Bando la wiki
JF-Expert Member
- May 23, 2023
- 349
- 951
Naona moto wa Chadema (Tundu Lissu) umewaka Tanzania nzima. Naona huu moto ni kama ule wa vijana wa Senegal Marais wa sasa (Rais na makamo wake) walivyo uwasha moto mpaka wakaingia ikulu ya Senegal.
Cha kufanya CHADEMA ni kutokulaza damu kuanzia sasa hivi mpaka uchaguzi mkuu 2025.
1. Maandamano yaendelee nchi nzima mkigawana mikoa.
2. Hoja ngumu ziendelee kutolewa mikutanoni na kwenye media mbalimbali hasa online TV kwa sababu hakuna TV iliyo huru kuwaunga mkono kwa kuogopa pini kutokana wizarani.
3. Mtangazie umma na polisi kwamba kura za uchaguzi wa wananchi zitalindwa na wananchi wenyewe kwa sababu katiba haijazuia wananchi kulinda kura zao.
4. Tume ihakikishe kila chumba cha kupigia kura kuna kuwa na wakala wa vyama kwa ajili ya kuhesabu kura na kuhakikisha usahihi wa kura zote halali.
Mizengwe kwa mawakala au ikijulikana kwamba kituo fulani hakukuwa na wakala wa chama, kura katika hicho kituo hazitatumbulika.
5. Kuwe na wenyeviti wa chama kuanzia ngazi ya mtaa, Tanzania nzima na mawasiliano yao yawe kwenye database makao makuu. Wenyeviti hawa watoe taarifa mara moja makao makuu kama kuna hujuma yoyote inatokea kwenye vituo vya kupigia kura ili viongozi makao makuu watoe tamko la kukemea kwa nguvu muda huo huo.
6. Mfungue kituo cha kuhesabu na kujumlisha kura zote kutoka kwenye kila kituo Tanzania nzima. Na muwatangazie Tume ya uchaguzi kwamba mahesabu yao yawe sawa na yenu kichume na hapo watakuwa wamechochea ukosefu wa amani katika nchi. Katiba haijazuia chama kuwa na tume yake kujumlisha kura zake kutoka kwa mawakala wao nchi nzima.
Hakuna muda mwepesi wa Upinzani kuingia ikulu kama 2025 endapo raisi aliyepo atagombea tena.
Tundu Lissu una kitu naona utatufaa Tanzania kupata unafuu kwenye masuala ya sheria kwa sababu wewe ni mbobevu kwenye upande huo wa sheria.
Sheria zetu ni mbovu zinazokandamiza raia wa kawaida huku wezi na wabadhirifu zikiwaacha pasipo kuwagusa. Tazama wezi wa ripoti za CAG bado wapo wanadunda huku wameiba pesa ambazo zingeweza kusaidia wananchi kupata hata mikopo banki kwa riba nafuu chini ya 10% wakaingiza kwenye biashara na kukuza uchumi wa nchi.
Sheria zetu ni mbovu zinawapa mamlaka wawekezaji uchwara wa kigeni kudai fidia ya mabilioni wanaposhindwa kufanya kazi.
Cha kufanya CHADEMA ni kutokulaza damu kuanzia sasa hivi mpaka uchaguzi mkuu 2025.
1. Maandamano yaendelee nchi nzima mkigawana mikoa.
2. Hoja ngumu ziendelee kutolewa mikutanoni na kwenye media mbalimbali hasa online TV kwa sababu hakuna TV iliyo huru kuwaunga mkono kwa kuogopa pini kutokana wizarani.
3. Mtangazie umma na polisi kwamba kura za uchaguzi wa wananchi zitalindwa na wananchi wenyewe kwa sababu katiba haijazuia wananchi kulinda kura zao.
4. Tume ihakikishe kila chumba cha kupigia kura kuna kuwa na wakala wa vyama kwa ajili ya kuhesabu kura na kuhakikisha usahihi wa kura zote halali.
Mizengwe kwa mawakala au ikijulikana kwamba kituo fulani hakukuwa na wakala wa chama, kura katika hicho kituo hazitatumbulika.
5. Kuwe na wenyeviti wa chama kuanzia ngazi ya mtaa, Tanzania nzima na mawasiliano yao yawe kwenye database makao makuu. Wenyeviti hawa watoe taarifa mara moja makao makuu kama kuna hujuma yoyote inatokea kwenye vituo vya kupigia kura ili viongozi makao makuu watoe tamko la kukemea kwa nguvu muda huo huo.
6. Mfungue kituo cha kuhesabu na kujumlisha kura zote kutoka kwenye kila kituo Tanzania nzima. Na muwatangazie Tume ya uchaguzi kwamba mahesabu yao yawe sawa na yenu kichume na hapo watakuwa wamechochea ukosefu wa amani katika nchi. Katiba haijazuia chama kuwa na tume yake kujumlisha kura zake kutoka kwa mawakala wao nchi nzima.
Hakuna muda mwepesi wa Upinzani kuingia ikulu kama 2025 endapo raisi aliyepo atagombea tena.
Tundu Lissu una kitu naona utatufaa Tanzania kupata unafuu kwenye masuala ya sheria kwa sababu wewe ni mbobevu kwenye upande huo wa sheria.
Sheria zetu ni mbovu zinazokandamiza raia wa kawaida huku wezi na wabadhirifu zikiwaacha pasipo kuwagusa. Tazama wezi wa ripoti za CAG bado wapo wanadunda huku wameiba pesa ambazo zingeweza kusaidia wananchi kupata hata mikopo banki kwa riba nafuu chini ya 10% wakaingiza kwenye biashara na kukuza uchumi wa nchi.
Sheria zetu ni mbovu zinawapa mamlaka wawekezaji uchwara wa kigeni kudai fidia ya mabilioni wanaposhindwa kufanya kazi.