Dar tu wamesanda mpaka sasa ni kama huduma ya msaada. Hela yako bado ikutoe kamasi.Vipi mikoani hamleti miendo ya kasi
Tunakushukuru kwa kupitia kwenye uzi huu,1. Gari chache sana saaaana mnakera. Sijui mnazipark vituoni au?
2. Kuna madereva wanajiona Miungu watu wanapita na "Out of Service" yaani.
3. Vingine mnajitahidi. Hope mtaboreka zaidi.
Asante sana mkuu kwa kutukaribishaKaribu JF DART Jitahidi Kujibu Hoja, Maswali, Madukuduku
Hapa Kuna Mengi Mkiwa Active Mtavuna Mbinu, Maarifa Michango Mbalimbali
Hasa Zinazohusu Majukumu Yenu
Ulitakiwa uyabainishe haya matatizo, ndiyo maana wamekuja, sasa ukiandika hivi tu, si utakua unafanana nao tu.Yaani ninyi ni wa kuomba maoni kweli.
Aisee hii dunia huwa haiishiwi vituko. Si mngeanza kwanza kurekebisha hali ya hovyo iliyopo ambayo hata haihitaji maoni. Baada ya hapo ndiyo mnatafuta maoni kutoka kwa watumiaji wa huduma.
Hali iliyopo haihitaji maoni ya watu sababu hali mliyo nayo inatokana na uwezo mdogo either kiutawala, kiubunifu, kiutendaji na kiuwwzo kama Kampani.
Kwa kifupi mna matatizo, malizeno kwanza matatizo yenu ndiyo mtujie wananchi tuwapatieni changamoto.
Tunashukuru kwa mchango wako, kwa sasa tuko katika mchakato wa kukamilisha sheria ya DART ambayo itatupa mamlaka ya kwenda kuanzisha huduma katika miji mingine mikubwa kama , Mwanza, Arusha, Mbeya, Dodoma, Tanga n.k. , kwahiyo wana Mwanza msiwe na wasi wasi tutawafikia.Asante kwa kuja.
Ni lini hayo mabasi mtayapeleka Mwanza pia ili wananchi wapate huduma ya usafiri..??
Sababu jiji la Mwanza limekua na tayari limechangamka na mkituletea hizo Bus zikaanzia route ya Kisesa, Igoma, Neshno, Buzuruga, Mabatini, Nata, Pepsi, Mkuyuni, Nyegezi, Buhongwa, Nyashishi hadi Usagara and Return.
Kama hawaoni basi hata nikiwapatia either hawataelewa au hawana nia bali wanatuchora tu.Ulitakiwa uyabainishe haya matatizo, ndiyo maana wamekuja, sasa ukiandika hivi tu, si utakua unafanana nao tu.
Sio kila kero kila mtu anakerekwa.
Mkuu umeongea kweli nyomi la jioni kwenye vituo vya mwendokasi ni hatari na vurugu tupuMimi naomba Mkurugenzi wenu na member wote wa menejiment waweke Tu utaratibu WA kupanda hayo mabasi kila wiki...
Wasitumie gari binafsi kila mwezi mara moja Kwa wiki nzima....mtapata majibu yote
Utaratibu wa matumizi ya kadi ilisitishwa kutokana na changamoto mbalimbali za kiufundi, kwa sasa mpango wa kurudisha kadi unakaribia kukamilika na mtajulishwa matumizi yake yataanza lini na namna ya kupata kadi hizo.Kwanini hamtumii Kadi?
Tunaahidi hatutawaangusha tutajitahidi kushirikiana na nyinyi katika kuboresha huduma zetu.Imekuwa vyema sana, but ushirikiano uwepo, tusije kuwa tunajiongelesha wenyewe.
Aache kukalia lile li prado lake apande mwendo kazi 😂😂😂 akipanda mniite mbwa nipo hapa nasubiri majibuMimi naomba Mkurugenzi wenu na member wote wa menejiment waweke Tu utaratibu WA kupanda hayo mabasi kila wiki...
Wasitumie gari binafsi kila mwezi mara moja Kwa wiki nzima....mtapata majibu yote
Shukrani.Tunaahidi hatutawaangusha tutajitahidi kushirikiana na nyinyi katika kuboresha huduma zetu.
Mkiwa active mtapata mengi sana. Ila msije mkaja na mambo ya wenzenu TANESCO ya kupewa changamoto walizonazo, wao badala ya kuhangaika na changamoto hizo, wanaanza mambo ya kutaka mtu aandike namba yake ya simu, anakoishi na jina lake kamili..!!!View attachment 2625074
DART Tumeanzisha ukurasa huu rasmi wa Wakala wa Mabasi Yaendayo Haraka (DART) kwa lengo la kupata maoni, ushauri , mrejesho na hata malalamiko yanayohusu huduma zetu. Aidha tunawahakikishia watumiaji wa huduma zetu kuwa maoni, ushauri, malalamiko, Pamoja na hoja zenu juu ya huduma zetu yatafanyiwa kazi kwa uharaka na hatua stahiki zitachukuliwa ili kuboresha huduma.
Kwa kupata msaada wa haraka kuhusu huduma zetu unaweza kutupigia simu 0800110147 ni bure. Kuanzia saa 11 alfajiri hadi saa tano na nusu usiku
Pia unaweza kutufuatilia katika tovuti ya www.dart.go.tz na mitandao yetu ya kijamii ya Wakala wa Mabasi Yaendayo Haraka ya FACEBOOK, INSTAGRAM, TWITTER, LINKEDIN, YOUTUBE.
Wakala wa Mabasi Yaendayo Haraka
Anuani
S.L.P 724, 16103
Ubungo Maji, Morogoro Road
Dar es Salaam, Tanzania
Barua pepe: info@dart.go.tz.
#usafiri wa umma nadhifu
#mwendokasi app