Dkt. Slaa: Freeman Mbowe aachane na Maridhiano maana hayafai, Katiba sio mali yake binafsi au mali ya Rais Samia

Na Mimi naongezea kwamba, chama chochote Cha siasa kiachane na harakati za kutafuta katiba ya wananchi, kwani katiba ya wananchi itatafutwa na wananchi wasio na mlengo wowote wa kisiasa, ili iweze kusimamia vyama vyote, vya kisiasa. Labda chadema itapendeza wakisimama kutafuta katiba ya chama Chao sio katiba ya wananchi.
Hakuna mwananchi yeyote yule atakayempambania Katiba mpya kama hajihusishi na chama chochote cha siasa.Na hakuna nchi yoyote ile duniani iliyowahi kupata Uhuru wake bila kuwa na chama chochote cha siasa.Vilaza wengi hufikiria kuwa mtu anapokuwa kwenye chama fulani cha siasa basi huyo mtu si chochote katika jamii maana akili yake hufikiria kwenye maslahi zaidi.Huu ni upungufu wa Akili Mwilini na ni ushamba uliopitiliza.
 
Ahsante Mzeee Slaa....
Nitasisitiza; Kuna mengi yaliyojificha nyuma ya pazia hili-Kuna mengi yatakayofichwa nyuma ya pazia hili linaloitwa Maridhiano. Ninaona migongano kati ya majabali wa Siasa nchini. Tutayaona wazi.

Nuff said.
again,
Thank you.
 
Namshauri Dr Slaa aanzishe chama ili afanye kile anachoona kinafaa kupitia chama chake mwenyewe. Huu utaratibu wa kurukia rukia ajenda za watu na kuzifanya kuwa za kwake hauleti maana yoyote kwa taifa.

Siasa za majitaka, mikiki mikiki na uongo wa mwembe yanga zimeshapitwa na wakati. Kwa sasa nchi imetulia aache watu wafanye kazi, na mambo yao kwa ueledi mkubwa na manufaa kwa taifa.
 
Unazani wananchi wenyewe watatafutaje katiba kama hakuna kiongozi wowote ambae atasiamia ...

Ni sawa na kusema wanafunzi waandae mitahala ya kufundishia wao wenyewe bila waalimu..

Sent from my M2010J19SI using JamiiForums mobile app
Viongozi wasitokane na vyama vya siasa. Kama ni wanasiasa wasitumie majukwwaa ya siasa ya vyama vyao huku wakitaka katiba ya wananchi. Viongozi wasiwe viongozi wa kisiasa, mfano eti chama flani kikiwa na mavazi ya chama Chao kusaka katiba ya wananchi.

Kumbuka katiba haitakiwi kuwa na mahusiano ya chama chochote kwani inatakiwa iwe ni Sheria mama Kwa vyama vyote bila upendeleo. Wakishaitwa wanachama wa chama flani wao watafute katiba ya vyama vyao, ila kama wanatafuta katiba ya wananchi wajivue uanachama hata kama wanavyama vyao, wawenutral ndio watafute katiba ya wananchi.
 
Najiuliza Kwa sauti je chadema uchaguzi ukishika dola kabla katiba haijabadilushwa watataka ibadilishwe?
 
Confrontational politics hazijawahi kuisaidia CDM sana sana zimewaumiza mno (Rip Mawazo, Saanane)......Mbowe apongezwe kwa hatua hii ya maridhiano angalau yataipa Chadema Uhuru wa kufanya siasa.
zitto junior
Yes hata kwa JPM tulipoenda Mwanza siku ya Uhuru ilikua ni kutafuta maridhiano haya haya tu. Sasa Leo yamepatikana tuanze tena kulumbana ya Nini?. Mbowe aachwe atafute suluhu mezani maana confrontational politics za Hawa waTZ waoga haziwezi zaa matunda. Hakuna haja ya mabavu kama mtu ni sikivu. So tuunge mkono maridhiano at least mpaka mwaka uishe tukiona hakuna jema Mnyika alisema watajitoa.
 
Akihojiwa na East Africa Radio asubuhi hii Aprili 20, 2023, Dkt Slaa amesema akipata nafasi ya kukutana na mwenyekiti wa CHADEMA Mhe. Freeman Mbowe atamshauri aachane na maridhiano kwa kuwa hayafai.


“Nikipata nafasi ya kukutana nitamwambia kwamba fuata principle za siasa safi, simamia, kwa sababu kwa sasa unatakiwa kuwapatia watanzania katiba mpya. Maridhiano hayafai” amesema

Amesisitiza, “Maridhiano hayafai kwasababu yanakaa zaidi ya mwaka, hakuna taarifa kwa wananchi. Maridhiano si mali ya Samia na ya Mbowe. Katiba inayodaiwa ni ya watanzania. Katiba si mali ya watu wawili, wala sio ya CCM na CHADEMA, ni ya watanzania. Watanzania lazima wajue wanataka katiba ya aina gani”
Dkt Slaa amesema amemsikia mara kadhaa Rais Samia akisema kuwa wataangalia katiba ya mwaka 1977 kwa kuwa Rasimu ya Warioba imepitwa na wakati, yeye anasema haya ni makosa makubwa sana.

“Someni preamble pale kwenye katiba mwanzoni imeandikwa nini, imeandikwa sisi watanzania tumeamua, kwenye katiba”

Kuhusu kusubiria uteuzi, amesema kwa umri wake hasubirii tena fursa hiyo, pia amemsfia Freeman Mbowe kuwa mwanasiasa mzuri, mkonge na mpambanaji wa siku nyingi.


Chanzo: East Africa Radio
Huyu mzee ninamsikilizaga sana kwa kujifunza
 
Huyu ndio mwanasiasa bora kuwahi kutokea TZ.
Dr Slaa anamisimamo isiyoyumba wala kuyumbishwa. Tumemiss aina ya siasa za huyu mzee.
Kaondoka CDM na chama kimekufa.
 
Akihojiwa na East Africa Radio asubuhi hii Aprili 20, 2023, Dkt Slaa amesema akipata nafasi ya kukutana na mwenyekiti wa CHADEMA Mhe. Freeman Mbowe atamshauri aachane na maridhiano kwa kuwa hayafai.


“Nikipata nafasi ya kukutana nitamwambia kwamba fuata principle za siasa safi, simamia, kwa sababu kwa sasa unatakiwa kuwapatia watanzania katiba mpya. Maridhiano hayafai” amesema

Amesisitiza, “Maridhiano hayafai kwasababu yanakaa zaidi ya mwaka, hakuna taarifa kwa wananchi. Maridhiano si mali ya Samia na ya Mbowe. Katiba inayodaiwa ni ya watanzania. Katiba si mali ya watu wawili, wala sio ya CCM na CHADEMA, ni ya watanzania. Watanzania lazima wajue wanataka katiba ya aina gani”
Dkt Slaa amesema amemsikia mara kadhaa Rais Samia akisema kuwa wataangalia katiba ya mwaka 1977 kwa kuwa Rasimu ya Warioba imepitwa na wakati, yeye anasema haya ni makosa makubwa sana.

“Someni preamble pale kwenye katiba mwanzoni imeandikwa nini, imeandikwa sisi watanzania tumeamua, kwenye katiba”

Kuhusu kusubiria uteuzi, amesema kwa umri wake hasubirii tena fursa hiyo, pia amemsfia Freeman Mbowe kuwa mwanasiasa mzuri, mkonge na mpambanaji wa siku nyingi.


Chanzo: East Africa Radio
Uyu mzee nae atulie , na ikiwezekana aongeze mke mwingine, si ndo uyu alikejeli sana chadema kipindi kahongwa na mwendazake ubalozi, Leo anaongea nini,

Ya chadema yalisha mshinda na ndo maana akafanya usaliti mkubwa ,siku nikutana naye atajuta , maana akikaa vibaya namzabua vibao,

Dr Slaa kaa kimia au anzisha chama chako
 
Namshauri Dr Slaa aanzishe chama ili afanye kile anachoona kinafaa kupitia chama chake mwenyewe. Huu utaratibu wa kurukia rukia ajenda za watu na kuzifanya kuwa za kwake hauleti maana yoyote kwa taifa.

Siasa za majitaka, mikiki mikiki na uongo wa mwembe yanga zimeshapitwa na wakati. Kwa sasa nchi imetulia aache watu wafanye kazi, na mambo yao kwa ueledi mkubwa na manufaa kwa taifa.
Agenda ya KATIBA mpya ni ya wananchi.

Si agenda ya CCM na CDM pekee.
 
Back
Top Bottom