugu kuto wasaidia tunalikuza tu. Huenda nao wanapitia hali ngumu kama sisi ila hawajasema
Usiseme hakuna jambo kama haujalipitia. Ipo hivi, kuna kubebwa halafu kuna kuwa pamoja yaani ile sapoti ya familia ya upendo. Maisha yanapokupiga na kukuchanganya familia yako wanatakiwa kuwa bega la kuegemea na chanzo cha faraja.

Sijui kama umeshawahi kutana na familia zenye upendo mzee. Mimi nimeshakutana nazo sana. Upendo ule wa asili sio maigizo.

Kaka anakuwa kaka kweli kiasi kwamba usipomuona wiki unajiskia upweke balaa. Dada ni dada kweli akiwa mbali roho inauma lazima umpigie simu kuongea nae ajue kuwa anaendelea poa ama la.

Ukiwa na shida akasikia mama yenu anakuzungumzia anachanganyikiwa anakupigia simu muda huo huo sababu anapata yale maumivu ya mdogo wangu huko alipo anaendeleaje na anafanya chochote ili akuweke sawa. Mama akisema ana elfu hamsini dada anasema muongezee na hii laki. Na anakupigia simu akikufariji na kukupa maneno ya faraja na kukutia moyo.

Kukuachia uteseke sio namna nzuri ya kukuimarisha bali ni kukufundisha kuishi bila ukaribu na familia yako na kutowajali kama ambavyo wao hawakujali.

Mbona marafiki hawatuachi iwe kwa hali au kwa mali? Ndugu anakuharibia kwa wengine kuwa huyo asitumiwe kitu atazoea kuomba omba muache apambane ndio uanaume.

Mbona nikifanikiwa na kuwa na uwezo ghafla yale maneno ya kusema kwenye shida mtu anatakiwa kukomaa mwenyewe ndio maisha yalivyo yanageuka kuwa lawama kwamba wewe una roho mbaya haujali ndugu zako, why double standards exists.
 
Nouma sana Mkuu mwenzetu. Ila njia rahisi ni kuweka msimamo wako wazi, nilijifunza namna ya kudili na mkuda/mnafiki ni kumwambia upfront unafiki wake. Usimlee kabisa mnafiki/mkuda au mtu wa husda pia mtu asiyekuheshimu usimchekee kabisa. Kuwa mkali chapu na umalizane naye mara moja, in a hardest way possible
Mimi nimeweka akiba ya maneno, nakwenda kwa ile principle kuwa maneno huumba na mpumbavu mkalie kimya ndilo jibu lake.

Kimsingi naepusha future confrontation na shida zisizo na kichwa wala miguu.
 
We acha ninayo pitia mungu ndo ujuaye .walikula pesa zangu sana ila sasa si kitu kwao .mungu nisaidie
Ndio maana watu wengine unakuta ni mkaksi kwa ndugu zake unajiuliza jamaa nduguze walimkosea nini. Aiseee yakikukuta ndio unaelewa kwann.

Maisha yanataka utulivu sana ili kupata majibu.
 
Yaani ndugu zako wote wakulaumu wewe tu bila sababu? Nyie ndiyo huwa mnapewa fedha mnazimaliza halafu mnarudi kutaka tena. Hao ndugu zako ni wewe uliwasaidia wakafika hapo walipo? Kama hukuwasaidia kwa nini unataka wakusaidie?
Usiombe haya mambo ya kukute. Katika watoto ambao sijasumbua familia ni mimi tokea nimeanza sekondari hadi namaliza chuo sijawahi tegemea nyumbani na sio kwamba hakukuwa na uwezo basi ni ile haiba yangu ya kupenda kujipanga na kufanya vitu vyangu bila kusumbua watu.

Ila kuna zengwe huwa zinatokea unakuwa hauzijibu halafu sumu inasambaa so watu wanakuchukulia kitofauti sio kwasababu unazingua ila ni kwasababu hawakusomi tu harakati zako. Sasa tabia au muda wa kujitetea mimi huwaga sina maana naona nikijitetea leo tena kesho litazuka lingine so huwa napiga kimya wakuniwazia hovyo awaze tu haina shida.
 
Hakika wewe utakuwa na matatizo. Maelezo yako ynaonyesha wewe ni mtu mshari. Anyways kila familia inakuwaga na mtoto mmoja wa dizaini yako
Mshari kivipi mzee mbona nakunyooshea maelezo kuwa nimejiweka kando ? Mshari huwa anawatafuta wenzake na kuwasha moto, usiklemishe kuwa kama wengi wakiwa na lao moja basi ndio wapo sahihi.

Hata kwenye Bible wanakwambia wapumbavu wengi wakitofautiana na wenye hekima wachache basi upumbavu ndio unakuwa common sense. So usishike kwamba kutofautiana na ndugu wote inakufanya wewe kuwa mkorofi.

Haujawahi kusikia kitu kinaitwa Black sheep?
 
Usiseme hakuna jambo kama haujalipitia. Ipo hivi, kuna kubebwa halafu kuna kuwa pamoja yaani ile sapoti ya familia ya upendo. Maisha yanapokupiga na kukuchanganya familia yako wanatakiwa kuwa bega la kuegemea na chanzo cha faraja.

Sijui kama umeshawahi kutana na familia zenye upendo mzee. Mimi nimeshakutana nazo sana. Upendo ule wa asili sio maigizo.

Kaka anakuwa kaka kweli kiasi kwamba usipomuona wiki unajiskia upweke balaa. Dada ni dada kweli akiwa mbali roho inauma lazima umpigie simu kuongea nae ajue kuwa anaendelea poa ama la.

Ukiwa na shida akasikia mama yenu anakuzungumzia anachanganyikiwa anakupigia simu muda huo huo sababu anapata yale maumivu ya mdogo wangu huko alipo anaendeleaje na anafanya chochote ili akuweke sawa. Mama akisema ana elfu hamsini dada anasema muongezee na hii laki. Na anakupigia simu akikufariji na kukupa maneno ya faraja na kukutia moyo.

Kukuachia uteseke sio namna nzuri ya kukuimarisha bali ni kukufundisha kuishi bila ukaribu na familia yako na kutowajali kama ambavyo wao hawakujali.

Mbona marafiki hawatuachi iwe kwa hali au kwa mali? Ndugu anakuharibia kwa wengine kuwa huyo asitumiwe kitu atazoea kuomba omba muache apambane ndio uanaume.

Mbona nikifanikiwa na kuwa na uwezo ghafla yale maneno ya kusema kwenye shida mtu anatakiwa kukomaa mwenyewe ndio maisha yalivyo yanageuka kuwa lawama kwamba wewe una roho mbaya haujali ndugu zako, why double standards exists.


Kibongo bongo familia za aina hizo ni chache sana.

Ndo maana wengine tumeamua kua na zero expectations kutoka kwa ndugu, hii inasaidia kutokuwachukia pale unapoona kama hawakujali ipasavyo.
 
Ukiwa alosto huna mia ya kutu wanakukwepa. Kipindi kile cha kujitafuta ukiwapiga kirungu cha buku ya nauli au bundle ili uweze kufanya mawasiliano wanakupa majibu ya kilokole.

Utasikia asiefanya kazi na asile. Au, wewe una mikono miwili na miguu miwili na macho mawili unaomba walemavu wafanyaje. Hapo umeomba haujamfosi. Na bado ataenda kukupiga majungu kwa ndugu wengine na pamoja watakuchukulia poa sana mixer dharau za wazi wazi. Utatumwa hadi mafuta ya kupikia dukani ili mradi wakuonyeshe wewe hauna maana sasa kwenye familia.

Unakubaliana na hali maana kama Yesu mwana wa MUNGU aliteswa na wanadamu sembuse mimi. Unapiga moyo konde unasema ngoja ufosi kupambana na mitaa na walimwengu kuliko kupambana na ndugu ambao wamekuonyesha kuwa kumbe si muda wote damu ni nzito kuliko maji.

Unaenda kwa wanao mtaani unawapa ya moyoni na kutubu sana. Wana wanaingia na huruma wanakushika mkono na hizo hizo buku buku za mawazo mixer kuingia madeni kwa niaba yako.

Unajikaza unaweka mitego sawa, uhakika wa elfu 10,30,50 80 na hata laki kwa wiki na mwezi unakuwepo. Unalipa madeni unajiimarisha kiuchumi. Muda wa shukrani nawatafuta wanangu maana siwezi watupa maana ndio walinishika mkono gizani. Tunakula kitimoto pamoja na hata kusaidiana shida ndogo ndogo bila husuda.

Ndugu wanaona post, simu zao zinapigwa wanasema unajiweka mbali na familia siku hizi. Umepata mafanikio unakula na marafiki siku ukianguka hao hawatakubeba wala kukuuguza ni sisi ndugu zako wa damu.

Hapo ndipo unajua si muda wote damu ni nzito kuliko maji. Unaamua kupiga kimya tu sms za kikuda kama hizo haujibu unaamua kuwa outcast maana sometimes familia ndizo chanzo cha watu kukosa uelekeo badala kuwa chanzo cha uelekeo.

Haya maisha haya.
Kweli tupu mkuu
 
Unaonesha wewe ni mtu wa vinyongo sana. Yatazame maisha kwa upana wake utajifunza kupotezea baadhi ya mambo. Maana hata hao marafiki uliowamwagia maua si wote na mara zote wanakuwa waaminifu, wapo wengi wanafiki. Ni kuwajua binadamu na namna ya kuishi nao.
 
sio kila mtu mwenye ajira anakuwa na hela sometimes mtu anaenda kazini kila siku lakini kipato chake kinamtosheleza kula na ada ya watoto

Sasa kwq mishahara yetu hii unakuta ndugu ameomba umsaidie milioni 1 au laki tano unaipata wapi mkuu

Mfano mimi mwezi uliopita kuna watu wameniomba
1.500,000
2.200,000
3.Na kuna dogo ananiomba ni mnunulie smartphone 300,000

Mimi binafsi nina plan ya kununua kiwanja niache mipango yangu nimejinyima karibu mwaka mzima uniletee mipango yako eti nipe hela nifungue buashara

Lakini kiuhalisia roho zetu zinatuuma kushindwa kusaidia ndugu zetu


Sasa kwa mtu ambaye hafanyi kazi au ndo anajitafuta akiomba msaada akianza kuzungushwa anazani watu wanambania

Mi binafsi mkuu nakuombea ufanikiwe ili uelewe hii situation

Inafika mwisho wa mwezi hadi wajomba kijijini wanakupigia wewe uwasaidie hela ya kula huo mzigo wote utauweza? na usipo saidia ni lawama kama hizi
 
Unaonesha wewe ni mtu wa vinyongo sana. Yatazame maisha kwa upana wake utajifunza kupotezea baadhi ya mambo. Maana hata hao marafiki uliowamwagia maua si wote na mara zote wanakuwa waaminifu, wapo wengi wanafiki. Ni kuwajua binadamu na namna ya kuishi nao.
"Yatazame maisha kwa upana wake utajifunza kupotezea baadhi ya mambo" kila mtu ajali tu biashara zake maana ubinadamu kazi sana
 


Kibongo bongo familia za aina hizo ni chache sana.

Ndo maana wengine tumeamua kua na zero expectations kutoka kwa ndugu, hii inasaidia kutokuwachukia pale unapoona kama hawakujali ipasavyo.
True mzee. Familia za upendo na amani ni chache sana aisee. Kuna familia hiyo hawana kitu mzee wao akafariki, akabakia bi mkubwa na vijana wake na mabinti. Mzee alikuwa na shamba mbili na kiwanja pale kinyerezi.

Mtoto mkubwa wa kiume wakakubaliana na mama yake wauze shamba moja kwa milioni 37 then wafanye maendeleo.

Bi mkubwa alikuwa anaumwa kansa na ilishamfika hatua mbaya akaona akakae huko kijijini kwao Tanga kwa ndugu zake. So kijana akawa amebakia kama kiongozi wa familia na pesa zote mikononi mwake. Lakini kutokana na upendo na utulivu walionao sijawahi kuona wakikorofishana na ni kama wamekubaliana kuwa huyo kaka yao asimamie show zote yeye. Hizo pesa atajua atafanya nini hawajaleta makelele.

Sasa nikawaza itokee kwenye aina hii ya familia kwanza hawatakubali hizo pesa zikae kwa yoyote wasema hebu hizi akae nazo mama. Na hapo sasa ni majungu na uchawa kwa bi mkubwa ili mwenye sumu kali dhidi ya wenzake ndie atatengeneza mazingira yeye ndie azipate.

Sasa ukitazama ni zile tabia za ubinafsi na uchoyo plus roho ya kwann ndizo hufanya baadhi ya familia zisiwe na maendeleo hata kama wazazi walipambana na kuwajenga watoto wao.

Unaweza kuta wamesomeshwa na hata kuendelezwa kibiashara na wana uwezo ila sasa kukaa chini na kusema sasa tuunde umoja wa kifamilia ili tupige hatua hapo sasa ndipo utashuhudia matabia ya kibinafsi yanaonekana.

Unakuta mtu mzima ila analeta ligi za kitoto kwenye familia. Ukisema ngoja nibadilishe furniture za home nimnunulie bi mkubwa electronics mpya na kadhalika. Mtu anaumia kabisa yaani na ni mama yenu wote, utaona anaumia yaani si kitu cha kuficha anaumia. Sasa unakuwa unajiuliza huyu ni mzima kiakili kweli?

Ukinunua vitu vya ndani ukaleta home ukatafuta na beki tatu ukamuweka, na kumpa maelekezo ya bajeti ili uweke mambo sawa unakuta ndugu yako wa kike mara na yeye katoka wapi huko sijui na yeye kaleta chakula wakati kile cha home ni cha kutosha, okay sio vibaya kaleta mzigo wa ziada wa chakula. Anaanza kumletea vituko dada wa kazi. Dada amepika wali yeye anapika ugali halafu anawaambia watoto wale ugali na watoto wanapenda wali. Yaani anapika chakula wakati kingine kimeshapikwa ili iweje, halafu bi mkubwa hakemei hii kitu.

Dada ananipigia simu ananiambia haya. Napiga simu home nauliza shida nini, bi mkubwa unaona anauma uma maneno tu. Unashindwa kuelewa.
 
Back
Top Bottom