Jidu La Mabambasi
JF-Expert Member
- Oct 20, 2014
- 15,386
- 24,358
Diwani mstaafu wa Kiromo anayeitwa Hassan Wembe, ambaye hana historia nzuri sana, amefanya jaribio la kihuni na kuudhi kwa kumzushia tuhuma za uongo aliyekuwa waziri Awamu ya Nne, mh. Shukuru Kawambwa.
Clip iliyorushwa mitandsoni na kusambaa kama moto wa nyika, ilikuwa ikimtuhumu ati Kawambwa ni dalali wa viwanja!
Imejulikana kuwa sababu ya mzozo ni uamuzi wa wanakijiji wa Kitopeni kuamua kufunga barabara yao kutokana na malori ya mchanga kuiharibu kabisa na kufan gari ndogo za wananchi kushindwa kupita.
Katika clip hiyo Diwani Hassan Wembe alidiriki kumvaa mwilini Kawambwa ambaye hakuonekana kubishana wala kurudisha maneno ya kuudhi ya mhuni Hassan Wembe.
Kwa tunaomfahamu Kawambwa toka alipokuwa wizarani (Miundombinu Ujenzi) huyu jamaa ni maji ya mtungi, hana presha au munkari.
Pengine kwa vile alikuwa mwalimu UDSM-Uhandisi.
Habari zilizopatikana ni kwamba katika hilo valangati la Diwani mstaafu Hassan Bwana alikuwepo jirani ya Kawambwa ambaye ni DSO mstaafu (Mkuu wa Usalama wilaya).
Na habari zinatonya kuwa huyu Wembe na grupu lake wamelala lupango.
Clip iliyorushwa mitandsoni na kusambaa kama moto wa nyika, ilikuwa ikimtuhumu ati Kawambwa ni dalali wa viwanja!
Imejulikana kuwa sababu ya mzozo ni uamuzi wa wanakijiji wa Kitopeni kuamua kufunga barabara yao kutokana na malori ya mchanga kuiharibu kabisa na kufan gari ndogo za wananchi kushindwa kupita.
Katika clip hiyo Diwani Hassan Wembe alidiriki kumvaa mwilini Kawambwa ambaye hakuonekana kubishana wala kurudisha maneno ya kuudhi ya mhuni Hassan Wembe.
Kwa tunaomfahamu Kawambwa toka alipokuwa wizarani (Miundombinu Ujenzi) huyu jamaa ni maji ya mtungi, hana presha au munkari.
Pengine kwa vile alikuwa mwalimu UDSM-Uhandisi.
Habari zilizopatikana ni kwamba katika hilo valangati la Diwani mstaafu Hassan Bwana alikuwepo jirani ya Kawambwa ambaye ni DSO mstaafu (Mkuu wa Usalama wilaya).
Na habari zinatonya kuwa huyu Wembe na grupu lake wamelala lupango.