Tuanzie kwenye uumbaji;Kivipi mkuu? Hebu eleza kwa upana.
Mwanamke aliumbwa kwa kutolewa sehemu ya ubavu wa mwanaume [Adam na Hawa],ndoa ya kwanza ilianzishwa hapo, Mungu akaagiza [mwanzo 2;24],.... naye ataambatana na mwenzake,....nao watakuwa mwili mmoja...agizo likakaziwa zaidi [marko 10;9],....alichokiunganisha MUNGU mwanadamu asikitenganishe.
Ni andiko lipi limemuongoza kuivunja ndoa yake kwa kisingizio cha kumtumikia Mungu?Ni Mungu yupi anayemtumikia,aliyeumba ndoa au anayevunja ndoa?Aliivunja ndoa yake ili akafungue kanisa lake,...-linalo/litakalo mtumikia Mungu yupi?
Ni wakati gani (tangu kuumbwa kwa ulimwengu) Mungu aliwahi kumweka mwanamke kuwa kiongozi wa kanisa/hekalu/sinagogi,kuwa mchungaji/kuhani?Atupe andiko lililo muongoza, kwasababu,hata Yesu Kristo alipokuwa duniani hakuwahi kubatilisha/kubadilisha mpango,sheria na kanuni za Mungu,na kwakulithibitisha hilo,kati ya mitume 12 aliowapa kazi ya kuzunguka ulimwenguni kuihubiri injili,hakuwepo mwanamke.Kiongozi wa kanisa ni mwakilishi wa YESU KRISTO aliye kichwa cha kanisa,.. mwanamke anatoa wapi jeuri ya kusimama madhabauni akiwa ni mchungaji/kuhani?Huku ni kumpinga MUNGU wazi wazi na kumtukuza Shetani/Ibilisi mwenye ajenda ya 50/50[serikalini hadi makanisani],haki za wanawake n.k., na kwakuwa siku hizi makanisa yamegeuka kuwa biashara nzuri,watu hawamhofii MUNGU,bali wanakazana kujikweza wao.
Kwa hiyo,yeyote anayekubaliana na mawazo na maamuzi ya huyu dada,asome maandiko vizuri kisha ajitafakari.