Hii ndio maana ya ndugu lawama

Zemanda

JF-Expert Member
Jan 10, 2021
6,564
13,778
Ukiwa alosto huna mia ya kutu wanakukwepa. Kipindi kile cha kujitafuta ukiwapiga kirungu cha buku ya nauli au bundle ili uweze kufanya mawasiliano wanakupa majibu ya kilokole.

Utasikia asiefanya kazi na asile. Au, wewe una mikono miwili na miguu miwili na macho mawili unaomba walemavu wafanyaje. Hapo umeomba haujamfosi. Na bado ataenda kukupiga majungu kwa ndugu wengine na pamoja watakuchukulia poa sana mixer dharau za wazi wazi. Utatumwa hadi mafuta ya kupikia dukani ili mradi wakuonyeshe wewe hauna maana sasa kwenye familia.

Unakubaliana na hali maana kama Yesu mwana wa MUNGU aliteswa na wanadamu sembuse mimi. Unapiga moyo konde unasema ngoja ufosi kupambana na mitaa na walimwengu kuliko kupambana na ndugu ambao wamekuonyesha kuwa kumbe si muda wote damu ni nzito kuliko maji.

Unaenda kwa wanao mtaani unawapa ya moyoni na kutubu sana. Wana wanaingia na huruma wanakushika mkono na hizo hizo buku buku za mawazo mixer kuingia madeni kwa niaba yako.

Unajikaza unaweka mitego sawa, uhakika wa elfu 10,30,50 80 na hata laki kwa wiki na mwezi unakuwepo. Unalipa madeni unajiimarisha kiuchumi. Muda wa shukrani nawatafuta wanangu maana siwezi watupa maana ndio walinishika mkono gizani. Tunakula kitimoto pamoja na hata kusaidiana shida ndogo ndogo bila husuda.

Ndugu wanaona post, simu zao zinapigwa wanasema unajiweka mbali na familia siku hizi. Umepata mafanikio unakula na marafiki siku ukianguka hao hawatakubeba wala kukuuguza ni sisi ndugu zako wa damu.

Hapo ndipo unajua si muda wote damu ni nzito kuliko maji. Unaamua kupiga kimya tu sms za kikuda kama hizo haujibu unaamua kuwa outcast maana sometimes familia ndizo chanzo cha watu kukosa uelekeo badala kuwa chanzo cha uelekeo.

Haya maisha haya.
 
Zemanda huwa nikona uzi wako naacha Kila kitu lazima niusome mpaka mwisho. Ni madini tupu. Mfano kwenye uzi huu umenizungumzia Mimi kabisa.
Tunapitia mengi sana. Watu wakiona tunabishana na kugombana humu wanahisi ni wakorofi kumbe muda mwingine tunapambana na maumivu yanayosababishwa na familia na wale tunaowaamini kwenye maisha.

Anyways, pole sana kwa yaliyokusibu. Mimi nimeamua kuwa outcast ziwezi ishi karibu na watu ambao wanifanya nijiulize hawa ni familia yangu au nilikuwa adopted.
 
Ndugu wa nyokooo.......

Hawana wanangu niliokutana kutana Kwenye harakati na kusapotiana Kwa Kila Hali mm km mm ndio nawaonaga ndugu zangu maana daaaa aiseé hatujawahi angushana akitokea yyt kt yetu anazinguaaa tunaweka chini tunabonga tunasongeshaa ..
Ila ma bro na ma sister na ma anko wengi wao n wanafiki haswaaaa...
 
Duh sijui ndugu wa aina hyo mna watoa wapi.

Mm kwetu ni masikini. Lkn katika safari ya kusoma kwangu. Sina ninacho wadai ndugu zangu. Walinibeba walivo weza wakaja kunitua SUA mwaka wa kwanza.

Siku nilivo kamilisha usajili na kuanza kupewa boom ndo ikawa mwisho wa mbeleko wakasema sasa umekua jibebe. Na kweli ilinisaidia kujitambua nikiwa chuo. Mpaka sasa sijawai lilia mtu shida, na nikikwama nakopa kama mdau yeyote yule.

Hivyo swala la ndugu kuto wasaidia tunalikuza tu. Huenda nao wanapitia hali ngumu kama sisi ila hawajasema
 
Nouma sana Mkuu mwenzetu. Ila njia rahisi ni kuweka msimamo wako wazi, nilijifunza namna ya kudili na mkuda/mnafiki ni kumwambia upfront unafiki wake. Usimlee kabisa mnafiki/mkuda au mtu wa husda pia mtu asiyekuheshimu usimchekee kabisa. Kuwa mkali chapu na umalizane naye mara moja, in a hardest way possible
 
Ukiwa alosto huna mia ya kutu wanakukwepa. Kipindi kile cha kujitafuta ukiwapiga kirungu cha buku ya nauli au bundle ili uweze kufanya mawasiliano wanakupa majibu ya kilokole.

Utasikia asiefanya kazi na asile. Au, wewe una mikono miwili na miguu miwili na macho mawili unaomba walemavu wafanyaje. Hapo umeomba haujamfosi. Na bado ataenda kukupiga majungu kwa ndugu wengine na pamoja watakuchukulia poa sana mixer dharau za wazi wazi. Utatumwa hadi mafuta ya kupikia dukani ili mradi wakuonyeshe wewe hauna maana sasa kwenye familia.

Unakubaliana na hali maana kama Yesu mwana wa MUNGU aliteswa na wanadamu sembuse mimi. Unapiga moyo konde unasema ngoja ufosi kupambana na mitaa na walimwengu kuliko kupambana na ndugu ambao wamekuonyesha kuwa kumbe si muda wote damu ni nzito kuliko maji.

Unaenda kwa wanao mtaani unawapa ya moyoni na kutubu sana. Wana wanaingia na huruma wanakushika mkono na hizo hizo buku buku za mawazo mixer kuingia madeni kwa niaba yako.

Unajikaza unaweka mitego sawa, uhakika wa elfu 10,30,50 80 na hata laki kwa wiki na mwezi unakuwepo. Unalipa madeni unajiimarisha kiuchumi. Muda wa shukrani nawatafuta wanangu maana siwezi watupa maana ndio walinishika mkono gizani. Tunakula kitimoto pamoja na hata kusaidiana shida ndogo ndogo bila husuda.

Ndugu wanaona post, simu zao zinapigwa wanasema unajiweka mbali na familia siku hizi. Umepata mafanikio unakula na marafiki siku ukianguka hao hawatakubeba wala kukuuguza ni sisi ndugu zako wa damu.

Hapo ndipo unajua si muda wote damu ni nzito kuliko maji. Unaamua kupiga kimya tu sms za kikuda kama hizo haujibu unaamua kuwa outcast maana sometimes familia ndizo chanzo cha watu kukosa uelekeo badala kuwa chanzo cha uelekeo.

Haya maisha haya.
We acha ninayo pitia mungu ndo ujuaye .walikula pesa zangu sana ila sasa si kitu kwao .mungu nisaidie
 
Tunapitia mengi sana. Watu wakiona tunabishana na kugombana humu wanahisi ni wakorofi kumbe muda mwingine tunapambana na maumivu yanayosababishwa na familia na wale tunaowaamini kwenye maisha.

Anyways, pole sana kwa yaliyokusibu. Mimi nimeamua kuwa outcast ziwezi ishi karibu na watu ambao wanifanya nijiulize hawa ni familia yangu au nilikuwa adopted.
💯
 
Kama hao mi nawakataa tu no shobo, niliekuwa nae juani ndo ntakuwa nae kivulini
Ushawahi ona ile umemaliza chuo halafu umekula alosto sasa ule muda watu wengine huwa unakuwa mrefu sana unaweza sota hata miaka 5 hadi 8 maisha yamekukataa unaishia kufanya mishe tu za hapa na pale.

Unakutana na matukio unakichezea unasema ngoja nirudishe mpira kwa kipa kwanza nianze upya. Sasa hapo ndio unakichezea balaa. Badala ya wanandugu kukusitiri wanakujengea fensi wakunyooshe.

Mara wakuunganishe kazi kwenye ofisi za watu za kujitolea wewe akili yako haipo kwenye kuajiriwa unataka kufanya biashara ukomae mwenyewe, mitaji hamna ukitaka washirikisha wanakutema kuwa wewe ni mvivu, mzembe, mjuaji, haushauriki.

So hapo ndipo ukiomba hata pesa sapoti ya nauli ya kwenda sehemu ile tafu unajibiwa kama sijui umeomba milioni.

Mixer kukufuatilia, kuongea mambo ya dharau mbele ya madogo hadi wanawajaza ujinga madogo wanaanza kukudharau adabu zinashuka inauma kichizi.

Unakuwa mtu wa kutafuta faraja kwa marafiki badala ya familia. Siblings wako wanakuwa ni watu wa kushindana na kuleta upinzani usio na kichwa wala miguu. Sababu tu ni haujakaa sawa kiuchumi na wao wanakuona kama threat sasa sijui threat ya namna gani maana wewe hauwachukii wala hauna time na mapungufu yao.

Mwisho wa siku umejikusanya umesepa kimya kimetawala wanaanza kufosi ukaribu. Sio sikukuu wala weekend siendi tena home. Bi mkubwa nazungumza nae kwenye simu tu na ninamtumia ninachojiskia kutuma sitaki kupangiwa na mtu maana si niliambiwa asiyefanya kazi na asile mbona wao hawajafanya kazi why wanataka kula sasa, sheria si ni ile ile?
 
Ndugu lawama maana yake ndio hii sasa. Wao lawama ni muhimu kuliko kukusaidia ufanikiwe.
Yaani ndugu zako wote wakulaumu wewe tu bila sababu? Nyie ndiyo huwa mnapewa fedha mnazimaliza halafu mnarudi kutaka tena. Hao ndugu zako ni wewe uliwasaidia wakafika hapo walipo? Kama hukuwasaidia kwa nini unataka wakusaidie?
 
Ushawahi ona ile umemaliza chuo halafu umekula alosto sasa ule muda watu wengine huwa unakuwa mrefu sana unaweza sota hata miaka 5 hadi 8 maisha yamekukataa unaishia kufanya mishe tu za hapa na pale.

Unakutana na matukio unakichezea unasema ngoja nirudishe mpira kwa kipa kwanza nianze upya. Sasa hapo ndio unakichezea balaa. Badala ya wanandugu kukusitiri wanakujengea fensi wakunyooshe.

Mara wakuunganishe kazi kwenye ofisi za watu za kujitolea wewe akili yako haipo kwenye kuajiriwa unataka kufanya biashara ukomae mwenyewe, mitaji hamna ukitaka washirikisha wanakutema kuwa wewe ni mvivu, mzembe, mjuaji, haushauriki.

So hapo ndipo ukiomba hata pesa sapoti ya nauli ya kwenda sehemu ile tafu unajibiwa kama sijui umeomba milioni.

Mixer kukufuatilia, kuongea mambo ya dharau mbele ya madogo hadi wanawajaza ujinga madogo wanaanza kukudharau adabu zinashuka inauma kichizi.

Unakuwa mtu wa kutafuta faraja kwa marafiki badala ya familia. Siblings wako wanakuwa ni watu wa kushindana na kuleta upinzani usio na kichwa wala miguu. Sababu tu ni haujakaa sawa kiuchumi na wao wanakuona kama threat sasa sijui threat ya namna gani maana wewe hauwachukii wala hauna time na mapungufu yao.

Mwisho wa siku umejikusanya umesepa kimya kimetawala wanaanza kufosi ukaribu. Sio sikukuu wala weekend siendi tena home. Bi mkubwa nazungumza nae kwenye simu tu na ninamtumia ninachojiskia kutuma sitaki kupangiwa na mtu maana si niliambiwa asiyefanya kazi na asile mbona wao hawajafanya kazi why wanataka kula sasa, sheria si ni ile ile?
Hakika wewe utakuwa na matatizo. Maelezo yako ynaonyesha wewe ni mtu mshari. Anyways kila familia inakuwaga na mtoto mmoja wa dizaini yako
 
Haya maisha usipojipambania mwenyewe hakuna atakaekupambania, hata washkaji nao sometime jau.

Nenda na anaeenda na wewe, mshike anaekushikilia pia.

Nilichojifunza watu wanaendana kama malengo yao yanafanana, interest na matatizo/changamoto zao ni za aina moja.

NB: UKIFANIKIWA USIWAONE WENGINE NI WAZEMBE, MAMBO KWA GROUND SIO MEPESI KWA KILA MTU.
 
Back
Top Bottom